Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,167
Katika karne za enzi zile, zile zamani kabisa, kitu cha thamani kilikuwa ni aidha dhahabu ama silva. Kila himaya ilijivuna kwa wingi wa dhahabu zao, utawala imara na shibe za watu.
Si zaidi ya hapo.
Lakini je, nini kinatokea pale kinapojiri kitu cha thamani zaidi? Ndio. Yani cha thamani kushinda hizo dhahabu, hizo silva, shibe na tawala imara zikiunganishwa zote kwa pamoja?
Kitu cha kuwatoa watu mate. Cha kuwanyima usingizi. Cha kufanya vita baina ya himaya na himaya?
Na ubaya basi kitu hicho kiwe kinamilikiwa na mtu mmoja tu. Na endapo kikikanyaga kwenye kiganja cha mtu mwingine kikamwongoza kunyonya damu za watu, kuwa kubuhu wa ulozi?
Sijamaliza, na hicho kitu kiwepesi akapewa mwanamke kama zawadi. Hajui kuendana nalo. Hajui yaliyomo. Na hata hajui hao waliompatia kama zawadi wamekitoa wapi!
Na kwa wakati huo, akiwa ameshapewa majukumu ya kuongoza himaya kubwa huko Uajemi iitwayo Goshen. Himaya iliyopo kwenye uadui mkubwa na himaya ya Devonship, iongozwayo na dhalimu na mlozi makbuhu aitwaye Jayit mwenye kisasi cha damu na Goshen!
Jayit aliyefukuzwa na kwenda kuiinua himaya yake binafsi isiyokuchwa jua. Jayit mwenye haja ya kuiweka Goshen chini ya miguu yake, hayo akiyatekeleza endapo akirudi Goshen kuteka mifupa ya marehemu babu na bibi yake kaburini!
Nisikuchoshe, niazime muda wako ambao hautauujutia, nikupeleke zama hizo za kutumia jua kama majira na panga kama silaha.
Ni hapa ... hapa... mpaka mwishowe.
Tantaw steve Mollel husna muba Money Talk Gentries Tumosa dumejeuri mTz mweusi @koncho 77 carbamazepine Evarist Massawe kisukari na wengineo mambo ni motoooo [emoji91] [emoji91]
Si zaidi ya hapo.
Lakini je, nini kinatokea pale kinapojiri kitu cha thamani zaidi? Ndio. Yani cha thamani kushinda hizo dhahabu, hizo silva, shibe na tawala imara zikiunganishwa zote kwa pamoja?
Kitu cha kuwatoa watu mate. Cha kuwanyima usingizi. Cha kufanya vita baina ya himaya na himaya?
Na ubaya basi kitu hicho kiwe kinamilikiwa na mtu mmoja tu. Na endapo kikikanyaga kwenye kiganja cha mtu mwingine kikamwongoza kunyonya damu za watu, kuwa kubuhu wa ulozi?
Sijamaliza, na hicho kitu kiwepesi akapewa mwanamke kama zawadi. Hajui kuendana nalo. Hajui yaliyomo. Na hata hajui hao waliompatia kama zawadi wamekitoa wapi!
Na kwa wakati huo, akiwa ameshapewa majukumu ya kuongoza himaya kubwa huko Uajemi iitwayo Goshen. Himaya iliyopo kwenye uadui mkubwa na himaya ya Devonship, iongozwayo na dhalimu na mlozi makbuhu aitwaye Jayit mwenye kisasi cha damu na Goshen!
Jayit aliyefukuzwa na kwenda kuiinua himaya yake binafsi isiyokuchwa jua. Jayit mwenye haja ya kuiweka Goshen chini ya miguu yake, hayo akiyatekeleza endapo akirudi Goshen kuteka mifupa ya marehemu babu na bibi yake kaburini!
Nisikuchoshe, niazime muda wako ambao hautauujutia, nikupeleke zama hizo za kutumia jua kama majira na panga kama silaha.
Ni hapa ... hapa... mpaka mwishowe.
Tantaw steve Mollel husna muba Money Talk Gentries Tumosa dumejeuri mTz mweusi @koncho 77 carbamazepine Evarist Massawe kisukari na wengineo mambo ni motoooo [emoji91] [emoji91]