Emmanuel Okwi astaafu soka la kulipwa

Emmanuel Okwi astaafu soka la kulipwa

PAYE

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2025
Posts
418
Reaction score
553
Nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Uganda, Emmanuel Arnold Okwi, ametangaza rasmi kustaafu soka la kulipwa baada ya miaka mingi ya mafanikio uwanjani. Kupitia ujumbe wake, Okwi amesema uamuzi huo ni miongoni mwa maamuzi magumu zaidi maishani mwake, akieleza kuwa soka halikuwa kazi tu bali lilikuwa ndoto, shauku na sehemu kubwa ya maisha yake.

Okwi amewashukuru klabu zote alizozichezea, makocha, wachezaji wenzake na mashabiki waliomuunga mkono katika safari yake ya soka. Pia amesema kuivaa jezi ya timu ya taifa ya Uganda na kupewa jukumu la unahodha ni heshima kubwa ambayo ataendelea kuithamini maisha yake yote.

Mshambuliaji huyo, ambaye aliwahi kung'ara pia akiwa na Simba SC ya Tanzania, amesema licha ya kustaafu kucheza, ataendelea kulitumikia soka kwa njia nyingine. Ameeleza kuwa hatua hiyo si mwisho wa safari yake kwenye mchezo huo, bali ni mwanzo wa sura mpya yenye lengo la kuchangia maendeleo ya soka na kuwahamasisha kizazi kijacho cha wachezaji.

THE GAME GAVE ME EVERYTHING! I LEAVE WITH GRATITUDE!! 🙏🏿❤️⚽️!!.jpg
 
Amestaafu akiwa na miaka mingapi mkuu😁?
Eti amestaafu akiwa na umri miaka 33! Utani wa ngumi huu 😀
Mwenzake Ronaldo alichagua kutofoji umri, leo bado anacheza na miaka yake 41! Sasa yeye uongo wake umeshindana na ukweli.
 
Watu wengine hawaonagi aibu kidanganya,ameanza kucheza nikiwa primary,nakaribia kustaafu eti yeye ana 33
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom