MISS TANZANIA
SEHEMU YA 18
MTUNZI : PATRICK.CK
CONTACT : 0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Margreth hebu nieleze Happy kaenda wapi?Najua ni lazima unafahamu alikoenda dada yako”
“mama mimi sijui kitu chochote.Kwani wewe alikuaga anakwenda wapi?
“Hakutaka kuniambia anakwenda kupumzika wapi.Lakini wewe ni lazima utakuwa unajua kwa sababu toka ametoka hospitali ni wewe tu ambaye unaongea naye.”
“Hapana mama sijui kitu chochote kile,alivyokwambia wewe na ndivyo alivyoniambia mimi”
“Na vipi kuhuisu shemeji yako Mike?Ina maana hukujua kama anawasili leo ili uende kumpokea?
“Du! Yaani mama nimeshasahau kabisa kama Mike anakuja leo.Vipi ameshafika?
“Saa nyingi sana.Ila nyie watoto!!!Yaani mwenzenu anakuja hamtaki hata kwenda kumpokea.Halafu kitu kingine cha ajabu,amempigia simu Happy mbele yangu na Happy kakataa kupokea na mwishowe akazima simu kabisa.Hivi kuna kitu gani kinaendelea?
“Mhhhh” Margreth akaguna.Akamwacha mama yake hapo sebuleni na kuingia chumbani kwake.akajifungia na kujaribu kumpigia Happy lakini simu yake ilikuwa tayari imezimwa.akajitupa kitandani.
ENDELEA...................
Ni saa tatu za usiku katika hoteli ya Kobe Village chumba namba 68 kilikuwa na mwanga hafifu wa bluu.Sauti ya muziki laini ilisikika kwa mbali.Chumba chote kilikuwa kikinukia uturi mzuri wenye harufu ya ajabu.Chumba hiki kwa sasa kilikuwa katika mkao wa mahaba mazito.
Juu ya kitanda kikubwa watu wawili walikuwa wamekumbatiana wakiwa katika mahaba mazito.
“Patrick” Happy akaita kwa sauti laini,nyororo ya kimahaba huku akimchezea chezea nywele za kifuani.
“Yes darling “ Patrick akaitikia
Happy ambaye tayari macho yake mazuri meupe yalikuwa yamelegea kama amekula kungu akasema
“Patrick najilaumu sana kwa kuamua kuondoka na kukuacha peke yako.Narudia tena kuomba msamaha kwa kitendo hiki cha kukuacha peke yako na wala sintachoka kufanya hivyo tena na tena kwa sababu ni kitendo ambacho kilisababisha mimi na wewe tukatengana.Kama nisingeondoka tungekuwa na maisha yetu ya raha mstarehe.Leo hii nahisi amani na raha ya ajabu.Raha ambayo nimeikosa kwa miaka mingi.Leo hii najisikia raha ya aina yake kama niliyokuwa nikiipata kipindi tukiwa shuleni.Msisimko niliokuwa nao kipindi kile pindi nikiwa karibu nawe bado haujapotea.Nikiwa nawe sihisi tatizo lolote.Nahisi raha kila mahali”
Patrick akatabasamu akausogeza mkono wake usoni na kurudisha nyuma nywele ndefu za binti huyu mrembo ambazo tayari zilikuwa zimevurugika kutokana na kuzichezea.
“Happy hata mimi ninajisikia hivyo hivyo.Sikutaka kuamini moja kwa moja kuwa hauko tena maishani kwangu.Nilimuomba Mungu anisaidie ili kabla siku zangu hazijaisha hapa duniani niwe nimekuona walau kwa mara ya mwisho.Mungu amesikia sala yangu na tayari amenijibu.Leo hii niko nawe tena.”
Patrick akamvuta Happy karibu zaidi na kumpiga busu zito mdomoni.
‘Patrick naomba nikuulize kitu na tafadhali naomba uwe wazi kwangu.usinifiche kitu hata kidogo”
“C’mon baby uliza chochote usihofu ,kwako hata siri za baba yangu nitakupa”
Wote wawili wakacheka.
“Umeshaanza utani wako nawe”
“Usijali mama uliza”
Happy akatulia kidogo kana kwamba anakumbuka kitu kisha akauliza.
“Hivi Patrick ni kwa nini uliamua kunidangaya kuwa umekufa?
Patrick akastuka,akainuka na kukaa kitandani jasho likaanza kumchuruzika.
“What !!! ….me?…Dead?…..why ? Patrick alijikuta akitamka maneno mfululizo huku akimtazama Happy..
“Happy nashindwa kuelewa ,eti nilifanya nini??!!……..
Happy aliuona mstuko mkubwa wa wazi katika sura ya Patrick akaanza kuogopa kwani alisikia Patrick ana matatizo ya moyo.akamsogelea akamkumbatia na kumbusu akamsugua sugua shingo na kuhakikisha ile hamaki aliyokuwa nayo Patrick imekwisha halafu akaendelea
“Kama unakumbuka kipindi nimeondoka kwenda kusoma tulikuwa tunawasiliana vizuri sana.Hii ilinipa faraja na kuupunguza umbali uliokuwapo kati yetu.Lakini ilitokea siku moja ambayo kwa kweli ni vigumu sana kuisahau katika maisha yangu.Ni siku hii ndiyo iliyobadili kabisa maisha yangu,siku niliyopokea barua toka kwa dada ambaye alijifahamiha kuwa alikuwa ni jirani yenu mlikokuwa mkiishi Sumbawanga.Katika barua hiyo alisema kuwa anasikitika kunitaarifu kuwa eti umefariki dunia ukiwa gerezani kwa maradhi ya kuhara”
Patrick akasimama na kushika kiuno.
“Happy please tell me it’s a joke”
Happy akamtazama kisha akasema.
“Its not a joke Patrick.Baada ya kupata taarifa ile nilipatwa na mstuko,sikutaka kusoma tena,na wala sikuona tena faida ya kushi.You were my everything.Kwa bahati nzuri baba na mama walisafiri haraka sana na kuja kunifariji na kunifanya niendelee kuishi kwani vinginevyo ningekwisha jiua muda mrefu.Patrick ,ilipita miaka mingi bila ya kuwa na furaha na amani moyoni mwangu.Furaha yangu ulikuwa ni wewe pekee.Nilikuwa nikiomba usiku na mchana kwamba taarifa ile isiwe ya kweli na kwamba siku moja ungejitokeza lakini siku zikaenda na hukutokea.Taratibu baada ya miaka kadhaa kupita nikakubaliana na matokeo kuwa tayari umekwisha fariki.Hatimaye baada ya kumaliza masomo nikarudi nyumbani na kitu chja kwanza kukifanya ilikuwa ni kutafuta mahala ulipozikwa.Nilienda mpaka Sumbawanga nikauliza nikaambiwa kuwa familia yako ilikwisha hama muda mrefu sana.Nikaenda tena kule Iringa ulikokuwa umefungwa nikaambiwa kuwa ulihamishwa gereza na kupelekwa Songea.Nikachapa mguu hadi Songea katika gereza ulilohamishiwa pale ndipo niipoufahamu ukweli.Niliwekwa wazi kuwa ulimaliza kifungo chako na ukaachiwa huru.Pale ndipo nilifahamau kwamba hukufa gerezani na kwamba kuna uwezekano mkubwa ukawa mzima.Pamoja na kuufahamu ukweli huo nilikonda kwa kujiuliza swali moja nililokosa mtu wa kunipa jibu,kwa nini unifanyie vile?.Sikujua sababu yaw ewe kuamua kunifanyia vile yaani kusingizia umekufa na kunifanya mimi niishi maisha ya kuteseka miaka yote hii.Nimekuwa nikimuomba Mungu anikutanishe nawe ili walau nifahamu sababu iliyopelekea unifanyie vile.Patrick you were the only man I real loved and trust.I gave myself to you .Please tell me why you did that ,I’ll understand.” Happy aliongea katika hali ya uchungu sana huku ameiweka mikonoyake kifuani kuonyesha machungu aliyokuwa akiyapata
Patrick jasho lilikuwa likimtiririka kama mtu aliyemaliza mbio ndefu.Ingawa chumbani mle mlikuwa na kiyoyozi lakini hakikusaidia kulipunguza joto alilokuwa akilisikia baada ya kuipata taarifa ile.Alisimama na kuzunguka zunguka humo chumbani.
“Happy ! sijui hata nianzie wapi.I’m confused”
Happy akamsogelea akachukua kitambaa na kumfuta jasho lililokuwa likitiririka kwa fujo.
“Please tell me Patrick.Tell me everything.I’ll understand” Happy akasema kwa sautiya upole sana
“Happy sina hakika kama utaniamini na kunielewa.Ukweli ni kwamba haya yote uliyoyasema wewe kwangu mimi ni mageni kabisa.Hakuna ninachoweza kukisema au kukitolea maelezo..Niliyatoa maisha yangu kwa ajili yako ,iweje leo nijifanye nimekufa?bado hainiingii akilini . Happy kumbuka nilikuwa radhi hata kuua japo sikukusudia kwa ajili ya upendo niliokuwa nao kwako iweje leo niamue kutunga kitu ambacho kimetutenganisha?Nashindwa kupata jibu.Katika maisha yangu hakuna kitu ambacho sikupenda kukiona kama kuona ukiumia na hilo unalifahamu fika.Sasa kwa nini basi niamue kuumiza moyo ako kwa kujifanya nimekufa?
Akatulia akafuta jasho.Happy akalifungua sanduku lake dogo akatoa bahasha ambayo ilikwisha anza kuchakaa pengine ni kutokana na kushikwa mara nyingi sana.akatoa karatasi iliyokuwamo ndani ya ile bahasha na kumkabidhi Patrick.
“Barua yenyewe hii hapa hebu isome”
Patrick akatumia dakika kadhaa kuisoma barua ile.Alipomaliza kuisoma akarudia tena na tena.Uso wake wote ukajaa machozi.Midomo ikawa ikimtetemeka kwa hasira,akashindwa kitu cha kuongea.
“Umeona Patrick? Hivyo ndivyo ilivyokuwa” akasema Happy
Kikapita kimya cha dakika kadhaa hapo ndani,kila mmoja akiwaza lake.Patrick akakumbuka toka siku ya kwanza alipokutana na Happy katika kituo cha basi Mbalamaziwa Iringa na hapo ndipo ulipoanzia urafiki wao.Picha za uhusiano wao wakiwa shuleni zikamjia mpaka siku ile alipomuokoa Happy toka katika mikono ya wabakaji .Akakumbuka pia siku alipohukumiwa kifungo cha miaka mitano gerezani na mpaka siku Happy aliyokuja kumuaga kuwa anakwenda Ulaya kusoma.Ghafla akakumbuka siku alipopata taarifa toka kwa Veronika kuwa Happy ameolewa na hatarudi tena Tanzania.Alikumbuka jinsi alivyozimia kutokana na taarifa ile.Machozi yakamtoka.
Patrick akakohoa kidogo kisha kwa sauti yenye kitetemeshi akasema
“Happy nimekusikia na nimekuelewa naomba sasa na mimi nikupe hadithi yangu.Naomba unisikilize kwa makini na unielewe”
“Baada ya wewe kwenda kusoma Ulaya,huku nyuma nilihamishwa gereza na kupelekwa Songea katika gereza jipya kabisa.Siku moja nilikuwa nimepangiwa kutengeneza mazingira katika nyumba ya mkuu wa gereza.Siku hiyo mkuu wa gereza hakuwepo.Nikiwa naendelea na kazi alitokea dada mmoja ambaye alionyesha kuwa na roho ya huruma sana.Alinikaribisha chai nzuri mchana huo aaknikaribisha chakula.Ni dada mcheshi,mchangamfu,na mwenye huruma.Kwa mujibu wa maelezo yake ni kuwa pale alikuwa amekuja kumsalimu mjomba wake ambaye ndiye yule mkuu wa gereza.Baadae alijitambulisha kwangu kuwa anaitwa Veronika.Taratibu mimi na Veronika tukawa marafiki.Nilimhadithia mkasa mzima wa maisha yangu kwa sababu nilitokea kumwamini.Ukiacha wazazi wangu Veronika ndiye mtu pekee aliyekuwa akinipa moyo,kunifariji na kunipa ushirikiano wa kutosha.Muda wake ulipoisha alirudi Dar es salaam kuendelea na shughuli zake aliahidi kuwa angekuwa anakuja mara kwa mara kunitazama.Kwa hiyo nikamuomba yeye awe ni kiungo baina yetu yaani mimi na wewe.Kwa kuwa yeye aliahidi kuja mara kwa mara kuniona nikaona ni bora mawasiliano yetu yaliyokuwa yameanza kufififa yawe yakipitia kwa Veronika.Nikaandika barua na kumkabidhi ili aende akaiposti afikapo Dar es salaam.Siku moja ambayo sintakuja kuisahau alikuja Vero na kuniambia kuwa alikuwa na taarifa ambazo si njema sana.Nilijikaza kiume na kumuomba anieleze.Vero aliniambia kuwa Barua aliyokutumia imerudishwa kwa kuwa haupo tena katika chuo kile ulichokuw ukisoma.Akaendelea kusema kuwa alielekezwa mahala ulipoamia na akakupigia simu lakini ukamjibu kwa kejeli kuwa huanmuda na mimi tena, na wala huna mategemeo ya kurudi tena Tanzania.Alizidi kudai kuwa alimtumia binamu yake aishiye huko huko marekani kufanya uchunguzi na akagundua kuwa tayari ulikuwa umeolewa na tayari ulikuwa ni mjamzito.Nilianguka na kuzimia Sikutaka kuamini moja kwa moja taarifa zile lakini kwa kuwa nilikuwa kifungoni sikua na la kufanya ili kuupata ukweli.Niliwaomba wazazi wangu wanisaidie kufanya uchunguzi juu ya jambo hili lakini wao ndio hawakutaka kabisa hata kunisikia nikilitamka jina lako tena.Siku zilikwenda bila ya mawasiliano yoyote baina yetu na taratibu nikaanza kuukubali ukweli kuwa haupo tena na mimi.Mpaka siku namaliza kifungo changu sikuwa nimepata barua yoyote toka kwako.Nilimaliza kifungo na nikaanza upya tena kuyatengeneza maisha yangu.Nikasoma ,nikamaliza na hatimaye nikaanza maisha yangu ya kujitegemea.Siku moja nikiwa natazama luninga ,warembo waliokuwa wakishiriki fainali za kumtafuta mrembo wa Tanzania walikuwa wakijinadi nilikuona ukipita.Sikuamini nikaanguka na kupoteza fahamu.Na ni hapo ndipo matatizo ya moyo yalipoanza.Hakuna mtu yeyote anayefahamu nini chanzo cha maradhi yangu zaidi ya rafiki yangu wa pekee Andrew.Nilijitahidi ili niweze kukuona siku ile ya shindano lakini kwa bahati mbaya mara tu uliponiona na wewe ukapatwa na mstuko ukaanguka na kupoteza fahamu.”
Patrick akanyamaza akamwangalia Happy usoni.Macho yake yalijaa machozi.Hadithi ya Patrick ilimchoma moyo sana.Donge kubwa likamkaba kooni.Hakuwa na la kufanya zaidi ya kulia.Patrick akamuonea huruma ,akamkaribia na kumfuta machozi kwa kitambaa chance.
“nyamaza Happy .Nyamaza mrembo wangu.Usilie tena.Hayo yameshapita”
Ilikuwa vigumu kwa Happy kunyamaza kutokana na hasira alizokuwa nazo.
“Nashindwa Patrick kunyamaza kutokana na ukatili niliofanyiwa .Ni bora mt aliyenifanyia hivi angeniua kabisa kuliko kuniacha nikiteseka kwa muda mrefu namna hii.”
Kimya kikapita .Patrick akasema
“Happy nafikiri mpaka hapa hakuna wa kumlaumu mwenzake kwa yaliyotokea.Kila mmoja amekwishapata picha halisi ya nini kilichotokea.Sisiti kusema kuwa Veronika ndiye chanzo kikubwa cha sisi kutengana.Nina imani kubwa kuwa ni yeye tu ndiye aliyeuvuruga uhusiano wetu kwa kutunga uongo huu mkubwa.Hakuna mwingine anayeweza kufanya kitu kama hiki zaidi yake.”
Patrick akainuka na kuelekea mezani huku akiwa amefura kwa hasira.
“I hate you Vero.I hate you..!!”
Alitamka maneno haya kwa hasira sana huku akitokwa na machozi.Happy aliyekuwa amekaa kitandani akaogopa.Hakuwahi kumuona Patrick akiwa katika hasira namna ile.Taratibu akamsogelea na kumshika mkono.
“Calm down Patrick.Its ok.”
“Happy I hate this woman so much.Ametutesa kwa kwa kipindi kirefu sana.Kwa nini? she must pay for this”
Happy akamwacha Patrick atulie kwanza na baada ya dakika kadhaa akasema.
“Patrick”
Patrick akastuka na kumwangalia Happy .
“Patrick” Happy akaita tena.
“Yes Happy nakusikiliza”
“After all that happened do you still love me?
Patrick akastuka kwa swali lile,akainuka na kumsogelea zaidi Happy ,akamshika mikono yake yote miwili akamtazama usoni.
“Happy ” akatulia kidogo halafu akaendelea.
“World do change,weather and climate do change,people do change,everything do change but Patrick never change.I’m the same Patrick you know,who loves you that much.Nothing has changed.Pamoja na yote yaliyotokea lakini I’ve never stoped loving you not for a second.Now that I’ve known the truth I love you even more.Do you still love me?
Kauli ile inamfanya Happy atoe machozi.Midomo inamtetemeka anashindwa kuomgea.Patrick akamuangalia machoni na kumuuliza tena.
“Happy am I still have a place in your heart ?
Happy akajikakamua na kusema
“Patrick you were the first man ever happened in my life.You were my first man I loved.You were the fisrt man to win my heart.I gave you my heart,my body,soul and everything.You were my angel,my Hero.No body will ever win my heart than u did.I’m everything I am because you loved me Patrick.Possibly there could be no Miss Tanzania Happy Kibaho now if its not for your love and sacrifices.Pamoja na yote yaliyotokea Patrick I still love you more and more.U still have chance in my heart,but I’m sorry Patrick….”
Happy akashindwa kujizuia kulia kwa sauti.
“Sorry? Sorry for what Happy ? Patrick akauliza
“Its complicated”
Patrick taratibu akahisi kama nguvu zinamuisha
“Complicated?How”
“Patrick baada ya kuamini kuwa tayari umekwisha kufa basi nikaamua kuwa na mpenzi mwingine.Mike cambell ndiye mpenzi wangu niliyenaye kwa sasa na tayari amekwisha nivisha pete ya uchumba.I’m so sorry Patrick”
Patrick alihisi kama vile kila kitu mle ndani kilikuwa kikizunguka.hakuamini kama ni kweli anaweza kumkosa Happy kirahisi rahisi namna ile.akaunyoosha mkono wa Happy na kuangalia kidoleni.Ni kweli Happy alikuwa na pete ya uchumba kidoleni.Patrick akaingalia huku machozi yakimlenga lenga.wakati Patrick akiwa ameduwaa akiiangalia ile pete ya uchumba kidoleni mwa Happy akashangaa Happy akikinyoosha kiganja chake na kukishika kidole kilichokuwa na pete ya uchumba.
“I’m right.Its complicated.Hata wewe hii si ni pete ya uchumba? Kila mmoja tayari amekwisha amua kuendelea na maisha yake.Kutokana na hali ilivyokuwa hakukuwa na matumaini ya kuonana tena.Hivyo hakuna mtu wa Kulaumiwa kwa maamuzi haya kati yetu sisi wawili.Kila mmoja hakuwa na njia nyingine zaidi ya kuamua kusahau yaliyopita na kusonga mbele na maisha yake.Kwa hiyo Patrick veronica ndiye mchumba wako?
Patrick akakabwa na donge kubwa kooni.akababaika ajibu nini.
“Happy ” Patrick akaita
“Happy nasikitika sana.Halikuwa kusudio langu kufanya hivi lakini kwa kipindi hicho sikuwa na jinsi ya kufanya niliamini kuwa tayari ndoto yetu ya kuwa pamoja imeshapotea .Niliamini moja kwa moja taarifa za vero na nikawa na hasira sana juu yako kwa kuamini kuwa ulikuwa umevunja ahadi yetu.Kweli kwa wakati huo ni Veronika pekee ndiye aliyekuwa ni mfariji wangu mkubwa.Ukaribu wetu ukaongezeka na taratibu tukajikuta tukihama toka katika urafiki wa kawaida na kuwa wapenzi.Kwa kiasi kikubwa alinisaidia kusahau mateso na maumivu niliyoyapata juu yako.Uhusiano wetu umedumu kwa muda mrefu sasa na tukaona ni bora tufunge ndoa kabisa.Hivi sasa tunavyoongea tayari maandalizi ya harusi yetu yako katika hatua zake za mwisho.Nafikiri mwezi ujao tarehe za kati kati nitafunga ndoa na vero.”
Happy alishindwa kujizuia kutoa kilio kikubwa.Patrick akamkumbatia.
“Patrick my first love.Patrick my angel,siwezi kuuzuia uchungu huu mkubwa ninaousikia moyoni mwangu.Ninaumia mno kwa kitendo hiki alichonifanyia mwanamke mwenzangu.Ni bora hata angeniua kabisa kuliko kunifanyia ukatili huu mkubwa.Patrick you were my life,and my breath.Veronika has taken you from me, my breath.Sikutegemea kama mwisho wetu ungekuwa hivi”
Happy aliongea kwa uchungu mwingi sana huku machozi mengi yakimtiririka.
“Patrick nimefurahi kuufahamu ukweli.Sikulaumu kwa yaliyotokea.Hukuwa na kosa na wala wewe hupaswi kinilaumu mimi.Kwa kuwa kila mmoja tayari amekwisha anza maisha yake mimi naona ni bora iwe hivyo.Kila mmoja atabaki ni historia kwa mwenzake.Ninachokuomba mpende zaidi Veronika.Kamwe usimfanyie jambo lolote lililo baya.Alifanya kosa,alidanganya na hii yote ni katika kulipigania penzi lako la kweli.Nakubali kushindwa.Sitaki kushindana na Vero sipendi na yeye aje aumie kama nilivyoumia mimi.Nafikiri mateso yangu ni makubwa na sidhani kama anaweza kuyavumilia kama mimi.Mimi namwachia Mungu kwani yeye………….”
“Happy ”Patrick akadakia
“No Patrick don’t say anything yet.I’m hurt.”
Chumba kilichokuwa katika hali ya mahaba mazito muda mfupi uliopita ,sasa kilikuwa ni sehemu yenye majonzi makubwa.Vilio vya chini chini ndivyo vilisikika.ILikuwa ni hali yenye kuhuzunisha sana kwa wapenzi hawa wa zamani.
Happy akamvuta Patrick karibu yake akamkumbatia kwa nguvu.Akamwachia na kumtazama usoni.Kwa sauti yenye kukata kata Happy akaimba
“Don’t,don’t go to your heart how feels.
Don’t be afraid of dreams not real,
Close ur eyes,pretend it’s just the two of us again,
Make belief, this moment’s here to stay,
Touch, touch me the way you used to do,
I know, I could be lie right here with you,
From now on ,you will be with someone else instead of me,
So tonight, let’s feel these memories.
So for the last, hold me now don’t cry, don’t say u were just, hold me now………
Time, time will be kind once we’re apart,
And ur tears, tears will no have place in ur heart.
I wish I,I could say how much I’ll miss you when ur gone,
All my love for yoy will go away……………
Happy akashindwa kuvumilia akaangua kilio kikubwa.
“No Happy !! Noo……This cant be”Patrick akasema kwa hasira.