Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,444
- Thread starter
- #41
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 28
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
" hapana Mike..Kwa sasa Happy amepumzika .Jambo hili lililomtokea ni jambo kubwa na zito kwa maana hiyo anahitaji kupewa muda wa kutosha ili aweze kutuliza kichwa chake...." akasema Margreth.
" Margreth naelewa kuna kitu unakifahamu lakini hutaki kuniambia.Kuna jambo gani linaendelea kimya kimya ?Na kwa nini hutaki kunieleza? Nimeyaona macho ya Happy pale kituo cha polisi na nimehisi kuna jambo amb........." Mike akakatishwa ghafla na Margreth.
" Mike tafadhali naomba uniache nipumzike.Nipigie baadae" Margreth akakakata simu.
" Jamani mbona happy ameleta mambo ! Mike anateseka sana kijana wa watu.Amekuja toka Marekani kwa lengo la kukaa na kufurahi na Happy lakini badala ya furaha imekuwa ni majonzi .Happy kwa nini umewatesa watu wengi namna hii? Kwa mara ya kwanza ninaona ingekuwa vyema kama wewe na Patrick msingekutana kabisa katika maisha yenu yaliyobakia" akawaza Margreth
ENDELEA………………..
Ni saa mbili za usiku bado Happy amejifungia chumbani kwake.Toka amerejea nyumbani hajatoka chumbani kwake na hajataka kuonana na mtu yeyote yule.usiku huu familia yake yote ilikuwa imekaa mezani ikijiandaa kwa ajili ya chakula cha usiku.
" Happy amekwisha taarifiwa kuja hapa mezani? akauliza mzee Kibaho baba yake Happy
" Nimejaribu kugonga mlango wake lakini amekataa kunifungulia.Nilipomgusia kuhusu suala la chakula amesema kwamba hasikii njaa.Nina wasi wasi sana na happy kwa sababu toka amerejea hapa nyumbani hajatia kitu chochote tumboni." akasema margreth.
" Ngoja nikamtoe huko chumbani.Asituumize vichwa huyu mtoto." akasema mama yake Happy akionekana kukasirika.
" hapana usiende..Ntakwenda mimi" akasema mzee Kibaho akainuka na kuelekea katika mlango wa chumba cha Happy akagonga mlango na kusema taratibu
" Happy mwanangu naomba unifungulie mlango nataka kuongea nawe." akasema mzee Kibaho.Happy hakujibu kitu.Mzee Kibaho akagonga tena mlango.
" Happy !! fungua mwanangu.."
Toka ndani ya chumba ikasikika sauti dhaifu ya Happy
" Daddy I want to be alone...I'm sorry"
" Happy nafahamu kwamba unahitaji nafasi ya kuwa peke yako lakini naomba niongee nawe dakika tatu tu"
Kikapita kimya kifupi mlango ukafunguliwa.Sura ya Happy ilikuwa imesawajika.Macho yake mazuri yalivimba na kuwa mekundu kwa kulia.Baba yake akashikwa na uchungu mwingi kwa hali ile aliyomkuta nayo mwanae akamkumbatia na kumfariji.
" Be strong my dear,you are going to be fine...you'll be ok" akasema mzee Kibaho huku akimpiga piga mwanae mgongoni .Kitendo kile kikaamsha tena kilio kwa Happy.Baba yake akamketisha katika sofa lililokuwamo mle chumbani na kumfuta machozi.
" Daddy why always me? akauliza Happy huku akilia.
" Happy mwanangu usilie ,usisikitike na wala kuhuzunika na kujiuliza kwa nini wewe? Nafahamu moyo unauma sana lakini naomba ufahamu kwamba matatizo tumeumbiwa sisi wanadamu na matatizo huja pasi na taarifa.Matatizo yanatukomaza na kutufanya tuwe majasiri hivyo kaza moyo mwanangu na yote yatakwisha.Sisi sote tuko pamoja nawe katika kipindi hiki kigumu kwako..we love you and we support you..."
Maneno yale ya mzee Kibaho yakamfariji sana Happy akafuta machozi .Mara akaingia mama yake akiwa na sahani iliyojaa chakula akaiweka mezani halafu akaenda kukaa pembeni ya Happy.
" Pole sana mwanangu.Huyu baradhuli anataka kukuharibia maisha yako..Kila nikikuona ninapatwa na hasira kali.Kwa nini atake kukusababishia matatizo makubwa namna hii? Ouh Happy mwanangu naomba umuogope kabisa kijana huyo..achana naye kabisa huyo shetani......."
Happy akayafikicha macho yake , akamtazama mama yake na kusema
" Mama tafadhali naomba usirudie tena kumtukana Patrick na kumuita shetani " akasema happy akionyesha kukerwa na kauli ile ya mama yake.
" Mwanangu ninaumia sana kukuona ukiwa katika hali hii.Nina hasira sana na huyo kijana ambaye ninamfananisha na shetani kwa sababu ametaka kukuingiza katika matatizo makubwa.Amesababisha ukalala polisi.Ameliharibu jina lako zuri.Happy mwanangu nakuomba uvunje kabisa urafiki na huyo kijana ..."
" Mom thats enough !!!..tafadhali naomba usiongee kitu ambacho hukifahamu..Naomba niwafahamishe wazazi wangu kwamba Patrick huyu ambaye mnasikia nilikuwa naye wakati tukio hilo linatokea ni yule yule ambaye alifungwa jela kwa ajili yangu.Patrick hakufa kama ilivyokuwa imezushwa."
Wazazi wake wakastuka sana kwa taarifa ile .Wakatazamana usoni. Happy akaendelea
"Katika tukio hilo naomba mfahamu kwamba ni mimi ndiye niliyemsukuma Veronika akajigonga ukutani na kupoteza maisha na wala si Patrick kama watu wanavyofahamu.Kwa kuniepusha mimi na adhabu ya kufungwa,kunyongwa au kifungo cha maisha jela,Patrick ameamua kuubeba yeye mzigo wote wa kesi hii na yeye kuonekana ndiye muuaji.Amefanya yote haya ili kuniweka mimi huru.I'm free now because of him..so this man doesnt deserve to be called a devil. Akasema Happy machozi yakaanza kumtiririka upya.
Hakuna aliyeongea tena wote wakaa kimya.Mzee Kibaho akambembeleza Happy ale chakula japo kidogo Happy akakubali akala chakula.Mama yake alikuwa ameshika tama akimtazama mwanae.
* * *
Ni saa tatu kasoro za usiku Savana alikuwa ndani ya chumba kimoja katika kituo cha polisi akizungumza na Patrick.
" Patrick kesho utapandishwa mahakamani kwa mara ya kwanza kusomewa shitaka halafu utapelekwa mahabusu katika gereza la Uwangwa. Hautaweza kupatiwa dhamana kutokana na uzito wa kosa lenyewe. Nasikitika sana Patrick kwa kupandishwa kizimbani lakini yote haya ni matakwa yako ...Lakini usijali nitatumia kila uwezo nilionao kuhakikisha kwamba unashinda kesi hii.." akasema Savana .Patrick akainama akafikiri kisha akasema
"Nashukuru sana Savana kwa msaada wako mkubwa.Jambo ulilonifanyia ni kubwa sana .Kuhakikisha kwamba Happy anaachiwa huru ni jambo kubwa sana kwangu." akasema Patrick huku akitabasamu
" Patrick mimi siwezi kupingana nawe katika maamuzi yako lakini bado nina mashaka sana na maamuzi uliyoyafanya ya kuamua kuubeba mzigo wa Happy..unafikiri yeye anakupenda kiasi cha kuweza kufanya kama ulivyofanya wewe?..anaweza kuyatoa maisha yake kwa ajili yako? akauliza Savana
" Ninamuamini Happy ananipenda na kwa hilo sina shaka naye.." akasema Patrick..
" Ndiyo unamuamini lakini una hakika kwamba anakupenda kiasi cha kuweza kuyatoa maisha yake kwa ajili yako? akauliza Savana.Patrick akanyamaza kimya.
" Patrick nimekuuliza makusudi swali hili kwa sababu wewe ni rafiki yangu,ninakujali na kukuthamini na ndiyo maana sitaki sadaka hii ya maisha yako uliyoitoa kwa ajili ya Happy iende bure..Nina wasi wasi sana lakini sitaki kuingilia masuala ya ndani ya moyo wako.Wewe ndiye mwamuzi wa maisha yako. Ninachotaka kukuhakikishia kwamba mimi na timu yangu tutasimama kidete na kwa uwezo wetu wote tulionao tutajitahidi kwa kila tuwezavyo kukutetea katika kesi hii..." akasema Savana na kuagana na Patrick akaondoka.Kichwa chake bado kilikuwa kizito mno kuhusiana na kesi hii ya Patrick.
" Patrick ananisikitisha sana .kila nikimuona ninaumia mno..kwa nini ayaweke maisha yake katika hatari kwa kosa la mtu mwingine? ..Patrick ni mtu wangu muhimu sana na nitafanya kila niwezalo ili kumsaidia ." akawaza Savana.
Saa tano za usiku Savana akawasili nyumbani kwake.Akashuka garini na kuelekea ndani.Msichana wake wa kazi alikuwepo sebuleni akimsubiri.Savana akasalimiana naye na kuelekea moja kwa moja chumbani kwake.Mumewe george tayari alikuwa amejilaza kitandani .Mara tu Savana alipoingia akamuendea George akamtikisa na George ambaye alikuwa ameanza kupitiwa na usingizi akaamka.Savana akambusu mumewe halafu akaelekea bafuni kaoga na kurejea kitandani.Akambusu mumewe na kugeukia upande wa pili tayari kwa kulala.
" Savana kuna jambo gani limekutokea katika siku hizi tatu? Nakuona umebadilika sana..Unachelewa kurudi na ukirudi unakuwa umechoka na hutaki hata kuongea na mimi tena.Una matatizo gani? George mume wa Savana akauliza
" George naomba uniache kwa sasa kichwa changu kina mambo mengi mazito" akasema Savana
" Savana naomba unisikilize.Mimi ni mumeo na nina haki ya kukuuliza .Siwezi kukuona ukichelewa kurudi nyumbani na hunielezi chochote .Huna tena muda na mimi mumeo.Unanipa wasi wasi sana Savana.Hebu angaliani hii ni saa ngapi unarejea nyumbani kama mke wa mtu? akauliza George ambaye alionekana kuanza kukasirika.
" George nina kesi ngumu ninayoisimamia kwa sasa .Patrick anashikiliwa kwa kosa la mauaji.." akasema Savana.
" Patrick !! akauliza George kwa mshangao.
" Ndiyo..Patrick..Ina maana hujasikia tukio lililotokea siku tatu zilizopita likimuhusisha Patrick na mauaji? akauliza Savana
" Patrick huyu ambaye aliwahi kuwa mpenzi wako? akauliza George
" Ndiye huyo...." akasema Savana.George akainuka na kumuangalia Savana usoni.
" Sasa nimepata picha halisi.Kumbe kuchelewa kote huku ni kwa ajili ya kesi ya aliyowahi kuwa mpenzi wako..Kwa maana hiyo yeye ni muhimu sana kuliko mimi mumeo ? akauliza George
" George tafadhali usiseme maneno hayo.Patrick ni rafiki yangu na mteja wangu vile vile kwa hiyo sina budi kuishughulikia kesi yake..Kuna tatizo gani kuisimamia kesi yake ? akasema Savana.
" Tatizo lipo..tena tatizo kubwa..Unasimamia kesi nyingi lakini hakuna hata siku moja umewahi kurejea nyumbani usiku kama huu..Yaani unamthamini Patrick ambaye ni muuaji kuliko hata mumeo? Lakini sioni kama ni jambo la ajabu kwa sababu nilihisi lazima jambo hili litatokea siku moja.Bado hujaweza kumtoa Patrick moyoni mwako.Pamoja na miaka hii yote kupita lakini bado hujafanikiwa kumtoa Patrick moyoni mwako..You still love him ...I'm so stupid" akasema George.Savana akainuka na kumtazama George kwa hasira
" George tafadhali naomba usiseme hivyo..Ndiyo niliwahi kuwa mpenzi wa Patrick lakini baada ya kukupata wewe nikaachana naye kwa sababu tayari yeye alikuwa na mpenzi wake Veronika.I'm with you now and not Patrick." akasema Savana
" Yes you are with me ..but am I in your heart? akauliza George
" george mambo gani hayo unayaongea leo? akauliza Savana.
" Savana nafahamu kabisa kwamba hujawahi kumsahau Patrick. Nimekununulia vito vingi vya thamani lakini mbona huvivai na unaendela kuvaa vile alivyokununulia Patrick? You still love him isnt it? akauliza George ambaye tayari alipandwa na hasira
" George ...!! akasema Savana.George akamkaribia Savana na kumuangalia usoni.
" Savana naomba uniangalie machoni na uniambie kwamba unanipenda na unanipenda mimi peke yangu.." akasema George.
" George mambo gani haya unayafanya? ...akauliza Savana
" Savana nimekuuliza swali mbona hunijibu? Huna jibu la kunipa?
Savana akabaki kimya akimtazama George huku akihema kwa nguvu.
" Nilijua tu.You never loved me.All this long you still love Patrick..." akasema George
" George hebu achana na hayo mawazo yako ya kijinga..You know I've always loved you..." akasema Savana.
" Do you love me Savana? Una hakika kwamba unanipenda? akauliza George
"yes I love you and you kow that" akajibu Savana
" Vizuri..sasa kama kweli unanipenda naomba ufanye yafuatayo..Nataka uachane kabisa na kusimamia kesi ya Patrick..Kama kweli mimi ni mumeo na unanipenda nataka uachane na ukae mbali kabisa na kesi hii" akasema George.Savana akainama akafikiri kisha akainua uso wake.macho yake yalijaa machozi.Akamuangalia George usoni kisha akatikisa kichwa.
"I'm sorry George I cant do that..siwezi kufanya hivyo unavyotaka nifanye...Patrick is my friend and he needs me now more than ever..siwezi kuacha kumtetea hata iweje.akasema Savana.George akamuangalia kwa makini usoni kisha akasema.
" Vizuri..huwezi kuacha kumtetea kwa sababu unampenda .Kama hivyo ndivyo naona ni bora nikuache huru uendelee kumtetea Patrick ashinde kesi na uje uishi naye hapa.Mimi nimechoshwa na vituko vyako Savana.Toka tumeanza kuishi pamoja mpaka leo hii ni vituko kila siku..Ni miaka mingapi mpaka leo na hutaki hata kusikia suala la mtoto? Nimechoka Savana.Nakuacha uendelee na huyo Patrick." akasema George huku akivaa nguo zake.Savana akasimama na kumuangalia George kwa macho makali.
" Mimi naondoka Savana..nitakuja kuchukua vitu vyangu kesho..Siwezi kuendelea kuishi nawe wakati moyo wako unampenda mtu mwingine..Siwezi kuendelea kugombania nafasi katika moyo wako..nafasi ambayo tayari amekwisha pewa mtu mwingine.Nimevumilia mengi na ninashukuru kwa kupata jibu leo kwamba chanzo cha haya yote ni Patrick..Nakutakia maisha mema na huyo mhalifu wako...." akasema George
" Dont you dare insult Patrick again infront of me...kwa taarifa yako ninampenda Patrick na nitafanya kila niwezalo niwe naye tena..You are nothing compared to him." akasema Savana kwa hasira..George akakasirika na kutaka kumnasa Savana kibao
" ukijaribu kunigusa nitahakikisha unaozea gerezani...." Savana akamtisha George ambaye alimuangalia kwa hasira kisha akaanza kuondoka.Savana machozi yakamtoka akajitupa kitandani kwa hasira
" Patrick siwezi kukuacha hasa kwa kipindi hiki..Niko tayari kwa lolote lile lakini si kuacha kukutetea..Hakuna mtu yeyote ambaye atanizuia nisikutetee ..Nitasimama nawe hadi dakika ya mwisho .That bastard George is right.sijaweza kukutoa katika moyo wangu hadi leo hii..I still love you so much Patrick.I'll make you love me Patrick and when this is over you'll be mine" akawaza Savana.
* * *
Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu ilifurika watu waliokuja kufuatilia kesi ya mauaji inayomkabili Patrick.Taarifa za Patrick kupandishwa kizimbani na kusomewa shitaka la mauaji zilisambaa kwa kasi na kupelekea idadi kubwa ya watu kujaa mahakamani .Patrick hakuwa mtu anayefahamika sana lakini kutokana na vyombo vya habari hususani magazeti kuandika habari ya tukio lile la kusababisha kifo watu wengi walitaka kumfahamu na hasa baada ya kuandikwa kwamba alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mrembo aliyeitikisa nchi kwa uzuri wake Miss Tanzania Happy kibaho.
Saa tano za asubuhi gari mbili za polisi zikawasili katika mahakama ya kisutu.Patrick akashushwa garini na kuingizwa mahakamani chini ya ulinzi mkali.Savana na jopo la mawakili wanaomtetea Patrick tayari walikwisha fika mahakamani kuanzia asubuhi .Siku hii Savana alionekana mkimya na mwenye mawazo mengi.
" Happy amekuja leo? Patrick akamuuliza Savana wakati wakisubiri kesi yake itajwe.
" Mpaka mida hii sijamuona bado .Inawezekana amefika lakini amejificha mahala akiogopa waandishi wa habari " akasema Savana.
"Ukifanikiwa kuonana naye mpe salamu zangu" akasema Patrick.
" masikini Patrick amejibebebsha mzigo mzito ambao si wake.Sina hakika kama happy anafahamu uzito wa mzigo huu alioubeba Patrick kwa ajili yake." akawaza Savana.
" Savana umefuatilia maendeleo ya baba yangu kule hospitali na kujua anaendeleaje? akauliza Patrick
" Hapana Patrick bado sijafuatilia lakini leo nikitoka hapa nitaelekea hospitali kwenda kumjulia hali baba yako": akasema Savana.
" Nimesababisha matatizo kwa watu wengi . Vero amefariki,baba yangu amelazwa hospitali ,na wengine wengi wameumia sana kwa ajili ya maamuzi yangu. I deserve this..ninastahili adhabu hii ya kukaa gerezani" akasema Patrick kwa sauti ndogo.Savana hakumjibu kitu bali akachukua faili lake na kuanza kumuelekeza Patrick jambo fulani.
Hatimaye kesi ya kusababisha kifo inayomkabili Patrick ikatajwa kwa mara ya kwanza .Mshitakiwa katika kesi hiyo ambaye ni Patrick akasomewa shitaka la kusababisha kifo cha Veronika na hakutakiwa kujibu chochote.Kesi ikapangwa kutajwa tena baada ya wiki tatu na mshitakiwa akaamriwa kupelekwa mahabusu katika gereza jipya la Uwangwa kigamboni.
" Usihofu Patrick .Kesi hii tunaifuatilia kwa umakini mkubwa .Niko pamoja nawe katika kila dakika.Naomba uondoe hofu na uniamini " .Akasema Savana akimpa moyo Patrick wakati akisubiri kupanda katika basi maalum la kubebea mahabusu na kupelekwa gerezani.
" Nakuamini Savana na sina shaka hata kidogo na wewe.Ulifanikiwa kuonana na Happy? akauliza Patrick
" happy sijaonana naye .Nadhani hajafika mahakamani siku ya leo" akasema Savana.
" Una mawasiliano yake" akauliza Patrick
" Nina namba za simu za mdogo wake Margreth.Nitampigia baadae nifahamu maendeleo yake" akasema Savana .Muda huo huo akaingia mmoja wa mawakili wanaounda jopo la kumteta Patrick akamuomba Savana waongozane kuna suala la kisheria linalohitaji ufumbuzi wa haraka.Savana akaagana na Patrick kwa ahadi ya kwenda kumtembelea gerezani kesho yake.
" kwa nini Happy hajafika mahakamani? Ana matatizo gani?Pengine ameshindwa kufika akiogopa macho ya watu " akawaza Patrick baada ya Savana kuondoka.
" Mama ,ndugu zangu na marafiki nimewaona mahakamani .Wote wamekuja kunifariji na kunipa moyo.Japokuwa nimewaudhi na kuwaumiza sana kwa mambo niliyoyafanya lakini bado wananipenda na wamekuja kunionyesha kwamba bado tuko pamoja.Ni familia ya Happy pekee ambayo haijafika mahakamani.Napatwa na wasi wasi nini kimetokea? I love Happy and I trust her with my life.." akawaza Patrick na mara sura ya Veronika ikamjia kichwani akafumba macho na kuuma meno.
" masikini Veronika sina taarifa atazikwa lini.Laiti nigekuwa na uwezo ningehudhuria mazishi yake lakini siwezi tena.Niko mikononi mwa sheria.Pumzika kwa amani vero.Utabaki ndani ya moyo wangu daima.Nitazikumbuka zile nyakati zote za furaha tulizowahi kuwa nazo katika mapenzi yetu. Daima nitaukumbuka upendo wako,ukarimu na ucheshi wako.Natambua ulinipenda kwa moyo wako wote.Kama siku moja nitabahatika kutoka gerezani nitalitafuta kaburi lako na kuweka maua meupe uliyokuwa unayapenda sana enzi za uhai wako,lakini kama nitahukumiwa kunyongwa au kufungwa maisha basi tutakutana mbinguni kwa baba.Pumzika kwa amani Veronika sikutegema kabisa kama mambo yangekuwa namna hii." akawaza Patrick huku akijizuia asidondoshe machozi.
Saa nane za mchana Patrick akapakiwa katika basi maalum la kubebea mahabusu na safari ya kuelekea gereza la Uwangwa ikaanza.Taratibu basi likaanza kuondoka.Kupitia dirishani Patrick akaweza kumuona mama yake ambaye alikuwa amekaa chini kutokana na kuishiwa nguvu,kaka yake Alois akiwa na mkewe,rafiki yake Andrew akiwa na mchumba wake Vick pamoja na ndugu wengine,na marafiki.Wengi walikuwa na nyuso za huzuni kubwa na wengie walishindwa kujizuia kutokwa na machozi.
Patrick akawapungia mkono na taratibu basi likaondoka maeneo ya mahakama kuelekea mahabusu katika gereza la Uwangwa ambako anakwenda kuanza maisha mapya.
SEHEMU YA 28
MTUNZI😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
" hapana Mike..Kwa sasa Happy amepumzika .Jambo hili lililomtokea ni jambo kubwa na zito kwa maana hiyo anahitaji kupewa muda wa kutosha ili aweze kutuliza kichwa chake...." akasema Margreth.
" Margreth naelewa kuna kitu unakifahamu lakini hutaki kuniambia.Kuna jambo gani linaendelea kimya kimya ?Na kwa nini hutaki kunieleza? Nimeyaona macho ya Happy pale kituo cha polisi na nimehisi kuna jambo amb........." Mike akakatishwa ghafla na Margreth.
" Mike tafadhali naomba uniache nipumzike.Nipigie baadae" Margreth akakakata simu.
" Jamani mbona happy ameleta mambo ! Mike anateseka sana kijana wa watu.Amekuja toka Marekani kwa lengo la kukaa na kufurahi na Happy lakini badala ya furaha imekuwa ni majonzi .Happy kwa nini umewatesa watu wengi namna hii? Kwa mara ya kwanza ninaona ingekuwa vyema kama wewe na Patrick msingekutana kabisa katika maisha yenu yaliyobakia" akawaza Margreth
ENDELEA………………..
Ni saa mbili za usiku bado Happy amejifungia chumbani kwake.Toka amerejea nyumbani hajatoka chumbani kwake na hajataka kuonana na mtu yeyote yule.usiku huu familia yake yote ilikuwa imekaa mezani ikijiandaa kwa ajili ya chakula cha usiku.
" Happy amekwisha taarifiwa kuja hapa mezani? akauliza mzee Kibaho baba yake Happy
" Nimejaribu kugonga mlango wake lakini amekataa kunifungulia.Nilipomgusia kuhusu suala la chakula amesema kwamba hasikii njaa.Nina wasi wasi sana na happy kwa sababu toka amerejea hapa nyumbani hajatia kitu chochote tumboni." akasema margreth.
" Ngoja nikamtoe huko chumbani.Asituumize vichwa huyu mtoto." akasema mama yake Happy akionekana kukasirika.
" hapana usiende..Ntakwenda mimi" akasema mzee Kibaho akainuka na kuelekea katika mlango wa chumba cha Happy akagonga mlango na kusema taratibu
" Happy mwanangu naomba unifungulie mlango nataka kuongea nawe." akasema mzee Kibaho.Happy hakujibu kitu.Mzee Kibaho akagonga tena mlango.
" Happy !! fungua mwanangu.."
Toka ndani ya chumba ikasikika sauti dhaifu ya Happy
" Daddy I want to be alone...I'm sorry"
" Happy nafahamu kwamba unahitaji nafasi ya kuwa peke yako lakini naomba niongee nawe dakika tatu tu"
Kikapita kimya kifupi mlango ukafunguliwa.Sura ya Happy ilikuwa imesawajika.Macho yake mazuri yalivimba na kuwa mekundu kwa kulia.Baba yake akashikwa na uchungu mwingi kwa hali ile aliyomkuta nayo mwanae akamkumbatia na kumfariji.
" Be strong my dear,you are going to be fine...you'll be ok" akasema mzee Kibaho huku akimpiga piga mwanae mgongoni .Kitendo kile kikaamsha tena kilio kwa Happy.Baba yake akamketisha katika sofa lililokuwamo mle chumbani na kumfuta machozi.
" Daddy why always me? akauliza Happy huku akilia.
" Happy mwanangu usilie ,usisikitike na wala kuhuzunika na kujiuliza kwa nini wewe? Nafahamu moyo unauma sana lakini naomba ufahamu kwamba matatizo tumeumbiwa sisi wanadamu na matatizo huja pasi na taarifa.Matatizo yanatukomaza na kutufanya tuwe majasiri hivyo kaza moyo mwanangu na yote yatakwisha.Sisi sote tuko pamoja nawe katika kipindi hiki kigumu kwako..we love you and we support you..."
Maneno yale ya mzee Kibaho yakamfariji sana Happy akafuta machozi .Mara akaingia mama yake akiwa na sahani iliyojaa chakula akaiweka mezani halafu akaenda kukaa pembeni ya Happy.
" Pole sana mwanangu.Huyu baradhuli anataka kukuharibia maisha yako..Kila nikikuona ninapatwa na hasira kali.Kwa nini atake kukusababishia matatizo makubwa namna hii? Ouh Happy mwanangu naomba umuogope kabisa kijana huyo..achana naye kabisa huyo shetani......."
Happy akayafikicha macho yake , akamtazama mama yake na kusema
" Mama tafadhali naomba usirudie tena kumtukana Patrick na kumuita shetani " akasema happy akionyesha kukerwa na kauli ile ya mama yake.
" Mwanangu ninaumia sana kukuona ukiwa katika hali hii.Nina hasira sana na huyo kijana ambaye ninamfananisha na shetani kwa sababu ametaka kukuingiza katika matatizo makubwa.Amesababisha ukalala polisi.Ameliharibu jina lako zuri.Happy mwanangu nakuomba uvunje kabisa urafiki na huyo kijana ..."
" Mom thats enough !!!..tafadhali naomba usiongee kitu ambacho hukifahamu..Naomba niwafahamishe wazazi wangu kwamba Patrick huyu ambaye mnasikia nilikuwa naye wakati tukio hilo linatokea ni yule yule ambaye alifungwa jela kwa ajili yangu.Patrick hakufa kama ilivyokuwa imezushwa."
Wazazi wake wakastuka sana kwa taarifa ile .Wakatazamana usoni. Happy akaendelea
"Katika tukio hilo naomba mfahamu kwamba ni mimi ndiye niliyemsukuma Veronika akajigonga ukutani na kupoteza maisha na wala si Patrick kama watu wanavyofahamu.Kwa kuniepusha mimi na adhabu ya kufungwa,kunyongwa au kifungo cha maisha jela,Patrick ameamua kuubeba yeye mzigo wote wa kesi hii na yeye kuonekana ndiye muuaji.Amefanya yote haya ili kuniweka mimi huru.I'm free now because of him..so this man doesnt deserve to be called a devil. Akasema Happy machozi yakaanza kumtiririka upya.
Hakuna aliyeongea tena wote wakaa kimya.Mzee Kibaho akambembeleza Happy ale chakula japo kidogo Happy akakubali akala chakula.Mama yake alikuwa ameshika tama akimtazama mwanae.
* * *
Ni saa tatu kasoro za usiku Savana alikuwa ndani ya chumba kimoja katika kituo cha polisi akizungumza na Patrick.
" Patrick kesho utapandishwa mahakamani kwa mara ya kwanza kusomewa shitaka halafu utapelekwa mahabusu katika gereza la Uwangwa. Hautaweza kupatiwa dhamana kutokana na uzito wa kosa lenyewe. Nasikitika sana Patrick kwa kupandishwa kizimbani lakini yote haya ni matakwa yako ...Lakini usijali nitatumia kila uwezo nilionao kuhakikisha kwamba unashinda kesi hii.." akasema Savana .Patrick akainama akafikiri kisha akasema
"Nashukuru sana Savana kwa msaada wako mkubwa.Jambo ulilonifanyia ni kubwa sana .Kuhakikisha kwamba Happy anaachiwa huru ni jambo kubwa sana kwangu." akasema Patrick huku akitabasamu
" Patrick mimi siwezi kupingana nawe katika maamuzi yako lakini bado nina mashaka sana na maamuzi uliyoyafanya ya kuamua kuubeba mzigo wa Happy..unafikiri yeye anakupenda kiasi cha kuweza kufanya kama ulivyofanya wewe?..anaweza kuyatoa maisha yake kwa ajili yako? akauliza Savana
" Ninamuamini Happy ananipenda na kwa hilo sina shaka naye.." akasema Patrick..
" Ndiyo unamuamini lakini una hakika kwamba anakupenda kiasi cha kuweza kuyatoa maisha yake kwa ajili yako? akauliza Savana.Patrick akanyamaza kimya.
" Patrick nimekuuliza makusudi swali hili kwa sababu wewe ni rafiki yangu,ninakujali na kukuthamini na ndiyo maana sitaki sadaka hii ya maisha yako uliyoitoa kwa ajili ya Happy iende bure..Nina wasi wasi sana lakini sitaki kuingilia masuala ya ndani ya moyo wako.Wewe ndiye mwamuzi wa maisha yako. Ninachotaka kukuhakikishia kwamba mimi na timu yangu tutasimama kidete na kwa uwezo wetu wote tulionao tutajitahidi kwa kila tuwezavyo kukutetea katika kesi hii..." akasema Savana na kuagana na Patrick akaondoka.Kichwa chake bado kilikuwa kizito mno kuhusiana na kesi hii ya Patrick.
" Patrick ananisikitisha sana .kila nikimuona ninaumia mno..kwa nini ayaweke maisha yake katika hatari kwa kosa la mtu mwingine? ..Patrick ni mtu wangu muhimu sana na nitafanya kila niwezalo ili kumsaidia ." akawaza Savana.
Saa tano za usiku Savana akawasili nyumbani kwake.Akashuka garini na kuelekea ndani.Msichana wake wa kazi alikuwepo sebuleni akimsubiri.Savana akasalimiana naye na kuelekea moja kwa moja chumbani kwake.Mumewe george tayari alikuwa amejilaza kitandani .Mara tu Savana alipoingia akamuendea George akamtikisa na George ambaye alikuwa ameanza kupitiwa na usingizi akaamka.Savana akambusu mumewe halafu akaelekea bafuni kaoga na kurejea kitandani.Akambusu mumewe na kugeukia upande wa pili tayari kwa kulala.
" Savana kuna jambo gani limekutokea katika siku hizi tatu? Nakuona umebadilika sana..Unachelewa kurudi na ukirudi unakuwa umechoka na hutaki hata kuongea na mimi tena.Una matatizo gani? George mume wa Savana akauliza
" George naomba uniache kwa sasa kichwa changu kina mambo mengi mazito" akasema Savana
" Savana naomba unisikilize.Mimi ni mumeo na nina haki ya kukuuliza .Siwezi kukuona ukichelewa kurudi nyumbani na hunielezi chochote .Huna tena muda na mimi mumeo.Unanipa wasi wasi sana Savana.Hebu angaliani hii ni saa ngapi unarejea nyumbani kama mke wa mtu? akauliza George ambaye alionekana kuanza kukasirika.
" George nina kesi ngumu ninayoisimamia kwa sasa .Patrick anashikiliwa kwa kosa la mauaji.." akasema Savana.
" Patrick !! akauliza George kwa mshangao.
" Ndiyo..Patrick..Ina maana hujasikia tukio lililotokea siku tatu zilizopita likimuhusisha Patrick na mauaji? akauliza Savana
" Patrick huyu ambaye aliwahi kuwa mpenzi wako? akauliza George
" Ndiye huyo...." akasema Savana.George akainuka na kumuangalia Savana usoni.
" Sasa nimepata picha halisi.Kumbe kuchelewa kote huku ni kwa ajili ya kesi ya aliyowahi kuwa mpenzi wako..Kwa maana hiyo yeye ni muhimu sana kuliko mimi mumeo ? akauliza George
" George tafadhali usiseme maneno hayo.Patrick ni rafiki yangu na mteja wangu vile vile kwa hiyo sina budi kuishughulikia kesi yake..Kuna tatizo gani kuisimamia kesi yake ? akasema Savana.
" Tatizo lipo..tena tatizo kubwa..Unasimamia kesi nyingi lakini hakuna hata siku moja umewahi kurejea nyumbani usiku kama huu..Yaani unamthamini Patrick ambaye ni muuaji kuliko hata mumeo? Lakini sioni kama ni jambo la ajabu kwa sababu nilihisi lazima jambo hili litatokea siku moja.Bado hujaweza kumtoa Patrick moyoni mwako.Pamoja na miaka hii yote kupita lakini bado hujafanikiwa kumtoa Patrick moyoni mwako..You still love him ...I'm so stupid" akasema George.Savana akainuka na kumtazama George kwa hasira
" George tafadhali naomba usiseme hivyo..Ndiyo niliwahi kuwa mpenzi wa Patrick lakini baada ya kukupata wewe nikaachana naye kwa sababu tayari yeye alikuwa na mpenzi wake Veronika.I'm with you now and not Patrick." akasema Savana
" Yes you are with me ..but am I in your heart? akauliza George
" george mambo gani hayo unayaongea leo? akauliza Savana.
" Savana nafahamu kabisa kwamba hujawahi kumsahau Patrick. Nimekununulia vito vingi vya thamani lakini mbona huvivai na unaendela kuvaa vile alivyokununulia Patrick? You still love him isnt it? akauliza George ambaye tayari alipandwa na hasira
" George ...!! akasema Savana.George akamkaribia Savana na kumuangalia usoni.
" Savana naomba uniangalie machoni na uniambie kwamba unanipenda na unanipenda mimi peke yangu.." akasema George.
" George mambo gani haya unayafanya? ...akauliza Savana
" Savana nimekuuliza swali mbona hunijibu? Huna jibu la kunipa?
Savana akabaki kimya akimtazama George huku akihema kwa nguvu.
" Nilijua tu.You never loved me.All this long you still love Patrick..." akasema George
" George hebu achana na hayo mawazo yako ya kijinga..You know I've always loved you..." akasema Savana.
" Do you love me Savana? Una hakika kwamba unanipenda? akauliza George
"yes I love you and you kow that" akajibu Savana
" Vizuri..sasa kama kweli unanipenda naomba ufanye yafuatayo..Nataka uachane kabisa na kusimamia kesi ya Patrick..Kama kweli mimi ni mumeo na unanipenda nataka uachane na ukae mbali kabisa na kesi hii" akasema George.Savana akainama akafikiri kisha akainua uso wake.macho yake yalijaa machozi.Akamuangalia George usoni kisha akatikisa kichwa.
"I'm sorry George I cant do that..siwezi kufanya hivyo unavyotaka nifanye...Patrick is my friend and he needs me now more than ever..siwezi kuacha kumtetea hata iweje.akasema Savana.George akamuangalia kwa makini usoni kisha akasema.
" Vizuri..huwezi kuacha kumtetea kwa sababu unampenda .Kama hivyo ndivyo naona ni bora nikuache huru uendelee kumtetea Patrick ashinde kesi na uje uishi naye hapa.Mimi nimechoshwa na vituko vyako Savana.Toka tumeanza kuishi pamoja mpaka leo hii ni vituko kila siku..Ni miaka mingapi mpaka leo na hutaki hata kusikia suala la mtoto? Nimechoka Savana.Nakuacha uendelee na huyo Patrick." akasema George huku akivaa nguo zake.Savana akasimama na kumuangalia George kwa macho makali.
" Mimi naondoka Savana..nitakuja kuchukua vitu vyangu kesho..Siwezi kuendelea kuishi nawe wakati moyo wako unampenda mtu mwingine..Siwezi kuendelea kugombania nafasi katika moyo wako..nafasi ambayo tayari amekwisha pewa mtu mwingine.Nimevumilia mengi na ninashukuru kwa kupata jibu leo kwamba chanzo cha haya yote ni Patrick..Nakutakia maisha mema na huyo mhalifu wako...." akasema George
" Dont you dare insult Patrick again infront of me...kwa taarifa yako ninampenda Patrick na nitafanya kila niwezalo niwe naye tena..You are nothing compared to him." akasema Savana kwa hasira..George akakasirika na kutaka kumnasa Savana kibao
" ukijaribu kunigusa nitahakikisha unaozea gerezani...." Savana akamtisha George ambaye alimuangalia kwa hasira kisha akaanza kuondoka.Savana machozi yakamtoka akajitupa kitandani kwa hasira
" Patrick siwezi kukuacha hasa kwa kipindi hiki..Niko tayari kwa lolote lile lakini si kuacha kukutetea..Hakuna mtu yeyote ambaye atanizuia nisikutetee ..Nitasimama nawe hadi dakika ya mwisho .That bastard George is right.sijaweza kukutoa katika moyo wangu hadi leo hii..I still love you so much Patrick.I'll make you love me Patrick and when this is over you'll be mine" akawaza Savana.
* * *
Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu ilifurika watu waliokuja kufuatilia kesi ya mauaji inayomkabili Patrick.Taarifa za Patrick kupandishwa kizimbani na kusomewa shitaka la mauaji zilisambaa kwa kasi na kupelekea idadi kubwa ya watu kujaa mahakamani .Patrick hakuwa mtu anayefahamika sana lakini kutokana na vyombo vya habari hususani magazeti kuandika habari ya tukio lile la kusababisha kifo watu wengi walitaka kumfahamu na hasa baada ya kuandikwa kwamba alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mrembo aliyeitikisa nchi kwa uzuri wake Miss Tanzania Happy kibaho.
Saa tano za asubuhi gari mbili za polisi zikawasili katika mahakama ya kisutu.Patrick akashushwa garini na kuingizwa mahakamani chini ya ulinzi mkali.Savana na jopo la mawakili wanaomtetea Patrick tayari walikwisha fika mahakamani kuanzia asubuhi .Siku hii Savana alionekana mkimya na mwenye mawazo mengi.
" Happy amekuja leo? Patrick akamuuliza Savana wakati wakisubiri kesi yake itajwe.
" Mpaka mida hii sijamuona bado .Inawezekana amefika lakini amejificha mahala akiogopa waandishi wa habari " akasema Savana.
"Ukifanikiwa kuonana naye mpe salamu zangu" akasema Patrick.
" masikini Patrick amejibebebsha mzigo mzito ambao si wake.Sina hakika kama happy anafahamu uzito wa mzigo huu alioubeba Patrick kwa ajili yake." akawaza Savana.
" Savana umefuatilia maendeleo ya baba yangu kule hospitali na kujua anaendeleaje? akauliza Patrick
" Hapana Patrick bado sijafuatilia lakini leo nikitoka hapa nitaelekea hospitali kwenda kumjulia hali baba yako": akasema Savana.
" Nimesababisha matatizo kwa watu wengi . Vero amefariki,baba yangu amelazwa hospitali ,na wengine wengi wameumia sana kwa ajili ya maamuzi yangu. I deserve this..ninastahili adhabu hii ya kukaa gerezani" akasema Patrick kwa sauti ndogo.Savana hakumjibu kitu bali akachukua faili lake na kuanza kumuelekeza Patrick jambo fulani.
Hatimaye kesi ya kusababisha kifo inayomkabili Patrick ikatajwa kwa mara ya kwanza .Mshitakiwa katika kesi hiyo ambaye ni Patrick akasomewa shitaka la kusababisha kifo cha Veronika na hakutakiwa kujibu chochote.Kesi ikapangwa kutajwa tena baada ya wiki tatu na mshitakiwa akaamriwa kupelekwa mahabusu katika gereza jipya la Uwangwa kigamboni.
" Usihofu Patrick .Kesi hii tunaifuatilia kwa umakini mkubwa .Niko pamoja nawe katika kila dakika.Naomba uondoe hofu na uniamini " .Akasema Savana akimpa moyo Patrick wakati akisubiri kupanda katika basi maalum la kubebea mahabusu na kupelekwa gerezani.
" Nakuamini Savana na sina shaka hata kidogo na wewe.Ulifanikiwa kuonana na Happy? akauliza Patrick
" happy sijaonana naye .Nadhani hajafika mahakamani siku ya leo" akasema Savana.
" Una mawasiliano yake" akauliza Patrick
" Nina namba za simu za mdogo wake Margreth.Nitampigia baadae nifahamu maendeleo yake" akasema Savana .Muda huo huo akaingia mmoja wa mawakili wanaounda jopo la kumteta Patrick akamuomba Savana waongozane kuna suala la kisheria linalohitaji ufumbuzi wa haraka.Savana akaagana na Patrick kwa ahadi ya kwenda kumtembelea gerezani kesho yake.
" kwa nini Happy hajafika mahakamani? Ana matatizo gani?Pengine ameshindwa kufika akiogopa macho ya watu " akawaza Patrick baada ya Savana kuondoka.
" Mama ,ndugu zangu na marafiki nimewaona mahakamani .Wote wamekuja kunifariji na kunipa moyo.Japokuwa nimewaudhi na kuwaumiza sana kwa mambo niliyoyafanya lakini bado wananipenda na wamekuja kunionyesha kwamba bado tuko pamoja.Ni familia ya Happy pekee ambayo haijafika mahakamani.Napatwa na wasi wasi nini kimetokea? I love Happy and I trust her with my life.." akawaza Patrick na mara sura ya Veronika ikamjia kichwani akafumba macho na kuuma meno.
" masikini Veronika sina taarifa atazikwa lini.Laiti nigekuwa na uwezo ningehudhuria mazishi yake lakini siwezi tena.Niko mikononi mwa sheria.Pumzika kwa amani vero.Utabaki ndani ya moyo wangu daima.Nitazikumbuka zile nyakati zote za furaha tulizowahi kuwa nazo katika mapenzi yetu. Daima nitaukumbuka upendo wako,ukarimu na ucheshi wako.Natambua ulinipenda kwa moyo wako wote.Kama siku moja nitabahatika kutoka gerezani nitalitafuta kaburi lako na kuweka maua meupe uliyokuwa unayapenda sana enzi za uhai wako,lakini kama nitahukumiwa kunyongwa au kufungwa maisha basi tutakutana mbinguni kwa baba.Pumzika kwa amani Veronika sikutegema kabisa kama mambo yangekuwa namna hii." akawaza Patrick huku akijizuia asidondoshe machozi.
Saa nane za mchana Patrick akapakiwa katika basi maalum la kubebea mahabusu na safari ya kuelekea gereza la Uwangwa ikaanza.Taratibu basi likaanza kuondoka.Kupitia dirishani Patrick akaweza kumuona mama yake ambaye alikuwa amekaa chini kutokana na kuishiwa nguvu,kaka yake Alois akiwa na mkewe,rafiki yake Andrew akiwa na mchumba wake Vick pamoja na ndugu wengine,na marafiki.Wengi walikuwa na nyuso za huzuni kubwa na wengie walishindwa kujizuia kutokwa na machozi.
Patrick akawapungia mkono na taratibu basi likaondoka maeneo ya mahakama kuelekea mahabusu katika gereza la Uwangwa ambako anakwenda kuanza maisha mapya.

