Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

SEHEMU YA 105

Dickson na Nandy walikuwa wakirudi jijini Dar es Salaam wakitoka katika Visiwa vya Zanzibar ambapo walikwenda kwa ajili ya fungate yao.
Mioyoni walikuwa na furaha tele kwani baada ya kupitia vikwazo mbalimbali hatimaye wawili hao walikuwa wameoana na kuwa pamoja.

Ndani ya boti kila mtu alikuwa akiwaangalia, hawakuamini kama watu hao ndiyo walikuwa wameoana huku mwanaume waliyekuwa wakimwangalia, aliyekuwa na sura nzuri ndiye aliyeamua kumuoa mpenzi wake huyo huku akiwa amepooza.

Walionekana kuwa na furaha kupita kawaida, mule ndani walikuwa wakizungumza mambo mengi na watu wengine, hawakusita kuwaambia kuhusu muujiza wa Mungu ambao angeufanya baadaye katika mwili wa Nandy.

Kila mtu aliiona imani yao, hawakutaka kuwa na hofu na kitu chochote kile kwani kwa kila kilichokuwa kikiendelea waliamini kwamba ulikuwa ni mtihani tu ambao mwisho wa siku kulikuwa na matokeo yake.

Walipofika Dar es Salaam, wakapokelewa na ndugu, jamaa na marafiki na kuelekea nyumbani. Maisha kama wanandoa yakaanza, kila siku Dickson alikuwa akienda kazini alipokuwa akisimamia biashara nyingi za baba yake na kurudi jioni.

Mapenzi yalikuwa motomoto, kila alipokuwa akirudi nyumbani alikuwa na zawadi kwa ajili ya mke wake huyo ambaye mpaka katika kipindi hicho hakukuwa na maendeleo yoyote mwilini mwake zaidi ya kuwa vilevile kama alivyokuwa kipindi cha nyuma.

Baada ya kukaa kwa siku kadhaa ndipo Dickson akapigiwa simu kutoka katika Kituo Kikuu cha Polisi na kuambiwa kwamba kulikuwa na mzigo wake kutoka gerezani.

Hakujua ulikuwa ni mzigo wa nini, hakujua alipelekewa na mtu gani. Muda huo aliopigiwa simu alikuwa akirudi nyumbani kwake, akakatisha safari, akakata kona na kuelekea huko.

Njiani alikuwa na mawazo mengi, alichanganyikiwa, alijitahidi kukumbuka kama kulikuwa na mtu aliyekuwa akimfahamu huko mpaka kutumiwa mzigo wake lakini hakukumbuka kitu chochote kile.
 
SEHEMU YA 106

Alipofika huko, akapewa bahasha ndogo ambapo kwa ndani kulikuwa na barua, hakutaka kufungulia hapo, akarudi kwenye gari, akaondoka, alipofika njiani kwenye foleni, akaifungua na kuanza kuisoma.

Ilitoka kwa Linda, msichana aliyekuwa amefungwa kifungo cha miaka sita gerezani. Dickson aliisoma barua ile, ilikuwa ni ya kugusa, iliyousisimua mwili wake, machozi yalishindwa kuzuilika, yakaanza kutiririka mashavuni mwake.
Maneno yaliyoandikwa katika barua ile ilimgusa kupita kawaida. Alipomaliza, akauegemea usukani na taa ziliporuhusu, akaondoka mahali hapo.

Alipofika nyumbani, kitendo cha Nandy kumuona tu akagundua kwamba kulikuwa na kitu, hakumzoea mume wake kuwa kwenye hali aliyokuwanayo, macho yake yalikuwa mekundu yaliyoonyesha ni kwa jinsi gani alikuwa amelia sana.
“Kuna nini mpenzi?” aliuliza Nandy kwa sauti ya chini.

Dickson hakujibu kitu, alichokifanya ni kuingiza mkono mfukoni na kumpa barua ile Nandy, akaipokea na kuanza kuisoma kwa umakini. Barua ile iliandikwa hivi...
Kwako Dickson.

Ninaomba msamaha kwa kila kitu kilichotokea baina yangu na yako. Ninaamini kwamba ni shetani ndiye aliyekuwa akiniendesha pasipo kujua kwamba hakukuwa na kitu kilichokuwa kikitesa duniani kama kumlazimisha mtu anayekupenda akupende.

Ninakuomba msamaha kwa hayo yote, kwa kuulazimisha moyo wake unipende msichana ambaye sikua chaguo lako, ninakuomba msamaha kwa hatua niliyochukua kwa kukusingizia kubaka, ni kitu ambacho kinaniumiza moyoni mpaka leo hii. Dickson, ninaomba msamaha sana.
Nandy anaendeleaje? Ni msichana mwenye sura nzuri ambaye ananijia kichwani mwangu kila siku, ni msichana ambaye ninakiri kwamba anastahili kuwa mke wako maisha yako yote.

Dickson, ninaomba uzungumze na Nandy, ninaomba umwambie anisamehe kwa kila kitu kilichotokea. Bila mimi, bila upumbavu wangu, bila wivu wangu wa kijinga leo hii Nandy angekuwa anatembea.

Niliumia nilipoona umenikataa, nikaamua kuchukua uamuzi mgumu wa kuyaondoa maisha ya msichana huyo. Ajali aliyoipata, haikuwa ya bahati mbaya, ilikuwa ni ajali ya kupangwa ambayo nilitaka niyaondoe maisha yake.
 
SEHEMU YA 107

Dickson! Moyo wangu unauma, ninajiona kuishi katika dunia ya peke yangu, ninajiona kuishi jehanamu kwenye maumivu makali ya nafsi yangu.
Ninajuta! Kwa kila kitu nilichokufanyia wewe na Nandy, ninastahili adhabu yoyote, hata kama nitauawa, ninastahili kwa kuwasababishia maisha mliyokuwanayo sasa hivi.

Dickson! Ninahitaji msamaha wako niwe na amani! Najua siwezi kubadilisha kitu chochote kile, najua siwezi kumpa afya Nandy, ila pamoja na hayo, ninahitaji msamaha wenu, ninahitaji muupoze moyo wangu kwa kunisamehe kwani najiona nina msalaba wa dhambi kichwani mwangu, nimechoka, ninahitaji muutue kwa kunisamehe tu.

Nimehukumiwa miaka sita gerezani, ni michache, kwa yale niliyowafanyia ninastahili hata kuhukumiwa kifo, Dickson! Ninahitaji msamaha wenu, ninahitaji kusamehewa japokuwa kwa yale niliyowafanyia inawezekana hayastahili kupokea msamaha wenu.
Ni mimi, Linda!

Mpaka anamaliza kuisoma barua ile, machozi yalikuwa yakimtoka Nandy, hakuamini kama Linda ndiye aliyemfanya kuwa kitandani akiteseka. Akamuita Dickson, akamsogelea na kumwambia amkumbatie, Dickson akafanya hivyo.

“Dickson! Pamoja na mateso ninayopata, pamoja na maisha yote ninayopitia, kwa moyo wangu mmoja, NIMEMSAMEHE LINDA!” alisema Nandy huku uso wake ukiwa kwenye tabasamu na machozi yakitiririka mashavuni mwake.
“Kweli?”

“Mungu ametufundisha kuhusu kusamehe! Yesu aliwasamehe watu waliomtesa, walimchoma mkuki, walimzomea na kumtemea mate na kumuua, mimi ni nani mpaka nissisamehe! Dickson, kama bado hujamsamehe Linda, naomba umsamehe ili awe na amani,” alisema nandy huku akiwa amekumbatiwa na mpenzi wake.

Dickson akamwambia wazi kwamba naye pia alimsamehe, hakuishia hapo tu, naye akamwandikia barua na kumwambia kuhusu msamaha, kwamba hawakuwa na kinyongo chochote kile.

Kwa kile alichokifanya Linda si kumkomoa Nandy bali alimsaidia kwani kipindi alichokuwa akipata ajali, Nandy alikuwa akienda kujiua, kwa maana hiyo, kama asingepata ajali hiyo kipindi hicho angekuwa marehemu.

