Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

SEHEMU YA 81

Linda alizaliwa katika familia ya kitajiri, wazazi wake walikuwa na pesa nyingi na ndiyo maana elimu zake zote alichukulia nje ya nchi barani Ulaya na Marekani.
Mbali na pesa za baba yake, naye alikuwa mfanyabiashara mzuri tu, maisha yake yalizungukwa na pesa na kila alipokuwa ni lugha ya pesa tu ndiyo aliyokuwa akiizungumza.

Alikuwa na kila kitu alichokuwa akikihitaji, wakati mwingine aliona kwamba alikuwa na uwezo wa kupata kila kitu kwa kuwa alikuwa na pesa. Aliamini kwamba unapokuwa na pesa unaweza kupata mapenzi ya dhati, unapokuwa na pesa unabadilisha hata chuki kuwa penzi na ndiyo maana alimuihitaji sana Dickson.

Kutumia pesa kwa vijana wale kwa kazi aliyotaka kuifanya hakukuwa na tatizo, alihitaji furaha ya milele, alihitaji kujiona akitabasamu mbele ya kioo na kitu pekee alichoamini kwamba kingempa tabasamu hilo hakikuwa kingine bali pesa.

Vijana hao baada ya kutumiwa pesa hawakutaka kubaki walipokuwa, wakaambiwa mahali alipokuwa akiishi Amina na kuanza kuelekea huko. Hakukuwa na tatizo kumpata, wasifu wake kwamba alikuwa na wowowo kubwa, mzuri wa sura, mweupe vilikuwa vitu vilivyowapa uhakika wa kumpata kwa urahisi kabisa.

Wakaondoka mpaka Manzese Midizini walipokuwa wameelekezwa, walifika mpaka nje ya nyumba ya akina Amina ambapo kulikuwa na duka na kujifanya kununua kitu huku wakimuulizia Amina kwa muuza duka huyo.

“Amina yupo?” aliuliza jamaa mmoja aliyeitwa Kudra.
“Ametoka sasa hivi!”
“Amekwenda wapi tena?” aliuliza.
“Sijui! Alikuja jamaa yake, akamchukua na kuondoka naye, kurudi nadhani ni usiku,” alijibu muuza duka.

“Poa haina noma.”
Kwa kuwa walipata uhakika kwamba msichana huyo angerudi usiku hawakutaka kuwa na hofu, wakaondoka na kuwasiliana na Linda na kumwambia kile walichoambiwa na muuza duka.

Hakukuwa na tatizo lolote lile, akawaambia kwamba wafanye kila liwezekanalo na mwisho wa siku msichana huyo apatikane kwani kama angefika mahakamani huku akiwa hajapewa mkwara wowote ule ilikuwa ni lazima aseme ukweli kwamba hakubakwa.
 
SEHEMU YA 82

“Yaani hakikisheni anapatikana, sawa?” alisema Linda.
“Sawa.”
Usiku wakarudi Manzese Midizini, hawakutaka kwenda mpaka nyumbani kwa akina Amina, walichokifanya ni kwenda katika baa fulani iliyokuwa jirani na mahali hapo na kutulia.

Ilipofika majira ya saa tano usiku wakaliona gari moja aina ya Toyota Vitz ikielekea nyumbani kwa akina Amina na kusimama. Hakuteremka mtu yeyote yule mpaka baada ya dakika tano mlango ukafunguliwa na Amina kuteremka.

Kwa jinsi alivyokuwa amevaa, hawakuwa na maswali kwamba huyo alikuwa mwenyewe au mtu mwingine. Alikuwa na wowowo, mzuri, mweupe ambaye kila alipokuwa akitembea ni kama wowowo lilitaka kudondoka.

Akaagana na mwanaume aliyekuwa ndani ya gari na kuelekea ndani ya nyumba hiyo. Walipohakikisha mwanaume huyo ameondoka, Kudra akaelekea kule na kumuulizia muuza duka.

“Ameingia sasa hivi!”
“Naomba uniitie,” alisema.
Hilo halikuwa tatizo, kijana huyo akamuita Amina ambaye alifika hapo nje na kukutana na Kudra. Alichokisema mwanaume huyo ni kwamba aliwahi kuonana naye na kuzungumza mengi halafu msichana huyo akamuelekeza nyumbani kwao na hivyo kumfuata.

Kwa Amina, hilo halikuwa tatizo, alikuwa mwanamke aliyependa sana wanaume, kwake, kutoa namba ya simu hakukuwa na tatizo lolote lile, alikuwa tayari kufanya kitu chochote kile lakini mwisho wa siku apate pesa.

