Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

SEHEMU YA 89

Hakuambiwa kitu chochote kile, maumivu yale yaliyokuwa moyoni mwake yaliendelea kubaki vilevile. Dickson aliyekuwa akimuendesha kwenye kiti chake, hakuwepo tena, kazi hiyo alikuwa akiifanya baba yake
Siku zikakatika mpaka kufikia siku ya kesi hiyo kusikilizwa mahakamani kwa upande wa shahidi.

Wazazi wa Dickson walikwenda mahakamani kama kawaida.
Walipoingia katika viunga vya mahakama, macho yao yalitua kwa Linda ambaye naye alifika kwa ajili ya kusikiliza kilichokuwa kikiendelea.

Alikuwa na Amina, muda mwingi alimkumbusha kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wake endapo tu asingezungumza kile walichokuwa wamekubaliana na mbaya zaidi Kudra na mwenzake walikuwa mahakamani hapo ili kama angekwenda kupingana nao, basi wangeondoka naye na kwenda kumuua.

Siku hizo Linda alionekana kuwa tofauti, hakuwa kama yule msichana ambaye walikuwa wakimfahamu kutokana na upole wake, katika siku hizo alibadilika na kuwa mtu mwingine kabisa.
Muda mwingi alionekana kuwa na hasira na alidhamiria kumfunga Dickson gerezani kwa sababu tu alikataa kukubaliana naye kuoana na wakati alikuwa akimpenda kwa moyo wa dhati.

Baada ya dakika kadhaa basi kubwa kutoka magereza likafika mahali hapo na moja kwa moja watuhumiwa ambao siku hiyo walikuwa wakisomewa kesi zao kuanza kuteremka, na miongoni mwa watuhumiwa hao alikuwemo Dickson.

Alionekana kuwa mnyonge, mikononi alikuwa na pingu, alipoteremshwa, macho yake yakaanza kuangalia huku na kule, kwa mbali aliwaona wazazi wake, alitamani kuwafuata na kuwauliza kuhusu hali aliyokuwa akiendelea nayo mpenzi wake.

Alimkumbuka Nandy, kwake, kila siku msichana huyo alikuwa akizunguka kichwani mwake, alihitaji sana kumuona na kumjulia hali kwani aliamini kwamba kusingekuwa na mtu ambaye angemjali kama alivyokuwa akimjali kabla ya kukamatwa.

Baada ya kuingizwa mahakamani, haraka sana kesi zikaanza kusikilizwa na kesi ya kwanza kabisa ilikuwa yake kwa kuwa kilichokuwa kikihitajika ni ushahidi tu.
 
SEHEMU YA 90

Marafiki zake, washirika wengine walikuwa wakimtembelea pale kitandani alipokuwa, kila mtu aliyekuwa akimwangalia, alimuonea huruma, Nandy huyu hakuwa yule wa zamani, mrembo, mwenye sauti kali ya kumuimbia Mungu.

Alibadilika, alifanana na mtu aliyekuwa akiumwa Ukimwi. Watu waliokuwa wakimuona walimfariji na kumwambia kwamba Mungu angemponya na kusimama tena kitu ambacho kwake kilionekana kuwa kigumu kufanyika kwa kuwa tu alilala kitandani kwa muda mrefu.

“Unaamini kwamba Mungu ni mponyaji?” aliuliza mchungaji Tumaini huku akimwangalia nandy.
“Ninaamini mchungaji!”
“Kwa moyo wako mmoja?”
“Nilifundishwa kumwamini Mungu tangu utotoni, katika maisha yangu yote ninamuamini Mungu kwamba ni mponyaji mchungaji,” alisema Nandy.

“Basi atakwenda kukupona kitandani hapa!”
“Naamini mtumishi wa Mungu!”
Huo ulikuwa mwezi wa tatu tangu alale kitandani, moyo wake ulikata tamaa na wakati mwingine kuhisi kama Mungu alimuacha ateseke kitandani pale kwa kuwa alijiingiza kwenye maisha ya dhambi.

Hakuacha kumlilia mpenzi wake, Dickson, alijua dhahiri kwamba kulikuwa na kitu kibaya kilichokuwa kikiendelea ambacho hakutakiwa kukijua.
“Baba!” alimuita baba yake.
“Naam binti yangu!”
“Unaweza kunisaidia kitu kimoja?”
“Kipi hicho?”

“Unaweza kuniambia ukweli wako wote?”
“Ndiyo binti yangu, siwezi kukudanganya!”
“Dickson yupo wapi? Kwa nini yupo mahakamani? Ana kesi gani?” aliuliza Nandy huku akimwangalia baba yake, mzee Gwamaka.

Hilo lilikuwa swali gumu kujibika, mzee huyo akanyamaza na kuangalia chini. Walikubaliana kwamba hawakutakiwa kumwambia Nandy ukweli juu ya kilichokuwa kikiendelea.

Nandy hakunyamaza, alimwambia baba yake kwamba alihitaji kuujua ukweli kwani alichoka kusubiri na mbaya zaidi kila mtu aliyekuwa akimuuliza hakuonekana kuwa tayari kumjibu.
“Amefungwa?” aliuliza Nandy.
“Hapana!”

“Sasa yupo wapi? Au ameniacha tena ili nife?” aliuliza.
“Hapana binti yangu! Dickson hawezi kukuacha!”
“Sasa yupo wapi?”
“Atakuja!”
“Najua! Yupo wapi kwa sasa?” aliendelea kuuliza.

Maswali hayo aliyokuwa akiyauliza yakaanza kumliza kitandani pale. Alihisi kitu chenye ncha kali kikiuchoma moyo wake. Alimkumbuka Dickson, kwake, mwanaume huyo alikuwa kila kitu.
 
SEHEMU YA 90

Marafiki zake, washirika wengine walikuwa wakimtembelea pale kitandani alipokuwa, kila mtu aliyekuwa akimwangalia, alimuonea huruma, Nandy huyu hakuwa yule wa zamani, mrembo, mwenye sauti kali ya kumuimbia Mungu.

Alibadilika, alifanana na mtu aliyekuwa akiumwa Ukimwi. Watu waliokuwa wakimuona walimfariji na kumwambia kwamba Mungu angemponya na kusimama tena kitu ambacho kwake kilionekana kuwa kigumu kufanyika kwa kuwa tu alilala kitandani kwa muda mrefu.

“Unaamini kwamba Mungu ni mponyaji?” aliuliza mchungaji Tumaini huku akimwangalia nandy.
“Ninaamini mchungaji!”
“Kwa moyo wako mmoja?”
“Nilifundishwa kumwamini Mungu tangu utotoni, katika maisha yangu yote ninamuamini Mungu kwamba ni mponyaji mchungaji,” alisema Nandy.

“Basi atakwenda kukupona kitandani hapa!”
“Naamini mtumishi wa Mungu!”
Huo ulikuwa mwezi wa tatu tangu alale kitandani, moyo wake ulikata tamaa na wakati mwingine kuhisi kama Mungu alimuacha ateseke kitandani pale kwa kuwa alijiingiza kwenye maisha ya dhambi.

Hakuacha kumlilia mpenzi wake, Dickson, alijua dhahiri kwamba kulikuwa na kitu kibaya kilichokuwa kikiendelea ambacho hakutakiwa kukijua.
“Baba!” alimuita baba yake.
“Naam binti yangu!”
“Unaweza kunisaidia kitu kimoja?”
“Kipi hicho?”

“Unaweza kuniambia ukweli wako wote?”
“Ndiyo binti yangu, siwezi kukudanganya!”
“Dickson yupo wapi? Kwa nini yupo mahakamani? Ana kesi gani?” aliuliza Nandy huku akimwangalia baba yake, mzee Gwamaka.

Hilo lilikuwa swali gumu kujibika, mzee huyo akanyamaza na kuangalia chini. Walikubaliana kwamba hawakutakiwa kumwambia Nandy ukweli juu ya kilichokuwa kikiendelea.

Nandy hakunyamaza, alimwambia baba yake kwamba alihitaji kuujua ukweli kwani alichoka kusubiri na mbaya zaidi kila mtu aliyekuwa akimuuliza hakuonekana kuwa tayari kumjibu.
“Amefungwa?” aliuliza Nandy.
“Hapana!”

“Sasa yupo wapi? Au ameniacha tena ili nife?” aliuliza.
“Hapana binti yangu! Dickson hawezi kukuacha!”
“Sasa yupo wapi?”
“Atakuja!”
“Najua! Yupo wapi kwa sasa?” aliendelea kuuliza.

Maswali hayo aliyokuwa akiyauliza yakaanza kumliza kitandani pale. Alihisi kitu chenye ncha kali kikiuchoma moyo wake. Alimkumbuka Dickson, kwake, mwanaume huyo alikuwa kila kitu.

Shunie hii umeirudia..
 
SEHEMU YA 91

Baada ya jaji kuingia, akaanza kuisoma kesi hiyo tangu ilipoanzia na mpaka ilipofikia na kitu pekee kilichokuwa kikisubiriwa kwa hamu ni ushahidi juu ya ile video iliyokuwa ikionekana, na mtu pekee ambaye alitakiwa kutoa ushahidi ni yule msichana aliyekuwa akionekana kwenye video ile, Amina.

Jaji akapewa taarifa kwamba msichana huyo alikuwemo mahakamani na hivyo alitakiwa kwenda kizimbani na kusema ukweli juu ya kile kilichokuwa kimetokea.
Hilo halikuwa tatizo, kwa unyonge, Amina akainuka na kuanza kuelekea katika kizimba kile huku akichechemea hali iliyomfanya kila mmoja kujua kwamba alikuwa na maumivu katika miguu yake.

Alipofika, akasimama na kujitambulisha, akajiapiza huku akinyanyua mkono wake wa kulia huku katika mkono wake wa kushoto akiwa ameshika Kitabu Kitakatifu cha Kuran.
“Na Allah anisaidie,” alisema baada ya kumaliza kujiapiza.

Mahakama ilitakiwa kuzungumza kila kitu kilichotokea siku hiyo mpaka kubakwa na mtuhumiwa. Kabla ya kuanza kusimulia, Amina akayapeleka macho yake na kumwangalia Dickson.

Aliumia mno, mwanaume huyo alikuwa amepungua kupita kawaida, kwa kusoteshwa rumande amefanyiwa kisa tu kumuacha mwanamke ambaye aliamini hakuwa wa ndoto yake
Amina hakutaka kumuona Dickson akifungwa gerezani kwa kosa ambalo hakulifanya, japokuwa aliambiwa kwamba angeweza kuuawa lakini alikuwa radhi lakini si kuona mwanaume huyo akichukuliwa na kwenda kufungwa.
Alichokifanya ni kuanza kusimulia kila kitu kilichotokea, jinsi alivyokwenda hotelini kuonana na Dickson kisha kukubaliana kwenda chumbani na kuanza kufanya mapenzi.

Watu wote mahakamani walikuwa kimya, walimsikiliza msichana huyo alivyokuwa akisimulia huku akilia kwani hakupenda kabisa kumuona Dickson akifungwa, kama Kudra na mwenzake walitaka kumuua alikuwa tayari kufa.

“Hakunibaka! Nilifanya naye mapenzi kwa hiyari yangu. Niliambiwa nijifanye kama nakataa, kwa mara ya kwanza sikujua maana ya mtu aliyenituma lakini baadaye nikagundua kwamba aliniambia nifanye vile kwa kuwa ilitakiwa nionekana kwamba nabakwa,” alisema Amina, kila mmoja alikuwa kimya, akaendelea:
 
SEHEMU YA 92

“Baadaye ndiyo nikaambiwa jinsi hali ilivyokuwa, nilishangaa, nilimwambia mtu huyo kwamba sikuwa tayari kwa kuwa nilikuwa nampenda Dickson lakini akanilazimisha sana, akahisi kwamba nisingezungumza kile alichotaka nizungumze hivyo akatuma watu waniteke na kunitesa, nikaunguzwa na kisu cha moto,” alisema Amina, hiyo haikutosha, akaanza kuonyesha majeraha yake mapajani. Wanawake waliokuwa humo wakaanza kutokwa na machozi, kwa jinsi Amina alivyokuwa amejeruhiwa kulimuumiza kila mtu.

“Nilionywa kwamba kama nisingesema kwamba nimebakwa basi ningeuawa! Hakimu, watu hao wapo hapa, ninatoa ushahidi na wanasikia na ninategemea baada ya hapa wanakwenda kuniua kama walivyoniahidi,” alisema Amina, watu wote humo ndani kuanza kuangalia.
“Unaweza kuwaonyesha watu wenyewe?” aliuliza jaji.

“Ndiyo!” alisema Amina na kuwanyooshea vidole Amina na vijana wake wawili, polisi wakawasogelea watu hao, akaendelea:
“Kiukweli sikubakwa, sikubakwa kabisa. Kama ningekuwa nimedhalilishwa kingono namna hiyo, ningekuwa muwazi, ila sikubakwa bali nilitumika kwa manufaa ya msichana huyo aliyetaka kuona yeye akiolewa na Dickson,” alisema Amina na kunyamaza.

Ndani ni kama kulikuwa na msiba, watu walishindwa kuvumilia, walikuwa wakimwangalia Amina, hawakuamini kuona msichana huyo akiwa amepitia mateso makubwa kiasi hicho.
Jaji mwenyewe kule alipokaa alishindwa kuvumilia, machozi yakaanza kujaa machoni mwake na kuanza kutiririka mashavuni kwani kile alichokisikia kilimuumiza mno.

Hakutaka kuchelewa, akamuita polisi mmoja ambapo akaambiwa kwamba ilikuwa ni lazima kwa watu hao watatu kukamatwa kwa makosa waliyokuwa wameyafanya, yaani yule shahidi aliyekuwa ameletwa mahali pale, alitoa ushahidi wake lakini wa kuwaingiza watu hao matatizoni.

Alipomaliza, kesi ikaendelea kwa jaji kuanza kuipitia tangu mwanzo ilipoanza mpaka hapo ilipoishia na kilichokuwa kimebaki kilikuwa kimoja tu, kutolewa hukumu ya kesi hiyo.

“Kama tulivyomsikia shahidi ambaye alikuwa na nguvu kwenye hitimisho ya kesi hii, hakubakwa, na sasa sioni ni kwa namna gani naweza kuendelea na hii kesi. Kwa mamlaka ya mahakama, ninamuachia huru ndugu Dickson kwa kuwa mahakama haikumkuta na hatia yoyote ile,” alisema hakimu na kui
 
SEHEMU YA 93

“Baadaye ndiyo nikaambiwa jinsi hali ilivyokuwa, nilishangaa, nilimwambia mtu huyo kwamba sikuwa tayari kwa kuwa nilikuwa nampenda Dickson lakini akanilazimisha sana, akahisi kwamba nisingezungumza kile alichotaka nizungumze hivyo akatuma watu waniteke na kunitesa, nikaunguzwa na kisu cha moto,” alisema Amina, hiyo haikutosha, akaanza kuonyesha majeraha yake mapajani. Wanawake waliokuwa humo wakaanza kutokwa na machozi, kwa jinsi Amina alivyokuwa amejeruhiwa kulimuumiza kila mtu.

“Nilionywa kwamba kama nisingesema kwamba nimebakwa basi ningeuawa! Hakimu, watu hao wapo hapa, ninatoa ushahidi na wanasikia na ninategemea baada ya hapa wanakwenda kuniua kama walivyoniahidi,” alisema Amina, watu wote humo ndani kuanza kuangalia.
“Unaweza kuwaonyesha watu wenyewe?” aliuliza jaji.

“Ndiyo!” alisema Amina na kuwanyooshea vidole Amina na vijana wake wawili, polisi wakawasogelea watu hao, akaendelea:
“Kiukweli sikubakwa, sikubakwa kabisa. Kama ningekuwa nimedhalilishwa kingono namna hiyo, ningekuwa muwazi, ila sikubakwa bali nilitumika kwa manufaa ya msichana huyo aliyetaka kuona yeye akiolewa na Dickson,” alisema Amina na kunyamaza.

Ndani ni kama kulikuwa na msiba, watu walishindwa kuvumilia, walikuwa wakimwangalia Amina, hawakuamini kuona msichana huyo akiwa amepitia mateso makubwa kiasi hicho.
Jaji mwenyewe kule alipokaa alishindwa kuvumilia, machozi yakaanza kujaa machoni mwake na kuanza kutiririka mashavuni kwani kile alichokisikia kilimuumiza mno.

Hakutaka kuchelewa, akamuita polisi mmoja ambapo akaambiwa kwamba ilikuwa ni lazima kwa watu hao watatu kukamatwa kwa makosa waliyokuwa wameyafanya, yaani yule shahidi aliyekuwa ameletwa mahali pale, alitoa ushahidi wake lakini wa kuwaingiza watu hao matatizoni.

Alipomaliza, kesi ikaendelea kwa jaji kuanza kuipitia tangu mwanzo ilipoanza mpaka hapo ilipoishia na kilichokuwa kimebaki kilikuwa kimoja tu, kutolewa hukumu ya kesi hiyo.

“Kama tulivyomsikia shahidi ambaye alikuwa na nguvu kwenye hitimisho ya kesi hii, hakubakwa, na sasa sioni ni kwa namna gani naweza kuendelea na hii kesi. Kwa mamlaka ya mahakama, ninamuachia huru ndugu Dickson kwa kuwa mahakama haikumkuta na hatia yoyote ile,” alisema hakimu na kui
 
SEHEMU YA 94

Dickson hakutaka kubaki mahali hapo, kulikuwa na kitu kimoja tu alichohitaji kukifahamu muda huo nacho kilikuwa ni afya ya mpenzi wake ambaye alimuacha kitandani kwa muda wa wiki kadhaa.

Akawachukua wazazi wake, wakapanda ndani ya gari na kuanza kuelekea nyumbani. Njiani walikuwa wakizungumza naye mambo mengi lakini mawazo yake yalikuwa kwa Nandy tu, alihitaji kumuona msichana huyo, kwake, hakukuwa na kitu chochote kile kilichokuwa na thamani zaidi ya huyo Nandy.

Walipofika, wakateremka, wakakuta geti likiwa wazi, walishangaa, wakaingia ndani, hakukuwa na mtu, mbaya zaidi hata mlinzi hakuwa mahali hapo.
Dickson akaufungua mlango na kuingia ndani, moja kwa moja akaelekea katika chumba alichokuwemo Nandy, hakuwemo humo, kitanda kilikuwa kitupu.

“Nandy! Nandy amekufa,” alisema huku akilishika shuka la kile kitanda alichokuwa amelalia Nandy.
Alichokifanya ni kuanza kuita, akaita na kuita, alichanganyikiwa, si yeye tu bali hata wazazi wake nao walichanganyikiwa. Walipotoka nje, wakakutana na mlinzi ambaye alikuwa amerudi nyumbani hapo huku akiwa anahema kwa nguvu kama mtu aliyetoka kukimbia mbio ndefu.

“Cosmas...kuna nini? Nandy yupo wapi?” aliuliza Dickson, tayari moyo wake ulikuwa na hofu kupita kawaida.
“Nandy? Nandy?” aliuliza mlinzi, kila alipotaka kuzungumza, mdomo ulikuwa mzito kufunguka.

Je, nini kimetokea?
 
SEHEMU YA 95

Nandy hakuwa na furaha hata kidogo, bado kichwa chake kilikuwa kikimfikiria mpenzi wake, Dickson ambaye muda huo hakuwa akijua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
Alitulia kwenye kitanda kile, alikuwa mtu wa kulala tu, hakuweza kuusogeza mwili wake kivyovyote vile, kama alivyokuwa kipindi cha nyuma ndivyo alivyokuwa mpaka kipindi hicho.

Baba yake ndiye aliyekuwa na majukumu ya kila kitu, ndiye aliyekuwa akimtoa kitandani hapo na kumgeuza, ndiye aliyekuwa akimlisha na kumfanyia mambo mengine.

Dickson, mwanaume wake wa dhati hakuwepo nyumbani na kitu pekee alichokuwa akikihitaji kipindi hicho ni kumuona tena mbele ya macho yake.
Baada ya kukaa kwa siku kadhaa, pale kitandani akaanza kujisikia vibaya, siku hiyo hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, kwa mara ya kwanza maumivu makali yakawa yanaupata mgongo wake.

Akaanza kupiga kelele za kuhitaji msaada, alikuwa akiumia kupita kawaida na pale kitandani mwili ukawa kama unapanda na kushuka.
Sauti yake ilisikika na mlinzi aliyekuwa getini, haraka sana akaelekea chumbani, hali aliyoikuta ilimuogopesha, kwa jinsi msichana huyo alivyokuwa kitandani pale ilionyesha kwamba alikuwa katika siku yake ya mwisho kuvuta pumzi ya dunia hii.

Mlinzi hakujua afanye nini kumsaidia zaidi ya kumpigia simu mzee Gwamaka ambaye akafika mahali hapo haraka sana.
“Vipi?” aliuliza mzee huyo, bado Nandy alikuwa kwenye hali ileile.
“Sijui nini kimetokea! Nimemkuta akiwa hivi, Mungu wangu! Anakufa?” aliuliza mlinzi huyo huku akitetemeka.

Nandy akaanza kutapika, mwisho kabisa mapovu yakaanza kumtoka. Alitisha kitandani pale na muda wowote ule alionekana kukata roho.
Mzee Gwamaka huku akiwa amechanganyikiwa akamnyanyua, akamtoa nje, mlinzi akaita Bajaj, ilipokuja, wakamuingiza ndani na kuanza kuondoka naye kuelekea hospitali.

Walipofika, machela ikaletwa, akapokelewa na kisha kuanza kusukumwa kuelekea ndani. Huko, akalazwa na kuanza kupewa huduma ya kwanza kabla ya matibabu kamili kuanza.
 
SEHEMU YA 96

Mzee gwamaka na mlinzi walikuwa nje kwenye benchi, kila mmoja alionekana kuwa na hofu na kuhisi kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wa Nandy kuendelea kuishi.

Pale walipokuwa, mzee Gwamaka aliikutanisha mikono yake na kuanza kumuomba Mungu, hakutaka kushuhudia mtoto wake akifa kitandani, alimuomba Mungu kwamba amponye kwa kuwa asingekuwa na mtu yeyote katika maisha yake.

“Mungu! Naomba usimchukue Nandy, nitabaki na nani mimi ukimchukua? Ni kweli anateseka, lakini naomba usimchukue, ninampenda sana binti yangu,” alisali mzee Gwamaka huku akiangalia juu.

Machozi ya uchungu yakaanza kumtoka kiasi kwamba hata mlinzi alimuonea huruma kwa kile kilichokuwa kikiendelea.
Wakati wakiendelea kuwa mahali hapo, mlinzi akakumbuka kwamba hakuwa amelifunga geti kwa ufunguo hicyo alitakiwa kurudi nyumbani na kulifunga. Akamuaga mzee Gwamaka na kurudi nyumbani huku akikimbia.

Huko ndipo alipokutana na Dickson pamoja na wazazi wake, alishangaa, hakuamini kama mwanaume huyo angetoka huko alipokuwa, alipoulizwa mahali alipokuwa Nandy, kwanza akatulia.
“Niambie! Nandy amekufa? Mbona hujibu, niambie Cosmas,” alisema Dickson huku akianza kutokwa na machozi.

Akawaambia kilichotokea, Dickson aliposikia, hakutaka kubaki mahali hapo tena, akatoka na kuanza kukimbia kuelekea hospitalini ambapo hakukuwa mbali kutoka mahali hapo.

Njiani, kichwa chake kilikuwa kikimfikiria msichana huyo tu, alikuwa tayari kupoteza kitu chochote katika maisha yake lakini si kumpoteza Nandy ambaye alikuwa mtu muhimu kupita kawaida.
Alimpoteza kwa mara ya kwanza, kilichotaka kutokea kilikuwa ni kumpoteza kwa mara ya pili tena milele kitu ambacho Dickson hakutaka kukubaliana nacho hata kidogo.

Hakuchukua dakika nyingi akafika katika hospitali hiyo, watu walikuwa wakimshangaa, alikuwa akitoka jasho huku akihema kama mbwa aliyekimbia mbio ndefu, akamkuta mzee Gwamaka akiwa amejiinamia kwenye benchi.

“Baba! Baba...niambie nini kinaendelea!” alisema Dickson huku akiwa amemsogelea mzee huyo ambapo baada ya kunyanyua uso, akashangaa kumuona Dickson.
“Dickson!”

“Baba! Niambie nini kinaendelea! Nandy anaendeleaje?” aliuliza.
“Ndiyo namsubiri daktari!”
 
SEHEMU YA 97

Dickson akatulia kwenye benchi, akaungana na mzee huyo kwenye dimbwi la mawazo, walikaa hapo kwa dakika kama arobaini ndipo mlango ukafunguliwa na daktari mmoja kutoka ambapo akawaambia awafuate ofisini kwake.

“Ila anaendeleaje?” aliuliza Dickson aliyekuwa na presha ya kutaka kufahamu kilichokuwa kikiendelea.
“Twendeni ofisini kwanza!”
“Amekufa?”
“Mtayajua huko!”

Dickson ndiye aliyekuwa na presha kubwa ya kutaka kufahamu kilichokuwa kikiendelea kwa mpenzi wake, baada ya mwendo mdogo, wakafika katika ofisi hiyo na kukaa katika viti.

“Huyu binti yako amepooza, si ndiyo?” alianza kwa kuuliza daktari.
“Ndiyo!”
“Ooh! Pole sana. Tumemchunguza kwa makini na kugundua kwamba ana tatizo liitwalo Sciatica,” alisema daktari.
“Ndiyo nini hilo?”

“Hili ni tatizo linalotokea kwenye uti wa mgongo wakati pingili za uti zimekuwa zimefinywa kwa kipindi kirefu. Hapo kuna sehemu kwenye uti wa mgongo inaitwa Lumbar stenosis ambayo hiyo huchukua mawasiliano kutoka sehemu moja ya uti wa mgongo na kupeleka sehemu nyingine,” alisema daktari.

“Dokta! Hayo majina unatuchanganya, hebu tuambie moja kwa moja, nini kinaendelea,” alisema Dickson.
“Ni kwamba mgonjwa wenu amepata tatizo la kwenye pingili, hii imesababishwa na kulala kwa kipindi kirefu, anatakiwa wakati mwingine ageuzwe na hata kukalishwa,” alisema.
“Lakini tunafanya hivyo!” alisema mzee Gwamaka.

“Basi mnafanya kidogo sana. Kwa siku, muacheni akae kitako hata kwa saa nne, si saa nyingi awe amelala tu,” alisema.
“Lakini atapona?”
“Uti wa mgongo au hili tatizo aliloletewa hapa?”
“Tatizo hili!”

“Hili linapona! Hakuna tatizo!”
“Na uti wa mgongo kwa ujumla?”
“Bado kwa kweli! Nimeangalia pingili zake, aisee inaweza kuchukua miaka na miaka,” alisema daktari huyo bila kuwaficha chochote kile.

Daktari aliwaambia mambo mengi kuhusu ugonjwa wa Nandy lakini mwisho wa siku akawaeleza ukweli kwamba msichana huyo asingeweza kupona tena.
 
SEHEMU YA 98

Hilo liliwauma lakini hawakuwa na la kufanya. Baada ya saa moja, daktari akawachukua na kuwapeleka katika chumba alicholazwa Nandy. Walipoingia na Nandy kuwaona, uso wake ukajawa na tabasamu pana, hakuamini kama kweli mpenzi wake angekuwa uraiani kama alivyomuona.

Dickson akatembea haraka kumfuata Nandy pale kitandani, alipomfikia, akamuinamia na kumbusu shavuni huku kila mmoja akionekana kuwa na furaha.
Siku hiyo alilala hospitalini hapo, usiku walikuwa wakiongea mambo mengi, walifurahishana huku Dickson akimwambia Nandy kwamba kuna siku angeweza kusimama tena na kukimbia kama zamani.

“Hivi ulikwishawahi kusoma stori ya Musa?” aliuliza Dickson.
“Nimesoma sana mpaka mapigo saba ambayo Mungu aliipiga Misri,” alijibu Nandy.
“Na ulisoma jinsi Waisrael walivyofika katika bahari ile Nyekundu?” aliuliza.
“Ndiyo!”
“Kuna muujiza gani Mungu aliufanya kupitia Musa?”

“Aliigawa bahari na Waisrael wakavuka katikati. Unamaanisha nini?”
“Ninamaanisha kwamba Mungu wetu tunayemuabudu ni mkuu, Mungu wetu ni Muweza, hakuna mtu au roho yoyote ile ambayo itashindana na Mungu aliye hai.

Unaposikia Mungu, jua unamzungumzia Mungu mwenye miujiza, Mungu asiyeshindwa, asiyesinzia wala kulala, Mungu ambaye anaweza kuifinyanga dunia na kuitupilia mbali ndani ya sekunde moja tu,” alisema Dickson.
“Kweli kabisa.”
 
SEHEMU YA 99

“Kama Mungu amefanya hayo yote, yeye ni nani mpaka ashindwe kuunganisha uti wako wa mgongo?” aliuliza Dickson.

“Hashindwi! Na hatowahi kushindwa!”
“Nandy! Unachotakiwa ni kufanya kitu kimoja tu, unatakiwa kuamini, Mungu huwa hashindwi, kuna watu wanaponywa Ukimwi, kuna watu wanafufuliwa, kuna watu wanaponywa magonjwa hatari kama kansa, huyo ndiye Mungu ambaye ninakwambia usiku wa leo kwamba hashindwi na hajawahi kushindwa, yeye anajua mfumo mzima wa mwili wako, damu inatoka wapi, inakwenda wapi na anajua vitu kwenye mwili wako ambavyo hata madaktari hawavijui, hebu jaribu kufikiria ni Mungu wa aina gani huyo,” alisema Dickson huku machozi yakimlenga, alipokuwa akizungumzia matendo makuu ya Mungu, alihisi nafsi yake ikielekea katika sehemu nyingine kabisa, sehemu yenye raha, amani, sehemu yenye tumaini, hali ambayo hakuwahi kukutana nayo katika maisha yake.

“Amen! Mungu ataniponya.”
“Mungu hajawahi kushindwa. Kuna siku Nandy utasimama kwa miguu yako na kumwambia kila mtu kwamba Mungu hajawahi kushindwa!” alisema.
“Amen!”
“Mungu hajawahi kushindwa!”
“Amen!”
“Mungu hajawahi kushindwa!”
“Amen”
“Utasimama kwa miguu yako na kuiambia dunia kwamba MUNGU HAJAWAHI KUSHINDWA.”

“Amen!” alisema Nandy kwa sauti juu iliyokuwa na imani kubwa katika maisha yake kwamba Mungu huyo aliyeigawanya bahari Nyekundu, hakuwahi kushindwa.
“Kuna siku utasimama!”
“Naamini! Kuna siku nitasimama tena, nitamuimbia Mungu na kucheza mbele yake! Ninaamini hilo,” alisema Nandy kwa ushujaa mkubwa.

Je, nini kitaendelea
 
SEHEMU YA 100

Moyo wa Dickson haukuacha kuuma, alimwambia Nandy kuhusu kumuamini Mungu kwa kila kilichokuwa kikiendelea kwamba kuna siku angepona kabisa na kutembea kama ilivyokuwa zamani.

Msichana huyo akaamini, hakuona kama Mungu angeweza kushindwa kitu chochote kile, katika maisha yake, hakukuwa na mtu au kitu alichokiamini zaidi ya Mungu.

Pale kitandani walipomaliza kuzungumza maneno kuhusu nguvu za Mungu, wakashikana mikono na kuanza kusali huku wakimpa shukrani Mungu kwa kile ambacho waliamini kuwa angekwenda kukifanya baada ya siku chache.

“Mungu! Tunakushukuru kwa kila kitu tulichokuwanacho, tunashukuru kwa haya maisha, tunashukuru kwa baraka hizi, tunashukuru kwa zile baraka ambazo bado hazijafika mikononi mwetu, tunashukuru kwa kila kitu, pia tunashukuru kwa uponyaji unaokwenda kumpa Nandy katika siku chache zijazo,” alisali Dickson huku akiwa ameshikana mkono na msichana huyo.

Maisha yaliendelea kama kawaida, kila siku Dickson alikuwa ndani ya chumba hicho, yeye ndiye aliyekuwa na kazi ya kumuogesha, kumbadilisha nguo, kumtembeza huku na kule kwenye kibaskeli chake na kumfanyia kila kitu ambacho alitakiwa kufanyiwa.

Kila ilipofika siku ya Jumapili, Dickson ndiye aliyekuwa akimwandaa msichana huyo na kuelekea kanisani. Huko, huku akiwa kitandani bado Nandy aliendelea kumuimbia Mungu.

Kila mtu aliyekuwa akimwangalia, alimshangaa, alibadilika, alikonda kupita kawaida, katika maisha yake, kitu ambacho alikuwa akikitegemea ni kwamba siku moja angepona na kutembea kama zamani.

Watu walimuombea, walimuomba Mungu kufanya uponyaji katika kitanda kile lakini bado Nandy aliendelea kuwa katika hali ileile.
Baada ya miezi minne mingine, mchungaji kutoka nchini Marekani, Richard Turnbull akafika nchini Tanzania na kuandaa mkutano mkubwa wa Injili.

Hiyo ikaonekana kuwa nafasi nyingine ya Mungu kufanya miujiza kwani miongoni mwa wachungaji waliokuwa na nguvu kutoka kwa Mungu alikuwa mchungaji huyo.

Kila alipokuwa akiandaa mikutano, wagonjwa waliponywa, viwete walitembea, viziwi walisikia na miujiza mingine mingi.
 
SEHEMU YA 101

Dickson akamchukua Nandy na kuanza kushiriki naye katika mkutano huo huku akiwa kwenye kiti chake. Wakati wagonjwa walipotwa na kuombewa, naye Nandy akataka kwenda kuombewa, lakini kitu cha ajabu ambacho kilimshtua ni kwamba Dickson hakutaka kumpeleka.
“Nipeleke nikaombewe,” alisema Nandy huku akimwangalia Dickson.

“Hapana! Moyo wangu unakuwa mzito!”
“Kwa nini? Ninataka kupona, Dickson, naomba unipeleke nikaombewe,” alisema Nandy huku akimwangalia Dickson, kwake, hiyo ndiyo ilikuwa nafasi yake ya kipekee ya kupokea uponyaji.

Bado Dickson alikuwa akikataa, Nandy alilia lakini hakutaka kulazimisha, hakutaka kumkasirisha Dickson, mpaka mkutano unaisha siku hiyo na kurudi nyumbani, Nandy hakuonekana kuwa kwenye hali ya kawaida.

Hiyo ilikuwa siku ya kwanza, siku ya pili ya mkutano ikaingia, hali ilikuwa vilevile, siku ya tatu na mpaka mkutano unaisha katika siku ya saba bado Dickson hakutaka kumpeleka Nandy kwenda kuombewa zaidi ya kukaa na kusikiliza Neno la Mungu.

Wakarudi nyumbani, Dickson alijua kwamba Nandy alikuwa amekasirika, alijua kwamba aliumia ila kitu alichokifanya ni kumchukua na kumpeleka nje, akaanza kumuendesha katika kibaskeli chake mpaka ufukweni ambapo hakukuwa mbali na walipokuwa wakiishi.

“Nandy! Kuna kitu ninataka kuzungumza nawe,” alisema Dickson huku akimwangalia Nandy.
“Kitu gani?”
“Niliisikia sauti ikiniambia moyoni mwangu kwamba sikutakiwa kukupeleka pale mbele katika mkutano na kuombewa. Nina uhakika ilikuwa ni sauti ya Mungu, ilisikika kwa upole mno moyoni mwangu tofauti na sauti nyingine, ila ilikuwa na nguvu ya ajabu,” alisema Dickson huku akimwangalia Nandy.
“Ilisemaje?”

“Iliniambia mengi, cha msingi kabisa ni kwamba Mungu anataka kupandikiza nguvu ya imani mioyoni mwetu. Kwa jinsi tulivyomuomba, tunatakiwa kumwamini kwamba atatenda muujiza, si mpaka mchungaji wa kimataifa amtumie kufanya miujiza, hata sisi pia tunaweza kufanya miujiza,” alisema Dickson huku uso wake ukiwa kwenye tabasamu pana.
“Nina imani, kuna siku atafanya muujiza,” alisema Nandy.

“Ila kuna kingine!”
“Kipi?”
 
SEHEMU YA 102

“Nandy! Wewe ni msichana wa kipekee, katika maisha yangu nimefikiria jambo moja muhimu, ninahitaji unipe nafasi moja tu,” alisema Dickson.
“Ipi?”
“Ya kuwa mume wako!”
“Unataka kunioa?”
“Ndiyo!”
“Mimi?”

“Nandy! Kwani wewe una nini?”
“Mimi ni mgonjwa, siwezi kufanya lolote lile!”
“Umesahau nilichokwambia kuhusu imani?”
“Nakumbuka!”
“Basi kumbuka kwamba wewe si mgonjwa tena, kuna siku utainuka na kuishangaza dunia,” alisema Dickson huku akimwangalia mpenzi wake huyo.

Kwa furaha Dickson akamkumbatia Nandy na kurudi nyumbani huku wakizungumza mambo mengi yaliyokuwa yakiendelea katika maisha yao.
Dickson hakutaka kubaki na jambo hilo moyoni mwake, alichokifanya ni kuwaambia wazazi wake kwamba alidhamiria kumwambia kuhusu mpenzi wake huy.

Wazazi wake waliposikia, hawakuamini lakini kwa yote hawakumzuia kijana wao kumuoa Nandy kwa kuwa kila walipokuwa wakimwangalia, alionekana kuwa na mapenzi ya dhati kwa mpenzi wake huyo.
Hakuishia kuwaambia wazazi wake tu bali alimwambia mpaka mzee Gwamaka kile kilichokuwa kikiendelea. Mzee huyo hakuamini, kwake ilionekana kama ndoto kwani pamoja na Dickson kumpenda mno binti yake bado hakutakiwa kumuoa kwa kuwa alikuwa kwenye hali ile.

Akamwambia kijana huyo ukweli kuhusu binti yake, hilo halikuwa tatizo kwa Dickson, hata kama mpenzi wake alikuwa kwenye hali hiyo, alikuwa radhi kumuoa lakini si kuona akiondoka tena mikononi mwao.

“Nitamuoa, hata kama hatorudi katika hali yake maisha yote bado nitahitaji kumuoa,” alisema Dickson huku akimwangalia mzee Gwamaka.
Huo ulikuwa uamuzi wake, hakutaka mtu yeyote amuingilie, alichokifanya ni kumwambia mchungaji, naye alishangazwa lakini hakuwa na jinsi.

Akatangaza kanisani, na baada ya miezi miwili, watu hao wakaoana huku Nandy akiwepo kwenye kiti, akavarishwa pete na hatimaye kuwa mume na mke.
Moyo wa Dickson ukaridhika, kwake hakuangalia afya, kwake hakuangalia watoto, kitu ambacho alikiangalia kwake ni upendo wa dhati kwa msichana huyo.
 
SEHEMU YA 103

Kila alipokuwa akimwangalia, hakuacha kumwambia kwamba alikuwa akimpenda kupita kawaida. Baada ya shere ya harusi kumalizika, wakaondoka na kuelekea Zanzibar kwa ajili ya kula fungate.

Ndoa aliyofunga na Nandy ikawa gumzo Tanzania nzima, hakukuwa na mtu aliyeamini kama kweli mwanaume huyo aliyekuwa na sura nzuri aliamua kufunga ndoa na msichana aliyekuwa kitandani huku akiwa amepooza.

Wanaume wengi wakatakiwa kujifunza, kwenye mapenzi, hukutakiwa kuangalia afya, kwenye mapenzi hukutakiwa kuangala watoto, kila kitu kilipangwa na Mungu kwani kulikuwa na watu wengi waliokuwa na afya, watoto lakini bado mioyo yao iliumizwa kila siku, bado macho yao yalitoa machozi na kutiririka mashavuni mwao kila siku.

“Jamani huyu kaka ana moyo wa chuma,” alisema msichana mmoja huku akiwaonyeshea gazeti wenzake.
“Mmh! Amemuoa mwanamke amepooza?”
“Ndiyo! Yaani hatofanya naye mapenzi, hatomzalia, lakini kidume kimeoa hivyohivyo,” alisema msichana huyo.
“Mmh!”

“Yaani nyie acheni. Ila mkaka yupo bomba, handsome la maana, huyu ukimpata hata kazini huendi, kumwangalia tu chumbani inatosha kujisikia umelipwa mshahara,” alisema msichana huyo.
“Hahaha!” wote wakabaki wakicheka.
 
SEHEMU YA 104

Kesi ilikuwa ngumu kwa Linda, mahakamani pale kesi ile iliendelea kila ilipokuwa wiki na hatimaye yeye na wenzake wakakutwa na kesi ya kujibu na hivyo hukumu ilipotoka, wakafungwa gerezani miaka sita kwa kosa la kutaka kuua kwa kukusudia.

Hiyo ilimuuma mno Linda, hakuamini kama msichana mrembo kama yeye, mwenye elimu yake, kutoka katika familia ya kitajiri alikuwa akienda gerezani.

Hilo lilimuuma kupita kawaida, aliondolewa mahakamani huku akilia, wazazi wake ambao walikuwa wakifuatilia kesi hiyo tangu mwanzo mpaka ilipomalizika, hawakuamini kama mahakama ingetoa hukumu hiyo ambayo kwao ilionekana kuwa kubwa kupita kawaida.

Linda akaanza maisha ya gerezani, alikosa penzi, akakosa kila kitu kizuri na mwisho wa siku kujikuta akiwa gerezani.
Moyo wake ulichoma mno na baada ya miezi kadhaa akiwa huko, akapata nafasi ya kusoma gazeti na kuiona habari iliyokuwa imetawala katika magazeti mengi kwamba mwanaume mwenye sura nzuri, mtoto wa kitajiri aliamua kumuoa mwanamke aliyekuwa kitandani amepooza.

Moyo wake uliumia. Kilichomuumiza si Dickson kumuoa Nandy bali kilichomuumiza ni kuona msichana Nandy akiwa kitandani kwa ujinga aliokuwa ameufanya.

Akajikuta akisikia hukumu nzito moyoni mwake, hakutaka kuona akiendelea kuumia kiasi kile bali alichokifanya ni kuchukua karatasi na kutaka kuwaandikia barua wawili hao, alihitaji kukiri kusababisha maisha ya msichana huyo kuwa kitandani lakini pia alihitaji kuwaomba msamaha kwa kila kitu kilichotokea. Baada ya dakika kadhaa, akapata kalamu na karatasi na kuanza kuandika barua hiyo kwenda kwa watu hao.

Je, nini kitaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom