Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,175
- Thread starter
- #321
SEHEMU YA 81
Linda alizaliwa katika familia ya kitajiri, wazazi wake walikuwa na pesa nyingi na ndiyo maana elimu zake zote alichukulia nje ya nchi barani Ulaya na Marekani.
Mbali na pesa za baba yake, naye alikuwa mfanyabiashara mzuri tu, maisha yake yalizungukwa na pesa na kila alipokuwa ni lugha ya pesa tu ndiyo aliyokuwa akiizungumza.
Alikuwa na kila kitu alichokuwa akikihitaji, wakati mwingine aliona kwamba alikuwa na uwezo wa kupata kila kitu kwa kuwa alikuwa na pesa. Aliamini kwamba unapokuwa na pesa unaweza kupata mapenzi ya dhati, unapokuwa na pesa unabadilisha hata chuki kuwa penzi na ndiyo maana alimuihitaji sana Dickson.
Kutumia pesa kwa vijana wale kwa kazi aliyotaka kuifanya hakukuwa na tatizo, alihitaji furaha ya milele, alihitaji kujiona akitabasamu mbele ya kioo na kitu pekee alichoamini kwamba kingempa tabasamu hilo hakikuwa kingine bali pesa.
Vijana hao baada ya kutumiwa pesa hawakutaka kubaki walipokuwa, wakaambiwa mahali alipokuwa akiishi Amina na kuanza kuelekea huko. Hakukuwa na tatizo kumpata, wasifu wake kwamba alikuwa na wowowo kubwa, mzuri wa sura, mweupe vilikuwa vitu vilivyowapa uhakika wa kumpata kwa urahisi kabisa.
Wakaondoka mpaka Manzese Midizini walipokuwa wameelekezwa, walifika mpaka nje ya nyumba ya akina Amina ambapo kulikuwa na duka na kujifanya kununua kitu huku wakimuulizia Amina kwa muuza duka huyo.
“Amina yupo?” aliuliza jamaa mmoja aliyeitwa Kudra.
“Ametoka sasa hivi!”
“Amekwenda wapi tena?” aliuliza.
“Sijui! Alikuja jamaa yake, akamchukua na kuondoka naye, kurudi nadhani ni usiku,” alijibu muuza duka.
“Poa haina noma.”
Kwa kuwa walipata uhakika kwamba msichana huyo angerudi usiku hawakutaka kuwa na hofu, wakaondoka na kuwasiliana na Linda na kumwambia kile walichoambiwa na muuza duka.
Hakukuwa na tatizo lolote lile, akawaambia kwamba wafanye kila liwezekanalo na mwisho wa siku msichana huyo apatikane kwani kama angefika mahakamani huku akiwa hajapewa mkwara wowote ule ilikuwa ni lazima aseme ukweli kwamba hakubakwa.
Linda alizaliwa katika familia ya kitajiri, wazazi wake walikuwa na pesa nyingi na ndiyo maana elimu zake zote alichukulia nje ya nchi barani Ulaya na Marekani.
Mbali na pesa za baba yake, naye alikuwa mfanyabiashara mzuri tu, maisha yake yalizungukwa na pesa na kila alipokuwa ni lugha ya pesa tu ndiyo aliyokuwa akiizungumza.
Alikuwa na kila kitu alichokuwa akikihitaji, wakati mwingine aliona kwamba alikuwa na uwezo wa kupata kila kitu kwa kuwa alikuwa na pesa. Aliamini kwamba unapokuwa na pesa unaweza kupata mapenzi ya dhati, unapokuwa na pesa unabadilisha hata chuki kuwa penzi na ndiyo maana alimuihitaji sana Dickson.
Kutumia pesa kwa vijana wale kwa kazi aliyotaka kuifanya hakukuwa na tatizo, alihitaji furaha ya milele, alihitaji kujiona akitabasamu mbele ya kioo na kitu pekee alichoamini kwamba kingempa tabasamu hilo hakikuwa kingine bali pesa.
Vijana hao baada ya kutumiwa pesa hawakutaka kubaki walipokuwa, wakaambiwa mahali alipokuwa akiishi Amina na kuanza kuelekea huko. Hakukuwa na tatizo kumpata, wasifu wake kwamba alikuwa na wowowo kubwa, mzuri wa sura, mweupe vilikuwa vitu vilivyowapa uhakika wa kumpata kwa urahisi kabisa.
Wakaondoka mpaka Manzese Midizini walipokuwa wameelekezwa, walifika mpaka nje ya nyumba ya akina Amina ambapo kulikuwa na duka na kujifanya kununua kitu huku wakimuulizia Amina kwa muuza duka huyo.
“Amina yupo?” aliuliza jamaa mmoja aliyeitwa Kudra.
“Ametoka sasa hivi!”
“Amekwenda wapi tena?” aliuliza.
“Sijui! Alikuja jamaa yake, akamchukua na kuondoka naye, kurudi nadhani ni usiku,” alijibu muuza duka.
“Poa haina noma.”
Kwa kuwa walipata uhakika kwamba msichana huyo angerudi usiku hawakutaka kuwa na hofu, wakaondoka na kuwasiliana na Linda na kumwambia kile walichoambiwa na muuza duka.
Hakukuwa na tatizo lolote lile, akawaambia kwamba wafanye kila liwezekanalo na mwisho wa siku msichana huyo apatikane kwani kama angefika mahakamani huku akiwa hajapewa mkwara wowote ule ilikuwa ni lazima aseme ukweli kwamba hakubakwa.