Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,444
- Thread starter
- #81
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 58
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Patrick kwanza naomba ufahamu kwamba hutakwenda gerezani.Hata kama ikitokea kwamba utahukumiwa kifungo basi itapambana hadi nihakikishe ninakutoa.Kuhusu kukusubiri usitie shaka kuhusu hilo.Niko tayari hata kutumia muda wangu wote uliobaki hapa duniani kukusubiri wewe tu kwa hiyo usiwe na hofu hata kidogo na hilo.” Akasema Savanna kwa sauti laini
Waliongea mambo mengi sana usiku huo .Savanna alijitahidi kwa kila alivyoweza kumpa moyo Patrick kuhusu hukumu yake siku itakayofuata.Huu ulikuwa ni usiku mgumu sana kwa Patrick.Alitumia muda mwingi kusali na kumuomba Mungu amuepushe na kifungo
ENDELEA……………..
Familia nzima ya mzee Kibaho ilikuwa imekusanyika kwa ajili ya kusali sala ya jioni kama ilivyo kawaida yao kukutana na kusali pamoja kabla ya kwenda kulala.Siku hii ya leo kulikuwa na maombi maalum ya kumuombea Patrick ambaye hukumu yake ilitegemewa kutolewa siku inayofuata.Pamoja na maombi haya ya familia lakini Happy yeye alikuwa na maombi yake binafsi ya kufunga na kusali kwa muda wa siku tatu akimuomba Mungu amsaidie Patrick achiwe huru.
Baada ya kumaliza maombi yale ya jioni Happy na mdogo wake Margreth wakaenda chumbani kwao.
“Margreth I’m so nervous.Nahisi kama mwili wangu unatetemeka kila nikifkiria whats going to happen tomorrow.” Akasema Happy Margreth aliyekuwa anapanga nguo katika kabati lake akaacha kazi ile na kumfuata Happy
“Do you believe in God? Akauliza Margreth
“Ofcourse I do “ akajibu Happy
“Vizuri.Kama unamuamini Mungu muache atende kazi yake.Hana sababu ya kuogopa hata kidogo.Mtumaini yeye siku zote” akasema Margreth
“Margreth I believe in God lakini nashidwa kujizuia kuwa na wasiwasi.Sifahamu kitakachotokea kesh😵uh Gosh! Akasema Happy
“Ilitakiwa mimi ndiye niwe nimesimama kizimbani siku ya kesho nikihukumiwa na si Patrick.Lakini Patrick ndiye anayehukumiwa badala yangu.Sijawahi kuona mtu mwenye upendo mkubwa na wa ajabu kama huyu.I’m so sorry I’ve lost him and I don’t know what to do to get him back.” Akasema Happy
“Happy tafadhali usiwaze sana kuhusu mambo hayo.Tusubiri kwanza hadi siku ya kesho tuone nini kitatokea na baada ya hapo tutajua nini cha kufanya” akasema Margreth
“Margret sina ujanja tena.Tayari nimekwisha mpoteza Patrick.” Akasema Happy na mara wote wakastushwa na mlio wa simu ya Margreth.Akaichukua na kutazama mpigani halafu akavuta pumzi ndefu
“Its mike” akasema
“Tell him I’m not around” akasema Happy
“Happy siku ya leo hii ni mara ya tatu anapiga simu na hutaki kuongea naye.Happy I dont want to lie anymore.Please talk to him” akasema Margreth
“Ouh My God I don’t know what to tell him” akasema Happy
“Tell him anything.Ana hamu sana ya kuongea nawe.Mike ni mchumba wako.Ukikataa kuongea naye unamuumiza sana na utamfanya ahisi kwamba huku mambo si shwari.Tafadhali ongea naye.” Akasema Margreth.Happy akachukua simu ile ambao bado iliendelea kuita akabonyeza kitufe cha kupokelea simu
“Hallow Mike” akasema Happy.Mara moja Mike akaitambua sauti ya Happy
“Hallo malaika wangu .” akasema Mike kwa furaha
“Unaendeleaje Mike? Akasema Happy
“Ninaendelea vizuri Happy.Nimefurahi sana kuisikia sauti yako.Unaendeleaje? akauliza Mike
“Naendelea vizuri Mike.”
“Nafurahi kusikia hivyo.I miss you a lot my angel” akasema Mike
“I miss you too” akajibu Hapy
”How’s Patrick? Akauliza Mike na kumfanya Happy asite kujibu
“Happy how’s Patrick? Uliniambia kwamba hukumu yake ni kesho?
“Ndiyo Mike hukumu yake ni kesho” akajibu Happy
“Utahudhuria mahakamani? Akauliza Mike
“Ndiyo Mike nitahudhuria kwani ndicho kitu pekee ambacho kimeniweka hapa hadi muda huu kwa hiyo siwezi kukosa mahakamani.” Akajibu Happy
“Are you guys talk often? Akauliza Mike
“Mike mbona una wasi wasi hivyo? Akauliza Happy
“Lazima niwe na wasi wasi mpenzi wangu kwa sababu nafahamu kwamba Patrick ana sehemu kubwa sana moyoni mwako kwa hiyo nashindwa kujizuia kuwa na wivu kila nikifikiria kwamba uko karibu naye na mnaweza mkaonana” akasema Mike
“Usihofu Mike.Mimi na Patrick kilichobaki ni historia tu kati yetu na hakuna chochote kinachoendelea.Tayari kila mmoja ameendelea na maisha yake.Tayari naye ana mchumba na wanategemea kufunga ndoa muda wowote.Kwa hiyo huna sababu ya kuhofu”
“Hizo ni habari njema sana.Kwa hiyo utarejea mara tu baada ya hukumu kutolewa?
“Ndiyo Mike.Ni hicho tu kilichokuwa kinaniweka hapa na baada ya siku ya kesho I’ll say goodbye to Tanzania and leave this blessed country for good.Mike kuna jambo nataka kukueleza” akajibu Happy
“Jambo gani Happy?
“Unakumbuka uliwahi kuniomba nifunge nawe ndoa na nikakwambia kwamba unisubiri hadi hapo nitakapokuwa tayari?
“Ndiyo Happy nakumbuka sana na sijawahi kukuuliza tena kuhusu suala lile kwa sababu nilitaka utafakari na kama ukiwa tayari basi unijibu”
“Mike naomba nikufahamishe kwamba tayari nimekwisha fanya maamuzi yangu na jibu langu ni ndiyo.Nitafunga ndoa nawe Mike” akasema Happy na Mike akaruka kwa furaha asiyaamini masikio yake.
“Ouh Happy kwa muda mrefu sana nimekuwa nikisubiri unitamkie maneno kama haya.Nimefurahi sana mpenzi wangu.Nitaanza maandalizi mara moja na kuwataarifu ndugu na jamaa kuhusu jambo hili jema.”
“Hapana Mike usimwambie mtu yeyote kwanza.Tutawaambia tutakapokuwa pamoja nitakaporudi”
“sawa malaika wangu.Chochote utakacho niamuru nitatii.Ninakupenda sana Happy.Ahsante sana”
“Hata mimi nakupenda sana Mike na ndiyo maana nahitaji kuwa nawe katika maisha yangu yote yaliyobaki hapa duniani” akasema Happy.Wakaagana na kukata simu
“Happy !! akaita Margreth
“Una hakika na hicho ulichokisema?
“Kitu gani Margreth?
“kwamba unataka kuolewa na Mike? Happy akainama na kusema
I don’t know Margreth but I think that’s the best way to do for now.”
“Happy kwa nini umemwambia Mike jambo ambalo huna uhakika nalo?
“Margreth I have to do this.I’ll learn to love Mike.” Akasema Happy.Margreth akainamisha kichwa akaonekana kusikitika
“Unasikitika nini Margreth?
“Ninasikitika kwa sababu you cant swallow back what you’ve promised Mike.Kwa maana hiyo basi unatakiwa usimame katika maneno yako.Lazima uolewe na Mike.Jitahidi usimuumize kama wakati ule.”
Happy akazama katika mawazo mengi na baada ya muda akasema
“Margrteh I’ve made my decision.I’ll marry Mike.Hakuna uwezekano tena wa kuwa na Patrick.I’ve lost him”
**********************
Ni dakika ya pili sasa toka alipoweka shingoni tai yake akitaka kuifunga.Alikuwa amesimama mbele ya kioo kikubwa cha kujtazamia .Sauti ndogo ya muziki ilikuwa inasikika.Patrick alikuwa anabubujikwa na machozi kutokana wimbo uliokuwa uitwao see you again wimbo ulioimbwa na Carrie underwood
I will see you again,woah
This is not where it ends
I will carry you with me oh
Till I see you again
Patrick akaimba kibwagizo cha wimbo ule na mara Savanna akaingia mle chumbani na kuuzima mziki ule
“Patrick mbona unajipa wakati mgumu namna hiyo? Kwa nini ujiumize moyo wako? Just relax.Everything will be fine.Stop torturing yourself.” Akasema Savanna huku akimfuta machozi
“Savanna malaika wangu I’m so scared .Nashindwa kujiuia kuwaza nini kitatokea endapo nitahukumiwa kifungo.Hii ni siku ngumu sana katika maisha yangu”
“Patrick usiwaze sana kuhusu nini kitatokea.Tujiandae kwa maamuzi yoyote yale yatakayotolewa na mahakama.I’ve done my level best as a lawyer lakini mahakama ndiyo yenye kutoa maamuzi.Endapo watatoa adhabu ya kifungo gerezani,tutakata rufaa kama nilivyokuahidi.I’m right here beside you ,you are not alone” akasema Savanna na kumbusu Patrick halafu akamfungia tai
“Now you look perfect.you are so handsome Patrick.I love you” akasema Savanna na kumbusu tena Patrick shavuni
Wakati Savanna akijiandaa Patrick alitoka mle chumbani na kwenda nje ya nyumba
“Ni katika nyumba hii furaha yangu ya maisha iliporejea tena.Endapo nitafungwa gerezani nitaikosa nyumba hii iliyojaa furaha amani na upendo.” Akawaza Patrick halafu akarejea ndani.Savanna alimaliza kujiandaa akajumuika na mpenzi wake mezani wakapata stafstahi
“Are you ready to go Patrick? Akauliza Savanna
“I’m ready” akajibu Patrick na kisha wakatoka wakaingia garini na kuondoka kuelekea mahakamani
* * * *
Saa tatu za asubuhi ilimkuta Sarah tayari amekwisha wasili mahakamani.Aliwahi sana kufika pale ili apate nafasi ya kuonana na Linah ambaye alimwahidi kumpigia simu na kumfahamisha kuhusiana na mpango wa namna watakavyoweza kumdhibiti Loniki asiweze kuutekeleza mpango wake wa kumdhuru Patrick endapo mahakama itamuachia huru,lakini toka walipoonana usiku ule Linah hakumpigia tena simu jambo lililoanza kumpa wasi wasi.Kilichompa wasiwasi zaidi simu ya Linah haikuwa ikipatikana na hakupafahamu mahala alipokuwa amehamia.Mtu pekee ambaye angeweza kumpa jibu la wapi alipo Linah ni Loniki lakini aliogopa kumuuliza chochote kutokana na mahusiano yao kutokuwa mazuri.Pale mahakamani alijaribu kuangaza huku na huko lakini hakumuona mtu yeyote wa familia yake.Akachukua simu na kumpigia mama yake.
“mama shikamoo’
“Marahaba Sarah.Hujambo?
“Sijambo mama”
“Uko wapi Sarah? Si unajua leo ni siku ya hukumu?
“Nafahamu mama.Tayari niko hapa mahakamani.”
“Mbona umewahi namna hiyo?
“Ndiyo mama nimeamua tu kuwahi.Unakuja mahakamani?
“Ndiyo ninakuja niko njiani”
“Uko na Loniki?
“Hapana.Loniki amekuja kuchukuliwa na rafiki yake asubuhi ya leo.Aliniaga kwamba kuna sehemu wanakwenda lakini hatachelewa kufika mahakamani”
“rafiki yake yupi unayemzungumzia? Akauliza Sarah
“Kwani Loniki ana rafiki mwingine zaidi ya Linah? Huyo ndiye aliyefika asubuhi na wakaondoka wote”
“Sawa mama.Mimi utanikuta hapa” akasema Sarah na kukata simu
“Kwa nini Linah hajawasiliana nami kama alivyoniahidi na simu yake haipatikani tena? Amekwenda wapi na Loniki asubuhi hii? Kuna kitu gani kinachoendelea? Inawezekana Linah akawa ameshindwa kupata njia ya kumdhibiti Loniki? Edapo sintakuwa nimeonana naye hadi hukumu itakapotolewa na mahakama ikamuachia huru Patrick basi sintakuwa na njia nyingine zaidi ya kulifikisha suala hili katika vyombo vya usalama.” Akawaza Sarah huku akijaribu kupiga tena namba za simu za Linah bila mafanikio
* * * *
“C’mon Khumalo what happened to you? “ akasema Loniki akiwa na simu mkononi akijaribu kupiga tena na tena namba za khumalo lakini kila alipopiga jibu lilikuwa moja tu
“Namba ya simu ya mteja unayempigia haipatikani kwa sasa.tafadhali jaribu tena baadae.”
“Damn it !!! “ akasema Loniki kwa hasira na kugonganisha mikono yake.Linah aliyekuwa katika usukani akamtazama bila kusema chochote akaendelea na kukanyaga mafuta
Loniki na Linah walikuwa wanaelekea nyumbani kwa Khumalo.Asubuhi na mapema Linah alimfuata Loniki nyumbani kwao na kumfahamisha kwamba Khumalo hakuwa anapatikana simuni,taarifa ambayo ilimstua sana Loniki na akaamuru wamfuate Khumalo nyumbani.Katika siku hii Loniki alimuhitaji sana Khumalo ili aweze kutekeleza mpango waliokuwa wameongea wa kumuua Patrick endapo mahakama ingemuachia huru.Linah alifuata kila alichokisema Loniki lakini moyoni alikuwa akifahamu wazi kwamba Khumalo hakuwepo na walipanga Khumalo atoweke baada ya kupokea fedha toka kwa Loniki.
“Huyu Khumalo mbona anaanza kunipa wasi wasi? Kwa nini hapatikani simuni wakati anajua fika kwamba leo ni siku ambayo Patrick anahukumiwa kwa hiyo lolote linaweza kutokea? Loniki akajiuliza maswali mfululizo.Linah ambaye siku hii ya leo alionekana kuwa mkimya na mwenye wasi wasi mwingi hakujibu chochote
“Say something Linah” akafoka Loniki
“Niseme nini Lonny? Khumalo hapatikani simuni .Tunachotakiwa ni kufika nyumbani kwake na kuangalia kama ana tatizo.Pengine labda simu yake ikawa na matatizo” akasema Linah
“What a stupid woman.Sihitaji tena urafiki na mjinga kama huyu.After today its over.Hanisaidii kitu chochote katika maisha yangu zaidi ya kuniingiza katika mambo ambayo yanaweza kuniletea matatizo.Amenishirikisha katika mipango yake ya visasi na kunisababishia dhambi kubwa .Kitendo cha kumdhalilisha Happy namna ile kinaniumiza sana hadi leo hii.Sitaki tena urafiki na huyu mjinga” akawaza Linah wakati wamekaribia kufika nyumbani kwa Khumalo
Walifika katika jumba la Khumalo.Linah akapiga honi ili wafunguliwe geti.Loniki baada ya kuona mlinzi anachelewa kutoka akafungua mlango wa gari na kushuka garini akaenda kubonyeza kengele ya getini.Baada ya muda kidogo mlango mdogo wa geti ukafunguliwa
“Habari yako? Akasema jamaa mnene aliyefungua geti
“Habari nzuri” akajibu Loniki
“Nikusaidie nini? Akauliza yule jamaa
“Nina shida na Khumalo.Ninaitwa Loniki na mwenzangu pale garini anaitwa Linah.Sisi ni marafiki zake na tuna biashara naye ya muhimu sana”
Una biashara gani na Khumalo?
“Kuna kazi nilikuwa nimeelewana naye aifanye ambayo anatakiwa aifanye leo lakini kitu cha kushangaza ni kwamba hapatikani katika simu hivyo tumeamua kuja hapa nyumbani kwake kuonana naye” akasema Loniki
“Samahani dada yangu.Khumalo hayupo amesafiri” akasema yule jamaa na kumfanya Loniki ahamaki
“Acha utani ndugu yangu.Khumalo amesafiri lini na bila kututaarifu?
“Khumalo hayupo dada amepatwa na safari ya ghafla na kuondoka usiku wa kuamkia leo.” Akasema yule kijana .
“Ouh gosh ! amesema atarudi lini? Akauliza Loniki ambaye alionekana kustushwa sana na jibu lile
“hakusema atarudi lini lakini mara nyingi huwa akisafiri humchukua hata zaidi ya miezi sita kurejea.” Akasema yule kijana na kuzidi kummaliza nguvu Loniki
“Hakuna namna ambayo tunaweza kumpata au kuwasiliana naye ili kama yeye hauypo basi vijana wake waifanye kazi tuliyokubaliana kwani tayari nimekwisha mlipa fedha zote alizozihitaji” akasema Loniki
“Khumalo akisafiri kumpata huwa ni kazi ngumu sana kwa sababu huwa hatulii katika sehemu moja”
Jibu lile likamnyong’onyeza kabisa Loniki akaegemea ukuta.Baada ya kutafakari akaagana na Yule kijana na kurejea tena garini
“ Damn it !!...akafoka Loniki baada ya kurejea garini.Alikuwa amekasirika sana na kijasho kilianza kumchuruzika
“amesemaje yule kijana? Khumalo yuko wapi? Akauliza Linah ambaye alikuwa amebaki garini
“Khumalo amesafiri usiku wa kuamkia leo na haijulikani kama atarejea hivi karibuni” akasema Loniki
“ How could he do that? Kwa nini aondoke kimya kimya bila kututaarifu wakati alijua kabisa tuna mkataba naye na tayari fedha zote alizozihitaji nimeshampatia?Kwa nini ametufanyia hivi?.” Akalalamika Loniki
“kwa hiyo tutafanya nini? Akauliza Linah
“Sina hakika kama ni kweli Khumalo amesafiri .Najua atakuwa amejificha mle ndani.” Akasema Loniki
“Hapana Loniki.Kama umeambiwa kwamba Khumalo hayupo ni kweli atakuwa amesafiri.”
Loniki akageuka akamtazama Linah kwa muda kisha akasema
“How could you believe him so easily?
“Kwa sababu ninamfahamu vizuri Khumalo.Ni mtu ambaye huwa muwazi siku zote na kama imetokea amesafiri ghafla namna hii basi lazima kuna sababu ya msingi sana iliyomuondoa hapa nchini usiku .Inawezekana labda alikuwa anakimbia vyombo vya usalama kutokana na shughulio anazozifanya” Akasema Linah
“you failed me Linah.Wewe ndiye uliyeniambia nimuamini Khumalo.Unaona sasa kitu ambacho ametufanyia? Nini kitafuata iwapo mahakama itamuachia Patrick huru? Linah siwezi kukubali kumuona Patrick akiachiwa huru na akendelea kula raha na Malaya wake huku mdogo wangu akiwa ameoza kaburini.Endesha gari tuondoke” akasema Loniki kwa ukali
“Tunaelekea wapi?
“Turudi nyumbani”
“Lonny huoni kama tutachelewa mahakamani? Nyumbani tunaenda kufanya nini? Akauliza Linah
“Nimesema endesha gari tunarudi nyumbani? Akafoka Lonny.Linah akageuza gari na safari ya kurejea nyumbani ikaanza.
Waliwasili nyumbani kwa akina Loniki na kwa haraka akashuka garini akaelekea moja kwa moja chumbani kwa mama yake.Kabati kubwa la nguo halikuwa limefungwa na funguo,akalifungua na kifungua droo ndogo ndani ya lile kabati halafu akatabasamu
“Nilijua tu lazima itakuwepo,Baba alikuwa na bastora mbili kabla hajafariki.Moja ni ile aliyoitumia Vero kutaka kumtoa uhai yule shetani na nyingine ni hii hapa.Kama Vero alimkosa siku ile,mimi sintamkosa leo.Nimehitimu mafunzo ya kulenga shabaha kwa hiyo nina uhakika mkubwa wa kuufumua ubongo wake leo endapo mahakama itamuachia huru” akawaza Lonny halafu akaibusu bastora ile
“Don’t fail me my baby.Do as I tell you to do” akasema Lonny kisha akaiweka bastora ile katika mkoba wake akachukua funguo za gari lililokuwa la Vero akatoka
“Shuka katika gari hilo .Tutatumia hili hapa” Loniki akamuamuru Linah ambaye alishuka na kuingia katika gari lile alilolitaka Lonny
“Drive” akasema Lonny
“Tunakwenda wapi Lonny? Mahakamani? Akauliza Linah
“Stop asking questions Linah.Endesha gari.Ndiyo tunakwenda mahakamani” akasema Lonny kwa ukali.
“Loniki tafadhali naomba usiwe na hasira na mimi.Nilimuamini Khumalo kwa kuwa ni mtu niliyewahi kufanya naye kazi mara kadhaa” akasema Linah Loniki akamtazama kwa jicho kali na kusema
“Save your breath Linah.Nitamalizana nawe baadae.Kwa sasa niache nifikirie kuhusu plan B” akasema Lonny
“Plan B? akauliza Linah
“Yes Plan B.Wewe na shetani mwenzio Khumalo mmenifanyia jambo baya sana kwa hiyo nitawaonyesha kwamba hata mimi nina uwezo wa kufanya hizi kazi.” Akasema Loniki
“Loniki tafadhali naomba tuheshimiane na usirudie tena kuniita mimi shetani.Kama mimi nitakuwa shetani wewe utakuwa nani? Akasema Linah kwa ukali huku akitaka kulisimamisha gari.
“Shut up you bastard.Usinipandishe hasira zangu muda huu.Kuanzia sasa utafanya kile nitakachokuamuru” akafoka Loniki huku akimuelekezea Linah bastora.Linah akatetemeka
“Ouh gosh ! Kumbe ana bastora..mshenzi huyu amedhamiria kweli kumuua Patrick endapo ataachiwa huru na mahakama.Lazima nifanye jambo kumzuia asifanye anavyotaka kufanya.Nitatafuta namna ya kuwasiliana na Sarah.Najua hadi hivi sasa atakuwa anajiuliza sana ni kwa nini sijampigia simu kumtaarifu chochote kama nilivyokuwa nimemuahidi.Kutwa nzima ya jana nililazimika kutoitumia ile laini yangu ya kawaida kwa sababu nilikuwa na huyu shetani muda wote kwa hiyo niliogopa asije gundua kwamba nilikuwa nawasiliana na Sarah.”akawaza Linah
SEHEMU YA 58
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Patrick kwanza naomba ufahamu kwamba hutakwenda gerezani.Hata kama ikitokea kwamba utahukumiwa kifungo basi itapambana hadi nihakikishe ninakutoa.Kuhusu kukusubiri usitie shaka kuhusu hilo.Niko tayari hata kutumia muda wangu wote uliobaki hapa duniani kukusubiri wewe tu kwa hiyo usiwe na hofu hata kidogo na hilo.” Akasema Savanna kwa sauti laini
Waliongea mambo mengi sana usiku huo .Savanna alijitahidi kwa kila alivyoweza kumpa moyo Patrick kuhusu hukumu yake siku itakayofuata.Huu ulikuwa ni usiku mgumu sana kwa Patrick.Alitumia muda mwingi kusali na kumuomba Mungu amuepushe na kifungo
ENDELEA……………..
Familia nzima ya mzee Kibaho ilikuwa imekusanyika kwa ajili ya kusali sala ya jioni kama ilivyo kawaida yao kukutana na kusali pamoja kabla ya kwenda kulala.Siku hii ya leo kulikuwa na maombi maalum ya kumuombea Patrick ambaye hukumu yake ilitegemewa kutolewa siku inayofuata.Pamoja na maombi haya ya familia lakini Happy yeye alikuwa na maombi yake binafsi ya kufunga na kusali kwa muda wa siku tatu akimuomba Mungu amsaidie Patrick achiwe huru.
Baada ya kumaliza maombi yale ya jioni Happy na mdogo wake Margreth wakaenda chumbani kwao.
“Margreth I’m so nervous.Nahisi kama mwili wangu unatetemeka kila nikifkiria whats going to happen tomorrow.” Akasema Happy Margreth aliyekuwa anapanga nguo katika kabati lake akaacha kazi ile na kumfuata Happy
“Do you believe in God? Akauliza Margreth
“Ofcourse I do “ akajibu Happy
“Vizuri.Kama unamuamini Mungu muache atende kazi yake.Hana sababu ya kuogopa hata kidogo.Mtumaini yeye siku zote” akasema Margreth
“Margreth I believe in God lakini nashidwa kujizuia kuwa na wasiwasi.Sifahamu kitakachotokea kesh😵uh Gosh! Akasema Happy
“Ilitakiwa mimi ndiye niwe nimesimama kizimbani siku ya kesho nikihukumiwa na si Patrick.Lakini Patrick ndiye anayehukumiwa badala yangu.Sijawahi kuona mtu mwenye upendo mkubwa na wa ajabu kama huyu.I’m so sorry I’ve lost him and I don’t know what to do to get him back.” Akasema Happy
“Happy tafadhali usiwaze sana kuhusu mambo hayo.Tusubiri kwanza hadi siku ya kesho tuone nini kitatokea na baada ya hapo tutajua nini cha kufanya” akasema Margreth
“Margret sina ujanja tena.Tayari nimekwisha mpoteza Patrick.” Akasema Happy na mara wote wakastushwa na mlio wa simu ya Margreth.Akaichukua na kutazama mpigani halafu akavuta pumzi ndefu
“Its mike” akasema
“Tell him I’m not around” akasema Happy
“Happy siku ya leo hii ni mara ya tatu anapiga simu na hutaki kuongea naye.Happy I dont want to lie anymore.Please talk to him” akasema Margreth
“Ouh My God I don’t know what to tell him” akasema Happy
“Tell him anything.Ana hamu sana ya kuongea nawe.Mike ni mchumba wako.Ukikataa kuongea naye unamuumiza sana na utamfanya ahisi kwamba huku mambo si shwari.Tafadhali ongea naye.” Akasema Margreth.Happy akachukua simu ile ambao bado iliendelea kuita akabonyeza kitufe cha kupokelea simu
“Hallow Mike” akasema Happy.Mara moja Mike akaitambua sauti ya Happy
“Hallo malaika wangu .” akasema Mike kwa furaha
“Unaendeleaje Mike? Akasema Happy
“Ninaendelea vizuri Happy.Nimefurahi sana kuisikia sauti yako.Unaendeleaje? akauliza Mike
“Naendelea vizuri Mike.”
“Nafurahi kusikia hivyo.I miss you a lot my angel” akasema Mike
“I miss you too” akajibu Hapy
”How’s Patrick? Akauliza Mike na kumfanya Happy asite kujibu
“Happy how’s Patrick? Uliniambia kwamba hukumu yake ni kesho?
“Ndiyo Mike hukumu yake ni kesho” akajibu Happy
“Utahudhuria mahakamani? Akauliza Mike
“Ndiyo Mike nitahudhuria kwani ndicho kitu pekee ambacho kimeniweka hapa hadi muda huu kwa hiyo siwezi kukosa mahakamani.” Akajibu Happy
“Are you guys talk often? Akauliza Mike
“Mike mbona una wasi wasi hivyo? Akauliza Happy
“Lazima niwe na wasi wasi mpenzi wangu kwa sababu nafahamu kwamba Patrick ana sehemu kubwa sana moyoni mwako kwa hiyo nashindwa kujizuia kuwa na wivu kila nikifikiria kwamba uko karibu naye na mnaweza mkaonana” akasema Mike
“Usihofu Mike.Mimi na Patrick kilichobaki ni historia tu kati yetu na hakuna chochote kinachoendelea.Tayari kila mmoja ameendelea na maisha yake.Tayari naye ana mchumba na wanategemea kufunga ndoa muda wowote.Kwa hiyo huna sababu ya kuhofu”
“Hizo ni habari njema sana.Kwa hiyo utarejea mara tu baada ya hukumu kutolewa?
“Ndiyo Mike.Ni hicho tu kilichokuwa kinaniweka hapa na baada ya siku ya kesho I’ll say goodbye to Tanzania and leave this blessed country for good.Mike kuna jambo nataka kukueleza” akajibu Happy
“Jambo gani Happy?
“Unakumbuka uliwahi kuniomba nifunge nawe ndoa na nikakwambia kwamba unisubiri hadi hapo nitakapokuwa tayari?
“Ndiyo Happy nakumbuka sana na sijawahi kukuuliza tena kuhusu suala lile kwa sababu nilitaka utafakari na kama ukiwa tayari basi unijibu”
“Mike naomba nikufahamishe kwamba tayari nimekwisha fanya maamuzi yangu na jibu langu ni ndiyo.Nitafunga ndoa nawe Mike” akasema Happy na Mike akaruka kwa furaha asiyaamini masikio yake.
“Ouh Happy kwa muda mrefu sana nimekuwa nikisubiri unitamkie maneno kama haya.Nimefurahi sana mpenzi wangu.Nitaanza maandalizi mara moja na kuwataarifu ndugu na jamaa kuhusu jambo hili jema.”
“Hapana Mike usimwambie mtu yeyote kwanza.Tutawaambia tutakapokuwa pamoja nitakaporudi”
“sawa malaika wangu.Chochote utakacho niamuru nitatii.Ninakupenda sana Happy.Ahsante sana”
“Hata mimi nakupenda sana Mike na ndiyo maana nahitaji kuwa nawe katika maisha yangu yote yaliyobaki hapa duniani” akasema Happy.Wakaagana na kukata simu
“Happy !! akaita Margreth
“Una hakika na hicho ulichokisema?
“Kitu gani Margreth?
“kwamba unataka kuolewa na Mike? Happy akainama na kusema
I don’t know Margreth but I think that’s the best way to do for now.”
“Happy kwa nini umemwambia Mike jambo ambalo huna uhakika nalo?
“Margreth I have to do this.I’ll learn to love Mike.” Akasema Happy.Margreth akainamisha kichwa akaonekana kusikitika
“Unasikitika nini Margreth?
“Ninasikitika kwa sababu you cant swallow back what you’ve promised Mike.Kwa maana hiyo basi unatakiwa usimame katika maneno yako.Lazima uolewe na Mike.Jitahidi usimuumize kama wakati ule.”
Happy akazama katika mawazo mengi na baada ya muda akasema
“Margrteh I’ve made my decision.I’ll marry Mike.Hakuna uwezekano tena wa kuwa na Patrick.I’ve lost him”
**********************
Ni dakika ya pili sasa toka alipoweka shingoni tai yake akitaka kuifunga.Alikuwa amesimama mbele ya kioo kikubwa cha kujtazamia .Sauti ndogo ya muziki ilikuwa inasikika.Patrick alikuwa anabubujikwa na machozi kutokana wimbo uliokuwa uitwao see you again wimbo ulioimbwa na Carrie underwood
I will see you again,woah
This is not where it ends
I will carry you with me oh
Till I see you again
Patrick akaimba kibwagizo cha wimbo ule na mara Savanna akaingia mle chumbani na kuuzima mziki ule
“Patrick mbona unajipa wakati mgumu namna hiyo? Kwa nini ujiumize moyo wako? Just relax.Everything will be fine.Stop torturing yourself.” Akasema Savanna huku akimfuta machozi
“Savanna malaika wangu I’m so scared .Nashindwa kujiuia kuwaza nini kitatokea endapo nitahukumiwa kifungo.Hii ni siku ngumu sana katika maisha yangu”
“Patrick usiwaze sana kuhusu nini kitatokea.Tujiandae kwa maamuzi yoyote yale yatakayotolewa na mahakama.I’ve done my level best as a lawyer lakini mahakama ndiyo yenye kutoa maamuzi.Endapo watatoa adhabu ya kifungo gerezani,tutakata rufaa kama nilivyokuahidi.I’m right here beside you ,you are not alone” akasema Savanna na kumbusu Patrick halafu akamfungia tai
“Now you look perfect.you are so handsome Patrick.I love you” akasema Savanna na kumbusu tena Patrick shavuni
Wakati Savanna akijiandaa Patrick alitoka mle chumbani na kwenda nje ya nyumba
“Ni katika nyumba hii furaha yangu ya maisha iliporejea tena.Endapo nitafungwa gerezani nitaikosa nyumba hii iliyojaa furaha amani na upendo.” Akawaza Patrick halafu akarejea ndani.Savanna alimaliza kujiandaa akajumuika na mpenzi wake mezani wakapata stafstahi
“Are you ready to go Patrick? Akauliza Savanna
“I’m ready” akajibu Patrick na kisha wakatoka wakaingia garini na kuondoka kuelekea mahakamani
* * * *
Saa tatu za asubuhi ilimkuta Sarah tayari amekwisha wasili mahakamani.Aliwahi sana kufika pale ili apate nafasi ya kuonana na Linah ambaye alimwahidi kumpigia simu na kumfahamisha kuhusiana na mpango wa namna watakavyoweza kumdhibiti Loniki asiweze kuutekeleza mpango wake wa kumdhuru Patrick endapo mahakama itamuachia huru,lakini toka walipoonana usiku ule Linah hakumpigia tena simu jambo lililoanza kumpa wasi wasi.Kilichompa wasiwasi zaidi simu ya Linah haikuwa ikipatikana na hakupafahamu mahala alipokuwa amehamia.Mtu pekee ambaye angeweza kumpa jibu la wapi alipo Linah ni Loniki lakini aliogopa kumuuliza chochote kutokana na mahusiano yao kutokuwa mazuri.Pale mahakamani alijaribu kuangaza huku na huko lakini hakumuona mtu yeyote wa familia yake.Akachukua simu na kumpigia mama yake.
“mama shikamoo’
“Marahaba Sarah.Hujambo?
“Sijambo mama”
“Uko wapi Sarah? Si unajua leo ni siku ya hukumu?
“Nafahamu mama.Tayari niko hapa mahakamani.”
“Mbona umewahi namna hiyo?
“Ndiyo mama nimeamua tu kuwahi.Unakuja mahakamani?
“Ndiyo ninakuja niko njiani”
“Uko na Loniki?
“Hapana.Loniki amekuja kuchukuliwa na rafiki yake asubuhi ya leo.Aliniaga kwamba kuna sehemu wanakwenda lakini hatachelewa kufika mahakamani”
“rafiki yake yupi unayemzungumzia? Akauliza Sarah
“Kwani Loniki ana rafiki mwingine zaidi ya Linah? Huyo ndiye aliyefika asubuhi na wakaondoka wote”
“Sawa mama.Mimi utanikuta hapa” akasema Sarah na kukata simu
“Kwa nini Linah hajawasiliana nami kama alivyoniahidi na simu yake haipatikani tena? Amekwenda wapi na Loniki asubuhi hii? Kuna kitu gani kinachoendelea? Inawezekana Linah akawa ameshindwa kupata njia ya kumdhibiti Loniki? Edapo sintakuwa nimeonana naye hadi hukumu itakapotolewa na mahakama ikamuachia huru Patrick basi sintakuwa na njia nyingine zaidi ya kulifikisha suala hili katika vyombo vya usalama.” Akawaza Sarah huku akijaribu kupiga tena namba za simu za Linah bila mafanikio
* * * *
“C’mon Khumalo what happened to you? “ akasema Loniki akiwa na simu mkononi akijaribu kupiga tena na tena namba za khumalo lakini kila alipopiga jibu lilikuwa moja tu
“Namba ya simu ya mteja unayempigia haipatikani kwa sasa.tafadhali jaribu tena baadae.”
“Damn it !!! “ akasema Loniki kwa hasira na kugonganisha mikono yake.Linah aliyekuwa katika usukani akamtazama bila kusema chochote akaendelea na kukanyaga mafuta
Loniki na Linah walikuwa wanaelekea nyumbani kwa Khumalo.Asubuhi na mapema Linah alimfuata Loniki nyumbani kwao na kumfahamisha kwamba Khumalo hakuwa anapatikana simuni,taarifa ambayo ilimstua sana Loniki na akaamuru wamfuate Khumalo nyumbani.Katika siku hii Loniki alimuhitaji sana Khumalo ili aweze kutekeleza mpango waliokuwa wameongea wa kumuua Patrick endapo mahakama ingemuachia huru.Linah alifuata kila alichokisema Loniki lakini moyoni alikuwa akifahamu wazi kwamba Khumalo hakuwepo na walipanga Khumalo atoweke baada ya kupokea fedha toka kwa Loniki.
“Huyu Khumalo mbona anaanza kunipa wasi wasi? Kwa nini hapatikani simuni wakati anajua fika kwamba leo ni siku ambayo Patrick anahukumiwa kwa hiyo lolote linaweza kutokea? Loniki akajiuliza maswali mfululizo.Linah ambaye siku hii ya leo alionekana kuwa mkimya na mwenye wasi wasi mwingi hakujibu chochote
“Say something Linah” akafoka Loniki
“Niseme nini Lonny? Khumalo hapatikani simuni .Tunachotakiwa ni kufika nyumbani kwake na kuangalia kama ana tatizo.Pengine labda simu yake ikawa na matatizo” akasema Linah
“What a stupid woman.Sihitaji tena urafiki na mjinga kama huyu.After today its over.Hanisaidii kitu chochote katika maisha yangu zaidi ya kuniingiza katika mambo ambayo yanaweza kuniletea matatizo.Amenishirikisha katika mipango yake ya visasi na kunisababishia dhambi kubwa .Kitendo cha kumdhalilisha Happy namna ile kinaniumiza sana hadi leo hii.Sitaki tena urafiki na huyu mjinga” akawaza Linah wakati wamekaribia kufika nyumbani kwa Khumalo
Walifika katika jumba la Khumalo.Linah akapiga honi ili wafunguliwe geti.Loniki baada ya kuona mlinzi anachelewa kutoka akafungua mlango wa gari na kushuka garini akaenda kubonyeza kengele ya getini.Baada ya muda kidogo mlango mdogo wa geti ukafunguliwa
“Habari yako? Akasema jamaa mnene aliyefungua geti
“Habari nzuri” akajibu Loniki
“Nikusaidie nini? Akauliza yule jamaa
“Nina shida na Khumalo.Ninaitwa Loniki na mwenzangu pale garini anaitwa Linah.Sisi ni marafiki zake na tuna biashara naye ya muhimu sana”
Una biashara gani na Khumalo?
“Kuna kazi nilikuwa nimeelewana naye aifanye ambayo anatakiwa aifanye leo lakini kitu cha kushangaza ni kwamba hapatikani katika simu hivyo tumeamua kuja hapa nyumbani kwake kuonana naye” akasema Loniki
“Samahani dada yangu.Khumalo hayupo amesafiri” akasema yule jamaa na kumfanya Loniki ahamaki
“Acha utani ndugu yangu.Khumalo amesafiri lini na bila kututaarifu?
“Khumalo hayupo dada amepatwa na safari ya ghafla na kuondoka usiku wa kuamkia leo.” Akasema yule kijana .
“Ouh gosh ! amesema atarudi lini? Akauliza Loniki ambaye alionekana kustushwa sana na jibu lile
“hakusema atarudi lini lakini mara nyingi huwa akisafiri humchukua hata zaidi ya miezi sita kurejea.” Akasema yule kijana na kuzidi kummaliza nguvu Loniki
“Hakuna namna ambayo tunaweza kumpata au kuwasiliana naye ili kama yeye hauypo basi vijana wake waifanye kazi tuliyokubaliana kwani tayari nimekwisha mlipa fedha zote alizozihitaji” akasema Loniki
“Khumalo akisafiri kumpata huwa ni kazi ngumu sana kwa sababu huwa hatulii katika sehemu moja”
Jibu lile likamnyong’onyeza kabisa Loniki akaegemea ukuta.Baada ya kutafakari akaagana na Yule kijana na kurejea tena garini
“ Damn it !!...akafoka Loniki baada ya kurejea garini.Alikuwa amekasirika sana na kijasho kilianza kumchuruzika
“amesemaje yule kijana? Khumalo yuko wapi? Akauliza Linah ambaye alikuwa amebaki garini
“Khumalo amesafiri usiku wa kuamkia leo na haijulikani kama atarejea hivi karibuni” akasema Loniki
“ How could he do that? Kwa nini aondoke kimya kimya bila kututaarifu wakati alijua kabisa tuna mkataba naye na tayari fedha zote alizozihitaji nimeshampatia?Kwa nini ametufanyia hivi?.” Akalalamika Loniki
“kwa hiyo tutafanya nini? Akauliza Linah
“Sina hakika kama ni kweli Khumalo amesafiri .Najua atakuwa amejificha mle ndani.” Akasema Loniki
“Hapana Loniki.Kama umeambiwa kwamba Khumalo hayupo ni kweli atakuwa amesafiri.”
Loniki akageuka akamtazama Linah kwa muda kisha akasema
“How could you believe him so easily?
“Kwa sababu ninamfahamu vizuri Khumalo.Ni mtu ambaye huwa muwazi siku zote na kama imetokea amesafiri ghafla namna hii basi lazima kuna sababu ya msingi sana iliyomuondoa hapa nchini usiku .Inawezekana labda alikuwa anakimbia vyombo vya usalama kutokana na shughulio anazozifanya” Akasema Linah
“you failed me Linah.Wewe ndiye uliyeniambia nimuamini Khumalo.Unaona sasa kitu ambacho ametufanyia? Nini kitafuata iwapo mahakama itamuachia Patrick huru? Linah siwezi kukubali kumuona Patrick akiachiwa huru na akendelea kula raha na Malaya wake huku mdogo wangu akiwa ameoza kaburini.Endesha gari tuondoke” akasema Loniki kwa ukali
“Tunaelekea wapi?
“Turudi nyumbani”
“Lonny huoni kama tutachelewa mahakamani? Nyumbani tunaenda kufanya nini? Akauliza Linah
“Nimesema endesha gari tunarudi nyumbani? Akafoka Lonny.Linah akageuza gari na safari ya kurejea nyumbani ikaanza.
Waliwasili nyumbani kwa akina Loniki na kwa haraka akashuka garini akaelekea moja kwa moja chumbani kwa mama yake.Kabati kubwa la nguo halikuwa limefungwa na funguo,akalifungua na kifungua droo ndogo ndani ya lile kabati halafu akatabasamu
“Nilijua tu lazima itakuwepo,Baba alikuwa na bastora mbili kabla hajafariki.Moja ni ile aliyoitumia Vero kutaka kumtoa uhai yule shetani na nyingine ni hii hapa.Kama Vero alimkosa siku ile,mimi sintamkosa leo.Nimehitimu mafunzo ya kulenga shabaha kwa hiyo nina uhakika mkubwa wa kuufumua ubongo wake leo endapo mahakama itamuachia huru” akawaza Lonny halafu akaibusu bastora ile
“Don’t fail me my baby.Do as I tell you to do” akasema Lonny kisha akaiweka bastora ile katika mkoba wake akachukua funguo za gari lililokuwa la Vero akatoka
“Shuka katika gari hilo .Tutatumia hili hapa” Loniki akamuamuru Linah ambaye alishuka na kuingia katika gari lile alilolitaka Lonny
“Drive” akasema Lonny
“Tunakwenda wapi Lonny? Mahakamani? Akauliza Linah
“Stop asking questions Linah.Endesha gari.Ndiyo tunakwenda mahakamani” akasema Lonny kwa ukali.
“Loniki tafadhali naomba usiwe na hasira na mimi.Nilimuamini Khumalo kwa kuwa ni mtu niliyewahi kufanya naye kazi mara kadhaa” akasema Linah Loniki akamtazama kwa jicho kali na kusema
“Save your breath Linah.Nitamalizana nawe baadae.Kwa sasa niache nifikirie kuhusu plan B” akasema Lonny
“Plan B? akauliza Linah
“Yes Plan B.Wewe na shetani mwenzio Khumalo mmenifanyia jambo baya sana kwa hiyo nitawaonyesha kwamba hata mimi nina uwezo wa kufanya hizi kazi.” Akasema Loniki
“Loniki tafadhali naomba tuheshimiane na usirudie tena kuniita mimi shetani.Kama mimi nitakuwa shetani wewe utakuwa nani? Akasema Linah kwa ukali huku akitaka kulisimamisha gari.
“Shut up you bastard.Usinipandishe hasira zangu muda huu.Kuanzia sasa utafanya kile nitakachokuamuru” akafoka Loniki huku akimuelekezea Linah bastora.Linah akatetemeka
“Ouh gosh ! Kumbe ana bastora..mshenzi huyu amedhamiria kweli kumuua Patrick endapo ataachiwa huru na mahakama.Lazima nifanye jambo kumzuia asifanye anavyotaka kufanya.Nitatafuta namna ya kuwasiliana na Sarah.Najua hadi hivi sasa atakuwa anajiuliza sana ni kwa nini sijampigia simu kumtaarifu chochote kama nilivyokuwa nimemuahidi.Kutwa nzima ya jana nililazimika kutoitumia ile laini yangu ya kawaida kwa sababu nilikuwa na huyu shetani muda wote kwa hiyo niliogopa asije gundua kwamba nilikuwa nawasiliana na Sarah.”akawaza Linah

