Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 6,306
- 11,687
Aliyekuwa Kada wa CHAUMMA, Patrick Assenga ametangaza kukihama chama hicho na kurejea Chama CHADEMA ambacho kimsingi ni chama alichokitumikia kwa miaka mingi kabla ya kuhama hapo
Akizungumza na Waandishi wa Habari leo, Jumanne Mei 26.2026, Assenga amesema maamuzi ya kurejea CHADEMA yamekuja baada ya tafakuri ya kina ambayo ameifanya na kujiridhisha pasipo na shaka kwamba CHAUMMA haina mwelekeo na dhamira ya kweli ya kuiondoa CCM madarakani, badala yake amebaini kuwa CHADEMA ndio chama pekee cha siasa chenye dhamira ya kweli kwa Watanzania na kinachoweza kuiondoa CCM madarakani na kushika Dola
Kupitia mkutano huo na Wanahabari, Assenga amewaomba radhi viongozi wa ngazi mbalimbali wa CHADEMA, wanachama na Watanzania kwa ujumla wake kwa maamuzi aliyokuwa ameyachukua hapo awali ya kukihama chama hicho, akiamini kwamba maamuzi hayo aliyafanya bila kutafakari kwa kina.
Pia soma
Patrick Assenga avuliwa Uanachama CHADEMA
- Patrick Assenga ajutia kuondoka CHADEMA, amlaumu Boniface Jacob kwa kutokusema ukweli mapema. Amuomba Mungu ampe ujasiri
Akizungumza na Waandishi wa Habari leo, Jumanne Mei 26.2026, Assenga amesema maamuzi ya kurejea CHADEMA yamekuja baada ya tafakuri ya kina ambayo ameifanya na kujiridhisha pasipo na shaka kwamba CHAUMMA haina mwelekeo na dhamira ya kweli ya kuiondoa CCM madarakani, badala yake amebaini kuwa CHADEMA ndio chama pekee cha siasa chenye dhamira ya kweli kwa Watanzania na kinachoweza kuiondoa CCM madarakani na kushika Dola
Kupitia mkutano huo na Wanahabari, Assenga amewaomba radhi viongozi wa ngazi mbalimbali wa CHADEMA, wanachama na Watanzania kwa ujumla wake kwa maamuzi aliyokuwa ameyachukua hapo awali ya kukihama chama hicho, akiamini kwamba maamuzi hayo aliyafanya bila kutafakari kwa kina.
Pia soma
Patrick Assenga avuliwa Uanachama CHADEMA
- Patrick Assenga ajutia kuondoka CHADEMA, amlaumu Boniface Jacob kwa kutokusema ukweli mapema. Amuomba Mungu ampe ujasiri
