Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,186
- Thread starter
- #1,181
*MKUFU WA MALKIA WA GOSHEN II --- 17*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Aliuondoa tu mwili wake nyumbani kwa 'kina Roboth, ila akili na moyo wake aliviacha huko. Aliendelea kuvuja machozi akijiuliza juu ya hali ya mpenzi wake, na hata akijuta kwanini alimshutumu na kumdhania ubaya.
Moyo wake ukawa mzito. Kichwa chake kikawa kinagonga kama saa ya ukutani. Joto la mwili wake likapanda. Usipite muda mrefu, akadondoka chini!
Kwa mbali kichwani kwake akawa anasikia watu wakicheka na kuteta. Hakuwa anawajua watu hawa ni wakina nani. Hakuwa na nguvu ya kunyanyuka kabisa. Na kabla hajapotea kabisa kwenye ulimwengu wa kupoteza fahamu, kwa mbali akasikia sauti ya daktari:
"Hatakiwi kufanya kazi yoyote ngumu, bali apumzike kwa muda mrefu. Mwili wake bado unahitaji muda kurejea katika hali yake ya kawaida."
Na mara akazima asisikie chochote tena.
ENDELEA
"Dada!" Sauti iliita. "Tatty! Tatty!" Fanty alimtikisa Tattiana huku akimtazama kana kwamba anahisi amefariki.
Alikuwa amefanikiwa kumfikisha binti huyo nyumbani kitandani muda si mrefu. Na ni kama bahati tu, muda mchache nyuma baada ya kuona dada yake hajarejea ndani na wakati muda ukiwa umeenda, akaona kuna haja ya kwenda kumtafuta huko kwa 'kina Roboth kabla wazazi hawajarejea na kumweka kikaangoni.
Njiani akamwona akiwa amezingirwa na watu waliokuwa wamepigwa butwaa kumwona binti huyo akiwa amejilaza chini. Akiwa ametaharuki kwa hofu, akasogea na kuangaza. Shukrani ziende kwa macho yake ambayo yalifanikiwa kukumbuka gauni alilotoka nalo dadaye.
Akamweka mgongoni na safari ya kwenda nyumbani ikafanyika kwa haraka, Fanty asipumzike kabisa barabarani. Akikimbia na kutembea upesi.
'Vipi kama nikaonekana na mama au baba? Vipi kama Tatty atakuwa amefariki? Itakuaje wakifahamu ameenda kumwona tena Roboth?Na wakija kugundua nilimruhusu kutoka?'
Maswali hayo yakamkosesha Fanty raha kabisa. Alipofanikiwa kufika nyumbani, akahisi kana kwamba amefika mbinguni. Hakuamini kukuta nyumba tupu! Akamlaza Fanty kitandani na sasa akihangaika kumwasha kabla wazazi hawajafika.
"Kwanini lakini Tatty unafanya hivi?" Akalalama. Alikuwa na hasira na huruma kwa pamoja. Akapata wazo la kwenda kuteka maji na kuyatumia kumwamshia dada yake, hakufanikiwa. Punde akasikia sauti ya farasi huko nje. Haraka akatoka ndani ya chumba na kwenda kuwalaki wazazi wake.
"Mgonjwa anaendeleaje?" Lilikuwa swali la kwanza baada ya salamu.
"Anaae - yupo vizuri! Vizuri tu." Fanty akafumuka kujibu akilazimisha tabasamu. "Amepumzika sasa chumbani kwake muda si mrefu sana."
"Sawa sawa!" Melkizedek akatikisa kichwa. "Anatakiwa apumzike sana kurejesha afya yake.
Wakaingia ndani na kujipatia mlo wa jioni pamoja kama familia, Tattiana akiwa ndiye pekee aliyekosekana kutimiza orodha.
"Nadhani inabidi umwite aje kula, hawezi akalala na tumbo tupu," mama akapendekeza. Fanty akatikisa kichwa akisema:
"Hapana! Ashakula muda mfupi kabla hajapumzika. Hataweza kula tena kwa sasa!"
"Una uhakika amekula vema?" Melkizedek akauliza.
"Ndio," Fanty akajibu. "Amekula chakula cha kutosha - sahani mbili!"
Wakamaliza kula, lakini kabla ya kwenda kulala, mama akaona ni vema endapo wamgemwona mtoto kwanza. Akalipendekeza hilo kwa mumewe baada ya kumdaka mkono wakiwa koridoni kupita kwenda kujipumzisha chumbani.
"Amepumzika, huoni tutamsumbua?" Melkizedek akauliza akiwa anarembua macho kwa mzigo wa usingizi.
"Hapana!" Mama akatikisa kichwa. "Tutaendaje kulala kwa amani na hata hatujamtia machoni?"
Wakafungua mlango taratibu na kuingia ndani ya chumba cha binti yao. Wakasogea karibu na kumwangalia kwa matumaini. Tattiana alikuwa amelala na gauni lake akionekana kama mtu aliyelevyeshwa na usingizi mzito.
Mama alimtazama kwa mazingatio, lakini baba baada ya kumwona tu binti, hata macho yake yakaanza kufumba fumba kwa usingizi. Hakuwa na cha kuhofia.
"Twende sasa," akamwambia mkewe.
"Tangulia, nakuja," mama akashauri. Naye Melkizedek hakubisha, akageuza na kwenda zake akitembea kwa kishindo.
Alipofunga mlango, Mama akaweka mgongo wa kiganja chake cha mkono kwenye paji la uso la Tattiana. Akamtazama na gauni lake vema, akaondoa shaka, kweli lilikuwa lina udongo na vumbi.
Kama hatoshi, Tattiana hakuna na mkufu aliompatia walipoenda kumchukua hospitalini.
Akatazama ndani ya chumba pengine alikuwa ameuvua na kuuhifadhi, napo hakuuona. Akapata shaka. Akaketi na kufikiri. Akatoka ndani ya chumba na kwenda moja kwa moja jikoni, akatazama chungu kikubwa cha chakula na mboga.
Akagundua kiasi cha chakula kilichopo hakihakisi idadi ya walaji. 'Sahani mbili' za Tattiana na chakula walichokula wao kisingebakiza lumbesa la chakula chunguni.
Akatazama na matunda. Hayakuguswa zaidi ya yale waliyokula wao mezani. Mama akapata uhakika kuwa Tattiana hajala, lakini hakutaka kusumbua, akaenda zake chumbani, akaoga na kujilaza kitandani.
"Melky," akamuita mumewe, kisha akasema: "Kuna kitu nahisi hakipo sawa."
Kimya.
"Melky," Akaita tena. Akanyanyuka na kumtazama mumewe, alikuwa amejilalia na mdomo akiwa ameachama. Hakuwa kwenye ulimwengu huu kabisa bali sayari ya njozi asifahamu hata lepe ya lile linaloendelea ulimwenguni mwa binadamu.
Mama akaishia kusonya na kugeukia upande wa pili kulala.
***
Usiku ukazidi kuwa mzito.
Ndani ya kasri ya mfalme wa Goshen kulikuwa kimya na patulivu. Walinzi walikuwa wamesimama kiukakamavu malangoni wakiwa wamebebelea mikuki mirefu yenye vishungi vyekundu.
Macho yao yalikuwa yanawaka kama taa, yakikodoa kama bundi. Walikuwa wameingia lindoni muda si mrefu sana kuwapokea wenzao waliokesha hapo mchana kutwa.
Kama haitoshi, wengine walikuwa wakirandaranda huko nje, kwa miguu na kwa farasi, lakini vyote katika hali ya ukimya, wakihakikisha usalama upo wa kutosha, hakuna kitu kitakachomnyima mfalme usingizi.
Ndani ya chumba cha kuvutia cha mfalme, mfalme alikuwa mpweke kitandani. Alikuwa amelala akiwa ameukumbatia mto wake mkubwa uliodariziwa kwa nyuzi za dhahabu. Kitanda kilikuwa kikubwa kuwa peke yake, vilevile na chumba pia.
Kwa mbali ungeweza kusikia sauti yake akikoroma. Alikuwa amepotelea usingizini kabisa. Kazi za wakti wa mchana zilimchosha mwili na akili.
Lakini leo hii, ilikuwa ni siku yake ya yeye kupata ujumbe. Akiwa amelowea usingizini, kwa mbali akasikia sauti ya kike ikimnong'oneza. Kwa mara ya kwanza hakusikia vema, ila sauti ile ikarudia sentensi moja mara tatu.
"Mfalme, kuna walozi ndani ya himaya yako ... mfalme, kuna walozi ndani ya himaya yako ... mfalme, kuna walozi ndani ya himaya yako."
Sauti hiyo ikakoma kama sekunde nne kisha ikasema tena:
"Wanakumywa damu na kuwaua watu ... wanakunywa damu na kuwaua watu ... wanakunywa damu na kuwaua watu."
Mfalme akasikia vema sana. Lakini sauti ile ikaacha kunong'oneza, ikafoka:
"Amka! Nenda Kawatafute!"
Mfalme akakurupuka toka usingizini. Akiwa ametoa macho akakodoa kutazama kushoto na kulia akihema. Kwa mbali akasikia vishindo vya miguu vikipotelea!
Basi akanyanyuka, akafungua mlango wake na kutupa macho. Hakuona kitu! Akatoka ndani ya chumba na kwenda kutazama. Huku na kule, hakubahatika kuona chochote alichoshuku. Akarudi chumbani na kuketi kitandani.
***
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Aliuondoa tu mwili wake nyumbani kwa 'kina Roboth, ila akili na moyo wake aliviacha huko. Aliendelea kuvuja machozi akijiuliza juu ya hali ya mpenzi wake, na hata akijuta kwanini alimshutumu na kumdhania ubaya.
Moyo wake ukawa mzito. Kichwa chake kikawa kinagonga kama saa ya ukutani. Joto la mwili wake likapanda. Usipite muda mrefu, akadondoka chini!
Kwa mbali kichwani kwake akawa anasikia watu wakicheka na kuteta. Hakuwa anawajua watu hawa ni wakina nani. Hakuwa na nguvu ya kunyanyuka kabisa. Na kabla hajapotea kabisa kwenye ulimwengu wa kupoteza fahamu, kwa mbali akasikia sauti ya daktari:
"Hatakiwi kufanya kazi yoyote ngumu, bali apumzike kwa muda mrefu. Mwili wake bado unahitaji muda kurejea katika hali yake ya kawaida."
Na mara akazima asisikie chochote tena.
ENDELEA
"Dada!" Sauti iliita. "Tatty! Tatty!" Fanty alimtikisa Tattiana huku akimtazama kana kwamba anahisi amefariki.
Alikuwa amefanikiwa kumfikisha binti huyo nyumbani kitandani muda si mrefu. Na ni kama bahati tu, muda mchache nyuma baada ya kuona dada yake hajarejea ndani na wakati muda ukiwa umeenda, akaona kuna haja ya kwenda kumtafuta huko kwa 'kina Roboth kabla wazazi hawajarejea na kumweka kikaangoni.
Njiani akamwona akiwa amezingirwa na watu waliokuwa wamepigwa butwaa kumwona binti huyo akiwa amejilaza chini. Akiwa ametaharuki kwa hofu, akasogea na kuangaza. Shukrani ziende kwa macho yake ambayo yalifanikiwa kukumbuka gauni alilotoka nalo dadaye.
Akamweka mgongoni na safari ya kwenda nyumbani ikafanyika kwa haraka, Fanty asipumzike kabisa barabarani. Akikimbia na kutembea upesi.
'Vipi kama nikaonekana na mama au baba? Vipi kama Tatty atakuwa amefariki? Itakuaje wakifahamu ameenda kumwona tena Roboth?Na wakija kugundua nilimruhusu kutoka?'
Maswali hayo yakamkosesha Fanty raha kabisa. Alipofanikiwa kufika nyumbani, akahisi kana kwamba amefika mbinguni. Hakuamini kukuta nyumba tupu! Akamlaza Fanty kitandani na sasa akihangaika kumwasha kabla wazazi hawajafika.
"Kwanini lakini Tatty unafanya hivi?" Akalalama. Alikuwa na hasira na huruma kwa pamoja. Akapata wazo la kwenda kuteka maji na kuyatumia kumwamshia dada yake, hakufanikiwa. Punde akasikia sauti ya farasi huko nje. Haraka akatoka ndani ya chumba na kwenda kuwalaki wazazi wake.
"Mgonjwa anaendeleaje?" Lilikuwa swali la kwanza baada ya salamu.
"Anaae - yupo vizuri! Vizuri tu." Fanty akafumuka kujibu akilazimisha tabasamu. "Amepumzika sasa chumbani kwake muda si mrefu sana."
"Sawa sawa!" Melkizedek akatikisa kichwa. "Anatakiwa apumzike sana kurejesha afya yake.
Wakaingia ndani na kujipatia mlo wa jioni pamoja kama familia, Tattiana akiwa ndiye pekee aliyekosekana kutimiza orodha.
"Nadhani inabidi umwite aje kula, hawezi akalala na tumbo tupu," mama akapendekeza. Fanty akatikisa kichwa akisema:
"Hapana! Ashakula muda mfupi kabla hajapumzika. Hataweza kula tena kwa sasa!"
"Una uhakika amekula vema?" Melkizedek akauliza.
"Ndio," Fanty akajibu. "Amekula chakula cha kutosha - sahani mbili!"
Wakamaliza kula, lakini kabla ya kwenda kulala, mama akaona ni vema endapo wamgemwona mtoto kwanza. Akalipendekeza hilo kwa mumewe baada ya kumdaka mkono wakiwa koridoni kupita kwenda kujipumzisha chumbani.
"Amepumzika, huoni tutamsumbua?" Melkizedek akauliza akiwa anarembua macho kwa mzigo wa usingizi.
"Hapana!" Mama akatikisa kichwa. "Tutaendaje kulala kwa amani na hata hatujamtia machoni?"
Wakafungua mlango taratibu na kuingia ndani ya chumba cha binti yao. Wakasogea karibu na kumwangalia kwa matumaini. Tattiana alikuwa amelala na gauni lake akionekana kama mtu aliyelevyeshwa na usingizi mzito.
Mama alimtazama kwa mazingatio, lakini baba baada ya kumwona tu binti, hata macho yake yakaanza kufumba fumba kwa usingizi. Hakuwa na cha kuhofia.
"Twende sasa," akamwambia mkewe.
"Tangulia, nakuja," mama akashauri. Naye Melkizedek hakubisha, akageuza na kwenda zake akitembea kwa kishindo.
Alipofunga mlango, Mama akaweka mgongo wa kiganja chake cha mkono kwenye paji la uso la Tattiana. Akamtazama na gauni lake vema, akaondoa shaka, kweli lilikuwa lina udongo na vumbi.
Kama hatoshi, Tattiana hakuna na mkufu aliompatia walipoenda kumchukua hospitalini.
Akatazama ndani ya chumba pengine alikuwa ameuvua na kuuhifadhi, napo hakuuona. Akapata shaka. Akaketi na kufikiri. Akatoka ndani ya chumba na kwenda moja kwa moja jikoni, akatazama chungu kikubwa cha chakula na mboga.
Akagundua kiasi cha chakula kilichopo hakihakisi idadi ya walaji. 'Sahani mbili' za Tattiana na chakula walichokula wao kisingebakiza lumbesa la chakula chunguni.
Akatazama na matunda. Hayakuguswa zaidi ya yale waliyokula wao mezani. Mama akapata uhakika kuwa Tattiana hajala, lakini hakutaka kusumbua, akaenda zake chumbani, akaoga na kujilaza kitandani.
"Melky," akamuita mumewe, kisha akasema: "Kuna kitu nahisi hakipo sawa."
Kimya.
"Melky," Akaita tena. Akanyanyuka na kumtazama mumewe, alikuwa amejilalia na mdomo akiwa ameachama. Hakuwa kwenye ulimwengu huu kabisa bali sayari ya njozi asifahamu hata lepe ya lile linaloendelea ulimwenguni mwa binadamu.
Mama akaishia kusonya na kugeukia upande wa pili kulala.
***
Usiku ukazidi kuwa mzito.
Ndani ya kasri ya mfalme wa Goshen kulikuwa kimya na patulivu. Walinzi walikuwa wamesimama kiukakamavu malangoni wakiwa wamebebelea mikuki mirefu yenye vishungi vyekundu.
Macho yao yalikuwa yanawaka kama taa, yakikodoa kama bundi. Walikuwa wameingia lindoni muda si mrefu sana kuwapokea wenzao waliokesha hapo mchana kutwa.
Kama haitoshi, wengine walikuwa wakirandaranda huko nje, kwa miguu na kwa farasi, lakini vyote katika hali ya ukimya, wakihakikisha usalama upo wa kutosha, hakuna kitu kitakachomnyima mfalme usingizi.
Ndani ya chumba cha kuvutia cha mfalme, mfalme alikuwa mpweke kitandani. Alikuwa amelala akiwa ameukumbatia mto wake mkubwa uliodariziwa kwa nyuzi za dhahabu. Kitanda kilikuwa kikubwa kuwa peke yake, vilevile na chumba pia.
Kwa mbali ungeweza kusikia sauti yake akikoroma. Alikuwa amepotelea usingizini kabisa. Kazi za wakti wa mchana zilimchosha mwili na akili.
Lakini leo hii, ilikuwa ni siku yake ya yeye kupata ujumbe. Akiwa amelowea usingizini, kwa mbali akasikia sauti ya kike ikimnong'oneza. Kwa mara ya kwanza hakusikia vema, ila sauti ile ikarudia sentensi moja mara tatu.
"Mfalme, kuna walozi ndani ya himaya yako ... mfalme, kuna walozi ndani ya himaya yako ... mfalme, kuna walozi ndani ya himaya yako."
Sauti hiyo ikakoma kama sekunde nne kisha ikasema tena:
"Wanakumywa damu na kuwaua watu ... wanakunywa damu na kuwaua watu ... wanakunywa damu na kuwaua watu."
Mfalme akasikia vema sana. Lakini sauti ile ikaacha kunong'oneza, ikafoka:
"Amka! Nenda Kawatafute!"
Mfalme akakurupuka toka usingizini. Akiwa ametoa macho akakodoa kutazama kushoto na kulia akihema. Kwa mbali akasikia vishindo vya miguu vikipotelea!
Basi akanyanyuka, akafungua mlango wake na kutupa macho. Hakuona kitu! Akatoka ndani ya chumba na kwenda kutazama. Huku na kule, hakubahatika kuona chochote alichoshuku. Akarudi chumbani na kuketi kitandani.
***