Simulizi: Miss Tanzania

Simulizi: Miss Tanzania

MISS TANZANIA
SEHEMU YA 28
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
" hapana Mike..Kwa sasa Happy amepumzika .Jambo hili lililomtokea ni jambo kubwa na zito kwa maana hiyo anahitaji kupewa muda wa kutosha ili aweze kutuliza kichwa chake...." akasema Margreth.
" Margreth naelewa kuna kitu unakifahamu lakini hutaki kuniambia.Kuna jambo gani linaendelea kimya kimya ?Na kwa nini hutaki kunieleza? Nimeyaona macho ya Happy pale kituo cha polisi na nimehisi kuna jambo amb........." Mike akakatishwa ghafla na Margreth.
" Mike tafadhali naomba uniache nipumzike.Nipigie baadae" Margreth akakakata simu.
" Jamani mbona happy ameleta mambo ! Mike anateseka sana kijana wa watu.Amekuja toka Marekani kwa lengo la kukaa na kufurahi na Happy lakini badala ya furaha imekuwa ni majonzi .Happy kwa nini umewatesa watu wengi namna hii? Kwa mara ya kwanza ninaona ingekuwa vyema kama wewe na Patrick msingekutana kabisa katika maisha yenu yaliyobakia" akawaza Margreth

ENDELEA………………..

Ni saa mbili za usiku bado Happy amejifungia chumbani kwake.Toka amerejea nyumbani hajatoka chumbani kwake na hajataka kuonana na mtu yeyote yule.usiku huu familia yake yote ilikuwa imekaa mezani ikijiandaa kwa ajili ya chakula cha usiku.
" Happy amekwisha taarifiwa kuja hapa mezani? akauliza mzee Kibaho baba yake Happy
" Nimejaribu kugonga mlango wake lakini amekataa kunifungulia.Nilipomgusia kuhusu suala la chakula amesema kwamba hasikii njaa.Nina wasi wasi sana na happy kwa sababu toka amerejea hapa nyumbani hajatia kitu chochote tumboni." akasema margreth.
" Ngoja nikamtoe huko chumbani.Asituumize vichwa huyu mtoto." akasema mama yake Happy akionekana kukasirika.
" hapana usiende..Ntakwenda mimi" akasema mzee Kibaho akainuka na kuelekea katika mlango wa chumba cha Happy akagonga mlango na kusema taratibu
" Happy mwanangu naomba unifungulie mlango nataka kuongea nawe." akasema mzee Kibaho.Happy hakujibu kitu.Mzee Kibaho akagonga tena mlango.
" Happy !! fungua mwanangu.."
Toka ndani ya chumba ikasikika sauti dhaifu ya Happy
" Daddy I want to be alone...I'm sorry"
" Happy nafahamu kwamba unahitaji nafasi ya kuwa peke yako lakini naomba niongee nawe dakika tatu tu"
Kikapita kimya kifupi mlango ukafunguliwa.Sura ya Happy ilikuwa imesawajika.Macho yake mazuri yalivimba na kuwa mekundu kwa kulia.Baba yake akashikwa na uchungu mwingi kwa hali ile aliyomkuta nayo mwanae akamkumbatia na kumfariji.
" Be strong my dear,you are going to be fine...you'll be ok" akasema mzee Kibaho huku akimpiga piga mwanae mgongoni .Kitendo kile kikaamsha tena kilio kwa Happy.Baba yake akamketisha katika sofa lililokuwamo mle chumbani na kumfuta machozi.
" Daddy why always me? akauliza Happy huku akilia.
" Happy mwanangu usilie ,usisikitike na wala kuhuzunika na kujiuliza kwa nini wewe? Nafahamu moyo unauma sana lakini naomba ufahamu kwamba matatizo tumeumbiwa sisi wanadamu na matatizo huja pasi na taarifa.Matatizo yanatukomaza na kutufanya tuwe majasiri hivyo kaza moyo mwanangu na yote yatakwisha.Sisi sote tuko pamoja nawe katika kipindi hiki kigumu kwako..we love you and we support you..."
Maneno yale ya mzee Kibaho yakamfariji sana Happy akafuta machozi .Mara akaingia mama yake akiwa na sahani iliyojaa chakula akaiweka mezani halafu akaenda kukaa pembeni ya Happy.
" Pole sana mwanangu.Huyu baradhuli anataka kukuharibia maisha yako..Kila nikikuona ninapatwa na hasira kali.Kwa nini atake kukusababishia matatizo makubwa namna hii? Ouh Happy mwanangu naomba umuogope kabisa kijana huyo..achana naye kabisa huyo shetani......."
Happy akayafikicha macho yake , akamtazama mama yake na kusema
" Mama tafadhali naomba usirudie tena kumtukana Patrick na kumuita shetani " akasema happy akionyesha kukerwa na kauli ile ya mama yake.
" Mwanangu ninaumia sana kukuona ukiwa katika hali hii.Nina hasira sana na huyo kijana ambaye ninamfananisha na shetani kwa sababu ametaka kukuingiza katika matatizo makubwa.Amesababisha ukalala polisi.Ameliharibu jina lako zuri.Happy mwanangu nakuomba uvunje kabisa urafiki na huyo kijana ..."
" Mom thats enough !!!..tafadhali naomba usiongee kitu ambacho hukifahamu..Naomba niwafahamishe wazazi wangu kwamba Patrick huyu ambaye mnasikia nilikuwa naye wakati tukio hilo linatokea ni yule yule ambaye alifungwa jela kwa ajili yangu.Patrick hakufa kama ilivyokuwa imezushwa."
Wazazi wake wakastuka sana kwa taarifa ile .Wakatazamana usoni. Happy akaendelea
"Katika tukio hilo naomba mfahamu kwamba ni mimi ndiye niliyemsukuma Veronika akajigonga ukutani na kupoteza maisha na wala si Patrick kama watu wanavyofahamu.Kwa kuniepusha mimi na adhabu ya kufungwa,kunyongwa au kifungo cha maisha jela,Patrick ameamua kuubeba yeye mzigo wote wa kesi hii na yeye kuonekana ndiye muuaji.Amefanya yote haya ili kuniweka mimi huru.I'm free now because of him..so this man doesnt deserve to be called a devil. Akasema Happy machozi yakaanza kumtiririka upya.
Hakuna aliyeongea tena wote wakaa kimya.Mzee Kibaho akambembeleza Happy ale chakula japo kidogo Happy akakubali akala chakula.Mama yake alikuwa ameshika tama akimtazama mwanae.

* * *
Ni saa tatu kasoro za usiku Savana alikuwa ndani ya chumba kimoja katika kituo cha polisi akizungumza na Patrick.
" Patrick kesho utapandishwa mahakamani kwa mara ya kwanza kusomewa shitaka halafu utapelekwa mahabusu katika gereza la Uwangwa. Hautaweza kupatiwa dhamana kutokana na uzito wa kosa lenyewe. Nasikitika sana Patrick kwa kupandishwa kizimbani lakini yote haya ni matakwa yako ...Lakini usijali nitatumia kila uwezo nilionao kuhakikisha kwamba unashinda kesi hii.." akasema Savana .Patrick akainama akafikiri kisha akasema
"Nashukuru sana Savana kwa msaada wako mkubwa.Jambo ulilonifanyia ni kubwa sana .Kuhakikisha kwamba Happy anaachiwa huru ni jambo kubwa sana kwangu." akasema Patrick huku akitabasamu
" Patrick mimi siwezi kupingana nawe katika maamuzi yako lakini bado nina mashaka sana na maamuzi uliyoyafanya ya kuamua kuubeba mzigo wa Happy..unafikiri yeye anakupenda kiasi cha kuweza kufanya kama ulivyofanya wewe?..anaweza kuyatoa maisha yake kwa ajili yako? akauliza Savana
" Ninamuamini Happy ananipenda na kwa hilo sina shaka naye.." akasema Patrick..
" Ndiyo unamuamini lakini una hakika kwamba anakupenda kiasi cha kuweza kuyatoa maisha yake kwa ajili yako? akauliza Savana.Patrick akanyamaza kimya.
" Patrick nimekuuliza makusudi swali hili kwa sababu wewe ni rafiki yangu,ninakujali na kukuthamini na ndiyo maana sitaki sadaka hii ya maisha yako uliyoitoa kwa ajili ya Happy iende bure..Nina wasi wasi sana lakini sitaki kuingilia masuala ya ndani ya moyo wako.Wewe ndiye mwamuzi wa maisha yako. Ninachotaka kukuhakikishia kwamba mimi na timu yangu tutasimama kidete na kwa uwezo wetu wote tulionao tutajitahidi kwa kila tuwezavyo kukutetea katika kesi hii..." akasema Savana na kuagana na Patrick akaondoka.Kichwa chake bado kilikuwa kizito mno kuhusiana na kesi hii ya Patrick.
" Patrick ananisikitisha sana .kila nikimuona ninaumia mno..kwa nini ayaweke maisha yake katika hatari kwa kosa la mtu mwingine? ..Patrick ni mtu wangu muhimu sana na nitafanya kila niwezalo ili kumsaidia ." akawaza Savana.
Saa tano za usiku Savana akawasili nyumbani kwake.Akashuka garini na kuelekea ndani.Msichana wake wa kazi alikuwepo sebuleni akimsubiri.Savana akasalimiana naye na kuelekea moja kwa moja chumbani kwake.Mumewe george tayari alikuwa amejilaza kitandani .Mara tu Savana alipoingia akamuendea George akamtikisa na George ambaye alikuwa ameanza kupitiwa na usingizi akaamka.Savana akambusu mumewe halafu akaelekea bafuni kaoga na kurejea kitandani.Akambusu mumewe na kugeukia upande wa pili tayari kwa kulala.
" Savana kuna jambo gani limekutokea katika siku hizi tatu? Nakuona umebadilika sana..Unachelewa kurudi na ukirudi unakuwa umechoka na hutaki hata kuongea na mimi tena.Una matatizo gani? George mume wa Savana akauliza
" George naomba uniache kwa sasa kichwa changu kina mambo mengi mazito" akasema Savana
" Savana naomba unisikilize.Mimi ni mumeo na nina haki ya kukuuliza .Siwezi kukuona ukichelewa kurudi nyumbani na hunielezi chochote .Huna tena muda na mimi mumeo.Unanipa wasi wasi sana Savana.Hebu angaliani hii ni saa ngapi unarejea nyumbani kama mke wa mtu? akauliza George ambaye alionekana kuanza kukasirika.
" George nina kesi ngumu ninayoisimamia kwa sasa .Patrick anashikiliwa kwa kosa la mauaji.." akasema Savana.
" Patrick !! akauliza George kwa mshangao.
" Ndiyo..Patrick..Ina maana hujasikia tukio lililotokea siku tatu zilizopita likimuhusisha Patrick na mauaji? akauliza Savana
" Patrick huyu ambaye aliwahi kuwa mpenzi wako? akauliza George
" Ndiye huyo...." akasema Savana.George akainuka na kumuangalia Savana usoni.
" Sasa nimepata picha halisi.Kumbe kuchelewa kote huku ni kwa ajili ya kesi ya aliyowahi kuwa mpenzi wako..Kwa maana hiyo yeye ni muhimu sana kuliko mimi mumeo ? akauliza George
" George tafadhali usiseme maneno hayo.Patrick ni rafiki yangu na mteja wangu vile vile kwa hiyo sina budi kuishughulikia kesi yake..Kuna tatizo gani kuisimamia kesi yake ? akasema Savana.
" Tatizo lipo..tena tatizo kubwa..Unasimamia kesi nyingi lakini hakuna hata siku moja umewahi kurejea nyumbani usiku kama huu..Yaani unamthamini Patrick ambaye ni muuaji kuliko hata mumeo? Lakini sioni kama ni jambo la ajabu kwa sababu nilihisi lazima jambo hili litatokea siku moja.Bado hujaweza kumtoa Patrick moyoni mwako.Pamoja na miaka hii yote kupita lakini bado hujafanikiwa kumtoa Patrick moyoni mwako..You still love him ...I'm so stupid" akasema George.Savana akainuka na kumtazama George kwa hasira
" George tafadhali naomba usiseme hivyo..Ndiyo niliwahi kuwa mpenzi wa Patrick lakini baada ya kukupata wewe nikaachana naye kwa sababu tayari yeye alikuwa na mpenzi wake Veronika.I'm with you now and not Patrick." akasema Savana
" Yes you are with me ..but am I in your heart? akauliza George
" george mambo gani hayo unayaongea leo? akauliza Savana.
" Savana nafahamu kabisa kwamba hujawahi kumsahau Patrick. Nimekununulia vito vingi vya thamani lakini mbona huvivai na unaendela kuvaa vile alivyokununulia Patrick? You still love him isnt it? akauliza George ambaye tayari alipandwa na hasira
" George ...!! akasema Savana.George akamkaribia Savana na kumuangalia usoni.
" Savana naomba uniangalie machoni na uniambie kwamba unanipenda na unanipenda mimi peke yangu.." akasema George.
" George mambo gani haya unayafanya? ...akauliza Savana
" Savana nimekuuliza swali mbona hunijibu? Huna jibu la kunipa?
Savana akabaki kimya akimtazama George huku akihema kwa nguvu.
" Nilijua tu.You never loved me.All this long you still love Patrick..." akasema George
" George hebu achana na hayo mawazo yako ya kijinga..You know I've always loved you..." akasema Savana.
" Do you love me Savana? Una hakika kwamba unanipenda? akauliza George
"yes I love you and you kow that" akajibu Savana
" Vizuri..sasa kama kweli unanipenda naomba ufanye yafuatayo..Nataka uachane kabisa na kusimamia kesi ya Patrick..Kama kweli mimi ni mumeo na unanipenda nataka uachane na ukae mbali kabisa na kesi hii" akasema George.Savana akainama akafikiri kisha akainua uso wake.macho yake yalijaa machozi.Akamuangalia George usoni kisha akatikisa kichwa.
"I'm sorry George I cant do that..siwezi kufanya hivyo unavyotaka nifanye...Patrick is my friend and he needs me now more than ever..siwezi kuacha kumtetea hata iweje.akasema Savana.George akamuangalia kwa makini usoni kisha akasema.
" Vizuri..huwezi kuacha kumtetea kwa sababu unampenda .Kama hivyo ndivyo naona ni bora nikuache huru uendelee kumtetea Patrick ashinde kesi na uje uishi naye hapa.Mimi nimechoshwa na vituko vyako Savana.Toka tumeanza kuishi pamoja mpaka leo hii ni vituko kila siku..Ni miaka mingapi mpaka leo na hutaki hata kusikia suala la mtoto? Nimechoka Savana.Nakuacha uendelee na huyo Patrick." akasema George huku akivaa nguo zake.Savana akasimama na kumuangalia George kwa macho makali.
" Mimi naondoka Savana..nitakuja kuchukua vitu vyangu kesho..Siwezi kuendelea kuishi nawe wakati moyo wako unampenda mtu mwingine..Siwezi kuendelea kugombania nafasi katika moyo wako..nafasi ambayo tayari amekwisha pewa mtu mwingine.Nimevumilia mengi na ninashukuru kwa kupata jibu leo kwamba chanzo cha haya yote ni Patrick..Nakutakia maisha mema na huyo mhalifu wako...." akasema George
" Dont you dare insult Patrick again infront of me...kwa taarifa yako ninampenda Patrick na nitafanya kila niwezalo niwe naye tena..You are nothing compared to him." akasema Savana kwa hasira..George akakasirika na kutaka kumnasa Savana kibao
" ukijaribu kunigusa nitahakikisha unaozea gerezani...." Savana akamtisha George ambaye alimuangalia kwa hasira kisha akaanza kuondoka.Savana machozi yakamtoka akajitupa kitandani kwa hasira
" Patrick siwezi kukuacha hasa kwa kipindi hiki..Niko tayari kwa lolote lile lakini si kuacha kukutetea..Hakuna mtu yeyote ambaye atanizuia nisikutetee ..Nitasimama nawe hadi dakika ya mwisho .That bastard George is right.sijaweza kukutoa katika moyo wangu hadi leo hii..I still love you so much Patrick.I'll make you love me Patrick and when this is over you'll be mine" akawaza Savana.

* * *
Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu ilifurika watu waliokuja kufuatilia kesi ya mauaji inayomkabili Patrick.Taarifa za Patrick kupandishwa kizimbani na kusomewa shitaka la mauaji zilisambaa kwa kasi na kupelekea idadi kubwa ya watu kujaa mahakamani .Patrick hakuwa mtu anayefahamika sana lakini kutokana na vyombo vya habari hususani magazeti kuandika habari ya tukio lile la kusababisha kifo watu wengi walitaka kumfahamu na hasa baada ya kuandikwa kwamba alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mrembo aliyeitikisa nchi kwa uzuri wake Miss Tanzania Happy kibaho.
Saa tano za asubuhi gari mbili za polisi zikawasili katika mahakama ya kisutu.Patrick akashushwa garini na kuingizwa mahakamani chini ya ulinzi mkali.Savana na jopo la mawakili wanaomtetea Patrick tayari walikwisha fika mahakamani kuanzia asubuhi .Siku hii Savana alionekana mkimya na mwenye mawazo mengi.
" Happy amekuja leo? Patrick akamuuliza Savana wakati wakisubiri kesi yake itajwe.
" Mpaka mida hii sijamuona bado .Inawezekana amefika lakini amejificha mahala akiogopa waandishi wa habari " akasema Savana.
"Ukifanikiwa kuonana naye mpe salamu zangu" akasema Patrick.
" masikini Patrick amejibebebsha mzigo mzito ambao si wake.Sina hakika kama happy anafahamu uzito wa mzigo huu alioubeba Patrick kwa ajili yake." akawaza Savana.
" Savana umefuatilia maendeleo ya baba yangu kule hospitali na kujua anaendeleaje? akauliza Patrick
" Hapana Patrick bado sijafuatilia lakini leo nikitoka hapa nitaelekea hospitali kwenda kumjulia hali baba yako": akasema Savana.
" Nimesababisha matatizo kwa watu wengi . Vero amefariki,baba yangu amelazwa hospitali ,na wengine wengi wameumia sana kwa ajili ya maamuzi yangu. I deserve this..ninastahili adhabu hii ya kukaa gerezani" akasema Patrick kwa sauti ndogo.Savana hakumjibu kitu bali akachukua faili lake na kuanza kumuelekeza Patrick jambo fulani.
Hatimaye kesi ya kusababisha kifo inayomkabili Patrick ikatajwa kwa mara ya kwanza .Mshitakiwa katika kesi hiyo ambaye ni Patrick akasomewa shitaka la kusababisha kifo cha Veronika na hakutakiwa kujibu chochote.Kesi ikapangwa kutajwa tena baada ya wiki tatu na mshitakiwa akaamriwa kupelekwa mahabusu katika gereza jipya la Uwangwa kigamboni.
" Usihofu Patrick .Kesi hii tunaifuatilia kwa umakini mkubwa .Niko pamoja nawe katika kila dakika.Naomba uondoe hofu na uniamini " .Akasema Savana akimpa moyo Patrick wakati akisubiri kupanda katika basi maalum la kubebea mahabusu na kupelekwa gerezani.
" Nakuamini Savana na sina shaka hata kidogo na wewe.Ulifanikiwa kuonana na Happy? akauliza Patrick
" happy sijaonana naye .Nadhani hajafika mahakamani siku ya leo" akasema Savana.
" Una mawasiliano yake" akauliza Patrick
" Nina namba za simu za mdogo wake Margreth.Nitampigia baadae nifahamu maendeleo yake" akasema Savana .Muda huo huo akaingia mmoja wa mawakili wanaounda jopo la kumteta Patrick akamuomba Savana waongozane kuna suala la kisheria linalohitaji ufumbuzi wa haraka.Savana akaagana na Patrick kwa ahadi ya kwenda kumtembelea gerezani kesho yake.
" kwa nini Happy hajafika mahakamani? Ana matatizo gani?Pengine ameshindwa kufika akiogopa macho ya watu " akawaza Patrick baada ya Savana kuondoka.
" Mama ,ndugu zangu na marafiki nimewaona mahakamani .Wote wamekuja kunifariji na kunipa moyo.Japokuwa nimewaudhi na kuwaumiza sana kwa mambo niliyoyafanya lakini bado wananipenda na wamekuja kunionyesha kwamba bado tuko pamoja.Ni familia ya Happy pekee ambayo haijafika mahakamani.Napatwa na wasi wasi nini kimetokea? I love Happy and I trust her with my life.." akawaza Patrick na mara sura ya Veronika ikamjia kichwani akafumba macho na kuuma meno.
" masikini Veronika sina taarifa atazikwa lini.Laiti nigekuwa na uwezo ningehudhuria mazishi yake lakini siwezi tena.Niko mikononi mwa sheria.Pumzika kwa amani vero.Utabaki ndani ya moyo wangu daima.Nitazikumbuka zile nyakati zote za furaha tulizowahi kuwa nazo katika mapenzi yetu. Daima nitaukumbuka upendo wako,ukarimu na ucheshi wako.Natambua ulinipenda kwa moyo wako wote.Kama siku moja nitabahatika kutoka gerezani nitalitafuta kaburi lako na kuweka maua meupe uliyokuwa unayapenda sana enzi za uhai wako,lakini kama nitahukumiwa kunyongwa au kufungwa maisha basi tutakutana mbinguni kwa baba.Pumzika kwa amani Veronika sikutegema kabisa kama mambo yangekuwa namna hii." akawaza Patrick huku akijizuia asidondoshe machozi.
Saa nane za mchana Patrick akapakiwa katika basi maalum la kubebea mahabusu na safari ya kuelekea gereza la Uwangwa ikaanza.Taratibu basi likaanza kuondoka.Kupitia dirishani Patrick akaweza kumuona mama yake ambaye alikuwa amekaa chini kutokana na kuishiwa nguvu,kaka yake Alois akiwa na mkewe,rafiki yake Andrew akiwa na mchumba wake Vick pamoja na ndugu wengine,na marafiki.Wengi walikuwa na nyuso za huzuni kubwa na wengie walishindwa kujizuia kutokwa na machozi.
Patrick akawapungia mkono na taratibu basi likaondoka maeneo ya mahakama kuelekea mahabusu katika gereza la Uwangwa ambako anakwenda kuanza maisha mapya.
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 29
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

Saa nane za mchana Patrick akapakiwa katika basi maalum la kubebea mahabusu na safari ya kuelekea gereza la Uwangwa ikaanza.Taratibu basi likaanza kuondoka.Kupitia dirishani Patrick akaweza kumuona mama yake ambaye alikuwa amekaa chini kutokana na kuishiwa nguvu,kaka yake Alois akiwa na mkewe,rafiki yake Andrew akiwa na mchumba wake Vick pamoja na ndugu wengine,na marafiki.Wengi walikuwa na nyuso za huzuni kubwa na wengie walishindwa kujizuia kutokwa na machozi.
Patrick akawapungia mkono na taratibu basi likaondoka maeneo ya mahakama kuelekea mahabusu katika gereza la Uwangwa ambako anakwenda kuanza maisha mapya

ENDELEA ………………

Gari moja aina ya Lexus lenye rangi nyeusi lilikuwa limeegeshwa katika mahakama ya kisutu.Hakuna mtu aliyekuwa ameitilia maanani gari ile wala kuifuatilia.Ndani ya gari ile yenye vioo vyeusi walikuwemo wasichana wawili waliokuwa wamekaa kimya.Mmoja wao alikuwa akitokwa na machozi
“Happy nyamaza kulia.You have to remain strong.Kulia hakutakusaidia chochote na wala hakutabadili hali halisi ya mambo.Ukumbuke vile vile kwamba tears is the sign of defeat.Usikubali kushindwa Happy.Simama imara na kumpa nguvu Patrick .Simama katika maamuzi yako.” Margreth akampa dada yake maneno ya faraja.
“Margreth najitahidi sana kujipa moyo na ujasiri lakini najikuta nikishindwa.Kila nikifikiria kuhusu tukio lile najikuta nikiangusha machozi.Nasikia uchungu mkubwa moyoni.namuonea huruma Patrick na wakati huo huo sijui nifanye kitu gani..ouh Patrick..!!!!..Amebeba jukumu zito sana .Amejitwisha mzigo wangu.Ni mimi ndiye niliyestahili kuwepo mahakamaini mida hii na si yeye lakini kwa upendo wake usio na kifani amejitolea kuubeba mzigo huu nilioustahili.Sijui nitaulipaje upendo huu mkubwa alionionyesha Patrick.I’m confused !!” akasema Happy.Margreth akamtazama halafu akamshika bega
“Happy huna haja ya kuendelea kulia .Unachotakiwa kufanya kwa sasa ni kukubaliana na kilichotokea na kujipanga kuikabili hali hii na kuona namna tutakavyoweza kumsaidia Patrick ambaye amefanya kitendo ambacho mimi nakiita ni cha kijasiri sana na ameyatoa maisha yake kwa ajili yako.Jukumu lako kwa sasa ni kumpa kila aina ya ushirikiano unaohitajika na kuhakikisha kwamba anashinda kesi.Kwa hiyo Happy nakushauri uwe jasiri sana na ujasiri wako ndicho kitu pekee cha kumpa Patrick nguvu ya kuhimili kukaa gerezani.” Akasema Margreth
“Margreth, si kwamba nashindwa kuwa jasiri ,lakini kuna nyakati ninajikuta nikiwa dhaifu sana hasa kila nikikumbuka mambo yaliyotokea.Things happened so fast.Sikutegemea kama mambo yangefika hapa yalipofika.”
“Huna haja ya kujilaumu Happy.Yaliyotokea yametokea na na kuna usemi usemao kwamba kila jambo hutokea kwa sababu.Ninaamini hata suala hili limetokea kwa sababu maalum pia.Jiulize ni kwa nini jambo hili limetokea sasa? Muda ambao zilibaki siku chache Patrick afunge ndoa na Vero? Huoni kwamba hapa kuna sababu kubwa ya nyie kukutana tena na mambo yakawa hivi yalivyokuwa ?.Happy kama kweli moyo wako unampenda Patrick na kama ndiye mwanaume wa maisha yako tafadhali simama imara katika msimamo wako huo.This is for your own life and your own happiness.” Akasema Margreth
“Nimekuelewa Maggy.Naomba nikuhakikishie kwamba ninampenda Patrick na ndiye mwanaume pekee wa maisha yangu .Sintaubadili msimamo wangu,I’ll fight for him.Nitas………..” Happy akanyamaza ghafla akaelekeza macho yake nje.Gari mbili za polisi zilikuwa zinaingia pale mahakamani na nyuma yake kulikuwa na basi la kijani ambalo ni maalum kwa kubebea mahabusu na kuwaleta mahakamani.Happy alibaki ameyakodolea macho magari yale.Alikosa neno la kusema.
“Nadhani mahabusu ndio wanaletwa mahakamani” akasema Margreth.
Happy bado aliendelea kuyakodolea macho magari yale hadi yaliposimama.Mapigo ya moyo wake yalibadilika na kuanza kwenda kwa kasi kubwa na machozi yakamtoka.
“Usilie Happy.Nilifahamu kwamba utaumia sana na ndiyo maana nikakuzuia usije mahakamani siku ya leo.Twende tuondoke maeneo haya.Turudi nyumbani ukapumzike” akasema Margreth
“No Maggy,let me stay here.I need to be here .I’m supposed to be here” akasema Happy.Katika mashavu yake ilionekana michirizi ya machozi yakitiririka.Baada ya dakika kama mbili hivi akainamisha kichwa
“I’m so stupid !!!..so stupid !!!!....” akasema Happy kwa uchungu huku akikipiga piga kichwa chake.
“Calm down Happy…..!!!!” akasema Margreth
“Maggy,I’m so stupid” akasema tena Happy kwa sauti ya masikitiko
“I’m so stupid Margreth..Mtu aliyeyatoa maisha yake kwa ajili yangu yuko mahakamani lakini ninashindwa kuingia mle ndani na kumuonyesha kwamba niko pamoja naye katika kipindi hiki kigumu kwake.Nashindwa kuonyesha ushirikiano.I’m real so stupid.” Akasema Happy
“You are not stupid Happy.Nakufahamu vizuri dada yangu.You are strong woman.You’ve been and you are always so strong so don’t become weak now.Huu ni wakati unaotakiwa kuwa na ujasiri wa hali ya juu sana.” Akasema Margreth.Happy akafuta machozi akauangalia mlango wa kuingilia mahakamani akakishika kitasa cha mlango wa gari.
“Maggy,I cant be such a stupid.Happy isn’t that coward.Naingia mahakamani” akasema Happy huku akiufungua mlango wa gari tayari kwa kushuka.Margreth akamzuia.
“Hapana Happy huwezi kushuka.”
“Kwa nini Maggy? Kwa nini nisiingie mahakamani? Patrick atajisikiaje asiponiona mahakamani leo? Please Maggy let me go”
“Happy,nafahamu umuhimu na ulazima wa wewe kuwepo mahakamani lakini siku ya leo sidhani kama itakuwa vyema uingie mle ndani.Kuna watu wengi leo na hasa waandishi wa habari ambao wanategemea kukuona mahakamani ili wakupige picha na kuzipamba kurasa zao za mbele.Nakushauri siku ya leo usiingie mahakamani badala yake unatakiwa kwenda kumtembelea Patrick gerezani kila mara na hapo ndipo utakapopata nguvu na ujasiri wa kuweza kuikabili hali hii na ndipo utakapoweza hata kuhudhuria mahakamani.Endapo utaingia mle ndani utashindwa kujizuia na utaangua kilio.Utazidi kuumia”
Happy akabaki kimya kwa muda wa kama dakika tatu hivi akitafakari
“Nahisi kuchanganyikiwa Margreth.Sijui nifanye nini “ akasema Happy
“twende tuondoke hapa.Twende turudi nyumbani ukapumzike”
“Nadhani hilo ni jambo la msingi kwa sasa.Nirudishe nyumbani nikapumzishe kichwa changu” akasema Happy na Margreth akawasha gari wakaondoka kurejea nyumbani.
“Usife moyo Happy ,mambo haya yatakwisha.Tuzidi kumuomba Mungu” Margreth akampa moyo dada yake wakiwa njiani kurejea nyumbani.
“Hii ni mara ya pili sasa Patrick anaingia gerezani kwa ajili yangu.Mara ya kwanza aliua bila kukusudia wakati akiniokoa nisidhalilishwe na genge la wahuni.Safari hii ni mimi ndiye niliyesababisha kifo lakini bado ameamua kuubeba mzigo huu wote wa mauaji na sijui hatima yake itakuwa nini.Huu ni upendo wa ajabu sana ambao sijawahi kuuona katika zama hizi.Sielewi ni kwa nini Patrick ananipenda namna hii kiasi cha kufanya haya anayoyafanya .Huu ni zaidi ya upendo ambao hauelezeki kwa maneno.Huyu ndiye mwanaume wa maisha yangu Nitampenda hadi mwisho wa uhai wangu.” Akawaza Happy akiwa amejiinamia.
“Nina deni kubwa sana kwa Patrick.Nimefanya kosa kubwa kutokuoenekana mahakamani siku ya leo.Sijui atakuwa amejisikiaje kwa kutoniona mahakamani .Najua alitegemea sana kuniona na ingemfariji sana kuona kwamba tuko pamoja katika wakati huu mgumu.Sintakubali suala kama hili lijitokeze tena.Kuanzia sasa sintaogopa mtu yeyote Yule.Nitasimama imara na Patrick hadi dakika ya mwisho.” Bado Happy aliendelea kuwa na mawazo mengi sana.Safari yao ilikuwa inaendelea kimya kimya.
Hatimaye wakafika nyumbani .Mtumishi wa ndani akawafungulia geti wakaingia.Mara tu walipoingia ndani Happy akapatwa na mstuko mwingine baada ya kuliona gari moja dogo jeupe lenye namba za kibalozi likiwa limeegeshwa mle ndani.Mapigo ya moyo yakabadilika na kuanza kumwenda mbio .
“Ouh Gosh ! Its Mike.” Akasema Happy huku uso wake ukiwa umebadilika.
“Sitaki kuonana na naye kwa sasa.Nitafanya nini Margreth?
“Usiogope Happy.Huna haja ya kumkimbia Mike.Onana naye ana kwa ana.” Akasema Margreth.
“I’m not ready Margreth .I’m not ready to face him yet” ( siko tayari Margreth.Siko tayari kuonana naye ana kwa ana”
“Hakuna namna nyingine ya kufanya Happy zaidi ya kuonana na Mike.Nadhani ni wakati muafaka sasa kwa Mike kuufahamu ukweli halisi.He loves you and he deserve to know the truth”( anakupenda na ana haki ya kuufahamu ukweli”
“Not now Margreth.Siko tayari kuongea lolote na Mike kwa sasa”
“Ok Happy kama kama hauko tayari kuongea naye lolote kwa saa siwezi kukulazimisha kufanya hivyo lakini hata hivyo twende ndani ukasalimiane naye halafu uende chumbani kwako.Mimi nitaongea naye na kumuelewesha kwamba akusubiri hadi hapo utakapokuwa tayari kuzungumza naye” akasema Margreth.Happy akavuta pumzi ndefu na kuufungua mlango wa gari akashuka.
Margreth ndiye aliyekuwa wa kwanza kuingia sebuleni akifuatiwa na Happy.Pale sebuleni alikuwepo mama yao pamoja na Mike.Mara tu Margreth na Happy walipoingia Mike akasimama na sura yake ikaonyesha tabasamu kwa mbali.
“Hallo Happy” Mike akamsalimu.
“Hallo Mike” Happy akajibu huku akiwa amekiinamisha kichwa chake chini.Mike akamsogelea na kutaka kumshika mkono lakini Happy akausogeza mkono wake ili Mike asiushike.
“Unajisikiaje Happy.” Akauliza Mike
“Naendelea vizuri .” akajibu Happy
“Nafurahi kusikia hivyo.Nimekuwa na wasi wasi mwingi sana juu ya maendeleo yako Happy.Nashindw…” Mike hakumaliza alichotaka kukisema Happy akamkatisha
“Mike tutaongea siku nyingine.Nimechoka sana naomba uniruhusu nikapumzike.tafadhali sana naomba unisamehe Mike” akaomba Happy halafu akaanza kutembea kuelekea chumbani kwake.
“Happy !!!....akaita Mike.Sura yake ilionyesha huzuni kubwa.
“Mike let her go.She need some rest” akasema Margreth.
“Margreth ninaumia sana nikimuona Happy akiwa katika hali hii.Sijawahi kumuona hata mara moja Happy akiwa hivi”
“Mike !“ akaita Margreth halafu akamsogelea karibu.Mike akageuka na kumtazama
“Happy anapita katika kipindi kigumu sana hivi sasa.Ni kipindi kigumu kupita vyote alivyowahi kupitia.Anahitaji kupewa muda wa kutosha wa kutuliza akili yake.Kwa muda huu hataweza kuongea lolote.Nakushauri Mike vuta subira hadi hapo atakapokuwa tayari ametulia na mtakaa mtaongea” akasema Margreth.Mama yake aliyekuwa amesimama karibu yao akakohoa kidogo na kusema
“Mike maneno ya Margreth ni ya msingi sana.Happy anahitaji muda wa kupumzisha akili yake.Mambo mengi mazito yamemtokea katika kipindi kifupi kwa hiyo bado anahitaji kuirejesha akili yake katika hali ya kawaida.Nakuomba Mike umvumilie mwenzio hadi hapo atakapokuwa tayari”
Mike akainama chini akafikiri kwa muda kisha akasema
“Nimesafiri toka Marekani mpaka hapa kwa lengo moja tu la kuwa karibu na Happy katika wakati ambao niliamini alikuwa ananihitaji sana.Nafahamu katika wakati mgumu kama huu Happy anahitaji mtu wa karibu wa kumfariji na kumfanya awe na furaha ndani ya moyo wake.Nashangaa sana kwa Happy kutokuonyesha dalili za kunihitaji katika wakati huu wa matatizo.Inaonekana kama vile ananikwepa” Akasema Mike kwa sauti ya masikitiko.
“Mike ninafahamu kwamba unampenda sana Happy na ndiyo maana umesafiri safari hii ndefu kwa lengo la kuwa naye katika matatizo yaliyompata.Ushauri wangu kwako ni kwamba muache Happy apumzike kwa siku ya leo na kesho kama atakuwa yuko vizuri basi mtakaa na kuongea kuhusiana na kinachoendelea hivi sasa.” Akasema mama yake Happy.Mike akainamisha kichwa akafikiri kwa muda halafu akainua kichwa na kusema
“Nimekuelewa mama.Nitamuacha Happy apumzike.Nitakuja tena kesho kumtembelea na kujua maendeleo yake.Naomba endapo kutatokea mabadiliko yoyote katika hali yake basi mnitaarifu mara moja ili kwa pamoja tusaidiane namna ya kufanya” Akasema Mike kisha wakaagana akaondoka Margreth akamsindikiza
“Margreth,moyo wangu umeumia sana kwa hali ya Happy.Mpaka hapa niko gizani na sielewi chochote kuhusiana na kilichotokea na kumpelekea Happy awe katika hali hii.Margreth unaweza ukanifahamisha japo kwa muhtasari ni kitu gani kilichotokea na kumfanya Happy awe katika hali hii? Kuna huyu mtu aitwaye Patrick ambaye Happy aliwasiliana naye tukiwa kule hotelini tukipata chakula cha mchana na Happy akabadilika ghafla ni nani? Akauliza Mike
“Mike sina maelezo yoyote ambayo yanaweza kukutosheleza kwa sasa.Kama mama alivyokushauri msubiri Happy atulize akili yake na atakueleza kila kitu kilichomsibu yeye mwenyewe.”akasema Margreth.Mike akamtazama usoni kwa makini na kumuuliza tena
“Kitu gani kinaendelea hapa Margreth? Kuna jambo naona unalifahamu lakini hutaki kunieleza.Unazidi kunipa wasi wasi.Naomba kama kuna kitu unakifahamu kinachomsumbua Happy nieleze ili kwa pamoja tuweze kukitafutia ufumbuzi.”
“Mike kama nilivyokwambia kwamba sina chochote cha kukwambia.Mwenye maelezo yote na anayeweza kukueleza kwa ufasasa na kwa kina juu ya kilichompata na kinachomsumbua ni Happy mwenyewe.Kwa hiyo naomba umsubiri yeye mwenyewe hadi hapo atakapokuwa tayari” akasema Margreth.
“Nimekuelewa Margreth.Nitakuja tena kesho kumuangalia Happy” akasema Mike na kuingia garini akaondoka.

*********************

Basi la kubeba mahabusu likiwa linaongozwa na magari mawili ya polisi liliendelea kuikata mitaa ya jiji hili la Dar es salaam likielekea maeneo ya Kigamboni.Patrick alikuwa mmoja wa mahabusu kumi waliokuwamo katika basi hili,wote walikabiliwa na kesi za mauaji.Wakati wote wa safari macho yake yalikuwa nje akitazama majengo mazuri ya jiji hili pamoja na pilika mbali mbali za kila siku
“ Patrick gerezani tena “ akasema kwa sauti ndogo na kisha akainama chini
“Sikutegemea kama mambo yangekuwa namna hii.Sikutegemea kama suala hili lingenirejesha tena gerezani” akaendelea kuwaza Patrick huku gari likienda kwa kasi.
“Kuna nyakati najiuliza ni kwa nini Happy ametokea tena kwa wakati huu? Baada ya kupita kwa miaka mingi iweje ajitokeze sasa? Yote haya yaliyotokea yametokea kwa sababu ya kuonekana kwake tena.Endapo asingetokea kwa wakati huu yasingetokea haya yote” Akawaza Patrick halafu akainua kichwa akatazama nje
“Kuna kitu kimoja ambacho kinanifanya niamini kwamba kutokea kwa Happy katika wakati huu ni kwa sababu maalum.Ilipangwa iwe hivi.Japokuwa vikwazo ni vingi lakini ni ukweli usiopingika kwamba mimi na Happy tumepangiwa tuwe pamoja na kamwe hatuwezi kutenganishwa.Vero hakuwa amepaumbwa kwa ajili yangu na ndiyo maana yametokea haya yaliyotokea.Ninaamini hivyo kwa sababu ya upendo mkubwa uliopo kati yangu na Happy.Licha ya kutengana kwa miaka mingi lakini tumeonana tena na kujikuta tukiwa bado tunapendana tena kwa kiwango kikubwa sana na ndiyo maana kwa pamoja mioyo yetu ilikuwa tayari hata kuachana na wapenzi wetu wa sasa kwa lengo moja tu la kuwa pamoja tena.Lakini pamoja na hayo yote bado kuna kitu kinachotutenganisha mimi na Happy.Hata hivyo kwa vyovyote vile itakavyokuwa sintabadili msimamo wangu.Nitasimama katika maamuzi yangu.Happy ndiye mwanamke pekee ambaye ninamuhitaji katika maisha yangu.Niko tayari kwa lolote lile hata kama ni kuhatarisha maisha yangu kwa ajili yake.Sitaki kuuficha ulimwengu juu ya mapenzi yangu mazito kwa Happy.Kwa wale wanaofahamu nini maana ya mapenzi ya kweli wataungana nami na kusimama upande wangu lakini wale wasioelewa maana ya penzi la kweli watanichukia ,watanibeza na kunilaani.Nitaubeba mzigo wa lawama ,chuki na laana zote nitakazopewa kwa sababu ya upendo wangu kwa Happy ulionipelekea nikafanya maamuzi haya niliyoyafanya.” Akawaza Patrick na mara sura ya Happy ikamjia kichwani, akatabasamu
“ I love you Happy and I will always love you my angel”( Nakupenda Happy na nitakupenda daima malaika wangu) akasema kimoyomoyo.Kwa sasa gari lilikuwa linalivuka daraja kuelekea Kigamboni liliko gereza kubwa la Uwangwa gereza ambalo hutumika kuwahifadhi watu wenye kesi kubwa kubwa hasa za mauaji.Kupitia dirishani Patrick aliweza kushuhudia namna watu walivyokuwa wakiendelea na shughuli zao za kiuchumi baharini.
“Mida hii nilipaswa niwe kazini nikiendelea na shughuli zangu kama watu wengine lakini niko garini naelekea gerezani.Mipango na malengo yangu yote ya maisha vimepotea.Sijilaumu kwa kilichotokea kwa sababu naamini ilipangwa iwe hivi.Nimefanya haya yote kwa sababu ya mwanamke ninayempenda kuliko wote duniani” akawaza Patrick na kuendelea kutazama nje huku gari likiendelea na safari yake kwa kasi.
“Nasikitika sana kwa kifo cha Vero.Sikutegemea kama suala hili lingesababisha Vero apoteze uhai wake.Inauma sana lakini sikuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya kuusikia moyo wangu na kuufuata.Moyo wangu umeniambia kwamba Happy ndiye mwanamke wa maisha yangu na siku zote moyo wangu huwa haunidanganyi.Hata hivyo kifo cha Vero kimeniumiza sana.Tukio hili ni moja kati ya matukio ambayo hayatafutika katika historia ya maisha yangu hadi naingia kaburini.” Akawaza Patrick.Sura ya Vero ikamjia akainamana na kufuta machozi.
“Bado nazikumbuka zile nyakati zetu za furaha enzi za uhai wake.Tulipendana sana na sikutegemea hata kidogo kwamba mwisho wetu ungekuwa namna hii.Inaniuma sana na siku zote nitaendelea kumkumbuika .Vero ni mwanamke ambaye nimetoka naye mbali toka nikiwa gerezani Songea.Alinisaidia sana wakati ule nikiwa gerezani .Alinifanya nisiyaone magumu maisha ya gereza.Hata wakati ule nilipoamini kwamba Happy amenisaliti bado Vero alisimama nami ,akanifariji na kunifanya nitake kuishi tena.Baada ya kutoka gerezani alijitahdi kwa kila alivyoweza kuhakikisha kwamba ninayaanza upya maisha yangu.Amekuwa na mchango mkubwa sana katika kuyajenga upya maisha yangu na ninaweza kusema kwamba ni mmoja kati ya watu waliochangia sana mimi kufika hapa nilipofika.Siku zote yeye ndiye alikuwa mfariji wangu,mshauri wangu na msimamizi wangu katika kila jambo ninalolifanya.Sina shaka na upendo wake kwangu.Vero alinipenda kwa moyo wake wote na alikuwa tayari kufanya lolote na kwa wakati wowote kwa ajili yangu.Nini kimetokea hadi yakatokea haya yaliyotokea?!!!...” Patrick akainama chini kichwa chake kilijaa mawazo na macho yake yalikuwa na machozi.
“ Nilimpenda sana Vero lakini Kosa moja tu alilolifanya ni kutunga ule uongo na kunitenganisha na Happy.Alifanya hivi bila kufahamu kwamba mimi na Happy ni watu ambao hakuna awezaye kututenganisha zaidi ya Mungu pekee.Tunapendana kwa dhati ya mioyo yetu na tayari mioyo yetu imekwisha ungana.Ouh Vero …..!!!!!” Patrick alisikia maumivu ya moyo kana kwamba kuna kisu kikali kinaukata.Wakati huo gari lilikuwa linamalizia kulivuka daraja la Kigamboni.
“Kwa nini Happy hajatokea mahakamani leo? Nilitegemea kumuona akiwa miongoni mwa watu waliokuja kusikiliza kesi yangu ikitajwa.Ningefarijika sana kama ningeiona sura yake.Inawezekana hakutokea mahakamani kwa sababu kuna jambo limemsibu.Inawezekana akawa ni mgonjwa.Ninamfahamu vizuri Happy asingeweza kukosa mahakamani leo lazima kuna jambo linamsumbua .Au inawezekana akawa anakwepa macho ya watu na waandishi wa habari ambao wengi walitegemea kumuona mahakamani leo.Maskini Happy ameingia katika matatizo makubwa.Tayari alikuwa na maisha yake mazuri yaliyotulia,alikuwa na machumba wake anayempenda, alikuwa na ndoto nyingi za maisha yake lakini baada tu ya kukutana na mimi ndoto zake zote zimepotea.Nasikitika sana kwa jambo hili.Hana muda mrefu toka amelitwaa taji la Miss Tanzania lakini katika kipindi hiki kifupi tayari amekwisha tengeneza vichwa vya habari kwa kuhusika kwake na tukio la kifo cha Vero.Sifa yake kama mrembo wa Taifa imepotea na kwa mara nyingine historia imejirudia kwa warembo wanaovishwa taji hili la kuingia katika kashfa .Simlaumu Happy kwa alichokifanya .Alikuwa akilipigania penzi lake la kweli .Alimsukuma Vero kwa lengo la kuniokoa mimi kwani ni wazi Vero alikuwa na kila dalili za kufanya tukio baya” Bado Patrick aliendelea kuwaza mambo mengi kuhusiana na tukio lile lililopelekea kifo cha Vero na yeye kukabiliwa na kesi ile ya kusababisha kifo.Kwa sasa gari lile la mahabusu lilikwisha ishika njia ya kuelekea gerezani.
“Japokuwa kuna watu ambao hawakubaliani moja kwa moja na maamuzi yangu ya kumtoa Happy katika kesi hii ambayo ilikuwa imkabili yeye na mzigo wote kuubeba mimi,bado sijutii kufanya hivyo hata kidogo kwa sababu hata siku moja sintakubali mwanamke nimpendaye aingie gerezani.Niko tayari kwa adhabu ya aina yoyote ile lakini si kumuona Happy akiteseka gerezani.Nitaipokea adhabu hiyo kwa mikono miwili kwa sababu nitakuwa nimeibeba adhabu ambayo alistahili kuibeba mwanamke ninayempenda kuliko wanawake wote duniani.”
Gari lilipunguza mwendo na kusimama.Akachungulia nje walikuwa wamesimama katika geti la kwanza la kuingilia hapo gerezani.
“Nakumbuka Savanna hakukubaliana nami kabisa katika uamuzi wangu huu wa kumtoa Happy katika kesi hii na jukumu lote kulibeba mimi.Nalikumbuka swali aliloniuliza kama je Happy naye yuko tayari kuyatoa maisha yake kwa ajili yangu kama mimi nilivyofanya kwake? Patrick akanyanyua kichwa akatazama nje.Gari liliruhusiwa kupita na kuendelea na safari ya kuelekea gerezani.
“Swali kama Happy yuko tayari kufanya kama nilivyofanya mimi ni swali gumu sana kulipatia jawabu lakini sina shaka na Happy.Japokuwa siwezi kuusemea moyo wake lakini nina uhakika kwamba anaweza akafanya lolote kwa ajili yangu kama alivyokubali kuuvunja uhusiano wake na mchumba wake kwa lengo moja tu la kuwa nami.Ninaamini ananipenda kwa dhati ya moyo wake .Patrick akawaza,akainua kichwa akatazama juu halafu akaninama tena chini.
“Sijui hali ya baba ikoje huko hospitali.Nimewaumiza watu wengi kwa maamuzi yangu.Kwanza ni familia yangu.Baba hali yake si nzuri hata kidogo.Ndugu zangu,marafiki wameumizwa sana na kitendo hiki cha kuuvunja uchumba wangu na Vero.Familia ya vero nayo imeumizwa sana kwanza kwa kuuvunja uchumba na mtoto wao na pili kwa kusababisha kifo cha binti yao.Ninaamini kamwe hawataweza kunisamehe kwa jambo hili.Familia ya Happy pia imeumizwa sana na jambo hili.Mtoto wao ameingia katika kashfa nzito ya kusababisha mauaji wakati wa ugomvi wa kimapenzi.Jina lake limechafuka.Hawakutegemea hata siku moja mtoto wao waliyemlea katika maadili aingie katika kashfa kubwa kama hii.Yote haya yamesababishwa na mimi.Mchumba wa Happy aitwaye Mike sifahamu atakuwa katika hali gani akiufahamu ukweli kwani sina hakika kama tayari Happy amekwisha muweka wazi kwamba uhusiano kati yao umefika mwisho.kwa ujumla nimeumiza watu wengi sana.Rafiki zangu walijitolea michango mingi mikubwa ili kuhakikisha kwamba harusi yangu inakuwa ya kihistoria .Wote hawa wameumizwa kwa kiwango cha juu kabisa na nina hakika itawachukua muda mrefu sana kunisamehe lakini pamoja na hayo sikuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya kuchukua maamuzi haya magumu niliyoyachukua kwa ajili ya kuipigania furaha ya maisha yangu.Siku zote yanapofanyika maamuzi magumu lazima wawepo watu watakaoathirika na maamuzi hayo na ndiyo maana yakaitwa ni maamuzi magumu.Natakiwa nisimame katika maamuzi yangu na nionyeshe msimamo japokuwa si kazi rahisi hata kidogo na inahitaji ujasiri mkubwa sana lakini hata hivyo lazima nifanye hivyo.Haya ni maisha yangu na ninachokipigania hapa ni furaha ya maisha yangu.Pumzika kwa amani Vero.Nitakukumbuka siku zote za maisha yangu na nina hakika huko uliko utanisamehe” Akawaza Patrick na kuyafuta machozi. Tayari gari lilikwisha fika gerezani.Mlango ukafunguliwa na mahabusu wote wakashushwa garini na kuingizwa gerezani
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 30
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Siku zote yanapofanyika maamuzi magumu lazima wawepo watu watakaoathirika na maamuzi hayo na ndiyo maana yakaitwa ni maamuzi magumu.Natakiwa nisimame katika maamuzi yangu na nionyeshe msimamo japokuwa si kazi rahisi hata kidogo na inahitaji ujasiri mkubwa sana lakini hata hivyo lazima nifanye hivyo.Haya ni maisha yangu na ninachokipigania hapa ni furaha ya maisha yangu.Pumzika kwa amani Vero.Nitakukumbuka siku zote za maisha yangu na nina hakika huko uliko utanisamehe” Akawaza Patrick na kuyafuta machozi. Tayari gari lilikwisha fika gerezani.Mlango ukafunguliwa na mahabusu wote wakashushwa garini na kuingizwa gerezani

ENDELEA………..

Akionekana ni mwenye haraka Savanna akawaaga mawakili wenzake ambao kwa pamoja wanamtetea Patrick kisha akaingia katika gari lake ,akaliweka lundo la vitabu na nyaraka katika kiti cha pembeni akaufunga mkanda akawasha gari na kuondoka maeneo ya mahakamani.
“Nitaisimamia kesi hii hadi nihakikishe Patrick anashinda.Ni kesi ambayo haiwezi kunisumbua hata kidogo.Nitafanya kila niwezalo kuhakikisha kwamba Patrick hafungwi.Patrick ni mtu wa muhimu sana kwangu .Nakumbuka wakati tukiwa bado na mahusiano ya kimapenzi alinipa penzi la kiwango cha juu mno na kumfanya awe ni mwanaume wa pekee kabisa kwangu.Anajua kupenda ,anajali,na anafahamu mwanamke anahitaji nini toka kwa mwanaume.Nathubutu kusema kwamba sijaona wa mfano wake.Japokuwa tulisitisha mahusiano yetu baada ya mimi kumpata George lakini mpaka leo hii sijaweza kumsahau hata kidogo.Kuna nyakati nikiwa nafanya mapenzi na George ninahisi kama ninaiona sura ya Patrick na mara kadhaa nimewahi kujisahau na kulitamka jina la Patrick kutokana na kuhisi uwepo wake karibu yangu.Wakati mwingine ili nipate hisia za kimapenzi lazima niivute taswira ya Patrick ndipo ninasisimka.Bado nampenda na sijafanikiwa kumtoa moyoni mwangu.Huu ni wakati wangu wa kumrudisha Patrick kwangu na kitu kikubwa kitakachonifanya nimrejeshe kwangu ni namna nitakavyomjali na kumpigania katika wakati huu mgumu .Anahitaji mtu wa kuwa naye karibu katika kipindi hiki na mtu huyo lazima niwe mimi.Nitakuwa naye karibu nitamfariji,na mwishowe atakuwa wangu tena.” Akawaza Savanna akiwa garini.
“Kwa nini Happy hajatokea mahakamani leo? Sina hakika kama anampenda Patrick kiasi cha kuweza kuyatoa maisha yake kama Patrick alivyofanya..Nikitoka hospitali nitakwenda kujua nini kimemsibu na kwa nini hakufika mahakamani siku ya leo.Nimeanza kuwa na wasi wasi sana na huyu Happy na nina imani baada ya muda si mrefu Patrick atakijutia kitendo chake cha kuubeba mzigo alioustahili Happy ambaye ameshindwa hata kufika mahakamani kuonyesha kwamba anajali.” Akawaza Savanna
Ilimchukua Savanna takribani saa moja kufika katika hospitali kuu ya magonjwa ya moyo alikolazwa baba yake Patrick.Akashuka garini na kutembea kwa kasi kuelekea katika vyumba vya wagonjwa walio katika uangalizi maalum.Kwa mbali akamuona Alois kaka yake Patrick akiwa nje akamsogelea.Alois alipomuona Savanna akakatisha maongezi na mtu aliyekuwa akiongea naye simuni.
“Hallo mheshimiwa “ Alois akamsalimu Savanna.Huku akitabasamu Savanna akasema
“Ouh Alois niite Savanna inatosha sana.”akasema Savanna
“Karibu sana Savanna.”
“Ahsante Alois” akajibu Savanna halafu kikapita kimya kifupi
“Alois tulionana kule mahakamani lakini hatukupata wasaa wa kuzungumza lolote .Pilika pilika zilikuwa nyingi sana.” Akasema savanna.
“Usijali Savanna,hata mimi niliona namna ulivyokuwa na shughuli nyingi.Ninafahamu ugumu uliopo katika kusimamia kesi kubwa kama hizi na ndiyo maana sikutaka kukusumbua.Hata hivyo Savanna naomba nikushukuru sana kwa kuamua kulibeba jukumu hili la kumtetea Patrick katika kesi hii ngumu” akasema Alois
“Ahsante Alois.Kesi inayomkabili Patrick ni kesi ngumu sana ,ni kesi ya mauaji lakini nitajitahidi kufanya kila niwezalo kuhakikisha kwamba Patrick anashinda kesi hii”
“Savanna,sisi kama familia tuko pamoja nawe na tuko tayari kulipa gharama zozote zile zinazohitajika katika kesi hii.”
“Patrick ni mtu wangu wa karibu sana na nimeamua kuifanya kazi hii bila malipo yoyote yale.Kitu pekee nitakachokihitaji toka kwenu kama familia ni kumpa Patrick ushirikiano mkubwa katika wakati huu.Mambo yote yaliyotokea na kusababisha tofauti katika familia naomba muyaweke pembeni kwa wakati huu.Kwa pamoja tutashinda jambo hili” akasema Savanna
“Usihofu kuhusu hilo Savanna.Patrick ni ndugu yetu na pamoja na yote aliyoyafanya lakini hatutaweza kumuacha.Tutatoa kila aina ya ushirikiano unaohitajika .Vipi kuhusu Yule binti Happy,mbona sijamuona mahakamani leo? Akauliza Alois
“Hata mimi sifahamu ni kwa nini hajatokea mahakamani leo”
“Savanna,sielewi ni kwa nini kila mara Patrick anapokuwa na huyu Happy lazima jambo baya limfike.Mara ya kwanza aliwahi kufungwa gerezani kwa kosa la kuua bila kukusudia akiwa na huyu huyu Happy.Safari hii amefanya tena kosa lile lile la mauaji akiwa na huyu huyu Happy.Ninahisi msichana huyu ana mkosi na ndiyo maana kila mara lazima mambo mabaya yamfike Patrick.Kitu kingine,sielewi ni kwa nini ameibuka katika wakati huu ambao tayari maisha ya Patrick yametulia na alikuwa anakaribia kufunga ndoa na Vero.Kuibuka kwake kumeharibu kila kitu ikiwamo na maisha ya Patrick.Vero amefariki na Patrick anakabiliwa na mashtaka ya mauaji..Ninamchukia sana Happy na sitaki hata kuonana naye uso kwa uso kwani ninaweza kughafirika na kufanya jambo baya linaloweza kuniletea matatizo.Naomba Mungu aniepushe kabisa nisikutane na Yule mwanamke uso kwa uso na hasa katika siku hizi za karibuni.” Akasema Alois kwa hasira.
“Alois,mambo haya yamekwisha tokea na hatupaswi kulaumiana kwa sasa.Tunachotakiwa kukifanya ni kukabiliana na hali halisi iliyojitokeza.Si Patrick wala Happy aliyetegemea wala kupanga kwamba kingetokea kifo cha Vero.Hakuna aliyejua kama mambo haya yangefika hapa yalipofika.”
“Nakubaliana nawe Savanna lakini moyo wangu unauma sana kwa jinsi huyu Happy alivyomuweka ndugu yangu katika matatizo makubwa.Sina hakika kama nitaweza kumsamehe .Si mimi tu bali hata familia yote kwa ujumla.Yeye ndiye chanzo cha haya yote.Ametusababishia jeraha kubwa ambalo litachukua muda sana kupona” akasema Alois
“Alois huna haja ya kumchukia Happy.Kama nilivyokueleza kwamba si Patrick wala Happy aliyetegemea kama jambo kama hili litatokea na kufika hapa yalipofika.Tuachane na hayo,nimekuja kujua hali ya mzee anaendeleaje?
“Hali ya mzee si nzuri hata kidogo.Baada tu ya kutoka mahakamani tulitaarifiwa kwamba hali yake ilikuwa inazidi kuwa mbaya.Muda mfupi uliopita amehamishiwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.Kwa ufupi hali yake bado si nzuri hata kidogo.Hapa tunasubiri madaktari watueleze nini kinaendelea.Tunafikiria hata kufanya mpango wa kumpeleka nje ya nchi lakini endapo italazimika kufanya hivyo.Mama na ndugu wengine wako kule ndani mimi nimechomoka mara moja kwa ajili ya kuja kupiga simu.” Akasema Alois
“Dah ! Poleni sana Alois.” Akasema Savanna halafu kikapita kimya kifupi Savanna akasema
“Alois kwa kuwa kinachosubiriwa kwa sasa ni taarifa ya madaktari kuhusiana na maendeleo ya mzee,mimi naona niondoke nikaendelee na shughuli nyingine.Utanifahamisha kuhusu maendeleo yake” Akasema Savanna na kubadilisha namba za simu na alois.
“Usihofu Savanna,lolote litakalotokea nitakutaarifu mara moja” akasema Alois kisha wakaagana na Savanna akaondoka.
“Kwa namna nilivyoiona sura ya Alois ,inaonyesha hali ya baba yake katu si nzuri.Mungu amsaidie mzee Yule apone haraka kwa sababu endapo ikatokea akafariki dunia mambo yatazidi kuwa mabaya sana kwa Patrick.” Akawaza Savanna wakati akiligeuza gari lake na kuondoka maeneo ya hospitali.
“Kwa sasa ngoja nikaonane na Happy nifahamu nini sababu iliyomfanya ashindwe kufika mahakamani siku ya leo.Nilikuwa namtazama Alois machoni wakati akiongea kuhusiana na namna anavyomchukia Happy,hakuwa akitania hata kidogo.Ni wazi anamchukia mno Happy toka moyoni.Suala hili linazidi kuchukua sura mpya kila uchao.Kwa hivi sasa mambo haya yatahamia katika famila.Chuki kubwa itajengeka baina ya familia hizi .Familia ya Happy katu haitaweza kutazamana na familia ya Patrick na ile ya Vero katu hawatakuja kuelewana na ile ya Patrick.Dah.!!....” akawaza Savanna na mara simu yake ikaita.Akatazama mpigaji alikuwa ni George
“I’m sorry George,siwezi kupokea simu yako kwa sasa.” Akasema Savanna na kuirusha simu pembeni.Simu ikaendelea kuita lakini hakusumbuka hata kuitazama tena.
“George aliniudhi sana kiasi kwamba sihitaji hata kuiona sura yake tena .Kwa sasa akili yangu yote nimeielekeza katika kitu kimoja tu.Kumsaidia Patrick ashinde kesi.Pamoja na kushinda kesi hii lakini nina kazi nyingine ngumu ya kumrudisha Patrick katika himaya yangu tena.Yeye ni mwanaume pekee ambaye aliwahi kunifikisha mawinguni kwa raha alizokuwa akinipa.Naapa pamoja na ugumu wote uliopo nitamrejesha kwangu.Najua moyo wake umekufa ukaoza kwa Happy lakini hii hainipi shida hata kidogo.Nitafanya kila niwezalo kumrejesha kwangu tena” akawaza Savanna

* * *

Mlio wa kengere ya getini ulimfanya Margreth ainuke sofani na kwenda kuangalia mtu aliyekuwa akigonga.Hakuamini alipokutana na msichana mmoja mrembo na wakili maarufu,Savanna
“Dada Savanna !!..shikamoo” akasema Margreth
“Marahaba Margreth.Habari yako?
“Habari yangu nzuri dada ” Akasema Margreth huku akilifungua geti na Savanna akaingiza gari ndani
“Karibu sana dada Savanna,karibu ndani” akasema Margreth akimuongoza Savanna kuelekea ndani
“Pole na matatizo dada ” akasema Margreth huku akimuwekea Savanna kinywaji mezani
“Nimekwisha poa Margreth.Poleni nanyi pia.Matatizo haya ni yetu sote.”
“Ahsante dada Savanna.” Akajibu Margreth halafu kikapita kimya kifupi.Savanna akasema
“Happy anaendeleaje? Sijamuona leo mahakamani.Patrick alipatwa na wasi wasi sana na akaniomba nifike nijue kilichomsibu” akasema Savanna
“Dada Savanna hali ya Happy si nzuri hata kidogo na ndiyo maana hata leo alishindwa kuingia mahakamani japokuwa alikuwepo pale mahakamani.Nadhani itakuwa vyema kama nitakupeleka chumbani kwake ukaongee naye wewe mwenyewe.” Akasema Margreth na kumuongoza Savanna kuelekea chumbani kwa Happy
“Karibu sana Savanna” akasema Happy akiwa amekaa kitandani.Macho yake yalikuwa mekundu na yamevimba kwa kulia.Nywele zake ndefu na nzuri zilikuwa zimetawanyika.Kwa ujumla alitia huruma sana mnyange huyu wa Taifa.
“Pole sana Happy” akasema Savanna
“Nimekwisha poa Savanna”
“Happy mimi si mkaaji sana,nimepita mara moja kujua hali yako baada ya kutokuona mahakani leo .Patrick alipatwa na wasi wasi mwingi na akanituma nifike nijue hali yako na kama kuna jambo limekusibu” akasema Savanna
“Savanna nilifika mahakamani leo lakini nilishindwa kuingia ndani ya mahakama” akasema Happy
“Kwa nini Happy? Akauliza Savanna
“Niliogopa kukutana na macho ya watu pamoja na waandishi wa habari.Niliogopa vile vile kukutana na ndugu za Patrick ambao sijui wangenitazamaje kwani moja kwa moja wanafahamu kwamba mimi ndiye chanzo cha matatizo yote yanayomkuta mtoto wao.Najua Patrick atakuwa na mawazo mengi sana kwa kutoniona mahakamani leo .I’m so stupid Savanna….I’m so stupid “ akasema Happy kwa masikitiko.Savanna akamtazama kwa makini na kusema
“Sikiliza Happy,huu si wakati wa kujilaumu kwa kilichotokea.Si wewe wala Patrick aliyetegemea mambo haya kufika hapa yalipofika.Yaliyotokea yameshatokea na hatupaswi kushughulika nayo ila tunachopaswa kushughulika nacho kwa sasa ni athari zilizotokana na kilichotokea.Patrick kwa upande wake tayari amekubaliana na kilichotokea na ndiyo maana ameamua kulibeba jukumu zima ambalo ulistahili ulibebe wewe,kwa hiyo basi nakushauri na wewe usimame imara na usimamie kile kilichowapelekea mkafika hapa mlipofika kwa ujasiri mkubwa.Ikabili jamii na usiogope kitu chochote kile.Usiogope kwamba utaonekanaje kwa kuivaa kofia hii ya Miss Tanzania.Kofia hii ni ya kupita tu kwa maana hiyo usiogope kupigwa picha ukiwa mahakamani ukisikiliza kesi ya Patrick.Kuanzia sasa futa machozi na usimame imara.Kumbuka utakuwa ni mmoja wa watu watakaosimama mahakamani kutoa ushahidi wao kwa hiyo jitahidi kuanzia sasa uwe jasiri”
Maneno yale ya Savanna yalimuingia Happy vilivyo.Akainama akatafakari
“Tumeelewana Happy ? akauliza Savanna
“Savanna nakushukuru sana kwanza kwa kuja kunitembelea.Ujio wako na maneno yako machache yenye nguvu vimenifanya nipate nguvu mpya.Nakuahidi sintalia tena.Nitasimama imara kumtetea Patrick.Siku zote nitakuwa karibu yake na kumpa moyo kwa sababu ameubeba mzigo mzito ulionistahili mimi.Nimefanya kosa kubwa sana kutokuingia mahamani leo .Savanna naomba uniombee msamaha kwa Patrick kwa kitendo hiki.Nilikuwa dhaifu sana kukabiliana na hali halisi” akasema Happy huku kwa mbali machozi yakimlenga.
“Usijali Happy,nitamuelewesha Patrick na atakuelewa ,ila kumbuka kuyafanyia kazi hayo niliyokwambia..Patrick needs you now more than ever.Anahitaji ushirikiano wetu sote kwa wakati huu .Kila mmoja kwa upande wake anatakiwa aonyeshe ushir…………………….” Savanna akanyamaza ghafla kutokana na mlio wa simu yake.Akaitoa na kutazama mpigaji alikuwa ni Alois kaka yake Patrick.Savanna akamtazama Happy usoni huku simu yake ikiendelea kuita.
“It’s Alois “ akasema Savanna kwa sauti ndogo
“Pokea usikie anataka kukueleza kitu gani.” Akasema Happy.Savanna akavuta pumzi ndefu halafu akabonyeza kitufe cha kupokelea simu.
“Hallo Alois “ akasema Savanna baada ya kupokea simu.Baada ya sekunde kadhaa taratibu Savanna akajikuta akishusha mkono wenye simu chini.Sura yake ilikuwa imebadilika ghafla.
“Ouh My God !! “ akasema Savanna na kuzidi kumuogopesha Happy
“Savanna kuna tatizo gani? Akauliza Happy ambaye alistushwa sana na mabadiliko yale ya ghafla ya Savanna aliyekuwa amesimama huku mkono wake wa kulia ukiwa kifuani .
“Savanna kuna tatizo gani? Mbona umebadilika ghafla.Kuna taarifa gani toka kwa Alois? Is Patrick ok? Akauliza Happy.
“Baba yake Patrick amefariki” akasema Savanna.Happy akaishiwa nguvu akajikuta akikaa kitandani.
“Ouh Mungu wangu ,mambo haya yanazidi kuwa makubwa kila siku” akasema Happy kwa wasi wasi
Savanna akiwa bado chumbani kwa Happy simu yake ikaita tena.Safari hii alikuwa ni Andrew.
“Hallo Andrew..!!” akasema Savanna baada ya kupokea simu
“Savanna kuna taarifa mbaya imenifikia sasa hivi.baba yake Patrick amefariki dunia.” Akasema Andrew.
“Hata mimi nimezipata taarifa hizo muda si mrefu .Alois amenipigia kunitaarifu kuhusu msiba huo.kwa sasa uko wapi?
“Niko ofisini kwangu lakini baada ya kupata taarifa hizi ninaelekea hospitali kupata uhakika zaidi na kujua nini kinachoendelea”
“Sawa Andrew hata mimi nakuja huko hospitali” akasema Savanna na kukata simu halafu akamfuata Happy pale kitandani.
“Happy naomba tafadhali usihuzunike sana wala kupata mstuko kwa jambo hili.Tulia na muombe Mungu akupe nguvu ya kuweza kuhimili mambo haya na yote yatakayokuja kwani hatujui nini kitatokea huko mbeleni.Hiki ni kipindi kigumu sana kwako ,kwa Patrick na kwetu sote.Endapo utakuwa na tatizo lolote lile nipigie simu haraka sana nitakusaidia.Kwa sasa ngoja nielekee hospitali ili kujua kinachoendelea huko.Akasema Savanna.
“Ahsante sana Savanna.Nashukuru kwa kuja kunitembelea na kunipa moyo.Nitazidi kumuomba Mungu anipe nguvu na kwa pamoja tuweze kukipita kipindi hiki kigumu sana.Kuhusu kifo hiki cha baba yake Patrick nimeshindwa nifanye nini,siwezi kulia wala kufanya lolote.Yote namuachia Mungu” akasema Happy kwa majonzi
“Usilie tena Happy.Kuwa jasiri .Mkabidhi Mungu matatizo yako yote naye atakushindia” akasema Savanna
“Savanna siwezi kukusindikiza.Miguu yangu haina nguvu hata ya kuinuka “Akasema Happy ,akaagana na Savanna akatoka mle chumbani akaelekea sebuleni ambako alimkuta Margreth
“Margreth ,tafadhali naomba uwe karibu sana na Happy ,anapitia kipindi kigumu sana hivi sasa na anahitaji uangalizi wa karibu mno.Tumepata taarifa mpya muda si mrefu baba yake Patrick amefariki dunia kwa shinikizo la damu.Taarifa hii imemstua sana Happy kwa hiyo naomba uwe karibu naye sana kumpa moyo.” Akasema Savanna.Margreth naye alistushwa sana na taarifa ile ya kifo cha baba yake Patrick.Baada ya maongezi mafupi na Margreth,Savanna akaondoka kuelekea hospitali.
“mambo yanazidi kuwa mambo.Suala hili limewaumiza watu wengi hadi hivi sasa.Sifahamu hatima yake ni nini kwani nina hakika chuki inazidi kuongezeka miongoni mwa familia hizi hasa baada ya kifo cha baba yake Patrick leo.Familia ya Patrick itaongeza chuki dhidi ya Happy kwa madai kwamba yeye ndiye chanzo cha haya yote yaliyotokea..Namuonea huruma sana Happy,yuko katika wakati mgumu mno.Patrick naye sijui atazipokeaje taarifa hizi za kifo cha baba yake.Najua ataumia mno” Akawaza Savanna akiwa njiani kuelekea hospitali kuu ya magonjwa ya moyo ili kukutana na ndugu za Patrick
“Bado sijapata taarifa zozote kuhusiana na msiba wa Veronika.Najua Patrick angependa afahamu kinachoendelea kule.Kuna wakati hata mimi najikuta nikiogopa kila nikifikiria jinsi Patrick, Happy pamoja na familia zao walivyo katika wakati mgumu.” Akawaza Savanna
 
Write your reply...daaaahh ngoja kwanza nijicheke" Aisee imekuwaje nimetoweka Jf" kiasi kwamba najikuta napitwa nahaya mahanjumati "...
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 31
MTUNZI😛ATRICK .CK
CONTACK:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“mambo yanazidi kuwa mambo.Suala hili limewaumiza watu wengi hadi hivi sasa.Sifahamu hatima yake ni nini kwani nina hakika chuki inazidi kuongezeka miongoni mwa familia hizi hasa baada ya kifo cha baba yake Patrick leo.Familia ya Patrick itaongeza chuki dhidi ya Happy kwa madai kwamba yeye ndiye chanzo cha haya yote yaliyotokea..Namuonea huruma sana Happy,yuko katika wakati mgumu mno.Patrick naye sijui atazipokeaje taarifa hizi za kifo cha baba yake.Najua ataumia mno” Akawaza Savanna akiwa njiani kuelekea hospitali kuu ya magonjwa ya moyo ili kukutana na ndugu za Patrick
“Bado sijapata taarifa zozote kuhusiana na msiba wa Veronika.Najua Patrick angependa afahamu kinachoendelea kule.Kuna wakati hata mimi najikuta nikiogopa kila nikifikiria jinsi Patrick, Happy pamoja na familia zao walivyo katika wakati mgumu.” Akawaza Savanna

ENDELEA……….

“Nilimuonya Patrick mapema sana kuhusiana na athari za jambo hili lakini alinipuuza na akaendelea na harakati zake za kuurejesha uhusiano wake na Happy.Nilifahamu mambo kama haya yangeweza kujitokeza kwa sababu uhusiano wake na Vero tayari ulikwisha kuwa mkubwa na kuota mizizi.Patrick hakutaka kunisikiliza.Laiti angenisikia mambo haya yote yasingetokea” akasema Andrew kwa masikitiko akiwa amesimama na Savanna pale katika hospitali kuu ya moyo.Vilio vya akina mama vilitawala eneo hili.Ilikuwa ni hali ya simanzi kubwa.
“Andrew huu si wakati wa kulaumiana kwa kilichotokea.Hakuna kati yao aliyefahamu kama mambo haya yangefika hapa yalipofika.” Akasema savanna
“ Savanna sikufichi mimi ni mmoja wa watu walioumizwa sana na kitendo hiki alichokifanya Patrick cha kuachana na Vero.Siwezi kuelezea nimeumia kiasi gani lakini naomba ufahamu kwamba nimeumizwa mno.Patrick ni rafiki yangu mkubwa sana lakini kwa hili alilolifanya nitazidi kumlaumu kila siku na pengine baada ya mambo haya kumalizika itanilazimu kuangalia upya kama nitaweza tena kuendelea na urafiki naye.Amekuwa ni mtu asiyetaka ushauri wa mtu yeyote yule .Nilimshauri sana na kumuonya kuhusiana na Yule mwanamke Happy lakini hakunisikia.Yote haya yamesababishwa na Happy. Kama asingejitokeza kwa wakati huu tusingekuwa katika matatizo haya tuliyomo sasa hivi.Namchukia sana Happy.Ninamchukia sana..!!!” akasema Andrew.
“Andrew,sote tumeumizwa na kitendo cha Patrick kuachana na Vero lakini hatupaswi kuelekeza lawama zote kwa Patrick au kwa Happy.Sote tunafanya makosa hapa duniani na sioni sababu ya kila mmoja kuelekeza chuki zake kwa Happy.Kila mtu ninayekutana naye anasema anamchukia Happy nani atakayesimama na kumtetea ? Nani yuko tayari kumsikiliza? Tusiwe wepesi wa kuhukumu namna hii.Hata yeye hakujua kama mambo haya yangetokea.Nawaombeni msimchukie Happy” Akasema Savanna halafu kikapita kimya kifupi
“Vipi una taarifa zozote kuhusiana na msiba wa Vero?
“Nilipanga niende leo ili kujua taratibu za mazishi zikoje.Nilitegemea pengine kungekuwa na ujumbe wa watu toka kwa familia ya akina Patrick kwenda kuwakilisha katika mazishi na kupeleka salamu za pole lakini kutokana na jambo lililojitokeza la kifo cha mzee sidhani kama hilo litawezekana tena.” Akasema Andrew
“Andrew kuna ulazima wa kutuma wajumbe kwenda kwa akina Vero kwani tayari familia hizi zilikwisha unganishwa na upendo uliokuwepo baina ya watoto wao.Hivi sasa kumetokea aina fulani ya chuki iliyoanza kujengeka miongoni mwa familia hizi mbili.Tusiache hilo litokee Andrew.We have to do something” akasema Savanna
“Tutafanya nini Savanna? Mambo haya ni ya kifamilia na hatupaswi kuingilia ugomvi wa familia hizi mbili.”
“Andrew,Patrick ni mtu wetu wa karibu kwa maana hiyo hatupaswi kuwa waoga ,tunachotakiwa kufanya ni kuishawishi familia yake wakubali kutuma ujumbe kwa akina Happy ili kwenda kuwaunga mkono na kupeleka salamu za pole,hii itasaidia sana katika kupunguza chuki na uhasama vilivyoanza kujengeka kutokana na tukio hili .Alois yuko wapi? Akauliza Savanna.Andrew akayaelekeza macho yake katika kundi la akina mama waliokuwa wakilia huku madaktari na wauguzi wakiendelea na jitihada za kuwanyamazisha kwani eneo lile halikuhitaji kelele.
“Inasikitisha sana “ akasema Savanna
“Inauma Savanna.Bado nitaendelea kumlaumu sana Patrick kwani yeye ndiye chanzo cha haya yote.Amesababisha maumivu kwa watu wengi.” Akasema Andrew.Magari matatu yakasogezwa karibu na akina mama wale waliokuwa wakilia,wakaombwa waingie katika magari yale na kuondolewa pale hospitali.Alois ambaye alikuwapo karibu na magari yale aliwaona Andrew na Savanna akawafuata
“Pole sana Alois “ wakasema kwa pamoja
“Ahsanteni sana.Ni kazi ya Mungu ambayo hakuna mwanadamu anayeweza kuipinga.Tunapaswa kushukuru kwa kila jambo kwani yeye ndiye mwenye kutoa na kutwaa” akasema Alois
“kwa kweli hali ya mzee haikuwa nzuri hata kidogo .Tulikuwa na mpango wa kumpeleka nje ya nchi kwa matibabu zaidi lakini madaktari walinihakikishia kwamba hali ya mzee haikuwa na tumaini la kupona kwani hata kama angepelekwa nje ya nchi uwezekano wa kupona ulikuwa mdogo sana.” Akasema Alois
“Poleni sana Alois.Inauma sana jamani.” Akasema Savanna kwa huzuni.Kikapita kimya cha muda mfupi
“Kwa hiyo nini kinaendelea hapa kwa sasa? Akauliza Andrew
“Kwa sasa kinachoendelea ni maandalizi ya shughuli za msiba pale nyumbani kwa mzee.Tunasubiri baada ya ndugu kukusanyika wote tutakaa na kupanga taratibu zote za mazishi .Mpaka sasa bado tunaendelea kusambaza taarifa hizi kwa ndugu jamaa na marafiki walioko hapa jijini na walio nje ya Dar es salaam.” Akasema Alois
“Alois kuna jambo nilitaka kulifahamu .Vipi kuhusiana na msiba wa Vero kuna taarifa zozote mmezipata? Kuna mtu yeyote ambaye ataiwakilisha familia yenu kule? Akauliza Savanna
“Kusema kweli bado sina taarifa zozote kuhusiana na kinachoendelea katika msiba wa Vero na wala bado hatujatuma mtu yeyote kwenda kutuwakilisha kule.Toka lilipotokea tukio hili kumekuwa na mvurugano mkubwa sana.Ahsante sana kwa kunikumbusha kuhusu jambo hili Savanna kwani japokuwa hata sisi tumefiwa na mzee lakini kuna ulazima mkubwa wa kutuma uwakilishi katika msiba wa Vero kwani halitakuwa jambo la busara endapo hatutatuma mtu yeyote kwenda kutuwakilisha.” Akasema Alois

*****************************

Saa moja za jioni dege la shirika la ndege la British airways likatua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam.Tayari kiza kimekwisha lifunika anga la jiji hili kuu la kiuchumi nchini Tanzania.
Dege lilisimama,mlango ukafunguliwa na abiria wakaanza kushuka .Miongoni mwa abiria walioshuka ndegeni alikuwa ni mwanamke mmoja aliyekuwa amevaa suti nyeusi.Macho yake yalikuwa mekundu na yamevimba.Alikuwa ameongozana na mwanaume mmoja wa kizungu na watoto wawili.Huyu alikuwa ni Loniki dada yake Vero aliyekuwa akiishi na kufanya kazi nchini Uingereza.Alikuwa amekuja nyumbani Tanzania kuhudhuria msiba wa mdogo wake akiwa ameongozana na mumewe na watoto wao wawili mapacha Patricia na Paula.
Loniki alionekana dhaifu na alikuwa anatembea taratibu.Pale uwanjani walipokelewa na ndugu waliokuwa wakiwasubiri na kuanza safari ya moja kwa moja kuelekea msibani.Hakukuwa na maongezi mengi katika gari watu wote walikuwa katika hali ya majonzi makubwa.
Hatimaye waliwasili nyumbani na vilio vikaamka upya.Loniki akapoteza fahamu kabla hata hajashuka garini.Akabebwa na kupelekwa sehemu yenye uwazi na kuanza kupatiwa msaada .Alipozinduka akapelekwa katika chumba alichokuwamo mama yake pamoja na akina mama kadhaa ambao walikuwa wakimsaidia.Alimkumbatia mama yake na wote wakaanza kulia kwa nguvu.Ilikuwa ni hali ya simanzi kubwa.
“Loniki mdogo wako amekwenda kama upepo.Bado siamini kama ni kweli Vero amekufa.Siamini kama mwanangu amefariki dunia.” Akasema mama yake Loniki huku akilia
“Mama inauma sana.Ni siku chache tu nimeagana naye akirejea Tanzania baada ya kufanya manunuzi ya vitu alivyohitaji kwa harusi yake.Sikujua kumbe ndiyo nilikuwa namuaga.Ilikuwa ni mara yangu ya mwisho kuongea naye.Masikini mdogo wangu ,nitampata wapi tena kama yeye? Loniki naye aliendelea kulia kwa nguvu
Sarah ambaye ndiye anayemfuata Loniki kwa kuzaliwa naye akawasili , akasalimiana na dada yake pamoja na familia yake .Baada ya kusalimiana,Loniki na Saraha wakaelekea bustanini kwa maongezi.
“Sarah moyo wangu umeumia sana kwa kifo cha Vero.Ninahisi ni kama vile roho yangu inataka kutoka.Vero alikuwa ni kila kitu kwangu.Nilimpenda mno kiasi kwamba nashindwa hata nifanye nini.Kama ningekuwa na uwezo wa kumrudisha hai ningefanya hivyo.Hebu nieleze Sarah ili nifahamu namna kifo cha Vero kilivyotokea kwa sababu najiona kama vile bado niko ndotoni.” Akasema Loniki
“Loniki kifo cha Vero kimetokea ghafla sana na hakuna aliyetegemea kama ingekuwa hivi.Nilipigiwa simu na mama siku moja kabla ya Vero kufariki akinitaka kama nina nafasi basi tuongozane kuelekea katika kikao kilichokuwa kimeitishwa nyumbani kwa wazazi wa Patrick kikao ambacho kilikuwa ni maalum kwa ajili ya kuongelea maandalizi ya mwisho ya harusi ya Vero na Patrick.Sikuwa na nafasi ya kuhudhuria kikao hicho hivyo nikamuomba shangazi aongozane na mama .Walifika kikaoni lakini mambo yakawa tofauti na walivyokuwa wametegemea.Wakati kikao kikiendelea Patrick alisimama na kuomba aongee machache.Wote walitarajia labda angeweza kuongelea kuhusiana na harusi yake lakini hakufanya hivyo na badala yake akaanza kutoa historia yake wapi alipotoka na katika historia hiyo alimtaja msichana mmoja aitwaye Happy kwamba aliwahi kuwa mpenzi wake wakati wakisoma na ndiye alikuwa sababu ya yeye kufungwa gerezani mara ya kwanza.Wakati Patrick akiwa gerezani kwa kosa la kuua bila kukusudia wakati akimuokoa Happy asibakwe na kundi la wahuni,Happy alihamia nchini Marekani kwa ajili ya masomo na hapo ndipo Patrick alipokutana na Vero alipokwenda kumtembelea mjomba kule gerezani Songea.Vero alitokea kumpenda Patrick na kama unavyojua Vero huwa akipenda anapenda kupita kiasi.Kwa kuwa alimpenda Patrick alifanya kila lillilowezekana na kujenga urafiki kati yao.Alipoondoka kule Songea kurejea Dar es salaam Patrick alimpatia barua ili aitume kwa Happy.Kwa kuwa tayari alikwisha mpenda Patrick na alikuwa akihitaji awe wake ,Vero hakuituma ile barua na badala yake aliandika barua nyingine ikimtaarifu Happy kamba Patrick amefariki dunia kwa ugonjwa wa kuhara akiwa gerezani.Baadae alikwenda tena kwa Patrick na kumtaarifu kwamba alipata taarifa kwamba Happy tayari ameamua kuolewa na mzungu na tayari ana ujauzito .Huo ukawa ni mwanzo wa Patrick na Happy kutengana na hivyo kumpelekea Patrick kumpa Vero nafasi moyoni mwake wakawa wapenzi na hatimaye uchumba na maandalizi ya ndoa yakaanza.” Sarah akatulia akamuangalia dada yake aliyekuwa amekaa kimya akimsikiliza kwa makini.
“Siku moja tulipata taarifa kwamba Patrick amepoteza fahamu kwa mstuko.Hakuna aliyefahamu sababu ya mstuko ule alioupata uliopelekea apoteze fahamu.Ukweli ni kwamba alipatwa na mstuko baada ya kumuona Happy mpenzi wake wa zamani katika runinga akishiriki kinyang’anyiro cha Miss Tanzania .Baadae Happy na Patrick walionana na ndipo ukweli ulipodhihirika kwamba ni Vero ndiye aliyewatenganisha kwa kutunga uongo.Kitendo hiki kilimchukiza sana Patrick na hivyo mbele ya wazazi ndugu na jamaa akatangaza kuuvunja uchumba kati yake na Vero.Baada ya kauli ile ya Patrick iliyopelekea watu kadhaa kupoteza fahamu,Vero aliondoka na kuelekea nyumbani halafu akachukua bastora ile iliyokuwa ya baba akamfuata Patrick hospitali.Hatujui alikuwa na lengo gani lakini kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio wanadai kwamba Vero alikuwa amedhamiria kuua kwani alikuwa amemuelekezea Patrick bastora na aliachia risasi moja iliyomkosa Happy.Baada ya tukio hilo Patrick na Vero walianza kupambana akiwa na lengo la kumnyang’anya silaha ile lakini katika purukushani hiyo Vero akajigonga ukutani na kufariki hapo hapo.Kwa hivi sasa Patrick anashikiliwa katika mahabusu ya gereza la Uwangwa na kesi yake tayari imekwisha tajwa mahakamani.Yule miss Tanzania Happy ameachiwa huru baada ya kuonekana hahusiki na tukio lile.Kwa ufupi hicho ndicho kilichotokea.Nimeumia sana Loniki.Nimelia mno hadi machozi yamekauka kabisa lakini hakuna namna nyingine ya kufanya zaidi ya kumuombea mdogo wetu apumzike kwa amani “ akasema Sarah.Loniki akainama na kufuta machozi.
“Sarah naomba uende chumbani kwangu katika kibegi kidogo cheusi utakuta kuna mkebe mdogo naomba uniletee” akasema Loniki ambaye machozi bado yaliendelea kumtoka.
Sarah akaenda chumbani na kurejea na mkebe ule mdogo alioutaka Loniki,akaufungua na kutoa sigara akawasha na kuanza kuvuta.Akapiga mikupuo kadhaa na kupuliza moshi mwingi hewani
“Sikutegemea kama Patrick angeweza kumfanyia Vero kitendo kama hiki.Wiki tatu tu kabla ya ndoa anavunja uchumba? Tena kwa sababu ya msichana ambaye ni Miss Tanzania? This is unfair.Hakumtendea haki Vero hata kidogo.Alimfanyia kitendo cha kinyama na kikatili sana.Ameniumiza mno na kwa maumivu haya ninayoyasikia sasa hivi sintaweza kumsamehe hadi siku naingia kaburini.Ameiondoa furaha na pambo la familia yetu.Tulimpenda mno Vero na tulimtunza zaidi ya tulivyojitunza wenyewe,iweje leo atokee Patrick na amtende Vero namna hii??? Patrick must pay for this..I swear in heaven and earth Patrick must pay..!!!!!.” Loniki akasema kwa hasira huku akipuliza moshi mwingi hewani.
“Tayari yuko mikononi mwa sheria na ninafahamu lazima sheria ichukue mkondo wake na haki itendeke” akasema Sarah.
“That’s not enough…,lazima yeye na yeyote aliyeshirikiana naye katika kumkatili uhai mdogo wangu vero ,walipe uovu walioutenda.Damu ya mdogo wangu haiwezi kupotea hivi hivi.They must pay.Sintaondoa mguu wangu Tanzania hadi pale nitakapohakikisha kwamba wote wamelipa.” Akasema Loniki kwa hasira huku machozi yakimtoka na mara akatokea shangazi yao.
“Loniki pole sana ,huu ni wakati mgumu sana.Tunatakiwa tumuombe Mungu atupe uvumilivu wa hali ya juu sana.Mambo haya haujui yataisha vipi kwa sababu tumepokea taarifa sasa hivi kwamba baba yake Patrick naye amefariki dunia kwa shinikizo la damu .” akasema shangazi yao
“What !!!!!!!.....baba yake Patrick naye amefariki dunia ? !! akauliza Sarah kwa mshangao
“Ndiyo Sarah ,amefariki dunia.Sijui Yule kijana alikuwa anafikiria nini hadi akafanya maamuzi haya ambayo yanaathiri maisha ya watu wengi?
“Ouh my God !! “ akasema Sarah huku akivuta pumzi ndefu.
“Hilo ni pigo kwa Patrick na bado yatakuja mengine makubwa zaidi” akasema Loniki
“Loniki usiseme hivyo.Tunatakiwa tumuombe sana Mungu atuepushe na mabalaa mengine yanayoweza kujitokeza kwa sababu jambo hili linaonekana ni kama limekuwa na mkosi Fulani.” Akasema Sarah ambaye kwa haiba yake ni mpole na huongea taratibu
“Sarah huna haja ya kumuonea huruma huyu shetani asiyekuwa na huruma hata kidogo.Amesababisha kifo cha mdogo wetu .Kama asingeuvunja uchumba wake na Vero basi ndugu yetu angekuwa hai hadi hivi sasa.Mimi simuonei huruma hata kidogo na ninaapa kwa miungu yote kwamba Patrick na huyo kahaba wake Happy watanitambua.They must pay “ akasema Loniki kwa ukali.
“Sarah naomba umtume mtu akanitafutie mvinyo mkali ,pengine unaweza kunisaidia kuyapunguza machungu haya ninayoyasikia.” Akasema Loniki.Sarah akainuka na kuondoka pale bustanini akamuacha Loniki na shangazi yake.
“Shangazi nimeumia sana lakini kwa sasa sintasema lolote kwa sababu bado tuko katika majonzi makubwa .Nitaongea baada ya kumaliza msiba huu.Ila naomba mtambue kwamba sijawahi kuumia moyo katika maisha yangu kama nilivyoumizwa na kifo cha Vero.Nimeumia sana.Nimelia sana na nitaendelea kulia kwa miaka mingi ijayo.Laiti uhai ungeweza kununuliwa basi ningetumia fedha zangu zote kuununua uhai wa Vero.” Akasema Loniki
“Kwa kweli bado siamini kama Yule kijana Patrick amefanya jambo kama hili alilolifanya.Siku zote nilimuona ni kijana mtaratibu na mwenye roho nzuri ya huruma na anayempenda Vero lakini kumbe ni kijana mwenye roho mbaya ya kishetani.” Akasema shangazi yake Loniki.
“Shangazi nina hakika kabisa kwamba haikuwa akili yake ya kawaida iliyomfanya Patrick akafanya alilolifanya.Japokuwa sijawahi kukaa naye kwa muda mrefu nikamfahamu vizuri lakini kwa kipindi kifupi nilichowahi kuonana naye nilimuona ni kijana mtaratibu sana na mwenye utu.Ninashawishika kuamini kwamba yule mwanamke Happy lazima atakuwa ametumia hata dawa ili kumvuruga Patrick akili na asijue jambo analolifanya.Hainiingii akilini hata kidogo kuamini eti kwamba Patrick aliamua kumuacha Vero kwa akili yake timamu tena wiki kadhaa kabla ya ndoa yao.Ninaapa kwenda hadi mwisho wa dunia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Patrick na Happy wamelipa kwa kitendo cha kumuua Vero.” Akasema kwa uchungu Loniki bado machozi yaliendelea kumtoka.Mkononi alikuwa na sigara yake akiivuta na kupuliza moshi hewani.
“Narudia tena kwamba sintaondoa mguu wangu Tanzania hadi nitakapohakikisha kwamba wote waliohusika na kifo cha mdogo wangu wamelipa nikianzia na Patrick na Happy.”
“Umefikiria kufanya nini Loniki” akauliza shangazi yake
“Shangazi ni mapema sana kusema nitafanya nini lakini nitakachokifanya kitakuwa ni fundisho kwao na familia zao.Tusubiri kwanza tumzike Veronika na halafu mtajua nitakachokifanya.” Akasema Loniki na muda huo huo Sarah akarejea akiwa na chupa ya mvinyo.Loniki akaipokea na kuinywa kwa pupa.
“Sarah nasikia uchungu mwingi ambao siwezi kuuelezea.Angekuwa ni mtu ambaye si jasiri tayari angekwisha kufa kwa uchungu huu ninaousikia.Uchungu huu na maumivu haya hayawezi kwenda bure bila ya kulipwa.Patrick amenifanya nijifunze ukatili na nitakuwa mkatili kama anavyotaka niwe ” Akasema Loniki.Sarah akaumuangalia dada yake na kusema
“Loniki naomba utulize moyo wako na usiwe na hasira namna hiyo.Sote tulimpenda sana Vero lakini hata kama ukiwaua wahusika ili kulipiza kisasi Vero hatarudi tena.Kilichobaki ni kusameheana ili maisha yaweze kuendelea .Tukumbuke kwamba hata Vero naye alifanya makosa.Alitunga uongo na kuwatenganisha Patrick na Happy.Hili ni jambo baya sana alifanya na ambalo limekuja kumgharimu maisha yake.Nakushauri dada yangu tuachane na haya mambo ya kulipiza visasi kwani hayatatusaidia kitu badala yake yatazidi kututia matatizoni.” Akasema sarah
“Maneno gani hayo unayaongea Sarah? Unaonekana umefurahishwa na kifo cha Vero .Sikuombi ushirikiano wako na wala sihitaji kushirikiana na mtu na hakuna mtu yeyote atakayenizuia wala kuyabadili mawazo yangu.Lazima wote waliohusika na kifo cha Vero walipe.” Akasema Loniki kwa ukali kisha akainuka na kuondoka.
“Shangazi mimi siafikiani kabisa na mawazo ya Lonny ya kulipiza kisasi kwa Patrick na Happy.Tukio limekwisha tokea ,tuliache lipite na maisha yaendelee kama kawaida.Aliyesababisha kifo hicho cha Vero tayari anashikiliwa na vyombo vya sheria ,kwa nini basi tuviingilie vyombo vya kutoa haki ? Sioni sababu yeyote ya kuendeleza uhasama baina ya familia zetu kwani tayari tulikwisha kuwa kama ndugu na hatupaswi kutengana kwa sababu ya tukio hili.Wa kulaumiwa hapa si Patrick na Happy pekee bali hata Vero naye alifanya makosa tena makubwa ya kuwatenganisha watu wawili waliopendana kwa dhati.Ukumbuke Patrick aliwahi kufungwa gerezani kwa ajili ya Happy , kwa maana hiyo aliumia sana alipotenganishwa na mtu aliyempenda kwa uongo wa Vero.Pamoja na kosa hilo alilolifanya lakini bado Vero alidhamiria kufanya mauaji.Kama asingefariki yeye basi angeweza kuwaua Patrick na Happy kwani tayari alikwisha dhamiria kufanya hivyo.Naomba shangazi mshawishi Loniki asituingize katika matatizo mengine zaidi“ akasema Sarah.Shangazi yake akamuangalia na kubetua midomo akasema
“Sarah wewe ni mtu wa ajabu sana na kama alivyosema Loniki unaonekana umefurahi kwa kifo cha mdogo wako.Kama kweli ungeumizwa na kifo cha Vero basi ungeweza kusimama na kumtetea kwa kuungana na Loniki kulipa kisasi kwa wale waliohusika na kusababisha kifo hicho.Umenishangaza sana hata mimi sikutegemea kabisa kusikia ukiongea maneno hayo” akasema shangazi
“Shangazi …..” akaita Sarah lakini tayari shangazi yake alikwisha inuka na kuanza kuondoka.
“Sihitaji kusikia upuuzi wowote toka kwako .Umenisikitisha sana Sarah” akasema shangazi yake huku akiondoka.
“wananishangaza sana hawa ndugu zangu kwa maamuzi yao na kutokuona mbali.Kisasi hakitatusaidia chochote na badala yake tutazidi kuongeza matatizo zaidi.Kama watalipiza kisasi wafanye wao ,mimi wasinishirikishe kabisa.Nahitaji kuishi kwa amani na sitaki kugombana na mtu yeyote.Sijui kwa nini wanashindwa kuona kwamba ni Vero ndiye chanzo cha haya yote” akawaza Sarah kisha naye akaondoka pale bustanini
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 32
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Sarah wewe ni mtu wa ajabu sana na kama alivyosema Loniki unaonekana umefurahi kwa kifo cha mdogo wako.Kama kweli ungeumizwa na kifo cha Vero basi ungeweza kusimama na kumtetea kwa kuungana na Loniki kulipa kisasi kwa wale waliohusika na kusababisha kifo hicho.Umenishangaza sana hata mimi sikutegemea kabisa kusikia ukiongea maneno hayo” akasema shangazi
“Shangazi …..” akaita Sarah lakini tayari shangazi yake alikwisha inuka na kuanza kuondoka.
“Sihitaji kusikia upuuzi wowote toka kwako .Umenisikitisha sana Sarah” akasema shangazi yake huku akiondoka.
“wananishangaza sana hawa ndugu zangu kwa maamuzi yao na kutokuona mbali.Kisasi hakitatusaidia chochote na badala yake tutazidi kuongeza matatizo zaidi.Kama watalipiza kisasi wafanye wao ,mimi wasinishirikishe kabisa.Nahitaji kuishi kwa amani na sitaki kugombana na mtu yeyote.Sijui kwa nini wanashindwa kuona kwamba ni Vero ndiye chanzo cha haya yote” akawaza Sarah kisha naye akaondoka pale bustanini

ENDELEA……………….

Baada ya kurejea toka katika mishughuliko yake ya siku ,mzee Raymond Kibaho baba mzazi wa Happy kibaho alitaka kufahamu kuhusiana na maendeleo ya mwanae.
“kama kawaida bado hakuna mabadiliko yoyote .Leo alikwenda mahakamani lakini hakuweza kuingia ndani ya mahakama na toka amerudi amejifungia chumbani kwake na hataki kuonana na mtu yeyote .Mtu pekee ambaye amekubali kuonana ni yule wakili wa Patrick” akasema mama Happy.Mzee Raymond akainama chini akafikiri kisha akasema
“Happy anahitaji msaada mkubwa sana wa kisaikolojia.Ngoja nikaonane naye” akasema mzee Raymond huku akitembea taratibu hadi katika mlango wa Happy akagonga lakini hakujibiwa.
“Happy my dear its me your father” akasema mzee Raymond na baada ya dakika mbili mlango ukafunguliwa.Happy alikuwa katika sura yenye majonzi makubwa sana.Baba alipomuona akastuka na kuogopa .Akamsogelea pale sofani alipokuwa amekaa akaketi pembeni yake.
“Happy mwanangu ni kwa nini unakuwa katika hali hiyo? Kwa nini unateseka kiasi hicho? Mimi baba yako na familia yote tunaumia sana tukikuona ukiwa katika hali hii.Wewe ndiye furaha yetu ,wewe ndiye mwanga wa nyumba yetu.Ukififia fahamu kwamba nyumba yetu haina mwanga tena.Tazama sasa nyumba iliyokuwa imetawaliwa na vicheko na furaha kubwa leo hii imekuwa ni nyumba ya simanzi na vilio kila kukicha.Happy wewe ndiye furaha yetu,ukilia nasi tunalia,ukicheka nasi tunacheka,,ukifurahi nasi tunafurahi pia.Tafadhali Happy nakuomba usiendelee kuumia moyo wako.You have to let it go.You have to live your life like it was before.Tuko nyumna yako na tutafanya kila tuwezalo kuhakikisha kwamba unarejea katika maisha yako ya kawaida.” Akasema mzee Kibaho
“Baba nakushukuru sana na nitaendelea kukushukuru siku zote kwa ushirikiano wako mkubwa unaonipa.Pamoja na upendo mkubwa toka kwa familia yangu lakini bado najikuta nikishindwa kuvumilia kila nikikumbuka kilichotokea.Picha ya tukio ilie imekuwa inanitesa usiku na mchana.Sikutegemea kamwe katika maisha yangu kama nitakuja kuua mtu.Kila nikifikiria kuhusu jambo hilo naumia sana.Kingine ambacho kinaniumiza akili yangu ni kila nimuwazapo Patrick.Sijui hatima yake itakuwa nini ,sifahamu atapata adhabu gani.Naumia sana dady” akasema Happy na kuanza kulia.
“Nyamaza kulia Happy.Be strong my daughter.You are always strong.Happy unahitaji ujasiri mkubwa sana na ili uwe na ujasiri unahitaji nguvu.Nguvu inakuja kwa kula chakula kwa hiyo naomba kuanzia sasa usizembee tena kula chakula.Ni chakula pekee ndicho kitakachokupa nguvu zitakokufanya uwe jasiri na kusimama imara kumtetea Patrick.He needs you now.He needs your support.So you cant support him while you are weak.Naomba inuka sasa twende mezani ukapate chakula “ akasema mzee Kibaho na kumshika Happy mkono wakaelekea katika chumba cha kulia chakula ambako Happy alijitahidi akala chakula
“Baba nakushukuru sana kwa kunipa moyo.Maneno yako uliyoniambia usiku huu na yale aliyonieleza Savanna yamenifanya nitambue nini natakiwa kufanya.Ninatakiwa kukabiliana na hali hii bila woga.Natakiwa kusimama na Patrick katika suala hili hadi mwisho.Amenionyesha upendo wa kweli kwa kukubali kuubeba mzigo mzito ambao hakuustahili.Ili kuweza kulifanikisha hilo nimewaza na kufikia maamuzi” Happy akanyamza akawatazama baba na mama yake waliokuwa kimya wakimsikiliza .Kila mtu alitaka kuyafahamu maamuzi anayotaka kuyachukua Happy.
“Nimeamua kulivua taji la Miss Tanzania.” Akasema Happy na kuwastua wote.Kila mmoja alimwangalia kwa mshangao mkubwa.Hakuna aliyetegemea kama Happy angefikiria kufanya jambo kama lile
“Nafahamu ni namna gani mlivyostushwa na maamuzi haya.Nimeamua kuchukua maamuzi haya magumu baada ya tafakari ya kina.Kwa kuhusika na tukio hili lililotokea tayari nimelitia doa taji la miss Tanzania.Kila siku magazeti na vyombo vya habari vinaripoti tukio hili kwa kutumia jina la Miss Tanzania badala ya Happy.Ili kuilinda heshima ya taji hili sina budi kulivua .Vile vile nimefikia maamuzi haya kwa ajili ya kupata muda zaidi wa kuwa na Patrick katika wakati huu mgumu tulionao.Nafahamu maamuzi haya yatawaumiza wengi lakini sina namna nyingine ya kufanya.Ninafanya hivi kwa ajili yangu mimi na nitawaomba Watanzania wanisamehe katika hili kwani nimewaangusha.Walikuwa na matarajio makubwa sana toka kwangu” akasema Happy.Bado wazazi wake waliendelea kumshangaa.
“Mwanangu Happy una hakika na maamuzi yako? Akauliza mama yake ambaye alikuwa anamtazama kwa macho makali.
“Ndiyo mama,nina hakika na maamuzi yangu.Ninafanya hivi kwa ajili yangu mimi na si kwa ajili ya mtu mwingine yeyote.Wapo watakaonibeza kwa maamuzi haya lakini sintabadili maamuzi yangu.Niko tayari kukabiliana na chochote kitakachojitokeza kutokana na maamuzi haya.” Akasema Happy
“Happy hata mimi bado nina wasi wasi sana kuhusiana na maamuzi haya.Naona kama umefanya maamuzi ya haraka sana.Kwa nini usisubiri kwanza kichwa chako kitulie ndipo ufanye maamuzi yenye kufaa? Akasema Margreth
“Hapana Margreth,sijafanya maamuzi ya haraka kwa kukurupuka kama unavyodhani.Nimefanya maamuzi haya nikiwa na akili zangu timamu na hii ni kwa faida yangu na Patrick.”
“Nimekusikia katika kila maongezi yako unamtaja Patrick.Vipi kuhusu Mike? Yeye mbona humpi nafasi ? Mike amekuwa nawe kwa miaka mingi sasa na tayari mmekwisha kuwa wachumba.Ametoka Marekani kwa ajili ya kuja kuungana nawe lakini hauonyeshi kufurahishwa na ujio wake hata kidogo.Kwwa nini unamfanyia hivyo mwenzio? Akauliza mama yake Happy.Bila kukwama kwama Happy akajibu.
“Mama na familia nzima kwa ujumla kuna jambo ambalo sikuwa nimeliweka wazi kwenu na ninaomba nitumie fursa hii kuliweka wazi mbele yenu.Nimeamua kuachana na Mike” akasema Happy.
“Unasema ?????!!!!....” mama yake akauliza kwa hamaki huku akisimama na kusababisha glasi kuanguka na kuvunjika.
“Unasemaje Happy ???? akauliza tena mama yake Happy
“Nimeamua kuachana na Mike” akasema Happy.Baba yake akatoa kitambaa na kujifuta jasho lililoanza kumchuruzika.
“Happy sikutegemea kama siku moja ungekuja kufanya maamuzi ya kipuuzi namna hii.Umenisikitisha sana mwanangu.Bado siamini kama maneno haya unayoyazungumza yametoka mdomoni mwako.Baada ya miaka hii yote kupita ukiwa na Mike leo hii unadiriki kusimama na kusema kamba Mike humtaki tena? Mike ambaye amekuwa nawe katika nyakati zote za shida na raha leo hii hana thamani tena kwako? Happy ni kitu gani kimekubadilisha namna hii? Huyo Patrick ambaye hakauki mdomoni mwako amekupa kitu gani cha kukufanya ubadilike namna hi??? “ akasema kwa ukali mama yake Happy
“Happy mimi sikubaliani kabisa na hicho unachotaka kukifanya.Ninakuapia iwapo utaachana na Mike basi tambua kwamba mimi si mama yako tena.” Akaendelea kufoka mama yake
“Mama haya ni maamuzi yangu mimi, kwa manufaa ya maisha yangu mimi mwenyewe.Mimi ndiye mwenye kufanya maamuzi ya nini nifanye na nani niwe naye katika maisha yangu.Nimemchagua Patrick na nitahakikisha ninafanya kila linalowezekana ili kuwa naye maishani.Mike ananipenda na hata mimi nampenda pia lakini moyo wangu hauko radhi kuendelea kuwa naye.Moyo wangu unamuhitaji Patrick pekee.Tafadhali mama naomba tusiyafanye mambo haya yawe magumu zaidi.Naomba nyote mkubaliane na maamuzi yangu” akasema Happy
“Happy usisikitike mwanangu.Mimi kama baba yako ninasema kwamba ninakubaliana na mawazo yako.Haya ni maisha yako na wewe ndiye mwamuzi wa nani ambaye unahitaji kuwa naye katika maisha yako.Kama kiongozi wa nyumba hii ,ninasema kwamba maamuzi ya Happy ndiyo ya mwisho na hakuna wa kuyapinga.Happy ninakuunga mkono na nitakuwa pamoja nawe katika kila maamuzi unayoyachukua kwa faida yako” akasema mzee KIbaho na kumfanya mke wake amuangalie kwa macho makali asiamini kile alichokisikia
“Ahsante sana baba .Nashukuru kwa kuniunga mkono.Nahitaji sana uungwaji mkono katika maamuzi magumu ninayoyafanya kwa ajili ya mustakabali mzima wa maisha yangu” akasema Happy
“Usijali mwanangu,tuko pamoja nawe katika kila jambo.Tunakuunga mkono katika maamuzi yote yenye faida katika maisha yako” akasema mzee Kibaho
“Baba ahsante sana” akasema Happy
“Happy wewe ni mwanetu na tuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba unakuwa na furaha siku zote za maisha yako na ni wajibu wetu kuungana nawe katika kila nyakati unazohitaji msaada wetu.Siku zote kumbuka kwamba wewe ndiye mwenye uamuzi na maisha yako.Kama Patrick ndiye mwanaume wa maisha yako na ambaye unahisi atakupa furaha katika maisha yako ,sisi hatuna kipingamizi hata kidogo.Kwa mara ya kwanza hata mimi naomba nikiri kwamba nimevutiwa na huyu kijana Patrick.Anaonekana ni kijana ambaye ana upendo wa dhati kwako .Kitendo cha kukubali kubeba dhamana yako ni kikubwa sana na ni watu wachache mno katika dunia ya sasa wanaoweza kufanya kitendo kama hiki.Ni kijana wa aina yake anayehitaji kuungwa mkono na kupewa moyo.Natamani nimuone tena huyu kijana kwani nakumbuka nilimuona miaka mingi iliyopita kipidi kile akiwa na kesi kule Iringa.” Akasema mzee Raymond Kibaho huku akiangaliwa kwa jicho kali na mke wake.
“Margreth say something !!!!!..Wewe umekaa kimya tu na hauchangii chochote.Au na wewe unakubaliana na maamuzi ya dada yako? Akauliza kwa ukali mama yake
“Mama ,mimi sina la kusema.Haya ni maamuzi yake binafsi na kama baba alivyosema kwamba Happy ndiye mwenye mamuzi na maisha yake.Mimi ninakubaliana na maamuzi anayoyachukua” akasema Margreth.
“Stupid !!!!!!!....” akasema mama Happy kwa ukali akainuka na kuondoka kuelekea chumbani huku akiongea peke yake.Alikuwa amekasirika mno
“Naomba msimjali mama yenu wanangu.Ninyi sasa hivi ni watu wazima na mnajua mnachokifanya katika maisha yenu.Mimi niko nyuma yenu na nitashirikiana nanyi katika kila hatua.Nataka binti zangu muishi maisha ya furaha na wala sintawapangia nani anawafaa katika maisha yenu.Kumbukeni hatima ya maisha yenu iko mikononi mwenu.Ninawapa uhuru wa kufanya machaguo yenye kufaa ili msije kujilaumu siku za usoni” akasema mzee Kibaho
“baba kuna taarifa nyingine ya kuhuzunisha” akasema Happy
“Taarifa gani hiyo?
“Baba yake Patrick amefariki dunia jioni ya leo”
“Unasema …….!!??” Mzee Kibaho akastuka
“Baba yake Patrick amefariki dunia .Nimeumizwa sana na taarifa hizi.Baba sikutegemea kama mambo haya yangefika hapa yalipofika.Sikujua kama maamuzi yetu yangetufikisha katika hali hii na kusababisha kupotelewa na wapendwa wetu.Kwanza alikuwa ni Vero na sasa ni baba mzazi wa Patrick na sijui ni nani atakayefuata kwa sababu suala hili kila uchao linachukua sura mpya” akasema Happy
“Nimestushwa sana na taarifa hii.Nini kimesababisha kifo chake? Akauliza mzee Kibaho
“ni shinikizo la damu”
“Ouh Mungu wangu ! Apumzike kwa amani mzee mwenzangu.Namkumbuka sana hasa wakati ule wa kesi ya Patrick wakati mnasoma alikuwa ni mtu mwenye ushirikiano mkubwa .Tulishirikiana vizuri sana” akasema mzee Raymond halafu kikapita kimya kifupi
“Happy nakuomba usihuzunike sana mwanangu na wala matukio haya yasikurudishe nyuma katika maamuzi yako.Najua mliamua kuchukua maamuzi haya wewe na Patrick kwa ajili ya furaha ya maisha yenu kwa hiyo usikatishwe tamaa na magumu yatakayotokana na maamuzi yenu.Mengi yatasemwa na mengi yatajitokeza ya kukatisha tamaa lakini ninachoweza kukushauri ni kwamba hata likitokea suala gumu kiasi gani simama imara katika maamuzi yako” akasema mzee Kibaho.
“Nitafanya hivyo baba” akasema Happy
“Kuhusu huyu kijana Mike,umekwisha muweka wazi kuhusu mpango wa kuachana naye? Akauliza mzee Kibaho
“Hapana baba ,bado sijamueleza chochote.Kila nikitaka kumweleza nashindwa”
“Ouh My dear,usiogope kufanya hivyo.Kuwa jasiri na umweleze ukweli ili afahamu angali bado mapema.Tafuta namna nzuri ya kumweleza ili aelewe.Najua si suala rahisi kumwambia lakini hakuna namna nyingine ya kufanya zaidi ya kumueleza ukweli.Patrick yeye amekwisha maliza sehemu yake na yametokea haya yaliyotokea .Wewe pia inakubidi ufanye upande wako.Mwambie ukweli wala usiogope kitakachotokea.Kuhusu hili suala la kulivua taji la Miss Tanzania umejipanga vipi?
“Nimekwisha wasiliana na mkurugenzi wangu na nimemweleza aniandalie mkutano na wandishi wa habari kesho saa nne asubuhi,kwa hiyo kesho nitalitangazia taifa azma yangu ya kulivua taji la Miss Tanzania.Baada ya hapo nitaonana na Mike na kumweleza ukweli.Kesho itakuwa ni siku yangu ngumu sana,sifahamu nini kitatokea hiyo kesho lakini lazima niyafanye haya yote” akasema Happy.Baba yake akamuangalia kisha akasema
“I’ll be with you”
“me too” akasema Margreth.Happy akatabasamu lile tabasamu lake adimu sana.
“Nashukuruni sana.I love you my family” akasema Happy.


* * *`

Taarifa za kifo cha baba yake Patrick zilisambaa kwa kasi kubwa.Watu walifika kwa wingi msibani nyumbani kwa Marehemu baada ya kuzipata taarifa hizi za kustusha.Wengi hawakuamini taarifa hizi na kuwafanya wafike wenyewe kuthibitisha kama ni kweli.Mtaa huu walioishi wazazi wa Patrick ulijaa watu na kutawaliwa na vilio.
Saa tatu za usiku gari moja lenye rangi ya fedha aina ya BMW likasimama nje ya nyumba ya wazazi wa Patrick na mwanadada aliyekuwa amejitanda mavazi meusi akashuka .Aliangaza angaza huku na huko kana kwamba kuna mtu alikuwa anamtafuta lakini hakujua aanzie wapi kutokana na idadi kubwa ya watu waliouwepo hapo msibani.Akachukua simu yake akazitafuta namba Fulani na kupiga
“Hallo Alois habari yako? Pole sana na matatizo.Mimi niko hapa nje ya nyumba nashindwa kuingia ndani kutokana na idadi kubwa ya watu” akasema mwanadada Yule .Baada ya kama dakika mbili akatokea Alois na kumfuata Yule dada
“Ouh Sarah !!!!..karibu sana” akasema Alois huku akikumbatiana na Sarah dada yake Vero.
“Pole sana Aloisi.Nimepata taarifa za msiba wa baba usiku huu .Nimestuka sana nikaona siwezi kulala bila kuja kutoa pole.” Akasema Sarah
“Ahsante sana kwa kufika Sarah.Mtatusamehe sana kwa kutoweza kufika katika msiba wa Vero wala kutuma mwakilishi.Toka matatizo haya yalipotokea tumekuwa na wakati mgumu sana kumuuguza mzee na leo jioni ametutoka” akasema Alois
“Poleni sana Alois na wala usijali kuhusu kutokufika msibani kwani bado zilikuwa zinaandaliwa taratibu ikiwa ni pamoja na kuwasubiri baadhi ya ndugu walioko nje ya nchi wafike .” akasema Sarah
“Hii ni kazi ya Mungu na siku zote haina makosa.” Akasema Alois
“Alois mimi si mkaaji sana ,nimepita tu kutoa pole kwa msiba huu .Naomba yaliyotokea yasiweze kutugawa na kutufanya tuwe na uhasama au visasi kwani sisi tayari ni ndugu na tutaendelea kuwa hivyo siku zote.Tusikubali kugawanywa kwa mambo haya waliyoyafanya wadogo zetu.” Akasema sarah
“Nakushukuru sana Sarah kwa kulitambua hilo.Ni kweli hayo usemayo kwamba hatupaswi kutenganishwa na tukio hili lililofanywa na wadogo zetu.Umoja na mshikamano wetu lazima vidumishwe siku zote”
“Kweli kabisa Alois.Hatupaswi kufikia hatua ya kuchukiana na kumtafuta mchawi ni nani.Wote tunasikitika kwa yaliyotokea lakini hatuna budi kuyasahau yote na kusonga mbele na maisha yetu.Alois ninaweza kupata nafasi ya kuonana na mama nimpe pole kwa usiku huu?
“Bado hayuko katika hali nzuri lakini twende tukamuone” akasema Alois na kumuongoza Sarah hadi ndani aliko mama yake.
“Mama, Sarah amekuja kukupa pole” Alois akamwambia mama yake
“Mama pole sana” akasema Sarah akiwa amepiga magoti na kumkumbatia mama yake Patrick.
“Ni kazi ya Mungu mwanangu haina makosa .Tunashukuru kwa yote” akasema mama yake Patrick huku machozi yakimtoka
Sarah alikaa mle chumbani kwa takribani dakika kumi na tano halafu akaaga
“Nashukuru sana mwanangu kwa kuja kunitazama.Mungu akubariki sana” akasema mama yake Patrick.
“Mama tuko pamoja katika wakati huu mgumu” akajibu Sarah na kutoka mle chumbani,akampigia simu Alois aliyekuwa na pilika nyingi usiku huu ambaye alifika mara moja.Wakati Alois akimsindikikiza Sarah wakapita karibu na mahala walipokuwa wamekaa Andrew na Savanna.
“Andrew huyu ni Sarah dada yake Vero.Amekuja kutupa pole baada ya kupata taarifa za kifo cha mzee.” Akasema Alois halafu akamgeukia Sarah
“Sarah hawa ni marafiki wakubwa wa Patrick.Huyu anaitwa Andrew na Yule pale anaitwa Savanna.”
“Poleni sana jamani,tuko pamoja katika matatizo haya yaliyotufika” akasema Sarah huku akipeana mikono na akina Andrew.
“Mpangilio mzima wa mazishi ya Vero ukoje? Akauliza Savanna
“Kilichokuwa kinasubiriwa ni ndugu waliokuwa mbali nje ya nchi wafike ili tuweze kupanga ratiba kamili ya mazishi.Dada Loniki tayari amekwisha fika na aliyebaki ni mjomba ambaye anaishi Urusi .Yeye tunamtegemea usiku wa leo lakini kwa mujibu wa kamati ya maandalizi imeamuliwa kwamba mazishi yatafanyika kesho kutwa katika makaburi ya kinondoni.Nadhani mpaka kesho tutapata ratiba kamili ya mazishi.Nitawafahamisheni kila kitu baada ya kuipata ratiba kamili” akasema Sarah halafu akaagana na akina Andrew akaelekea katika gari lake.
“Sarah tutatuma ujumbe wa watu wachache kuja kuungana nanyi katika mazishi .Sisi bado hatujapanga tarehe kamili ya mazishi ya mzee bado kuna ndugu wa muhimu tunawasubiri toka mikoani.Watakapofika wote ndipo itakapopangwa siku ya mazishi.Nitakutaarfu juu ya tarehe ya kuzika” akasema Alois
“Sawa Alois tutaendelea kutaarifiana na kujulishana kinachoendelea” akasema Sarah halafu akaingia katika gari lake na kuondoka
“Sasa moyo wangu una amani.Nimefarijika sana kwa kuwapa pole familia ya Patrick.Sitaki kuishi kwa visasi na hasama kama anavyotaka Loniki.Ninafikiria pia baada ya mazishi ya Vero nikaonane na Happy nimfariji na kumpa moyo kwani kwa muda huu nina imani atakuwa katika wakati mgumu sana .Palipo na ukweli lazima tuuseme,Vero alifanya kosa kubwa sana kutunga uongo na kuwatenganisha Patrick na Happy.Hawa walikuwa wanapendana na wana historia ndefu katika mapenzi yao.Simlaumu Patrick kwa maamuzi aliyoyafanya kwani alifanya vile kwa ajili ya kuitafuta furaha ya moyo wake ambayo nina hakika anaipata akiwa na Happy na ndiyo sababu hata baada ya kupita miaka mingi bado hajaweza kumsahau” akawaza Sarah wakati akirejea nyumbani kwako kutokea nyumbani kwa wazazi wa Patrick alikoenda kutoa pole.
“Nimefurahishwa na kufarijika sana na ujio wa Sarah.Sikuwa nimetegemea kabisa kama kuna ndugu yeyote wa Vero angeweza kuungana nasi katika kipindi hiki kigumu.” Akasema Alois baada ya Sarah kuondoka.
“Sarah ni mtu mwelewa sana.Ameonyesha moyo wa uungwana “ akasema Savanna
“Tutatuma ujumbe wa watu wachache ukatuwakilishe siku ya mazishi ili tusije onekana kwamba hatukushirikiana nao katika mazishi ya mtoto wao.” Akasema Alois
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 33
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Hawa walikuwa wanapendana na wana historia ndefu katika mapenzi yao.Simlaumu Patrick kwa maamuzi aliyoyafanya kwani alifanya vile kwa ajili ya kuitafuta furaha ya moyo wake ambayo nina hakika anaipata akiwa na Happy na ndiyo sababu hata baada ya kupita miaka mingi bado hajaweza kumsahau” akawaza Sarah wakati akirejea nyumbani kwako kutokea nyumbani kwa wazazi wa Patrick alikoenda kutoa pole.
“Nimefurahishwa na kufarijika sana na ujio wa Sarah.Sikuwa nimetegemea kabisa kama kuna ndugu yeyote wa Vero angeweza kuungana nasi katika kipindi hiki kigumu.” Akasema Alois baada ya Sarah kuondoka.
“Sarah ni mtu mwelewa sana.Ameonyesha moyo wa uungwana “ akasema Savanna
“Tutatuma ujumbe wa watu wachache ukatuwakilishe siku ya mazishi ili tusije onekana kwamba hatukushirikiana nao katika mazishi ya mtoto wao.” Akasema Alois

ENDELEA…………

Saa tano na dakika kumi na tisa za usiku kwa mujibu wa saa aliyokuwa ameivaa mkononi,Savanna akawasili nyumbani kwake.Alistuka sana baada ya kukuta taa za ndani zinawaka.
“Ouh Gosh ! nani kawasha taa za ndani? Ina maana niliondoka asubuhi bila kuzima taa? Akajiuliza
“ Inawezekana ni kweli niliondoka bila kuzima taa kwa sababu kichwa changu kwa sasa kina mambo mengi mazito.Kesi hii ya Patrick imenifanya nisahau kila kitu.” Akawaza Savanna huku akishuka garini na kuelekea getini.Alistuka baada ya kutoliona kufuli ambalo hutumia kufungia geti.
“Gosh ! kufuli liko wapi? Akajiuliza Savanna huku moyo ukimuenda mbio.
“Kuna wezi wamevunja,wameingia ndani wakaiba?!!..Savanna akaogopa sana
“Ngoja nimpigie simu Kamanda Zuberi anitumie askari.Lazima ndani kwangu nitakuwa nimeibiwa.” akawaza Savanna huku akirudi garini na kuchukua simu .Alizitafuta namba za Zuberi lakini akasita kupiga
“Kwa nini niogope? Hii ni nyumba yangu na sioni sababu ya kuogopa.Ngoja niingie ndani nikatazame kama kumeibwa au vipi ndipo nimpigie simu afande Zuberi.Naweza kuwasumbua askari kumbe ni mimi nilisahau hata kufunga geti.” Akawaza Savanna halafu akashuka garini akalifungua geti.Bila kuogopa akaliingiza ndani gari halafu akafunga geti.Alijaribu kuusukuma mlango wa kuingilia sebuleni lakini ulikuwa wazi na kwa ndani sauti ya muziki ikasikika.Akaingia sebuleni kwa tahadhari.Akapatwa na mshangao mkubwa uliochanganyika na hasira baada ya kumkuta George amejilaza katika sofa pale sebuleni.
“Its’ you again !!!!!......” akasema Savanna kwa hamaki.George hakujibu kitu akabaki akitabasamu.
“Nini kimekurudisha humu kwangu George? Nani kakupa ruhusa ya kuingia humu wakati mimi sipo? Akauliza Savanna kwa ukali.George akatabasamu ,akacheka kidogo na kusema
“Nimerudi kwangu mpenzi..Aren’t you Happy that I‘m back? You didn’t miss me? Akasema George halafu akainuka pale sofani na kumuendea Savanna akataka kumkumbatia.Savanna akamsukuma kwa hasira
“George please get out of here now !!!!” akafoka Savanna
“George sitaki tena kukuona ndani ya nyumba yangu.Uliondoka hapa kwa kashfa na matusi .Nimekwisha choka nawe George naomba uondoke haraka sana.Sikuhitaji hapa kwangu na katika maisha yangu pia.” Akafoka Savanna
“Savanna tafadhali nakuomba upunguze hasira na tukae tuongee tuyamalize mambo haya.I love you Savanna and I cant live without you.Please my love forgive me.Najua nilikosea sana naomba unisamehe” akasema George
“George kichwa changu kina mambo mengi sana kwa sasa na sitaki uwe ni moja ya matatizo yangu.Naomba uondoke uende zako.Sina chochote cha kuongea nawe George.Please go !” akasema Savanna kwa hasira
“Savanna leo hii unadiriki kunitamkia maneno hayo? Muda huu wote tumeishi pamoja kwa amani na upendo leo hii unanitamkia maneno hayo?
“George tafadhali nimechoka sana nahitaji kupumzika.Please go..!!!!!!!” akasema Savanna huku akiufungua mlango na kumfanyia George ishara atoke nje.
“Savanna kweli umeamua kunifukuza?
“ George please go !!..naomba uende”
“ Najua haya yote ni kwa sababu ya Patrick”
“ Vyovyote utakavyofikiria George lakini sihitaji tena kuwa nawe.Tafadhali ondoka”
“Nashukuru sana Savanna kwa mambo uliyonifanyia.Nakutakia maisha mema na huyo Patrick.Akasema George huku akitoka taratibu.Savanna akamfungulia geti akaenda zake.
“ Kesho nitaajiri walinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi waanze kuilinda nyumba yangu.Sitaki huyu mtu awe anakuja hapa kwangu.Vile vile nitabadilisha vitasa vyote vya nyumba nzima kwani tayari anazo funguo zote za nyumba yangu kitu ambacho ni hatari sana.Sihitaji kabisa mawasiliano yoyote naye.Simuhitaji katika maisha yangu.Akili yangu yote kwa sasa inamuwaza Patrick pekee” akawaza Savanna huku akielekea chumbani kwake baada ya George kuondoka.Aliingia bafuni akajimwagia maji halafu akajilaza kitandani.Kichwa chake kilitawaliwa na picha moja tu,picha ya Patrick.
“I’ll get you out Patrick.Nitafanya kila niwezalo kukakikisha kwamba unashinda kesi.Hii ni nafasi yangu nyingine ya kumpata Patrick na safari hii atakuwa wangu peke yangu” akawaza Savanna kisha taratibu usingizi ukamchukua akalala.

* * * *

Saa tatu za asubuhi Patrick macho yake yalikuwa mekundu na kichwa kilimuuma sana kwa mawazo mengi aliyokuwa akiwaza.Hakuweza kupata usingizi usiku alikesha akiwaza hatima ya maisha yake .
Mlango wa chumba chake kilichokuwa na watu wanne ukafunguliwa na akaitwa,akatoka akaongozana na askari magereza wawili akapelekwa katika chumba kimoja kilichokuwa na meza ndogo na viti viwili .Ndani ya chumba kile akakutana na sura ya Savanna.Akafarijika sana kwa kuonana na Savanna ambaye aliinuka na kumkumbatia.
“Pole sana Patrick.” Akasema Savanna
“Ahsante sana Savanna.Nimefurahi umekuja.Nimefarijika sana.Nilikuwa na usiku mrefu mno na sijaweza kupata usingizi kabisa.”
“Pole Patrick.Jitahidi usiwaze sana kuhusu suala hili.Sisi tupo na tunalishughulikia hadi mwisho wake.Habari za toka jana?
“Habari ni kama hivyo nilivyokueleza,mawazo mengi nasikia kama kichwa kinataka kupasuka.Namshukuru Mungu kumekucha salama.”
“Patrick,naomba usijisikie vibaya na wala usithubutu kuyaruhusu mawazo mengi kiasi cha kukukosesha usingizi. Suala hili liko mikononi mwangu ninalishughulikia kwa nguvu na uwezo wangu wote na ninakuahidi kwamba tutashinda.Naomba uniamini kwamba tutashinda kesi hii” akasema Savanna
“Ninakuamini sana Savanna.Moyo wangu hauna wasi wasi hata chembe kuhusu wewe,lakini mawazo mengi yanakuja kila nikikumbuka mambo haya namna yalivyotokea na nini itakuwa hatima yake.Sura ya Vero inanijia kila dakika.Nashindwa kabisa kuitoa kichwani kwangu.Sikutegemea kama angeweza kufikwa na umauti .It looks like she’s haunting me.Ninamfikiria pia Happy.Alikuwa na maisha yake mazuri tu na mpenzi wake lakini alipokutana na mimi ameingia katika matatizo makubwa.Namfikiria baba yangu hospitali.Nawafikiria ndugu zangu,ninafikiria mambo mengi sana na ndiyo maana siwezi kabisa kupata usingizi.” Akasema Patrick.Savanna akamtazama usoni kwa muda kisha akasema
“Patrick kuanzia sasa naomba usifikirie tena kuhusu mambo haya.Kifanye kichwa chako kiwe huru na usikubali kufungwa na mawazo yoyote yale.Yaliyotokea yamekwisha tokea na tuangalie ya mbele.”
“Nakuelewa Savanna hata mimi sitaki kuumiza kichwa changu kwa mawazo mengi lakini nashindwa kabisa kuyaepuka mawazo haya.Anyway tuachane na hayo,vipi ulifanikiwa kupita hospitali na kujua maendeleo ya baba yangu? Ulifanikiwa kuonana na Happy? Vipi kuhusu Vero una taarifa zozote kuhusiana na kinachoendelea kwao? Patrick akauliza maswali mfululizo.
“Happy nilifanikiwa kuonana naye jana.Nilimfuata nyumbani kwao.Anaendelea vizuri.Jana alikuwepo katika viwanja vya mahakama lakini hakuweza kuingia ndani ya mahakama .Bado ana mstuko kwa mambo yaliyotokea na bado inamuwia ugumu kukabiliana na hali halisi.Nimeongea naye kwa kirefu nikamuelewesha kwamba anatakiwa asimame imara kuikabili hali halisi.Nashukuru alinielewa na ameahidi kutokuogopa kitu chochote tena.Ameahidi kukutembelea mara kwa mara hapa gerezani .” Savanna akamuangalia Patrick kwa muda kisha akaendelea.
“Kuhusu Vero ni kwamba atazikwa kesho kutwa katika makaburi ya Kinondoni.Hii ni kwa mujibu wa dada yake Sarah.”
“Ulifanikiwa kuonana na Sarah? Ulienda nyumbani kwao? Akauliza Patrick.
“Hapana sikwenda nyumbani kwao.Alikuja pale nyumbani jana usiku kutoa pole ya msiba….. akasema Savanna na kustuka.
“Mbona umestuka Savanna? Saraha alikuja kutoa pole ya msiba wa nani nyumbani kwetu? Akauliza Patrick huku akimtazama Savanna kwa wasi wasi.Savanna hakujibu kitu akabaki anamuangalia.
“Nijibu Savanna,msiba wa nani ambao Sarah alikuja kutoa pole?
“Patrick !!!.. akaita Savanna
“Naomba uwe mvumilivu sana”
“Savanna mbona unaniogopesha? Nini kimetokea” Nani kafariki tena?Akauliza Patrick huku akimtazama Savanna kwa wasi wasi.
“Patrick ,baba yako amefariki dunia jana jioni.” Akasema Savanna.
Patrick akaishiwa nguvu akabaki anamuangalia Savanna.Alishindwa aseme nini.Savanna akaogopa kwani aliwahi kusikia kwamba Patrick aliwahi kupatwa na matatizo ya mstuko wa moyo
Dakika zaidi ya tatu zilikatika bila ya Patrick kuongea lolote.Alikuwa katika mawazo mazito.
“Are you ok Patrick? Akauliza Savanna
“I’m ok Savanna though I’m deeply hurt.Nashindwa niseme nini,nashindwa nilie au vipi.Tayari nimelia machozi mengi sana na sitaki kulia tena.Hata kama nikilia kwa sauti kama ya radi my dady wont come back.He’s gone.He’s dead.Ninachotakiwa kufanya ni kuwa jasiri na kukabiliana na kila kitakachokuja mbele yangu.Huu ni mwanzo tu nina imani mengi bado yatakuja huko mbeleni.” Akasema Patrick kwa sauti ya upole.Savanna akainuka na kusimama nyuma yake akamshika mabega
“Patrick tuko pamoja katika mambo haya na kamwe usijihisi mpweke.Any time you need someone by your side I’ll be right there for you”
“Ahsante sana Savanna .Sina cha kukulipa kwa wema wako huu mkubwa.Umenionyesha ni namna gani rafiki wa kweli anapaswa kuwa.Wewe ni rafiki wa kweli.Umeweza kusimama nami hata katika nyakati zile ngumu zaidi ambazo wengine wameshindwa.Ahsante sana Savanna siku zote utakuwa hapa moyoni mwangu” akasema Patrick maneno ambayo yalimfariji sana Savanna.
“Usihofu Patrick wewe ni mtu muhimu sana kwangu.Tatizo lako ni langu .Na kwa maana hiyo basi nitafanya kila niwezalo hadi nihakikishe kwamba unakuwa huru.Sintalala usingizi hadi nihakikishe kwamba umekuwa huru” akasema Savanna
“Savanna ,ujio wako umenipa faraja sana japokuwa kidonda cha moyo kimezidi kuongezeka kwa taarifa ya kifo cha baba.Naomba ufanye kila linalowezekana ili niweze kutoka humu ndani.Nina ndoto nyingi sana ambazo zote zitapotea iwapo nitaendelea kukaa gerezani”
“Patrick nimekwisha kuahidi kwamba nitafanya kila linalowezekana ili ushinde hii kesi.Naomba uniamini”
Maongezi kati ya Savanna na Patrick yalichukua zaidi ya nusu saa halafu Patrick akarejeshwa tena mahabusu.Savanna akaondoka .

****************************

Ukumbi mdogo wa mikutano wa Korongo hoteli ulifurika waandishi wa habari wakisubiri kusikia kile walichoitiwa na mkurugenzi wa Miss Tanzania.Waandishi wa habari toka vyombo mbali mbali vya habari walikuwepo hapa ukumbini kuanzia saa mbili za asubuhi.Hii ilionyesha ni kwa jinsi gani walivyokuwa na hamu ya kusikia kile walichoitiwa.Kwa takribani siku kadhaa sasa mrembo mpya wa Tanzania Happy Kibaho amekuwa akitawala vyombo vya habari ,kuhusiana na kuhusika kwake katika ugomvi uliosababisha kifo cha Veronika Rugi aliyekuwa mchumba wa Patrick.Mengi yalikuwa yameandikwa kuhusiana na na tukio hili lakini si miss Tanzania Happy kibaho wala mkurugenzi wake au mtu yeyote toka katika kamati ya Miss Tanzania aliyejitokeza katika vyombo vya habari na kuongea lolote kuhusiana na jambo hili.
Maongezi ya hapa na pale yalitawala miongoni mwa waandishi wa habari wakati wakimsubiri mkurugenzi wa Miss Tanzania.Saa nne kamili za asubuhi juu ya alama ,gari la mkurugenzi wa miss Tanzania likawasili pale hotelini.Akiwa ameongozana na wajumbe watatu wa kamati ya miss Tanzania wakashuka na kuelekea moja kwa moja katika ukumbi wa mikutano kulikokuwa kumejaa waandishi wa habari.Kama ilivyo kawaida yake mkurugenzi huyu akataniana na waandishi wa habari kadhaa .Alikuwa akifahamiana na waandishi wengi wa habari.
Saa nne na nusu akaingia ukumbini mrembo wa Tanzania Happy kibaho akiwa ameongozana na mdogo wake Margreth pamoja na baba yake mzee Raymond Kibaho.Happy aliyekuwa amevaa suruali ya jeans nyeusi ,shati dogo jeusi na miwani mikubwa myeusi iliyoyafunika kabisa macho yake ,alikuwa aking’aa kwa mianga ya kamera za waandishi wa habari waliokuwa wakimpiga picha katika kila hatua aliyopiga.Alisalimiana na na mkurugenzi wake kisha akaelekezwa sehemu ya kuketi.Sura yake haikuwa na lile tabasamu lake lililozoeleka .Picha nyingi ziliendelea kupigwa wakati akiwa amekaa.
“Ndugu waandishi wa habari toka katika vyombo mbali mbali vya habari” alifungua mkutano mkurugenzi wa miss Tanzania.Ukumbi wote ukawa kimya ukimsikiliza.
“Awali ya yote napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru sana nyote kwa kuitika mwito na kufika kwa wingi.Sikutegemea kama kungekuwa na idadi kubwa namna hii ya waandishi.Papo hapo napenda kuwaomba radhi kwa kuchelewa kidogo kuanza mkutano wetu kutokana na sababu zisizoweza kuzuilika.” Akanyamaza kidogo na kuendelea.
“Ndugu zangu waandishi wa habari ,tumewaiteni hapa asubuhi ya leo kwa ajili ya kuweka sawa baadhi ya mambo.Kama mnavyofahamu kwamba kwa siku chache zilizopita mrembo wetu mpya wa Taifa Happy kibaho amekuwa akiandikwa sana katika vyombo vya habari kuhusiana na tukio Fulani ambalo nisingependa kuliongelea hapa lakini naamini nyote mnalifahamu.Kwa muda huu wote amekuwa kimya na hajaongea lolote na hata sisi kama kamati ya Miss Tanzania hatujasema lolote kwani suala lililotokea halihusiani na miss Tanzania bali ni suala binafsi la Happy Kibaho .Kwa hiyo basi mkutano huu wa siku ya leo ni wa Happy Kibaho ambaye ana jambo la kuongea nanyi wanahabari na watanzania wote hususani wale mashabiki wake.Bila kupoteza wakati naomba nimkaribishe Miss Tanzania Happy Kibaho aweze kuzungumza nanyi.Karibu Happy” Akasema mkurugenzi wa miss Tanzania akamsogezea kipaza sauti Happy aliyekuwa amekaa pembeni yake.Akakohoa kidogo kurekebisha koo lake kisha akasema.
“Ndugu zangu waandishi wa habari awali ya yote na mimi ningependa kwanza kuwashukuru kwa kufika kwenu kwa wingi ili kusikia ni kitu gani nimewaitia hapa siku ya leo.” Akanyamaza kidogo halafu akaendelea.
“Kwa siku kadhaa zilizopita kulitokea tukio ambalo mimi nilihusishwa nalo.Ni tukio la ugomvi lililosababisha kifo cha msichana mmoja aitwaye Veronika.Mengi yameandikwa na kusemwa kuhusiana na tukio lile .Kwa kuwa suala hili liko mahakamani ninaomba niliongelee kwa ufupi sana.Ukweli halisi ni kwamba mimi na Patrick ni marafiki na wapenzi wa muda mrefu sana.Urafiki wetu ulianza toka tukiwa shuleni.Tulikutana,tukapendana na kuwa wapenzi.
Lilitokea tukio baya ambalo lilipelekea Patick kufungwa gerezani baada ya kusababisha kifo wakati akipambana na genge la wahuni waliokuwa wakitaka kunidhalilisha kijinsia.Wakati akiwa gerezani nilipata nafasi ya masomo nchini Marekani na hapo ndipo yalipotokea ya kutokea ambayo nisingependa kuyaongelea hapa na nikapotezana na Patrick kwa kipindi kirefu hadi tulipokutana tena hivi karibuni ambapo tulibaini kitu kilichotutenganisha .Naomba nikiri kwenu waandishiwa habari na watanzania kwamba mimi na Patrick tunapenda kwa dhati ya mioyo yetu na ndiyo maana hata baada ya kutengana kwa muda mrefu lakini bado tumejikuta tukiendelea kupendana zaidi na zaidi na hii ndiyo sababu iliyosababisha ugomvi uliopelekea kutokea haya yaliyotokea.” Happy akanyamaza kidogo akameza mate na kuendelea
“Kuhusika kwangu katika tukio hili kumeniathiri kwa kiasi kikubwa kisaikolojia mimi binafsi na kumelitia doa taji la miss Tanzania nililolivaa kwa sababu katika kila habari inayoandikwa kuhusiana na tukio hili inaandikwa kama Miss Tanzania na si kama Happy Kibaho.Familia yangu pia imekuwa na wakati mgumu sana toka tukio hili limetokea na ninawashukuru kwa sababu wamekuwa nami katika kila dakika na wamekuwa wakinipa ushirikiano mkubwa sana.” akanyamaza kidogo na kuendelea.
“Ndugu waadishi wa habari ,tukio hili lilinihusu mimi kama Happy Kibaho na si kama miss Tanzania.Kuendelea kuandika habari kwa kutumia kichwa cha miss Tanzania ,hakutendei haki taji hili kubwa la urembo hapa nchini,waandaji na kamati nzima ya miss Tanzania.Kwa hali hiyo nimekaa ,nikatafakari na familia yangu nikafikia maamuzi ambayo ninataka kuyaweka wazi kwa watanzania.” Happy akanyamaza akawatazama waandishi wa habari ambao walikuwa kimya wakimsikiliza.
“Baada ya tafakari nzito nimeamua kuchukua maamuzi magumu ili kuilinda heshima ya taji hili kubwa la miss Tanzania na tasnia nzima ya urembo hapa nchini.Nimeamua kulivua taji la miss Tanzania” Happy akanyamaza na kuwatazama waandishi wa habari ambao walionyesha mshangao mkubwa na minong’ono ikasikika kati yao.
“Ndugu zangu waandishi wa habari na watanzania ,najua mmestushwa sana na maamuzi haya hasa ikizingatiwa kwamba sina muda mrefu toka nimelivaa taji hili.Nimechukua maamuzi haya ili kuilinda heshima ya taji hili kubwa kabisa la urembo hapa nchini.Nawaomba watanzania wenzangu walioniamini na kuniona ninafaa kulibeba taji hili wanisamehe sana kwa kuwaangusha.Waliniamini sana na kunipatia taji hili na ndiyo maana kwa heshima yao nimeamua kulivua taji hili ili hata kama ni kuendelea kuandikwa basi niandikwe kama Happy Kibaho na si kama miss Tanzania.Asubuhi ya leo nimewasilisha barua ya kulivua taji langu kwa mkurugenzi mkuu wa Miss Tanzania na ninasubiri hatua itakayofuata.Ndugu zangu waandishi wa habari ni hilo tu ambao nimewaitieni hapa siku ya leo.” Akasema Happy na kisha mkurugenzi wake akachukua kipaza sauti.
“Ndugu zangu waandishi wa habari,nadhani nyote mmesikia alichokisema Happy.Hii ni taarifa ya kustusha mno na hata sisi kama kamati tumestushwa sana na taarifa hii.Kitu ninachotaka mkifahamu ni kwamba haya ni maamuzi binafsi ya Happy na sisi kama viongozi wake tutayaheshimu na kuyapa uzito unaostahili na baada ya kuyatafakari tutatoa taarifa kamili.Kwa kuwa bado tuko katika mstuko kutokana na maamuzi haya ya Happy ,nawaombeni ndugu zangu waandishi wa habari mkutano wetu uishie hapa siku ya leo.Hakutakuwa na maswali yoyote kwa Happy kwa sababu hayuko katika wakati mzuri wa kujibu swali lolote .Tumuache akapumzike na ninawaahidi kufanya tena mkutano mwingine na nitawaalikeni nyote na mtapata fursa ya kuuliza maswali mengi mtakavyo.” Akasema mkurugenzi wa miss Tanzania huku akisimama halafu Happy naye akasimama na kuondoka mle ukumbini kwa kupitia mlango wa nyuma kwa lengo la kukwepa kuonana na waandishi wa habari.
“mkurugenzi nashukuru sana .Tutazidi kuwasiliana” akasema Happy akimpa mkono mkurugenzi wake wa Miss Tanzania.
“Happy pole sana.Ninakuomba usihofu chochote ,leo hii hii tunaanza kulifanyia kazi suala lako na tutakutaarifu maamuzi ya kamati lakini nakuhakikishia kamba tutayaheshimu mawazo yako” akasema mkurugenzi
Happy akiongozana na baba yake pamoja na mdogo wake Margreth wakatembea kwa haraka kuelekea katika gari lao huku wakipigwa picha na waandishi wa habari .
“Thank you guys for your support” akasema Happy akiwaambia baba yake na Margreth wakati wakiondoka pale hotelini.
“ Uwepo wenu umenipa nguvu sana leo.”
“Happy sisi kama familia tutasimama pamoja nawe katika kipindi hiki kigumu na hatutakuacha hata sekunde moja.” Akasema mzee Raymond,Happy akatabasamu na kumgeukia mdogo ake aliyekuwa amekaa kiti cha nyuma
“Margreth ahsante sana kwa ushirikiano wako.”
“Usijali Happy.Siku zote tuko pamoja nawe .Ni jukumu letu kama familia kusimama pamoja nawe “Happy akainama chini akazama ghafla katika mawazo.
“Unawaza nini Happy? Akauliza mzee Raymond
“Bado kuna suala linaniumiza kichwa sana.Suala la kukutana na Mike linanitatiza ninashindwa namna nitakavyomtamkia kwamba mimi na yeye basi .Inauma sana baba Mike ananipenda kwa moyo wake wote.Naogopa sana kuumiza moyo wake” akasema Happy
“Happy my dear,usiogope.Nafahamu ugumu uliopo lakini hakuna njia nyingine ya kufanya,you have to do it.Unatakiwa uwe jasiri ili uweze kukabiliana na masuala mazito kama haya.Mweleze Mike ukweli wa moyo wako na ninakuhakikishia kwamba utakapomueleza utajisikia huru .Utaumia moyo lakini hii ni kwa faida yako mwenyewe kwa furaha ya moyo wako.Kumbuka hapa unaitafuta furaha ya maisha yako ambayo ni Patrick kwa hiyo usiogope hata kidogo kusimama imara katika suala lolote linalohusiana na mustakabali mzima wa maisha yako na Patrick.” akasema mzee Kibaho .
“Ahsante sana baba kwa kunipa moyo.” Akasema Happy kisha akachukua simu yake na kuzitafuta namba za simu atumiazo Mike akiwa Tanzania akapiga
“Hallo Happy unaendeleaje malaika wangu? Akasema Mike kwa furaha baada ya kupokea simu.
“Naendelea vizuri sana Mike.Tayari umeshafika hapo hotelini kama tulivyokubaliana?
“Ndiyo Happy.Nimekwisha fika muda mrefu ninakusubiri wewe mpenzi wangu.Nina hamu sana ya kuongea nawe” akasema Mike
“Niko njiani nakuja Mike.Naomba uendelee kunisubiri” akasema Happy na kukata simu akainama na kuvuta pumzi ndefu.
“Be strong Happy.You can do it” akasema mzee Kibaho
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 34
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT 0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Ahsante sana baba kwa kunipa moyo.” Akasema Happy kisha akachukua simu yake na kuzitafuta namba za simu atumiazo Mike akiwa Tanzania akapiga
“Hallo Happy unaendeleaje malaika wangu? Akasema Mike kwa furaha baada ya kupokea simu.
“Naendelea vizuri sana Mike.Tayari umeshafika hapo hotelini kama tulivyokubaliana?
“Ndiyo Happy.Nimekwisha fika muda mrefu ninakusubiri wewe mpenzi wangu.Nina hamu sana ya kuongea nawe” akasema Mike
“Niko njiani nakuja Mike.Naomba uendelee kunisubiri” akasema Happy na kukata simu akainama na kuvuta pumzi ndefu.
“Be strong Happy.You can do it” akasema mzee Kibaho

ENDELEA…………..

Saa saba na robo za mchana Happy na familia yake waliwasili Nady Villa Park moja kati ya hoteli maarufu jijini Dar es salaam.Wote watatu wakashuka garini na kuingia hotelini
“Usiogope Happy.Just be strong” akasema mzee Raymond akizidi kumpa moyo binti yake.Waliingia hotelini hadi katika meza aliyokuwa amekaa Mike wakasalimiana halafu Rayomond na Margreth wakaenda kuketi katika meza zilizokuwa nje ya hoteli na kuwaacha Happy na Mike peke yao
“Baba nina wasi wasi na Happy .Sijui kama ataweza kumweleza ukweli Mike” akasema Margreth.
“Usiwe na wasi wasi Margreth.Ninamfahamu Happy,she’s a strong woman.I know she can handle this” akasema mzee Kibaho huku akiyafuta macho yake baada ya kuvua miwani
“Sikutegemea kama siku moja Happy angeweza kuwa katika wakati mgumu kama huu alionao sasa hivi.Hata hivyo ninamshukuru sana huyo kijana Patrick kwa moyo wake wa upendo wa kuamua kuubeba yeye mzigo huu mzito alioustahili Happy.Ninaamini Patrick ana mapenzi ya dhati kwa Happy kwa sababu katika dunia ya sasa ni watu wachache sana wenye kuweza kufanya kitendo kama alichokifanya yeye. Na ndiyo maana ninaona kuna kila sababu ya kuwasaidia ili waweze kuwa pamoja.Patrick ni kijana sahihi kwa Happy.” akasema mzee Raymond.
“Baba ,Patrick na Happy wanapendana mno na hakuna mtu au kitu chochote zaidi ya kifo kitakachoweza kuwatenganisha.Mapenzi yao yalianza miaka mingi iliyopita na hata ilipotokea wakatenganishwa kwa uongo wa Vero ,hakuna aliyeweza kumsahau mwenzake.Nakumbuka Happy hakukaukiwa machozi kila siku akimlilia Patrick na ndiyo maana siku ile alipotwaa taji la mss Tanzania alipoteza fahamu baada ya kumuona Patrick” akasema Margreth.
“Hii ndiyo ilikuwa sababu ya Happy kupoteza fahamu siku ile?? Akauliza mzee Kibaho huku akishangaa.
“Ndiyo baba.Hii ndiyo sababu pekee ya Happy kupoteza fahamu siku ile.Mapenzi ya Patrick na Happy ni mazito sana na ndiyo maana haikumuwia ugumu Patrick kuubeba mzigo wote wa kesi aliyoistahili Happy.Ninachosikitika ni kwamba hata Mike anampenda sana Happy na ndiyo maana amesafiri kutoka marekani na kuja hapa kuungana naye katika matatizo.” Akasema Margreth.Mzee Kibaho akavuta pumzi ndefu na kusema
“Ni wakati mgumu sana kwa Happy lakini ni vyema kumuacha yeye mwenyewe afanye maamuzi yenye kufaa kwa mustakabali mzima wa maisha yake na tayari amekwisha amua kuwa na Patrick”
Ukimya mkubwa ulikuwa umetawala meza waliyokuwa wamekaa Mike na Happy.Ilionekana kana kamba walikuwa wakitegeana kuongea.Ni Mike ndiye aliyeanzisha maongezi.
“Happy nimefurahi sana kupata nafasi hii kukutana nawe leo hii kwa chakula cha mchana” akaanzisha mazungumzo Mike.Happy akajilazimisha kutabasamu na kusema
“Hata mimi nimefurahi sana Mike kwa kupata wasaa huu wa kukaa pamoja nawe.Ni muda mrefu umepita toka tulipokaa pamoja kama hivi.Nimekuwa nikitamani sana kuipata nafasi hii lakini toka ulipokuja nimekuwa nikikabiliwa na mfululizo wa matukio kiasi cha kushindwa kabisa kupata nafasi kama hii.Utanisamehe sana Mike” akasema Happy
“Happy kwanza kabisa napenda nikupe pole nyingi kwa matatizo na hongera nyingi kwa kushinda taji kubwa la urembo nchini.Haikuwa kazi rahisi kuwashinda warembo wote uliochuana nao.Hongera sana Happy.Michelle pamoja na wazazi wangu wanakupa hongera nyingi sana.” Akasema Mike
“Ahsante sana Mike”
“Vile vile nakupa pole sana kwa mfululizo wa matukio yaliyoambatana na ushindi wako huu.Nilipata taarifa kwamba ulipoteza fahamu ukumbini .Niliogopa sana ikanilazimu nifanye safari ya dharura kwani nilijua kwa nyakati kama hizi unanihitaji sana.Nimekuja ili niwe karibu nawe Happy kama mpenzi wako ,nikufariji na kukuonyesha upendo.” Akasema Mike
“Nashukuru sana Mike” Happy akajibu kwa ufupi
“Happy ni wajibu wangu kufanya hivi .Nina imani hata wewe ungefanya hivi endapo ungesikia kwamba kuna jambo limenitokea.Naamini ungekuja marekani mara moja” Akasema Mike na mara muhudumu akafika na kuanza kuandaa meza.Baada ya meza kuandaliwa wakaanza kula
“Pole sana kwa matatizo Happy.Ninaumia sana kila nikuonapo ukiwa katika mawazo mengi na machozi yasiyokauka.Ile sura yako ya kimalaika yenye tabasamu lisilofutika imetoweka ghafla.Happy ni kitu gani hasa kilichotokea na kupelekea uwe katika hali hii? Niko gizani sielewi nini kimekupata malaika wangu.Moyo wangu unaumia,natamani nifanye kitu kukurejesha katika hali yako ya kawaida lakini sielewi nianzie wapi.Happy mpenzi wangu naomba tafadhali unifahamishe nini hasa kimekusibu? Niko tayari kukusikiliza na niko tayari kwenda hadi mwisho wa dunia hii ili kuirejesha tena furaha ya maisha yako.” Akasema Mike.Happy akakiweka kijiko mezani halafu akamtazama Mike usoni
“Mike nashindwa nianzie wapi .Mambo mengi yametokea katika kipindi kifupi sana”
“Jitahidi Happy na unipe walau picha ya kilichotokea na kinachoendelea hivi sasa na kwa pamoja tutafute namna ya kuweza kuyatatua.” Akasema Mike.Happy akainama
“Help me Lord.This is so difficult but I have to do it” akawaza Happy halafu akainua kichwa.
“Mike matatizo yalianza usiku ule niliposhinda taji la miss Tanzania.Mara tu nilipotangazwa mshindi watu wengi walikuja kunipongeza kwa ushindi wangu lakini miongoni mwa waliokuja kunipongeza nilimuona mtu ambaye alinipelekea nikapatwa na mstuko na kupoteza fahamu” akasema Happy.
“Ulimuona mtu ambaye alikustua hadi ukapoteza fahamu? !!!! ..mtu wa namna gani huyo aliyekustua na kukusababishia matatizo haya makubwa? Was it a ghost? Akasema Mike na kumfanya Happy atabasamu kwa mbali.
“It wasn’t a ghost.I saw a human being” akasema Happy.Mike naye akaweka kijiko chake mezani na kuendelea kumtazama Happy.
“Mike I saw a person whom I believed he is dead” akasema Happy( Mike nilimuona mtu niliyeamini alikwishafariki)
“What ?!!!!..You saw a dead person? That’s a ghost Happy !! You saw a ghost” akasema Mike.(Nini ?!!!!..Ulimuona mtu aliyekwishafariki? Uo ni mzimu Happy)
“Mike sikuona mzimu.NIlimuona binadamu ambaye nilidhani kwamba amefariki miaka mingi iliyopita” Happy akasisitiza
“Ni nani huyo ambaye ulimuona?Hili ni jambo la kushangaza sana”
“I saw Patrick”(Nilimuona Patrick) akasema Happy .Sura ya Mike ikaonyesha mstuko wa dhahiri.Midomo ilikuwa inamtetemeka na kushindwa kuongea.Baada ya dakika moja Mike akasema
“Ulimuona Patrick!!! Ni Patrick yupi huyo uliyemuona Happy?
Happy akakohoa kidogo na kusema
“Kama utakumbuka kwamba niliwahi kuwa na mpenzi wangu ambaye alikuwa ni kila kitu kwangu na ambaye niliamini alifariki dunia akiwa gerezani.Huyo ndiye niliyemuona.” Akasema Happy na kuzidi kumchanganya Mike
“No ! Happy you must be mistaken.Patrick is dead and there is no way he can come back.What you saw must be a ghost” akasema Mike( Hapana ! Happy ulikosea.Patrick amekwishafariki na hakuna namna anayoweza kurejea.Ulichokiona ni mzimu)
“Mike,Patrick ni mzima hajafa na hakufa kama taarifa ile niliyoipata ilivyokuwa inasema.Ilikuwa ni taarifa ya uongo iliyoandikwa na mtu ambaye lengo lake lilikuwa ni kunitenganisha naye.Baada ya kurudi toka marekani nililazimika kutafuta mahala alipozikwa ili na mimi nikaweke shada la maua kama ishara ya upendo wangu kwake lakini taarifa nilizozipata toka katika magereza aliyokuwa amefungwa ni kwamba Patrick hakufariki akiwa gerezani bali alimaliza kifungo chake akiwa mzima wa afya.Hapo ndipo nilipoamini kwamba Patrick alikuwa mzima.Kwa bahati nzuri siku ile ya fainali alijitokeza mbele yangu.” Akasema Happy
“Happy bado siamini kama ni kweli hayo unayoniambia.Inawezekana akawa ni mtu ambaye amefanana na Patrick na anataka kukudanganya kwamba yeye ni Patrick.” Akasema Mike kwa sauti ya juu.Happy akaendelea kumtazama .Mike akachukua glasi ya mvinyo akagugumia mvinyo wote na kusema
“Happy my love nakuomba utulize mawazo .Achana kabisa na huyo mtu anayejiita yeye ni Patrick.Patrick halisi alikwisha kufa na hatarudi tena duniani.”
“Mike naomba uniamini kwamba mtu nilimuona
Patrick halisi na nilifanikiwa kuonana naye,nikaongea naye”
“What !! ..Mike akashtuka
“Nilikutana na Patrick na nikathibitisha kwamba ni yeye kweli na si mzimu wake”
“Ulikutana naye wapi? Mliongea nini? Mike akauliza maswali mfululizo
“Siwezi kukwambia kila kitu kwamba nilikutana naye vipi na wapi lakini naomba ufahamu kwamba nilikutana naye na ni mzima na hakufa kama ilivyokuwa imedaiwa”
“Jesus Christ !!!!!!....” akasema Mike huku mikono yake akiwa ameikunja na kuiweka kifuani
“Happy una hakika kweli kwamba mtu uliyeonana naye ni Patrick? Mike akauliza tena
“Ndiyo Mike.Mtu niliyeonana naye ni Patrick” akajibu Happy halafu kikapita kimya kifupi.
“Huyo mtu aliyekuandikia ujumbe ule kwamba Patrick amefariki dunia ni nani? Umekwisha mfahamu?
“Ndiyo Mike,tumekwisha mjua mtu huyo.Ni Vero ambaye alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Patrick”
“Ouh Gosh !! ..where is she? She’s a monster..Anatakiwa akamatwe akashtakiwe kwa kosa alilolifanya ambalo lingeweza kupelekea hata kupoteza uhai wa mtu.Nilikuwepo wakati ule ulipopata taarifa hizi za kifo cha Patrick na niliyashuhudia mateso uliyoyapata.That woman must pay.Show me where she is and I can make her pay” akasema Mike kwa ukali
“There is no need Mike..She’s gone now.She’s dead” akasema Happy na Mike akashusha pumzi kikapita kimya kifupi Happy akasema
“Mike ni kweli kwamba nilipata mateso makubwa sana wakati ule nilipopata taarifa za kifo cha Patrick,wewe ulikuwepo na uliyashuhudia mateso niliyoyapata.Ni wewe na Michelle mliokuwa wafariji wangu.Mateso yote yale yalitokana na upendo wangu mkubwa kwa Patrick na ndiyo maana kuna nyakati sikuona hata faida ya kuendelea kuishi tena duniani kwa sababu sikuamini kama kuna maisha bila ya Patrick.” Happy akanyamaza akamtazama Mike ambaye uso wake ulianza kuloa jasho
“Its hard but I have to do it” akawaza Happy
“Mike naomba niwe wazi kwako kwamba baada tu ya kukutana na Patrick kumbu kumbu zangu zote za nyuma zimerudi ghafla .Understad that I’m a human being and sometimes I’m weak.” Akasema Happy
“Whats that suppose to mean Happy ? (Hiyo inamaanisha nini Happy? akauliza Mike kwa wasi wasi huku akimtazama Happy usoni
“Mike I’m so sorry to tell you this but me and Patrick we’re back together” ( Mike samahani kwa kukueleza hili lakini mimi na Patrick tumerejesha mahusiano yetu)
Mike akastuka mno kwa maneno yale .
“Happy sijakusikia vizuri umesema nini? !!
“Nimesema kwamba mimi na Patrick tumerejesha mahusiano yetu ya awali” akasema Happy.Mike akaonekana kuchanganyikiwa ghafla
“Happy !!!..bado siamini..Kwa nini umefanya hivi? Kwa nini umenifanyia hivi? Siamini Happy kama ni wewe kweli ambaye unaweza ukanifanyia mambo haya.How can you do that to me????!!!!.. Mike aliongea kwa masikitiko makubwa sana na macho yake yalilengwa na machozi.
“Happy naamini unanitania na si kweli hayo unayoniambia..Huwezi kunifanyia hivi Happy.Ninakufahamu vizuri hauwezi kufanya kitu kama hicho.Ninakupenda zaidi ya nafsi yangu Happy tafadhali naomba uniambie kwamba unanitania” akasema Mike huku machozi yakianza kumtoka katika macho yake.
“Mike mimi ni binadamu na ninahitaji moyo wangu uwe na furaha siku zote.Mike nafahamu unanipenda tena kwa moyo wako wote na hata mimi ninakupenda vile vile.Umekuwa na mimi kwa kipindi kirefu sasa.Umenijali na kunionyesha mapenzi ya hali ya juu sana.Siku zote niliamini kwamba baada ya Patrick kufariki wewe ndiye mwanaume wa maisha yangu lakini baada ya kukutana na Patrick tena nimejikuta nikiwa dhaifu kwake.Patrick ndiye alikuwa mwanaume wangu wa kwanza kumpenda na kumkabidhi moyo wangu na ndiyo maana hadi leo hii sijaweza kumtoa moyoni mwangu.Mike naomba ufahamu kwamba si rahisi kufanya mamuzi magumu kama haya hasa kwa mtu anayekupenda lakini nimeamua kuusikia na kuufuata moyo wangu unavyonituma.Moyo wangu unamtaka Patrick.Mike this is for the best of me.Naomba Mike kama unanipenda na unanitaka niwe na furaha naomba unielewe na uniruhusu niwe na Patrick” akasema Happy.
“ No ! No ! No Happy you cant do this to me.Huwezi kuniacha kamwe Happy.Ninakupenda na wewe ni wangu peke yangu.Sintakubali kamwe mtu yeyote Yule anitenganishe na wewe.” Akasema Mike huku akiinuka na kumshika Happy mikono.
“Mike ..!!” Happy akataka kusema jambo lakini Mike akamzuia
“Happy naomba naomba usiseme chochote kwa sababu kila neno utakaloendelea kuliongea hapa linazidi kuniumiza.Mimi na wewe kamwe hatutaweza kuachana” akasema Mike huku akiwa ameing’ang’ania mikono ya Happy.
“Mike naomba utulie na unisikilize “ akaomba Happy
“Happy nitakusikilizza kama una jambo lingine la kuniambia lakini si kuachana na mimi.Ninakupenda Happy ,wewe ni zaidi ya maisha yangu.Sikutegemea hata siku moja kama ungenitamkia maneno kama haya.” Akasema Mike.
“Baada ya miaka hii yote ya kuwa pamoja na kufikia hatua ya kukuvalisha pete ya uchumba iweje leo Happy uamue kuniacha ? You want to leave me just because of a man who rose from death? No Happy !! That wont happen.You cant leave me because of good for nothing ghost” (Unataka kuniacha kwa sababu ya mtu aliyeibuka toka kifoni? Hapana Happy !! hilo haliwezi kutokea.Huwezi kuniacha kwa sababu ya mzimu “ akasema Mike kwa ukali.Maneno yale yalimchoma sana Happy akasimama kwa hasira.
“Mike naomba iwe ni mara ya kwanza na ya mwisho kutoa maneno machafu na ya kejeli kwa Patrick.Yeye ndiye aliyeushika moyo wangu na sintakubali mtu yeyote Yule atoe matamshi ya kumkosea heshima.Kama unanipenda nadhani utakuwa unaijali pia furaha ya moyo wangu ambayo ninaipata nikiwa na Patrick.” Akasema Happy kwa ukali.Mike naye akasimama kwa jazba
“You are selfish Happy.You never thought about me at all.What about my happiness? You are my happiness.How could you be so cruel? ( Wewe ni mbinafsi Happy.Hufikiri kabisa kuhusu mimi.Vipi kuhusu furaha yangu na mimi? Wewe ndiye furaha yangu.Mbona unakuwa mkatili hivyo? Akafoka Mike.
“Mike naomba unielewe kwamba moyo wangu umefanya maamuzi magumu sana ya kuamua kuuvunja uhusiano wetu ambao umedumu kwa muda mrefu.Naomba unisamehe sana Mike kwani sintaweza kuyabadili maamuzi yangu .I’m sorry Mike that we have to end up this way.Nitakurejeshea gharama zote ulizotumia katika safari yako ya kuja Tanzania.” Akasema Happy
“Utanirudishia pesa lakini vipi kuhusu moyo wangu ambao hauwezi kuishi bila ya wewe? Hakuna pesa inayoweza kufikia thamani ya penzi langu kwako.Sihitaji pesa au kitu kingine chochote kile.Nakuhitaji wewe tu.My life is nothing without you.” Akasema Mike
“Mike ,please don’t make this too hard for me.Nina matatizo makubwa kwa sasa na ninaomba tafadhali usilifanye suala hili likawa tatizo.Kama kweli unanipenda Mike naomba uniruhusu nifanye kila ninachokihitaji kwa moyo wangu.Ninampenda Patrick na ninamuhitaji katika maisha yangu.Mimi na wewe tutaendelea kuwa marafiki” Akasema Happy
“Happy sitaki kuwa rafiki yako.Nataka kuwa mwanaume wa maisha yako.Tafadhali niambie ni kitu gani umekikosa toka kwangu? Kuna jambo lolote baya nimewahi kukufanyia? Au niambie nikufanyie kitu gani ili uwe na furaha na uendelee kuwa na mimi? Niambie Happy niko tayari kufanya chochote kile kwa ajili yako.” Akasema Mike.Happy machozi yalikuwa yanamtoka.Alikuwa na wakati mgumu sana.
“Mike umenipa kila kitu nilichokihitaji katika maisha yangu.Umekuwa pembeni yangu na kusimama pamoja nami hata katika nyakati zile ngumu kabisa.Thamani yako kwangu na katika maisha yangu ni kubwa sana lakini pamoja na hayo Mike naomba uniamini kwamba Patrick ndiyo furaha yangu.Ndiye maisha yangu ,ndiye kila kitu kwangu.” Akasema Happy.Mike akamtazama kwa macho ya huruma .
“Sasa ndiyo natambua kwamba kwa muda huu wote umekuwa ukinidanganya kwamba unanipenda kumbe hukuwa na hata chembe ya upendo kwangu.Ulinidanganya.Nilikuwa kipofu,nilipofushwa na uzuri wako wa tausi kumbe ndani ni kahaba na shetani usiye na hata chembe ya huruma.Hakukuw……” kabla hajamaliza sentensi yake Happy akamnasa kibao kikali
“Naomba usirudie tena kutamka maneno hayo uliyoyatamka.Usinifananishe mimi na shetani au kuniita kahaba.Nilikupenda Mike na nilikuwa tayari kuwa nawe katika maisha yangu yote na wala sijawahi kukudanganya hata mara moja.” Akasema Mike na mara Mike akagonga meza kwa hasira
“You lied to me Happy all this long and all its because of this stupid ghost.” Mike akaongea kwa sauti kubwa .Macho yake yalikuwa yamebadilika na kuwa mekundu.Alikuwa na hasira zisizomithilika.Wateja waliokuwa wakiendelea kupata chakula katika meza za pembeni wakageuza vichwa vyao kuangalia kilichokuwa kinaendelea kati ya Mike na Happy.
Happy naye alipandwa na hasira baada ya maneno yale ya kejeli toka kwa Mike.Machozi yalikuwa yanamtoka.Taratibu akatoa katika mkoba wake pete ya uchumba aliyovishwa na Mike na kuiweka mezani.
“Mike nakurudishia pete yako ya uchumba uliyonivisha.Ahsante sana kwa yote.Utanisamehe kwa maamuzi haya magumu.This is for the best of me” akasema Happy na kuchukua mkoba wake.Mike akamshika mkono akamzuia asiondoke.
“Huwezi kwenda Happy.Huwezi kuondoka na kuniacha hapa.You’ll never leave me Happy.You’ll always be mine” akasema Mike
“Mike let me go !!!!....” Akasema Happy kwa sauti huku akiuvuta kwa nguvu mkono wake ili kujinasua toka katika mikono ya Mike. Alitumia nguvu nyingi kujivuta na kujinasua toka katika mikono ya mike na kumpelekea kukosa mhimili akaangukia meza ya jirani na kumwaga vinywaji.Watu wote mle hotelini wakasimama kuangalia kilichokuwa kinaendelea.Happy akasimama na kwa haraka wahudumu wa hoteli wakafika na kumshika Mike.Happy akatoka kwa kasi huku akilia.Mzee Raymond na Margreth walistuka sana baada ya kumuona Happy anatoka mle hotelini huku analia.Kwa haraka wakamfuata
“Happy kumetokea nini? Mike amekupiga? Akauliza mzee Raymond.Happy hakujibu kitu akaendelea kulia.Baba yake akamshika mkono na kumuongoza hadi katika gari.
“Nyamaza kulia Happy.” Akasema mzee Kibaho.Happy akanyamaza kulia akafuta machozi.
“Tuondoke dady” akasema Happy
Mzee Raymond akawasha gari na kuondoka pale hotelini.
“Nini kimetokea mle hotelini? Ulifanikiwa kumweleza Mike ukweli? akauliza mzee Raymond baada ya kusimama katika foleni.
“I did it dady.Its over now” akasema Happy.Baba yake akamuangalia na kusema
“Pole sana Happy.Najua haikuwa kazi rahisi lakini umeweza kuifanya.Endelea kuwa na ujasiri huo katika kuipigania furaha ya moyo wako.Wakati mwingine tunapoitafuta furaha ya mioyo yetu inatulazimu kuchukua maamuzi magumu kama uliyoyachukua na siku zote katika maamuzi magumu lazima wawepo watu watakaoathiriwa na maamuzi hayo.Mike alikuelewa? Amekubali kwa moyo mmoja muachane?” Akasema mzee Raymond.
“It was painful dady.So painful.Sikutegemea kumuumiza Mike kiasi kile.He loves me so much .” Happy akashindwa kujizuia akaanza kulia.
“Nyamaza kulia Happy.Its over now.Yes its painfull but you did the right thing.Hupaswi kulia kabisa kama moyoni mwako una nia ya dhati na Patrick ambaye naye alifanya kama ulivyofanya wewe na kupelekea mwenzake kupoteza maisha.Mnapita katika kipindi kigumu sana lakini haya yote yana mwisho na yatakwisha tu” akasema mzee Raymond.
“Happy ,kama anavyosema baba ,vumilia katika kipindi hiki kigumu cha mpito na mambo haya yatakwisha tu.” Akasema Margreth ambaye muda mwingi alikuwa kimya
“Margreth najitahidi sana kuvumilia lakini kuna nyakati najikuta nikishidwa kuvumilia hasa kila nikikumbuka ugumu uliopo mbele yetu.Hata hivyo I’m still strong “ akasema Happy.Magari yaliyokuwa yamesimama katika foleni yakaanza kwenda safari ikaendelea.walifika nyumbani Happy akaomba aachwe peke yake akajifungia chumbani kwake
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 35
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Nyamaza kulia Happy.Its over now.Yes its painfull but you did the right thing.Hupaswi kulia kabisa kama moyoni mwako una nia ya dhati na Patrick ambaye naye alifanya kama ulivyofanya wewe na kupelekea mwenzake kupoteza maisha.Mnapita katika kipindi kigumu sana lakini haya yote yana mwisho na yatakwisha tu” akasema mzee Raymond.
“Happy ,kama anavyosema baba ,vumilia katika kipindi hiki kigumu cha mpito na mambo haya yatakwisha tu.” Akasema Margreth ambaye muda mwingi alikuwa kimya
“Margreth najitahidi sana kuvumilia lakini kuna nyakati najikuta nikishidwa kuvumilia hasa kila nikikumbuka ugumu uliopo mbele yetu.Hata hivyo I’m still strong “ akasema Happy.Magari yaliyokuwa yamesimama katika foleni yakaanza kwenda safari ikaendelea.walifika nyumbani Happy akaomba aachwe peke yake akajifungia chumbani kwake.

ENDELEA………….

Mike alicharuka na kuanza kupambana na wahudumu wa hoteli akiwataka wamuachie ili amfuate mchumba wake Happy.Walinzi wa hoteli wakafika haraka baada ya vurugu kuwa kubwa na kumkamata Mike ambaye alikuwa katika hali ya kuchanganyikiwa kwani alikuwa anaongea mfululizo maneno yasiyoeleweka.
Ili asiendelee kuwabugudhi wateja wengine waliokuwa wakijipatia mlo,Mike akapelekwa hadi katika chumba kimojawapo cha hoteli ile kwa lengo la kumpumzisha.Jasho jingi lilikuwa linamtoka hali iliyowafanya viongozi wa hoteli wamuite daktari haraka ili amfanyie uchunguzi Mike kuona kama ana tatizo lolote baya.
Daktari alifika haraka na kumpima Mike lakini hakukuwa na tatizo lolote la kiafya, akapendekeza ingekuwa vyema kama angendelea kupatiwa mapumziko kwani tatizo alilokuwa nalo lilionekana ni hasira za kupita kiasi.Mike aliendelea kuwa mbishi na hakutaka kuendelea kukaa pale hotelini.Akaomba apatiwe hesabu ya hasara iliyopatikana kwa vyombo mbali mbali kuvunjika wakati wa vurugu ile ili alipe.Baada ya kulipa,Mike akaruhusiwa kuondoka.Aliingia katika gari lake akakaa kama dakika mbili hivi akitafakari halafu akaliwasha na kuondoka kwa kasi.
“ Sikutegemea hata kidogo kama Happy angeweza kunifanyia kitu cha namna hii.Mpaka hivi sasa ninaona ni kama ndoto na si kitu cha kweli.Happy huyu niliyemfahamu na kumpenda kwa moyo wangu wote leo amenifanyia kitu cha namna hii??!!!!!..baso siamini.Pengine baada ya akili yangu kukaa na kutulia nitapata jibu nini cha kufanya.Pengine labda alikuwa ananitania ili kunipima kama nina mapenzi ya kweli kwake.” Akawaza Mike
“ Kwa nini Happy amekuwa mkatili namna hii? Kwa nini amesahau ni namna gani ninampenda .Kwa miaka hii yote niliyokuwa naye,nimemuonyesha mapenzi ya kiwango cha juu sana nikitazamia kwamba yeye ndiye mwanamke wa maisha yangu lakini kumbe nilikuwa najidanganya.Inaniuma sana….” Akawaza Mike huku akiendesha gari lake na mara kikasikika kishindo na gari lake likasimama ghafla.Akastuka kama mtu aliyekuwa usingizini na kuangalia kilichokuwa kimetokea.Ilikuwa ni ajali.Alikuwa ameligonga kwa nyuma gari lililokuwa mbele yake.
“ Ouh my God ….!!!!!!..” akasema Mike akiwa hajui la kufanya.Watu tayari walikwisha fika kwa wingi katika eneo la tukio ili kuishuhudia ajali ile.Bado Mike alikuwa garini na hakuthubutu kushuka.Alikuwa amechanganyikiwa na mikono yake ilikuwa inamtetemeka.
Askari wa kikosi cha usalama barabarani waliokuwepo karibu na eneo lile wakafika mara moja.Jamaa aliyegongewa gari lake na Mike akatoa maelezo ya namna ajali ile ilivyotokea halafu mmoja wa polisi akamfuata Mike katika gari lake na kugonga katika kioo akamtaka afungue mlango na ashuke garini.Bado Mike aligoma kushuka garini hali iliyomlazimu askari Yule kugonga kwa nguvu zaidi ili kumstua Mike aliyekuwa ameinamia usukani.
Ghafla kikatokea kitendo ambacho kiliwashangaza watu wote waliokuwepo eneo la tukio.Mike alifungua mlango akashuka akiwa na hasira kama mbogo na kuanza kumvurumishia makonde askari Yule wa usalama barabarani.Iliwalazimu raia waliokuwa wamesimama pembeni kuingilia kati na kumdhibiti Mike asiendelee kufanya kitendo kile .Mike akawekwa chini ya ulinzi.Akili yake haikuwa sawa sawa na hakujua alichokuwa anakifanya.Askari polisi waliokuwa doria walitaarifiwa kuhusu tukio lile na wakafika mara moja.Jitihada za kumuhoji Mike zikashindikana baada ya kushindwa kutoa ushirikiano.Kila alichoulizwa hakuwa tayari kujibu.Polisi wakalazimika kumpakia katika gari lao na kuondoka naye kuelekea kituoni.
Baada ya masaa mawili Mike alitulia na kurejea katika hali ya kawaida na hivyo kuwapa polisi fursa ya kumuhoji na ndipo walipogundua kwamba Mike alikuwa ni raia wa Marekani hivyo wakapiga simu katika ubalozi wa marekani ambao walikiri kumfahamu Mike na wakafika pale kituoni mara moja ili kutafuta namna ya kuweza kulimaliza suala lile lililokuwa linamkabili.

* * *

Kikao cha mwisho cha maandalizi ya mazishi ya Veronika kilikuwa kinaendelea nyumbani kwao.Wakati wakiendelea na upangaji wa ratiba nzima ya mazishi ,akaingia mmoja kati ya ndugu na kumuita Sarah pembeni.
“Sarah kuna wageni wamekuja wamesema kwamba wametoka kwa akina Patrick wamekuja kutoa pole,wanahitaji kukuona”
Sarah akamfuata dada yake Loniki aliyekuwa anamuangalia kwa jicho kali akamvuta pembeni.
“Loniki kuna ujumbe wa watu umekuja toka kwa akina Patrick wamekuja kutoa pole” akasema Sarah na mara sura ya Loniki ikabadilika ghafla.
“Wako wapi? Akauliza Loniki kwa ukali
“Sikiliza Loniki,hakuna sababu ya kukasirika kwa ujio wa watu hawa.Wamekuja kwa nia njema ya kuungana nasi katika wakati huu mgumu kwani tayari wao na sisi tulikwisha kuwa kama ndugu.Kukataa kuwapokea au kuwatendea kitendo chochote kile kisichokuwa cha kistaarabu kutajenga picha ambayo si nzuri na inaweza ikawa ni mwanzo wa chuki na uhasama baina yetu.Hata wao pia wameumizwa na kilichotokea kwani nao pia wamempoteza mzee wao.”
“Sarah sikuelewi kabisa ni kwa nini umekuwa ukimtetea sana Patrick na familia yake? Hutaki kabisa kusikia lolote likiongelewa kuhusiana na Patrick.Inaonekana hujaguswa kabisa na kifo cha Vero” akasema Loniki kwa ukali
“Loniki unakosea unaposema kwamba sijaguswa na kifo cha Vero.Nimeguswa sana lakini sioni sababu yoyote ya kumchukia Patrick au familia yake.Ni kweli amesababisha kifo cha mdogo wetu lakini tayari anashikiliwa na vyombo vya dola ili haki itendeke.Kwa kuwa tunasubiri maamuzi ya vyombo vyenye kutoa haki hatuna sababu ya kuendeleza chuki na uhasama baina ya familia zetu kwani hazitatusaidia kitu na hata tukichukiana hatutaweza kuwarejeshea watu wetu waliopoteza uhai” akasema Sarah
Loniki akaonekana kuchukizwa na kauli ile ya Sarah .Hakutaka tena kuendelea na maongezi akamfuata shangazi yake.
“Shangazi wako wapi wageni waliotoka kwa akina Patrick?
Shangazi yake ambaye amekuwa akikubaliana na kila anachokisema Loniki akamuongoza hadi nje walikokuwa wamekaa wajumbe toka kwa akina Patrick.Walikuwepo wanaume watatu na wanawake watatu na wote alikuwa wanaongozwa na Andrew rafiki mkubwa wa Patrick
“Wageni ni hawa hapa” akasema shangazi yake Loniki.
“Habari zenu? Loniki akawasalmu akina Andrew huku akiwaangalia kwa jicho la chuki
“Habari zetu nzuri ,poleni sana” wakajibu
“Tumekwisha poa” akajibu Loniki halafu kikapita kimya cha sekunde kadhaa akasema.
“Ninyi ndio mliotoka kwa akina Patrick? i
“Ndiyo sisi” akajibu mmoja wa wazee
“Tunashukuru mmefika lakini kwa bahati mbaya hatuhitaji mtu au muwakilishi yeyote toka katika familia ile.Uhusiano baina yetu na ninyi ulikwisha pale mtoto wenu alipomuua ndugu yetu kwa makusudi.Naombeni mkawaambie kwamba hatuna haja na pole zenu na wala hatuhitaji kufarijiwa nanyi.Tuacheni na msiba wetu” akasema Loniki.Kila mtu alibaki amepigwa na butwaa
“Sikiliza dada” akasema Andrew
“Tumekuja hapa kwa lengo zuri la kuungana nanyi katika msiba.Hata sisi tumeguswa na kuumia kama mlivyoumia ninyi.Tunaomba tafadhali mtupokee na mzipokee salamu zetu za pole.” akasema Andrew
“Hatuhitaji salamu zenu za pole.Mmetuulia mwanetu tuacheni tulie wenyewe,Nendeni nanyi mkalie na mzee wenu” akasema Loniki
“Bado mnaendelea kushangaa hapa? Nimesema ondokeni hatuwataki hapa msibani.” Akasema Loniki kwa ukali na mara akatokea Sarah
“Andrew nawashukuru sana kwa kufika kwenu ,lakini nawaomba tu muondoke ili kuepusha matatizo.Loniki bado ana hasira nyingi ,nadhani baada ya shughuli za mazishi kuna ulazima wa kukaa na kuliangalia sula hili kwa undani ili lisije likaleta uhasama baina ya familia zetu.Samahani sana jamani.” Akasema Sarah
“Ahsante sana Sarah.Tumekuelewa ,tunaondoka lakini naomba umfahamishe dada yako kwamba kitendo alichokifanya si cha kiungwana hata kidogo” akasema Andrew halafu wakapanda gari na kuondoka.
“Sarah unaonekana kifo cha Vero hakuijakuumiza kabisa.Umenisikitisha mno .Naumia kila wakati unapochagua kukaa upande wa akina Patrick.Who’s Patrick to you? Loniki akamwambia Sarah kwa ukali baada ya akina Andrew kuondoka.Sarah akaonekana kukerwa sana na maneno yale ya dada yake.
“Loniki naomba ufahamu kwamba sisi sote tulimpenda sana Vero na tuna uchungu mkubwa kwa kifo chake.Usitake uonekane kwamba una uchungu zaidi kupita watu wote hapa.Kitendo ulichokifanya si cha kiungwana hata kidogo.Watu wale wamekuja kwa nia njema tu ya kuungana nasi katika msiba lakini umewatimua bila sababu ya msingi.Mimi sintakubaliana hata kidogo na mambo kama haya ya kuendeleza chuki na uhasama baina yetu.”
“Sarah mimi na wewe tutaongea baada ya kumalizika kwa msiba” akasema Loniki na kuondoka akiwa amefura kwa hasira.
“Kama tusipokuwa makini tunaweza kujikuta tukiwa katika uadui mkubwa baina ya familia zetu.Hata kama tukiwachukia familia ya Patrick lakini hii haitatusaidia kumrejesha Vero.Nitapambana na Loniki katika suala hili na wala sintamuogopa kwa sababu endapo tutamuacha afanye anavyotaka kufanya anaweza akatupeleka mahala tusikotaka kwenda.” Akawaza Sarah
Baada ya kuachana na Sarah ,Loniki akaenda moja kwa moja hadi katika chumba alichokuwamo mama yake.
“Mama kuna watu wamekuja toka katika familia ya akina Patrick wanasema eti wamekuja kutupa pole.”
“Wako wapi ? Mmewakaribisha?
“Mimi nimewafukuza”
“Umefanya vizuri sana Loniki.” Akasema mama yake kwa sauti ndogo.Sauti yake ilikuwa inakwama kwama kutokana na kulia kwa muda mrefu.
“Mtoto wao amenisababishia kidonda ambacho hakitapona kamwe.Nilimpenda sana Vero na siku zote nilimtunza na kumlinda kama mboni ya jicho langu.Vero alikuwa ni mshauri wangu,furaha yangu,alikuwa ni kila kitu kwangu na sikutegemea kama angeondoka mapema namna hii .Ninamchukia sana yule kijana.Ameyafanya maisha yangu yote yaliyobaki hapa duniani yawe magumu na ya mateso makubwa.Nitamchukia hadi siku ninaingia kaburini na sitaki hata kuiona familia yake,Umefanya vizuri kuwatimua” akasema mama yake Loniki.
“Basi mama imetosha usiwaze sana ,nakuahidi Patrick lazima atalipa uovu wake.Siku hizi malipo ni hapa hapa duniani.Mtenda ubaya hulipwa kwa ubaya.” Akasema Loniki na kumkumbatia mama yake.
Andrew pamoja na ujumbe wote uliotumwa kupeleka salamu za pole kwa akina Vero walirejea nyumbani kwa wazazi wa Patrick kulikokuwa na umati mkubwa wa watu.Baada tu ya kushuka garini Andrew akamfuata Alois
“Mbona mmerejea mapema namna hii? Akauliza Alois
“Mambo yamekwenda tofauti kabisa na matarajio yetu”
“Nini kimetokea?
“Tumefukuzwa”
“Mmefukuzwa ?!!..” akauliza Alois
“Ndiyo Alois ,tumefukuzwa na dada mkubwa wa Vero.Amesema hataki kumuona mtu yeyote anayehusiana na Patrick katika msiba wa mdogo wake.Namshukuru sana Sarah kwa sababu ndiye aliyetokea na kutuomba tuondoke ili kuepusha shari kwa sababu Yule dada yake alikuwa tayari kufanya lolote ili kutuondoa pale.” Taarifa ile ilimstua sana Alois akasimama na kushika kiuno.
“Dah !! haya mambo yanazidi kuchukua sura mpa kila siku.Lakini nilitegemea jambo kama hili lingeweza kutokea.Poleni sana.Tuendeleeni na taratibu za kushughulikia msiba wa baba na tusiumize vichwa vyetu kwa yaliyotokea huko kwa akina Vero.” Akasema Alois

* * *

Saa ya ukutani ilionyesha ilikwisha timu saa mbili za usiku.Margreth alikuwa ameketi sebuleni akisubiri kutazama taarifa ya habari.Pamoja naye alikuwepo baba yake mzee Raymond Kibaho na mama yake. Happy alikuwa amejifungia chumbani kwake.
“Mtu mmoja afikishwa kituo cha polisi kwa tuhuma za kumshambulia askari wa usalama barabarani” Hii ilikuwa ni moja ya taarifa zilizokuwemo katika muhtasari wa habari.Margreth akastuka mno baada ya kuitazama habari ile.
“Mike..!!!! Baba ni Mike..Ouh My God !!!!” akapiga kelele Margreth.Mzee Raymond naye alistuka baada ya kuiona picha ya Mike akiwa anashushwa katika gari la polisi.Kwa haraka Margreth akainuka pale sofani na kukimbia kuelekea chumbani kwa Happy
“Happy twende ukamuone Mike.” Akasema Margreth
“Mike kafanya nini? Akauliza Happy kwa wasi wasi
“Amefikishwa kituo cha polisi” akasema Margreth
“Ouh My God !!!! akasema Happy huku akiinuka kitandani na kukimbia kuelekea sebuleni
“Mtu mmoja ambaye ni raia wa Marekani amefikishwa katika kituo cha polisi kwa kosa la kumshambulia na kumjeruhi askari wa kikosi cha usalama barabarani.” Ilisema taarifa ile na kuendelea
“Mtu huyo aliyefahamika kama Mike Cambell ambaye ni raia wa Marekani ,alitenda kosa hilo baada ya kusababisha ajali na alipotaka kuhojiwa na askari huyo wa usalama barabarani alimvamia na kuanza kumshambulia.” Wakati taarifa ile ikiendelea kusomwa,picha zilikuwa zinamuonyesha Mike akishushwa toka katika gari la polisi na kuingizwa kituoni.
“Mungu wangu.!! Yote haya yamesababishwa na mimi” akasema Happy na kuondoka kwa kasi kurejea chumbani kwake.Macho yake yalijaa machozi.Margreth akainuka na kutaka kumfuata lakini baba yake akamzuia.
“Let her cry all out..Let her be alone for now” akasema mzee Kibaho.
“Namuonea huruma Happy ana wakati mgumu sana” akasema Margreth
“Naomba ufahamu Margreth kwamba furaha ya maisha siku zote ina gharama zake.Happy anaipigania furaha ya maisha yake kwa hiyo anapaswa kuwa na ujasiri wa hali ya juu sana.Kwa sasa muache aendelee kulia na atakapoamka asubuhi atakuwa katika hali nzuri” akasema mzee Kibaho
“Baba nina wasi wasi anaweza hata akajidhuru.mambo yaliyoko kichwani kwake kwa sasa ni mengi “
“Hapana Margreth,Happy hawezi kufanya jambo kama hilo la kipuuzi.Anampenda Patrick kwa hiyo hawezi katu kufanya kitu kama hicho.”
Baada ya kuingia chumbani Happy alijitupa kitandani na kuanza kulia.
“Ouh Mungu wangu mambo haya yatakwisha lini? Nini itakuwa hatima ya mambo haya? Kila uchao kuna jambo jipya linaibuka.Ni kwa sababu ya suala hili tumekwishawapoteza watu wawili hadi hivi sasa na bado hatujui nini kitakachokuja mbele yetu.Leo Mike amekamatwa kwa kumshambulia polisi.Kesho kitatokea kitu gani?Najua Mike alifanya kitendo kile kutokana na hasira alizokuwa nazo baada ya kusitisha uhusiano baina yetu.Hakutegemea kama siku moja mimi naye tungefika mwisho.” Akawaza Happy huku akiendelea kulia.
“Sikuwahi kuota kama siku moja ningekuwa katika wakati huu mgumu.Sikutegemea kama siku moja ningeua mtu.Ouh My God please forgive me..This is getting too much for me.Naona kama akili yangu haifanyi kazi tena.Naona kama uwezo wake wa kufikiri umefika mwisho.I’m confused and I don’t know what to do any more.” akawaza Happy halafu akatoka na kuelekea jikoni akamkuta Pendo mfanyakazi wao wa ndani akiendelea na shughuli zake za usafi.
“Pendo baba huwa anaweka wapi chupa zake za pombe? Akauliza Happy huku akiyafungua makabati ya jikoni.
“Huwa zinakaa kule katika chumba cha kulia chakula” akasema Pendo, Happy akatoka kwa haraka akaeleka katika ukumbi wa chakula akalifungua kabati kubwa na kutoa chupa ya mvinyo akaenda nayo chumbani kwake.Hali aliyokuwa nayo Happy ilimstua sana Pendo hakuwahi kumuona hata siku moja akiwa katika hali ile na hakuwahi kumuona Happy akinywa pombe kali.Aliogopa sana akaacha kazi zote alizokuwa anafanya na kuelekea sebuleni.
“Pendo kuna nini ? Mbona umekuja kwa kasi namna hiyo? Akauliza mzee Raymond.
“Baba ni dada Happy” akasema Pendo akiwa na wasi wasi.
“Happy kafanya nini?
“Amekuja jikoni akiwa analia akachukua chupa moja ya pombe na kwenda nayo chumbani kwake.” Akasema Pendo.
“Ouh My God !!!..” akasema mzee Raymond na kuinuka akaeleka chumbani kwa Happy
Happy alimimina mvinyo ule mkali katika glasi na kuishika mkononi.Akaitazama glasi ile huku akitoa machozi
“Pengine hii inaweza kunisaidia kuniondolea mzigo huu wa mawazo.” Akawaza Happy na kabla hajaipeleka glasi ile mdomoni akaingia baba yake na kumshika mkono akamnyang’anya ile glani na kuiweka mezani
“Happy unafanya nini??
“Daddy niache ninywe.Nahisi kama akili yangu imefika mwisho wake wa kufikiri.I don’t know what to do anymore” akasema Happy.Mzee Raymond akaketi pembeni yake
“Happy please don’t do this.Hii si njia sahihi ya suluhisho la matatizo yote yanayokukabili kwa sasa.Kunywa pombe kunaongeza matatizo na si kuyapunguza.Happy unatakiwa usimame imara na ukabiliane na kila jambo linalotokea.To win this you have to be strong.Nakuomba usife moyo Happy.Inuka ,simama na upambane hadi mwisho.” Akaseme amzee Kibaho
“Dady ,najitahidi sana lakini nashindwa.I’ve been so strong but not anymore.I’m so weak now.I cant fight, I cant do anything,I’m confused” akasema Happy
“Happy mwanangu naomba ujitahidi na usimame imara na hasa katika wakati huu.Patrick yuko gerezani .He’s alone and lonely.He neesds you.He needs your support.If you cant be strong for yourself then be strong for Patrick” akasema mzee Raymond
Kauli ile ya mzee Raymond ikamchoma sana Happy aliyekuwa ameinama akilia akainua uso wake na kufuta machozi.
“Happy umenielewa?
“Nimekuelewa baba.Samahani kwa kitu nilichotaka kukifanya.Nilidhani kutumia pombe kungekuwa ni suluhisho la kuniondolea mawazo mazito niliyonayo.I wont do that again dady.I promise..” akasema Happy
“Nafurahi kusikia hivyo Happy.tafadhali jipe moyo ,simama imara na sisi tuko nyuma yako katika kila hatua.Tutakupa kila aina ya ushirikiano unaouhitaji toka kwetu”
“Ahsante sana baba .Japokuwa suala hili ni gumu lakini nitajitahidi kwa kadiri niwezavyo kukabiliana nalo hadi dakika ya mwisho.Sikushawishiwa na mtu kufanya maamuzi haya .Niliamua mimi mwenyewe kwa hiari yangu kuachana na Mike na kurudiana na Patrick kwa hiyo inanilazimu nisimame imara katika kukipigania kile kilichonifanya nikachukua maamuzi haya..Najua Mike ameumia sana na yote aliyofanya leo ni kwa sababu yangu.Hakutegemea kama mimi naye tungeachana.Atanisamehe kwa maamuzi haya .” akasema Happy
“Nimefurahishwa na kauli yako Happy.kama nilivyokwambia mchana wa leo kwamba kuna wakati katika maisha yetu tunalazimika kufanya maamuzi magumu na maamuzi hayo magumu siku zote huwa yana athari zake.Lazima wawepo watu watakaoathirika na maamuzi hayo na ndiyo mana yakaitwa ni maamuzi magumu.Ninachokushauri kwa sasa achana na mambo yote yanayojitokeza au yatakayojitokeza na badala yake akili yako ielekeze katika jambo moja tu kulipigania penzi lako na Patrick.Pambana kila uwezavyo kuhakikisha kwamba Patrick anakuwa huru na hatimaye muishi maisha yenye furaha kubwa .Dont ever give up fighting.Mengi yametokea na mengi yatatokea lakini usiyape uzito bali macho na akili yako vielekeze kwa Patrick ambaye anateseka gerezani” akasema mzee Raymond.
“Baba nimekuelewa na ninakuahidi kwamba kuanzia sasa sintalia tena.I’ll be strong.Nimekwisha lia vya kutosha.Ahsante sana kwa kunifanya nitambue kwamba kulia hakutanisaidia lolote zaidi ya kuniongezea maumivu ya moyo” akasema Happy
“kesho tunakwenda kumuona Patrick gerezani,uko tayari kuonana naye? Akauliza mzee Raymond
“Niko tayari baba.Niko tayari kuonana na mtu ambaye ameushika moyo wangu.Nina imani hata haya mateso na maumivu ya moyo niliyonayo sasa yatapungua kama si kuisha kabisa nitakapomuona Patrick”
“Ok Happy kesho nitakupeleka Uwangwa Prison kuonana na Patrick.Nina imani hata naye pia ana hamu kubwa ya kuonana nawe.Margreth utapenda kuongozana nasi?
“Hapana baba kwa siku ya kesho nitakuwa kazini.Nitakwenda kumtembelea siku nyingine”akajibu Margreth.
Baada ya maongezi yaliyochukua zaidi ya saa moja,Happy akajikuta akitabasamu tena.Mzee Raymond akaichukua ile chupa ya mvinyo na kutoka mle chumbani akamuacha Happy akiwa na mdogo wake Margreth
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 36
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“kesho tunakwenda kumuona Patrick gerezani,uko tayari kuonana naye? Akauliza mzee Raymond
“Niko tayari baba.Niko tayari kuonana na mtu ambaye ameushika moyo wangu.Nina imani hata haya mateso na maumivu ya moyo niliyonayo sasa yatapungua kama si kuisha kabisa nitakapomuona Patrick”
“Ok Happy kesho nitakupeleka Uwangwa Prison kuonana na Patrick.Nina imani hata naye pia ana hamu kubwa ya kuonana nawe.Margreth utapenda kuongozana nasi?
“Hapana baba kwa siku ya kesho nitakuwa kazini.Nitakwenda kumtembelea siku nyingine”akajibu Margreth.
Baada ya maongezi yaliyochukua zaidi ya saa moja,Happy akajikuta akitabasamu tena.Mzee Raymond akaichukua ile chupa ya mvinyo na kutoka mle chumbani akamuacha Happy akiwa na mdogo wake Margreth.

ENDELEA…………………

Saa ya ukutani ilionyesha ni saa tatu za asubuhi.Happy Kibaho alikuwa mbele ya kioo kikubwa akijitazama.Siku hii ya leo alikuwa ameamka asubuhi sana na kuanza kujiandaa kwa ajili ya safari ya kuelekea katika gereza la Uwangwa kuonana na Patrick
“Moyo wangu una furaha sana na wasi wasi pia.Sijui Patrick atakuwa katika hali gani.Sijui itakuwaje nitakapomuona “ akawaza Happy akiwa amesimama mbele ya kioo kikubwa.
Wakiwa bado wanajiandaa ,ikasikika kengele ya getini.Pendo mfanyakazi wa ndani akaenda kufungua geti akakutana na gari lenye namba za kibalozi likiambatana na gari moja la polisi..Aliogopa na kutaka kufunga geti na kurudi ndani lakini toka katika gari lile lenye namba za kibalozi akashuka Mike.
“Maafisa naomba dakika tano tu niagane na mtu wangu wa muhimu sana” akasema Mike akiwaomba maafisa wa polisi alioambatana nao halafu akamfuata Pendo
“Happy yuko wapi? Akauliza Mike
“Yuko chumbani kwake” akajibu Pendo kwa wasi wasi
“Naomba ukamuite” akasema Mike huku akiingia ndani.Mara tu alipoingia sebuleni akakutana na mzee Raymond wakasalimiana.
“Pole sana Mike kwa yaliyotokea.”
“Nashukuru sana mzee” akajibu Mike.Hakutaka maongezi mengi na mzee Kibaho.
“Mzee nimepita mara moja kuonana na Happy na kumuaga……….” Kabla hajaendelea Happy akatokea pale sebuleni.Alikuwa na uso wenye wasi wasi mwingi.Akamtazama Mike na macho yake yakalengwa na machozi.Akamfuata na kumkumbatia.
“Mike I’m sorry……” akasema Happy
“You don’t have to be sorry Happy “ akajibu Mike.Wakatazamana kwa muda halafu Mike akasema
“Happy sina muda mrefu wa kukaa hapa.Nimekuja mara moja kukuaga.Ninaondoka kurejea Marekani sasa hivi.”
“Ouh Mike I’m sorry..!!!!.” akasema Happy huku machozi yakimtoka.
“Tafadhali usilie Happy.I’m ok now” akasema Mike
“Mike jambo gani hasa lilitokea? Niliona katika taarifa ya habari jana usiku kwamba ulipatwa na matatizo ukapelekwa polisi.Niliumia sana Mike.”
“Jana uliponiacha pale hotelini nilikuwa katika hali ya kuchanganyikiwa.Sikutambua nilichokuwa nakifanya.Nilishikiliwa kwa muda pale hotelini na waliponiachia niliondoka nikiwa na mawazo mengi sana na nilipokuwa barabarani nilisababisha ajali.Sifahamu ilitokeaje lakini nilijikuta nikimshambulia afisa wa usalama barabarani na kumsababishia majeraha.Nilikamatwa na kupelekwa polisi.Nawashukuru viongozi wangu wa ubalozi wa Marekani kwa jitihada zao za kunisaidia katika tatizo hili.Baada ya jitihada kubwa za kidiplomasia hatimaye serikali ya Tanzania imeamua kuniachia huru lakini imeniamuru niondoke nchini haraka sana na nisirejee tena hapa Tanzania.Nimeona nisiondoke bila ya kuja kukuona na kukuaga Happy.Utanisamehe sana kwani sikutegemea kama ningeweza kufanya kitendo kama kile cha uvunjifu wa sheria.Unanifahamu vizuri mimi si mtu wa vurugu na hii ilitokea kutokana na kughafirika tu.” akasema Mike
“Ouh Mike nisamehe sana mimi kwani ndiye chanzo cha haya yote.Bila mimi yasingekukuta mambo haya .” akasema Happy
“Usijilaumu Happy.Ni ujinga wangu ndio uliopelekea nikafanya kitendo cha kijinga namna ile.I shouldn’t ‘ve done that.Anyway sitaki kuliongelea sana hilo .Yameshatokea na tuyaache yapite.Happy nimekuja kukuaga.Nilikuja hapa Tanzania kwa ajili yako kwa hiyo siwezi kuondoka bila ya kuja kukuaga hata kama yametokea haya yaliyotokea.Nadhani hii itakuwa ni mara yetu ya mwisho kuoanana kwani nimepigwa marufuku kurejea Tanzania tena.Pamoja na kuondoka kwangu lakini naomba ufahamu kwamba moyo wangu bado unakupenda sana na nitaendelea kukupenda siku zote na kwa sababu ya upendo wangu kwako nayakubali maamuzi yako.Nakuacha uwe na Patrick kama ulivyoomba.Japokuwa nimeumizwa sana na suala hili lakini sina namna nyingine ya kuweza kuyabadili mawazo yako.Kitu kimoja tu ambacho naomba ukifahamu ni kwamba siku zote utaendelea kuwepo moyoni mwangu na unakaribishwa muda wowote kama una hitaji kuongea nami au aina yoyote ya msaada toka kwangu.I’ll always be there for you Happy because I love you” akasema Mike akiwa ameishika mikono ya Happy ambaye machozi yalikuwa yanamchuruzika.Mike akamfuta Happy machozi kwa mikono yake halafu akainama na kumbusu shavuni.
“Kwa heri Happy.” Akasema Mike na kugeuka akaanza kuondoka..Kabla hajafika mlangoni Happy akaita
“Mike !!!.” Mike akageuka
“Hutajali kama nikikusindikiza uwanjani? ..akasema Happy Mike akatabasamu na kusema
“Sintajali Happy” akajibu Mike Happy akakimbia chumbani kwake akachukua funguo ya gari lake
“I’ll go with you” akasema mzee Raymond.Happy akatabasamu.Wakaingia garini na safari ya kuelekea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere ikaanza.
“Nasikitika sana baba kwa mambo haya yaliyomkuta Mike.Am……………….” akasema Happy lakini kabla hajaendelea mbele baba yake ambaye alikuwa anaendesha gari ile akasema
“Usisikitike Happy.Kama nilivyokueleza jana usiku kwamba kwa sasa elekeza akili yako katika jambo moja tu nalo ni Patrick.Haya mambo mengine usiyape nafasi ya kukuumiza kichwa chako..Mike ni kijana mzuri ambaye ninaamini atapata mwanamke mwingine .Usiwaze sana kuhusu Mike.” Akasema mzee Raymond.
“Hata hivyo namshukuru Mike amenielewa na ameahidi hatanisumbua tena.Amebariki uhusiano wangu na Patrick.” Akasema Happy huku akitabasamu .baba yake naye akatabasamu
“Siamini kama leo hii ninaondolewa nchini Tanzania nikiwa chini ya ulinzi wa polisi.Nakijutia kitendo nilichokifanya.Nilifanya kitendo cha kijinga sana ambacho nitaendelea kukijutia katika maisha yangu yote.Lakini yote haya yamesababishwa na Happy.Wakati ninafanya kitendo kile sikuwa katika akili yangu ya kawaida.maamuzi yale ya Happy yalikuwa yameichanganya sana akili yangu .Sikutegemea kama mapenzi yangu na Happy yangetufikisha katika hatua hii.Sikutegemea kama siku moja tungeachana kirahisi rahisi namna hii.Bado naona ni kama ndoto kutokana na jinsi tulivyokuwa tunapendana.Nilimpenda Happy kwa moyo wangu wote na nilikuwa tayari kufanya jambo lolote lile kwa ajili yake.Kwa upande mwingine simlaumu sana kwa maamuzi haya kwa sababu ameufuata moyo wake.Kama alivyosema yeye mwenyewe kwamba Patrick ndiye furaha ya maisha yake kwa hiyo sina budi kuyaheshimu maamuzi yake.Lakini sintamsahau hata kidogo.Itanichukua miaka mingi kumtoa Happy moyoni mwangu na ninaamini siku moja nitamsahau na nitampata mwanamke ambaye ameumbwa kwa ajili yangu.” Mike alikuwa akiwaza wakati wakielekea uwanja wa ndege.
Walifika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere na baada ya kushuka garini Mike akamfuata Happy akamshika mikono
“Happy nashukuru sana kwa kunisindikiza.You can go home now.I’ll be fine” akasema Mike.Macho ya Happy yalilengwa na machozi.
“Mike naomba unisamehe sana kwa yote yaliyotokea.Sik…………………………” akasema Happy lakini Mike akamzuia asiendelee.
“Shhhhhhhhhhh…!!!!...Usisikitike Happy kuhusu kilichotokea.Nimetafakari kwa kina na kukuelewa kwamba unaitafuta furaha ya moyo wako ambayo ni Patrick na kwa hilo mimi sina tatizo .Ninaamini kwamba wewe na Patrick hakuna kitakachoweza kuwatenganisha tena.Kitu pekee ninachokuomba Happy ni kwamba mpende Patrick kwa moyo wako wote. You’ ve made a huge sacrifice so don’t you ever let it be for nothing.Fight till the end” akasema Mike.
Happy hakusema kitu alikuwa anatokwa na machozi.
“Happy usijali kuhusu mimi.Japokuwa moyo wangu umevunjika vipande lakini nitajitahidi kwa kadiri niwezavyo ili kulitibu jeraha hili litakalochukua muda mrefu kupona.Ninachokushauri kwa sasa ,mpiganie Patrick ili aweze kutoka gerezani.” Akasema Mike na kugeuka baada ya ofisa mmoja wa ubalozi kumsogelea na kumfanyia ishara kwamba muda unakwenda.
“Happy muda wangu umekwisha,natakiwa kuondoka sasa lakini kabla sijandoka kuna kitu ambacho nataka kukuomba”
“Omba chochote Mike” akasema Happy
“Ninaomba niendelee kuwa rafiki yako”
“Mike siku zote utabaki kuwa rafiki na mtu wa karibu sana kwangu.” Happy akashindwa kuendelea akaanza kulia
“Nashukuru sana Happy.Muda wowote ukinihitaji unafahamu namna ya kunipata.Ubaki salama Happy.” Akasema Mike halafu akamkumbatia Happy na kumbusu shavuni na kuondoka.Happy akamtazama Mike hadi alipopotea kabisa katika macho yake.Bado machozi yaliendelea kumtoka.
“ It’s ok ..!! let him go “ akasema mzee Kibaho.
“ Inatosha sasa.Nyamaza kulia.” Mzee Kibaho akamshika mkono Happy na kumfungulia mlango wa gari akaingia kisha wakaondoka pale uwanjani.
“Tunaelekea Uwangwa Prison.Uko tayari kuonana na Patrick? Akuliza mzee Kibaho.
“Niko tayari baba” akajibu Happy

************************

Ni siku ya mazishi ya Veronika.Toka alfajiri nyumbani kwao kumekuwa ni sehemu yenye pilika nyingi.Kila kitu kilikwisha tayarishwa na kilichokuwa kinasubiriwa na muda tu wa kuanza shughuli hii.Ndugu ,jama na marafki waliokuwa wakisubiriwa tayari walikwisha fika wote.
Saa tatu za asubuhi ,Sarah akampigia simu Alois kaka yake Patrick
“ Hallow Sarah” akasema Alois baada ya kupokea simu
“Alois nimekupigia kukutaarifu kwamba leo tunamzika Vero.Atazikwa katika makaburi ya kinondoni.Ratiba inaonyesha kwamba baada ya mwili kuchukuliwa toka hospitali ya muhimbili , utaletwa hapa nyumbani kwa ajili ya kuagwa na baadaye utapelekwa kanisani kwa ajili ya ibada ya misa na kisha tutaelekea makaburini.Nilitaka kujua kama kuna mtu yeyote ambaye atatumwa kuja kuwakilisha ..” akasema Sarah
“Sarah ningependa sana kutuma uwakilishi lakini ninasita kufanya hivyo kutokana na kilichotokea jana.Wajumbe tuliowatuma kuja kutuwakilisha walifukuzwa na Loniki na kuambiwa kwamba hatutakiwi kabisa kuonekana katika msiba wa Vero kwani mwanetu amemuua ndugu yenu makusudi.Sarah nasikitika sana kwa jambo hili.”
“Alois samahani sana kwa kilichotokea jana.Hata mimi siafiki jambo kama lile na sikulipenda hata kidogo.Hatupaswi kujenga chuki na uhasama baina yetu.Sote tumeumizwa na jambo hili kwa hiyo kuna kila ulazima wa kushirikiana katika kipindi hiki kigumu.Alois naomba usikate tamaa ,sisi tayari tulikwisha kuwa ndugu kwa hiyo nakuomba ufanye juu chini utume watu ambao watakuja kumuwakilisha Patrick katika mazishi ya mchumba wake.Watakapofika wanitafute mimi na si mtu mwingine yeyote” akasema Sarah.
“Nimekuelewa Sarah nitatuma ujumbe wa watu kuja kutuwakilisha na kumuwakilisha Patrick .Ningeweza kuja hata mimi mwenyewe lakini bado naendelea kupokea wageni mbali mbali kwa sababu mimi ndiye mtoto mkubwa wa mzee..”
“Usijali Alois .Kwa sasa tunaelekea hospitali ya Muhimbili kuuchukua mwili na kisha tutarejea hapa nyumbani kwa ajili ya taratibu za kuuaga.” Akasema Sarah akaagana na Alois na kukata simu.
Baada ya kumaliza kuongea na Sarah,Alois akampigia simu Andrew ambaye alikuwa katika majukumu mengine pale msibani na kumtaka waonane mara moja
“Andrew nimetoka kuongea na Sarah muda si mrefu ,leo ndiyo siku ya mazishi ya Vero .Ameniomba nitume ujumbe wa watu kwenda kutuwakilisha..Una mawazo gani kuhusu hilo?
Andrew akainama akafikiri kidogo na kusema
“Ni wazo zuri lakini bado nina wasi wasi na kilichotokea jana.Loniki dada mkubwa wa Vero alitufukuza na kutuonya kwamba tusikanyage tena pale msibani.Lakini kama Sarah amesisitiza kwamba utume ujumbe ,basi fanya hivyo.Teua ujumbe wa watu wachache na uwatume kutuwakilisha katika mazishi”
Alois akainama na kufikiri kidogo halafu akasema
“Andrew itabidi uongoze ujumbe utakaokwenda kutuwakilisha huko.” Akasema Alois
“Sawa Alois.Sina tatizo na hilo.” akasema Andrew na muda huo huo akaingia Savanna.Wakasalimiana na kumfahamisha kilichokuwa knaendelea.
“Ninaomba na mimi niungane na ujumbe huo utakaokwenda nyumbani kwa akina Vero katika mazishi.” Akasema Savanna
“Usijali Savanna tutakuwa sote” akasema Andrew huku akiitoa simu yake iliyokuwa inaita na kusogea pembeni
“Savanna,Patrick alikuwa katika hali gani ulipompa taarifa za kifo cha mzee? Akauliza alois
“Alistuka sana.Japokuwa alijaribu kujikaza lakini aliumia mno moyoni.Vifo viwili vya watu wake muhimu vimetokea kwa haraka sana lazima atakuwa na maumivu makubwa moyoni.” Akasema Savanna.
“Namuonea huruma sana mdogo wangu.Tayari alikuwa na maisha yake mazuri na yenye furaha akiwa na Vero lakini mara tu alipojitokeza huyu Happy kila kitu kimeharibika” akasema Alois kwa masikitiko.
“Usisikitike sana alois.Huwezi fahamu ni kwa nini mambo haya yametokea sasa.” Akasema Savanna

* * *

Msafara wa gari zaidi ya tano uliondoka nyumbani kwa akina Vero kuelekea hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kuuchukua mwili wa Vero.Katika msafara huo walikuwepo pia Loniki na Sarah dada zake Vero.Katika gari walilokuwa wamepanda,Loniki alikuwa na chupa ya mvinyo akiendelea kunywa.Macho yalikuwa yamemvimba kutokana na kulia.Toka asubuhi amekuwa akinywa mvinyo huu mkali ili kumsaidia kumpunguzia uchungu wa kifo cha mdogo wake.
“Loniki tafadhali naomba usiendelee kunywa huo mvinyo.” Akasema Sarah lakini Loniki akajibu kwa ukali
“Let me drink…Huwezi kujua uchungu nilionao.Nilimpenda sana Vero lakini Patrick amemkatili uhai wake.Nina uchungu mwingi sana na ambao sina hakika kama unaweza kuelezeka” akasema Loniki.Akainua chupa yake ya mvinyo akapiga funda moja na kusema
“Nina hasira sana na Patrick.Yeye ndiye aliyesababisha uchungu wote huu.Sisemi zaidi nasubiri kwanza masuala ya msiba yamalizike” akasema Loniki,Sarah akamtazama hakutaka kumsemesha tena.Safari ikaendelea.
Walifika hospitali ya Taifa ya Muhimbili .Pale walikutana na watu ambao walikwisha tangulia ili kwenda kukamilisha taratibu za kuuchukua mwili wa Vero.
Saa sita za mchana taratibu zikakamilika na mwili wa Vero ukawa tayari kwa kuchukuliwa.Ndugu jamaa na marafiki waliofika pale Muhimbili walipata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho.Vero alikuwa amelala ndani ya jeneza lake la gharama kubwa akiwa amevalishwa gauni lake la harusi alilokuwa amelinunua uingereza kwa ajili ya kulivaa siku ya harusi yake na Patrick.Loniki alishindwa kujizuia akaanguka na kupoteza fahamu.Kwa muda wa dakika chache eneo lote la Muhimbili liligeuka sehemu ya vilio.Loniki na baadhi ya akina mama waliopoteza fahamu walipatiwa msaada na baada ya kuzinduka safari ya kuelekea nyumbani ikaanza
 
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 37
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Saa sita za mchana taratibu zikakamilika na mwili wa Vero ukawa tayari kwa kuchukuliwa.Ndugu jamaa na marafiki waliofika pale Muhimbili walipata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho.Vero alikuwa amelala ndani ya jeneza lake la gharama kubwa akiwa amevalishwa gauni lake la harusi alilokuwa amelinunua uingereza kwa ajili ya kulivaa siku ya harusi yake na Patrick.Loniki alishindwa kujizuia akaanguka na kupoteza fahamu.Kwa muda wa dakika chache eneo lote la Muhimbili liligeuka sehemu ya vilio.Loniki na baadhi ya akina mama waliopoteza fahamu walipatiwa msaada na baada ya kuzinduka safari ya kuelekea nyumbani ikaanza.

ENDELEA………..

Saa tano za asubuhi Happy kibaho akiwa ameongozana na baba yake mzee Raymond Kibaho wakawasili katika gereza la Uwangwa kwa lengo la kumuona Patrick.Kama zilivyo taratibu za gereza hili walijiandikisha majina yao ikiwa ni pamoja na kuchukua alama za vidole kisha wakapelekwa katika sehemu maalum kwa ajili ya kuonana na mahabusu.Happy moyo wake ulikuwa unamuenda mbio sana
“Jitahidi ujizuie usiangushe chozi.Patrick anahitaji kukuona ukiwa katika uso mkavu.” Akasema mzee Kibaho wakati wameketi wakimsubiri Patrick aletwe.Happy hakujibu kitu,alimtazama baba yake kisha akavuta pumzi ndefu.
Baada ya dakika tano akatokea Patrick akiwa ameongozana na askari magereza.Mara tu Happy alipomuona Patrick akajikuta akisimama na kutamka kwa sauti ndogo yenye mshangao ndani yake
“Patrick …..!!!!!!! akasema Happy
Patrick akaelekezwa sehemu ya kukaa na Yule askari.
“Patrick una dakika ishirini za kuongea na wageni wako” akasema Yule askari akasogea pembeni na kumpa nafasi ya kuongea na wageni wake kwa uhuru na mara Patrick na Happy wakakumbatiana kwa nguvu.
Happy alishindwa kujizuia akaangusha machozi
“Nyamaza usilie Happy.Usilie tena malaika wangu.Inatosha” akasema Patrick huku akimfuta Happy machozi kwa mikono yake.Happy akamkumbatia tena kwa nguvu.Baada ya kama dakika tatu Patrick akamshika mkono na kumketisha chini.Macho ya Happy bado yaliendelea kudondosha machozi.
“Stop crying Happy.Its enough now.Umekwisha lia vya kutosha” akasema Patrick huku akimpiga piga Happy mgongoni.Alipogeuza shingo yake akagonganisha macho na mzee Raymond Kibaho.
“Pole sana Patrick” akasema mzee Raymond huku akisogea na kumpa mkono Patrick
“Nashukuru sana mzee.Nimekwisha poa” akasema Patrick na kujilazimisha kutabasamu
“Usife moyo kijana wangu.Matatizo ni sehemu ya maisha yetu wanadamu na hatuna budi kukabiliana nayo kila yanapotokea.Tuko pamoja Patrick na wala usijali tutashirikiana katika kila jambo na mwisho kuhakikisha kwamba mambo haya yanakwisha.” Akasema mzee Raymond .
“Nashukuru sana mzee kwa ushirikiano wako.Mungu atasaidia na mambo haya yatakwisha” akasema Patrick halafu akamgeukia Happy aliyekuwa ameinama akilia kimya kimya.
“Patrick naomba niwaache wenyewe muongee nitakuwa hapo nje” akasema mzee Kibaho na kutoka nje akawapa nafasi Patrick na Happy yakuongea mambo yao kwa uhuru.
“Pole sana Patrick” akasema Happy baada ya baba yake kutoka nje.
“Ahsante sana malaika wangu.Nimefarijika sana nimekuona tena.Vipi unaendeleaje?
“Hata mimi nimefarijika sana kukuona tena Patrick.Ninashukuru Mungu ananisaidia ninaendelea vizuri japokuwa si rahisi.Nakumbana na magumu mengi sana.”
“Pole sana Happy.Ninafahamu ni namna gani ulivyo na wakati mgumu.Utanisamehe mpenzi wangu halikuwa kusudio langu kukuweka katika wakati mgumu namna hii.Sikutegemea kama maamuzi yangu yangetufikisha hapa tulipo sasa” akasema Patrick kwa uchungu.
“Usiseme hivyo Patrick.Haya hayakuwa maamuzi yako peke yako.Tulifanya maamuzi haya sote wawili kwa hiyo usijilaumu kwa kilichotokea na wala hakuna haja ya kujilaumu au kumlaumu mtu yeyote kwa maamuzi yetu.Tuachane na yaliyotokea na tuangalie namna ya kukabiliana na yale yajayo.” Akasema Happy halafu wakatazamana kwa sekunde kadhaa.
“Pole sana kwa msiba wa baba “ akasema Happy
“Ahsante sana Happy nimekwisha poa.Yote haya ni mapenzi ya Mungu” akasema Patrick halafu kikapita kimya kifupi.
“Happy ninaomba uwe mvumilivu sana katika kipindi hiki .Tunapita katika kipindi kigumu mno katika maisha yetu.Nayafahamu mateso na maumivu uliyonayo ,lakini naomba nikuhakikishie kwamba siku moja mambo haya yote yatakwisha na ndoto yetu ya siku nyingi ya kuwa pamoja itatimia.Safari ya kuelekea kuitimiza ndoto yetu si rahisi hata kidogo imejaa vikwazo vingi na majaribu mengi.Tukiwa na imani na kusimama katika msimamo wetu ,tutayashinda haya yote.Yatupasa kuwa wavumilivu sana hasa katika wakati huu” akasema Patrick.
“Patrick ,naomba nikiri kamba mambo katu si rahisi hata kidogo.Haya masuala ni mazito na katika maisha yangu sikutegemea kukumbana na kipindi kigumu kama hiki.Kuna nyakati inaniwia ugumu kuyabeba mambo haya na ninajikuta nikiwa dhaifu lakini namshukuru sana Mungu kwani amekuwa ndiyo nguzo yangu na kwa sababu yake kila siku nimekuwa nikipata nguvu za kusonga mbele.Kuna nyakati ninakata tamaa lakini ninapokumbuka sura yako na upendo wako mkubwa kwangu ninapatwa na nguvu za ajabu za kupambana hadi mwisho.Patrick napenda kukuhakikishia kwamba niko imara sasa na sintalia tena na ninakuahidi kwamba nitalipigania penzi letu hadi dakika ya mwisho.Nitahakikisha kwa kila iwezekanavyo tunatimiza ndoto yetu ya kuwa pamoja.Patrick nakupenda sana na nitakupenda hadi mwisho wa uhai wangu” akasema Happy na kwa mbali sura ya Patrick ikajenga tabasamu
“Nashukuru sana Happy kwa ujasiri wako.Nitazidi kukuombea ili uweze kupata ujasiri zaidi wa kuweza kukabiliana na kila gumu linalojitokeza.” Akasema Patrick,kikapita kimya cha sekunde kadhaa wakitazamana.
“Patrick kuna mambo ambayo yametokea katika siku hizi chache ambayo nadhani ingekuwa vyema kama ungeyafahamu” akasema Happy na kukaa kimya kidogo akamtazama Patrick.
“mambo gani malaika wangu? Akauliza Patrick
“ Nimelivua taji la Miss Tanzania”
“What…..!!!!!” Patrick akashangaa
“Happy umefanya nini tena? Kwa nini umechukua maamuzi hayo? Akauliza Patrick
“Patrick si wewe peke yako uliyestushwa na maamuzi haya ya kulivua taji la Miss Tanzania .Wengi wamestushwa sana na maamuzi haya kwani haijawahi kutokea katika historia kwa mrembo kulivua taji kubwa kama hili.Sikuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya kulirudisha taji lile kwa wenyewe ili kuendelea kuilinda heshima yake” akasema Happy.Patrick akamshika mkono na kumtazama usoni
“Happy kwa nini umefanya hivyo? Haikuwa rahisi kulishinda taji lile kubwa na muhimu kwako.Kwa nini umelivua haraka namna hii?
“Toka siku yalipoanza matatizo haya,nilikuwa ni kama mtu niliyechanganyikiwa.Sikujua nifanye nini ili kuweza kukabiliana na hali hii.I was so weak.Siku ile ulipopandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza nilifika mahakamani lakini sikuweza kuingia ndani .Nilibaki ndani ya gari.Nilikuwa mtu wa kujifungia ndani na kulia.Namshukuru sana Savanna kwa sababu alinitembelea nyumbani akanifariji na kuniambia maneno ambayo yalinifanya nipate nguvu na tumaini tena.Nilifikiria sana kuhusu mustakabali mzima wa maisha yangu na namna nitakavyoweza kukabiliana na suala hili lililojitokeza nikaamua kuyaweka kando mambo yote ikiwemo na taji la miss Tanzania ili nibaki naangalia suala moja tu la kesi yako.Patrick thamani yako ni kubwa sana kwangu kuliko taji la miss Tanzania au kitu chochote kile na ndiyo maana sikujuta na wala sijutii maamuzi yangu.Moyo wangu una amani kabisa kwa sababu nimefanya hivyo ili niweze kuwa na muda mwingi wa kushughulika na mtu ninayempenda kuliko wote hapa duniani.Niliwataarifu familia yangu na wakakubaliana nami.Nawashukuru sana kwani wamekuwa na mimi karibu sana na kunipa nguvu.Niliwasiliana na wakuu wangu nikawaeleza ,japokuwa ilikuwa vigumu kwao kukubali lakini waliiona hoja ya msingi katika maombi yangu na wakakubali japo kwa shingo upande.Jana nilifanya mkutano na waandishi wa habari na kutangaza rasmi kwamba nimelivua taji la miss Tanzania.” Patrick akamkumbatia Happy na kusema
“Happy,sipati neno la kusema kuelezea furaha yangu.Nilikuwa na wasi wasi mwingi baada ya kutokuona mahakamani siku ile ya kesi yangu ilipotajwa.Nilimtuma Savanna aje akuangalie .Nashukuru kukuona ukiwa unaendelea vizuri japokuwa nimeumizwa na maamuzi hayo mazito uliyoyachukua ya kulivua taji lile muhimu sana kwako” akasema Patrick.
“Patrick huna sababu ya kuhuzunika kwa maamuzi haya.Hakuna mtu yeyote aliyenishurutisha kufanya hivi .Nimefanya hivi kutokana na thamani yako kwangu,kwa sababu ninakupenda kuliko mtu yeyote duniani” akasema Happy halafu akaishika mikono ya Patrick na kuibusu
“Vipi kuhusu maendeleo ya kesi” akauliza Happy
“Bado sijapata picha halisi kuhusiana na mwenendo mzima wa kesi kwa sababu bado iko katika hatua za awali za kutajwa.Bado upande wa mashtaka wanaendelea kukusanya ushahidi wa kutosha.Savanna amenipa moyo kwamba kesi hii haina ugumu kwake.Ninamuamini Savanna ni wakili maarufu sana na hajawahi kushindwa kesi toka ameanza kazi hii ya uwakili.Nina uhakika mkubwa wa kushinda”
Happy akamtazama Patrick usoni na kuuliza
“Do you trust her ?
“Yes I do.Savanna ni mmoja wa mawakili mahiri sana hapa nchini.Amekuwa akishughulika na kesi mbali mbali kubwa kubwa na haijawahi kutokea akashindwa kesi.Kwa nini umeuliza? Una wasi wasi naye?
“Never mind….I was just curious.Nilitaka nifahamu tu uwezo wake katika kuisimamia kesi hii.Do you know each other for long ? akauliza Happy
“Yes we know each other for long.She’s my friend.Tumekuwa marafiki kwa muda mrefu sana sasa.Why do you ask? Don’t you trust her?
“Si hivyo Patrick.Nahitaji tu kumfahamu vizuri.Tunahitaji wakili mahiri katika kesi hii ambaye ataweza kuisimamia na kuhakikisha tunashinda.Savanna atahitaji shilingi ngapi katika kuisimamia kesi hii hadi mwisho? Nahitaji na mimi nitie mchango wangu katika kumlipa wakili atakaye simamia kesi hii” Akauliza Happy
“Usihofu Happy kuhusu malipo ya Savanna.Hakutakuwa na malipo yoyote kwa sababu Savanna anaifanya kazi hii bila malipo yoyote.Amejitolea yeye mwenyewe kuzibeba gharama zote za kesi hii.Huo ni mchango wake kwangu”
“Patrick..!!!..” Happy akashangaa
“Anawezaje kuisimamia kesi kubwa kama hii bila kuhitaji malipo yoyote? Happy akauliza
“Kama nilivyokwambia Happy kwamba mimi na Savanna ni marafiki wa siku nyingi na amejitolea kuifanya kazi hii bure kabisa bila malipo yoyote yale.Tunachotakiwa kufanya ni kumpa ushirikiano anaouhitaji na kwa pamoja tutashinda.” Akasema Patrick halafu akageuza shingo yake akamtazama askari magereza aliyekuwa amesimama pembeni kidogo akiangalia saa yake.
“Happy naona hatutakuwa na muda mrefu zaidi wa kuongea.Ninachokuomba usiwe na wasi wasi wowote kuhusu mimi.Niko salama na ninaendelea vizuri.Nimefarijika sana kwa kuja kunitazama.Nitafurahi zaidi kama ukija kunitazama mara kwa mara.Kuhusu kesi yangu nakuhakikishia kwa mara nyingine tena kamba usiwe na wasi wasi wowote ule.Savanna atashughulikia kila kitu.Ninachokuomba jaribu kuwa naye karibu ili aweze kukufahamisha kila kinachoendelea kuhusiana na kesi hii.”
“Ouh Patrick my angel ,natamani niendelee kukaa nawe hapa japo kwa siku nzima.Najisikia vibaya sana kuondoka na kukuacha peke yak😵uh my darling sijui hata nifanye nini…” Happy akasema huku machozi yakimlenga lenga
“Usihofu kuhusu mimi Happy.Niko salama na ninapata kila ninachokihitaji.Savanna anafahamika sana hapa na kwa hiyo kwa heshima yake ninapata huduma nzuri tofauti na mahabusu wengine.Kwa hiyo nakuomba uwe na amani ya moyo.Kitu cha msingi ni kuongeza maombi ili mambo haya yaweze kufikia mwisho ila usisahau kuwasiliana na Savanna mara kwa mara.Kama kuna chochote ninachotaka kukwambia nitakuwa namtumia hata yeye kwa sababu yeye huja hapa gerezani kila siku na kunitazama na kuniletea taarifa mbali mbali kuhusiana na kesi yangu.”
“Patrick nitakuja mara kwa mara kukutazama.Nitashirikiana na Savanna kwa ukaribu sana kama ulivyosisitiza.” Akasema Happy halafu akamkumbatia Patrick.
“Mama,muda umekwisha.Patrick anatakiwa kurudishwa ndani” akasema Yule askari magereza aliyekuwa akimlinda Patrick.
Happy na Patrick wakabusiana na kisha akainuka na taratibu akaanza kuelekea mahabusu.Happy akamtazama huku machozi yakimtoka hadi alipopotea kabisa
“It’s ok Happy” akasema mzee Kibaho huku akimshika bega mwanae na taratibu akamshika mkono wakatoka mle ndani.
“Dady nimefarijika na kuumia pia baada ya kumuona Patrick” akasema Happy wakiwa garini wakiondoka .
“Ninaamini hata Patrick amefurahishwa na kufarijika sana baada ya kukuona.Nilimtazama machoni alishindwa kuificha furaha yake.Vipi kuhusu mwenendo wa kesi ?
“Kwa mujibu wa maelezo yake ni kwamba kesi inakwenda vizuri na amenitaka nisiwe na wasi wasi kwa sababu wakili anayemtetea ni mahiri sana katika kuzisimamia kesi kama hizi.Lakini dady bado nina wasi wasi kama kweli Savanna anaweza akaifanya kazi hii ipasavyo.Ninafikiria kumtafuta wakili mwingine ili aungane na Savanna katika kuisimamia kesi hii”
“Kwa nini unakuwa na wasi wasi kuhusiana na wakili anayemtetea Patrick? Una shaka na uwezo wake?
“Sina shaka na uwezo wake lakini nina wasi wasi kidogo kwani hahitaji hata senti moja katika kuisimamia kesi hii.Amejitolea kuifanya kazi hii bure kabisa bila malipo”
“Bila malipo??? Mzee Raymond naye akashangaa
“Ndiyo dady.Amedai kwamba hatahitaji hata senti moja na yeye ndiye atakayegharamia gharama zote za kesi hii” akasema Happy
“Kama Patrick anayoimani na huyo wakili wake basi hakuna tatizo .Kitu cha msingi ni kutoa ushirikiano kwa haraka pale utakapohitajika.Tukisema tutafute tena wakili mwingine kwa sasa inaweza ikaleta tatizo na familia ya Patrick.” Akasema mzee Kibaho.
“Nakubaliana nawe baba.Inaweza ikaleta mgongano mkubwa baina yetu.Kitu pekee ninachoona cha msingi ni kuwa karibu na Savanna kama Patrick alivyosema.” Akasema Happy halafu akachukua simu na kuzitafuta namba za simu za Savanna akapiga
“Hallo Happy !..” akasema Savanna baada ya kupokea simu
“Hallow Savanna habari yako?
“Habari yangu nzuri Happy.Unaendeleaje?
“Ninaendelea vizuri Savanna.Nimetoka kumuona Patrick”
“Vizuri sana Happy.Namna hiyo utamfanya Patrick afarijike na kupunguza mawazo”
“Savanna uko wapi mida hii? Ninaweza kupata nafasi ya kuonana nawe leo hii? Akasema Happy
“Kwa sasa niko nyumbani kwa akina vero.Mazishi yake yanafanyika leo.Na hivi sasa tunausubiri mwili wa marehemu uwasili ili tuanze zoezi la kutoa heshima za mwisho na baadae tuelekee kanisani na kisha makaburini kwenda kumpumzisha.” Akasema Savanna,kikapita kimya kifupi.Taarifa ile ilimstua sana Happy na kutonesha kidonda cha moyo,akaangusha machozi.
“Happy.!!!..akaita Savanna
“Savanna .!!!!” Happy akataka kusema kitu lakini akashindwa.
“Happy nitakutafuta baada ya mazishi.Nitakuja nyumbani kwenu kukuona.Kwa sasa vimeanza vilio ,mwili wa marehemu umewasili.” Akasema Savanna Happy hakujibu kitu akakata simu.
“Kitu gani kinakuliza Happy? Akauliza mzee Raymond.
“Vero anazikwa leo..” akasema Happy halafu akainama.Mzee Raymond akavuta pumzi ndefu ,akageuza shingo na kumtazama mwanae.
“Happy ,usiwaze sana kuhusu jambo hili.Jitahidi kusahau kuhusu hilo tukio.Kwa sasa elekeza nguvu zako katika kuhakikisha kwamba Patrick anatoka gerezani” akasema mzee Kibaho.
“Dady ,its difficult to forget about what happened that night.Mimi ndiye niliyemuua Vero.Bila mimi Vero angekuwa hai mpaka hivi sasa.” Akasema Happy huku akilia.Mzee Raymond akapunguza mwendo wa gari na kuliegesha pembeni.
“Happy tafadhali nyamaza kulia.Hukukusudia kufanya jambo lile.Ile ni ajali kama ajali nyingine.Ulimsukuma Vero kwa ajili ya kumsaidia Patrick na hukudhamiria kumuua .Usijilaumu sana kwa kilichotokea ”akasema mzee Raymond.Happy akainua kichwa chake na kufuta machozi
“Nimekusikia baba lakini moyo wangu unauma sana.” Akasema Happy.Mzee Raymond akamtazama halafu akawasha gari na safari ikaendelea.

* * *

Eneo lote liligubikwa na sauti za vilio baada ya msafara wa magari kuwasili nyumbani kwa akina Vero ukitokea
hospitali ya taifa ya Muhimbili kuchukua mwili wa Vero.Gari maalum lililokuwa na mwili wa Vero likapewa nafasi na halafu jeneza zuri jeupe lenye nakshi za kupendeza likashushwa toka garini na kuingizwa ndani.Mahala hapa hapakuwa na masikilizano tena kutokana na vilio vingi na wengine walianguka na kupoteza fahamu.Kwa wale ambao bado walikuwa hawaamini kama ni kweli Vero alikuwa amefariki dunia sasa waliamini baada ya kuliona jeneza lile na kuzidisha vilio.Ilichukua zaidi ya nusu saa kuwatuliza waombolezaji na kisha muongoza shughuli akawasomea ratiba nzima ya mazishi.
Joel Armendo mjomba wa Vero akapanda jukwaani na kusoma historia ya marehemu halafu zikafuata nyimbo za maombolezo toka katika kwaya aliyokuwa akiimbia Vero.Baada ya kwaya kumaliza wimbo wa maombolezo ,kikafuata kipindi cha kutoa salamu za rambi rambi.Watu na vikundi mbali mbali walipanda na kutoa rambi rmbi zao na kumuelezea Vero kama binti aliyekuwa mfano wa kuigwa katika jamii.Wote walielezea namna walivyokuwa wameguswa na kifo kile.Baada ya watu na vikundi mbali mbali kumaliza kutoa salamu zao za rambi rambi,mwongoza shughuli akachukua kipaza sauti na kusema
“Tunawashukuru nyote kwa salamu zenu za rambi rambi na namna mlivyoguswa na msiba huu mzito.” Akanyamaza kidogo halafu akasema
“Kama mlivyosikia histora ya marehemu kwamba hadi anakutwa na mauti alikuwa na mchumba aitwaye Patrick ambaye walikuwa katika maandalizi ya mwisho ya kufunga ndoa.Kutokana na tukio hili kwa sasa Patrick anashikiliwa na vyombo vya usalama lakini pamoja na kwamba yuko gerezani ametuma salamu zake za rambi rambi kwa msiba huu mzito wa mchumba wake.Tunao hapa wawakilishi toka familia ya Patrick ambao wamekuja kuungana nasi katika mazishi ya binti yetu.Papo hapo bila kusahau ni kwamba Patrick naye amempoteza baba yake mzazi siku ya jana kwa hiyo kijana huyu amekutwa na misiba miwili hivi sasa.Kabla hatujaingia katika zoezi la kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu,naomba kwa heshima kubwa niwaite hapa jukwaani wawakilishi toka familia ya Patrick.Karibuni sana ndugu zetu” akasema muongoza shughuli na minong’ono ikaanza kusikika.
Taratibu Andrew na Savanna wakapanda jukwaani.Andrew akakabidhiwa kipaza sauti.
“Ndugu waombolezaji,tumesimama hapa mbele yenu kuwakilisha salamu nyingi za pole kwa familia hii kufuatia kifo cha mpendwa wao Veronika. Sipati neno la kusema kuelezea uchungu tulionao sisi kama familia ya Patrick kwa kifo hiki cha ghafla cha Veronika.Sote tulimpenda sana na kumjali kama ndugu yetu,shemeji yetu,mchumba wa ndugu yetu Patrick.Hakuna aliyefahamu kama yangetokea haya yaliyotoea.Naomba mfahamu kwamba tumeumizwa sana na kifo hiki.Hii ni kazi ya Mungu na siku zote haina makosa.” Akasema Andrew halafu akanyamaza kidogo akawatazama waombolezaji waliokuwa kimya wakimsikiliza.
“Wakati ,hata sisi kama familia tukiwa katika taharuki juu ya kilichotokea,hata sisi pia tumempoteza mzee wetu ,baba mzazi wa Patrick.Haya ni majonzi makubwa na familia zetu kwa sasa zinapitia kipindi kigumu sana.Hatuna cha kufanya zaidi ya kuziombea roho za wapendwa wetu zipumzike kwa amani.” Akanyamaza kwa sekunde kadhaa halafu akasema
“Baada ya tukio lile lililopelekea umauti wa Vero,Patrick anashikiliwa na vyombo vya usalama na tayari kesi yake imeanza kutajwa na tuna hakika kwamba haki itatendeka.Nawaomba ndugu zangu tuviachie vyombo vya kutoa haki vifanye kazi yake.Najua kwa tukio kama hili yataibuka mambo mengi sana,chuki,visasi,uhasama lakini nawasihi ndugu zangu tusifike huko.Sisi tayari ni ndugu kwa hiyo tusikubali hata kidogo tukio hili likatugawa na kujenga chuki miongoni mwetu.Tuendelee kushikamana katika nyakati hizi ngumu tulizonazo na tuepuke kuishi kwa hasama na kulipizana kisasi.Visasi havitaweza kuurudisha uhai wa wapendwa wetu.Binafsi nimekuwa rafiki mkubwa wa Patrick na Vero kwa muda mrefu sana na ninawafahamu kiundani.Ninayafahamu mapenzi yao pengine kuliko mtu mwingine yeyote kutokana na ukaribu wangu kwao.Kilichotokea hata mimi bado ninaona kama ndoto.” Andrew akanyamaza kisha akaendelea.
“Akiwa gerezani,Patrick ametuma salamu zake za rambi rambi kwa familia,ndugu jamaa na marafiki wa Vero.Baada ya salamu hizo za familia napenda sasa nikabidhi mchango wetu wa pole wa shilingi milioni tatu na papo hapo kuwataarifu kwamba baba mzazi wa Patrick atazikwa kesho .Kwa wale mtakaoweza kufika karibuni sana kuungana nasi katika kumpumzisha mzee wetu.” Akamaliza Andrew halafu akachukua bahasha na kumkabidhi muongoza shughuli kisha yeye na Savanna wakashuka jukwaani.Katika sehemu waliyokuwa wamekaa familia ya Vero,Loniki dada mkubwa wa Vero alikuwa amefura kwa hasira wakati Andrew akitoa salamu zile za rambi rambi.Sarah aliyekuwa amekaa pembeni yake alimtuliza na kumuomba asifanye jambo lolote la aibu mbele ya umati ule mkubwa wa watu.
Zoezi la kuuaga mwili wa marehemu likaanza na kuchukua muda mrefu zaidi ya ilivyokuwa imetazamiwa kutokana na umati mkubwa wa watu.Baada ya zoezi kukamilika ,waombolezaji wakapata chakula kisha ukaanza utaratibu wa kuelekea kanisani kwa ajili ya ibada.Magari yakapangwa vizuri na kisha jeneza lenye mwili wa Vero likatolewa ndani na kuingiza katika gari maalum na safari ya kuelekea kanisani ikaanza.Vilio viliendelea kusikika toka kwa akina mama waliokuwa wakilipungia mkono jeneza lenye mwili wa Vero wakati likiondolewa kwani ilikuwa ni mara yao ya mwisho kumuona tena mpendwa wao.Watu waliingia katika magari na safari ya kuelekea kanisani ikaanza.Ulikuwa msururu mrefu wa magari na wengine ambao hawakutaka kupanda magari walikuwa wakitembea kwa miguu kwa sababu kanisa halikuwa mbali na makazi ya akina Vero.
Hata kabla ya kuwasili kwa mwili wa marehemu kanisani,tayari kanisa lilikwisha jaa watu.Hii ilionyesha ni jinsi gani kifo cha Vero kilivyowagusa watu wengi.
Jeneza likashushwa garini na kuingizwa kanisani na kabla ya kuanza kwa ibada ikatolewa tena nafasi nyingine ya kutoa heshima za mwisho kwa wale ambao hawakuipata nafasi hiyo nyumbani.Zoezi hili lililazimika kusitishwa kutokana na idadi kubwa ya watu hivyo .Ibada ilichukua takribani saa moja halafu safari ya kuelekea makaburini kwa ajili ya kuhitimisha safari ya mwisho ya Vero ikaanza.Saa kumi za jioni waliwasili makaburini na ikafanyika ibada ya makaburini na taratibu mwili wa Vero ukashushwa kaburini.Lilikuwa ni tukio lililowafanya watu wengi wapoteze fahamu.Miongoni mwa watu waliopoteza fahamu alikuwa ni Loniki.Hii ilikuwa ni mara ya tatu katika siku hii kupoteza fahamu.Kifo hiki cha Vero kilikuwa kimemuumiza mno.
Familia na watu wa karibu wa marehemu wakatupa udongo kaburini na kisha likaanza zoezi la kulifunika kaburi.Baada ya zoezi lile lililofanywa na mafundi mahiri kukamilika ,yakawekwa mashada ya maua halafu Padre akalibariki kaburi na kisha watu wakatawanyika na kurejea msibani kwa ajili ya kuendelea na taratibu nyingine.Safari ya Vero duniani ikafikia mwisho.
 
Back
Top Bottom