Hakuwa akimjua mwanaume huyo lakini akajikuta akianza kutoa tabasamu na kumuuliza maswali ambayo yalikuwa mepesi mno kujibika kwa Kudra.
“Sasa ndiyo unifuate usiku jamani?” aliuliza kwa sauti yake nyembamba.
“Nilikuja mchana, hukuwepo. Muulize dogo,” alisema Kudra, hapohapo muuza duka akadakia.

“Alikuja, ulikuwa umeondoka!”
“Umesikia! Hatuwezi kukaa sehemu kuongea?” alimuuliza.
“Mmh! Usiku huu?”
“Ndiyo! Kidogo tu!”

“Hapana!”
Alichokifanya Kudra ni kuingiza mkono mfukoni, akatoa bunda la pesa na kuchomoa shilingi elfu ishirini na kumpa muuza duka na kumshukuru kwa msaada wake wa kumuitia Amina na kuzungumza naye.
 
SEHEMU YA 83

Pesa hizo zilikuwa kama mtego, Amina alipoziona, moyo wake ukanyong’onyea, tamaa ikamshika kiasi kwamba mpaka yeye mwenyewe akajikuta akijilaumu kwa kukataa kutoka na mwanaume yule kwenda kuzungumza.

“Lakini isiwe mbali,” alisema Amina na wakati alikaa kabla, tayari Kudra akajua kabisa pesa zililainisha kila kitu.
“Pale tuu baa.”
Akamchukua na kuondoka naye. Amina alikuwa akijichekeshachekesha tu, pesa iliharibu kila kitu, akamsahau mwanaume aliyekuwa amemleta nyumbani pale na gari, aliangukia katika penzi la mwanaume mwingine kabisa.

Wakaelekea katika baa ile ambapo akakutana na mwanaume mwingine aliyetambulishwa kama rafiki wa Kudra na kuanza kuongea. Usiku huo ulikuwa ni wa kupombeka tu, walikuywa sana pombe, chakula. Amina aliamua kumchuna, alihisi kwamba kwa usiku huo angemaliza kibunda chote cha pesa kitu ambacho hakikuwa kweli kabisa.

Pombe zikamchukua, akaanza kupiga pombe kali kiasi kwamba mpaka inafika saa saba usiku, hakuwa akielewa kitu chochote kilichokuwa kikiendelea mahali hapo.
“Dullah! Kwanza tukamle uroda, mimi siwezi kuvumilia na hilo wowowo,” alisema Kudra.

Wakamchukua, wakamuingiza ndani ya gari na kumpeleka katika jumba moja waliloliandaa. Njiani, kila mtu alikuwa akifikiria kufanya mapenzi na msichana huyo, aliwatamanisha, wowowo lake, mapaja yake makubwa na meupe, kifua chake kidogo kiliwachanganya kupita kawaida.

Walipofika, hawakutaka kuchelewa, wakamlaza kitandani na kuanza kufanya naye mapenzi usiku mzima na walipomaliza, wakamfunga kamba.
Asubuhi ilipofika, Amina akashtuka, mwili wake ulikuwa ukijisikia uchovu kupita kawaida. Alishangaa mahali alipokuwa, alikuwa kitandani huku akiwa amefungwa kamba katika kitanda hicho cha chuma.

Hakujua ni mahali gani na alifikije. Akaanza kuvuta kumbukumbu, akakumbuka kwamba usiku uliopita alizungumza na mwanaume aliyekuwa na pesa ambaye alimchukua na kumpeleka baa na kuanza kunywa naye huku akiwa na rafiki wa mwanaume huyo na baada ya hapo hakujua ni kitu gani kilikuwa kimeendelea.

Kitandani pale kulikuwa na mipira ya kiume iliyokuwa imetumika. Hiyo ilionyesha kwamba mwanaume aliyekuwa amemleta chumbani pale alifanya naye mapenzi pasipo kujitambua.
 
Huyu Amina huyuuu.!! Tamaa za mihelaa zitampoonza.!! Azidi hadi tamaa ya Fisi duuh.!!
 
SEHEMU YA 84

Akaanza kupiga kelele mfululizo. Mara mlango ukafunguliwa na Kudra kuingia huku akiwa na bakuli la supu, akakaa kitandani na kumwangalia Amina.
“Vipi? Mbona unatupigia kelele?” aliuliza Kudra huku akimwangalia Amina.
“Nimefanya nini? Naomba mniache niondoke,” alisema Amina huku akianza kulia katika kitanda kile alipokuwa amefungwa.

“Hujafanya kitu! Subiri!” alisema Kudra, hakutaka kubaki ndani ya chumba hicho, akatoka.
Amina akabaki peke yake, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea mpaka mwanaume huyo na mwenzake kumchukua na kumfunga kamba ndani ya chumba hicho.

Alibaki akilia, mahali alipokuwa hakukuwa na dalili za kupata msaada wowote ule. Alijutia uamuzi wake wa kukubaliana na mwanaume yule na kumfuata kule alipokuwa kisa tu pesa alizokuwa amezishika.

Baada ya dakika kadhaa, Kudra akarudi chumbani humo akiwa na jiko la mkaa lililokuwa na moto huku kwa ndani akiwa ameweka kisu kilichokuwa kikiunguzwa na moto ule.

Amina akatetemeka, akahisi kabisa huo ndiyo ulikuwa mwisho wake. Akaanza kuomba msamaha japokuwa hakujua ni kosa gani alikuwa amelifanya. Kudra hakuzungumza kitu, alikuwa akiendelea kufanya mambo yake huku akinywa juisi.

Akamuita mwenzake ambaye akaja mahali hapo haraka sana na kuanza kuongea naye. Akamwambia kwamba ilikuwa ni lazima kuanza kazi yao kwani muda ulikuwa ukienda na kama wangechelewa kila kitu kingeharibika.
“Upo hapa kwa sababu moja tu,” alisema Kudra.

“Naomba mnionee huruma!”
“Upo hapa kwa sababu unataka kumgeukia bosi wetu mahakamani. Video inaonyesha kwamba umebakwa lakini unataka kumsaliti mahakamani na wakati amekulipa pesa nyingi sana,” alisema Kudra.
 
SEHEMU YA 85

Hapo ndipo Amina akapata majibu juu ya kilichokuwa kikiendelea. Alikuwa mahali hapo kwa sababu ya Linda ambaye alihitaji kumsikia akizungumza uongo mahakamani kama walivyokuwa wamekubaliana.

Alilia sana, aliamini kwamba alikuwa akifanya kila kitu kwa ajili ya kumsaidia msichana huyo lakini mwisho wa siku akawatuma watu wamteke na kumfungia ndani ya chumba hicho.

Japokuwa alilia sana lakini hakuachwa. Baada ya kumwangalia na kumsikiliza alivyokuwa akipiga kelele, Kudra akachukua kisu kile kutoka kwenye jiko na kukaa kitandani.

“Ili usizungumze ni lazima tufanye hili kwanza, tunaanza miguuni, tunapanda juu mpaka mapajani, mwisho wa siku tunamalizia kwenye kizazi chako, cha muhimu ni kutuambia kwamba utasema kile tunachohitaji wewe kusema mahakamani,” alisema Kudra.

“Nitasemaaaaaaa...” alisema Amina huku akitetemeka.
“Unatudanganya, kwanza acha tucheze huu mchezo unaoitwa burn burn,” alisema Kudra, hapohapo akakichukua kisu kile kilichokuwa kimeunguzwa mpaka kuwa chekundu na kumuwekea Amina kwenye mguu wake wa kulia kwenye nyama za nyuma ya mguu.

Amina akapiga kelele za maumivu, kisu kilimuunguza kupita kawaida, Kudra hakutaka kuacha, alihakikisha kwamba pindi watakapomwachia msichana huyo mahali hapo basi aende kufanya kile walichotaka akifanye.

Kama alivyomwambia ndivyo alivyofanya, akaanza kupanda juu, kila hatua alikuwa akimuunguza mno. Kisu kilipokuwa kikipoa, kilirudishwa kwenye jiko, wakawa wanapiga stori, kilipopata moto akakichukua na kumuunguza msichana huyo mpaka kwenye paja hali iliyompa maumivu makali Amina kiasi kwamba akahisi kama Kudra alikuwa ameukata mguu wake.

Unajua nini kiliendelea?
 
Kuna binti yangu nilimzaa WAKATI wa balehe anaitwa Linda!! Haki ya Nani naenda mbadilisha jina hata akaitwe Namshitu! Huyu Ni Linda wa nne mwenye roho mbaya namsikia
 
Kuna binti yangu nilimzaa WAKATI wa balehe anaitwa Linda!! Haki ya Nani naenda mbadilisha jina hata akaitwe Namshitu! Huyu Ni Linda wa nne mwenye roho mbaya namsikia
Muite "NANGATHU" au "NAKIVONA"
 
SEHEMU YA 86

Amina alikuwa kwenye maumivu makali, mapaja yake yaliunguzwa kwa kisu kile kilichokuwa cha moto, alilia sana, aliomba msamaha na msaada lakini hakukuwa na mtu aliyemsikiliza.

Moyo wake uliumia, aliendelea kujuta kwa kile kilichokuwa kimetokea, hakuamini kama kushirikiana na Linda kucheza mchezo ule mchafu ungemfanya kuwa mahali hapo akipokea mateso makali namna hiyo.

Mashavu yake yalilowanishwa na machozi, alijua kwamba angeonewa huruma na kuachwa lakini wanaume wale ndiyo kwanza waliendelea kumtesa zaidi kiasi kwamba akahisi dunia chungu.

Walimuuliza maswali mengi juu ya kile kilichokuwa kikiendelea mahakamani, walimwambia wazi kwamba hawakutaka kusikia akikataa kuwa hakubakwa, alitakiwa kuzungumza uongo na kukubaliana na mahakama kama alibakwa kitu ambacho alikubaliana nao kwa asilimia mia moja.

“Nimekubali, nitafanya mnavyotaka,” alisema Amina, alikuwa hoi, hata sauti aliyokuwa akiitumia aliongea kwa chini sana.
“Na ukitugeuka, tutakuleta tena ndani ya hiki chumba na kukumaliza kabisa, huwezi kucheza na akili zetu,” alisema Kudra.

Amina akafunguliwa kamba alizokuwa amefungwa na kutolewa nje ambapo akapakizwa ndani ya gari na kuanza kurudishwa nyumbani.

Njiani, alikuwa akiambiwa kwamba ilikuwa ni lazima azungumze kile walichomtaka kuzungumza kwani vinginevyo kama wangerudi kwa mara ya pili wasingekuwa na huruma naye hata kidogo.

Amina akakubaliana nao, alipofikishwa nyumbani, akateremshwa na kuelekea pembeni, akakaa na kuanza kuugulia maumivu makali ya mapaja yake.
Pale chini alipokuwa alikuwa akilia kama mtoto, alishindwa kutembea vizuri kwani kwa jinsi mapaja yake yalivyokuwa yameunguzwa ilikuwa ni balaa.

Kwa waliokuwa wakimfahamu wakamfuata na kumuuliza kilichokuwa kikiendelea, hakutaka kuufumbua mdomo wake na kuwaambia kilichotokea kwani alihisi kabisa kitu ambacho kingefuata ni kutekwa na kuuawa kama alivyoambiwa.
Hapo nje, akabebwa na kupelekwa ndani, alipoingia tu, simu yake ikaanza kuita, akaichukua na kuangalia kioo, namba ya Linda ilikuwa ikionekana.
 
SEHEMU YA 87

Moyo wake ulichukia, hasira zikampanda, hakuamini kama msichana huyo angempigia simu tena kwani kwa njama alizokuwa amezifanya ziliubadilisha moyo wake kabisa na kuona kwamba Linda hakuwa msichana mwenye huruma kama vile alivyokuwa akihisi hapo mwanzo.

Akaanza kuzungumza naye, msichana huyo alimwambia kwa kile alichokipata kutoka kwa vijana wake kilikuwa kama trela na picha lenyewe lingekuja baada ya kusema mahakamani kwamba hakubakwa.

Moyo wake ulimchoma mno, hakutaka kuona akitoa ushahidi wa uongo mahakamani lakini kutokana na vitisho vikali alivyokuwa akipewa vilimfanya kuwa na hofu na kuona kabisa kwamba mauti ilikuwa ikimjia mbele yake.

“Dada Linda, nitafanya unachokitaka,” alisema Amina huku akionekana kuwa na hofu.
“Na usipofanya! Yaani ndiyo nitakuonyeshea sura yangu ya kishetani inafananaje,” alisema Linda kwa sauti iliyokuwa na hasira tele.

*** Wazazi wa Dickson hawakuamini baada ya kuona kwamba mtu aliyefungua kesi ile mahakamani dhidi ya mtoto wao alikuwa msichana Linda. Walimfahamu msichana huyo, alikuwa mpenzi wa mtoto wao ambaye kila siku alionekana kuwa na shauku ya kuolewa na kijana wao.

Hawakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea nyuma ya pazia. Walijaribu kumpigia simu kwa lengo la kuzungumza naye ili kama ikiwezekana basi afute kesi ile mahakamani lakini msichana huyo hakuwa akipokea.

Hilo liliendelea kuwatia wasiwasi kwamba kijana wao alikuwa akienda kufungwa. Wao kama wazazi walikuwa wakifanya kazi kwa nafasi yao, walimtafuta sana msichana huyo kwenye simu na hata kwenda nyumbani kwao mara kwa mara lakini huko napo hawakubahatika kuonana naye.

Kesi ile iliwatia tumbo joto, walikaa kama na mzee Gwamaka na kukubaliana kuwa hawakutakiwa kumwambia ukweli Nandy kwa kuwa angeumia sana hasa baada ya kuambiwa kwamba mpenzi wake alisimama mahakamani kwa kuwa alikuwa amebaka.

Waliendelea kumfariji msichana huyo kitandani alipokuwa. Alikonda mno, alionekana kukosa tumaini, hakuwa na uhakika wa kupona na alijiona kabisa akiendelea kuteseka kitandani hapo kwa maisha yake yote duniani.
 
SEHEMU YA 88

Marafiki zake, washirika wengine walikuwa wakimtembelea pale kitandani alipokuwa, kila mtu aliyekuwa akimwangalia, alimuonea huruma, Nandy huyu hakuwa yule wa zamani, mrembo, mwenye sauti kali ya kumuimbia Mungu.

Alibadilika, alifanana na mtu aliyekuwa akiumwa Ukimwi. Watu waliokuwa wakimuona walimfariji na kumwambia kwamba Mungu angemponya na kusimama tena kitu ambacho kwake kilionekana kuwa kigumu kufanyika kwa kuwa tu alilala kitandani kwa muda mrefu.

“Unaamini kwamba Mungu ni mponyaji?” aliuliza mchungaji Tumaini huku akimwangalia nandy.
“Ninaamini mchungaji!”
“Kwa moyo wako mmoja?”
“Nilifundishwa kumwamini Mungu tangu utotoni, katika maisha yangu yote ninamuamini Mungu kwamba ni mponyaji mchungaji,” alisema Nandy.
“Basi atakwenda kukupona kitandani hapa!”

“Naamini mtumishi wa Mungu!”
Huo ulikuwa mwezi wa tatu tangu alale kitandani, moyo wake ulikata tamaa na wakati mwingine kuhisi kama Mungu alimuacha ateseke kitandani pale kwa kuwa alijiingiza kwenye maisha ya dhambi.
Hakuacha kumlilia mpenzi wake, Dickson, alijua dhahiri kwamba kulikuwa na kitu kibaya kilichokuwa kikiendelea ambacho hakutakiwa kukijua.

“Baba!” alimuita baba yake.
“Naam binti yangu!”
“Unaweza kunisaidia kitu kimoja?”
“Kipi hicho?”
“Unaweza kuniambia ukweli wako wote?”
“Ndiyo binti yangu, siwezi kukudanganya!”

“Dickson yupo wapi? Kwa nini yupo mahakamani? Ana kesi gani?” aliuliza Nandy huku akimwangalia baba yake, mzee Gwamaka.

Hilo lilikuwa swali gumu kujibika, mzee huyo akanyamaza na kuangalia chini. Walikubaliana kwamba hawakutakiwa kumwambia Nandy ukweli juu ya kilichokuwa kikiendelea.

Nandy hakunyamaza, alimwambia baba yake kwamba alihitaji kuujua ukweli kwani alichoka kusubiri na mbaya zaidi kila mtu aliyekuwa akimuuliza hakuonekana kuwa tayari kumjibu.
“Amefungwa?” aliuliza Nandy.
“Hapana!”

“Sasa yupo wapi? Au ameniacha tena ili nife?” aliuliza.
“Hapana binti yangu! Dickson hawezi kukuacha!”
“Sasa yupo wapi?”

“Atakuja!”
“Najua! Yupo wapi kwa sasa?” aliendelea kuuliza.
Maswali hayo aliyokuwa akiyauliza yakaanza kumliza kitandani pale. Alihisi kitu chenye ncha kali kikiuchoma moyo wake. Alimkumbuka Dickson, kwake, mwanaume huyo alikuwa kila kitu.
 
Linda pumbafu Sana anasababisha watu kupata maumivu bila hatia,,, Mkwe ahsante tena mama
 
Kuna binti yangu nilimzaa WAKATI wa balehe anaitwa Linda!! Haki ya Nani naenda mbadilisha jina hata akaitwe Namshitu! Huyu Ni Linda wa nne mwenye roho mbaya namsikia
Ahahahhhh
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom