Simulizi: Miss Tanzania

Simulizi: Miss Tanzania

MISS TANZANIA
SEHEMU YA 58
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Patrick kwanza naomba ufahamu kwamba hutakwenda gerezani.Hata kama ikitokea kwamba utahukumiwa kifungo basi itapambana hadi nihakikishe ninakutoa.Kuhusu kukusubiri usitie shaka kuhusu hilo.Niko tayari hata kutumia muda wangu wote uliobaki hapa duniani kukusubiri wewe tu kwa hiyo usiwe na hofu hata kidogo na hilo.” Akasema Savanna kwa sauti laini
Waliongea mambo mengi sana usiku huo .Savanna alijitahidi kwa kila alivyoweza kumpa moyo Patrick kuhusu hukumu yake siku itakayofuata.Huu ulikuwa ni usiku mgumu sana kwa Patrick.Alitumia muda mwingi kusali na kumuomba Mungu amuepushe na kifungo

ENDELEA……………..

Familia nzima ya mzee Kibaho ilikuwa imekusanyika kwa ajili ya kusali sala ya jioni kama ilivyo kawaida yao kukutana na kusali pamoja kabla ya kwenda kulala.Siku hii ya leo kulikuwa na maombi maalum ya kumuombea Patrick ambaye hukumu yake ilitegemewa kutolewa siku inayofuata.Pamoja na maombi haya ya familia lakini Happy yeye alikuwa na maombi yake binafsi ya kufunga na kusali kwa muda wa siku tatu akimuomba Mungu amsaidie Patrick achiwe huru.
Baada ya kumaliza maombi yale ya jioni Happy na mdogo wake Margreth wakaenda chumbani kwao.
“Margreth I’m so nervous.Nahisi kama mwili wangu unatetemeka kila nikifkiria whats going to happen tomorrow.” Akasema Happy Margreth aliyekuwa anapanga nguo katika kabati lake akaacha kazi ile na kumfuata Happy
“Do you believe in God? Akauliza Margreth
“Ofcourse I do “ akajibu Happy
“Vizuri.Kama unamuamini Mungu muache atende kazi yake.Hana sababu ya kuogopa hata kidogo.Mtumaini yeye siku zote” akasema Margreth
“Margreth I believe in God lakini nashidwa kujizuia kuwa na wasiwasi.Sifahamu kitakachotokea kesh😵uh Gosh! Akasema Happy
“Ilitakiwa mimi ndiye niwe nimesimama kizimbani siku ya kesho nikihukumiwa na si Patrick.Lakini Patrick ndiye anayehukumiwa badala yangu.Sijawahi kuona mtu mwenye upendo mkubwa na wa ajabu kama huyu.I’m so sorry I’ve lost him and I don’t know what to do to get him back.” Akasema Happy
“Happy tafadhali usiwaze sana kuhusu mambo hayo.Tusubiri kwanza hadi siku ya kesho tuone nini kitatokea na baada ya hapo tutajua nini cha kufanya” akasema Margreth
“Margret sina ujanja tena.Tayari nimekwisha mpoteza Patrick.” Akasema Happy na mara wote wakastushwa na mlio wa simu ya Margreth.Akaichukua na kutazama mpigani halafu akavuta pumzi ndefu
“Its mike” akasema
“Tell him I’m not around” akasema Happy
“Happy siku ya leo hii ni mara ya tatu anapiga simu na hutaki kuongea naye.Happy I dont want to lie anymore.Please talk to him” akasema Margreth
“Ouh My God I don’t know what to tell him” akasema Happy
“Tell him anything.Ana hamu sana ya kuongea nawe.Mike ni mchumba wako.Ukikataa kuongea naye unamuumiza sana na utamfanya ahisi kwamba huku mambo si shwari.Tafadhali ongea naye.” Akasema Margreth.Happy akachukua simu ile ambao bado iliendelea kuita akabonyeza kitufe cha kupokelea simu
“Hallow Mike” akasema Happy.Mara moja Mike akaitambua sauti ya Happy
“Hallo malaika wangu .” akasema Mike kwa furaha
“Unaendeleaje Mike? Akasema Happy
“Ninaendelea vizuri Happy.Nimefurahi sana kuisikia sauti yako.Unaendeleaje? akauliza Mike
“Naendelea vizuri Mike.”
“Nafurahi kusikia hivyo.I miss you a lot my angel” akasema Mike
“I miss you too” akajibu Hapy
”How’s Patrick? Akauliza Mike na kumfanya Happy asite kujibu
“Happy how’s Patrick? Uliniambia kwamba hukumu yake ni kesho?
“Ndiyo Mike hukumu yake ni kesho” akajibu Happy
“Utahudhuria mahakamani? Akauliza Mike
“Ndiyo Mike nitahudhuria kwani ndicho kitu pekee ambacho kimeniweka hapa hadi muda huu kwa hiyo siwezi kukosa mahakamani.” Akajibu Happy
“Are you guys talk often? Akauliza Mike
“Mike mbona una wasi wasi hivyo? Akauliza Happy
“Lazima niwe na wasi wasi mpenzi wangu kwa sababu nafahamu kwamba Patrick ana sehemu kubwa sana moyoni mwako kwa hiyo nashindwa kujizuia kuwa na wivu kila nikifikiria kwamba uko karibu naye na mnaweza mkaonana” akasema Mike
“Usihofu Mike.Mimi na Patrick kilichobaki ni historia tu kati yetu na hakuna chochote kinachoendelea.Tayari kila mmoja ameendelea na maisha yake.Tayari naye ana mchumba na wanategemea kufunga ndoa muda wowote.Kwa hiyo huna sababu ya kuhofu”
“Hizo ni habari njema sana.Kwa hiyo utarejea mara tu baada ya hukumu kutolewa?
“Ndiyo Mike.Ni hicho tu kilichokuwa kinaniweka hapa na baada ya siku ya kesho I’ll say goodbye to Tanzania and leave this blessed country for good.Mike kuna jambo nataka kukueleza” akajibu Happy
“Jambo gani Happy?
“Unakumbuka uliwahi kuniomba nifunge nawe ndoa na nikakwambia kwamba unisubiri hadi hapo nitakapokuwa tayari?
“Ndiyo Happy nakumbuka sana na sijawahi kukuuliza tena kuhusu suala lile kwa sababu nilitaka utafakari na kama ukiwa tayari basi unijibu”
“Mike naomba nikufahamishe kwamba tayari nimekwisha fanya maamuzi yangu na jibu langu ni ndiyo.Nitafunga ndoa nawe Mike” akasema Happy na Mike akaruka kwa furaha asiyaamini masikio yake.
“Ouh Happy kwa muda mrefu sana nimekuwa nikisubiri unitamkie maneno kama haya.Nimefurahi sana mpenzi wangu.Nitaanza maandalizi mara moja na kuwataarifu ndugu na jamaa kuhusu jambo hili jema.”
“Hapana Mike usimwambie mtu yeyote kwanza.Tutawaambia tutakapokuwa pamoja nitakaporudi”
“sawa malaika wangu.Chochote utakacho niamuru nitatii.Ninakupenda sana Happy.Ahsante sana”
“Hata mimi nakupenda sana Mike na ndiyo maana nahitaji kuwa nawe katika maisha yangu yote yaliyobaki hapa duniani” akasema Happy.Wakaagana na kukata simu
“Happy !! akaita Margreth
“Una hakika na hicho ulichokisema?
“Kitu gani Margreth?
“kwamba unataka kuolewa na Mike? Happy akainama na kusema
I don’t know Margreth but I think that’s the best way to do for now.”
“Happy kwa nini umemwambia Mike jambo ambalo huna uhakika nalo?
“Margreth I have to do this.I’ll learn to love Mike.” Akasema Happy.Margreth akainamisha kichwa akaonekana kusikitika
“Unasikitika nini Margreth?
“Ninasikitika kwa sababu you cant swallow back what you’ve promised Mike.Kwa maana hiyo basi unatakiwa usimame katika maneno yako.Lazima uolewe na Mike.Jitahidi usimuumize kama wakati ule.”
Happy akazama katika mawazo mengi na baada ya muda akasema
“Margrteh I’ve made my decision.I’ll marry Mike.Hakuna uwezekano tena wa kuwa na Patrick.I’ve lost him”

**********************

Ni dakika ya pili sasa toka alipoweka shingoni tai yake akitaka kuifunga.Alikuwa amesimama mbele ya kioo kikubwa cha kujtazamia .Sauti ndogo ya muziki ilikuwa inasikika.Patrick alikuwa anabubujikwa na machozi kutokana wimbo uliokuwa uitwao see you again wimbo ulioimbwa na Carrie underwood
I will see you again,woah
This is not where it ends
I will carry you with me oh
Till I see you again
Patrick akaimba kibwagizo cha wimbo ule na mara Savanna akaingia mle chumbani na kuuzima mziki ule
“Patrick mbona unajipa wakati mgumu namna hiyo? Kwa nini ujiumize moyo wako? Just relax.Everything will be fine.Stop torturing yourself.” Akasema Savanna huku akimfuta machozi
“Savanna malaika wangu I’m so scared .Nashindwa kujiuia kuwaza nini kitatokea endapo nitahukumiwa kifungo.Hii ni siku ngumu sana katika maisha yangu”
“Patrick usiwaze sana kuhusu nini kitatokea.Tujiandae kwa maamuzi yoyote yale yatakayotolewa na mahakama.I’ve done my level best as a lawyer lakini mahakama ndiyo yenye kutoa maamuzi.Endapo watatoa adhabu ya kifungo gerezani,tutakata rufaa kama nilivyokuahidi.I’m right here beside you ,you are not alone” akasema Savanna na kumbusu Patrick halafu akamfungia tai
“Now you look perfect.you are so handsome Patrick.I love you” akasema Savanna na kumbusu tena Patrick shavuni
Wakati Savanna akijiandaa Patrick alitoka mle chumbani na kwenda nje ya nyumba
“Ni katika nyumba hii furaha yangu ya maisha iliporejea tena.Endapo nitafungwa gerezani nitaikosa nyumba hii iliyojaa furaha amani na upendo.” Akawaza Patrick halafu akarejea ndani.Savanna alimaliza kujiandaa akajumuika na mpenzi wake mezani wakapata stafstahi
“Are you ready to go Patrick? Akauliza Savanna
“I’m ready” akajibu Patrick na kisha wakatoka wakaingia garini na kuondoka kuelekea mahakamani


* * * *

Saa tatu za asubuhi ilimkuta Sarah tayari amekwisha wasili mahakamani.Aliwahi sana kufika pale ili apate nafasi ya kuonana na Linah ambaye alimwahidi kumpigia simu na kumfahamisha kuhusiana na mpango wa namna watakavyoweza kumdhibiti Loniki asiweze kuutekeleza mpango wake wa kumdhuru Patrick endapo mahakama itamuachia huru,lakini toka walipoonana usiku ule Linah hakumpigia tena simu jambo lililoanza kumpa wasi wasi.Kilichompa wasiwasi zaidi simu ya Linah haikuwa ikipatikana na hakupafahamu mahala alipokuwa amehamia.Mtu pekee ambaye angeweza kumpa jibu la wapi alipo Linah ni Loniki lakini aliogopa kumuuliza chochote kutokana na mahusiano yao kutokuwa mazuri.Pale mahakamani alijaribu kuangaza huku na huko lakini hakumuona mtu yeyote wa familia yake.Akachukua simu na kumpigia mama yake.
“mama shikamoo’
“Marahaba Sarah.Hujambo?
“Sijambo mama”
“Uko wapi Sarah? Si unajua leo ni siku ya hukumu?
“Nafahamu mama.Tayari niko hapa mahakamani.”
“Mbona umewahi namna hiyo?
“Ndiyo mama nimeamua tu kuwahi.Unakuja mahakamani?
“Ndiyo ninakuja niko njiani”
“Uko na Loniki?
“Hapana.Loniki amekuja kuchukuliwa na rafiki yake asubuhi ya leo.Aliniaga kwamba kuna sehemu wanakwenda lakini hatachelewa kufika mahakamani”
“rafiki yake yupi unayemzungumzia? Akauliza Sarah
“Kwani Loniki ana rafiki mwingine zaidi ya Linah? Huyo ndiye aliyefika asubuhi na wakaondoka wote”
“Sawa mama.Mimi utanikuta hapa” akasema Sarah na kukata simu
“Kwa nini Linah hajawasiliana nami kama alivyoniahidi na simu yake haipatikani tena? Amekwenda wapi na Loniki asubuhi hii? Kuna kitu gani kinachoendelea? Inawezekana Linah akawa ameshindwa kupata njia ya kumdhibiti Loniki? Edapo sintakuwa nimeonana naye hadi hukumu itakapotolewa na mahakama ikamuachia huru Patrick basi sintakuwa na njia nyingine zaidi ya kulifikisha suala hili katika vyombo vya usalama.” Akawaza Sarah huku akijaribu kupiga tena namba za simu za Linah bila mafanikio

* * * *

“C’mon Khumalo what happened to you? “ akasema Loniki akiwa na simu mkononi akijaribu kupiga tena na tena namba za khumalo lakini kila alipopiga jibu lilikuwa moja tu
“Namba ya simu ya mteja unayempigia haipatikani kwa sasa.tafadhali jaribu tena baadae.”
“Damn it !!! “ akasema Loniki kwa hasira na kugonganisha mikono yake.Linah aliyekuwa katika usukani akamtazama bila kusema chochote akaendelea na kukanyaga mafuta
Loniki na Linah walikuwa wanaelekea nyumbani kwa Khumalo.Asubuhi na mapema Linah alimfuata Loniki nyumbani kwao na kumfahamisha kwamba Khumalo hakuwa anapatikana simuni,taarifa ambayo ilimstua sana Loniki na akaamuru wamfuate Khumalo nyumbani.Katika siku hii Loniki alimuhitaji sana Khumalo ili aweze kutekeleza mpango waliokuwa wameongea wa kumuua Patrick endapo mahakama ingemuachia huru.Linah alifuata kila alichokisema Loniki lakini moyoni alikuwa akifahamu wazi kwamba Khumalo hakuwepo na walipanga Khumalo atoweke baada ya kupokea fedha toka kwa Loniki.
“Huyu Khumalo mbona anaanza kunipa wasi wasi? Kwa nini hapatikani simuni wakati anajua fika kwamba leo ni siku ambayo Patrick anahukumiwa kwa hiyo lolote linaweza kutokea? Loniki akajiuliza maswali mfululizo.Linah ambaye siku hii ya leo alionekana kuwa mkimya na mwenye wasi wasi mwingi hakujibu chochote
“Say something Linah” akafoka Loniki
“Niseme nini Lonny? Khumalo hapatikani simuni .Tunachotakiwa ni kufika nyumbani kwake na kuangalia kama ana tatizo.Pengine labda simu yake ikawa na matatizo” akasema Linah
“What a stupid woman.Sihitaji tena urafiki na mjinga kama huyu.After today its over.Hanisaidii kitu chochote katika maisha yangu zaidi ya kuniingiza katika mambo ambayo yanaweza kuniletea matatizo.Amenishirikisha katika mipango yake ya visasi na kunisababishia dhambi kubwa .Kitendo cha kumdhalilisha Happy namna ile kinaniumiza sana hadi leo hii.Sitaki tena urafiki na huyu mjinga” akawaza Linah wakati wamekaribia kufika nyumbani kwa Khumalo
Walifika katika jumba la Khumalo.Linah akapiga honi ili wafunguliwe geti.Loniki baada ya kuona mlinzi anachelewa kutoka akafungua mlango wa gari na kushuka garini akaenda kubonyeza kengele ya getini.Baada ya muda kidogo mlango mdogo wa geti ukafunguliwa
“Habari yako? Akasema jamaa mnene aliyefungua geti
“Habari nzuri” akajibu Loniki
“Nikusaidie nini? Akauliza yule jamaa
“Nina shida na Khumalo.Ninaitwa Loniki na mwenzangu pale garini anaitwa Linah.Sisi ni marafiki zake na tuna biashara naye ya muhimu sana”
Una biashara gani na Khumalo?
“Kuna kazi nilikuwa nimeelewana naye aifanye ambayo anatakiwa aifanye leo lakini kitu cha kushangaza ni kwamba hapatikani katika simu hivyo tumeamua kuja hapa nyumbani kwake kuonana naye” akasema Loniki
“Samahani dada yangu.Khumalo hayupo amesafiri” akasema yule jamaa na kumfanya Loniki ahamaki
“Acha utani ndugu yangu.Khumalo amesafiri lini na bila kututaarifu?
“Khumalo hayupo dada amepatwa na safari ya ghafla na kuondoka usiku wa kuamkia leo.” Akasema yule kijana .
“Ouh gosh ! amesema atarudi lini? Akauliza Loniki ambaye alionekana kustushwa sana na jibu lile
“hakusema atarudi lini lakini mara nyingi huwa akisafiri humchukua hata zaidi ya miezi sita kurejea.” Akasema yule kijana na kuzidi kummaliza nguvu Loniki
“Hakuna namna ambayo tunaweza kumpata au kuwasiliana naye ili kama yeye hauypo basi vijana wake waifanye kazi tuliyokubaliana kwani tayari nimekwisha mlipa fedha zote alizozihitaji” akasema Loniki
“Khumalo akisafiri kumpata huwa ni kazi ngumu sana kwa sababu huwa hatulii katika sehemu moja”
Jibu lile likamnyong’onyeza kabisa Loniki akaegemea ukuta.Baada ya kutafakari akaagana na Yule kijana na kurejea tena garini
“ Damn it !!...akafoka Loniki baada ya kurejea garini.Alikuwa amekasirika sana na kijasho kilianza kumchuruzika
“amesemaje yule kijana? Khumalo yuko wapi? Akauliza Linah ambaye alikuwa amebaki garini
“Khumalo amesafiri usiku wa kuamkia leo na haijulikani kama atarejea hivi karibuni” akasema Loniki
“ How could he do that? Kwa nini aondoke kimya kimya bila kututaarifu wakati alijua kabisa tuna mkataba naye na tayari fedha zote alizozihitaji nimeshampatia?Kwa nini ametufanyia hivi?.” Akalalamika Loniki
“kwa hiyo tutafanya nini? Akauliza Linah
“Sina hakika kama ni kweli Khumalo amesafiri .Najua atakuwa amejificha mle ndani.” Akasema Loniki
“Hapana Loniki.Kama umeambiwa kwamba Khumalo hayupo ni kweli atakuwa amesafiri.”
Loniki akageuka akamtazama Linah kwa muda kisha akasema
“How could you believe him so easily?
“Kwa sababu ninamfahamu vizuri Khumalo.Ni mtu ambaye huwa muwazi siku zote na kama imetokea amesafiri ghafla namna hii basi lazima kuna sababu ya msingi sana iliyomuondoa hapa nchini usiku .Inawezekana labda alikuwa anakimbia vyombo vya usalama kutokana na shughulio anazozifanya” Akasema Linah
“you failed me Linah.Wewe ndiye uliyeniambia nimuamini Khumalo.Unaona sasa kitu ambacho ametufanyia? Nini kitafuata iwapo mahakama itamuachia Patrick huru? Linah siwezi kukubali kumuona Patrick akiachiwa huru na akendelea kula raha na Malaya wake huku mdogo wangu akiwa ameoza kaburini.Endesha gari tuondoke” akasema Loniki kwa ukali
“Tunaelekea wapi?
“Turudi nyumbani”
“Lonny huoni kama tutachelewa mahakamani? Nyumbani tunaenda kufanya nini? Akauliza Linah
“Nimesema endesha gari tunarudi nyumbani? Akafoka Lonny.Linah akageuza gari na safari ya kurejea nyumbani ikaanza.
Waliwasili nyumbani kwa akina Loniki na kwa haraka akashuka garini akaelekea moja kwa moja chumbani kwa mama yake.Kabati kubwa la nguo halikuwa limefungwa na funguo,akalifungua na kifungua droo ndogo ndani ya lile kabati halafu akatabasamu
“Nilijua tu lazima itakuwepo,Baba alikuwa na bastora mbili kabla hajafariki.Moja ni ile aliyoitumia Vero kutaka kumtoa uhai yule shetani na nyingine ni hii hapa.Kama Vero alimkosa siku ile,mimi sintamkosa leo.Nimehitimu mafunzo ya kulenga shabaha kwa hiyo nina uhakika mkubwa wa kuufumua ubongo wake leo endapo mahakama itamuachia huru” akawaza Lonny halafu akaibusu bastora ile
“Don’t fail me my baby.Do as I tell you to do” akasema Lonny kisha akaiweka bastora ile katika mkoba wake akachukua funguo za gari lililokuwa la Vero akatoka
“Shuka katika gari hilo .Tutatumia hili hapa” Loniki akamuamuru Linah ambaye alishuka na kuingia katika gari lile alilolitaka Lonny
“Drive” akasema Lonny
“Tunakwenda wapi Lonny? Mahakamani? Akauliza Linah
“Stop asking questions Linah.Endesha gari.Ndiyo tunakwenda mahakamani” akasema Lonny kwa ukali.
“Loniki tafadhali naomba usiwe na hasira na mimi.Nilimuamini Khumalo kwa kuwa ni mtu niliyewahi kufanya naye kazi mara kadhaa” akasema Linah Loniki akamtazama kwa jicho kali na kusema
“Save your breath Linah.Nitamalizana nawe baadae.Kwa sasa niache nifikirie kuhusu plan B” akasema Lonny
“Plan B? akauliza Linah
“Yes Plan B.Wewe na shetani mwenzio Khumalo mmenifanyia jambo baya sana kwa hiyo nitawaonyesha kwamba hata mimi nina uwezo wa kufanya hizi kazi.” Akasema Loniki
“Loniki tafadhali naomba tuheshimiane na usirudie tena kuniita mimi shetani.Kama mimi nitakuwa shetani wewe utakuwa nani? Akasema Linah kwa ukali huku akitaka kulisimamisha gari.
“Shut up you bastard.Usinipandishe hasira zangu muda huu.Kuanzia sasa utafanya kile nitakachokuamuru” akafoka Loniki huku akimuelekezea Linah bastora.Linah akatetemeka
“Ouh gosh ! Kumbe ana bastora..mshenzi huyu amedhamiria kweli kumuua Patrick endapo ataachiwa huru na mahakama.Lazima nifanye jambo kumzuia asifanye anavyotaka kufanya.Nitatafuta namna ya kuwasiliana na Sarah.Najua hadi hivi sasa atakuwa anajiuliza sana ni kwa nini sijampigia simu kumtaarifu chochote kama nilivyokuwa nimemuahidi.Kutwa nzima ya jana nililazimika kutoitumia ile laini yangu ya kawaida kwa sababu nilikuwa na huyu shetani muda wote kwa hiyo niliogopa asije gundua kwamba nilikuwa nawasiliana na Sarah.”akawaza Linah
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 59
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Ouh gosh ! Kumbe ana bastora..mshenzi huyu amedhamiria kweli kumuua Patrick endapo ataachiwa huru na mahakama.Lazima nifanye jambo kumzuia asifanye anavyotaka kufanya.Nitatafuta namna ya kuwasiliana na Sarah.Najua hadi hivi sasa atakuwa anajiuliza sana ni kwa nini sijampigia simu kumtaarifu chochote kama nilivyokuwa nimemuahidi.Kutwa nzima ya jana nililazimika kutoitumia ile laini yangu ya kawaida kwa sababu nilikuwa na huyu shetani muda wote kwa hiyo niliogopa asije gundua kwamba nilikuwa nawasiliana na Sarah.”akawaza Linah

ENDELEA……………..

Kadiri muda ulivyokuwa unasonga ndivyo idadi ya watu ilivyokuwa inaongezeka mahakamani.Mpaka kufikia saa nne za asubuhi idadi ya watu ilikuwa kubwa.Sarah ambaye aliwahi sana kufika mahakamani macho yake hayakubanduka katika geti la kungilia akijaribu kuangaza kama atamuona Loniki na Linah
Akiwa bado ameyaelekeza macho yake katika geti la kuingilia mahakamani,aliziona gari tatu zikiingia.Alizifuatilia kwa macho hadi katika maegesho.Toka katika gari zile ikashuka familia ya Patrick ikiongozwa na mama yake,pamoja na ndugu wengine.Bila kupoteza muda Sarah apiga hatua na kuwafuata mahala walipo akawasabahi.Wakati akiongea na familia ya Patrick gari la mama yake likawasili pale mahakamni.Baada ya kuegeshwa mama yake Sarah akashuka garini akiongozana na akina mama wanne.Mahali alikoegesha gari si mbali sana na pale alipokuwa amesimama Sarah akiongea na familia ya Patrick.Mama yake Sarah akamuona mwanae na kumtazama kwa jicho kali bila kusema chochote .Tayari alikuwa katika uadui mkubwa na familia ya Patrick.Sarah akawaaga familia ya Patrick na kwenda kuungana na mama yake.
“Sarah unachokifanya si kitu kizuri hata kidogo” akasema mama yake kwa ukali
“Kwa nini mama?
“Kwa nini unadiriki kuungana na wale watu ambao unafahamu fika kwamba ni maadui zetu? Mtoto wao amemuua mdogo wako.Hupaswi kuandamana nao hata kidogo na hii ndiyo sababu inayokufanya wewe na dada yako Loniki msielewane”
“Mama mimi sipendezwi hata kidogo na tabia yenu hii ya kuichukia familia ya Patrick.Mambo yamekwisha tokea na tusubiri hukumu ya Mahakama muda mfupi ujao.Binafsi sina chuki yoyote na familia ile na ndiyo maana nashirikiana nao kwa moyo mkunjufu.” Akasema Sarah na mama yake akamtazama kwa jicho kali na kusonya halafu akapiga hatua kuondoa zake na wale akina mama aliokuwa ameambatana nao na kumuacha Sarah akiwa amesimama peke yake
Gari moja jeusi likaingia pale mahakamani na kuelekea sehemu ya maegesho.Ndani ya gari lile alikuwemo Happy Kibaho na familia yake.Wote wakaendelea kubaki ndani ya gari wakisubiri muda wa kusomwa hukumu ufike .Happy aliogopa kushuka garini kuwakwepa waandishi wa habari waliokuwa wakimtafuta usiku na mchana ili kumuhoji bila mafanikio.
Happy na familia yake wakiwa bado ndani ya gari,katika geti la kuingilia pale mahakamani likaingia gari moja la kifahari aina ya Mercedece benz s 320 CDI 4 MATIC ya rangi nyeusi na kwenda kuegesha si mbali sana na mahala walipokuwa wameegesha gari akina Happy.Baada ya sekunde kadhaa. Milango ya gari lile la kifahari sana ikafunguliwa akashuka Patrick na Savanna.Patrick alikuwa mevaa suti nyeusi iliyomkaa vyema na miwani myeusi kuyaziba macho yake.Savanna naye halikadhalika alivaa suti ya rangi nyeusi.Mara tu waliposhuka waandishi wa habari waliwazingira na kuanza kuwapiga picha.Hawakuwajali wakashikana mikono na kuelekea moja kwa moja ndani ya jengo la mahakama.
Akiwa ndani ya gari na familia yake Happy akawashuhudia Patrick na Savanna wakiingia mahakamani.Ni wazi alikuwa anaumia sana moyoni.Familia yote ilikuwa kimya kabisa.Hawakutaka kusema kwa kuogopa Happy asije umia zaidi
“Mimi ndiye niliyepaswa kumsindikiza Patrick mahakamani leo.Nasikitika sana kumpoteza Patrick” akawaza Happy
Nusu saa baadae watu wakaanza kuingia mahakamani kwani hukumu ilitarajiwa kuanza kusomwa muda wowote.Happy na familia yake wakashuka garini na kuungana na watu wengine waliokuwa wanaingia ndani ya mahakama.Wapiga picha bila kuchelewa wakaanza kumpiga picha Happy wakati akitembea kuingia ndani ya mahakama akiwa na familia yake.Ukumbi wa mahakama ulifurika watu
Saa tano na dakika kumi jopo la majaji watatu wa mahakama kuu wakiongozwa na Jaji Gregory Mkaga wakaingia mahakamani.Watu wote walikuwa kimya kabisa wakisilikiza.
Saa sita na dakika ishirini na saba Loniki na Linah wakawasili mahakamani.Walikuwa wamechelewa sana na tayari mahakama ilikuwa inaendelea.Loniki akaitoa bastora yake katika mkoba akaitazama kisha akairudisha mkobani.
“Twende tuingie mahakamani.” Akaamuru Loniki ,wakashuka na kuingia mahakamani huku mkoba uliokuwa na bastora ukibaki ndani ya gari
Hatimaye muda wa kusomwa hukumu ukawadia.Hiki kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwa watu wote.Patrick alikuwa anatetemeka mwili huku akiomba kimoyo moyo Mungu amsaidie na amuepushe na kifungo.Happy alikuwa ameweka mkono wake wa kulia katika sehemu ya kifua mahala ulipo moyo.Alihisi mwili mzima kumtetemeka.Kila mtu pale mahakamani kiroho kilimdunda
“God please help Patrick and help me too.I don’t know what’s going to happen if Patrick will go to jail.” Happy akaomba kimya kimya.
Loniki ambaye alikuwa amesimama nyuma kabisa ya chumba cha mahakama kwa kukosa nafasi ya kukaa mikono yake ilikuwa inamtoka jasho
“Hiki ndicho kipindi cha kubaini nini kitatokea.I’m not scared to kill him if the court will set him free.I swear I’ll kill him today” akawaza Loniki huku moyo wake ukimwenda mbio sana.Linah ambaye naye aliokuwa amesimama pembeni ya Loniki miguu yake ilikuwa inamtetemeka.Alikua akitafuta njia ambayo angeitumia ili kumdhibiti Loniki asiweze kutimiza lengo lake la kumuua Patrick endapo angeachiwa huru na mahakama.Alifikiria kuwataarifu polisi kuhusu suala lile lakini akaogopa kwamba huenda hata naye lingemletea matatizo kwani alihusika kwa kiasi kikubwa katika mipango yote ya loniki
“Njia pekee hapa ni kuwasiliana na Sarah lakini nitawasiliana naye vipi wakati Loniki tayari amenibana? I Must find a way,ngoja kwanza hukumu itolewe” akawaza Linah
Savanna aliyekuwa amekaa mbele kabisa alikuwa kimya.Japokuwa anajiamini kwa kazi kubwa aliyoifanya akishirikiana na jopo la mawakili kutoka kampuni yake ya uwakili,alishindwa kujizuia kuogopa kwani hakujua nini kinakwenda kutokea muda mfupi unaokuja.
“Ee Mungu ,nakuachia wewe kila kitu.Nimeifanya kazi yangu ya kumtetea Parick kwa uwezo wangu wote ulionijalia lakini wewe ndiye mwamuzi wa yote.Kama ni kwa mapenzi yako Patrick aende gerezani sina tatizo lakini kama ikikupendeza naomba Patrick aachiwe huru.Hakutenda kosa hili na zaidi ya yote ninamuhitaji sana katika maisha yangu” Savanna naye alikuwa amefunga mikono yake kifuani akifanya maombi ya kimya kimya akisubiri hukumu..Huu ulikuwa ni wakati wa kila mtu kuomba kile alichokuwa anakitaka kitokee
Kwa mujibu wa kifungu cha 326(1) b cha sheria ya mwenendo wa mashtaka sura ya 20 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 mahakama kuu kanda ya Dar es salaam ilimuachia huru Patrick baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani na upande wa utetezi kwamba kifo cha Vero kilitokea kwa bahati mbaya kati kati ya purukushani za kunyang’anyana silaha ambayo Vero alitaka kuitumia katika kufanya mauaji.
“Yametimia.Twende tuondoke” Loniki akamuamuru Linah wakatoka nje na moja kwa moja wakaelekea katika gari lao.Baada ya kuingia garini Loniki akainama na kulia sana
“He killed my sister..!!! why they let him go??? Why???!!!!!!!...Loniki alilia kwa uchungu
“Vero nitakulipizia kisasi.Siwezi kukubali mtu aliyekukatili uhai wako aendelee kuwa hai.” Akasema Loniki kwa uchungu
“Pamoja na kutoa mamilioni ya fedha ili huyu shetani afungwe gerezani lakini bado imeshindikana.You failed me Linah..You failed me.I knew this would happen…!! Thank you” akasema Loniki.
“Lonny mimi si wa kulaumiwa hata kidogo haya ni maamuzi ya mahakama.Kazi yangu ilikuwa ni kusuka mipango ya kumfunga Patrick lakini kama majaji wameamua hivi na tayari wamekwisha kula hela yetu basi kuna kila ulazima wa kuwauliza kulikoni mambo yawe hivi? Akasema Linah
“Shut up Linah..! Hakuna haja ya kuwatafuta tena hao majaji.Tayari nimekwisha poteza mamilioni ya fedha ambazo hazitaweza kurudi na hakuna chochote kilichofanyika.” Akasema Loniki kwa ukali
Watu sasa walianza kutoka mahakamani.Mama yake Loniki naye alitoka mahakamani akiongozana na akina mama wanne waliokuwa wamemshikilia.Alikuwa analia,aliumizwa sana na maamuzi yale ya mahakama.Lonny akamtazama mama yake kwa uchungu akainama na kufuta machozi
“Nilijua toka mwanzo jambo kama hili linaweza kutokea na ndiyo maana sikutaka kusubiri hukumu ya mahakama.Hakuna hukumu ya haki itakayotendeka na ndiyo maana nikaamua kutafuta hukumu yangu mwenyewe lakini wewe Linah na Khumalo mkanizuia nisifanye nilivyokuwa natka kufanya..Umeona sasa kilichotokea? Muuaji wa mdogo wangu ameachiwa huru..” akasema Loniki kwa uchungu.
Watu sasa walikuwa wengi nje ya mahakama.Wengi hususani ndugu jamaa na rafiki wa Patrick walikuwa na furaha na walionekana wakipongezana.Waliifurahia hukumu ile na kuipongeza mahakama kwa kutenda haki.Happy naye alitoka mahakani akiongozana na familia yake. Uso wake ulikuwa umepambwa na tabasamu pana sana licha ya machozi kuendelea kumtiririka.Alikuwa analia kwa furaha ya Patrick kuachiwa huru.Ili kumuepusha Happy na maswali ya waandishi wa habari wakaelekea moja kwa moja katika gari lao lakini Happy akagoma kuingia
“Happy mambo yamekwisha hapa mahakamani.Ingia garini tuondoke” akasema mzee Kibaho
“No dady.!I have to talk to Patrick before I leave.May be its going to be my last talk to him” akasema Happy
Wakiwa ndani ya gari wakiangalia kilichokuwa kinaendela,Loniki na LInah wakamshuhudia Sarah akimpa mkono mama yake Patrick.Kiendo kile kikazidi kumuumiza Loniki
“ After Patrick,that bastard will be next.I must teach her a lesson.Simtambui tena Saraha kama ndugu yangu.I don’t know her anymore” akasema Loniki kwa hasira.Vicheko na kupongezana viliendelea nje ya mahakama na hatimaye baada ya muda Patrick naye akatoka akiwa ameongozana na Savanna.Watu walimpongeza na kumsifu Savanna kwa umahiri wake .Kwa mara nyingine tena alidhihirisha umahiri wake katika masuala ya sheria.
Wakati mambo haya yote yakiendelea,Happy alikuwa nyuma ya gari lao akiandika kitu katika kijitabu chake kidogo.alipomaliza akaichana ile karatasi na kuishika mkononi na kuanza kupiga hatua kuelekea katika umati ule wa watu alikokuwa Patrick bila kujali waandishio wa habair na wapiga picha waliokuwa wakimpiga picha katika kila hatua aliyopiga..Savanna ndiye aliyekuwa wa kwanza kumuona Happy karibu na mahala walipokuwa wamesimama
“Happy!” akasema Savanna na kumfuata Happy akamshika mkono akamkumbatia na kupiga piga mgongoni.
“Hongera sana Savanna.Nimeikubali kazi yako.Wewe ni mmoja kati ya wanasheria mahiri kabisa hapa nchini”
“Thank you” akajibu Savanna
“Namshukuru sana Mungu kwa kushinda kesi hii” Akasema Savanna na mara Patrick akatokea
“Happy ! akasema Patrick
“Patrick ! …akasema Happy halafu wakakumbatiana kwa furaha.Savanna ambaye alikuwa amesimama pembeni yao akatabasamu .Happy akasogeza mdomo wake hadi karibu na sikio la Parick akamnong’oneza jambo.
“Hongera sana Patrick.Thank you that you saved me,you saved my life.I’ll always be thankfull to you” akasema Happy halafu akatumbukiza kitu katika mfuko wa koti la Patrick.Taratibu huku machozi yakimtoka Happy akamuachia Patrick na kuanza kuondoka huku Savanna na Patrick wakimtazama
“dady its over now.Tunaweza kuondoka” akasema Happy baada ya kuingia garini
“Ahsante Mungu kwa kusikia kilio chetu na hatimaye Patrick yuko huru.Nina furaha na uchungu kwa wakati mmoja.Ninafuraha kwa kuwa Patrick ameachiwa huru kwa sababu hakutenda kosa lolote .Aliubeba mzigo wangu mimi.Ninalia kwa uchungu kwa sababu hivi sasa ningekuwa pembeni yake tunaufurahia ushindi huu kwa pamoja na pengine ungekuwa ni mwanzo wa kuelekea kutimiza ndoto zetu nyingi tulizokuwa naz😵uh gosh ! there will be no dreams anymore.There is no us.I’ve lost Patrick”akawaza Happy.
.Zaidi ya nusu saa bado zoezi la kupongzana liliendelea pale nje ya mahakama.
“Patrick tumekaa sana hapa.Sherehe hizi zinatakiwa zikaendelee nyumbani.Tunatakiwa tuandae sherehe ya kukupongeza.Leo nina furaha sana” akasema Alois kaka yake Patrick.Patrick akatabasamu halafu akamvuta Savanna karibu yake na kusema
“Nadhani yatubidi tuelekee nyumbani kwanza .Nataka nikapunzishe kichwa changu na kumshukuru malaika wangu huyu ambaye ameniwezesha leo niwe huru tena.Nina deni kubwa kwa Savanna.Amepambana kufa na kupona hadi nimeshinda kesi.Nadhani muda huu ni maalum kwa ajili yetu na jioni ya leo tutakuja nyumbani kwa ajili ya kuwashukuru familia nzima” akasema Patrick
“kama ni hivyo basi tutaandaa sherehe ndogo jioni ya leo.Tafadhali hakikisha hukosi kufika nyumbani jioni ya leo” akasema Alois
Patrick akamfuata mama yake aliyekuwa amezungukwa na akina mama wengine ,akamvuta pembeni
“mama mimi naondoka.Nimeongea na Alois nitakuja nyumbani jioni ya leo kwa ajili ya kutoa shukrani zangu kwenu kwa msaada wenu mkubwa katika kipindi chote hiki cha matatizo yangu.”
“Nilidhani tunaondoka wote na kwenda nyumbani? Tunahitaji sana kukaa kama familia leo ni siku yetu kubwa sana” akasema mama yake Patrick
“Ninafahamu hilo mama lakini kwa sasa nahitaji kupumzika kidogo na kumshukuru Mungu.Nitakuja jioni na tutajumuika pamoja” akasema Patrick halafu akaagana na mama yake akamshika mkono Savanna na kuingia katika gari lao na kuondoka
“washa gari.We follow them” akaamuru Loniki ambaye alikuwa garini na Linah .Bila ubishi Linah akawasha gari na kuanza kuwafuata akina Patrick
Sarah bado aliendelea kuangaza macho pale mahakami akitegemea kumuona Linah.Muda wote alikuwa roho juu kila alipokumbuka maneno ya Linah kwamba Loniki amedhamiria kufanya jambo baya endapo mahakama itamuachia huru Patrick.
“Inawezekana Linah alikuwa ananidanganya? Hapana ,Linah hakuwa ananidananya na katu hawezi kufanya hivyo.Ninaheshimiana naye sana na katu hawezi kuthubutu kucheza na akili yangu namna hii.Ninashawishika kuyaamini maneno yake.Lakini mbona hakunipigia simu kama alivyokuwa ameniahidi? Na simu yake kwa nini haipatikani tena?” akawaza Sarah huku akiangaza angaza na mara akawaona Patrick na Savanna wakiingia katika gari lao la kifahari wakaondoka pale mahakamani..Sarah akahisi kama nywele zinamsisimka.Alitamani awakimbilie na kumuonya Patrick kuhusu taarifa za kuwepo kwa mpango wa kumuua lakini akaogopa kwa kuwa hakuwa bado na ushahidi wa kutosha wa jambo hilo.Mtu pekee ambaye angeweza kulithibitisha hilo alikuwa ni Linah .
“Natamani nimweleze Patrick kuhusiana na mambo aliyonieleza Linah lakini naogopa.Linah yuko wapi ? akawaza Sarah na mara simu yake ikaita.Alikuwa ni shangazi yake.Sarah akaguna kidogo halafu akaipokea
“Hallow shangazi”
“Sarah uko wapi?
“Niko bado hapa mahakamani”
“Sarah njoo nyumbani mara moja.Hali ya mama yako si nzuri hata kidgo.Mtaarifu na Loniki kama utamuona kwa sababu ninajaribu kumpigia simu lakini simu yake haipatikani.Ulimuona mahakamani leo?
“Hapana sikumuona mahakamani na sina hakika kama alikuja”
“Hata mimi sikumuona sijui yuko wapi.Fanya haraka uje nyumbani” akasema shangazi yake Sarah.
“Sawa shangazi ninakuja sasa hivi” akasema Sarah na kwa haraka akaelekea katika gari lake.

* * * *

Savanna alikuwa anaendesha gari huku machozi yakimtoka
“Unalia nini malaika wangu? Akauliza Patrick
“Patrick machozi haya ya furaha yanatoka yenyewe na hasa nikikumbuka kazi kubwa iliyofanyika.To be honest haikuwa kesi rahisi.Ni moja kati ya kesi ambazo zimewahi kuniumiza kichwa change mno.Thanx God its over” akasema Savanna
“Savanna nina deni kubwa sana kwako na wale wote ambao mmepigana kufa na kupona kuhakikisha kwamba ninakuwa huru tena.Savanna umepambana vilivyo.Sioni kitu cha kukulipa mpenzi wangu.” Akasema Patrick
“Patrick ninaombi moja tu kwako”
“Omba chochote Savanna.”
“Katika watu ambao utawashukuru,usisaha kumshukuru pia Happy.Alifanya jambo kubwa sana..Ushahidi wake ulichangia sana kuipa nguvu hoja ya yetu na kuishawishi mahakama kukuacha huru”
Mara tu Savanna alipolitaja jina la Happy mara moja Patrick akakumbuka kitu.wakati akiwa wamekumbatiana Happy aliweka kitu fulani katika mfuko wake wa koti.Akaingiza mkono mfukoni na kutoa kikaratasi kidogo
“Whats that? Akauliza Savanna
“Ni karatasi Happy aliiweka mfukoni “akasema Patrick halafu akaikunjua karatasi ile na kuisoma.
Kwako Patrick
Nina kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa siku ya leo.Ninafuraha kubwa nisiyoweza kuielezea.Nashukuru mahakama kwa maamuzi yake.Namshukuru sana Savanna kwa kupambana hadi umeachiwa huru.
Patrick nimeamua kukuandikia maneno haya machache kwa sababu sintapata tena nafasi ya kuongea nawe ana kwa ana.This might be our last contact.Maneno machache ninayotaka kukueleza ni kwamba Patrick you are a great man.I’m proud of you.Ninafuraha kukutana na mtu kama wewe katika maisha yangu.
Patrick you saved me.You saved my life.Ninashukuru sana kwa upendo wako usioelezeka wala kupimika.Sina kitu cha kukulipa kwa wema ulionitendea na upendo ulionionyesha toka tulipoonana na kufahamiana.Ninaapa kwamba hatatokea mwanaume ambaye atanionyesha upendo kama ulinionyesha wewe .Nitakuombea siku zote kwa Mungu ili uwe na furaha katika maisha yako.I know Savanna will take a good care of you.You deserve someone better than me,you deserve her.
Patrick we had lots of dreams togeth.I want you to fullfil all the dreams we had.Get married to Savanna and you live a good and Happy life.
Mwisho kabisa ninaomba toka ndani ya moyo wako unisamehe kwa makosa yote niliyokukosea.
I will always miss you
Kiss and goodbye
Happy

Alimaliza kuisoma barua ile na kuirudia tena kwa mara ya pili halafu akaikunja na kuiweka mfukoni
“Anasemaje Happy? Akauliza Savanna.Patrick hakujibu kitu akaitoa barua ile na kumpatia
“utasoma mwenyewe alichokiandika”
Savanna hakuisoma barua ile kwa kuwa alikuwa anaendesha gari akaiweka pembeni kwa lengo la kuisoma baadae
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 60
MTUNZI: PATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Alimaliza kuisoma barua ile na kuirudia tena kwa mara ya pili halafu akaikunja na kuiweka mfukoni
“Anasemaje Happy? Akauliza Savanna.Patrick hakujibu kitu akaitoa barua ile na kumpatia
“utasoma mwenyewe alichokiandika”
Savanna hakuisoma barua ile kwa kuwa alikuwa anaendesha gari akaiweka pembeni kwa lengo la kuisoma baadae

ENDELEA……………..

Toka mahakamani Patrick na Loniki wakaelekea moja kwa moja makaburini ambako Patrick alitaka kuweka maua katika kaburi la Vero .Waliegesha gari na kushuka wakaelekea lilipo kaburi la Vero.Akiwa na maua mkononi,Patrick akasimama mbele ya kaburi la Vero.Akalitazama kaburi lile kwa makini halafu akapiga magoti na kuyaweka maua aliyokuja nayo.
Savanna alijisogeza pembeni na kumuacha Patrick peke yake pale kaburini
“He needs to be alone” akawaza Savanna na kusogea pembeni
Wakati Patrick akiwa amepiga magoti katika kaburi la Veronika,gari walilokuwamo Linah na Loniki nalo likawasili.Walikuwa wakiwafuata kwa nyuma akina Patrick.Loniki akaitoa bastora yake akaishika mkononi
“Stay in the car” akasema Loniki na kuufungua mlango lakini kabla hajashusha mguu chini akasikia sauti za watu wakiimba wakielekea kule makaburini
“Whats that ? You hear something? Akauliza Loniki
“Nasikia kama sauti za nyimbo” akajibu Linah mara ukatokea msafara wa watu waliokuwa wanakuja kuzika
“ouh gosh !! akasema Loniki kwa ghadhabu
“Mpango wote umeharibika”
“Damn ..!!!..akazidi kulalama Loniki.Msafara ule wa magari ukazidi kukaribia ,Loniki akafunga mlango wa gari.
Sauti zile za watu wakiimba zikamstua pia Patrick,akasitisha maombi yake na kuinuka
“Twende tuondoke Savanna” akasema Patrick wakaingia katika gari laona kuondoka pale makaburini.Loniki na Linah wakaendela kuwafuatilia kwa nyuma
“ Kama si watu hawa kunivuruga ningemtundika risasi Patick juu ya kaburi la mdogo wangu.Ana bahati sana lakini kabla jua halijazama jioni ya leo lazima niitoe roho yake” akasema Lonki.Linah hakujibu kitu alikuwa anatetemeka kwa ndani.Hakujua angewezaje kumuokoa Patrick kwani Loniki alikwisha dhamiria kufanya mauaji
Toka makaburini Patrick na Savanna wakaelekea moja kwa moja nyumbani .Patrick alikuwa na kazi kubwa ya kupokea simu nyingi nyingi za pongezi toka kwa watu mbalimbali kwa kesi ile kumalizika
“Itanichukua siku nzima ya leo kupokea salamu mbali mbali toka kwa watu.Nimefarijika sana kwa pongezi na pole nyingi toka kwa watu mbalimbali” akasema Patrick kwa furaha
“Bado pongezi zangu mimi” akasema Savanna na wote wakacheka .Waliendelea na safari yao bila kufahamu kwamba walikuwa wanafuatiliwa na akina Loniki
Walifika nyumbani kwao na kusimamisha gari nje ya geti wakisubiri geti lifunguliwe.
“Nahisi wamekuja nyumbani kwao.This is the time” akasema Loniki
Linah akasimamisha gari nyuma ya gari la akina Patrick waliokuwa wanasubiri kufunguliwa geti.
“Wait for me here.Dont do anything stupid to ruin my plan.” akasema Loniki halafu akaichukua bastora yake akaificha kiunoni na kuchomoa funguo ya gari akashuka.Akapiga hatua chache na kulifikia gari la akina Patrick.Akagonga kioo cha mbele upande aliokaa Patrick ambaye aligeuza kichwa na kupatwa na mstuko mkubwa.Aliitambua sura ya mtu aliyekuwa amesimama nje ya gari.
“Loniki ..!!! akasema Patrick kwa mshangao.Hakuwa ametegemea kumuona Loniki sehemu ile na kwa wakati ule.Ni muda mrefu hajawahi kuonana na Loniki.Savanna naye akageuka na kumtazama Loniki.Mara moja akaikumbuka sura ile.Alikumbuka kuiona sura ile katika msiba wa Vero.
“What is she doing here ? akajiuliza Loniki.
Patrick akafungua mlango wa gari na kushuka huku sura yake ikionyesha wasi wasi
“Hallow Patrick.How are you? Ite been a while “ akasema Loniki huku akilazimisha kutabasamu
“Kweli ni muda mrefu sana hatujaonana Loniki.Karibu sana” akasema Patrick.
Geti lilifunguliwa na Savanna akaliingiza gari ndani.Alipatwa na wasi wasi mwingi kuhusiana na ujio ule wa ghafla wa Loniki
“Karibu ndani Loniki” akasema Patrick na kumuongoza Loniki kuelekea ndani
“Ahsante sana” akajibu Loniki na kumfuata Patrick kuelekea ndani
“wow ! Patrick una nyumba nzuri sana.Hongera” akasema Loniki
“ahsante sana “ akajibu Patrick.Bado aliendelea kuwa na wasi wasi kuhusiana na ujio ule wa ghafla wa Loniki
“Hallow I’m Savanna” Savanna akamsalimu Loniki
“Ouh I’m glad to meet you Savanna.You are Patrick’s lawyer right?
“Yes ! “ akajibu Savanna
“Naitwa Loniki.Ni dada wa Veronika.Nimepita hapa mara moja kuwasalimu na kutoa pongezi zangu kwa Patrick na kuongea naye machache ili tuyamalize yaliyopita na tuanze maisha mapya.” Akasema Loniki na kumfanya Patrick atabasamu
Mara tu alipohakikisha kwamba Loniki ameingia ndani na akina Patrick,Linah akachukua simu yake akaiwasha na kuzitafuta namba za simu za Sarah
“ouh my God naomba nimpate Sarah.” Akawaza Linah huku akibonyeza kitufe cha kupigia simu na simu ikaanza kuita.Iliita mara ya kwanza na kukatika bila kupokelewa. Akapiga tena
“Ouh C’mon Sarah pick up the phone” akasema Linah na mara simu ikapokelewa.
“Hallow Linah.Umepotelea wapi?Nimekutafuta mahakamani sijakuona.Nini kinaendelea ? Mbona hatujawasiliana tena?
Huku akihema kwa nguvu Linah akasema
“Sikiliza Sarah hatuna muda wa kupoteza tena.Loniki yuko hapa nyumbani anakoishi Patrick na Savanna.Ana bastora ameificha na akina Patrick hawajui chochote.She’s going to kill Patrick.Tafadhali fanya kila unaloweza ufike hapa mara moja ila nakuomba tafadhali usipite polisi.Ukija na polisi mambo yanaweza kuwa mabaya zaidi.Tafadhali Sarah fanya haraka” akasema Lnah
“Ouh Mungu wangu ! hebu nielekeze mahala nyumba hiyo ilipo” akasema Sarah huku mwili ukimtetemeka.Linah akamuelekeza mahala nyumba ya Savanna ilipo
“Ahsante Linah nakuja sasa hivi.Na wewe unafanya nini hapo? Kwanini usikimbie kuyanusuru maisha yako?
“Natamani sana nikimbie lakini funguo ya gari anayo yeye na amenifungia ndani ya gari”
“C’mon Linah fanya unavyoweza na uondoke humo ndani ya gari.Lazima Loniki atakuua tu.”
“Siwezi kuondoka Sarah.Nataka nijue kila kinachoendelea hapa.” Akasema Linah
“Sawa Linah ninakuja hapo sasa hivi” akajibu Saraha na kukata simu.Akageuza gari na kuanza safari ya kuelekea mahala alikoelekezwa
Akiwa njiani kuelekea nyumbani kwa Savanna akachukua simu na kumpigia shangazi yake
“Shangazi naomba unisikilize vizuri.Muda huu Loniki yuko nyumbani kwa Patrick .Amekwenda kwa lengo la kumuua na sekunde yoyote kuanzia sasa anaweza akafanya hivyo.Ana bastora ameificha .Shangazi tunatakiwa tumzuie asifanye unyama huo anaotaka kuufanya”
“Hebu nielekeze mahala huko aliko Loniki,mbona anataka kutuletea matatizo mengine makubwa? Akasema shangazi yake kwa mstuko
Sarah akamuelekeza shangazi yake mahala nyumba ya Savanna ilipo.Mara tu alipomaliza kuongea na Sarah simuni mama yake Loniki ambaye alikuwa pembeni yake akamkazia macho na kumuuliza
“Nini kimetokea? Kuna tatizo gani?
“Loniki amekwenda nyumbani kwa Patrick .Anataka kumuua ana bastora”
Mama yake akastuka na kupata nguvu za ghafla akainuka na kuelekea chumbani kwake akafungua kabati lake kubwa la nguo na mara moyo wake ukaanza kwenda mbio
“Ouh Mungu wangu ! Loniki amechukua bastora iliyokuwa humu”
Baada ya kuongea na shangazi yake,Sarah akazitafuta namba za simu za Alois na kumpigia akamfahamisha juu ya tukio hilo
“Please Alois we have to save Patrick.Loniki ana silaha na muda wowote anaweza akamuua ” akasisitiza Sarah
“Sarah nakuja huko sasa hivi” akajibu Alois

* * * *

“Habari za siku nyingi Loniki? Akasema Patrick
“habari nzuri Patrick.Ni muda mrefu sana hatujaonana.Nimerudi juzi na kilichonirudisha ni kuhudhuria siku ya leo”.akasema Loniki halafu kimya kifupi kikatanda
“Patrick mimi si mkaaji sana.Nimeona kabla sijarudi London nipite hapa nikusalimu na kukupa pole kwa matatizo yaliyokupata.Pamoja na hayo….” Lonik akainuka na kuwatazama Patrick na Savanna
“Pamoja na hayo nimekuja pia kukuaga Patrick”
“Are you leaving so soon? Akauliza Patrick
“Yah ! soon I’ll be going but today its you who is going.Patrick I’vecome to kill you” akasema Loniki na kwa kasi ya aina yake akatoa bastora yake na kuwalenga Patrick na Savanna
“Loniki ..!! Unafanya nini? Akauliza Patrick kwa mstuko
“shut up !! akafoka Loniki kwa ukali
Patrick na Savanna wakaangaliana kwa woga.Wote walikuwa wanatetemeka .Macho ya Loniki hayakuonyesha masihara hata kidogo.
“Ouh Mungu wangu mambo gani haya yananitokea? Please help me God.Ee Mungu umekuwa unaniokoa katika kila ovu,naomba usiniache katika hili pia.” Patrick akaomba kimoyo moyo huku mwili ukitetemeka
Mara mtumishi wa ndani akaingia pale sebuleni kwa kasi na sinia la vinywaji bila kujua kilichokuwa kinaendelea,ghafla akastuka baada ya kumuona Loniki amewaelekezea Patrick na Savanna bastora ,sinia la vinywaji likamponyoka na kuanguka chini.Loniki akamgeukia
“Ukijaribu kukimbia nakupiga risasi.Kaa pale na ufanye vile nitakavyokuamuru” Loniki akamwambia kwa ukali yule mtumishi wa ndani ambaye alikuwa anatetemeka.
“Pigeni magoti wote” akaamuru Loniki.
“Loniki please don’t kill us.Nitakupa kiasi chochote cha pesa unachohitaji ….!! “ akasema Savanna huku akitetemeka .Machozi mengi yalikuwa yanamtoka
“Shut up !!..akafoka Loniki na kumtazama Yule mfanyakazi wa ndani
“wewe ! Kata ule waya wa umeme na uwafunge hawa mikono kwa nyuma.!! Loniki akamuamuru yule mfanyakazi ambaye kwa woga aliokuwa nao aliitekeleza amri ile kwa haraka.Akawafunga Patrick na Savanna mikono kwa nyuma kwa kutumia waya
“Loniki tafadali naomba usitudhuru.Tumekukosea kitu gani hadi utufanye hivi?” akaomba Patrick.Kauli ile ikaonyesha uzidi kumpandisha hasira Loniki
“Huna haya mshenzi wewe.Ulimuua mdogo wangu bila kosa.Niliapa kulipa kisasi kwa wale wote walioukatili uhai wa mdogo wangu.I loved her so much.Ni kwa sababu ya mapenzi yangu kwake ndiyo maana niliweka ahadi ya kulipa kisasi.Kifo chake kiliniuma sana.How could you kill her like that? Don’t you have a soul you bastard? She loved you with all her heart and in return you killed her.I cant let you walk again.Ndani ya sekunde kadhaa zijazo utaungana naye mbele za haki mshenzi wewe” akasema Loniki na kumtemea Patrick mate usoni.
“Loniki Patrick hakufanya lolote.Hakumua Veronika.Ngoja nkwambie ukw……” akasema Savanna lakini kabla hajamaliza sentensi yake ukasikika mlio wa risasi.Wote wakaanguka na kulala chini.Taratibu Patrick akafumbua macho ,pembeni yake alikuwa amelala Savanna na damu nyingi zikimtoka
“Savanna !! Savanna !! Savannaaaaa..!!!!! “ akaita Patrick huku akilia
“Hiyo ndiyo adhabu yako kuku wewe.Wewe ndiye uliyeishawishi Mahakama imuachie huru huyu mshenzi.Hii ndiyo hukumu yako” akasema Loniki huku akiusogelea mwili wa Savanna pale chini na kuupiga teke.Patrick alikuwa amelala sakafuni mikono yake imefungwa kwa nyuma hivyo hakuweza kufanya lolote.Pembeni yake mwanamke aliyempenda sana alikuwa amelalia dimbwi la damu.
“shetani wewe !! how could you do this? I’m going to kill you !! “ Patrick akasema ghadhabu.
“Usihofu Patrick.In few minutes you’ll join her” akasema Loniki
Mlio ule wa risasi ulimstua sana Linah aliyekuwa amefungiwa garini
“Ouh Mungu wangu tayari Lonny amemuua Patrick” akasema Linah na kuchukua simu yake akampigia Sarah
“Saraha umefika wapi?
“Tayari nimefika maeneo haya.Ndani ya dakika moja nitakuwa nimewasili hapo nyumbani”
“Hurry up ! Tayari risasi moja imelia ndani”
“Ouh my God ! ..akasema Sarah na kuongeza mwendo wa gari.Mikono yake ilikuwa inamtetemeka.
“Nilisikia uchungu sana kwa kifo cha Vero.Hakuna mtu niliyempenda kama yeye.Nataka ukamjibu ni kwa nini ulimsaliti? Kabla hujamuua aliumia sana moyo wake kwa usaliti uliomfanyia. Mateso na maumivu ya moyo aliyoyapata siku ile nataka uyapate nawe leo hii. You’ll die in agony ..! akasema Loniki
“Lonny ..!! Unafanya nini? Akasema kwa sauti Sarah.Loniki akastuka mno baada ya kumuona Sarah pale.Hasira zikampanda mara dufu
“Lonny please ! naomba tafadhali usimuue Patrick..Dont……!!!! akasema Sarah lakini Loniki akamkatisha
“imekuwa vizuri umekuja mwenyewe ushuhudie namna ninavyo mlipia Vero kisasi.Nataka ushuhudie namna Patrick anavyokufa kwa maumivu” akasema Loniki kwa hasira huku mkono wake ukimtetemeka.
“Loniki tafadhali usimuue Patrick.Please I beg you my sister don’t do that..!!! akaomba Sarah huku akipiga magoti
“Sarah sikutambui tena kama ndugu yangu.I don’t know you anymore.Kwa kitendo chako cha kushirikiana na huyu nguruwe wewe si ndugu yangu.Nakukana duniani na ahera.Nina kuchukia sana na baada ya Patrick itakuwa ni zamu yako wewe na Linah…She betrayed me…!!!!
Bila kusita Loniki akaachia risasi kumuelekea Patrick akaanguka chini pembeni ya Savanna.Mlio ule wa risasi ukawastua Linah na Sarah ambao walianguka chini.Baada ya sekunde kadhaa Sarah aliyekuwa anatetemeka mwili akainua kichwa.Hakuamini alichokiona.Patrick alikuwa ameanguka pembeni ya Savanna akiwa katika dimbwi la damu
“Ouh Mungu wangu ..Lonny umemuua Patrick.Umemuua Patrick.Lonny !!! “ akapiga ukelele Sarah na kuinuka akaanza kupiga hatua kumfuata Loniki.
“Sarah simama hapo hapo,usipige hata hatua moja.” Akasema Loniki kwa ukali
“Are you going to shoot me? Akasema Sarah huku akitembea kumuendea Loniki
“Sarah tafadhali naomba usipige hatua hata moja.I’ll shoot you..!!!!! akasema Loniki kwa ukali
“Sarah usijaribu kumsogelea atakupiga risasi ,anamaanisha anachokisema“ Linah aliyekuwa amejibanza pembeni ya mlango akamuonya Sarah
“Shoot me Lonny.Kama mimi si ndugu yako nipige risasi” akasema Sarah huku akipiga hatua kumuendea Patrick aliyekuwa amelala pale sakafuni
“Sarah don’t force me to kill you.Stay where you are” akasema tena Loniki kwa ukali
“Shoot me ..!!! akasema Sarah huku akiunyanyua mguu wake lakini kabla hajaushusha chini ukasikia tena mlio wa risasi.Sarah akaanguka chini.Alikuwa anavuja damu nyingi.Loniki akaushusha chini mkono wake uliokuwa na bastora.Alikuwa anatetemeka
“gosh !! nimemuua ndugu yangu..!! akasema Loniki na kuitupa chini bastora yake akamkimbilia Sarah aliyekuwa amelala chini damu nyingi ikimtoka
“Sarah..! Sarah..!!! Saraaaahhhh….!! Akaita Loniki kwa sauti kubwa huku akilia.Alimuinua mdogo wake na kumuweka magotini pake huku akilia kwa nguvu.
“Sarah !’m sorry ..!!!..I’m sorry sarah ..!! …Please forgive me ..!! ..Loniki aliendelea kulia kwa nguvu.Pembeni ya mlango Linah alikuwa ameanguka na kuzirai
Mara katika mlango mkubwa wa sebuleni akaingia Aloisi akiwa ameongozana na askari waliokuwa wamevalia fulana za kujikinga na risasi.Sebule yote ilikuwa imetapakaa damu.Watu watatu walikuwa wamelalia damu.Loniki bado aliendelea kulia kwa nguvu.Askari polisi wakaiokota bastora ile ya Loniki aliyokuwa ameitupa pembeni.
Magari mawili ya wagonjwa yakafika haraka sana .Patrick,Savanna,Sarah,Linah na msichana wa kazi wakapakiwa katika magari na kukimbizwa hospitali.Eneo lote lilitawaliwa na vilio wakati miili inatolewa ndani.Loniki alionekana kama mtu aliyechanganyikiwa.Alikuwa anaongea maneno mfululizo yasiyoeleweka.Polisi walifanya uchunguzi wao wa kina ndani ya ile nyumba na wakiwa katika harakati za uchunguzi mara akawasili mama yake Loniki lakini mara tu alipokutana na umati mkubwa wa watu pale nje akaanguka na kupoteza fahamu.
Baada ya kukamlisha uchunghuzi wao askari polisi wakaondoak na Loniki ambaye bado alionean kama my aliyechanganyikiwa.

* * * *

St Patrick hospital moja ya hospitali kubwa na mpya jijini Dar ambayo hivi karibuni serikali imeitangaza kuwa hospitali ya rufaa iligeuka uwanja wa heka heka baada ya majeruhi wa shambulio la risasi kufikishwa pale hospitalini.Haraka haraka walikimbiza katika chumba cha wagonjwa mahututi kwa ajili ya kuokoa maisha yao.Madaktari wote mabingwa wa upasuaji wakaitwa mara moja ili kuongeza nguvu katika kuokoa maisha ya majeruhi wale.
Vipimo vya awali vilibaini kwamba Savanna tayari amekwisha fariki dunia kabla ya kufikishwa pale hospitali.Patrick na Sarah ambao walionekana kuwa hai wakakimbizwa katika chumba cha upasuaji kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji wa dharura.Katika chumba kingine cha wagonjwa wa dharura ,Linah na mfanyakazi wa ndani wa Savanna walikuwa wanaendelea vizuri baada ya kuzimia kutokana na mstuko walioupata.Tayari walikuwa chini ya uangalizi wa polisi kwani ni watu pekee ambao walilishuhudia tukio zima lilivyotokea.
Taarifa za kutokea shambulio la risasi nyumbani kwa wakili maarufu Savanna Francis Kito zilisambaa kwa kasi na kusababisha idadi kubwa ya watu kumiminika St Patrick hospital ili kuhakikisha kuhusu taarifa hizo.Walinzi waliokuwepo getini walizuia watu kuingia hospitalini hapo isipokuwa wale wagonjwa wa dharura
Alois akiwa njiani kuelekea hospitali alipatwa na wazo la kuwapigia nyumbani kwao na kuwafahamisha kilichotokea.Akapunguza mwendo wa gari na kumpigia simu mama yake.
“Hallo Alois mbona umeondoka ghafla na hujaniaga unaelekea wapi?Tunahitaji chupa tatu za shampeni pamoja na bia za kopo.Naomba wakati unarudi ununue vitu hivyo uje navyo.” Akasema mama yale.Alois akavuta pumzi ndefu na kufikiri kwa muda
“Alois umesikia “ akauliza tena mama yake
“mama .!! akaita Alois
“Nini Alois? Kama hutaweza niambie ili nimtume mtu mwingne”
“Si hivyo ,mama ila kuna tatizo limetokea”
“Tatizo gani tena?
“mama hakutakuwa na sherehe yoyote tena” akasema Alois
“Alois mbona unanistua? Kwa nini kusiwe na sherehe?
“Patrick amepatwa na matatizo”
“matatizo ?? mama yake akashangaa
“Ndiyo mama”
“Matatizo gani? Akauliza mama yake kwa wasi wasi.Alois akavuta pumzi ndefu na kusema
“Patrick amepigwa risasi….”
“Ouh Mun………..” kabla hajamliza sentensi yake akaanguka ghafla na kupoteza fahamu
“mama .!! mama..!! mama..!!!!’ akaita Alois lakini hakujibiwa.Akaogopa na kukata simu akampigia mke wake akamuomba amuangalie mama yake.
“mama ameanguka ghafla na amepoteza fahamu.Hatujui tatizo ni nini lakini alionekana alikuwa anaongea na simu kwani simu yake imeanguka pembeni na imesambaratika.Uko wapi Alois? Akasema Sesilia mke wa Alois
“Sikiliza mke wangu” akasema alois
“Kuanzia sasa hivi sitisheni shughuli zote kuhusiana na sherehe mliyokuwa mnaiandaa.Hakutakuwa na sherehe tena.Kitu kingine nakuomba uendeshe gari na mumpeleke mama haraka katika hospitali ya karibu kwa Dr Khan ili apatiwe matibabu ya haraka”
“Alois wewe uko wapi? Akauliza Sesi kwa wasi wasi
“Siwezi kuja huko nyumbani sasa hivi.Kuna jambo limetokea nitakutaarifu baadae.Ukishafika hospitali tafadhali nipigie simu” akasema Alois na kukata simu.Mwili bado uliendelea kumtetemeka
“Mambo gani haya yanatupata katika familia yetu? Hata kabla machungu ya kuondokewa na baba hayajapoa ,tunapatwa na tatizo lingine.Ouh Mungu naomba umponye Patrick.Tafadhali usimchukue kwa wakati huu” akaomba Alois.
Mara tu alipofika hospitali alijitambulisha mapokezi na kuomba kuonana na daktari ili aweze kupatiwa taarifa za maendeleo ya mgonjwa wake lakini alitaarifiwa kwamba kwa muda ule asingeweza kumuona daktari kwa kuwa walikuwa katika chumba cha upasuaji wakijaribu kuokoa maisha ya Patrick na Sarah.Alois akapelekwa katika sehemu ya mapumziko katika ofisi ya mganga mkuu akimsubiri amalize upasuaji .Akiwa amepumzika katika sofa jeusi lililokuwa nje ya ofisi ya mganga mkuu simu yake ikaita.Alikuwa ni mke wake.
“Hallow Secy .Tayari mmefika hospitali?
“Ndiyo Alois tumefika lakini kuna tatizo lingine limejitokeza.Dr Khan amempima akagundua kwamba tatizo la mama ni zaidi ya kupoteza fahamu kwa hiyo ametuandikia tumpeleke katika hospitali ya rufaa ya jeshi pale wana wataalamu wazuri na vifaa na wanaweza wakabaini kwa haraka tatizo la mama.Hivi sasa tuko njiani tunaelekea huko hospitali”
“Ouh Mungu wangu ! kwa hiyo Dr Khan hajasema lolote kwamba linaweza kuwa ni tatizo gani?
“Hapana hajasema lolote isipokuwa ametuandikia makaratasi ya kwenda nayo huko na sijui kaandika nini”
“Unaionaje hali ya mama?
“hali yake haina mabadiliko yoyote”
“Uko na nani hapo karibu?
“Niko na ndugu wengine hapa .Wewe uko wapi? Njoo Alois hali hii mimi inaniogopesha sana” akasema Secilia
“Sesilia naomba uwe na ujasiri hasa kwa wakati huu .Mimi nitakuja lakini kwa sasa niko sehemu fulani.Ukifika hospitali nitaarifu kuna jambo nitakuelezea lakini nataka wakati uko peke yako”
“Alois nini kinaendelea?”
“Nitakwambia baadae.Ukifika hospitali nijulishe” akasema Alois na kukata simu.Jasho lilikuwa linamtiririka
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 61
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Hapana hajasema lolote isipokuwa ametuandikia makaratasi ya kwenda nayo huko na sijui kaandika nini”
“Unaionaje hali ya mama?
“hali yake haina mabadiliko yoyote”
“Uko na nani hapo karibu?
“Niko na ndugu wengine hapa .Wewe uko wapi? Njoo Alois hali hii mimi inaniogopesha sana” akasema Secilia
“Sesilia naomba uwe na ujasiri hasa kwa wakati huu .Mimi nitakuja lakini kwa sasa niko sehemu fulani.Ukifika hospitali nitaarifu kuna jambo nitakuelezea lakini nataka wakati uko peke yako”
“Alois nini kinaendelea?”
“Nitakwambia baadae.Ukifika hospitali nijulishe” akasema Alois na kukata simu.Jasho lilikuwa linamtiririka

ENDELEA………………..

Takribani masaa mawili yamekwisha pita sasa toka Alois alipofika hapa hospitali.Bado Patrick alikuwa katika chumba cha upasuaji.Madaktari walikuwa na kazi ngumu ya kujaribu kuokoa maisha yake na Sarah.Alois alishindwa kukaa akasimama na kuzunguka zunguka .Akiwa bado katika mawazo mengi simu yake ikaita
“Hallow Secy.Nipe habari za huko “ akasema Alois
“Tumemfikisha mama hapa hospitali na tayari madaktari wamempokea na wanaendelea kumfanyia uchunguzi.Hali ya mama si nzuri hata kidogo.Hapa nilipo ninatetemeka.Kwa jinsi anavyoonekana lolote linaweza likatokea.” Akasema Secilia
“Secy be strong my love.Tunapita katika kipindi kigumu sana. Sasa hivi.Just be strong Secy I’ll join you soon”
“Alois kuna jambo gani huko uliko kiasi kwamba huwezi kufika hapa hospitali? Uliniambia kuna jambo unataka kunieleza ni jambo gani hilo?
“Secy tafadhali naomba usipge ukulele wowote na kuwastua watu wengine.Kuna tukio limetokea.Patrick amepigwa risasi” akasema Alois
“Whaaat ….!!!!!!!! Sesilia akastuka na taratibu akaona nguvu zinamuisha akajikuta akikaa chini.Ilimchukua zaidi ya dakika moja Sesilia kuongea tena
“Kapigwa risasi na nani?
“kapigwa risasi na Loniki dada yake Vero.Yeye,Savanna na Sarah wote wamepigwa risasi”
“Ouh gosh..! anaendeleaje? Ni mzima?
Mpaka hivi sasa bado madaktari wanaendelea na upasuaji wakijaribu kuyaokoa maisha yao.Siwezi kusema chochote kwa sasa.Nitakujulisha baadae nini kinachoendelea hapa”
“Alois tafadhali naomba uniambie kama Patrick bado yuko hai” akasema Sesilia
“Sesi siwezi kusema lolote kwa sasa na ndiyo maana nimeogopa kumwambia mtu yeyote kwanza kuhofia yasije yakatokea kama yaliyotokea kwa mama”
“Ulimwambia mama? Akauliza Sesi
“Nilimpigia simu na kumpa taarifa hizi na ndiyo sababu ya kuanguka na kupoteza fahamu”
Sesi alisikika akili simuni na baada ya muda akasema
“promise me Alois that Patrick will be fine” Akasema Sesi
“I don’t know my love.I real don’t know.Tunachotakiwa kufanya kwa sasa ni kumuombea .Nitakupa taarifa zaidi baada ya kuonana na madaktari”
“Alois I’m coming there to join you .Nimepatwa na mstuko mkubwa sana” akasema Sesilia
“Hapana usije huku hospitali.Kaa hapo hapo hospitali baada tu ya kupata taarifa za huku nitakuja huko mara moja” akasema Alois


* * * *

Ni saa mbili za usiku.Happy alikuwa amejilaza sofani akiongeza sauti ya runinga ili aweze kutazama taarifa ya habari.Pamoja naye pale sebuleni alikuwepo mzee Kibaho, na Margreth.Mama yao alikuwa jikoni akisaidiana na Pendo mtumishi wa ndani kuandaa chakula cha jioni
“Pengine.Katika taarifa ya habari ya leo watatangaza maamuzi ya mahakama ya kumuachia huru Patrick” akasema Happy
“Kulikuwa na waandishi wengi wa habari pale mahakamani kwa hiyo nina uhakika mkubwa lazima hii itakuwa ni moja ya habari za leo” akasema Margreth huku akicheka kicheko kidogo
“Wakili maarufu nchini amefariki dunia kwa kupigwa risasi”
“Kenya yaongeza askari wake nchini Somalia”
Hivyo vilikuwa ni vichwa vya habari vilivyosomwa katika muhtasari wa habari.
“Wakili gani maarufu kapigwa risasi? Akauliza Happy na kukaa vizuri ili aitazame vizuri taarifa ile ya habari.
Baada ya muhtasari ule wa habari ikafuata habari kamili
“Wakili maarufu nchini Bi Savanna Francis Kito amefariki dunia kwa kupigwa risasi nyumbani kwake alasiri ya leo.Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi wa kanda maalum ya Dare s salaam,wakili Savanna amepigwa risasi muda mfupi baada ya kuwasili nyumbani kwake akitokea mahakamani ambako alikuwa akimtetea mtu ambaye anadaiwa ni mpenzi wake aliyekuwa anakabliwa na shitaka la kuua bila kukusudia na kumuwezesha kushinda kesi hiyo.Pamoja na Savanna watu wengine waliopigwa risasi na ambao hali zao zinasemekana ni tete ni mpenzi wake Patrick ,pamoja na mtu mwingine aliyejulikana kwa jina moja tu la Sarah.Jeshi la polisi linamshikilia mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina moja tu la Loniki kwa kuhusika na tukio hilo.Enzi za uhai wake,Savanna alikuwa anamiliki kampuni ya uwakili iliyojizolea sifa kemkem ndani na nje ya nchi kutokana n uamahiri wake wa kusimamia kesi kubwa kubwa.Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peoni Amina
Mara tu taarifa ile ilipomalizika,kila mtu pale sebuleni hakuamini alichokitazama.Ghafla kikasikika kishindo Happy alianguka na kupoteza fahamu.Kikaibuka kizaa zaa kingine pale sebuleni.Margreth alipiga kelele kubwa na kumstua mama yao aliyekuwa jikoni ,akatoka mbio na kuja sebuleni na kumkuta mwanae akiwa amelala chini hana fahamu.Mzee Kibaho akaendelea kumpatia huduma ya kwanza.Wote kwa pamoja wakashirikiana kumpatia Happy huduma ya kwanza ili azinduke.
Hatmaye baada ya jitihada kubwa za wote pale sebuleni Happy akazinduka.Mama yake akamkumbata kwa nguvu.
“Mama wamemuua Patrick….Patrick amepigwa risasi..!!.Ouh Patr…….” Happy akaangua kilio
“Usilie Happy.Nyamaza kulia .Patrick bado yuko hai,hajafa” akasema mzee Kibaho
“Patrick amekufa? Akauliza kwa mshangao mama yake Happy
“Patrick na Savanna wamepigwa risasi alasiri ya leo baada ya kufika nyumbani kwao wakitokea mahakamani.Savanna yule wakili wake amefariki dunia na Patrick hali yake inasemekena si nzuri.” Akasema mzee Kibaho.Mke wake akashika kichwa kwa mikono yake
“Ouh Jamani.! Nani amefanya ukatili wa namna hii? Savanna amekufa? Hata siamini” akasema mama yake Happy
“Mama nitampata wapi Patrick? Wamemuua mpemzi wangu.Wamemuua Patrick..why they killed him?...Happy akaendelea kulia
“Happy Patrick hajafa.” Akasema mzee Kibaho akijaribu kumtuliza mwanae
“Patrick is dead.They killed him.I need to die too…” akasema Happy
“Happy taarifa ile inasema kwamba aliyethibitishwa kufa mpaka sasa hivi ni Savanna lakini Patrick na mtu mwingine wao bado wazima ingawa hali zao si nzuri.Kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa Patrick akapona.Nyamaza kulia mwanangu na tumuombee Patrick” akasema mzee Kibaho ambaye hata naye alikuwa anatetemeka kwa ndani.Alisikia uchungu mkubwa sana.
“dady take me to hospital..I need to confirm this..” akasema Happy huku akiinuka.lakini miguu yake haikuwa na nguvu akaanguka .
“Pumzika Happy.Hali yako si nzuri .Naomba uniamini nikwambiayo,Patrick hajafa.Tulia na kesho asubuhi tutafuatilia taarifa hizi” akasema mzee Kibaho
Happy hakujibu tena.Aliendelea kulia.Familia nzima ilikuwa kimya na kila mmoja alikuwa anawaza lake.Taarifa ile iliwastua sana.Margreth alikuwa amekaa chini.Hakuweza kuongea lolote.Ni machozi tu ndiyo yalikuwa yanamtoka.Alimfahamu Patrick kwa muda mrefu sana.Alifahamu ni namna gani alivyokuwa mtu muhimu kwa dada yake Happy.Alivuta kumbu kumbu na kukumbuka sura ya Patrick pale mahakamni.Kila alipoikumbuka sura ya Patrick na Savanna machozi yalizidi kumtoka.Mama yao naye alikuwa amekaa sofani akitoa mchozi.
“Siku zote nilikuwa namsema vibaya sana Patrick.Nilimuona kama mtu mbaya aliyekuwa akimsababishia mabalaa mwanangu Happy.Masikini Patrick nani lakini aliyemfanyia unyama huu ? Alikuwa ni kijana mpole na asiye penda ugomvi na mtu.Alimpenda sana Happy hadi akaamua kukaa gerezani badala yake.Happy atakuwa katika wakati mgumu sana kwani najua pamoja na yote yaliyotokea lakini bado anampenda mno Patrick.Kama Patrick atafariki maisha yake hayatakuwa na furaha tena”
Akawaza mama yake Happy huku akimtazama mwanae Happy aliyekuwa amekaa juu ya zulia akiendelea kulia.Mzee Kibaho alijitahidi kutokuwaonyesha mstuko alioupata na kuendelea kuwapa moyo familia yake lakini kwa ndani alikuwa anatetemeka.Alitoka pale sebuleni na kuelekea chumbani kwake Akatoa kitambaa na kujifuta machozi.Alibaki amesimama kwa takribani dakika mbili akiangalia juu.Kichwa chake kilijaa mawazo mengi.
“Ouh Jamani nani huyu ambaye amemfanyia Patrick jambo baya kama hili ? nani huyu anayetaka kumuua Patrick.Namfahamu yule kijana hana ugomvi na mtu yeyote kwa nini basi afanyiwe kitendo cha kinyama kama hiki? Mungu wangu naomba umponye Patrick.Usimchukue sasa hivi” akawaza mzee Kibaho na kukumbuka kitu alichokuja kuchukua mle chumbani.Akafungua kabati lake dogo na kuchukua vidonge viwili vya usingizi na kurejea sebuleni akampatia Happy.Lengo lake lilikuwa kumsaidia Happy ili aweze kulala.Happy akazipokea dawa zile akameza na kisha mzee Kibaho akamshika mkono akampeleka chumbani kupumzika na kisha kurejea sebuleni.Mara simu ya Margreth ikaanza kuita.Aliitazama simu ile ikiita lakini hakuwa na nguvu za kuinuka mahala alipokaa na kwenda kuipokea .Mzee Kibaho akaichukua na kutazama mpigaji.Alikuwa ni Mike
“Hallow Mike” akasema mzee Kibaho
“Ouh kumbe ni wewe baba, shikamoo”
“marahaba Mike,habari za huko?
“Habari za huku nzuri.habari za Tanzania?
“Tanzania kwema tu”
“baba,Margreth uko naye karibu?
“Mike,Margreth yupo lakini ameshindwa kupokea simu yako muda huu.Kuna matatizo yametokea”
“matatizo gani baba? akauliza Mike kwa wasi wasi
“Ni kuhusu Patrick”
“Patrick amefanya nini? Happy aliniambia kwamba leo ilikuwa ni hukumu yake.Amehukumiwa kifungo?
“Patrick hajafungwa.Mahakama imemuachia huru “
“Hizo ni habari njema sana.Nini basi kimemtokea?
“Patrick amepigwa risasi” akasema mzee Kibaho.Kimya kikatanda simuni .Baada ya muda Mike ambaye sauti yake ilionyesha mstuko mkubwa akauliza
“Nani kafanya tukio hilo?Vipi hali yake?
“Mpaka sasa hivi kuna mtu mmoja ambaye anashikiliwa na polisi na inaaminika ndiye aliyefanya tukio hilo.Hali yake bado haijulikani lakini kwa kujibu wa taarifa iliyopatikana toka hospitali alikokimbizwa ni kwamba hali yake ni mahututi na madaktari wanajitahidi kujaribu kuokoa maisha yake.”
“Ouh Mungu wangu.!!!! Happy yuko wapi? Amekwisha zipata taarifa hizi?
“Ndiyo amezipata taarifa hizi .Alistuka na kupoteza fahamu.Hivi sasa nimempa dawa za usingizi amelala.Mike nadhani ingekuwa vyema kama tungewasiliana kesho kwa sababu kwa sasa watu wote bado tuko katika taharuki” akasema mzee Kibaho
“Ahsante baba.Nashukuru sana kwa taarifa.Poleni sana.Tafadhali naombeni mnitaarifu kila kinachoendelea na kama kuna kitu ninaweza kusaidia.Nimestushwa sana na taarifa hizi”
‘Usijali Mike tutakufahamisha” akasma mzee Kibaho na kukata simu

* * * *

Mlango wa chumba cha upasuaji ulifunguliwa na kitanda cha magurudumu kikatolewa na kupelekwa katika jingo la wagonjwa wa uangalizi maalum.Ilikuwa ni saa tatu na robo za usiku.Upasuaji aliofanyiwa Patrick ulichukua muda mrefu kukamilika
Alois bado alikuwa katika ofisi ya mganga mkuu akisubiri upasuaji umalizike ili ajue kinachoendelea.Akiwa bado amejiinamia akitafakari mara akatokea daktari mkuu akiwa ameongozana na maafisa watatu wa polisi.
“natumai utakuwa ndugu Alois” akasema daktari yule bingwa huku akimpa mkono Alois
“Ndiye mimi dokta” akajibu Alois.
“Nimepewa taarifa zako kule chini.Pole sana kwa kunisubiri kwa muda mrefu.Karibu ofisini” akasema daktari na Alois pamoja na wale maafisa wa polisi wakaingia ofisini
“Ndugu zangu huyu hapa ni Alois .Kwa taarifa nilizopewa ni kwamba yeye ni ndugu wa Patrick yule majeruhi tuliyemaliza kumshughulikia hivi punde.Alois hawa ni maafisa wa polisi wakiongozwa na mkaguzi Ernest Kengele” Dokta Ezekiel majala akafanya utambulisho mfupi halafu akaendelea
“Ndugu zangu nimewaiteni hapa kuwapeni taarifa ya awali ya maendeleo ya wagonjwa walioletwa hapa.Tulipokea watu watano watatu kati yao walikuwa wamejeruhiwa vibaya sana kwa risasi ,mmoja kati ya hao waliojeruhiwa alikuwa amekwisha fariki.Jina lake ni Savanna .Alifariki kabla hata ya kufikishwa hapa hospitali.Wagojwa wengine wawili hawakuwa na majeraha yoyote isipkuwa walikuwa wamepoteza fahamu kutokana na mstuko.Hawa tuliwapatia msaada na tayari wamekwisha zinduka na wanaisaidia polisi hivi sasa.” Akasema Dr Ezekiel akawatazama watu wote mle ofisini na kuendelea
“Wagonjwa wawili waliokuwa wamejeruhiwa vibaya sana kwa risasi tuliwafanyia upasuaji.Mmoja ambaye ni mwanamke alikuwa amepigwa risasi katika bega la kushoto. Kwa bahati nzuri haikuweza kuleta madhara makubwa.Patrick yeye ndiye aliyekuwa amejeruhiwa vibaya sana.Nadhani lengo la mtu aliyemshambulia lilikuwa ni kumuua kwani alilenga kuupiga moyo lakini kwa bahati nzuri risasi ilipita pembeni kidogo ya moyo na hivyo kujeruhi baadhi ya msihipa..Tunaendelea kumuangalia kwa karibu zaidi na endapo italazimika kufanya tena upasuaji mwingine basi tutafanya hivyo lakini kwa sasa siwezi kusema lolote kwani tumuweka katika mashine ya kumsaidia kupumua.Ninapenda kuwahakikishia kwamba tutafanya kila tuwezalo ili kuokoa maisha yake..” Akasema Dr Ezekiel.

* * * *

Baada ya kutoka hospitali alikolazwa Patrick,Alois akaeleka moja kwa moja katika hospitali ya jeshi alikopelekwa mama yake.Nje ya hospitali ile alikutana na kundi kubwa la akina mama na ndugu wengine waliofika pale baada ya kupata taarifa za kilichotokea.Wengi wao walikuwa wanatokwa na machozi.Alois akawasalimu na walitaka kujua kilichokuwa kinaendelae huko alikotoka kwani tayari taarifa zilikwisha sambaa kwamba Patrick amepigwa risasi.Aliwaeleza hali ya Patrick ilivyo na kuwapa moyo .
“Vipi maendeleo ya mama? Kuna taarifa zozote toka kwa madaktari?Alosi akamuuliza mke wake
“Mpaka mida hii bado hakuna taarifa zozote tulizopewa ,bado madaktari wanaendelea kumfanyia uchunguzi wa kina kujua tatizo lake na wametuomba tuwasubiri hapa” Akasema Secilia.Alois akainamisha kichwa.Alihisi kuchanganyikiwa.
“Alois ni nani aliyempiga Patrick risasi? Tayari amekamatwa? Akauliza Secilia
“Kwa mujibu wa polisi mpaka sasa hivi wanawashikilia watu watatu ambao walikutwa eneo la tukio lakini aliyefanya tukio hilo ni Loniki dada yake Vero.Nasikitika sikuwahi kufika mapema eneo la tukio pengine ningeweza kulizuia tukio hili lisitokee”
“Ulitaarifiwa kuhusu tukio hilo? Akauliza Secilia huku akionekana kushangaa
“Muda mfupi kabla ya tukio kutokea,Sarah alinipigia simu na kunitaarifu kwamba niende haraka nyumbani kwa Savanna kwani Loniki alikuwepo kule na alikuwa amedhamiria kumdhuru Patrick.Niliondoka nyumbani haraka bila kuaga au kumwamba mtu yeyote na nilipofika eneo la tukio tayari Loniki alikwisha fanya alichotaka kukifanya”
“Loniki mwenyewe amekamatwa? Akauliza Secilia huku akimuma meno kwa hasira
“Naye ni miongoni mwa watu wanaoshikiliwa na jeshi la polisi” akasema Alois halafu wote wakakaa kimya baada ya kutolea daktari ambaye aliwataka ndugu wa karibu wa mgonjwa wamfuate ofisini.Alois,Secilia na akina mama wengine wawili wakaongozana na daktari hadi ofisini kwake.
“Poleni sana ndugu zangu kwa matatizo” akaanzisha mazungumzo daktari
“Ndugu zangu nimewaiteni ili niwape taarifa kuhusu mgonjwa wenu.Tumempokea mgonjwa akiwa katika hali ya kutokujitambua na tumemfanyia uchunguzi ili kujua tatizo lake.Tumegundua kwamba mgonjwa wenu amepatwa na tatizo la kupooza upande wa kulia.”
“Ouh Mungu wangu …!! Alois akastuka na kushika kichwa chake.Hakuwa ametegemea taarifa ile.Secilia alishindwa kujizuia akaangua kilio.Mmoja wa akina mama akamtoa nje
“Poleni sana ndugu zangu lakini huu ni ugonjwa wa kawaida na unaweza kumpata mtu yeyote na hasa watu ambao umri wao ni mkubwa .Tayari tumekwisha muanzishia matibabu na msiwe na wasi wasi .Hapa tunao madaktari bingwa wa magonjwa haya na nina imani atapona na kurejea katika hali yake ya kawaida” akasema daktari.


* * * *

Saa kumi na mbili za asubuhi tayari Happy alikwisha amka.Alilala usingizi mzito kutokana na dawa za usingizi alizokuwa amepewa.Familia nzima ilikwisha amka mapema na kujiandaa kwa ajili ya kwenda hospitali kufuatilia hali ya Patrick.Walipokuwa tayari wakaingia garini na kuondoka kuelekea hospitali
“Ee Mungu naomba msaidie Patrick apone.Naomba usimchukue mapema .Ni mwanaume wa pekee kabisa hapa duniani.Bado tunamuhitaji mno katika maisha yetu.Please Lord help me,don’t take Patrick now”” Happy alikuwa anaomba kimya kimya wakati wakielekea hospitali
Waliwasili hospitali na kukuta kundi kubwa la watu waliokuwa wamekuja kuwaona ndugu zao waliolazwa hapo hospitalini.Hawakujua ni wapi wangeweza kupata taarifa za maendeleo ya Patrick.Mzee Kibaho akaenda mapokezi akaongea na wauguzi waliokuwapo pale na kuelekezwa katika jengo ambalo ni maalum kwa wagonjwa walio mahututi.Haraka haraka mzee Kibaho na familia yake wakaelekea upande ule.Kulikuwa na idadi kubwa ya watu ambao walikuwa wamesimama nje ya jengo lile.Wakiwa wamesimama pale nje mara Alois akatoka ndani ya lile jengo.Ndugu ,jamaa na marafiki waliokuwepo pale kufuatilia hali ya Patrick wakamzunguka.Alois alionekana kuwa na haraka.Aliwatuliza watu wale waliokuwa wamemzunguka na kuwaambia kwamba Patrick alikuwa anaendelea vizuri kisha akawaacha watu wale na kuanza kutembea kwa kasi.Happy akamkimbilia na kumuita
“Alois .!!!” alois akageuka na kukutana na sura iliyosawajika ya Happy
“ Happy ..!!! akasema Alois kwa mshangao.Mara moja familia nzima ya Happy ikamfuata.Alois akasalimiana nao wote
“Pole sana Alois “ akasema mzee Kibaho
“Tumekwisha poa mzee “ akajibu Alois
“Vipi maendeleo ya Patrick? Akauliza Happy
“Hali yake si mbaya sana kwa mujibu wa madkatari ingawa bado yuko katika mashine ya kumsaidia kupumia.” Akasema Alois
“My God please save him “akasema Happy huku akishindwa kujizuia kuangusha machozi
“Usihofu Happy.Tunatakiwa tumuombee sana” akasema alois
“Aliyefanya unyama huu tayari amekamatwa? Akauliza kwa hasira mzee Kbaho
“Ni Loniki dada yake Vero.Tayari anashikiliwa na jeshi la polisi pamoja na watu wengine wawili.” Akasema Alois na kuchukua namba za simu za mzee Kibaho kwa ajili ya mawasiliano.Kabla hajaondoka Happy akamuuliza
“Alois is there anything I can do to help? Akauliza Happy.Alois akasita kidogo halafu akajibu
“Happy nashukuru sana lakini kwa sasa naomba upumzike nitakapokuhitaji nitakutaarifu”
“Alosi I need to help.Patrick is my friend.He’s here ni my heart.Please let me do something for him” akasema Happy huku akilia
Alois akafikiri kidogo na kusema
“Ok Happy.Ahsante sana kwa msaada wako.Hivi tunavyoongea mama yetu amelazwa hospitali amepatwa na tatizo la kupooza upande mmoja baada ya kupata taarifa za Patrick kupigwa risasi.Naomba uende pale na usaidiane na wale akina mama wanaoendelea kumuuguza .I know you are strong woman.Wengi wao wanashindwa kuvumilia wakimuona mama.Ninaimani utawapa moyo na kuwatuliza.Pale utamkuta Secilia mke wangu mimi nitakuja baadae natakiwa kituo cha polisi” akasema Alois.Familia ya Happy wakaonekana kustushwa na taarifa ile ya ugonjwa wa mama yake Patrick
“Alois nashukuru sana kwa nafasi hii.Ninaelekea huko sasa hivi.As far as I’m doing this for Patrick I’l be strong” akasema Happy huku akifuta machozi
“Ahsante sana Happy.Nitampigia simu Secilia ambaye yuko kule toka alfajiri kumfahamisha.Utasaidiana naye kwani yeye ndiye niliyemkabidhi majukumu yote ya kule” akasema Alois na kumpatia Happy namba za simu za Secilia na kuodoka.Happy na familai yake nao wakaondoka


* * * *

Saa tatu za asubuhi Alois akawasili katika kituo cha polisi kama alivyokuwa ameombwa.Saa nne za asubuhi akaitwa katika ofisi ya upelelezi.
“Alois nimekuita hapa ili kukupa taarifa za awali kuhusiana na uchunguzi wa tukio la jana.Jeshi la polisi hadi hivi sasa linawashikilia watu watatu .Mmoja anaitwa Linah na mwingine ni Loniki na mwingine ni mfanyakazi wa ndani wa Savanna aitwaye Chiku.Linah na huyu mfanyakazi wa ndani wa Savanna ambao hali zao zinaendelea vizuri wataletwa hapa kwa ajili ya mahojiano.Loniki tunaendelea kumshkilia hapa kituoni toka jana ingawa anaonekana kama ni mtu aliyechanganyikiwa.Tunafanya utaratibu wa kumfanyia uchunguzi wa wa kina wa akili yake.Jeshi la polisi litampeleka katika hospitali kuu ya magonjwa ya akili .Pamoja na hayo bado tunandelea na uchunguzi wetu wa kina ili kubaini wale wote waliohusika katika tukio hili.Nashukuru sana kwa ushirikiano wako na endapo utakuwa na taarifa nyingine zaidi ambazo zitaweza kutusaidia tafadhali usisite kutufahamisha mara moja” akasema Inspekta Kengele na baada ya mahojiano kidogo Alois akaondoka
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 62
MTUNZI: PATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Loniki tunaendelea kumshkilia hapa kituoni toka jana ingawa anaonekana kama ni mtu aliyechanganyikiwa.Tunafanya utaratibu wa kumfanyia uchunguzi wa wa kina wa akili yake.Jeshi la polisi litampeleka katika hospitali kuu ya magonjwa ya akili .Pamoja na hayo bado tunandelea na uchunguzi wetu wa kina ili kubaini wale wote waliohusika katika tukio hili.Nashukuru sana kwa ushirikiano wako na endapo utakuwa na taarifa nyingine zaidi ambazo zitaweza kutusaidia tafadhali usisite kutufahamisha mara moja” akasema Inspekta Kengele na baada ya mahojiano kidogo Alois akaondoka

ENDELEA……………

Saa saba za mchana katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere ndege ya shirika la ndege la Afrimerica linalofanya safari zake kati ya nchi za Amerika na Afrika ikatua.Miongoni mwa abiria walioshuka katika ndege hiyo ni bwana na bibi Francis serverine Kito wakiambatana na binti yao Maria.Hawa ni wazazi wa Savanna.Wote walikuwa na sura za majonzi sana
Familia ya mzee Francis Kito imekuwa ikiishi nchini Marekani kwa muda mrefu sasa ambako waanamiliki biashara kadhaa kubwa.
Kisha shuka ndegeni familia hii ililakiwa na vilio toka kwa ndugu na jamaa waliokuwepo pale uwanjani kuwapokea..Toka uwanja wa ndege msafara wa magari ukaelekea moja kwa moja nyumbani kwao Mbezi ambako ndiko kulikuwa na msiba wa Savanna.Watu walikuwa ni wengi sana.Savanna alifahamika na watu wengi katika kipindi kifupi alichofanya kazi yake ya uwakili.Alijizolea sifa kemkem ndani na je ya nchi kutokana na umahiri wake katika sheria.Baada ya kuwasili nyumbani kwao ,eneo lote lilitawaliwa na vilio.Watu wengi ilikuwa ni mara ya kwanza kuwaona wazazi wa Savanna.Wengi wa marafiki na hata watu wa karibu yake hawakufahamu kama wazazi wa Savanna wanaishi nchini Marekani na ni watu matajiri na wenye uwezo mkubwa .Siku zote Savanna kupenda kuweka wazi kuhusiana na familia yake.Hakupenda kujivuna kwa utajiri wa familia yake na siku zote alipambana ili apate mafanikio kuwa nguvu zake na kwa kiasi kikubwa alifanikiwa katika hilo.
Baaa ya vilio kupungua,kikaitishwa kikao cha ndugu kwa ajili ya kuanza maandalizi ya mazishi.Mpaka wakati huo bado mwili wa Savanna haukuwa umekabidhiwa rasmi kwa familia yake Jeshi la polisi liliendelea na uchunguzi wake.

* * * *

Alois alikuwa amesimama huku mkono mmoja akiwa ameuegemeza katika nguzo.Kichwa chake alikuwa amekiinamisha chini.Alikuwa na mawazo mengi.
“Alois ..!! akaita mke wake aliyekuwa amekaa pembeni yake akiwa na Happy wakisubiri mgonjwa aliyekuwa katika chumba cha vipimo
“Alois ! akaita tena Secilia lakini Alois alionekana kuwa mbali sana kimawazo.Secy akamsogelea na kumshika bega.
“Usiwaze sana Alois.Mungu yupo atatusaidia na tutakivuka kipindi hiki kigumu
“Nashindwa kujizuia kuwaza Secy.Hali za mama na Patrick bado ni tete.Mimi ndiye mkubwa wa familia niliyebaki lazima kichwa kiniume lazima niwaze” akasema Alois.Mke wake akamtazama kwa macho ya huruma na kusema
“Alois nadhani ni vyema niende kwanza nyumbani nikawatazame watoto kwa sababu toka nilipoondoka asubuhi sijui wako katika hali gani.Utabaki hapa na Happy” akasema Secy
“Ahsante sana mke wangu .Nashukuru umekumbuka hata watoto.Kwa sasa mimi akili yangu yote inawaza wagonjwa wangu.Funguo hizi hapa za gari mimi nitatumia gari la Happy si amekuja nalo?
“Ndiyo amekuja na gari” akajibu Secy
“Endapo kutakuwa na mabadiliko yoyote sintakutaarifu mara moja” akasema Alois
Baada ya Secy kuondoka Alois akaenda kukaa katika sofa alilokuwa amekaa Happy ambaye michirizi ya machozi ilionekana mashavuni mwake.
“Happy usilie.Huu ni wakati ambao tunatakiwa kuwa majasiri na kumuomba sana Mungu ili wagonjwa wetu waweze kupata nafuu.” Akasema Alois
“Alois kuna nyakati ninashindwa kuvumilia kutokwa na machozi.Patrick ni mtu wangu wa muhimu sana japokuwa mambo mengi yametokea kati yetu lakini yeye bado ni mtu mwenye nafasi kubwa na ya pekee kabisa moyoni mwangu.He’s my first man to love na sijawahi kumpenda mtu mwingine yeyote kama ninavyompenda yeye.Naomba nikiri kwako Alois kwamba bado ninampenda sana Patrick kwa moyo wangu wote na ndiyo maana ninaumia sana moyoni kwani sikupata nafasi ya kukaa naye na kuongea mambo kuhusu mambo yaliyotokea kati yetu.Alois tell me Patrick wont die because I need to tell him the truth” akasema Happy na kuanza kulia
“Nyamaza kulia Happy.Patrick is strong and a fighter.He will fight this.He’ll live for us who love him so much.Ni ukweli gani unaotaka kumweleza?
Happy akafuta machozi na kusema
“Toka nimerudi nimekuwa nikitafuta nafasi ya kukutana naye ili nimweleze ukweli kuhusiana na kilichotokea kati yetu lakini imeshindikana kwa sisi kukutna tena kwa sababu Patrick ana hasira na mimi .Please Patrick fight for your life.I need you back.You need to hear the truth.” Akasema Happy
“Happy ni jambo gani hilo ambalo ulitaka kumweleza Patrick.You can tell me” akasema Alois
“Ni kuhusu zile picha zangu zilizosambazwa magazetini na mitandaoni ambazo ndizo chanzo cha mimi na Patrick kutengana tena”Alois akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Kuna nini kuhusu zile picha?
Happy akafuta machozi na kusema
“Unakumbuka siku ile ambayo mlinikuta gerezani na mama akanitolea maneno ya ukali na akanifukuza?
“Ndiyo nakumbuka siku ile.Kitendo kile cha mama hata mimi sikukifurahia”
“Basi nilipondoka pale gerezani nikiwa katika daraja la Kigamboni nikirejea,nilitekwa na watu nisiowajua .Walinifunga kitambaa usoni na kunipeleka mahala nisipopajua.Waliniweka katika chumba kimoja kikubwa..Niliambiwa kwamba kuna mtu ambaye aliwatuma kufanya kazi ile na kwamba natakiwa nifanye anavyotaka mtu huyo ama sivyo Patrick angeuliwa .Walisema kwamba kuna mtu ambaye ameandaliwa gerezani na ana chakula chenye sumu kali na andapo ningekataa kufanya wanavyotaka basi Patrick angeuawa.Waliniambia ili nimuokoe Patrick asife kwa sumu lazima nifanye mapenzi na watu wawili.Sikuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya kukubali kwa kuwa sikujua kama walikuwa wananiambia kweli au walikuwa wanatania.Nilifanya mapenzi na watu wale bila kujua kwamba walikuwa wananirekodi na kunipiga picha.Kesho yake picha zilitoka magazetini na video ile kusambazwa mitandaoni.Niliumia sana Alois.Nilifahamu kwamba lengo la watu wale lilikuwa kunidhalilisha.Nilifadhaika sana.Nilikata tamaa ya kuendelea kuishi nikaamua kunywa sumu ili niondoke duniani lakini haikuwa mipango ya Mungu nife mapema.Nilikimbizwa hospitali nikatibiwa na kupona.Namshukuru sana Savanna kwani ni yeye ambaye alinishauri niende kupumzika nje ya nchi ili kuiepuka aibu kubwa niliyoipata.Nilikubali na kuona ndiyo njia pekee kwa wakati ule.I was so stupid to run away and leave Patrick alone.Alinikodishia ndege hadi Rwanda pamoja na kulipia gharama zote za hoteli kubwa niliyokaa .Toka pale Kigali nilienda kuishi nchini Marekani ambako bado ninaishi hadi hivi sasa.Nimerudi Tanzania kwa lengo moja tu la kutoa ushahidi wangu katika kesi hii ya Patrick.Nimekuwa nikitafuta nafasi ya kuonana na Patrick ana kwa ana na kuongea iliniweze kumueleza ukweli ulivyo lakini imekuwa ngumu sana kuonana naye.Kinachonisikitisha zaidi ni kwamba tayari Patrick ananichukia sana kwa kudhani kwamba nilifanya kitendo kile kwa kukusudia .Ni kweli naweza kuwa nilifanya makosa kuondoka na kumuacha peke yake gerezani na kwa muda huu wote sijawahi hata kumtafuta na kumueleza ukweli halisi lakini najua sikufanya kitendo kile kwa makusudi.Nilifanya vile kwa ajili ya kumlinda yeye mwenyewe.Sikujua kama watu wale walioniteka na kuniamuru nifanye vile walikuwa wanatania au vipi.Mimi ni msichana ninayejiheshimu sana na katu siwezi kutenda matendo kama yale kwa hiari yangu. ” Akasema Happy na kumuacha Alois akishangaa
“Happy ! kwa nini hukusema toka mapema kuhusu jambo hili na umesubiri hadi hivi sasa? Kwa nini usingeweka wazi ili uchunguzi ufanyike mara moja na wahusika waweze kubainika na kufikishwa katika mikono ya sheria? Nikweli Patrick aliumia sana kwa kitendo kile na hasa ulipoondoka bila kutoa taarifa yoyote.Aliteseka mno na kukata tamaa ya kuishi tena baada ya kupelekewa picha zile gerezani.Ulifanya kosa kubwa kuondoka.Hivi ni visa toka kwa maadui zenu na ulipaswa usimame imara na upambane.Hukutakiwa kukimbia na kumuacha Patrick peke yake na kumfanya aamini kwamba ulifanya kitendo kile kwa makusudi kabisa.Kitendo cha kukimbia kimewapa ushindi maadui zenu ambao hawapendi kuwaona mkiwa pamoja.Lengo lao limefanikiwa na kwa hivi saa hamko pamoja tena.…Ouh gosh ..!!” akasema Alois
“Nilikuwa nafikiria sana kuhusu kusema ukweli lakini kila nilipofikiria kufanya hivyo nilishindwa kwa sababu siwafahamu watu hao waliofanya kitendo kile na nilidhani nisingeweza kuliweka wazi jambo hili kwa jamii ikanielewa hivyo nikaona ni bora niliache tu kama lilivyo.” Akasema Happy.Alois akatoa simu yake na kumpigia Inspekta Kengele
“Hallow Alois” akasema Kengele baada ya kupokea simu
“Samahani kwa kukusumbua afande,kuna taarifa nimeipata sasa hivi toka kwa msichana mmoja aitwaye Happy Kibaho aliyewahi kuwa Miss Tanzania na mpenzi wa Patrick”
“Taarifa gani hiyo Alois?
“Amenieleza kwamba aliwahi kutekwa na watu wasiojulikana akapelekwa sehemu ambayo haifahamu na kulazimishwa kufanya mapenzi na watu wawili kwa madai kwamba asipofanya hivyo Patrick angeuawa.Ili kumnusuru Patrick ambaye kwa wakati huo alikuwa gerezani Happy alikubali kufanya walivyotaka hao watu na kumbe wakati akifanya mapenzi na watu hao walikuwa wakimrekodi na kumpiga picha na kisha kuzisambaza katika vyombo vya habari na kwenye mitandao ya kijamii.Nimeona nikupe taarifa hizi kuhusu jambo hili pengine waliomfanyia hivi Happy ndio hao hao waliotaka kumuua Patrick” akasema Alois
“Ahsante sana kwa taarifa Alois lakini hata sisi tayari tumeipata taarifa hiyo”
“Mmeipata taarifa hiyo? Alois akashangaa
“Ndiyo Alois.Kuna mwanamke mmoja anaitwa Linah ambaye tunamshikilia kuhusiana na tukio hili lililotokea.Huyu tulimkuta katika eneo la tukio akiwa hana fahamu.Baada ya mahojiano,Linah amekiri kwamba Loniki ndiye aliyehusika kuratibu mambo yote hayo na hata kutekwa kwa Happy na kufanyiwa kitendo hicho alichofanyiwa.Anekiri kwamba Loniki ndiye aliyemuua Savanna na kuwajeruhi Patrick na Sarah kwa risasi kwa lengo la kulipiza kisasi kwa kifo cha mdogo wake Vero.Hivi sasa tunamtafuta mtu mmoja anayefahamika kwa jina moja tu la Khumalo ambaye amekimbia na hajulikani alipo.Huyu inasemekana ni mfanyabiashara wa madawa ya kulevya na amekuwa akijihusisha vile vile na vitendo vya ujambazi pamoja na kuwachezesha mabinti wadogo filamu za ngono na kwenda kuziuza nje ya nchi.Khumalo ndiye aliyefanikisha kutekwa kwa Happy na kufanyiwa udhalilishaji ule mkubwa.Kwa sasa tunaelekeza nguvu zote kumtafuta yeye tukishirikiana na polisi wa kimataifa.Tutamuhitaji Happy baadae kwa ajili ya mahojiano ya kina kuhusiana na kilichotokea.” Akasema Inspekta Kengele
“Ahsante sana kwa taarifa hizo afande.Happy niko naye hapa nitakuja naye kituoni hapo baadae”
“Ahsante Alois.Tutazidi kufahamishana kama kuna jambo lolote litajitokeza” akasema Kengele na kukata simu.Alois akavuta pumzi ndefu
“ayari polisi wana taarifa hizo na wamekwisha mfahamu mtu aliyefanya kitendo kile” akasema Alois
“Wamemfahamu? Ni nani huyo shetani aliyenidhalilisha namna ile na kunitenganisha na Patrick ? Nani kawapa taarifa hizo? Akauliza Happy
“Kuna mwanamke mmoja anaitwa Linah ambaye naye alikutwa eneo la tukio akiwa amezimia.Baada ya kuhojiwa amekiri kwamba Loniki ndiye aliyeratibu mpango mzima wa kutaka kumuua Patrick na hata kutekwa kwako na kufanyiwa kitendo kile.Lengo lake likiwa ni kutaka kulipiza kisasi kwa kifo cha mdogo wake Vero”
“Ouh jamani kwa nini lakini afanye vile” akauliza Happy kwa hasira
“Alitaka kulipiza kisasi kwa kifo cha mdogo wake.Polisi pia wanamtafuta mtu mmoja aitwaye Khumalo ambaye ndiye aliyefanikisha mpango huo .Inasemekana Khumalo amekuwa akiwachezesha filamu za ngono wasichana wadogo na kwenda kuziuza nje ya nchi” akasema Alois na Happy akashindwa kujizuia kulia kwa nguvu
“Nyamaza kulia Happy.Tayari waliofanya kitendo kile wamekwisha bainika na watafikishwa katika mkono wa sheria.Lazima haki tendeke.Pole sana Happy.hakuna aliyekuwa akifahamu chochote kuhusiana na tukio lile.Wengi tulikulaani tulipozioan picha zile katika magazeti lakini hatukuufahamu ukweli halisi” akasema Alois
“Alois nina uchungu mwingi sana moyoni.Kwa nini wanitende vile? Hata kama wamejulikana lakini tayari wamekwisha niweka jeraha lisilopona moyoni.Tayari wamekwishaziharibu ndoto zangu zote za kuwa na Patrick .Hata kama wakifungwa lakini hawataweza kuliponya jeraha walilonisababishia moyoni labda kama wakiweza kunirejeshea tena Patrick.Walipofanya nikatengana naye waliyaharibu kabisa masha yangu.Alois ninampenda Patrick .Mimi na yeye tumetoka mbali tuna historia ndefu na ndiyo maana hata baada ya kutengana kwa muda mrefu tulipokutana tu tukajikuta tukiwa wapenzi tena.Kuna kitu kinaishi mioyoni mwetu na hakuna awezaye kukiondoa.Kuachana na wapenzi wetu na kurudiana tena halikuwa jambo rahisi hata kidogo.It was a huge sacrifice lakini tuliweza kufanya hivyo kwa sababu tunapendana .Inaniuma sana kuona yale yote tuliyoyafanya yamekuwa kazi bure.We cant be together anymore.It hurt ..it hurt so much” akasema Happy kwa uchungu
“ Pole sana Happy..Tumuombe Patrick apone ili aufahamu ukweli..Anahitaji kuufahamu ukweli halisi kuhusu nini kilichotokea.Pole sana kwa tukio lile baya kabisa ambalo lilisababisha jamii nzima ikuchukie na kukuhukumu bila kuujua ukweli” akasema Alois na mara akatokea daktari na kuwaita ofisini kwake

* * * *

Tayari jua limekwisha chwea na kiza kimeanza kutanda.Alois na Happy waliwaaga madaktari na wauguzi na kuondoka.Katika hospitali hii hairuhusiwi mtu ambaye si mgonjwa au mfanyakazi wa hospitali kuwepo hapa usiku.Waliingia katika gari la Happy na kuanza safari ya kuelekea katika hospitali alikolazwa Patrick.Safari ilikuwa ya kimya kmya hadi walipofika hospitali na kuonana na daktari wa zamu ambaye aliwafahamisha kwamba hali ya Patrick bado haikuwa na mabadiliko yoyote
“Tuzidi kumuombea Mungu amsaidie.Sisi hapa hospitali tunafanya kila tuwezalo kuhakikisha kwamba hali yake inarejea kuwa nzuri na kama litatokea la kutokea basi ni mapenzi yake Mungu lakini nina uhakika mkubwa kwamba Patrick atarejea katika hali yake ya kawaida hivi karibuni.Yule mwenzake Sarah anaendelea vizuri na tayari tumemuondoa toka katika wodi ya wagonjwa mahututi na tumemuhamishia katika chumba cha kawaida.Kwa siku ya leo ameweza hata kuongea na ndugu zake waliomtembelea.Hata Patrick nina uhakika mkubwa kwamba atapata nafuu muda si mrefu” akasema daktari yule ambaye kitambulisho alichovaa kilionyesha anaitwa Lomayaki Laiza
Toka katika jengo la wagonjwa mahututi Alois na Happy wakaelekea moja kwa moja hadi katika chumba alikohamishiwa Sarah ambako walikutana na ndugu zake wengine waliokuwapo ili kumuuguza.Happy aliogopa sna kuwepo mahala pale akamuacha Alois na kuelekea katika viti vya mapokezi.Alois alisita kuingia ndani kwani toka kilipotokea kifo cha Vero mahusiano ya familia zao hayakuwa mazuri hata kidogo.Mara mlango wa chumba ukafunguliwa na mama yake sarah akatoka
“karibu baba” akasema
“Ahsante sana mama,shikamoo”
“marahaba Alois.Pole sana kwa matatizo’
“ahsante mama .Poleni nanyi”
“Ahsante Alois.Vipi hali ya Patrick anaendelaje?
“Hali yake bado haina mabadiliko yoyote.Bado anasaidiwa kupumia kwa mashine.Lakini madaktari wanasema kwamba atapata nafuu hivi karibuni”
“Namuombea Patrick apone.Sijui ni shetani gani aliyezipitia familia zetu.Alois usinione ninaongea hivi lakini nina uchungu mkubwa sana.Nimelia sana kwa tukio hili.Nimenusurika kumpoteza tena mtoto mwingine.Alois nilitaka kupoteza maisha nilipopata taarifa hizi.Mpaka sasa sielewi ni ujasiri wa namna gani uliompelekea Loniki akafanya kitendo kama hiki.Najua alikuwa ameumizwa na kifo cha mdogo wake lakini sikutegemea kama siku moja angeweza kufanya kitendo cha kinyama kama hiki.” Akasema mama yake Sarah
“Hata mimi inanishanaza sana kwa nini Loniki aliamua kufanya vile.Sikutegemea kama Loniki angeweza kujenga chuki kubwa kama ile.Kifo cha Vero kilituumiza sote,ukiacha Vero hata sisi tulimpoteza baba yetu kwa hiyo hata sisi pia tulikuwa katika wakati mgumu sana. Na hatukutakiwa kuweka chuki kati yetu.Kitendo hiki cha Loniki kimepelekea mama yetu apatwe na mstuko na kupooza upande mmoja.”
“Ouh Jamani..!!! mama yake Loniki akastuka
“Amelazwa hospitali gani?
“amelazwa katika hospitali kuu ya jeshi”
“Vipi hali yake?
“hali yake bado ni tete.Hawezi kuongea au kufanya jambo lolote”
“Pole sana Alois.Najua uko katika wakati mgumu mno wa kuwauguza mama na ndugu yako.Mungu atakupa nguvu Alois na atatusaidia kuyashinda majaribu haya yanayozikumba familia zetu sasa hivi “
“Nashukuru mama .Mungu atatusaidia na watapona.Vipi Sarah anaendelaje?
“Maendeleo yake si mabaya na leo hii ameweza hata kuongea kidogo .Hivi sasa amelala.Namshukuru Mungu hali yake inaendelea vizuri kwa sasa’
“Tunashukuru sana kama hali yake inaendelea vizuri.Nitapita tena kumjulia hali kesho asubuhi”
“Nashukuru sana Alois kwa kutujulia hali”
“Usijali mama tuko pamoja katika wakati huu mgumu”
Alois akamfuata Happy wakaondoka
“ kesho asubuhi mimi nitawahi huku hospitali ili kufahamu maendelo ya Patrick halafuniende kujua hali ya mama.Kesho Cecy, atakwernda kazini kwao ili kona endapo ataweza kupatiwa ruhusa ya mwezi mmoja.”
“ Mimi nitawaho hospitali kumuona mama.Utanikuta kule” akasema Happy
“Happy usisumbuke sana.Unaweza ukapumzika hadimida ya mchana”
“ hapana Alois,nitawahi hospoitali kujua hai a mama.We’re together in this” akasema Happy
“ Ahsante sana Happy” akasema Alis
Kwa kuwa Alois hakuwa na gari ilimbidi Happy ampeleke kwanza nyumbani kwake halafu ndipo aendelee na safari yake ya kwenda nyumbani.

* * * *

Saa nne za asubuhi siku iliyofuata mwili wa Savanna ukakabidhiwa kwa familia yake kwa ajili ya kuendelea na taratibu za mazishi.Jackson Mkikwa mmoja kati ya mawakili wanaofanya kazi katika kampuni ya uwakili ya Savanna aliupokea mwili huo kwa niaba ya familia.Baada ya kukabidhiwa mwili wa Savanna toka jeshi la polisi,ukapelekwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili wa ajili ya kuhifadhiwa hadi hapo taratibu za mazishi zitakapokamilika.Alois alikuwa ni mmoja wa watu waliokuwepo wakati mwili wa Savanna ukikabidhiwa kwa famila na baada ya kushuhudia tukio lile akaondoka kuelekea hospitali ya jeshi alikolazwa mama yake.
“Patrick anaendeleaje? Akauliza Happy baada ya Alois kufika pale hospitali.Happy alikwisha fika pale hospitalini toka saa kumi na mbili za asubuhi
“Bado hali yake iko vile vile.Hakuna mabadilliko yoyote.Vipi hali ya mama? Akauliza Alois
“Mama naye anaendelea vizuri.Kuumekuwa na mabadiliko kidogo katika hali yake” akasema Happy
“eee Mungu tusaidie wagonjwa wetu waweze kupata nafuu ya haraka.” Alois akasema na kutaka kuelekea katika chumba cha mgonjwa lakini Happy akamzuia
“Tumeambiwa tusubiri nje wakati madaktari wanaendelea kumuhudumia mgojwa” akasema Happy.Kikapita kimya kifupi
“Ulimtembelea Sarah leo asubuhi? Happy akauliza
“sikuweza kupata nafasi ya kwenda kumuona.Baada ya kutoka kumuona Patrick nilikuwa na maafisa wa polisi hivyo sikuweza kufika chumbani kwa Sarah.” Akasema Alois
“Mungu atamsaidia na atapona sambamba na Patrick na mama.Kuna taarifa yoyote mpya toka polisi kuhusiana na Khumalo?
“Hapna sijapata taarifa zozote kuhusiana na Khumalo ila mwili wa Savanna umekabidhiwa kwa familia yake baada ya kumalizika kwa uchunguzi” akasema Alois
“Masikini Savanna.Umepata taarifa zozote kuhusiana na taratibu za mazishi?
“Taratibu zinaendelea na kwa mujibu wa Jackson ambaye ndiye aliyeupokea mwili huo kwa niaba ya famlia ,ratiba ya mazishi itatolewa leo baada ya kikao cha ndugu kwani hawakuwa wamepanga chochote kuhusiana na siku ya kumzika Savanna..Pamoja na hayo nina wazo moja”
“wazo gani?
“Ninafikiria kwamba itakuwa vyema iwapo tutakwenda kutoa pole kwa wazazi wa Savanna ambao tayari wamekwisha fika toka marekani wanakoishi.Savanna alikuwa ni mtu wetu wa karibu sana kwa hiyo pamoja na kwamba hata sisi tuko katika wakati mgumu lakini lazima tushiriki kikamilifu katika msiba wake”
“Ni weli Alois.Hilo ni wazo la msingi sana .Tunaweza kuutumia muda huu ambao madaktari wanaendelea na taratibu zao kwenda msibani” akasema Happy.Alois na Happy wakawaaga akina mama waliokuwapo pale hospitali kisha wakaondoka kuelekea nyumbani kwa wazazi wa Savanna ambako ndiko kulikuwa na msiba.Kifo hiki cha Savanna kilitangazwa sana na vyombo vya habari.Savanna alikuwa ni mtu aliyejizolea sifa nyingi kutokana na uwezo na umahiri wake mkubwa katika kusimamia kesi mbali mabli kubwa kubwa nchini.Kutokana na sifa hizo watu wengi walistushwa sana na kifo chake cha ghafla hivyo kupafanya nyumbani kwao pafurike watu
Alois na Happy walifika msibani wakashuka garini na kuingia ndani kwa lengo la kutoa pole kwa familia ya Savanna.Mara tu Happy alipoonekana pale msibani ,minong’ono ikaanza.Happy alikwisha izoea hali hii na haikumpa shida yoyote.Walijitambulisha kwa msimamizi wa shughuli za pale nyumbani ambaye aliwapeleka moja kwa moja katika chumba ambacho alikuwemo mama yake Savanna na mdogo wake Savanna aitwaye Maria.Alois na Happy wakatoa pole kwa wafiwa na baada ya hapo wakapelekwa bustanini ambako baba yake Savanna alikuwa amekaa na baadhi ya wazee.Alois na Happy wakatambulishwa kwake.
“karibuni sana vijana wangu.Nafurahi kuwaona.Kumbe wewe ndiye Happy?
“Ndiye mimi baba” akajibu Happy huku akishangaa ni wapi mzee yule alikomfahamia
“Nafurahi kukuona.Savanna aliwahi kunieleza kuhusu matatizo uliyoyapata na akaniomba ukakae katika hoteli yetu iliyoko Kigali.” Akasema baba yake Savanna na kumfanya Happy astuke.Hakuwa akifahamu kama hoteli ile aliyokuwa akikaa jijini Kigali ilikuwa ni ya akina Savanna
“Ndiyo baba.Niliwahi kupata matatizo makubwa wakati fulani na Savanna ndiye mtu pekee aliyenisaidia sana wakati ule.Msaada wake ulikuwa mkubwa na siku zote atabaki kuwa moyoni mwangu kutokana na moyo wake wa huruma “ akasema Happy
“Nimefarijika sana kwa ujio wenu vijana wangu.Nawapa pole vile vile kwa matatizo mliyoyapata na kufiwa na rafiki yenu.Tunamuombea Mungu Patrick aweze kupona na nina imani Mungu atamsaidia na atapona.Baada ya kumaliza taratibu za kumhifadhi mwanangu basi nitatafuta wasaa na kuja kuwatembelea wagonjwa wote”
“Ahsante sana mzee.Tunakuombea kwa Mungu vile vile akupe nguvu na ustahimilivu wewe na familia yako katika kipndi hiki kibumu.Ni wakati mgumu sana kwetu sote lakini Mungu yuko pamoja nasi” akasema Alois
“Ni kweli vijana wangu.Mimi na familia yangu tuko katika wakati mgumu sana.Kifo cha Savanna kimetuumiza mno na hasa kutokana na mazingira yake.Tulimpenda mno Savanna na tulikuwa na mipango mingi mizuri kwa ajili yake lakini ndiyo hivyo tena ,yameshatokea haya na kutokea,hatuna tena kitu cha kufanya.Haya yote ni mapenzi ya Mungu “ Akasma baba yake Savanna kisha wakaagana na kuondoka
“Savanna hakuwahi kunieleza kama hoteli ile niliyokuwa nakaa kule Kigali ni mali yao.Aliniambia kwamba anafahamiana na mmiliki wa hoteli ile.Ouh Savanna ! Siwezi kuusahau msada ule mkubwa alionisaidia wakati ule.Amekufa wakati ambao bado anahitajika sana.She was too young to die” akasema Happy na macho yake yakalengwa na machozi
“Nilimfahamu Savanna baada ya kuanza kuisimamia kesi ya Patrick.Alikuwa karibu na familia yetu katika kipindi chote cha kesi.Ametufanyia mambo mengi makubwa ambayo si rahis kuyalipa.Alikuwa ni mtu wa kipekee sana.Kitu kinachoinishangaza ni kwamba katikak umfahamu kote Savanna,hata siku moja sikuwahi kusikia akiongelea kuhusu uwezo mkubwa wa kifedha wa familia yake na wala sikufahamu kama alikuwa na mdogo wake ambaye wamefanana kama mapacha.Kwa kweli tumeondokewa na mtu muhimu sana.Katika uhai wake hakupenda kujikweza wala kujivuna” akasema alois wakiwa garini wakirejea toka nyumbani kwa akina Savanna
“Itamchukua Patrick muda mrefu kurejea katika hali yake ya kawaida baada ya kufahamu kamba Savanna amefariki dunia” akasema Alois
“Yah ! atakuwa na wakati mgumu sana.Alimpenda mno Savanna.” Akasema Happy.
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 63
MTUNZI: PATRICK.CK
CONTACT: 0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Alikuwa ni mtu wa kipekee sana.Kitu kinachoinishangaza ni kwamba katikak umfahamu kote Savanna,hata siku moja sikuwahi kusikia akiongelea kuhusu uwezo mkubwa wa kifedha wa familia yake na wala sikufahamu kama alikuwa na mdogo wake ambaye wamefanana kama mapacha.Kwa kweli tumeondokewa na mtu muhimu sana.Katika uhai wake hakupenda kujikweza wala kujivuna” akasema alois wakiwa garini wakirejea toka nyumbani kwa akina Savanna
“Itamchukua Patrick muda mrefu kurejea katika hali yake ya kawaida baada ya kufahamu kamba Savanna amefariki dunia” akasema Alois
“Yah ! atakuwa na wakati mgumu sana.Alimpenda mno Savanna.” Akasema Happy.

ENDELEA……………….

Ni siku ya sita sasa toka lilipotokea shambulio la silaha na kusabisha kifo cha Savanna.Patrick alikwisha anza kupata nafuu na alikwisha ondolewa ile mashine iliyokuwa inamsaidia kupumua.Sarah naye alikuwa anaendelea vizuri na ilitegemewa muda wowote angeruhusiwa kurejea nyumbani
“Ni siku ya jumamosi,siku tulivu iliyotawaliwa na kijua kikali,siku ambayo wakili mashuhuri nchini,Savanna alikuwa anazikwa.Watu walikuwa ni wengi sana.Saa sita mchana mwili wa Savanna ukawasili nyumbani ukitokea hospitali ulikokuwa umehifadhiwa.Ulipokelewa kwa vilio toka kwa umati mkubwa wa watu waliokuwa wamekuja kuungana na familia katika kumsindikiza Savanna katika safari yake ya mwisho.Salamu za rambi rambi zilitolewa toka kwwa watu mbali mbali waliohudhuria,akiwemo waziri wa sheria na katiba aliyeiwakilisha serikali na ambaye alikuwa rafiki wa karibu wa Savanna.Baada ya salamu nyingi za rambi rambi toka kwa watu mbali mbali likafuata zoezi la kuuaga mwili wa marehemu.Wengi walipoteza fahamu katika zoezi hili.Zoezi la kuaga mwili lilipokamilika ibada ya kumuombea marehemu ikafanyika hapo hapo nyumbani na kisha mwili wa marehemu ukapakiwa garini na safari ya kumsindikiza Savanna katika nyumba yake ya milele ikaanza.Ulikuwa ni msafara mrefu wa magari kuelekea makaburini.Alois,mke wake Secilia,Happy pamoja na baadhi ya ndugu zao walikuwepo pia.
Hatimaye mwili wa Savanna ukashushwa kaburini.Watu wengi walipoteza fahamu katika hatua hii.Ilikuwa vigumu kuamini kama ni kweli Savanna hawatamuona tena.Kaburi likafunikwa na hatimaye watu mbali mbali wakaweka shada zao za maua juu ya kaburi.Shughuli za mazishi zilikamilika na watu wakatawanyika.Wengi wakarejea nyumbani kwa wafiwa na wengine wakaelekea makwao.Safari ya Savanna duniani ikaishia hapo

* * * *

Hali ya Patrick iliendelea kuimarika siku hadi siku na hatimaye akatolewa katika chumba cha wagonjwa mahututi na kuhamishiwa katika chumba cha wagonjwa wa kawaida.Sarah alikwisha ruhusiwa kurejea nyumbani baada ya hali yake kuwa nzuri
Watu wengi walikuwa wakimtembelea Patrick hospitali na kumjulia hali na kumtakia uponaji wa haraka.Happy alikuwa ni mtu wa kwanza kila siku kumtembelea na kumjulia hali na hakukosa asubuhi mchana na jioni.Chumba cha Patrick kilijaa maua na kadi za kumtakia uponaji wa haraka toka kwa watu mbali mbali waliokuwa wanamtembelea.
Toka amepata nafuu na kuhamishiwa katika chumba cha kawaida,Patrick amekuwa akitembelewa na watu wengi kila siku lakini katik watu wote waliomtembelea kuna watu wawili ambao hakuwaona .Ni mama yake pamoja na Savanna
“Kwa muda mrefu sasa sijamuona mama yangu yuko wapi? Hafahamu kama ninaumwa na nimelazwa hospiali? Kitu kingine kinachonishangaza hakuna mtu ambaye anataka kunieleza mpenzi wangu Savanna anaendeleaje kwa sababu kwa mujibu wa kumbu kumbu zangu,Loniki alimpiga risasi muda mfupi kabla hajanipiga mimi.Savanna anaendeleaje? Yuko wapi? Patrick akajiuliza maswali haya lakini akakosa jibu
“Nitamuuliza Alois” akasema Patrick
“Bado siamini kama Loniki angeweza kufanya kitendo kama kile.Itanichukua muda mrefu sana kuisahau ile siku.Mpaka hivi sasa naona ni kama muujiza mimi kuwa hai.Huu ni muujiza mkubwa Mungu amenitendea.Nilikiona kifo.Nilihisi tayari nimekufa.Nilisikia risasi ikinipenya mwilini .Hili ni tukio baya kabisa kuwahi kunitokea” akasema Patrick na kuuma meno kwa hasira.Mara picha ya Savanna akiwa amelala katika dimbwi la damu ikamjia
“Ouh Savanna ! Kwa nini Loniki alimpiga risasi? Kama alikuwa anataka kulipiza kisasi angenipiga mimi na si Savanna ambaye hahusiani chochote na kilichotokea kati yangu na Vero..I’ll never forgive Loniki for what she did to Savanna.I swear I’ll never forgive her.Amemuumiza mtu ambaye ninampenda na hastahili kabisa kuumizwa.Kama ni kisasi angelipiza kwangu mimi na Happy na si Savanna”
Mara tu alipolikumbuka jina la Happy akahisi kama mwili wote unamsimka
“Happy amekuwa akija kunitazama kila siku asubuhi mchana na jioni.Masikini Happy nimetoka naye mbali sana .Sikutegemea kama siku moja tungefikia hatua kama tuliyofikia ya kuishi kama hatujuani.Sikutegemea kama ingetokea siku ningemchukia Happy.Nilimpenda kwa moyo wangu wote lakini sielewi ni shetani gani alimwingia na kumfanya aamue kufanya ule uchafu na kwa aibu aliyoipata akatoweka bila hata kuniaga.Kila nikilikumbuka jambo hili naumia sana.Aliniacha nikiteseka peke yangu gerezani kwa kosa ambalo sikulitenda.Nikifikiria maumivu niliyoyapata najikuta nashindwa kabisa kumsamehe Happy.Mimi na yeye tuna historia ndefu na mapenzi yasiyoelezeka lakini vyote vilikwisha siku alipoamua kunitelekeza gerezani .Ni Savanna ndiye aliyekuwa nami kila sekunde na amepambana na mimi kuhakikisha ninashinda kesi.Aliiona thamani yangu kwake na ndiyo maana alikuwa radhi kufanya kila aliloweza kunisaidia.Savanna anastahili nafasi kubwa na ya pekee kabisa moyoni mwangu.Sina haja ya kuendelea kumuwaza Happy mtu ambaye aliamua kuniacha na kwenda kurudiana na mchumba wake Mike.Mimi na yeye tutaendelea kuwa marafiki tu.” Akawaza Patrick. Halafu akageuza shingo yake na kutazama pembeni kulikokuwa na lundo la maua aliyokuja nayo Happy.Patrick akanyoosha mkono na kuyavuta maua yale akaichukua kadi iliyokuwa imefungwa pamoja na yale maua.Ilikuwa na maneno matamu ya kumtakia uponaji wa haraka.Patrick akatabasmu na kuiweka pembeni.

* * * *

Siku zilizidi kusonga kwa kasi na hali ya Patrick iliendelea kuimarika siku hadi siku.Tayari alikwisha pewa taarifa kuhusiana na kifo cha Savanna.Alois alimweleza ukweli kwamba Savanna alifariki katika tukio lile Hii ilikuwa ni taarifa mbaya sana kwa Patrick kuwahi kuisikia.Ilimuumiza kupita kiasi na kumfanya apatwe na tatizo la kupoteza fahamu mara kwa mara kwa siku tatu mfululizo.Alionekana ni kama mtu ambaye alichanganyikiwa akili na madaktari walihofia pengine hali ile ingeweza kuathiri maendeleo ya afya yake kwa kiasi kikubwa.
Ilikuwa ni siku ya jumapili siku ambayo watu wengi huitumia kwa ajili ya kuwatembelea ndugu jamaa na marafiki walioko mahospitalini.Hospitali ya St Patrick ilikuwa na idadi kubwa ya watu waliokuja kuwatembelea wagonjwa wao.Chumba cha Patrick kilikuwa kimejaa watu waliokuja kumjulia hali.Ni kawaida ya chumba hiki kujaa watu kila siku wanaokuja kumpa pole Patrick. Lakini kwa siku hii ya leo idadi iliongezeka.Muda wa kuruhusiwa kuwatembelea wagonjwa ulimalizika na watu wakaombwa waondoke pale hospitali
Dakika kama arobaini toka muda uliopangwa kuwaona wagonjwa kumalizika Alois aliyekuwa amebaki na mgonjwa akapigiwa simu .Alikuwa ni mzee Francis Kito baba mzazi wa Savanna
“Shikamoo mzee” akasema Alois
“marahaba Alois hujambo?
“Sijambo mzee”
“Vipi mgonjwa anaendeleaje?
“Anaendelea vizuri sana”
“nafurahi kusikia hivyo. Alois nilikuahidi kwamba siku moja nitamtembelea mgonjwa hapo hospitalini.Sikuweza kufanya hivyo mapema kutokana na mambo kuwa mengi.Kwa kuwa leo nina nafasi nimeona nije nimtazame Patrick niongee naye kidogo.Niko hapa getini naomba uje unichukue” akasema mzee Kito.Kwa haraka Alois akaenda getini na kuichukua familia ya mzee Kito akawaongoza kuelekea katika chumba cha Patrick
Patrick alikuwa amejilaza kitandani kwake akizisoma baadhi ya kadi za kumtakia uponaji wa haraka alizoletewa na watu mbalimbali mara mlango ukafunguliwa na akaingia Alois akiwa ameongozana na familia ya mzee Francis.Patrick akastuka na mapigo ya moyo wake kumwenda mbio na kuhisi kama amemuona Savanna baada ya kugonganisha macho na Maria mdogo wake Savanna.
“Patrick kuna wageni wamekuja kukutembela.Huyu ni mzee Francisi Kito baba mzazi wa Savanna.Huyu ni mama yake mzazi Savanna na huyu hapa anaitwa Maria ni mdogo wake Savanna.Baba ,mama na Maria huyu ndiye Patrick na tunamshukuru Mungu kwa sasa hali yake inaendelea vizuri na kwa mujibu wa madaktari muda wowote anaweza akaruhusiwa kurejea nyumbani” Alois akafanya utambulisho Familia ya mzee Francis wakamsalimu Patrick na kumpa pole nyingi kwanza kwa tukio lililotokea na pili kwa kuondokewa na mpenzi wake Savanna
“Patrick utatusamehe sana kwa kutoweza kufika hapa mapema kukujulia hali.Hilo lilitokana na mambo kuwa mengi sana na hivyo kukosa kabisa nafasi ya kuja.Kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwetu kama familia kwa kumpoteza mtoto wetu ,hata hivyo tulikuwa tunawasiliana na Alois ambaye alikuwa akitupa taarifa za maendeleo yako” akasema mzee Francis Kito
“Nafahamu baba.Nafahamu ni jinsi gani mlivyokuwa na wakati mgumu.” Akasema Patrick huku akijifuta jasho usoni
“Kama alivyotangulia kusema Alois,sisi ndiyo familia ya Savanna.Kwa muda mrefu sasa tunaishi nchini Marekani.Tuna miradi yetu kule na vile vile tumefanya uwekezaji kadhaa katika baadhi ya nchi za Afrika na asia.” Akasema mzee Kito
“Nashukuru sana kuwafahamu.Savanna aliniambia kwamba wazazi wake wanaishi Marekani lakini hakuwahi kunieleza wanaishi sehemu gani ya Marekani .Katika mipango yetu tulipanga baada ya kesi kumalizika tungefunga safari kuja Marekani kwa ajili ya utambulisho na kuomba Baraka zenu kabla ya kufunga ndoa,nasikitika kwamba hili halikuweza kufanikiwa”akasema Patrick kwa uchungu
“Pole sana Patrick.Haya ndiyo mambo ya dunia.Savanna hakupenda sana kuwa tegemezi.Siku zote alipenda kufanya kile ambacho alikipenda na ndiyo maana baada ya kumaliza masomo yake ya sheria alirejea nchini Tanzania na kuanza kufanya kazi ya uwakili.Alipenda sana kuwa mwanasheria na ndoto yake ilikuwa ni siku moja awe mwanasheria mkubwa Nadhani ndoto yake hii kwa kiasi fulani ilitimia.Savanna alipenda kuishi maisha anayoyataka yeye na siku zote aliithamini sana furaha ya moyo wake.Mara nyingi alikuwa akitupigia simu na kutueleza ni jinsi gani ulivyoweza kuyafanya maisha yake yawe na furaha.Hata sisi tulifurahi sana kumuona mtoto wetu akiwa na furaha kubwa namna ile.Mimi binafsi aliwahi kunielea namna gani alivyokuwa anakupenda na mipango yenu yote ya baadae,Nasikitika kwamba mipango yenu yote mliyoipanga imeishia njiani.Pamoja na Savanna kutokuwpo leo hii lakini maisha hayana budi kuendelea.Sote tutakufa na tuamini kwamba siku moja tutakutana naye katika makazi ya milele.” Akasema mzee Kibaho.Patrick machozi yalikuwa yanamtoka.Alikosa neno la kusema.Mzee Kito akasema
“Patrick..!
“Naam baba” akasema Patrick
“Utatuwia radhi sana kwa sababu siku ya leo tutakuwa tumekurejeshea machungu ya kuondokewa na mtu uliyempenda sana”
“usijali baba.Najaribu kuizoea hali hii lakini inaniwia vigumu sana.Nadhani itanichukua muda mrefu kuizoea” akasema Patrick.Mama yake Savanna akashindwa kujizuia akatokwa na machozi,akafungua mlango na kutoka mle chumbani
“Patrick pamoja na kukujulia hali,kuna jambo moja ambalo tumekuja kukueleza.Ni kwamba tunategemea kuondoka katika siku mbili zijazo kurejea Marekani.Tumekaa Tanzania kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.Maisha hayana budi kuendelea.Patrick tunaomba ufahamu kwamba kwa sasa wewe ni mwanetu.Tunakuhesabu kama mmoja wa wanafamilia.Ulikuwa ni sehemu muhimu ya maisha ya mtoto wetu kwa hiyo hata baada ya yeye kutangulia mbele za haki lakini bado tutaendelea kuvienzi na kuvithamini vitu vyote vilivyokuwa na thamani kubwa kwake.Patrick tunakukabidhi mali zote za Savanna zilzoko hapa nchini na nje ya nchi.Hapa Tanzania alikuwa na nyumba tatu.Moja ni ile aliyokuwa akiishi na nyingine mbili amezipangisha kwa mashirika.Vile vile alikuwa na magari matatu,tunakukabidhi pia kampuni yake ya uwakili pamoja na kiwanda cha kusindika nyama na kile ambacho alikuwa katika mpango wa kukifungua cha kutengeneza maji ya kunywa.Vyote hivi ni mali yako na tunakuomba uviendeleze na uvitunze kama njia moja ya kumuenzi mtu aliyekuwa muhimu sana kwako.Wanasheria wetu wanaendelea kufuatilia mali zake nyingine zilizoko nje ya nchi ikiwa ni pamoja na fedha ambazo alikuwa akiweka katika mabenki kadhaa ya ndani na nje ya nchi na watakapokamilisha kazi hii tutakutaarifu.” Mzee Kito akanyamaza kidogo na kuendelea
“Tuna miradi ya uwekezaji ya familia ambayo kila mwaka hugawana kiasi cha faida inayopatikana katika uwekezaji huo.Kila mwanafamilia hupata mgao wao.Kuanzia sasa wewe ndiye utakayekuwa ukichukua fungu la Savanna.” Akasema mzee Kito .Patrick alikosa neno la kusema ni machozi tu yaliyokuwa yanamtoka.Akajitahidi akafuta machozi na kusema
“Baba,mama na Maria sipati neno zuri la kuweza kutoa shukrani zangu kwenu kwanza kwa kuja kunijulia hali.Pili nashukuru sana kwa maamuzi yenu ya kunitambua mimi kama mwanafamilia yenu.Ninayakubali na kuyapokea maamuzi hayo ya familia na ninawaahidi kwamba katika siku zote za maisha yangu nitamuenzi Savanna kama lulu ya pekee kabisa kuwahi kutokea katika maisha yangu.Mali zote nitazitunza na kuziheshimu na kuziendeleza.Ndoto zake zote nitajitahidi kuzitimiza na kulifanya jina la Savanna litukuke kila siku.Sina neno zaidi la kusema zaidi ya hayo machache.Ahsanteni sana na Mungu awabariki” akasema Patrick huku machozi yakimtoka
“Patrick tunakushukuru kwa maneno yako mazito ya shukrani.Tutakuwa tukiwasiliana nawe mara kwa mara kujua hali yako na endapo utakuwa na tatizo lolote usisite kutueleza.Sisi ni wazazi wako na tutakusadia.Kitu cha mwisho ambacho nataka kukueleza ni kwamba Savanna is gone.She’ll never come back.So you have to live your life.You have to move on with your life.Be Happy and enjoy life.That’s the best thing Savanna wants you to do now.” Akasema mzee Kito
“Nimekulewa baba na nitajitahdi kuyafanyia kazi hayo maneno uliyonieleza japokuwa ni vigumu sana.I’ll be Happy for her.I’ll live my life the way she wanted me to” akasema Patrick
Familia ya Franis kito ikaagana na Patrick na kisha wakaondoka na kumuacha akindelea kubujikwa na machozi .Ujio ule ulimkumbusha mambo mengi kuhusu mpenzi wake Savanna.

* * * *

Hatimaye Patrick akaruhusiwa kutoka hospitali.Hali yake ilikuwa nzuri sasa.Ndugu zake kadhaa walikuwepo hospitali pamoja na Happy wakati akiruhusiwa kurejea nyumbani.Wakati wakiondoka Alois alimtaka apande gari moja na Happy lakini kwa mshangao wa wengi,Patrick alikataa na kupanda gari la Alois
Toka hospitali waliekea moja kwa moja katika hospitali ya jeshi alikolazwa mama yake ambaye mpaka wakati huo hakuweza bado kuongea japokuwa hali yake ilikuwa inaendelea vizuri kutokana na mazoezi aliyokuwa akipewa .Patrick alilia machozi mengi kumuona mama yake akiwa katika hali ile
siku iliyofuata Alois na Happy wakampeleka Patrick katika kaburi la Savanna.Patrick alilia sana siku hii.Ilimbidi Alois atumie nguvu kumuondoa pale kaburini akamrudisha nyumbani kwani hakutaka kabisa kuondoka pale kaburini.Toka siku ile Patrick alipenda kuutumia muda mwingi akiwa mwenyewe.
Siku moja jumamosi Happy alifika nyumbani kwa akina Patrick akiwa na maua na kumfuata Patrick bustanini alikokuwa ametulia akisoma kitabu, akamsalimu na kumpatia yale maua.
“Happy kuna jambo nataka kukuuliza” akasema Patrick baada ya kuyapokea yale maua ya Happy
“Uliza usihofu”
“Why are you doing this to me? Kwa muda mrefu sasa umekuwa karibu kufuatilia hali yangu toka nikiwa hospitali na hata sasa.Nakushukuru sana kwa hilo lakini najiuliza ni kwa nini unayafanya haya sasa? Ni njia ya kutafuta msamaha wangu? Au unatafuta tena ukaribu na mimi? akauliza Patrick ambaye alionekana ni mwenye hasira.Happy alibabaika akashindwa ajibu nini
“Answer me Happy.what do you want from me? Akauliza tena Patrick
“Patrick I’m not doing this for you.I’m doing this for me.
“You feel guilty,isnt it? Akauliza Patrick kwa ukali
“You feel guilty for what you did to me,right? Happy machozi yakaanza kumtoka
“Patrick you are my friend.Pamoja na yote yaliyotokea lakini bado una thamani kubwa sana katika maisha yangu.Bado una nafasi ya peke ndani ya moyo wangu na ndiyo maana unaniona niko hapa leo.Its not easy for me to be here but I have to be here,I have to do this” Akasema Happy.Patrick akamtazama kwa jicho kali Happy akaendelea
“Patrick ninafahamu ni jinsi gani unavyoumia moyoni na hasa unaponiona hapa mbele yako.Patrick nisingeweza kuusogeza tena uso wangu mbele yako lakini kinachonifanya niwe hapa karibu yako ni moyo wangu ambao hauna furaha bila ya kukuona.Patrick kuna mambo mengi yametokea kati yetu na nimekuwa nikitafuta nafasi ya kukaa na kuongea nawe kuhusiana na kilichotokea kati yetu lakini umekataa kunipa hata hiyo hafasi ya kuongea nawe tena.Why do you hate me so much? Why don’t you listen to what I want to tell you? Don’t you have any feelings for me in your hear anymore?
Patrick aliyekuwa ameinamisha kichwa chini akainua kichwa na kumtazama Happy kwa hasira
“Feelings ???!!..you don’t have to talk about feelings because you dont know what it real means.You want to know what I feel inside me when I see you? It’s hate.I hate you Happy.I hate you so much.Happy nilikupenda sana nikawa tayari kuacha kila kitu kwa ajili yako,nikaubeba mzigo mzito wa kesi iliyokuwa ikukabili wewe, lakini ni kitu gani umenilipa kwa haya yote? Nothing .!!!!!!! Badala yake umepiga picha chafu na kuzisambaza na kama haitoshi ukaamua kunikimbia na kuniacha peke yangu nikiozea gerezani.Najua ulitegemea ningefungwa gerezani ili uendelee kula raha za dunia na mabwana zako lakini watu walioiona thamani yangu kwao wamenipigania na hatimaye leo hii niko huru tena.Kwa hayo yote hebu jiulize Happy una sababu yoyote ya kutaka kupata nafasi ya kuongea na mimi? You dont deserve even a second of my time.Ninashukuru kwa msaada wako mkubwa wakati ninaumwa lakini kwa sasa nimekwisha pona na ninakuomba kitu kimoja tu,leave me alone.I want to be alone.I don’t need you and I don’t love you anymore.You never loved me it was all lies” akasema Patrick kwa ukali
Happy machozi yalikuwa yanamtiririka.
“Patrick kwa nini unanifanyia hivi? Why are you doing this to me?
“Because you are a monster and you don’t deserve a second chance !! Tafadhali ondoka mbele ya macho yangu Malaya mkubwa wewe !!!!” akasema Partrik kwa ukali na kumfanya Happy azidi kulia kwa nguvu.
Patrick najua unanichukia na sitaki kukulazimisha kwamba unisamehe.Ahsante kwa matusi yote uliyonitukana.Nitaondoka Patrick kama ulivyoniamuru and this time it’ll be for good.You’ll never see me again in your life but before I leave please give me five minutes .Kuna jambo ambalo bado hujalifahamu.Please listen to me and then I’ll go and leave you alone …” akasema Happy.Patrick akamtazama kwa macho makali
“Happy tafadhali ondoka.Kuzidi kukaa hapa unazidi kunichafua.Ninakuchukia kama ninavyomchikia shetani.” Akafoka Patrick.Happy akampigia magoti na kuendelea kumlilia .Patrick kwa hasira akamsukuma akangukia katika majani.
“Patrick .!!!!!!.. akaita Alois ambaye alitokea ghafla
“Unafanya nini ?? akauliza Alois kisha akamfuata Happy pale chini alipokuwa ameanguka akilia.Akamuinua.
“Inuka Happy.Pole,sana” akasema Alois.Happy akafuta machozi na kumtazama Patrick aliyekuwa amefura kwa hasira
“Patrick I’m leaving.I’m so sorry for everything and I’ll never bother you again.You’ll never see me again in your life. Good bye Patick” akasema Happy na kuondoka kwa kasi.Alois akamuangalia Patrick kwa macho makali
😛atrick umefanya nini? Nilikuwa nimesimama nimesikia matusi yote uliyomtukana Happy.kwa nini ulifanya vile?Happy hakustahili matusi kashfa na maneno yale makali” akasema Alois.Huku akihema kwa kasi Patrick akajibu.
“Yule Malaya hastahili hata dakaka ya kuongea na mimi.Namchukia Happy.Namchukia sana na nikimuona tena hapa nitamfanyia kitu kibaya sana” akasema Patrick.Alois akamtazama kwa makini na kusema
“Patrick umefanya kosa kubwa ambalo utajilaumu sana.ulitakiwa umsikilize alitaka kukueleza kitu gani”
“Katika siku zote za maisha yangu nitasikitika sana kumpoteza Savanna mwanamke ambaye alinipenda kwa dhati na kunijali na si huyu chui mwenye ngozi ya kondoo”
“Patrick ulitakiwa umpe nafasi Happy ya kukueleza alichotaka kukueleza.Kuna kitu ambacho bado hukifahamu” akasema Alois
“Hana jambo lolote la kunieleza kahaba Yule.” Akasema Patrick kwa ukali.Alois akaonyesha kukasirishwa na kauli ile
“Tafadhali Patrick naomba iwe mwanzo na mwisho kumuita Happy Kahaba.Show her some respect.Toka matatizo haya yametokea amekuwa nasi bega kwa bega.Hakuna siku aliyopumzika.Hakuna rafiki yako hata mmoja ambaye amethubutu kufanya kazi kubwa kama aliyoifanya Happy.Ni mtu ambaye anahitaji shukrani za pekee badala ya matusi uliyomporomoshea.Zaidi ya yote unafahamu masahibu aliyokumbana nayo?? Unafahamu ????..akauliza Alois kwa ukali
“Sifahamu !! akajibu Patrick
“Kama hufahamu kwa nini basi hukumpa nafasi ya kumsikiliza? Alois akauliza kwa ukali.Patrick hakujibu kitu
“Kama hufahamu Happy alitaka kukwambia nini,basi nisikilize kwa makini halafu wewe mwenyewe utafanya maamuzi.” Akasema Alois na kuanza kumuelezea Patrick mkasa mzima uliompata Happy.Mpaka anamaliza kumuelezea Patrick alikuwa amejiinamia asijue la kufanya
“Ouh Mungu wangu,hayo yote unayoaniambia Alois ni ya kweli?
“Huo ni ukweli halisi”
“Savanna alifahamu kila kitu kwa nini hakuniambia ukweli? Ni kweli nilimchukia sana Happy na sikutaka tena kumuona katika maisha yangu.Sikuufahamu ukweli .Ulikuwa sahihi Alois I was wrong .I made a big mistake” akasema Patrick na kuinama chini.
“Nitafanya nini sasa? Akauliza Patrick.Alois akamtazama na kusema
“Naomba uniambie ukweli wa moyo wako .Ni kweli unamchukia Happy na hutaki kumuona tena katika maisha yako? Ni kweli yale mapenzi yote uliyokuwa nayo kwake yamekwisha kabisa? Be honest with me” akasema Alois
Patrick akainama akafikiri na kusema
“Alois pamoja na mambo yote yaliyotokea lakini siku zote Happy amekuwa moyoni mwangu.Nafasi yake bado ipo katika moyo wangu.Nilidhani tayari nimekwisha msahau Happy lakini baada ya kumuona mahakamani siku alipotoa ushahidi wake ndipo nilipogundua kwamba Happy bado ana nafasi kwangu lakini kutokana na mambo aliyoyafanya sikuwa na hamu hata ya kumuona tena” akasema Patrick
“Do you still love her? Akauliza Alois
“Alois what do you expect me to say? You know the answer.I still love her” akasema Patrick
“Nimepata nafasi ya kuwa karibu na Happy na amenieleza undani wake.Bado anakupenda sana.Ninaweza kukushauri kwamba kwa kuwa hivi sasa Savanna hayupo tena na kama bado hujampa nafasi yake mtu mwingine nakushauri umfikirie Happy.Ni mwanamke ambaye unahitaji kuwa naye katika maisha yako.Mmetoka mbali na mnafahamiana vizuri.Msamehe kwa alichokifanya na mfungue ukurasa mpya wa maisha yenu.You need to be Happy .Mtu pekee ambaye anaweza akakupa furaha ya maisha baada ya Savanna ni Happy” akasema Alois
“Nakubaliana nawe Alois.Mimi na Happy kamwe hatuwezi kutengana.Kila mara kuna nguvu ambayo inatutenganisha lakini kunatokea tena nguvu nyingine ambayo inatuunganisha tena.Ukianza kufuatilia matukio yaliyotokea toka nimefahamiana na Happy utakubaliana na haya nikwambiayo.Halafu kitu kingine kinacholeta ugumu ni kwamba tayari Happy amekwisha rudiana na Mike mchumba wake wa zamani kwa hiyo uwezekano wa kumpata tena ni mdogo sana” akasema Patrick

“Patrick unatakiwa umtafute Happy na uongee naye Nina imani mtayaweka sawa mambo haya”
“Alois tafadhali naomba unisaidie niweze kuongea tena na Happy.Please help me Alois” akasema Patrick
Alois hakujibu kitu akachukua simu yake na kuzitafuta namba za simu za Happy akapiga lakini simu yake haikupatikana tena.
“Simu yake haipatikani tena” akasema alois
“Namfuata nyumbani kwao.Tafadhali naomba uambatane nami.” akasema Patrick na kwa pamoja wakaingia katika gari la Alois wakaondoka kuelekea kwa akina Happy
“Alois nitahakikisha wale wote waliomfanyia Happy kitendo hiki cha udhalilishaji wanafungwa gerezani” akasema Patrick
“Usijali kuhusu hilo Patrick.Kuna taarifa nimezipata leo kwamba Khumalo amekamatwa na polisi wa kimataifa akijaribu kuingia nchini Afrika kusini.Anarudishwa nchini kujibu tuhuma zinazomkabili.Haki itatendeka na jina la Happy litasafishwa na hesima yake itarudi” akasema Alois
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 64
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT0764294499

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Alois wakaondoka kuelekea kwa akina Happy
“Alois nitahakikisha wale wote waliomfanyia Happy kitendo hiki cha udhalilishaji wanafungwa gerezani” akasema Patrick
“Usijali kuhusu hilo Patrick.Kuna taarifa nimezipata leo kwamba Khumalo amekamatwa na polisi wa kimataifa akijaribu kuingia nchini Afrika kusini.Anarudishwa nchini kujibu tuhuma zinazomkabili.Haki itatendeka na jina la Happy litasafishwa na hesima yake itarudi” akasema Alois

ENDELEA……………..

Kila aliyekuwepo ndani alistushwa na hali aliyorudi nayo Happy.Japokuwa alikuwa amevaa miwani myeusi lakini michirizi ya machozi ilionekana katika mashavu yake.Mama yake ambaye alikuwa wa kwanza kumuona wakati akishuka garini akastuka na kudhani labda kuna taarifa mbaya.
“Happy kuna nini? Akauliza
Happy hakujibu kitu akatembea kwa kasi kuelekea chumbani kwake,mama yake akamfuata
“Happy mbona umetustua namna hiyo? Kuna jambo gani huko utokako? Patrick mzima?
“Patrick mzima mama” akajibu Happy huku akifuta machozi
Mama yake akavuta pumzi ndefu baada ya kusikia kwamba Patrick ni mzima
“Ouh ahsante Mungu nilifikiri kuna tatizo limetokea.Sasa kinachokuliza kitu gani?
“Mama tutaongea baadae.I need to be alone “ akasema Happy,Mama yake akamtazama na kutoka mle chumbani.
Baada ya mama yake kutoka mle chumbani Happy akafunga mlango halafu akalifungua sanduku lake akatoa bahasha iliyokuwa na picha ya Patrick.Akaitazama picha ile kwa muda huku machozi yakimtoka.
“Patrick kwa nini kila mara ninateseka kwa ajili yako? Nimejitahidi kukusahau lakini nimeshindwa.Nimeendelea kuwa mtumwa wa penzi lako.Nimejaribu kuendelea na maisha yangu bila ya wewe lakini nimeshindwa kwa sababu kila ninapojaribu kupiga hatua ,wewe hutokea mbele yangu na kunirudisha nyuma.Hii ina maanisha kwamba nitaendelea kuteseka hadi mwisho wa maisha yangu.Patrick kama ungefahamu ni namna gani ninakupenda usingethubutu kunitamkia maneno yale makali.” Akasema Happy kwa sauti ndogo huku akiitazama ile picha.Akaiweka picha ile pembeni,na kufuta machozi
“You don’t deserve a second chance.!! Tafadhali ondoka mbele ya macho yangu Malaya mkubwa wewe.!!!
Maneno haya aliyotamka Parick yakajirudia tena kichwani kwake.Akafuta machozi
“Patrick midomo yako mizuri ambayo siku zote imekuwa ikinitamkia maneno matamu na kunifanya nijione malkia katika himaya ya mfalme lakini leo hii siamini kama imetamka maneno hayo mazito. Hata kama nilikosea,hukupaswa kunitamkia maneno kama yale” akasema Happy kwa uchungu
“I saw your eyes.May be you are right that I’ve to stay away from your life.” Akaendelea kusema Happy akaishika tena picha ile ya Patrick
“Pengine hii inaweza kuwa njia bora zaidi kwa mimi kuendelea na maisha yangu nikiwa na amani bila ya wewe.You are right I don’t deserve you.Kila mara unapokuwa nami lazima ukutane na matatizo.Ni wakati sasa wa kuachana nawe Patrick.Ni wakati wa kufungua ukurasa mpya wa maisha yangu.Bado wako watu wanaonipenda na kunijali.Nilimuahidi Mike kwamba nitakaporejea Marekani tutafunga ndoa.Nadhani hili ndilo jambo la msingi kwa sasa.Nitajifunza kumpenda Mike kwa moyo wangu wote kwa sababu naye ananijali na kunithamini na zaidi ya yote ananipenda sana.I have to let you go Patrick.It hurt but I have to do it and leave you alone.” Akasema Happy huku akiichana katikati picha ile ya Patrick
Wakati Happy akiwa chumbani kwake,nje ya nyumba yao ikasikika honi ya gari.Mama yake akaenda kufungua mlango na kustuka kwa kuiona sura ya Patrick .Mara moja akajua kuna jambo limetokea.
“Patrick !!..akasema kwa mshangao
“mama shikamoo” akasema Patrick
“Marahaba Patrick.Karibuni ndani” akasema mama yake Happy na kuwakaribisha Patrick na Alois ndani
“Habari za hapa ? akauliza Patrick
“Habari za hapa nzuri.Vipi unaendeleaje?Nimestuka sana nilipokuona” akasema mama Happy ambaye bado aliendela kuwa na mstuko kwa ujio ule wa Patrick
“Namshukuru Mungu ninaendelea vizuri.” Akajibu Patrick halafu kikapita kimya kifupi
“Mama Happy tumemkuta? Akauliza Patrick
“Happy yupo.Ngoja nikamute”
Mama Happy akainuka nakuelekea chumbani kwa Happy.Aligonga mlango na Happy akaufungua.Alistuka kwa hali aliyomkuta nayo.
“Happy una tatizo gani?
“Sina tatizo lolote mama.Tatizo langu limekwisha” akajibu Happy huku akifuta machozi
“Patrick amekuja,anahitaji kukuona”
Happy akastuka na kumuangalia mama yake
“Umemwambia kwamba nipo?
“Ndiyo Happy.Nimemweleza kwamba upo ndani”
“Mama naomba mwambie kwamba sitaki kuonana naye.Sina muda wa kuonana naye na aondoke zake“
“Happy ! ! mama yake akasangaa
“Nini kimetokea? Kwa nini hutaki kuonana na Patrick leo? Mmekorofishana ?
“Mama sitaki kuonana na Patrick.Mimi na yeye basi.Nashukuru yuko mzima na anaendelea vizuri sasa.Sitaki kusikia lolote kuhusiana na Patrick.It’s over between us.” akasema Happy.Mama yake akamsogelea na kumshika mkono
“Niambie Happy nini kimetokea? Kila siku unaondoka hapa na kwenda kwa Patrick lakini leo umerudi unalia.nini kimetokea huko ?
“Usihofu mama hakuna kitu chochote kibaya kilichotokea .Nimeamua tu sitaki kuonana na Patrick tena.Mwambie aondoke haraka hapa nyumbani” akasema Happy.mama yake akarejea tena sebuleni
“Patrick nini kimetokea ? Happy aliniaga kwamba anakuja kwako leo asubuhi lakini nikashangaa anarudi akiwa analia.Kila nikimuuliza hataki kunijibu.Nini kimetokea kati yenu? Mmegombana? Nimemweleza kwamba uko hapa na unahitaji kuonana naye lakini amekataa kata kata na amesema uondoke haraka sana wewe na yeye basi.Nini kimetokea? Tafadhalio naomba uniweke wazi”
“Mama ni kweli kuna jambo limetokea kati yangu na yeye na ndiyo maana nimekuja hapa ili tuweze kuliongea na kulimaliza.Naomba unisaidie mama niweze kuonana naye”
“Nashindwa nikusaidiaje mwanangu kwa sababu Happy amekataa kabisa kuonana nawe.”
Patrick akainama na kufikiri kisha akasema
“Mama naomba unipeleke chumbani kwa Happy nikaongee naye huko huko”
“Tafadhali baba naomba usiende huko.Naogopa kusijetokea matatizo”
“Hakuna tatizo lolote linaloweza kutokea.Naomba unipeleke mama” akasisitiza Patrick.Mama yake Happy akamuongoza Patrick hadi chumbani kwa Happy na kumkuta Happy akiwa amejiinamia kitandani akilia
“Mama kwa nini umemleta huyu chumbani kwangu ??Akauliza Happy ka ukali
“Happy naomba muongee na kumaliza tofauti zenu.Patrick amekuja hapa ili muongee na msawazishe kilichotokea.Tafadhali nawaombeni msigombane.Ongeeni mambo yenu na muelewane”
“Mama naomba mtoe huyu mtu nje.Sitaki kumuona tena katika maisha yangu” akasema Happy kwa ukali
“Mama naomba utuache wenyewe” akasema Patrick na mama yake Happy akatoka mle chumbani.Patrick akafunga mlango
“Patrick go out.Get out of my room” akasema Happy kwa ukali
“Happy naomba unisikilize .Nimekuja hapa kuongea na wewe.Nimekuja kuomba samahani kwa maneno niliyoyasema.Happy naomba unisamehe kwa maneno yote niliyoyasema.” Akasema Patrick
“ Patrick sihitaji kuongea nawe kitu chochote tena.tafadhali ondoka”
“Happy naomba unielewe.Sintaondoka humu chumbani mpaka pale utakaponisikiliza ninachotaka kukwambia.Tafadhali Happy usilifanye jambo hili kuwa gumu kwangu. Tafadhali naomba unisikilize malaika wangu.” Akasema Patrick huku akipiga magoti kumsihi Happy atulize hasira na wakae waongee
Happy akastuka ghafla na kumtazama Patrick usoni.
“what you’ve just said? Am I your angel ? No you are mistaken.Mimi ni mwanamke Malaya na siwezi kuwa malaika wako.Please Patrick stand up and go and don’t dare look for me again in your life.It’s over between us.It’s been all lies.You said yourself ” akasema Happy
“Happy tafadhali naomba unisikilize.Nilitamka maneno yale machafu kutokana hasira nilizokuwa nazo.Sikuwa naufahamu ukweli halisi.Nisamehe sana Happy”
“Now do you know the truth?
“Yes ! I know the truth.Alois told me everything”
“Do you believe what he told you?
“You tell me! Is all that true? Akauliza Patrick .Happy akainama chini akafuta machozi
“Yes..thats the truth”
“Ouh Happy ! Kwa nini hukunieleza mapema? Kwa nini ukaniacha nikiteseka muda huu wote na kujenga chuki juu yako? Nilitamani hata kujitoa uhai wangu kwa kitendo kile nikiamini ulikifanya kwa makusudi.Endapo ungekimbia na kunieleza ukweli mapema wala tusingefika hapa tulipofika sasa hivi.” akasema kwa uchungu Patrick
“Nilijua Savanna atakueleza ukweli wote kwa sababu yeye alifahamu kila kitu kilichotokea na yeye ndiye aliyeratibu safari ya mimi kuondoka hapa nchini kwenda Kigali Rwanda.” Akasema Happy
“Baada ya tukio lile nilipatwa na uchungu mkubwa sana nilikata tamaa hata ya kuendelea kuishi.Nilifanya jaribio la kujitoa uhai kwa kunywa sumu lakini niliwahishwa hospitali na wakayanusuru maisha yangu.Patrick naomba uelewe kwamba haikuwa dhamira yangu kuondoka na kukuacha peke yako ukiteseka kwa kosa ambalo nililitenda mimi lakini kutokana na tukio lile nililazimika kuondoka kuikwepa aibu kubwa niliyoipata.Nilikata tama kabisa ya kuendelea na mahusino yetu na niliamua kukukabidhi kwa Savanna .Niliamini anakupenda na wewe unampenda na kwake utakuwa katika mikono salama.Siku zote nilizokaa mbali nawe niliteseka sana na sikuwa na amani hata kidogo hadi nilipokuja kukuona tena .Patrick naomba unisamehe kwa matatizo yote niliyokusabishia.Nimekuwa chanzo cha matatizo mengi katika maisha yako.Nina imani pamoja na mateso na maumivu yote niliyokuletea utatafuta ndani ya moyo wako nafasi ya kunisamehe ili niweze kuishi kwa amani.Najua siwezi kuulipa wema wako wote ulionitendea na sijui nifaye nini ili niweze kuifuta taswira hii mbaya ambayo tayari imejengeka kichwani kwako. Nilichokifanya ni kitua mbacho hakisameheki japo sikuwa na namna nyingine ya kufanya.Niliamini ninafanya vile kuokoa maisha ya mwanaume nimpendaye.Nimekuumiza sana Patrick.” Happy akashindwa kuendelea akaanza kulia.Patrick akamfuata na kumkumbatia
“Please Happy forgive me for everything.Sikuwa naufahamu ukweli.” akasema Patrick
“Patrick ni mimi ndiye unayetakiwa kunisamehe kwa kuwa nimekukosea sana na kukusababishia mateso makubwa.Patrick I deserve any punishment from you and the best punishment is to stay away from you…” akasema Happy
“Shhhhhhhhhhh..!!!! Please Happy don’t say anything.Kamwe hustahili mateso au adhabu ya aina yoyote ile ila waliokutenda kitendo kile na kukusababishia mateso makubwa namna hii lazima wapate adhabu kali sana.” Akasema Patrick huku akiendelea kumkumbatia Happy kwa nguvu
“so have you forgiven me? Akauliza Happy
“Yes ! Yes ! I’ve forgiven you.Have you forgiven me? Akauliza Patrick
“Niliumia sana kwa maneno uliyonitamkia leo.Nimelia sana lakini mwisho wa siku pamoja na machungu yote bado nimejikuta nikiendelea kuwa mtumwa kwako.Nitaendelea kuwa mtumwa kwako kwa maisha yangu yote .Patrick kamwe siwezi kuwa na hasira au kinyongo kwako.You are forgiven” akasema Happy.Wakakumbatiana kwa nguvu zaidi
“Happy pamoja na yote yaliyotokea kati yetu lakini moyo wangu unashindwa kabisa kukusahau.Hata pale nilipoamini kwamba tayari umeamua kunikimbia na nikaamua kuwa na Savanna bado niliendelea kukukumbuka.Happy tumepitia matatizo mengi na kila pale tulipotenganishwa na nguvu za dunia lakini tunajikuta tumekutanishwa tena katika mazingira ya ajabu ajabu.Happy we’re meant to be together.Nothing than death can separate us in this world.” Akasema Patrick
“Patrick do I still have a place in your heart? Akauliza Happy
“Happy bado nafasi yako ni kubwa sana katika moyo wangu.Siku zote utaendelea kuwa na nafasi ya pekee kabisa ndani ya moyo wangu.Happy nakupenda sana na nitakupenda daima” akasema Patrick
“Ouh Patrick I love you so so so much” akasema Happy na kumbusu Patrick kisha wakakumbatiana kwa nguvu.
“After today nothing will separate us again” akasema Patrck.Happy machozi yakiwatoka wote wawili
“Nini kinakuliza Happy? Akauliza Patrick
“Huwezi kujua ni jinsi gani nilivyoteseka kwa ajili yako Patrick.Siamini kama leo hii niko nawe tena. Niliamini tayari nimekwisha kupoteza na sintakuona tena maishani mwangu lakini kwa nguvu za Mungu niko nawe tena .Nakubaliana nawe kwamba hakuna kitu kinachoweza kututenganisha zaidi ya kifo katika hii dunia.Tumeumbwa ili tuwe wawili” akasema Happy.Patrick akamuangalia usoni na kusema
“Niliambiwa na Savanna kwamba ulikuwa umerudiana na Mike.Ni kweli? Akauliza Patrick.Swali lile likamstua Happy akamuachia Patrick na kutazama chini.
“Ni kweli.Nilirudiana na Mike kwa sababu alinisaidia kuingia tena Marekani Alinishawishi nirudiane naye tena na kwa kuwa sikuwa na mategemeo ya kurejea tena Tanzania nilikubali kurudiana naye.Naomba unielewe Patrick kwamba nilirudiana na Mike si kwa ajili ya mapenzi bali kwa ajili ya kutafuta msaada .I lied to him.I’ll have to say sorry.Najua ataumia sana lakini sina namna nyingine.Siwezi tena kurejea Marekani na siwezi kuendelea kuwa naye tena.Nitaongea naye na atanielewa.Hawezi kunifuata Tanzania kwa sababu amepigwa marufuku asikanyage ardhi ya Tanzania” Akasema Happy.Patrick akaonyesha wasi wasi
“Patrick naomba unielewe kwamba katika dunia hii mwanaume nimpendaye ni wewe pekee na ambaye umejaa moyoni mwangu.Tafadhali naomba unipokee tena katika moyo wako.Naomba nafasi nyingine tena” akasema Happy
Patric akamvuta Happy karibu yake akamkumbatia
“Huna haja ya kuomba nafasi ndani ya moyo wangu.Siku zote nafasi yako ipo hapa ndani ya moyo wangu.Karibu tena ndani ya moyo wangu Happy” akasema Patrick na kumpa Happy busu zito kisha wakakumbatiana kwa nguvu.Ukurasa mpya ukafunguliwa tena kati ya Patrick na Happy

* * * *

“Mimi Patrick ,katika imani,uaminifu na upendo,nakuchukua wewe Happy Kibaho kuwa mke wangu wa ndoa,kushirikiana nawe mipango ya Mungu katika maisha yetu ya pamoja tukiunganishwa katika kristu,Kwa msaada wa Mungu naomba anipe nguvu niwe kiongozi imara wa kiroho katika maisha yetu,katika raha na shida,ugonjwa na afya,furaha na huzuni,mpaka kifo kitutenganishe.Ninakupa kila nilichonacho na mapenzi yangu yote katika jina la yesu kristu.Kwa pete hii ninafunga kiapo changu cha kukupenda wewe Happy Kibaho,Mungu anisaidie kukilinda kiapo hiki,kwa jina la baba na la mwana na la roho mtakatifu Amen.”
Kanisa zima lililokuwa limefurika watu likalipuka kwa kelele za shangwe na vigele gele vingi baada ya Patrick kula kiapo chake mbele ya kanisa huku akimvisha Happy pete ya ndoa.Hii ilikuwa ni siku yao kubwa sana ambayo waliiota kwa muda mrefu.Ni siku waliyofunga pingu za maisha.Miezi mitano imekwiwha pita toka walipokutana tena.Hakukuwa tena na kikwazo chochote cha kuwazuia kufunga ndoa hivyo taratibu zikafanyika ili kuwawezesha kufunga ndoa.
Baada ya kutoka kanisani,ilifuata sherehe iliyohudhuriwa na watu wachache akiwemo Sarah dada yake Veronika pamoja na wazazi wa Savanna.Sherehe hii ilihusisha baadhi ya ndugu wa karibu na marafiki wachache tu.Baada sherehe kumalizika walipanda ndege kuelekea kisiwani Zanzibar kwa ajili ya fungate.

MIEZI 12 BAADAE

Ni saa tatu za usiku katika hospitali ya St Theresa,watoto mapacha wa kike wanazaliwa.Furaha ya Happy ilikuwa haielezeki kwa kuwapata watoto hawa mapacha.Mumewe Patrick ambaye alikuwepo pale hospitali alikuwa pia na furaha iliyopitiliza.
“Wataitwa Babrah na Brenda” akasema Patrick akitaja majina ya watoto wake
Maisha yaliendea kuwa ya furaha kubwa kwa familia hii.Mwezi wa pili baada ya kujifungua ,Mahakama ilitoa hukumu kwa wale wote waliohusika na tukio lililosabisha kifo cha Savanna.Mahakama ilimtia hatiani Loniki kwa kosa la kuua kwa kukusudia na kumhukumu adhabu ya kifungo cha maisha jela.Khumalo ambaye naye alishiriki katika mipango ya Loniki ya kumteka na kumdhallisha Happy,pamoja na kujihusisha na biashara za madawa ya kulevya,ujambazi na kutengeneza filamu za ngono alihukumiwa kifungo cha miaka hamsini gerezani na kazi ngumu.Vijana sita ambao walikuwa wakishirikiana naye walifungwa miaka thelathini kila mmoja kwa kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya.Mahakama pia ilimtia hatiani Linah kwa kujihusiha na njama za kuteka na kudhalilisha na kumhukumu miaka mitano jela.
Baada ya adhabu ile kutolewa,vilifuata vilio toka kwa ndugu na jamaa wa washtakiwa.Mzee Francis Kito na familia yake ambao walikuwepo mahakamni walipeana mikono ya pongezi na Patrick
“haki imetendeka” akasema mzee Kito huku akimkumbatia mke wake
“mahakama imetenda haki” akajibu Patrick
“Siwezi kusema kwamba nimefurahi kwa adhabu hii kwa sababu bado haiwezi kunirejeshea mwanangu Savanna.Lakini hata hivyo hizi ni sheria za nchi na lazima zifuatwe.Kwa upande wangu mimi nimekwisha wasamehe wale wote waliomuua mwanangu na sina kinyongo nao tena” akasema mzee Francis Kito.
Wakati wakiendelea kupeana pongezi kwa hukumu ile ,mara akatokea Sarah ambaye macho yake yalikuwa mekundu.Alikuwa Amelia sana.
“Pole sana Sarah.Hata mimi namuonea huruma sana Loniki lakini hakuna namna nyingine ya kufanya ili kugeuza maamuzi haya ya mahakama.” Akasema Patrick
“Hakuna lolote tunaloweza kulifanya Patrick.Mahakama imefanya kazi yake.Loniki alitenda kitendo cha kikatili sana.Nikikumbuka siku ile ninasikia uchungu mkubwa sana alitaka kutuua sote wawili.Ninaumia moyoni kumuona ndugu yangu wa damu akienda kutumikia adhabu ya kifungo cha maisha gerezani lakini kwa upande wa pili anastahili adhabu ile kutokana na mambo aliyoyafanya.Siku zote nilikuwa nikimmuonya na kumkanya kuhusu mambo ya kulipiza kisasi lakini hakunisikia.” Akasema Sarah
“Binafsi nimekwisha msamehe kwa kosa alilolitenda.Sina kinyongo naye tena cha aina yoyote” akasema Patrick
“hata mimi nimekwisha msamehe muda mrefu” akasema Sarah huku akijifuta machozi
“Patrick nimekuja kukuaga.Ninaondoka nchini”
“Unaondoka nchini? Unakwenda wapi?
“Mume wanu amehamishiwa nchini Holland kikazi kwa hiyo na mimi sina budi kumfuata.Kilichoniweka hapa hadi muda huu ni kusubiri hukumu hii .Kwa sasa baada ya hukumu kutolewa sina tena kitu cha kuendelea kusubuiri.Yanibidi niondoke nikaungane na familia yangu.Nadhani itanisaidia pia kulisahau tukio lile lililotokea.Nilinusurika kuuawa na ndugu yangu wa damu.Tukio lile limeniathiri sana kisaikolojia.Nadhani nahitaji mapumziko na kutuliza akili yangu mbali na hapa nyumbani.Tutakuwa tukiwasiliana mara kwa mara” akasema Sarah
“Nakubaliana nawe Sarah.Tukio lile ni moja ya tukio baya kabisa na unahitaji mapumziko.Nakutakia kila la heri huko uendako.Tuzidi kuombeana na kuwasiliana.Nitakuwa nikimtembelea mama mara kwa mara.Bado ni mama yangu na kwa sasa ambapo Loniki na wewe nyote hampo anahitaji mtu wa kumfariji kwa hiyo nitachukua nafasi yenu.Kwa heri Sarah” akasema Patrick akakumbatiana na Sarah wakaagana akaondoka
Hakukuwa tena na kitu chochote cha kusubiri pale mahakamani Patric na mkewe Happy wakaingia garini na kuondoka.

MWISHO…..
 
Back
Top Bottom