Hayo ndiyo yaliyoendelea. Mungu aliwapa muda mrefu wa kusubiri, Nandy aliendelea kukaa kitandani kwa miaka mitatu mfululizo ndipo mabadiliko yakaanza kuonekana mwilini mwake.
 
SEHEMU YA 108

Kitu cha kwanza kabisa kufanya kazi kilikuwa ni vidole vyake vya miguu, vilianza kuchezacheza. Alishtuka, hakuamini, akamuita dada wa kazi na kumwambia ampigie simu Dickson.
“Mwambie vidole viecheza,” alisema huku akionekana kutokuamini.
“Unasemaje dada? Vidole vimecheza?” aliuliza dada wa kazi huku akionekana kutokuamini.

“Ndiyo! Mpigie simu kumwambia aje,” alisema Nandy.
Hayo yalikuwa ni mabadiliko ya mwanzo, yakaendelea kutokea zaidi na zaidi, baada ya wiki mbili, Mungu akazidi kufanya miujiza mwilini mwake, akaendelea kuonyesha nguvu zake kwa kupitia imani ambayo alijiwekea msichana huyo.

Kuanzia kiunoni kushuka chini kukaanza kufanya kazi, ilikuwa ni furaha tele kwa msichana huyo. Pale kitandani alipokuwa alikuwa akimuimbia Mungu matendo makuu aliyokuwa akiyafanya mwilini mwake.
Alitamani kuinuka na kurukaruka, kwa kilichokuwa kikiendelea mwilini mwake hakuamini na baada ya miezi miwili, Nandy akapona kabisa.

Kilichokuwa kimemponya hakikuwa uwezo wa madaktari, kilichomponya hakikuwa ujanja wake wala kitu chochote zaidi ya imani yake na nguvu ya msamaha aliyokuwanayo moyoni mwake.

“Nitayazungumzia matendo ya Mungu maishani mwangu,” alisema Nandy huku akiwa amesimama mbele ya kanisa, alishika kinasa sauti huku machozi yakimbubujika.
Alikonda sana, hakujali, kitu pekee alichokuwanacho kichwani mwake ni kwamba aliponywa ugonjwa uliokuwa ukimsumbua kwa miaka mingi.

Mume wake alikuwa pembeni yake, kila alipomwangalia, alimuona mwanaume shujaa aliyekuwa tayari kufanya lolote lile kwa ajili yake.
Hapohapo kanisani, akamsogelea na kumkumbatia, akaliambia kanisa kwamba miongoni mwa watu waliopata bahati ya kuwa na mume jasiri, aliyejua kupenda, alikuwa yeye.

“Ni imani ndiyo iliyoniponya,” alisema kila alipokuwa akiulizwa. Hakuacha kulia kwa furaha, kila alipokuwa akiyakumbuka matendo makuu ya Mungu, alibaki akimsifu tu.

MWISHO.

Nashukuru sana kwa kuifuatilia hadithi hii ambayo naamini imewafundisha mambo mengi tu. Kwa yale mazuri, yachukueni ila kwa yale mabaya naomba muyaache. Ahsanteni sana kwa kunifuatilia. Love you all.
 
Ahsante shunie daaa hadithi inamafunzo mengi mnoo
Kumwomba mungu bila kuchoka
Kuwa mvumilivu
Kusamehe
Kuwa na ujasiri/imani
Kuacha michepuko kuacha Tamara,kuridhika
Kuwa na upendo
Kuwa makini wakati wakufanya maamuzi

N.k

Story nzuri mnooo kwa kweli nimeipenda.

Keep it up
Shunie
 
Ahsante shunie daaa hadithi inamafunzo mengi mnoo
Kumwomba mungu bila kuchoka
Kuwa mvumilivu
Kusamehe
Kuwa na ujasiri/imani
Kuacha michepuko kuacha Tamara,kuridhika
Kuwa na upendo
Kuwa makini wakati wakufanya maamuzi

N.k

Story nzuri mnooo kwa kweli nimeipenda.

Keep it up
Shunie
Asante mpenzi inafundisha mno na kuelimisha
 
Mkwe hujawahi kiniangusha mpnz, na sema ahsante sana kwa msisitizo nasema NAHAVACHE MCHEKU [emoji23][emoji23][emoji23]
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom