SIMULIZI: Mkufu wa Malkia wa Goshen

MKUFU WA MALKIA WA GOSHEN 011

Simulizi za series


Upepo ulipuliza kando, Tititat akabadili mwelekeo. Hii ilikuwa kheri tena ya haja kwani kwa sasa shari ya kukumbana na aidha Nedal au Zura ilikuwa finyu ya mraba. Na ikawa hivyo Tititat asimwone yeyote isipokuwa miili ya wale wafu – wajumbe waliouwawa na Nedal.
Aliona eneo hilo akiwa umbali wa hatua kama hamsini. Sauti ya fisi ilibeba hisia zake na kumfanya atazame eneo hilo. Roho yake ilimtuma ajongee papo na mwili wake ukatii, basi akasogea.

Alituama eneoni hapo kwa muda akiperuzi na macho yake. Hakuona cha maana basi akaendelea na safari yake. Lakini kichwa chake hakikutaka kubanduka kwenye tukio hilo. Aliendelea kuwaza miili ile kiasi kwamba alijiona mwehu. Watakuwa tu ni masikini waliofia njiani! Alijipa ahueni. Lakini makazi ya watu yana umbali kiasi gani cha kuwafanya wafie jangwani? Basi watakuwa wameuawa! Akahitimisha na wazo hilo jepesi japokuwa bado lilinanga kichwa chake.

Dhamira yake kuja kule ilikuwa ni kumtafuta tu yule aliyeagizwa amtafute – Malkia Sandarus, maana ana kitu cha thamani ambacho mfalme wake, Jayit, amekibashiri. Kitu ambacho kinawindwa. Kitu ambacho hakijulikani ni kipi. Ajabu hili! Uwezo hulevya.

Ni kwa wakati huo, Zura, mwanamke pekee aliyekuwa ndani ya jangwa, alikuwa amejilaza juu ya mchanga wa jangwa akiwa amejifunika shuka dhoofu. Baridi lilikuwa kali na likamtenda akajikunyata. Farasi wake aliketi kando ila bado yeye macho yake yakiwa wazi, akiyatupa huku na kule.

Kwa muda huo kulikuwa tulivu na si ajabu hata wewe ukadhani ndio muda mwema wa kujipumzisha.

Si kwamba Zura alikuwa amesahau yale aliyoyaona ya miili ya wafu, la hasha! Macho yake yaligoma kufumba kwa kuhofia usalama wake. Mkono wake wa kuume ulikuwa umeshikilia kisu chake kidogo alichokiweka kiunoni ya kwamba kwa lolote litakalojiri basi atajitutumua kujiokoa.

Alitenda vivyo kwa masaa kama manne, macho yaangaza. Lakini Mungu hakuwa mjinga kuweka usingizi uambatane na kufunga macho, kwani nayo yahitaji kupumzika. Basi taratibu Zura akawa anashindwa kuyaokoa macho yake na usingizi, akalala! ‘kajoto’ alikojitengenezea kwa kujikumbatia mwenyewe na kujitandaza shuka kakampa ahueni, hakujua hata ni muda gani mkono wake uliacha kisu.

Aliufaidi huo usingizi kwa lisaa limoja tu kabla hajashtushwa kwa kukosa hewa! Kabla ya tukio hilo, farasi alilia lakini Zura hakusikia. Shingo yake ilikabwa vilivyo kiasi cha kutoa macho akipapatika kutaka kujikomboa. Uso wake uliunda huruma na mbashara aliona uso wa mtoa roho.

“Shhh! Nyamazaa!” Sauti ya kiume ilinong’oneza masikio ya Zura. Alikuwa ni Nedal akimtenda mwanamke huyo. Usiniulize alifika hapo muda gani maana sitakuwa na jibu.

Mikono minene ya mwanaume huyo ilikuwa imeficha shingo ya Zura barabara, uso wa mwanamke huyo ukachomoza mishipa ya damu kana kwamba mito juu ya ramani. Kwa namna alivyokuwa amebanwa, alisahau hata kama ana kisu. Mikono yake yote ilikuwa inang’ang’ana kuivuta mikono ya Nedal, kazi ambayo haikuonyesha dalili yoyote ya kuleta matunda.

Ikiwa imebakia sekunde sasa Zura afariki, twaweza sema hivyo, mara alijikuta akipata ahueni ya ghafla baada ya mikono mizito ya Nedal kubanduka shingoni mwake! Hakuamini kama amepona. Farasi alimtwanga Nedal teke zito la kichwani, Nedal akazirai.

Kabla ya kufanya lolote, Zura akahangaika kwanza kuvuta pumzi kwa nguvu zake zote. Alikohoa na kukohoa. Alishikilia shingo yake iliyokuwa inamdai maumivu makali. Kwa muda wa kama dakika tatu alikuwa anavuta pumzi tu.

Alichomoa kisu chake akamtazama Nedal aliyekuwa amezirai. Alijitahidi kumng’amua mtu huyo lakini hakuwepo kumbukumbuni mwake hivyo akashindwa kuelewa ni sababu gani ilivyomfanya mwanaume huyo atake kumuua. Alitaka kummaliza kwa kumkobeka kisu cha kifua, akashindwa. Roho yake ya huruma ilikuwa kubwa kuliko ya ukatili.

Alinyanyuka akampongeza farasi wake kwa kumbata kabla hajamkwea na kuondoka toka hapo kwa kasi kubwa.

Hakusimama mpaka pale farasi alipochoka, akashuka toka mgongoni mwa mnyama huyo akawa anatembea. Hakutaka kulala kabisa japokuwa mwili ulikuwa unahitaji hiyo huduma. Alihofia, tena maradufu! Aliuona usingizi kama kifo.

Alitembea kwa muda wa lisaa akipambana na pepo kali ya jangwa. Ila ghafla akiwemo metembezini, akajikuta akizama kwenye tego. Alikanyaga eneo fulani ambalo lilimomonyoka upesi na kummeza kana kwamba mdomo wa mamba. Si yeye wala farasi wake aliyebakia kwenye uso wa dunia!

Palikuwa kimya ghafla usiwaze kama kulikuwa kuna viumbe hai hapo sekunde tano nyuma.
.
.
.
.
***

.
.
.
.***
.
.
.
.
.
Masaa mawili tangu pale jua lilipochomoza, Rhoda anaamka toka kwenye usingizi mzito.
Ni ndani ya chumba kikubwa mno chenye samani za gharama ndefu mathalani kitanda kikubwa na kipana, madirisha makubwa, kabati kubwa, vigoda na viti vya kujipumzishia.

Rhoda alitazama huku na kule. Hakuwa anajua pale alipo wala hakujua amefikaje, lakini punde akili yake pevu ilimwambia yu ndani ya hekalu ya mfalme, ndiyo! Hakuna chumba chochote chaweza kuwa vile ndani ya himaya yote ya Goshen. Japokuwa Rhoda hajawahi kutembelea vyumba vyote ndani ya himaya ya Goshen, aliamini hivyo.

Pasipo juhudi tabasamu likachipuka usoni mwake. Hatimaye amefanikiwa! Aliwaza. Kwahiyo malkia Vedas amesadiki yale aliyomwambia? Ndio!

Alifuata dirisha mojawapo akaangaza kutazama nje. Uso wake ulijawa tabasamu. Alijiona yuko juu ya dunia. Alitazama karibia himaya yote ya Goshen asiamini. Niko ndotoni au? Hapana bwana! Alipepesa macho yake ahakikishe kama anaota. Alitabasamu mpaka jino la mwisho.

Mara mlango ulifunguliwa, akaingia mwanaume mmoja jabali akiwa amevalia nguo za watunza usalama. Alikuwa ni mojawapo wa wanaume wale waliomkomboa Rhoda toka kwenye mikono ya wauaji. Alimtazama Rhoda na macho makavu akisema:
“Nifuate!”

Kisha akaondoka. Rhoda alimfuata mwanaume huyo mpaka mahali penye kibaraza kinachotazama kaskazini mwa himaya ya Goshen. Hapo alimkuta Vedas akiwa na mwanaume mmoja mgeni machoni: alikuwa ni mrefu, mwili wa kiume, nywele nyeupe, macho yenye kiini cha kijani na kidevu pacha akiwa amevalia nguo iliyomkaa vema.

Alikuwa ndiye mwanaume yule Jayit aliyemwona kwenye rada zake akifanya mapenzi na Vedas.

Rhoda alitoa heshima yake kwa malkia kabla hajaamriwa aketi chini. “Nimehakiki yale uliyoyasema ni kweli,” alisema malkia Vedas.

“Na kutokana na uzalendo wako basi nimeamua kukutunuku kwa hilo.”

Rhoda aligundua ya kwamba malkia alituma wanajeshi wake wamfuatilie baada ya kutoka pale hekaluni akiamini ya kwamba kama ni kweli yale aliyoyasema basi ni lazima wazee wale dhalimu wa baraza wangechukua hatua na kujiingiza mkenge.

Lakini zaidi ya hapo, Rhoda akajuzwa kuwa wazee hao tayari wameshauawa. Mbaya si wale tu wadhalimu, bali wote. Miili yao ilikuwa nje inaning’inia kwenye vitanzi. Hapo Rhoda akaguswa, lakini pia akashangazwa na roho ya Vedas. “Nimeona nikupe nafasi kubwa sana kwenye usalama,” alisema Vedas. wakati akiongea hayo alikuwa anatazama himaya yake.

“Lakini kabla ya kukupa nafasi hiyo, nataka nihakikishwe zaidi juu ya uwezo wako. Kwahiyo kwa mwezi huu wote utakuwa chini ya uangalizi wangu. Utakuwa ukiishi kwako kama kawaida lakini huduma zako zote zikitokea hapa. Utakuwa unafanya kazi zako kama kawaida lakini lengo lako likiwa ni moja tu – kuwa jicho langu la ndani.

Kuna watu wengi kwenye himaya hii. Si wote wenye nia nzuri na mimi, na si wote wenye nia nzuri na Goshen. Na bahati mbaya sipo kila mahali kuhakikisha hilo.

Nahitaji kuona kila mahali. Nahitaji kumsikia kila mtu. Kutimiza hilo basi nakuhitaji wewe. Kwa kazi yako unayoifanya, upo karibu sana na midomo ya watu. Nataka uniletee kila wanachokiteta.”

Baada ya maelezo hayo, Rhoda aliondoka zake kurudi nyumbani. Alipewa dinari nyingi sana za kumfaya afanye chochote anachotaka maishani. Aliagizwa aboreshe kazi yake ya mama n’tilie na kila baada ya siku mbili awe analeta mrejesho wa yale anayoyasikia na kuyaona. “Una uhakika hili litafanya kazi?” Aliuliza Vedas akimtazama mwanaume aliyekuwa kando yake.

Mwanaume huyo alitabasamu. Hakuwa na papara. Macho yake yalikuwa yanatazama uwanda wa Goshen. Ukimwita Phares, utakuwa hujakosea. Phares, mwanaume wa chupa; Phares, mwanaume aliyeghaniwa na malkia Vedas; Phares, mwanaume asiye na makazi bali kwenye ulozi wa Vedas; mwanaume ambaye Vedas anamwamini kuliko yeyote.

“Pasi na shaka, itafanya kazi,” alijibu Phares. “Na kama isipofanya kazi basi ndiyo itakuwa fursa yako ya kutimiza haja yako ya kummaliza.” Malkia Vedas alitabasamu kwa mbali, ila tabasamu lake hilo halikudumu likajifinya na kuunda uso wa kazi.

Siri ilikuwa sirini.
Malkia Vedas anapata kufahamu mahusiano ya Rhoda na marehemu Fursa. Jambo hili analing’amua baada ya kutonywa na mojawapo wa wanajeshi wake ambaye alikuwa anajua juu ya mahusiano hayo yaliyokuwa ya siri. Malkia anataka kummaliza Vedas akiwa usingizini, lakini Phares anamsihi amwache hai kwani ana matumizi ya faida kabla ya kumalizwa.
.
.
.
. ***
.
.
.
Ilikuwa ni zaidi ya juma moja lakini si zaidi ya mwezi tangu Sultan alipowasili kwenye himaya yake, tawala kubwa Arabuni, akiwa amebebelea vipuri kadha wa kadha vya dhahabu alivyotoka navyo Osheni.

Alikuwa hana furaha na mtingwa wa mawazo. Lakini pia mkimya aliyependa kujitenga mara kwa mara. Mke mkubwa wa Sultan anasumbuliwa sana na hili jambo. Anatamani kujua kinachomsibu mumewe japokuwa zoezi hilo limekuwa gumu kila mara anapojaribu.

Ndani ya siku hiyo, Sultan anashindwa kuendelea kubeba jambo hilo kifuani. Alimwita mkewe mkubwa akamtaka aketi pembezoni. Alimweleza juu ya mkufu wa himaya ya wasioonekana, ambao habarize alizikuta Osheni, na jitihada zake alizofanya kuuweka mkufu huyo kimyani.

Anatatizwa na ukimya wa mjumbe wake, na hajui ni nini shida haswa. Kwa namna kubwa anahisi ameshaupoteza. “Huenda mjumbe wangu akawa ameshauwawa,” alisema Sultan. Uso wake ulikuwa mwekundu, macho yake yakilegea kwa uchovu.

Mke wake alimsogelea karibu zaidi akamwekea mkono begani. “Mbona hukunambia hili jambo mapema mpenzi?” “Na sikutaka hata kulisema. Hili ni jambo la siri, na nyie wanawake hamna vifua.” “Ila si mimi, Sultan.” Alijigamba mke mkubwa. “Ni siri zako ngapi naziweka kwenye uvungu wa kifua changu?” “Najua ni nyingi ila hii ni kubwa zaidi. Hili jambo ni watu wachache sana wanalijua, na kama lingekuwa linajulikana na wengi lingeshazua vita.” Mke akaguna. Alishusha pumzi ndefu na kuivuta. Alikunja sura yake akijaribu kuchekecha jambo alilolikumbuka.
“Mpenzi!” aliita.

Sultan akaitika kwa kumtazama mke wake huyo; mwanamke mtu mzima ila mwenye uzuri kwa kukusisimua moyo; mwanamke aliyekuwa amejiremba itakiwavyo kila kitu kikiwa kwenye kiti chake.

“Lakini unaonaje ukajaribu kwa Al Karim!”
alisema mke.

“Al Karim?” Aliuliza Sultan akitafakari. “Ndio, kwa Al Karim. Hakuna asiyejua habari zake zinazovuma kutokea kaskazini. Mjuvi na mtaalamu wa ramli. Kwanini usiende kumweleza shida yako? Bila shaka atajihisi fahari kumhudumia Sultan.”

Sultan alinyamaza akiwazua. Baada ya dakika mbili alirudisha macho yake kwa mkewe akauliza: “Tunaweza tukamwamini kweli?”

“Bila shaka,” akajibu mke mkubwa. “Ni binamu yangu, mtoto halisi wa mjomba wangu, kaka wa kwanza wa baba yangu. Endapo nikimtaka afunge mdomo, basi atatenda.” Sultan alishawishika kuchukua hiyo njia. Siku iliyofuata, asubuhi na mapema, akadamka pamoja na mkewe mkubwa wakaongozana na msafara wake kuelekea kaskazini mwa himaya yake kubwa.

Alitumia siku moja njiani kabla ya kufika kwenye nyumba kuukuu ya bwana Al Karim. Alipewa mapokezi makubwa sana japokuwa alikuja kwa kush’tukiza. Walichinjwa wanyama kadhaa na mivinyo ikamwagikia vinywani.

Jioni ya siku hiyo, akiwa na Al Karim pekee, Sultan alieleza haja yake ya moyo iliyomleta pale. Haja hiyo ikamshtua Al Karim kwa kina. Macho yalimtoka pima na mdomo wake ukaachama.

“Sultan, ni kweli usemayo?” “Pasi na shaka, Sultan hawezi kuongopa.”

“Ni wangapi wajua kuhusu hili?”

“Wachache mno.”

“Lakini Sultan, wajua ni namna gani mkufu huu waweza leta balaa?”

“Najua, lakini ni vema tukafikiria mema yake kwanza kabla ya mabaya.”

“Sultan wangu,” Al Karim aliita kwa sauti ya upole. “Endapo kama wenye nao wataamka, basi watatuteketeza wote.” Alionya.
“Kivipi?” Sultan akauliza.

“Huu mkufu ni wa himaya ya wasioonekana. Hakuna himaya yoyote inayoweza kuwazuia hawa. Endapo kama wakija kudai chao, himaya yetu itageuka kuwa majivu!”

“Na vipi kwa himaya hizo watakaoumiliki? Huoni watatugeuza sisi majivu kabla ya hao wasioonekana?” Mzozo huu uliishia kwa Sultan kushinda akitumia madaraka yake kama silaha.

Al Karim alipiga ramli akitumia kioo chake cha ajabu, akauona mwili wa mjumbe wa Sultan ukiwa umebakia mifupa sasa. Alijaribu kuutafuta mkufu lakini hakuuona. Sultan akamwagiza amtafute Zura.

Zoezi hilo lilichukua kama dakika tatu, kioo kikawa giza. Al Karim alitikisa kichwa chake, akasema:
“Sultan, hatuwezi kumpata!” “Unamaanisha nini?” “Huyo Zura hayupo duniani!” Sultan akakunja uso.
.
.
.
.
.
****
.
.
.
Kazi kazi! Lako jicho.
Twende kazi
 
MKUFU WA MALKIA WA GOSHEN 012

Simulizi za series




“Una maanisha nini?” Sultan alitamba.
“Hayupo kwenye uso wa dunia,” Al Karim akajibu. “Yani simwoni kwenye rada zangu.”
Sultan akashusha pumzi ndefu. Alikuna ndevu zake kidevuni akibinua mdomo.

“Inawezekana akawa amejificha ama amefichwa,” alidadavua Al Karim.

“Kama angelikuwa amefariki basi ningelijua.”
“Sasa tunafanyaje?” akauliza Sultan.

“Nitamtuma wakala wangu mwaminifu amtafute,” akajibu Al Karim kisha akaenda kwenye chumba chake chenye mlango mweupe. Humo akatoka na kitu cha pembetatu kilichofunikwa na kitambaa chekundu.

“Nini hicho?” Sultan aliwahi kusibu.
“Ni wakala wangu mwaminifu,” Al Karim akajibu na kisha akafunua kitambaa kile chekundu.

Lilikuwa ni banda dogo la chuma lenye umbo la pembe tatu likiwa limemtunza bundi mweupe mwenye macho mekundu. Ndege huyo alikuwa anatisha kumtazama, si tu kwasababu alikuwa ni bundi, hapana! Kichwa chake kilikuwa kimebebelea pembe ndogo juu ya macho yake makubwa kama mayai ya mbuni. Ukubwa wake ulitosha kujaza banda. Na alipopanua bawa, rangi nyekundu ilionekana ubavuni.

Al Karim alisema maneno kadhaa ya Kiyunani kisha akafungua banda la bundi huyo aliyetoka na kutuama juu ya bega la kushoto la Al Karim.

“Ndiye huyo?” Sultan aliuliza. Al Karim akatikisa kichwa.

“Ndiye yeye – wakala wangu mwaminifu. Macho yake ni yangu. Mabawa yake ni miguu yangu.”

Al Karim alimtuliza bundi wake mkononi kisha akamtaka Sultan aseme nani anataka amuone. Sultan akadadavua mazingira na umbo la Zura, Al Karim naye akatia neno lake papo na kumwachia huru bundi aliyerukia angani.

“Kazi imekwisha, Sultan,” alisema Al Karim. “Ntakupa mrejesho pale litakapopatikana jambo.”

Siku iliyofwata, asubuhi na mapema, Sultan akaondoka kurudi kwenye makazi yake. Hakuwa na matumaini makubwa juu ya kupatikana kwa mkufu.

Mkewe mkubwa alimsihi atulizane kila jambo litakuwa sawa, kwani Al Karim hajawahi kushindwa jambo. Hakuna rekodi ya jambo lolote lililowahi kuzidi uwezowe. Hapo angalau Sultan akawa ametua hofu kwa kiasi chake.
.
.
.
.
.
.
***
.
.
.
.
.
.
Siku mbili zinapita hakuna ambacho Tititat anakipata katika himaya ya masonara. Amezunguka sana kumtafuta Malkia lakini hakufanikiwa. Baada ya kufanya upelelezi wake mdogo anajikuta makaburini, juu ya kaburi la Malkia Sandarus. Alizikiwa hapo. Simulizi yake iliishia hapo.

Ulikuwa ni muda wa usiku mwepesi wa saa moja. Hakukuwa na mtu makaburini isipokuwa Tititat aliyeonekana anawaza jambo la kufanya muda si mrefu mbeleni. Baada ya kutimiza dakika kumi na tano katika eneo hilo pasipo kuona mtu, Tititat alianza kuchimba kaburi la Malkia akitumia mikono yake.

Kwa kasi kubwa alitenda zoezi hilo pasipo kuchoka. Halikuwa la ajabu hilo kwasababu muda huo ndio ulikuwa muda wao, wana Jayit, kuwa na nguvu; muda wa usiku! Kama amefungiwa mota alichimba kaburi, akaufikia mwili dakika tano tu.

Aliupekua mwili huo pote, hakuona kitu: hakukuwa na cha thamani! Sasa kile kitu cha thamani, kisichojulikana, alichotumwa na mfalme wake atakipatia wapi? Alijiona anashindwa.

Akiwa ndani ya shimo la kaburi, anasikia sauti za watu wawili wakiwa wanateta. Walikuwa ni vijakazi wa Msonara mkubwa. Walikuwa wametoka matembezini na sasa wanarejea kwenye makao yao haraka kabla ya mkuu wao hajafika.
.
.
Huko walipotoka walikuwa wamekunywa na kujilewea kwahiyo midomo yao haikuwa na stara, wala vichwa vyao havikuwa vinachambua vema mazingira waliyomo.
.
.
Walikuwa wanahororoja kuhusu mkufu. Habari hizo walizisikia kwa mkuu wao ambaye anahangaika mno kuutia mkononi. Mmojawao alimuuliza mwenzake kama mwenzao aliyemfwatilia Zura amekwisharejea.
.
.
Hapo mjibuji mwenye mdomo ‘pochi’ akaanza kufumbua mambo ambayo yalimvuta Tititat.

“Bado hajarejea, nahisi atakuwa tayari amekufa!”

“Umejuaje?”

“Muda wote huo hakuna taarifa yoyote ile. Unadhani kuna nini tena hapo? … ila kweli nakwambia, mkuu wetu kuna muda hana akili hata punje!”

“Enh!”

“Ohoo! Nakwambia ukweli. Hivi yeye kabisa kwa akili yake akawaamini wanawake wale mafukara watakuwa na kitu cha thamani kama kile? Eiiiish! Upuuzi!”

“Tatizo lako unapenda sana kudharau watu wewe! Mi naamini atakuwa amejiridhisha kwanza kabla ya kuamua vile.”

“Waii! Nakwambia tena, kuna muda mkuu wetu hana akili; zote huenda makalioni!”

“Akiupata je huo mkufu, n’kufanyaje?”

“Ntakununulia bilauri kumi na tano za pombe!”

“Kwa mshahara gani unaolipwa? Mie nitataka bilauri mbili tu.”

“Na asipoupata wewe utanipa ngapi?”

“Kumi na tano!”

Walikuwa tayari wamesogea mbali. Tititat alichungulia akaona sasa ni salama kwake kutoka ndani ya shimo. Alirudishia udongo alioutoa ndani ya kaburi hilo haraka kisha akaondoka kuwafwatilia wajumbe wale waropokaji.

Alitembea kwa uangalifu mno kiasi kwamba wajumbe walevi wasingewaza kama kuna mtu nyuma yao. Hata kama wangeliwaza hivyo na kutazama, bila shaka wasingelimuona yeyote kwa jinsi Tititat alivyokuwa amefanana na kiza.
.
.
Walifika getini kwa nyumba ya Msonara wakaingia ndani. Tititat alitazama eneo hilo kwa umakini na akaanza kupanga namna ya kuingia humo apate kuonana na Msonara mkubwa. Aliamini kwa kupitia msonara huyo, atapata majibu kadhaa ya maswali yatakayomsaidia kupata kitu cha thamani, ambacho tayari alishakijua ni mkufu.
.
.
Ilichukua dakika kumi tu, Tititat akawa tayari yupo ndani ya jengo la Msonara mkubwa lenye ulinzi wa haja. Hatukujua kaingiaje ila tunaona miili ya walinzi ikiwa chini imelala haijitambui au inavuja damu pomoni. Hakuna kelele yoyote iliyosikika mpaka Msonara mkubwa anafikiwa ndani ya chumba chake alimokuwemo na mwanamke mmoja mrembo mrefu mwembamba.
.
.
Kabla Msonara hajashangaa, alikuwa tayari amekabwa ngeta nzito wakati mwanamke wake akiwa amezirai kwa kumwona tu Tititat.
.
.
“Mkufu upo wapi?” aliuliza Tititat.
.
.
Kwa sekunde tu Msonara mkubwa alikuwa anavuja jasho, macho yamemtoka pima akipata uchungu wa roho kunyofoka.
.
.
Tititat alifungua mikono yake kumwacha mwanaume huyo avute hewa. Kwa papara Msonara akahema akikohoa. Tititat alirudia tena swali lake akimtazama Msonara usoni:
“Mkufu upo wapi?”
.
.
“Sijui,” alijibu Msonara mkubwa. “sijui ulipo!”
.
.
Tititat akadaka tena shingo ya mwanaume huyo na kuiminya kwanguvu. Macho ya Msonara yalipanda juu kwenda ubongoni. Tititat alimwacha tena avute hewa, kisha akarudia swali lake.

“Mi mwenyewe nautafuta, sijui ulipo!”
.
.

“Unautafutia wapi?”
.

“Kuna wanawake wawili ndio walikuwa na taarifa na huo mkufu. Mmoja amekwishafariki, mmoja amekwenda zake. Sijui ameenda wapi!”
.
.
Tititat alidaka tena shingo ya Msonara. Kabla hajaiminya, Msonara aliropoka:
“Ngoja weee, nasema baba!”
.
.
Tititat akamwacha.
.
.
“Kweli sijui! Sijui wapi alipoelekea, ila walinambia wametokea Goshen, nadhani huko ndipo atakuwa anaelekea. Nimemtuma mjumbe wangu amfwatilie.”
.
.
Tititat alinyanyuka akatoka ndani ya chumba hicho. Alimwendea farasi wake aliiyekuwa amemfungia porini, akamkwea na kisha kuanza safari akirudia njia aliyokuja nayo.
.
.
Kituo chake cha kwanza kilikuwa kwenye ile mizoga aliyoiona jangwani. Alimsimamisha farasi wake hapo akatazama. Ni mifupa tu ndiyo ilikuwa imebakia. Alijiuliza mizoga ile ilikuwa ya nani, akakumbuka maneno ya wale wajumbe walevi, mmoja anaweza akawa mjumbe wa Msonara. Na je huyo wa pili? Anaweza akawa ndiye huyo mwanamke? Nani kawaua?
.
.
Aliondoka na maswali yake hayo kichwani akibashiri kuyapatia majibu mbele kwa mbele. Aliamini kama mwanamke huyo, Zura, atakuwa hai basi atamwona kabla hata hajafika Goshen, hata kama alifunga safari hiyo kwa muda. Hilo kwake lilikuwa inawezekana maana yeye hakuwa na mapumziko njiani: farasi wake alikuwa hachoki wala yeye vilevile.
.
.
.
.
.
.
***
.
.
.
.
.
Dhumuni la Rhoda halikuwa limepotea. Wakati huu wa usiku akiwa ndani ya mgahawa wake mkubwa na unaovutia, alikuwa anawaza na kuwazua juu ya malkia Vedas. Ndio, bado alitaka kummaliza. Hiyo ndiyo ilikuwa haja ya moyo wake. Lakini sasa alikuwa na wazo jipya, kuutwaa ule mkufu uliotuama kwenye kifua cha mwanamke huyo.

Aliwasikia vema wale wazee wa baraza wakinadi mkufu ule kwamba ndio unaompa kiburi mwanamke huyo kwani hapo kabla, kipindi akiwa mke wa mfalme, hakuwa hivyo.
Sasa kuutwaa mkufu huo maana yake ni nini? Kumfanya malkia awe mdhaifu: kumfanya asiwe na sifa ya kuongoza: kumfanya malkia ajione mtupu.
.
.
Yeye, Rhoda, hakuwa na haja ya kutawala Goshen, kama ingelitokea hilo basi ingelikuwa bonasi kwake. Hakumpenda Vedas toka rohoni, alishindwa kabisa kulizuia hilo kuonekana.
.
.
Kumwona mwanamke huyo anatawala, kwake lilikuwa ni jambo la kushoto mno.
Mawazo yalimtinda sana, ila kwakuwa sasa hivi alikuwa na wafanyakazi lukuki ambao walikuwa wakimfanyia kazi, basi hilo halikuathiri biashara yake kwa vyovyote vile.
.
.
Kazi yake ya usimamizi haikuhitaji kuwa macho muda wote, bali tu uwepo wake eneo la kazi.
.
.
Akiwa humo mawazoni, alirudishwa fahamuni na sauti kali ya kicheko. Akiwa amekunja sura alimtazama mteja aliyekuwa anacheka hivyo. Alitamani kumfukuza lakini alishindwa.
.
.
Alimtazama mteja huyo kana kwamba mama amtizamavyo mwana mkaidi. Aliishia kusonya na kuendelea kupepesa macho yake kwa wateja wengine.
.
.
Kwenye kona kabisa ya mashariki mwa mgahawa, aliwaona wanaume watatu wasio na nywele kichwani. Walikuwa wamevalia nguo zilizowakaa vema, mikononi zikiwa zimejaladiwa na ngozi. .
.
Viatu vyao vilikuwa vikubwa lakini imara. Migongoni mwao walikuwa wamebebelea majambia marefu. Na kwenye kingo za viuno vya walikuwa wana visu virefu vilivyofunikwa na vifuko vya ngozi.
Pasipo na shaka robo, wanaume hao walikuwa ni wanajeshi wa himaya fulani, ama basi ni mesenari wa mtu fulani ama taasisi fulani kubwa. Rhoda alivutiwa sana kuwatazama, na akili yake ilimjuza akaamini kuna jambo anaweza kupata toka kwenye vinywa vya wanaume hao.
.
.
Alisogea karibu akaweka masikio yake bayana kusikia. Kwa muda wanaume wale waliteta maongezi yasiyokuwa na maana nzito kwa Rhoda. Mwishowe Rhoda akaamua kujitoa kimasomaso kwa kujongea kwenye meza ya wanaume hao. .
.
Alijitambulisha yeye ni nani eneo hilo na akaomba ruhusa ya kuketi.
.
.
“Samahni kwa usumbufu, nimeona ni sura ngeni mgahawani mwangu. Nikaona sio shida endapo tukafahamiana.”
.
.
Uzuri na ustaarabu wa kuigiza wa Rhoda uliwateka wanaume wale. Pasipo hata kusita wakajinasibu ya kwamba wao ni wapita njia tu wakitokea huko magharibi ya mbali kabisa. Wamepita hapo kula baada ya kuambiwa ndio mahali bora kabisa.
.
.
“Ahsanteni sana,” Rhoda alisema. “Nimefurahia sana uwepo wenu hapa kwani bila shaka utapanua biashara yangu kwa kwenda kusambaza habari njema kunihusu.”
.
.
Waliendelea kula na kunywa wakiteta ya hapa na pale. Baada ya muda mfupi Rhoda akaanza kupata yale anayoyataka.
.
. “Ni himaya kama tatu zimeshapitiwa na jeshi hilo la usiku. Zimeachwa hazina hazina yoyote na watu wameuawa wengi mno!” alisema mwanaume mmoja.
.
.
Alikuwa anatoa taarifa ya huko walikotoka: namna gani himaya kadhaa zilivyoachwa hazijiwezi baada ya kuvamiwa na jeshi kubwa la usiku: jeshi lililosemwa kama lenye nguvu na halizuiliki.

“Watu wa huko wanasema wavamizi hao walikuwa wanatisha. Walikuwa wenye kasi kiasi cha kumaliza kazi yao ndani ya himaya nzima kwa muda usiozidi dakika kumi tu!” alisema mwanaume mwingine akitafuna kipande cha nyama.
.
.
“Inaaminika jeshi hilo litaendelea kupita kwenye himaya kadha wa kadha. Mpaka sasa wameshapita kwenye himaya tatu, na haingii akilini kama wataishia hapo.”
.
.
Taarifa hiyo ilimsisimua Rhoda, na aliona ni sahihi kabisa endapo angemtaarifu malkia Vedas. Ndio, hakuwa anampenda mwanamke huyo ila aliona anastahili kupata taarifa hiyo kwa usalama wa raia wengine na hata wake ndani ya himaya.
.
.
Hakungoja muda mrefu baada ya wageni wake kuondoka, alijikusanya akaenda kwenye hekalu la malkia, pasipo na mushkeli akaruhusiwa kuingia ndani. Aliketi mahali pa mapokezi wakati kijumbe akiwa ameenda kutoa taarifa juu ya ugeni wake.
.
.
Baada ya dakika mbili akatokea Phares. Alikuwa amevalia taulo tu kifua chake chenye manyoya kikiwa wazi. Alikuwa ametoka kuoga: mwili wake ulikuwa umetambaliwa na maji. Hakuwa amevaa nguo ya ndani, maungo yake yakawa yamejichora tauloni.
.
.
Alimkarimu Rhoda kwa tabasamu. Alimwambia Malkia ametoka kidogo kwahiyo anaweza akamweleza tu shida yake. Rhoda hakupenda kumwambia hilo jambo Phares, ila kwakuwa hakuwa na namna, ilimlazimu atende hivyo.
.
.
Bahati njema, akiwa kati ya maelezo malkia Vedas akawasili. Alighafirika kumwona Phares yupo vile, kimwonekano, na kisha yu karibu na Rhoda. Kwa namna fulani aliona Rhoda anaweza kumkwapua mwanaume huyo kama alivyofanya kwa Fursa. Wivu ulimjaa. Na macho yake dhahiri yalionyesha hivyo.

Phares aliondoka zake upesi akamwacha malkia Vedas na Rhoda. Alinadi anakwenda kuvaa nguo na kujiweka sawa. Alipopotelea ndani, malkia Vedas akamuuliza Rhoda:
.
.
“Umeona nini?”
.
.
“Wapi, malkia wangu?” Rhoda akajibu na swali.
.
.
“Umeona nini kwa yule mwanaume?”
.
.
“Sijaona kitu, malkia.”
.
.
Vedas akamtazama Rhoda machoni. alitamani kumwambia kuhusu habari za Fursa ila akafanikiwa kuzuia mdomo wake.
.
.
“Umekuja kuleta habari gani?”
.
.
Rhoda akamweleza kila kitu juu yay ale aliyoyasikia kule mgahawani. Vedas alishtushwa na hizo taarifa. Aliapa atazifanyia kazi, na akampongeza Rhoda kwa kazi aliyofanya.
Ila kuna kitu bado kilikuwa machoni mwake.
.
.
.
.
.
.
***
.
.
.
.
. “Nimeonaa!” Ilikuwa ni sauti kali ya bibi mlozi ikibweka. Sauti hiyo ilitoka nje ya nyumba yao kubwa kuukuu iliyo ndani ya himaya ya wachawi, Tanashe.
.
. “Umeona nini?” wenzake wawili waliuliza kwa pamoja. Mmoja alikuwa hana macho; mmoja alikuwa nalo moja wakati yule aliyepaza sauti akiwa na macho mawili.
.
.
“Nimemuona Malkia Sandarus!” alipaza tena sauti. Bibi yule ambaye alikuwa hana jicho haraka akaunyoosha mkono wake na kunyofoa jicho moja toka kwa yule mwenye mawili, akalipachika kwake.
.
.
“Umemuona wapi?” wenzake wakauliza tena kwa uso uliolowa hamu.
.
.
Walikuwa ndani ya sebule yao inayonuka mizoga. Moshi ulikuwa umetanda ukitokea kwenye pipa lao, uwani, lililokuwa linapika chakula chao cha usiku.
.
.
“Nimemuona kwenye rada zangu za macho mawili na kioo msumbusi. Yupo Osheni!”
“Hilo tunalijua, ndio yupo Osheni.” Wenzake wakadakia.
.
.
“Hapana! Siyo kama vile nyie mjuavyo. Yupo Osheni, lakini tayari amekufa! Amefukiwa ndani ya ardhi!”
.
.
Bibi mmoja akajikuta ametabasamu.
.
.
“Kwahiyo unataka kusema …”
.
.
“Ndio!” yule msemaji mkuu akadakia.
. . “Tunaweza tukamtumia sasa. tunaweza tukamfanya akawa kikaragosi chetu!”
.
.
.
. .
.
.
Kazi kazi! Lako jicho.
Safi
 
MKUFU WA MALKIA WA GOSHEN -- 016
Simulizi za series


Haraka Phares akiongozana mbele kabisa na mwanaume yule mshahidi, walielekea kule kuliponasibiwa kuonekana kwa Malkia. Hii ilikuwa ajabu na kila mtu alitaka ashuhudie muujiza huu, hivyo wengi wakaenda.
.
.
Walifika huko wakahaha. Walizivunja shingo zao kwa kutafuta, walizungusha macho yao kwa kusaka, patupu! Hakukuwepo yeyote.
.
.
“Una uhakika ni hapa?” Phares alimuuliza mshahidi.
.
.
Wengine walikuwa tayari wameanza kupuuza, na hata kujutia juhudi zao kwenda eneo lile.
.
.
“Ndiyo ni hapa!” Alisisitiza mshahidi. “Nilikuja kukojoa nikamwona.”
.
.
Mkuu wa jeshi alisonya. Aliamuru mshahidi atiwe pingu na kufungiwa ndani kabla hajaleta madhara mengine, amri ikatimizwa. Watu waliondoka toka eneo hilo la tukio akiachwa Phares pekee.
.
.
Mwanaume huyo aliendelea kutazama huku na kule, bado hakuamini kama mwanaume yule ni mwehu kwa kuona tukio alilolisema. Alijongea huku na kule akiangaza. Mara akaona nyayo za mtu kwenye mchanga mzito wa tope. Alizitazama vema nyayo hizo akagundua ni za mguu wa kike.
.
.
Alipata maswali juu ya nyayo hizo, ila muda wa kutafuta majibu hakuwa nao, akaondoka kurejea kule hemani kwa ajili ya kuandaa mipango kabambe ya kujilinda. Hili swala aliliweka kama kiporo.
.
.
Hemani mipangoni, kwanza, akaagiza watu wote wanaoishi karibu na mpaka wakae ndani kwa muda wote huo wa usiku, asionekane yeyote akiwa anazurura. Vilabu vyote vya pombe vifungwe mapema, na atakayekaidi ataadhibiwa vikali. Agizo likatekelezwa ndani ya muda mfupi tu.

Baada ya hapo mitaro mirefu ilichimbwa kwa awamu mbili, ya kwanza karibia na mpaka, ikikaribiana kabisa na mashimo ya awali, ya pili ikiwa hatua kadhaa mbele. Jeshi lilijigawa makundi tatu katika idadi ifuatayo:
.
.
la kwanza lililokaribu na mpaka lilikuwa na wanajeshi wengi, la pili lililotenganisha na la kwanza kwa mfereji mrefu, lilikuwa na wachache ukilinganisha na la kwanza, la tatu pia vile vile likifuata mtindo huo wa kupunguza idadi.
.
.
Mbali na hapo, wanajeshi watatu walikuwa mbele ya mpaka. Hawa walikuwa mahususi kwa ajili ya kutambua hatari upesi na kutoa taarifa. Njia hii ilionekana yenye ufanisi zaidi ukilinganisha na mtu mmoja kukaa mtini kutazama, japokuwa ilikuwa ndiyo yenye hatari zaidi.
.
.
Kwenye mifereji mirefu iliyochimbwa, ilisakafiwa na majani makavu. Majani haya yakaloweshwa na mafuta ya taa. Yaliwekwa juu katika mfumo wa kwamba, kama wewe ni mgeni basi hauwezi ukatambua hilo.
.
.
Mipango yote hiyo ilifanyika ndani ya dakika kumi tu! Phares aliasisi na kusimamia kila jambo. Wanajeshi wakaelimishwa namna ya kujipanga na kupambana. Baada ya hapo kukawa kimya kila mtu akiketi mahala pake alipotakiwa kuwepo kwa mujibu wa mpango, kisha kukawa kimya cha kifo.
.
.
Ndani ya nyumba ndogo ambayo haipo mbali sana na mpaka, takribani kama nusu maili, mwanaume aliyekuwa amevalia shati chakavu lenye kifungo kimoja, suruali kuukuu inayoishia kwenye enka ya miguu, alikuwapo sebuleni akinywa pombe iliyotunzwa ndani ya chupa ya hovyo.

Nywele zake zilikuwa vurugu. Aliketi kwenye kiti kana kwamba mgonjwa mahututi asubiriaye kumuona tabibu kwa hali zote. Ila kwa namna alivyokuwa anapeleka chupa mdomoni na kugida, ndipo ingekuacha mdomo wazi kwa kujiuliza anatolea wapi nguvu hiyo?
.
.
Mwanaume huyo, asiyeeleweka ni aliyekula chumvi nyingi au lah, alinyanyuka toka kochini baada ya kuhakikisha amemaliza kinywaji chote kilichomo ndani ya chupa. Alipindua mdomo wa chupa akaungalizia chini, hakukuwa na kitu. Alilaani. Alijivuta kuelekea jikoni, akiwa njiani macho yake yakamtaarifu kuna mtu amekatiza dirishani.
.
.
Nani! Alishtuka na moyo wake. Taarifa ilitolewa muda si mrefu kwamba haitakiwi yeyote kuwapo nje ya nyumba kwa usiku mzima, sasa huyo aliyekatiza ni nani? Ni adui? Au ni mwananchi ambaye hana habari?
.
.
Haraka mwanaume huyo, mlevi, alikimbilia upande wa pili wa nyumba yake, dirishani akatupa macho njiani. Mara akamuona yule aliyekuwa anakatiza. Alikuwa ni mwanamke ndani ya nguo kuukuu. Hakumtambua mwanamke huyo ni nani, lakini alitamani kumfahamu. Akili yake ya kilevi ilimtuma apaze sauti kuita, akafanya hivyo.
.
.
Sauti ya mwanamke iliyotoka jikoni, inaweza kuwa ya mkewe, ikamkaripia mlevi huyo dhidi ya kupiga kelele. Asikome mwanaume huyo akaendelea kuita. Mara mwanamke akageuka. Hakuwa mbali sana na nyumba lakini mwanga wa muda huo ulikuwa hafifu kuonekana vema.
.
.
“Hairuhusiwi kuzurura nje we mwanamke! Nenda kwako upesi!”
.
.
Mwanamke huyo alisimama, kama mwanasesere, akamtazama mlevi huyo pasipo kusema jambo. Mlevi alitwaa ginga la moto lililokuwa linaning’inia ukutani mwake, akaonyeshea kule alipo mwanamke yule. Hapo ndo akamwona.

Malkia Sandarus!
.
.
Haraka mlevi alikimbilia jikoni kumwambia mke wake alichokiona. Ni kama vile pombe iliyeyuka kichwani. Macho yalikuwa yamemtoka, uso ukibebelea kitendawili. Mke wake alimpuuza, hakumwamini. Mlevi aliendelea kumsumbua mkewe mpaka pale alipokubali kwenda naye kutazama. Mke alirusha macho nje ya dirisha, hakumuona mtu. Alisonya akalaani akiondoka kwenda jikoni.
.
.
Mlevi alibaki akitazama pale dirishani kama vile mtu asiyeamini. Alifikicha macho yake, akatikisa kichwa. Alitazama na kutazama, hakuona mtu. Mwishowe aliamua kurudi kwenye kiti chake.
.
.
“Naomba chupa nyingineee!” alipiga kelele.
.
.
“Hiyo uliyokunywa inakupa mawenge, unataka nyingine!” mkewe akafoka. “Embu nenda kalale huko!”
.
.
“Nimemuona kweli! Naapa!”
.
.
“Kalalee!” Mke alifoka tena.
.
.
Katika kambi ya jeshi huko mpakani, kilikuwa ni kimya kirefu sasa baada ya kila kitu kusukwa na kupangwa vema. Mpaka muda huo walikuwa tayari wamedumu kwenye ulimwengu wa ububu kwa takribani robo saa na huku hakuna lolote lililotukia. Ukimya huo ukahamisha mawazo ya Phares.
.
.
Aliwaza kumhusu Vedas huko kasrini. Nafsi yake ilimsuta kwanini hakumuaga mwanamke huyo. Lakini kilichomshangaza na kumpa maswali zaidi, ni kwanini mwanamke huyo hajaja kumuulizia mpaka muda huo?
.
.
Ameshindwa hata kutuma watu kuja kumtazama kama yupo hapo kambini? Au amechoka ukaidi wake ameamua amwache? Hakupata jibu.
.
.
Alichojua ni kwamba amekosea, na aliona sehemu pekee ya kurekebisha makosa yake ni kushinda vita. Atarudi nyumbani akiwa na tabasamu pana, atapanua mikono yake amkumbatie malkia.

Alidumu fikirani kwa ziada ya dakika kumi, mambo yakaanza kuwika. Sauti kali ya filimbi iliita kuwashtua. Filimbi hiyo ilikuwa ni kiashiria cha ujio wa adui. Haraka kila mtu alipasha mwili wake moto tayari kwa ajili ya pambano.
.
.
“Wanakujaa!” Sauti ilisikika kwanguvu. “Hawaonekanii!” Taarifa nyingine ikaja upesi. Vishindo vya watu lukuki wanaokuja vilisumbua masikio ya kila mmoja, lakini hakuna aliyefanikiwa kuona wageni hao. “Shikilia mpangooo!” alipaza Phares. Mstari wa kwanza wa wanajeshi ukakaa tenge kwa ajili ya kuwakabili maadui.
.

Jeshi la Jayit, lililokuwa linaonekana kwa uhafifu, lilikuja kwa kasi mno, vishindo vyao vilieleza. Wakiwa hawana hili wala lile, lukuki waliparamia na kuzama ndani ya mfereji mrefu wa kwanza. Haraka moto ulitupiwa humo, kufumba na kufumbua likatokea tanuru kubwa! Viumbe wote waliozamia humo waliteketezwa kama makaratasi wakipiga yowe kali.
.
.

Kwa wanajeshi kadhaa, wa Jayit, waliofanikiwa kuvuka mfereji huo wa kwanza nao hawakufika mbali wakadhibitiwa kwa urahisi. Moto uliokuwa unawaka kwa pupa nyuma yao ulitoa mwanga mkali ambao uliwaonyesha vizuri wanajeshi hao mbele ya macho ya wanajeshi wa Goshen, waliotumia wingi na silaha zao kuwamaliza.
.
.
Baada ya kumalizika kwa zoezi hilo, kundi lote la kwanza la wanajeshi wa Goshen likalala chini ghafla. Wanajeshi wote wa Jayit waliovuka mfereji wa kwanza, pasipo matarajio, wakaanza kupokea mvua ya mishale ya moto. Hata wale ambao walikuwa bado hawajavuka, nao waliteketezwa kwa mishale hiyo iliyoshushwa kwa fujo.
Wakati mapambano yakiendelea, kundi la pili liliungana na la kwanza kuwaongezea nguvu, mfereji wa pili ukawashwa moto. Sasa mapambano yakawa yanatukia katikati ya mifereji miwili yenye kuwaka moto, na huku kundi moja tu la jeshi la Goshen, lile la tatu, likiwa ndio limebaki pasipo kuguswa. Kundi hilo kazi yao ilikuwa ni kuwadungua wanajeshi wa Jayit kwa ncha za mishale.
.
.
Kutokana na kuwekwa katikati ya moto, wanajeshi wa Jayit walishindwa kurudi walipotokea, wala kuingia ndani ya Goshen. Kushambuliwa kwa kushtukizwa kuliwapukutisha wapambanaji wao wengi, na hali ya kuwekwa hadharani na mwanga wa moto, kulirahisisha kazi kwa wana Goshen, ikawa kama wanapambana na wanadamu wenzao.
.
.
Vita ilidumu kwa muda wa dakika arobaini na tano tu, ushindi mnono ukaenda kwa Goshen. Ni wapambanji wanne tu wa Jayit ndio waliobaki hai wakikimbia kuokoa nafsi zao, ikiwemo kamanda wao mkuu mpya, bwana Raiden. Salama ya wanaume hao ilikuwa ni kutoingia kwenye uwanja wa vita, wao walibakia kando wakitazama.
.
.
“Waacheni wakaupeleke ujumbe,” alisema Phares akiwakataza wanajeshi kuwafukuzia maadui hao. Walifurahia ushindi, Phares akiteka nyoyo za wapambanaji kwa michoro na mipango yake thabiti iliyozaa matunda. Walimnanyua kama mtoto wakamrusha juu juu kama kitenesi.
.
.
Hakukaa tena hapo, Phares akaaga anataka kurudi kasrini baada ya kazi yake kuisha. Akisindikizwa na wanaume watatu wenye silaha, akaondoka zake akitumia farasi wenye nguvu waliokuwa wanakimbia kama upepo.
Hakudumu sana njiani akawasili kasrini. Alikuwa na tabasamu pana usoni, na pia mwenye nguvu na hamu ya kueleza yale aliyotoka kukumbana nayo alikotoka, haswa ushindi. Haraka alishuka toka kwenye mgongo wa farasi akakimbilia ndani. Lakini kuna kitu hakikuwa sawa, na pengine furaha yake aliyokuwa nayo ilimfanya asichambue mazingira vema.
.
.
Mbele ya uzio mkubwa wa kasri walikuwapo walinzi kama kawaida, wakisimama kwa ukakamavu huku wakishikilia silaha zao, hata ndani ya uzio vilevile hali ilikuwa vivyo hivyo, wanaume waliobebelea silaha wakisimama kwa ukakamavu. Lakini baada ya kupita ngazi ya kwanza kwenda chumba cha juu cha malkia, hakuonekana tena mlinzi yeyote. Hii haikuwa kawaida.
.
.
Phares alinyoosha miguu yake mpaka mlangoni mwa chumba cha malkia alipoubetua kitasa na kuzama ndani. Alikaribishwa na vitu vilivyokuwa shaghalabaghala, mathalani meza ilivyovunjika na bilauri kadhaa za maua zikiwa chini. Hapo ndipo moyo wake ukalipuka kwa hofu, bup!
.
.
Haraka alikimbia akarusha macho yake kitandani, huko akauona mwili wa malkia Vedas ukiwa umelala, na vitu zaidi vilivyovunjika na kuwa hovyo. Aliuendea mwili wa malkia akiita, lakini hakukuwa na jibu. Alisogea karibu zaidi, sasa kwa hofu, akagundua jambo chungu alilogoma kuamini kwa hapo awali. Malkia alikuwa amekufa!
.
.
Majeraha kadhaa yalikuwa usoni mwa marehemu; pua na mdomo wake vilikuwa vinachuruza damu, nywele zake zilikuwa hovyo na gauni lake alilolivaa lilikuwa limechanwa kifuani. Lakini zaidi ya yote, hakuwa na mkufu!
Phares aliushika mwili wa Vedas, akagundua bado ni wa moto. Hii ilimaanisha ameuawa muda si mrefu. Haraka alitoka ndani ya chumba akawaita walinzi na kuwapasha habari. Alikuja kugundua walinzi wa karibu wa malkia walikuwa wamejeruhiwa vibaya, na hata wengine kufa, na kufungiwa ndani ya stoo.
.
.
Haraka alitoa agizo la mipaka yote kufungwa, doria na msako kufanyika mpaka muuaji apatikane.
.
.
Wamkamate mtu yeyote yule watakayemuhisi, yeyote yule atakayekuwa anafanana na Malkia Sandarus!
.
.
.
.
.
.
.
.
***
.
.
.
.
.
.
.
Ni furaha iliyoje kwa vikongwe wa Tanashe! Macho yao sasa yalikuwa yanaona kitu walichokuwa wanakitafuta kwa muda mrefu, na si kingine hiko bali ni mkufu.
.
.
Kwa kupitia kioo chao cha kilozi, waliona vyote vilivyojiri. Furaha yao ilikuwa kubwa zaidi kwasababu sasa walikuwa wamelipiza kisasi kwa mwanamke aliyewafanyia mchezo mchafu wa kuwasaliti, bibie Vedas, basi vinywa vyao vyenye upungufu mkubwa wa meno vikawa wazi muda wote kwa tabasamu na macheko. Kazi pekee sasa iliyokuwa imebakia mikononi mwao, ikawa ni kuuingiza mwili wa Malkia ndani ya himaya ya wachawi, Tanashe.
.
.
Kazi hii haikuwa nyepesi kama mtu anavyoweza kudhani. Tamu ni kwamba vikongwe hawa wa Tanashe walitambua hilo jambo na hawakutaka kumwaga supu ingali wamebakiza fundo moja.
.
.
Ramli zao zilisogeza miguu na mikono ya Malkia upesi. Hawakutaka kuharibu umakini wao kwa fanikio la fataki. Malkia akiwa amebakiza kama nusu kilomita kuingia ndani ya Tanashe, ghafla anakutana na wanajeshi watatu, wanamuamuru asimame papo hapo.
Wanajeshi hawa walikuwa juu ya migongo ya farasi wakiwa wameshikilia viginga vya moto. Kwenye mapaja yao walikuwa wamebebelea mifuko ya jambia ndefu. Macho yao yaliyokuwa na shaka yalimtazama mwanamke waliyemsimamisha, ambaye alikuwa ameinamisha chini uso wake.
.
.
“Wewe nani na unaelekea wapi?” aliuliza mwanajeshi mmoja kwa sauti ya ukali. Kimya, hakukuwa na majibu.
.
.

Wanajeshi wakachomoa jambia zao. “Wewe!” alifoka mwanajeshi mwingine akipiga bega la mwili wa Malkia kwa bapa la jambia.
.
.
“Hujasikia ulichoulizwa? – wewe nani, unatoka wapi na unaelekea wapi?” Hakukuwa na majibu.
.
.
Wanajeshi walitazamana kwa nyuso za mashaka. Mmoja alijivika ujasiri akashuka chini, akatumia ncha ya jambia lake kunyanyua uso wa mwanamke waliyemsimamisha. Uso uliposimama, wakamuona Malkia Sandarus. Ajabu! Ndio, hawakuwa wanafananisha.
.
.
Kabla wanajeshi wale hawajatoka kwenye taharuki, mwanaume aliyekuwa karibu alinyanyuliwa mithili ya mtoto. Alirushwa kwanguvu kuwakumba wenzake aliowadondosha chini kama matofali. Kabla wanaume hao hawajajikusanya, tayari mwili wa Malkia ulikuwa umetwaa jambia la mmojawao, na katika kasi ya ajabu, ukawamaliza wanajeshi wale kana kwamba wadudu.
.
.
Farasi mmoja alichukuliwa, mwili wa Malkia ukajiweka juuye na kisha kuondoka kwa kasi kumalizia safari ya Tanashe. Farasi aliachwa mpakani, Malkia akazama ndani ya himaya.
.
.
Alitembea kwa muda mdogo tu kabla ya kukomea mbele ya mlango wa nyumba ya vikongwe. Alipokelewa kwa shangwe kubwa, na baada tu ya mkufu kutwaliwa na vikongwe wale, alipoteza nguvu na kuanguka chini kama mzigo, vikongwe wakambebelea na kumuingiza ndani.

“Hana kazi tena, tumuue!” alisema kikongwe mmoja. Ilikuwa ni vigumu kuwatofautisha maana kila mmoja alikuwa na jicho moja, wakivalia mashuka meusi.
.
.
“Hapana!” akawaka mwingine. “Usiwe mpumbavu asiye na akili. Unajua kabisa mkufu huu huendana na damu ya huyu kiumbe. Tukimmaliza ni vipi tutapata utawala wa mkufu?” Kweli.
.
.
Damu ya Malkia ilikuwa inahitajika, ama basi kiungo chake kwa ajili ya kukamilisha ibada. Ila vikongwe hawa hawakuona haja ya kuharakisha hivyo. Walitoka kufanya kazi kubwa kwa muda wote huo na wakaona haja ya wao kupumzika kisha kumalizia zoezi lao kesho yake usiku. Waliona linapendeza hili, wakakubaliana.
.
.
Muda ukiwa unaendelea kuyoyoma, huko mbali ya jengo kubwa la kuogofya la vikongwe hawa, anakatiza fisi mkubwa. Fisi huyu alikuwa anaperuzi na kuzurura huku na kule. Lakini ghafla, akiwa kazini, anakutana na nyayo juu ya ardhi. Ananusa nyayo hizo, anasikia ladha ya binadamu. Anafuatilia nyayo hizo taratibu, zinamuelekeza mpaka kwenye jengo la walozi vikongwe.
.
.
Fisi huyo alisimama, umbali wa kama hatua thelathini, akarusha macho yake kutazama jengo la vikongwe. Alitazama hapo kwa muda pasipo kuona kitu, ila kabla hajaondoka, anapata fursa ya kuuona mwili wa Malkia kwa kupitia dirishani. Si kwamba alikuwa amesogea karibu, la hasha! Aliliona hilo wakati vikongwe wakiupeleka mwili huo chumbani.
.
.
Fisi alijikuta akibweka kidogo kwa bumbuwazi, kisha haraka akaondoka toka eneo hilo kwa mbio kali.
.
.
.
.
.
.
.
.
FISI HUYU NI NANI, NA ANAELEKEA WAPI? JE NI WA BWANA FAKI? - BWANA MWENYE JESHI LA FISI NDANI YA TANASHE? UNAMKUMBUKA FAKI?
.
.
.
NI NINI PHARES ATAFANYA BAADA YA KIFO CHA VEDAS? NI NINI RHODA NAYE ATAFANYA? HIMAYA YA GOSHEN ITAKUWAJE BAADA YA MKUFU KUKWAPULIWA?
.
.
.
.
.
MKUFU UKIWAPO TANASHE, KUNA SHIDA YEYOTE ITAJIRI? NA JE MKAIDI JAYIT ATAKUBALI KUSHINDWA NA GOSHEN?
 
MKUFU WA MALKIA II -- MWISHO

Simulizi za series


ILIPOISHIA

Mapambano makubwa yakazuka! Ila askari wale wa Venis wangewezaje kupambana na watu wasioonekana?? Ndani ya nusu saa, wakajikuta wote wakiwa wameshauawa! Hakuna hata mmoja aliyebaki anahema.

Napo ndipo Jayit akakoma kucheka. Akakaza uso wake na kumsogelea Venis. Akamuuliza, "ulikuwa unasema??"

ENDELEA

Basi Venis akatazama nyuma yake, hakukuwa kumebakiwa na mtu hata mmoja, lakini hakujita, akajikaza na kumsogelea Jayit, akamwambia anataka kuichukua na kuiweka Goshen mikononi mwake.

Jayit akatabasamu. Akamwambia mwanamke huyo kuwa hana huo uwezo, na kamwe hawezi kumtikisa kwani yeye bado yu mchanga.

"Mimi ni Jayit! Jabali la kwenye miamba. Siwezi kutikiswa na yeyote yule juu ya uso wa dunia. Hata wewe naweza kukumaliza kwa kutumia mkono wangu mmoja tu!"

Venis akang'ata meno kwa hasira! Na mara akaanza kupambana na Jayit, hakuna askari aliyethubutu kuwasogelea maana walipigana katika ulimwengu wao wa tofauti kabisa!

Walipigana kwa ustadi wa ulozi, walipigania hewani pasipo kugusa ardhi. Na wakiwa kwenye pambano hilo, upepo mkali ukazuka, wale askari wote wakalazwa chini, wasione kinachoendelea. Katikati ya Jayit na Venis kulikuwa na kitu kama mduara wenye mwale mkali uliokuwa unawaumiza macho kila walipojaribu kuangaza.

Ila mara, wakamwona Jayit akiwa ametupwa nje ya mwale huo unaong'aa. Akadondoka chini kama mzigo wa kuni, kisha akalalama kwa maumivu na kukohoa mara mbili.

Akatazama mwale wa mwanga angani, mara ukanyauka na Venis akaonekana akiwa amesimama anaelea. Mkononi mwake alikuwa amebebelea moto uunguzao ila yeye usimguse!

Kabla Jayit hajafanya jambo, mara Venis akatupa mikono yake kwenda kwa jeshi la Jayit! Askari mamia wakashikwa na moto kana kwamba wamemiminiwa petroli.

Wakawaka haswa. Wakapiga kelele kali za maumivu wakikimbia huku na huko!

Venis akacheka akielekezea kichwa chake angani. Mikono yake inayowaka moto alikuwa ameitanua kana kwamba ndege anayetaka kupaa.

Alikuwa ana haja ya kucheka. Alimjulia adui yake. Alifanikiwa kujua siri ya kumsumbua Jayit, jabali la mwamba, ya kwamba alikuwa ni mdhaifu awapo mwangani. Jayit ni mtu wa giza, mtu wa kiza. Hawezi kuwa na nguvu zake akiwa mwangani!

Na basi kulitambua hilo, Venis akajizingira na mwanga mkali. Kisha akamshambulia Jayit kwa upanga wake wa kilozi.

Askari wa Jayit wakamezwa na hofu. Waliona sasa wanakwisha. Venis akawatazama tena kisha akawamwagia moto pasipo huruma. Wakaungua mamia kwa mamia. Wakakimbia huku na huko wakilia!

Venis aliporudisha uso wake kumtazama Jayit, akastaajabu hayupo! Akatazama kila pande, Jayit hakuonekana. Basi kwa hofu akaanza kurusha moto kila upande, kushoto na kulia, juu na chini!!

Akaangaza akikunja shingo huku na kule akitoa macho yake yanayotisha!

Sasa akawa amepatikana. Hatimaye akarudi kwenye kiwanja cha kujidai cha Jayit maana mwanaume huyo mlozi alikuwa amefichama akiwa anamtazama, akimvizia kumpa shambulio kali litakalomwacha hoi hajiwezi.

Basi kufumba na kufumbua, mara akahisi mtu nyuma ya mgongo wake. Kabla hajashtuka, akadidimiziwa kisu mgongoni kikatokea tumboni!

Akaachama mdomo na kutoa macho ya kifo. Jayit akamfunika kinywa na kiganja chake kipana kisha akampulizia upepo masikioni kisha akachomoa kisu chake na kumwacha Venis adondoke chini.

Ila bado hakuwa amekufa.

**

"Mke wa mfalme ametoroka!" Askari mmoja alifoka. Lucy akafungua mlango na kuchungulia kwa jicho moja. Koridoni akawaona askari watatu waliobebelea mikuki, walikuwa wanapashana habari za kutoroka kwa Tattiana na mama yake.

"Lazima tuwatafute," askari mmoja akasema akiwa na uso wa woga. "Mfalme hatotuelewa. Atatuua. Hima twende!"

Mara wote watatu wakatokomea wakikimbia upesi. Basi Lucy akafungua mlango zaidi na kutoka. Mkononi mwake alikuwa amebebelea kitabu kile KIKUU. Alikuwa ametoka kukiiba!

Haraka akashika njia kukimbilia chumba chake. Alipokamata kona ya kwanza akakutana na askari. Akasimama haraka, wakatazamana. Askari akatazama mkononi, akaona kitabu kile KIKUU mkononi mwa Lucy.

Kabla hajafanya kitu, Lucy akamuwahi kwa kumpiga ma kitabu kichwani. Askari akadondoka chini kwa kuzirai! Lucy akaendelea kukimbia na mwisho wa siku akaingia chumbani na kujifungia.

Haikuwa ngumu sana kwani askari hawakuwapo wengi kasrini. Waliosaliani kama kumi tu kwa idadi.

Basi haraka, Lucy akafungua kitabu kile KIKUU na kuanza kupekua. Kilikuwa ni kikubwa mno. Hakuna kitabu kikubwa cha kilozi kama hiki. Kutafuta kitu unachokitaka, ilihitaji utulivu mkubwa na muda haswa.

Ila Lucy alikuwa tayari alimradi lengo tu litimie! Lengo la kupata chami ya kumfanya Mfalme ampende. Asisikie wala kuona yeyote zaidi yake tu!


**

"Kazana!" Mama alisema akitazama mbele. Tattiana alikuwa amechoka kukimbia. Miguu inamuuma. Anahisi mwili wake umekuwa mzito kupitiliza!

Walikuwa ndani ya msitu wakikimbia kutafuta himaya nyingine wanusuru nafsi zao. Walikuwa wanafahamu fika kama wakishindwa kutoroka siku hii basi hawatakuja kufanikiwa milele. Hii ndiyo ilikuwa siku pekee. Vita iliyozuka, iliwapa mwanya wa kujivinjari na kutimiza mpango wao kwa wepesi.

Tattiana akasimama akihema kama mbwa. Akashika kiuno chake akipambana kupata hewa.

"Nimechoka!" Akanena kwa tabu. "Nimechoka, mama!"

Mama naye akadaka kiuno chake, alikuwa amechoka mno. Ila hakuwa na budi kuendelea kukimbia. Akamsisitizia mwanae aamke waendelee kukimbia kwani la sivyo, watakutwa hapo na kukamatwa.

Tattiana akashindwa kabisa kuendelea. Aliomba aheme kwanza. Wakangoja kwa sekunde kama ishirini hivi, na mara wakasikia sauti ya kishindo cha watu wakija! Wakashtuka. Walikuwa ni askari wa Jayit. Wale wanaume watatu.

Basi Tattiana na mama yake wakaanza kujikongoja kukimbia. Mwendo wao ulikuwa hafifu maana walichoka sana. Na hawakuwa wanaona vema mule msituni kutokana na kiza.

Kwa hivyo ndani ya muda mfupi tu, wale askari watatu wakawaona.

"Wale kule!"

Wakakimbia kwa kasi na kuwanyaka.

"Mlidhani mnaweza kutoroka kirahisi hivyo?" Askari mmoja akawauliza kwa kebehi. Wakaangua kicheko. Tattiana na mama yake wakalia wakiwaomba wawaachilie, ila askari hawakujali. Wakawaswaga waende mbele!

Wakasonga hatua kumi tu, mara askari mmoja akapigwa na jiwe kubwa la kichwa. Akadondoka chini maiti! Wenzake wakatahamaki na kuangaza.

Huku na huko, huku na huko, mara wakatokea Oragon na Ottoman! Mikononi mwao walikuwa wamebebelea magongo makubwa. Wakawafokea wale askari wa Jayit wawaachilie wanawake hao mateka haraka iwezekanavyo!

Wale askari wakacheka. Mikononi mwao walikuwa wamebebelea jambia ndefu zinazong'aa. Alafu wakina Oragon wamebebelea magongo na kuwatishia. Lilichekesha hili!

"Mtatufanya nini tusipotii amri yenu?" Akauliza askari mmoja.

"Tutawamaliza!" Akajibu Oragon akijikaza.

Basi wale askari wakawavamia wakina Oragon na kuanza kupambana nao. Vijana hao hawakuwa na ujuzi wowote wa sanaa ya mapambano. Pili, hawakuwa na silaha ya kivita, kwa hivyo, Walikuwa wanapigana kwa nasibu. Kwa wazi wasingeweza kufua dafu kwa wale majabali!

Basi baada ya muda mfupi, Oragon akawa amesimikwa jambia ya tumbo. Akapiga kelele kali ya maumivu. Ottoman akawehuka kwa hasira lakini hakuwa na cha kufanya.

Aliambulia kumtwanga askari mmoja gongo la kichwa na kumdondosha chini, ila naye akawahiwa kusimikwa jambia ya kifua. Akadondoka chini akimimina damu pomoni.

Askari pekee aliyebakia, ambaye ndiye alimsimika jambia, akamsogelea na kumtazama kwa kebehi. Akatabasamu.

Ila mara ghafla, akakitwa na jiwe kubwa kichwani. Lile lililomkita mwenzake wa awali. Akadondoka chini na kufa papo!

Alikuwa ni mama Tattiana ndiye aliyemsulubu. Haraka akiongozana na mwanae, wakamfuata Ottoman kumjulia hali.

"Ottoman!" Mama Tattiana akaita. Ottoman akatabasamu. Kaka yake Oragon alikuwa tayari ameshakata kauli.

Ottoman akamtazama Tattiana kwa macho yake yanayofifia. Kisha akasema kwa kinywa chake kinachotema damu.

"Nisamehe, Tattiana."

Tattiana akavuja machozi. Akamshika Ottoman mkono. Ottoman akafariki.

Tattiana akiwa hapo anamtazama Ottoman, mara akabanwa na uchungu wa kujifungua. Akalia kwa maumivu makubwa. Mama yake akajaribu kumtuliza na kumsaidia.

Ndani ya muda mfupi akajifungua kiumbe cha ajabu. Binadamu si, mnyama si.

Akiwa mjawa wa hasira za kisasi, Tattiana akanyaka jambia ya wale askari, kisha akamchoma kifuani yule mwana aliyemzaa, mara mbili pasipo kujiuliza!!

**

Kule uwanja wa vita ...


Puuh!! Venis alidondoka chini kama mzigo, Jayit akanyoosha mikono yake juu, askari wake wakapiga kelele kuu ya ushindi.

Sasa Venis hakuweza kuamka tena. Alikuwa ameshindwa! Alikuwa amechakazwa vya kutosha. Hakuwa na ulozi wowote mwili mwake kumnusuru na kadhia hii.

Upepo ambao Jayit aliupuliza kwenye tundu lake la masikio ulimmaliza na kumgeuza kuwa mtu wa kawaida mbele ya jabali huyo.

Jayit akacheka sana. Akapiga kifua chake konde kwanguvu na kumtazama Venis aliye hoi hajiwezi. Akasema,

"Mimi ni jabali! Jabali wa kiza kikuu. Hakuna anayeweza kupambana nami akatoka na uhai! Kaskazini ya dunia. Kusini ya dunia. Si magharibi wala mashariki! ... hakuna!"

Mara akashtuhwa na sauti ya kike. "yupo wa kupambana nawe!"

Akageuka haraka na kuangaza. Upande wake wa magharibi akamwona Malkia Sandarus akiwa anakuja, anatembea kwa madaha. Pembeni yake walikuwapo Fluffy, Zura, Alk na Seth!

Kichwani Malkia alikuwa amevalia kofia ya Pharao, na kifuani mwake ana mkufu wake amali.

Jayit akatazama vema. Watu hao hawakuwa na jeshi. Na wala mikononi mwao hawakuwa na silaha! Zaidi Malkia alikuwa ameshikilia kamba kumvuta farasi wake.

Basi akacheka. Akauliza, "na wewe ni nani??"

Malkia hakujibu mpaka alipomsogelea karibu. Akamwambia, "Mimi ni Malkia Sandarus. Jinamizi ndotoni mwako. Mtawala wa haki wa Goshen. Nimerudi nyumbani."

"Malkia Sandarus?" Jayit akavuta kumbukumbu. Alah! Akamkumbuka. Akacheka zaidi na kumuuliza, "haujionei huruma kukaa mbele yangu? Jabali wa miamba?"

Malkia akatabasamu. Kisha akatikisa kichwa chake na kusema, "yakupasa wewe ndiye ujionee huruma. Umewachezea wanangu vya kutosha. Sasa mama yao yupo hapa. Kwa usalama wa uhai wako, kimbilia Tanashe kabla sijaruhusu mikono yangu ikutawanye!"

Jayit akaguna kwa dharau. Akatazama kando ya Malkia na kusema,

"Naona umejipanga haswa!"

Askari wake wakaangua kicheko.

Malkia akamwambia, "Basi na kwakuwa umekuwa mkaidi, acha nikufunze!"

Akatanua mikono yake, mara ardhi ikaanza kutikisika. Kufumba na kufumbua, watu wakaanza kutokea chini ya ardhi!

Mamia! ... mamia! ... mamia! ... maelfu! Maelfu!! Maelfu!!

Jayit akaachama kwa kushangaa. Akasema: "jeshi la wafu!!" Hakika akapaliwa na hofu.

Haraka akatekenya ulozi wake na kupotea eneoni mara moja, akaacha jeshi lake likiwa limezingirwa na maelfu ya askari waliokufa miaka nenda rudi huko nyuma!

Jeshi nalo likatwaliwa na woga. Hawakuwahi kuona mifupa ikiwa imesimama. Inaongea. Inatembea. Inabebelea silaha!!

Basi jemedari wao, bwana Phares, akajitutumua, na kuwaamuru washambulie. Loh!! Wakakutana na kitu wasichokitarajia. Kitu ambacho hawakuwahi kukutana nacho kwenye uwanja wowote wa vita!

Utapambanaje na watu wasiokufa?? Hata pale walipopotea kimazingara, askari wa jeshi la wafu nao wakazama ardhini na kutambua nyendo zao. Wakawamaliza!!

Ndani ya muda mfupi maiti zikazagaa na kufunika ardhi. Malkia akatanua mikono yake, na kufumba macho. Mara hao maiti wakaanza kunyanyuka na kujiunga jeshi la wafu!

Wote.


**


Akiwa na uso wenye hofu, alifungua makabati na kila droo. Hakuona kitabu!!

Akashika nywele zake akiwa amewehukwa. Alichanganyikiwa haswa. Kitabu kiko wapi?? Alikihitaji kupambana na jeshi la wafu!

Alikihitaji kupata chami ya kumudu jeshi lile la kutisha! Jeshi la watu wasiokufa!!

Akainamisha mgongo wake atazame uvunguni, hakukiona, alipoamka akakutana uso kwa uso na Malkia!

Pia uso kwa uso na ncha ya jambia iliyomtoboa kifua.

Akapiga kelele za kuugulia. Kama haitoshi, Malkia akachomoa jambia yake upesi kisha akamfyeka kichwa. Mwili wa Jayit ukadondoka chini, kichwa kikimbilia uvunguni!

Basi jua likarejea angani, kukawa kweupe. Mabaki yote ya Jayit yakaungua kwa kushindwa kustahimili mwanga wa jua, hakuna hata chembe ya Devonship iliyobaki! Wote waliungua na kugeuka majivu!

Watu wote wa Goshen wakafunguliwa toka vifungoni. Nao wakambeba Malkia juu wakamzungusha himaya nzima kwa furaha kubwa! Hata wakina Tattiana wakasikia kelele hizo, nao wakajikokota kushuhudia.

Malkia alikuwa amerudi!

Goshen ilikuwa imerudi, hatimaye.
Nzuri sana, na inamafunzo lukuki, ubarikiwe sana 👏👏🔥🔥👍
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom