Simulizi: Soka Lilivyonikutanisha Na Shetani

Simulizi: Soka Lilivyonikutanisha Na Shetani

Dah! Huyu jamaa ukimfikiria sana unashindwa umuweke kundi gani.
 
 

Ubarikiwe hii sijaiona...


Cc: mahondaw
 
Sehemu ya 88

“Baba huyu anaitwa Ajibu, ndiye mwanaume niliyekuwa nakwambia habari zake,” alimwambia yule mzee, sikujua aliposema ‘Ndio mwanaume niliyekuwa nakwambia habari zake’ aliwahi kumweleza nini baba yake.

“Shikamoo baba,”nilimsalimu mzee huyo.
Mzee alinikata jicho baya hakuitikia salamu yangu badala yake akaniuliza:
“Unataka nini?” Sauti yake ilikuwa na viashiria vyote vya shari.

“Aaaaah! Baba umeanza, swali gani hilo unamuuliza mgeni?” Lawalawa alimkemea mzee huyo, naye akafunga mdomo. Ilivyoonesha ni kama mwanamke huyo ndiye alikuwa kiongozi wa familia hiyo.

Niliketi sofani moyoni nikiwa na furaha ya kuonana na Lawalawa, mwanamke wa ndoto zangu. Sikujali gubu la kikongwe yule.

Mwanamke huyo chochara mwenye asili ya Kiarabu na Kibantu wa Unyamwezini, aliniandalia sharubati baridi ya tende na mkate. Wakati nakula kitafunwa kile alikuja na kuketi kando yangu.

Tukaanza tena maongezi:
“Ajibu, nimehangaika mno kukusaka mpenzi, ulikuwa wapi wewe?” “Nilikuwa katika mihangaiko tu ya maisha.”
“Sikuwahi kuwa na raha tangu nilipobaini nafsi yangu imelimisi penzi lako.”
“Kweli?”

“Haki ya Mungu nakuapia Ajibu.”
Aliposema kauli hiyo, kimoyo moyo nikakiri, kweli Mganga Majeed Mapaka kutoka Unguja ni Kiboko. Mpumbavu mimi nilishangilia moyoni kwa kuona nimepata nilichokitaka maishani.

Kumroga msichana huyo na kumleta upande wangu, lilikuwa ni jambo zuri. Sikufirikia matokeo ya ubaya wa ushirikina niliokuwa najihusisha nao, nilichokuwa nakitaka ni jambo langu kuwa.

Wakati tunaongea baba yake alikuwa kimya, hakuwa na nguvu kabisa mbele ya mwanaye huyo niliyekwisha mchanganya akili, uso wake ulionesha kuchukizwa na mambo aliyokua akizungumza mtoto wake, lakini angemfanya nini na umri ule.
Nyumbani hapo kulikuwa na watu watatu ama wanne, wafanyakazi wawili wa ndani, mzee yule kikongwe sambasamba na Lawalawa mwenyewe, ilikuwa ni nyumba kubwa iliyokaliwa na watu wachache.

“Ajibu nahitaji niishi na wewe tena, kama zamani, nahitaji kuishi na wewe hapa nyumbani, kwenye nyumba hii.” Lawalawa aliendelea kunieleza, alionekana kuwa katika kina kirefu cha huba, hakuwa akijiweza tena mbele yangu.
 
Sehemu ya 89

MWANAMKE huyo alilaza kichwa chake kifuani mwangu huku jasho likimchuruzika maungoni mwake.Yule babu kizee alitizama tukio hilo kwa jicho baya.

Kimoyomoyo niliendelea kushangilia moyoni. Dawa ya mganga wa Unguja imefanya kazi. Kitendo cha mwanamke huyo kuzama juu yangu ilikuwa ni ushindi mkubwa. Hilo ndilo nilikuwa nalitaji maishani.

“Vipi kuhusu mumeo Lawalawa?” Nilimuliza tukiwa pale sebuleni.
“Hebu ninyi watoto kuweni na adabu, mnaongea mambo gani hapa. Haya ondokeni hapa.” Mara yule mzee aliyekuwa akiniangalia kwa jicho baya, alifoka. Alishindwa kabisa kuvumilia kuona mahaba niliyokuwa nikionyeshana mwanamke huyo.

Lawalawa, alijitoa maungoni mwangu, akanishika mkono na kuniongoza hadi chumbani mwake. “Ajibu huyu mzee ana gubu sana huyu.” “ Baba yako anaonesha kabisa hanipendi.”

“Usijali, kwa kuwa mimi nakupenda hakuna wa kuniuzuia kuishi na wewe.” Alisema Lawalawa.

“Haya nambie Lawalawa, imekuwaje kati yako na mumeo?”
“Simtaki tena.” Mwanamke huyo alisema bila kigugumizi. “Eeh!. Kwa nini?”
“Kwa sababu simpendi.”

“Sasa kama humpendi kwa nini ulifunga naye ndoa?”
“Ajibu,nilishawishiwa na baba yangu, lakini kwa sasa siwezi tena kurudi kwake,” alisema.
Ukimya mfupi ukapita baina yetu kisha nikamuuliza.

“Ulizaa naye watoto wangapi huyo mumeo?”
“Wawili tu.”
“Wako wapi sasa hao watoto wako?”
“Kwa baba yao, wanaishi nchini Yemen, niliwacha huko kwa ajili yako mpenzi?” alisema.

Kwa kweli nilijikuta hadi natetemeka, nguvu za giza nilizokuwa nimezitumia kumroga mwanamke huyo ili aje kwangu na anipende zilikuwa zimemkamata hasa.
Kitendo cha kuwaacha watoto wake na mumewe wa ndoa kwa ajili yangu halikuwa jambo la kawaida. “Ajibu wewe hukuwahi kuoa tangu nilipokuacha kipindi kile?” Lawalawa naye alihoji.

“Sitaki nikudanganye Lawalawa, ulivyoniacha nilipata mwanamke, ndiye nilikuwa naishi naye.” “Kwa hiyo bado upo naye?”
“Ndiyo, bado niko naye, lakini kuanzia sasa simtaki tena.”
Niliongea kama mpumbavu na kweli nilikuwa mpumbavu kwenye penzi la Lawalawa.

Mwanamke huyo alinikumbatia huku akionekana kuwa na hisia kali za mapenzi.
Kwa kuwa na mimi nilikuwa nampenda mno Lawalawa, kama nilivyosema nilikuwa kama mwendawazimu.
 
Sehemu ya 90

Kufumba na kufumbua, tukajikuta tupo kitandani, tukiwa kama tulivyozaliwa. Dakika chache badaaye, tukawa tunaelea kwenye bahari kubwa ya huba.

Mambo yote hayo yalifanyika harakaharaka sana nyumbani kwao Lawalawa, mjini Tabora. Kuanzia siku hiyo niliishi na Lawalawa nyumbani kwao pale bila woga wowote.

Nilikuwa mario.
Hakuna nilichokuwa naogopa wala kujali, moyo wangu na mapenzi yangu yalikuwa kwa mwanamke huyo. Mara nyingi mke wangu Pili aliyekuwa mjini Kigoma kila aliponipigia simu niliishia kumdanganya kwamba aisone kimya niko bize na biashara.

Kuna wakati nilipoona simu za mke wangu zinanitia karaha, nikawa nazima simu. Wakati mwingine akawa akipiga simu sipokei. Kuna wakati nikawa namkatia simu. “Itabidi ubadilishe namba ya simu. Unaonaje?”siku moja Lawalawa alinishauri baada ya kero kuzidi.

“Uko sahihi, nitafanya kama utakavyo Lawalawa.”
Siku hiyo hiyo nilisajili laini nyingine, ile ya mwanzo nikaitupilia mbali. Mke wangu Pili, hakunipata tena.

Wiki ilipita. Kama mzaha maisha yangu na Lawalawa yaliendelea nyumbani kwao. Tuliishi vziuri mimi na yeye, ingawa gubu kubwa ilikuwa ni yule babu kizee.

Baba yake na Lawalawa, ambaye akama nilivyosimulia awali alikuwa mzee sana. Hakupenda kabisa mahusiano yetu. Mara kadhaa alikuwa akinilaani kwa kitendo cha kumtoa mtoto wake kwa mumewe wa ndoa na kuishi naye kwao nikiwa nalelewa.

“Mungu akulaani we’ ibilisi, umeharibu ndoa ya mwanangu, kama haitoshi unaendelea kumpotosha mwanangu.”
Mzee huyo aliniambia maneno hayo. Hata hivyo angenifanya nini?mtu mwenyewe alikwishajiishia anangojea siku zake chache zilizosalia ajifie.

Kwa hiyo maneno ya babu kizee huyo hayakunizuia mpumbavu mimi kuendelea kuishi na mwanaye ndani ya nyumba yake.

Siku moja Lawalawa aliniita na kuniambia jambo moja. Alisema:
“Nimewakumbuka wanangu Ajibu.” “Sasa?” nikamaka.

“Unaonaje nikienda kuwaona.” “Huko nchini Yemeni wanakoishi na baba yao?”
 
aisee bora kubaki single kuliko kuolewa na mtu kama ajibu,.
 
Sehemu ya 90

Kufumba na kufumbua, tukajikuta tupo kitandani, tukiwa kama tulivyozaliwa. Dakika chache badaaye, tukawa tunaelea kwenye bahari kubwa ya huba.

Mambo yote hayo yalifanyika harakaharaka sana nyumbani kwao Lawalawa, mjini Tabora. Kuanzia siku hiyo niliishi na Lawalawa nyumbani kwao pale bila woga wowote.

Nilikuwa mario.
Hakuna nilichokuwa naogopa wala kujali, moyo wangu na mapenzi yangu yalikuwa kwa mwanamke huyo. Mara nyingi mke wangu Pili aliyekuwa mjini Kigoma kila aliponipigia simu niliishia kumdanganya kwamba aisone kimya niko bize na biashara.

Kuna wakati nilipoona simu za mke wangu zinanitia karaha, nikawa nazima simu. Wakati mwingine akawa akipiga simu sipokei. Kuna wakati nikawa namkatia simu. “Itabidi ubadilishe namba ya simu. Unaonaje?”siku moja Lawalawa alinishauri baada ya kero kuzidi.

“Uko sahihi, nitafanya kama utakavyo Lawalawa.”
Siku hiyo hiyo nilisajili laini nyingine, ile ya mwanzo nikaitupilia mbali. Mke wangu Pili, hakunipata tena.

Wiki ilipita. Kama mzaha maisha yangu na Lawalawa yaliendelea nyumbani kwao. Tuliishi vziuri mimi na yeye, ingawa gubu kubwa ilikuwa ni yule babu kizee.

Baba yake na Lawalawa, ambaye akama nilivyosimulia awali alikuwa mzee sana. Hakupenda kabisa mahusiano yetu. Mara kadhaa alikuwa akinilaani kwa kitendo cha kumtoa mtoto wake kwa mumewe wa ndoa na kuishi naye kwao nikiwa nalelewa.

“Mungu akulaani we’ ibilisi, umeharibu ndoa ya mwanangu, kama haitoshi unaendelea kumpotosha mwanangu.”
Mzee huyo aliniambia maneno hayo. Hata hivyo angenifanya nini?mtu mwenyewe alikwishajiishia anangojea siku zake chache zilizosalia ajifie.

Kwa hiyo maneno ya babu kizee huyo hayakunizuia mpumbavu mimi kuendelea kuishi na mwanaye ndani ya nyumba yake.

Siku moja Lawalawa aliniita na kuniambia jambo moja. Alisema:
“Nimewakumbuka wanangu Ajibu.” “Sasa?” nikamaka.

“Unaonaje nikienda kuwaona.” “Huko nchini Yemeni wanakoishi na baba yao?”
Nyingine lini,?
 
Sehemu ya 91

Ndio huko huko,” alijibu.
“Hujipendi Lawalawa.” “Kivipi Ajibu?”
“Ulimwacha mumeo na watoto, ukaja kwangu. Leo unataka urudi kwenye nchi ya watu.Nchi yenye sheria kali,kuwaona wanao, unaakili kweli?

Huko utachukuliwa kama mzinifu tu, huna utakalofanikiwa nakwambia, mumeo atakufukuza kama mbwa.””

“Hawezi!” “Kwa nini unasema hawezi?”
“Mume wangu ananipenda sana Ajibu, ni yeye ambaye jana amenitumia email, amesema amenikumbuka mno, ameomba anitumie tiketi ya ndege nirudi kwake.”

“Na wewe ukamkubalia?” nilimuuliza kwa wahaka. Wivu ukanishika moyoni, sikutaka kabisa kumkosa kiumbe yule chotara. Nilikuwa nampenda sana binti huyo mrembo.

“Sijakubali, ila nimeona kabla ya kufanya lolote nikuombe ruhusa.”
“Hapana mimi siko tayari. Sitaki kabisa uniache mpenzi, umesikia?” “Nimekusikia Ajibu. Nitafanya utakavyo.”
“Pia sitaki mawasiliano baina yenu, sawa?”

“Sawa mpenzi.” Mwanamke huyo alinitii.
Siku zilikwenda, sikusikia tena Lawalawa akinieleza habari za kwenda kuwaona watoto wake.

Miezi kadhaa ilipita baada ya mambo yote hayo kutokea. Hapa nimesahau kueleza ajambo moja. Tangu nifike mjini Tabora au niseme tangu nianze kuishi na mpenzi wangu Lawalawa, huwa sina kazi yoyote.

Mimi ni kula na kulala. Labda na kumpenda Lawalawa. Hilo ndilo nililokuwa nalijua nyakati hizo. Kwa kweli nilikuwa mwanaume mshenzi.

Mambo yote muhimu alikuwa akisimamia mpenzi wangu huyo. Naweza kusema kipindi chote, nilikuwa ‘mario’ niliyeshindikana.

Mara nyingi nyakati za jioni huwa napenda kwenda katika viwanja mbambali vya mpira, hasa kile kiwanja cha Ally Hassani Mwinyi kufuatilia mazoezi ya timu mbalimbali. Huwa nashikwa na misisimko kila nionapo watu wakicheza mpira.

Lakini kwa kuwa nilikwisha achana na mchezo wa soka, sikuwa na la kufanya, niliishia kufuatilia watu wakicheza, baada ya hapo narudi nyumbani, huko nakuta kila kitu mezani. Nakula, nawekewa maji ya kuoga, kisha mapumziko yangu nayamalizia chumbani na Lawalawa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom