Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,175
- Thread starter
- #341
SEHEMU YA 89
Hakuambiwa kitu chochote kile, maumivu yale yaliyokuwa moyoni mwake yaliendelea kubaki vilevile. Dickson aliyekuwa akimuendesha kwenye kiti chake, hakuwepo tena, kazi hiyo alikuwa akiifanya baba yake
Siku zikakatika mpaka kufikia siku ya kesi hiyo kusikilizwa mahakamani kwa upande wa shahidi.
Wazazi wa Dickson walikwenda mahakamani kama kawaida.
Walipoingia katika viunga vya mahakama, macho yao yalitua kwa Linda ambaye naye alifika kwa ajili ya kusikiliza kilichokuwa kikiendelea.
Alikuwa na Amina, muda mwingi alimkumbusha kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wake endapo tu asingezungumza kile walichokuwa wamekubaliana na mbaya zaidi Kudra na mwenzake walikuwa mahakamani hapo ili kama angekwenda kupingana nao, basi wangeondoka naye na kwenda kumuua.
Siku hizo Linda alionekana kuwa tofauti, hakuwa kama yule msichana ambaye walikuwa wakimfahamu kutokana na upole wake, katika siku hizo alibadilika na kuwa mtu mwingine kabisa.
Muda mwingi alionekana kuwa na hasira na alidhamiria kumfunga Dickson gerezani kwa sababu tu alikataa kukubaliana naye kuoana na wakati alikuwa akimpenda kwa moyo wa dhati.
Baada ya dakika kadhaa basi kubwa kutoka magereza likafika mahali hapo na moja kwa moja watuhumiwa ambao siku hiyo walikuwa wakisomewa kesi zao kuanza kuteremka, na miongoni mwa watuhumiwa hao alikuwemo Dickson.
Alionekana kuwa mnyonge, mikononi alikuwa na pingu, alipoteremshwa, macho yake yakaanza kuangalia huku na kule, kwa mbali aliwaona wazazi wake, alitamani kuwafuata na kuwauliza kuhusu hali aliyokuwa akiendelea nayo mpenzi wake.
Alimkumbuka Nandy, kwake, kila siku msichana huyo alikuwa akizunguka kichwani mwake, alihitaji sana kumuona na kumjulia hali kwani aliamini kwamba kusingekuwa na mtu ambaye angemjali kama alivyokuwa akimjali kabla ya kukamatwa.
Baada ya kuingizwa mahakamani, haraka sana kesi zikaanza kusikilizwa na kesi ya kwanza kabisa ilikuwa yake kwa kuwa kilichokuwa kikihitajika ni ushahidi tu.
Hakuambiwa kitu chochote kile, maumivu yale yaliyokuwa moyoni mwake yaliendelea kubaki vilevile. Dickson aliyekuwa akimuendesha kwenye kiti chake, hakuwepo tena, kazi hiyo alikuwa akiifanya baba yake
Siku zikakatika mpaka kufikia siku ya kesi hiyo kusikilizwa mahakamani kwa upande wa shahidi.
Wazazi wa Dickson walikwenda mahakamani kama kawaida.
Walipoingia katika viunga vya mahakama, macho yao yalitua kwa Linda ambaye naye alifika kwa ajili ya kusikiliza kilichokuwa kikiendelea.
Alikuwa na Amina, muda mwingi alimkumbusha kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wake endapo tu asingezungumza kile walichokuwa wamekubaliana na mbaya zaidi Kudra na mwenzake walikuwa mahakamani hapo ili kama angekwenda kupingana nao, basi wangeondoka naye na kwenda kumuua.
Siku hizo Linda alionekana kuwa tofauti, hakuwa kama yule msichana ambaye walikuwa wakimfahamu kutokana na upole wake, katika siku hizo alibadilika na kuwa mtu mwingine kabisa.
Muda mwingi alionekana kuwa na hasira na alidhamiria kumfunga Dickson gerezani kwa sababu tu alikataa kukubaliana naye kuoana na wakati alikuwa akimpenda kwa moyo wa dhati.
Baada ya dakika kadhaa basi kubwa kutoka magereza likafika mahali hapo na moja kwa moja watuhumiwa ambao siku hiyo walikuwa wakisomewa kesi zao kuanza kuteremka, na miongoni mwa watuhumiwa hao alikuwemo Dickson.
Alionekana kuwa mnyonge, mikononi alikuwa na pingu, alipoteremshwa, macho yake yakaanza kuangalia huku na kule, kwa mbali aliwaona wazazi wake, alitamani kuwafuata na kuwauliza kuhusu hali aliyokuwa akiendelea nayo mpenzi wake.
Alimkumbuka Nandy, kwake, kila siku msichana huyo alikuwa akizunguka kichwani mwake, alihitaji sana kumuona na kumjulia hali kwani aliamini kwamba kusingekuwa na mtu ambaye angemjali kama alivyokuwa akimjali kabla ya kukamatwa.
Baada ya kuingizwa mahakamani, haraka sana kesi zikaanza kusikilizwa na kesi ya kwanza kabisa ilikuwa yake kwa kuwa kilichokuwa kikihitajika ni ushahidi tu.