Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,444
- Thread starter
- #61
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 38
MTUNZI 😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Jeneza likashushwa garini na kuingizwa kanisani na kabla ya kuanza kwa ibada ikatolewa tena nafasi nyingine ya kutoa heshima za mwisho kwa wale ambao hawakuipata nafasi hiyo nyumbani.Zoezi hili lililazimika kusitishwa kutokana na idadi kubwa ya watu hivyo .Ibada ilichukua takribani saa moja halafu safari ya kuelekea makaburini kwa ajili ya kuhitimisha safari ya mwisho ya Vero ikaanza.Saa kumi za jioni waliwasili makaburini na ikafanyika ibada ya makaburini na taratibu mwili wa Vero ukashushwa kaburini.Lilikuwa ni tukio lililowafanya watu wengi wapoteze fahamu.Miongoni mwa watu waliopoteza fahamu alikuwa ni Loniki.Hii ilikuwa ni mara ya tatu katika siku hii kupoteza fahamu.Kifo hiki cha Vero kilikuwa kimemuumiza mno.
Familia na watu wa karibu wa marehemu wakatupa udongo kaburini na kisha likaanza zoezi la kulifunika kaburi.Baada ya zoezi lile lililofanywa na mafundi mahiri kukamilika ,yakawekwa mashada ya maua halafu Padre akalibariki kaburi na kisha watu wakatawanyika na kurejea msibani kwa ajili ya kuendelea na taratibu nyingine.Safari ya Vero duniani ikafikia mwisho.
ENDELEA………………
“Andrew ninaondoka ,ninahitaji kuonana na Happy jioni hii” akasema Savanna muda mfupi tu baada ya kurejea nyumbani kwa akina Patrick wakitokea katika mazishi ya Vero
“Sawa Savanna.Tutaonana kesho.Patrick anafahamu kama baba yake anazikwa kesho?
“Sina hakika kama anafahamu ,lakini nitamfahamisha nitakapomtembelea kesho asubuhi.”
“Ukionana naye kesho mpe salamu zangu nyingi.Nitakwenda kumtembelea baada ya kumalizika kwa shughuli hizi za msiba wa mzee” akasema Andrew kisha Savanna akaingia garini na kuondoka kuelekea nyumbani kwa akina Happy.
“Kwa kweli hata mimi niliumia sana katika mazishi ya Vero.She was so pretty.Maskini Vero,amekufa na uzuri wake.Happy alistahili adhabu kwa kosa alilolifanya.Sielewi ni kwa nini Patrick ameamua kujitwisha yeye mzigo huu mzito ambao hakuustahili” akawaza Savanna akiwa njiani kuelekea kwa akina Happy
“Hata hivyo nitamsaidia Patrick kwa kila namna nitakavyoweza na atashinda hii kesi.Ninayafanya haya yote kwa sababu ya upendo wangu kwake.Ninampenda sana Patrick.Toka tulipoamua kusitisha mahusiano yetu baada ya mimi kumpata George ,bado sijaweza kabisa kumtoa Patrick moyoni mwangu.Hii ni nafasi yangu ya kumrudisha tena Patrick kwangu.Nitashinda hii kesi na Patrick lazima awe wangu tena.Happy hastahili kuwa na Patrick tena.” Akaendelea kuwaza Savanna.
Jua tayari lilikwisha punguza nuru yake kuashiria kwamba muda wowote litazama kulipisha giza lichukue nafasi yake.Savanna akafika nyumbani kwa akina Happy akafunguliwa geti na kuingia ndani.Akapokewa na mtumishi wa ndani
“Happy nimemkuta? Akauliza Savanna
“Ndiyo umemkuta.Karibu ndani ngoja nikamuite” akasema Yule msichana na kuelekea chumbani kwa Happy akamtaarifu kwamba Savanna amekwisha fika.Happy akatoka chumbani kwake na kuelekea sebuleni
“Karibu sana Savanna.” Akasema Happy huku akitabasamu
“Nashukuru sana Happy.Unaendeleaje?
“Ninaendelea vizuri Savanna.Namshukuru Mungu kwani ninazidi kupata nguvu kila siku”
“Nafurahi kusikia hivyo Happy.Ni jambo la faraja sana kuona hali yako inaboreka siku hadi siku” akasema Savanna.Kikapita kimya kifupi halafu Savanna akasema
“Happy ,nilisikia kwamba umelivua taji la Miss Tanzania..”
“Ndiyo Savanna.Niliamua kulivua taji lile ili kuendelea kulipa heshima yake kwa sababu kila neno baya lilikuwa linasemwa kwa kutanguliwa na miss Tanzania badala ya Happy.Nilifikiria na kuona haitakuwa busara kama taji la miss Tanzania likaendelea kuchafuliwa. Nikaona ni bora nilivue.”
“Pole Happy.Haya yalikuwa ni maamuzi magumu sana”
“Nimekwisha poa Savanna.Sikuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya kulirudisha taji lile.” Akasema Happy
“Nimetoka katika mazishi ya Vero.Mimi na Andrew tuliiwakilisha familia ya Patrick katika mazishi.” Akasema Savanna.Happy hakujibu kitu akainama chini
“Happy nimepita mara moja kukuona kama ulivyokuwa umeomba.” Akasema Savanna ,Happy akainua kichwa.
“Samahani Savanna kwa kukusumbua.Ni kweli nilihitaji kuonana nawe kwa maongezi ya muhimu”
Akasema Happy
“Nakusikiliza Happy” akajibu Savanna.Happy akainama kidogo akafikiri na kusema
“Leo nimekwenda kuonana na Patrick gerezani.Tumeongea japo si kwa muda mrefu .Nilijaribu kumuuliza kuhusiana na maendeleo ya kesi na akanitoa wasi wasi na kusema kwamba mambo yote kuhusiana na kesi hii ameyaacha mikononi mwako.Amenihakikishia kwamba wewe ni wakili mahiri na kesi kama hii haiwezi kukusumbua hata kidogo.Kuna kitu aliniambia vile vile kilichonistua kidogo eti kwamba umekataa malipo yoyote na kwamba unaifanya kazi hii bure kabisa.Ni kweli?
Savanna akatabasamu kidogo na kusema
“Ni kweli Happy.Mimi ndiye ninayeisimamia kesi ya Patrick nikishirikiana na mawakili wazoefu toka katika kampuni yangu ya uwakili.Kuhusu malipo ni kweli kama alivyokwambia Patrick.Sihitaji kulipwa hata senti moja.Nimejitolea kuifanya kazi hii bure kwa sababu Patrick ni rafiki yangu mkubwa na wa siku nyingi.Kuna tatizo lolote katika suala hilo? Akauliza Savanna
“Hakuna tatizo Savanna.Nilihitaji tu kupata uhakika toka kwako kwa sababu haikuniingia akilini mtu kusitisha shughuli zake nyingine na kuisimamia kesi hii ngumu bila kuhitaji kulipwa hata shilingi moja.Labda naomba niwe wazi kwako Savanna kwamba moyo wangu hauna amani hata kidogo nikimuona Patrick gerezani.Ninataka kufanya kila linalowezekana ili Patrick ashinde kesi na atoke gerezani na ndiyo maana ninahitaji kuwa na uhakika kuhusiana na mtu anayeisimamia kesi yake.Kwa maana hiyo Savanna kama kuna kiasi chochote cha pesa ambacho ungependa kulipwa usisite kuniambia na nitakupatia.” Akasema Happy.Savanna akacheka kidogo halafu akamtazama Happy na kusema
“Happy mimi na wewe tumekutana na kufahamiana hivi karibuni baada ya kutokea tukio hili hata hivyo nadhani bado haujanifahamu vizuri.Mimi na Patrick tumekutana miaka mingi iliyopita,na tunafahamiana vyema. Sipendi kujisifu lakini mimi ni wakili mwenye uwezo mkubwa wa kusimamia kesi kubwa na karibu katika kesi zote ambazo tumewahi kusimamia mimi na kampuni yangu hatujawahi kushindwa.Ni kutokana na umahiri huo katika sheria nimeweza kukusaidia hata wewe kuondokana na kesi hii inayomkabili Patrick ambayo ulistahili uibebe wewe.Patrick ananifahamu vizuri na ndiyo maana hakusita kuiweka hatima ya kesi yake mikononi mwangu.Kuhusu malipo bado narudia tena kwamba sihitaji chochote.Ninafanya kazi hii kwa moyo kumsaidia rafiki yangu na si kwa ajili ya kutengeneza fedha.Ninazo pesa za kutosha na hata nikikwambia unilipe kama unavyotaka ,can you afford to pay me 100 millions? Akauliza Savanna akionyesha wazi kukerwa na maneno yale ya Happy.Happy akainama chini.
“Can you pay me 100 milions Happy? Akauliza tena Savanna
“Savanna samahani kama nimekuudhi ,lakini halikuwa kusudio langu kufanya hivyo.Lengo langu nilitaka niwe na uhakika kuhusu utetezi wa Patrick.” Akasema Happy
“One more thing.Who are you Happy? Akauliza Savanna huku sauti yake ikionyesha kuanza kubadilika.Happy akakaa kimya
“You are not even a member of Patrick’s family,….!!” Akasema Savanna.
“Savanna samahani kama kwa kukuuliza vile nimekukera.Niliuliza kwa lengo zuri tu” akajibu Happy
“Happy nimeshangazwa sana na namna ulivyoonyesha wasi wasi kwangu.Umesahau kwamba mimi ndiye niliyesababisha wewe uwe huru mpaka wakati huu na Patrick awe gerezani.” Akasema Savanna halafu akakaa kimya akamtazama Happy
“Kesho asubuhi,nitakwenda kumtembelea Patrick na nitamwambia kwamba najitoa katika kesi hii kwa sababu umeonyesha kutokuniamini nadhani litakuwa jambo la busara kama utaitumia nafasi hiyo kumuweka wakili unayemtaka wewe ambaye atafanya kazi hii kwa malipo tofauti na mimi ambaye sihitaji hata senti moja” akasema Savanna
“Savanna nakuomba usifanye hivyo.Usimweleze chochote Patrick.Atazidi kuumia.Nakuomba sana Savanna usimwambie Patrick chochote.” Akasema Happy
“Happy ahsante sana.Mimi naondoka.Kumbe umenipotezea muda wangu mwingi kwa kuja kunieleza mambo kama haya.!!!! Akasema Savanna huku akiinuka na kutoka mle sebuleni.Happy alikuwa ameinamisha kichwa.
“Bastard !!!..” akasema Savanna kwa hasira baada ya kuingia katika gari lake.
“Sijawahi kudharauliwa hata siku moja kuhusiana na kazi yangu na sipendi mtu aidharau taaluma yangu.Sikuwa nimetaka kukasirika lakini Happy amenikasirisha sana.Yeye ni nani hata anifanyie mahojiano na kuhoji uwezo wangu? akawaza Savanna.
“I will destroy you Happy.nitahakikisha Patrick humpati tena” Akawaza Savanna.
* * *
Baada ya kurejea nyumbani toka katika mazishi ya Vero Loniki hakutaka tena kuongea wala konana na mtu yeyote .Akajifungia chumbani kwake.
“Siyo ndoto tena kama nilivyokuwa nadhani.Ni kweli Vero amekwenda na sintamuona tena.Nilimpenda kupita kiasi na hii ni sababu inayonifaya niumie kiasi hiki.Vero amekufa , amekwenda na uzuri wake.Sintampata tena ndugu kama yeye.Patrick ameniondolea furaha ya maisha yangu na kwa hili sintamsamehe hadi siku naingia kaburini na lazima nihakikishe nimemlipia kisasi mdogo wangu.Kitendo alichofanyiwa na Yule shetani si cha kibinadamu na hakivumiliki hata kidogo na ninaapa kwa miungu yote kwamba lazima yeye na wale wote walioshiriki kumuua ndugu yangu wanalipa.Damu ya Vero haiwezi kupotea bure.They must pay ..!!!!!” akasema kwa hasira Loniki huku akigonganisha mikono yake.Akainuka kitandani akaendea kabatini akachukua pakiti la sigara akachomoa moja na kuanza kuvuta huku akipuliza moshi mwingi hewani.
“Sarah naye lazima atanieleza ni kwa nini kila mara amekuwa mtetezi mkubwa wa Patrick. Hata amediriki kuwaalika watu wake msibani.Anaonekana hana uchungu wowote na kifo cha Vero.Lazima naye nipambane naye.Zile fedha zilizotoka kwa akina Patrick nazo lazima zirudi zilikotoka .Itakuwa ni dhihaka kubwa kuzikubali pesa zilizotoka kwa watu waliomuua ndugu yetu.Sintakubali kamwe fedha zile ziendelee kukaa mikononi mwetu.Kama hawatazirejesha zilikotoka nitazirejesha mimi.” Akawaza Loniki huku akiendelea kuvuta sigara kwa fujo.
“Sintarejea London hadi nihakikishe wale wote walioshiriki katika kumuua Vero wamelipa uovu wao.Lazima walipe.Siihitaji hiyo haki ya mahakama,nitaitafuta haki kwa namna ninayojua mimi mwenyewe.” Akawaza Loniki huku akiendelea kupuliza moshi mwingi wa sigara hewani. Akafungua mlango na kutoka mle chumbani akamtafuta shangazi yake
“Shangazi naomba simu yako kuna mtu nahitaji kuwasiliana naye” akasema Loniki na shangazi yake akampa simu Loniki akarejea chumbani kwake akuchukua kitabu ambacho huandika kumbu kumbu zake mbali mbali akautafuta ukurasa ambao ameandika namba mbali mbali za simu akazipata namba alizokuwa anazitafuta akaziandika katika simu na kupiga
“Hallow Linah,Loniki hapa naongea” akasema Loniki baada ya simu kupokelewa.
“wow ! Loniki.!!....ni wewe kweli? Siamini .Umekuja lini shoga yangu.Na mbona umerudi kimya kimya? Akauliza Linah
“ Linah ina maana hujasikia matatizo yaliyonipata?
“Matatizo !!!.Linah akashangaa
“ Ndiyo Linah.Ina maana huna taarifa zozote?
“Mbona unanistua Lonny? Mimi sina taarifa zozote kwa sababu nimerudi mchana wa leo toka Nairobi kuna mizigo yangu ilikwama pale kwa hiyo sifahamu chochote na wala sijajua kama umerudi.Nini kimetokea Lonny?
“Linah nilipatwa na msiba mzito”
“Msiba !!! Linah akastuka
“Pole sana Lonny.Nani kafariki?
“Vero amefariki dunia !
“Vero !? ..Vero huyu mdogo wako?
“Ndiyo.”
“Acha masihara Lonny.”
“Si masihara Linah.Ni kweli Vero amefariki dunia na ni kifo ambacho kimetangazwa sana na nchi nzima wanajua kama Vero amefariki dunia na jioni ya leo tumetoka kumzika katika makaburi ya Kinondoni.”
Kimya kifupi kikapita.Linah akavuta pumzi ndefu na kusema
“Loniki umenistua sana .Bado siamini kama uliyonieleza ni ya kweli”
“Sikudanganyi Linah.Ni kweli kabisa Vero amefariki dunia.Vero hatunaye tena.”
“Ouh my Gosh !!!”
“pole sana Lonny.Kwa kweli ni msiba mzito sana na wala sina taarifa zozote.Loniki nitajitahidi nifike hapo nyumbani kesho asubuhi kwa sababu kwa sasa niko mbali kidogo ”
“Nitashukuru sana kama ukifika Linah ninahitaji sana kukuona.Nina maongezi nawe ya muhimu sana”
“Usijali Lonny nitafika hiyo kesho bila kukosa.Mpe pole sana mama na Sarah”
“Ahsante sana Linah ,tutaonana hiyo kesho” akasema Loniki na kukata simu,akachukua sigara nyingine katika pakiti na kuiwasha akaendelea kuvuta
SEHEMU YA 38
MTUNZI 😛ATRICK.CK
CONTACT:0764294499
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Jeneza likashushwa garini na kuingizwa kanisani na kabla ya kuanza kwa ibada ikatolewa tena nafasi nyingine ya kutoa heshima za mwisho kwa wale ambao hawakuipata nafasi hiyo nyumbani.Zoezi hili lililazimika kusitishwa kutokana na idadi kubwa ya watu hivyo .Ibada ilichukua takribani saa moja halafu safari ya kuelekea makaburini kwa ajili ya kuhitimisha safari ya mwisho ya Vero ikaanza.Saa kumi za jioni waliwasili makaburini na ikafanyika ibada ya makaburini na taratibu mwili wa Vero ukashushwa kaburini.Lilikuwa ni tukio lililowafanya watu wengi wapoteze fahamu.Miongoni mwa watu waliopoteza fahamu alikuwa ni Loniki.Hii ilikuwa ni mara ya tatu katika siku hii kupoteza fahamu.Kifo hiki cha Vero kilikuwa kimemuumiza mno.
Familia na watu wa karibu wa marehemu wakatupa udongo kaburini na kisha likaanza zoezi la kulifunika kaburi.Baada ya zoezi lile lililofanywa na mafundi mahiri kukamilika ,yakawekwa mashada ya maua halafu Padre akalibariki kaburi na kisha watu wakatawanyika na kurejea msibani kwa ajili ya kuendelea na taratibu nyingine.Safari ya Vero duniani ikafikia mwisho.
ENDELEA………………
“Andrew ninaondoka ,ninahitaji kuonana na Happy jioni hii” akasema Savanna muda mfupi tu baada ya kurejea nyumbani kwa akina Patrick wakitokea katika mazishi ya Vero
“Sawa Savanna.Tutaonana kesho.Patrick anafahamu kama baba yake anazikwa kesho?
“Sina hakika kama anafahamu ,lakini nitamfahamisha nitakapomtembelea kesho asubuhi.”
“Ukionana naye kesho mpe salamu zangu nyingi.Nitakwenda kumtembelea baada ya kumalizika kwa shughuli hizi za msiba wa mzee” akasema Andrew kisha Savanna akaingia garini na kuondoka kuelekea nyumbani kwa akina Happy.
“Kwa kweli hata mimi niliumia sana katika mazishi ya Vero.She was so pretty.Maskini Vero,amekufa na uzuri wake.Happy alistahili adhabu kwa kosa alilolifanya.Sielewi ni kwa nini Patrick ameamua kujitwisha yeye mzigo huu mzito ambao hakuustahili” akawaza Savanna akiwa njiani kuelekea kwa akina Happy
“Hata hivyo nitamsaidia Patrick kwa kila namna nitakavyoweza na atashinda hii kesi.Ninayafanya haya yote kwa sababu ya upendo wangu kwake.Ninampenda sana Patrick.Toka tulipoamua kusitisha mahusiano yetu baada ya mimi kumpata George ,bado sijaweza kabisa kumtoa Patrick moyoni mwangu.Hii ni nafasi yangu ya kumrudisha tena Patrick kwangu.Nitashinda hii kesi na Patrick lazima awe wangu tena.Happy hastahili kuwa na Patrick tena.” Akaendelea kuwaza Savanna.
Jua tayari lilikwisha punguza nuru yake kuashiria kwamba muda wowote litazama kulipisha giza lichukue nafasi yake.Savanna akafika nyumbani kwa akina Happy akafunguliwa geti na kuingia ndani.Akapokewa na mtumishi wa ndani
“Happy nimemkuta? Akauliza Savanna
“Ndiyo umemkuta.Karibu ndani ngoja nikamuite” akasema Yule msichana na kuelekea chumbani kwa Happy akamtaarifu kwamba Savanna amekwisha fika.Happy akatoka chumbani kwake na kuelekea sebuleni
“Karibu sana Savanna.” Akasema Happy huku akitabasamu
“Nashukuru sana Happy.Unaendeleaje?
“Ninaendelea vizuri Savanna.Namshukuru Mungu kwani ninazidi kupata nguvu kila siku”
“Nafurahi kusikia hivyo Happy.Ni jambo la faraja sana kuona hali yako inaboreka siku hadi siku” akasema Savanna.Kikapita kimya kifupi halafu Savanna akasema
“Happy ,nilisikia kwamba umelivua taji la Miss Tanzania..”
“Ndiyo Savanna.Niliamua kulivua taji lile ili kuendelea kulipa heshima yake kwa sababu kila neno baya lilikuwa linasemwa kwa kutanguliwa na miss Tanzania badala ya Happy.Nilifikiria na kuona haitakuwa busara kama taji la miss Tanzania likaendelea kuchafuliwa. Nikaona ni bora nilivue.”
“Pole Happy.Haya yalikuwa ni maamuzi magumu sana”
“Nimekwisha poa Savanna.Sikuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya kulirudisha taji lile.” Akasema Happy
“Nimetoka katika mazishi ya Vero.Mimi na Andrew tuliiwakilisha familia ya Patrick katika mazishi.” Akasema Savanna.Happy hakujibu kitu akainama chini
“Happy nimepita mara moja kukuona kama ulivyokuwa umeomba.” Akasema Savanna ,Happy akainua kichwa.
“Samahani Savanna kwa kukusumbua.Ni kweli nilihitaji kuonana nawe kwa maongezi ya muhimu”
Akasema Happy
“Nakusikiliza Happy” akajibu Savanna.Happy akainama kidogo akafikiri na kusema
“Leo nimekwenda kuonana na Patrick gerezani.Tumeongea japo si kwa muda mrefu .Nilijaribu kumuuliza kuhusiana na maendeleo ya kesi na akanitoa wasi wasi na kusema kwamba mambo yote kuhusiana na kesi hii ameyaacha mikononi mwako.Amenihakikishia kwamba wewe ni wakili mahiri na kesi kama hii haiwezi kukusumbua hata kidogo.Kuna kitu aliniambia vile vile kilichonistua kidogo eti kwamba umekataa malipo yoyote na kwamba unaifanya kazi hii bure kabisa.Ni kweli?
Savanna akatabasamu kidogo na kusema
“Ni kweli Happy.Mimi ndiye ninayeisimamia kesi ya Patrick nikishirikiana na mawakili wazoefu toka katika kampuni yangu ya uwakili.Kuhusu malipo ni kweli kama alivyokwambia Patrick.Sihitaji kulipwa hata senti moja.Nimejitolea kuifanya kazi hii bure kwa sababu Patrick ni rafiki yangu mkubwa na wa siku nyingi.Kuna tatizo lolote katika suala hilo? Akauliza Savanna
“Hakuna tatizo Savanna.Nilihitaji tu kupata uhakika toka kwako kwa sababu haikuniingia akilini mtu kusitisha shughuli zake nyingine na kuisimamia kesi hii ngumu bila kuhitaji kulipwa hata shilingi moja.Labda naomba niwe wazi kwako Savanna kwamba moyo wangu hauna amani hata kidogo nikimuona Patrick gerezani.Ninataka kufanya kila linalowezekana ili Patrick ashinde kesi na atoke gerezani na ndiyo maana ninahitaji kuwa na uhakika kuhusiana na mtu anayeisimamia kesi yake.Kwa maana hiyo Savanna kama kuna kiasi chochote cha pesa ambacho ungependa kulipwa usisite kuniambia na nitakupatia.” Akasema Happy.Savanna akacheka kidogo halafu akamtazama Happy na kusema
“Happy mimi na wewe tumekutana na kufahamiana hivi karibuni baada ya kutokea tukio hili hata hivyo nadhani bado haujanifahamu vizuri.Mimi na Patrick tumekutana miaka mingi iliyopita,na tunafahamiana vyema. Sipendi kujisifu lakini mimi ni wakili mwenye uwezo mkubwa wa kusimamia kesi kubwa na karibu katika kesi zote ambazo tumewahi kusimamia mimi na kampuni yangu hatujawahi kushindwa.Ni kutokana na umahiri huo katika sheria nimeweza kukusaidia hata wewe kuondokana na kesi hii inayomkabili Patrick ambayo ulistahili uibebe wewe.Patrick ananifahamu vizuri na ndiyo maana hakusita kuiweka hatima ya kesi yake mikononi mwangu.Kuhusu malipo bado narudia tena kwamba sihitaji chochote.Ninafanya kazi hii kwa moyo kumsaidia rafiki yangu na si kwa ajili ya kutengeneza fedha.Ninazo pesa za kutosha na hata nikikwambia unilipe kama unavyotaka ,can you afford to pay me 100 millions? Akauliza Savanna akionyesha wazi kukerwa na maneno yale ya Happy.Happy akainama chini.
“Can you pay me 100 milions Happy? Akauliza tena Savanna
“Savanna samahani kama nimekuudhi ,lakini halikuwa kusudio langu kufanya hivyo.Lengo langu nilitaka niwe na uhakika kuhusu utetezi wa Patrick.” Akasema Happy
“One more thing.Who are you Happy? Akauliza Savanna huku sauti yake ikionyesha kuanza kubadilika.Happy akakaa kimya
“You are not even a member of Patrick’s family,….!!” Akasema Savanna.
“Savanna samahani kama kwa kukuuliza vile nimekukera.Niliuliza kwa lengo zuri tu” akajibu Happy
“Happy nimeshangazwa sana na namna ulivyoonyesha wasi wasi kwangu.Umesahau kwamba mimi ndiye niliyesababisha wewe uwe huru mpaka wakati huu na Patrick awe gerezani.” Akasema Savanna halafu akakaa kimya akamtazama Happy
“Kesho asubuhi,nitakwenda kumtembelea Patrick na nitamwambia kwamba najitoa katika kesi hii kwa sababu umeonyesha kutokuniamini nadhani litakuwa jambo la busara kama utaitumia nafasi hiyo kumuweka wakili unayemtaka wewe ambaye atafanya kazi hii kwa malipo tofauti na mimi ambaye sihitaji hata senti moja” akasema Savanna
“Savanna nakuomba usifanye hivyo.Usimweleze chochote Patrick.Atazidi kuumia.Nakuomba sana Savanna usimwambie Patrick chochote.” Akasema Happy
“Happy ahsante sana.Mimi naondoka.Kumbe umenipotezea muda wangu mwingi kwa kuja kunieleza mambo kama haya.!!!! Akasema Savanna huku akiinuka na kutoka mle sebuleni.Happy alikuwa ameinamisha kichwa.
“Bastard !!!..” akasema Savanna kwa hasira baada ya kuingia katika gari lake.
“Sijawahi kudharauliwa hata siku moja kuhusiana na kazi yangu na sipendi mtu aidharau taaluma yangu.Sikuwa nimetaka kukasirika lakini Happy amenikasirisha sana.Yeye ni nani hata anifanyie mahojiano na kuhoji uwezo wangu? akawaza Savanna.
“I will destroy you Happy.nitahakikisha Patrick humpati tena” Akawaza Savanna.
* * *
Baada ya kurejea nyumbani toka katika mazishi ya Vero Loniki hakutaka tena kuongea wala konana na mtu yeyote .Akajifungia chumbani kwake.
“Siyo ndoto tena kama nilivyokuwa nadhani.Ni kweli Vero amekwenda na sintamuona tena.Nilimpenda kupita kiasi na hii ni sababu inayonifaya niumie kiasi hiki.Vero amekufa , amekwenda na uzuri wake.Sintampata tena ndugu kama yeye.Patrick ameniondolea furaha ya maisha yangu na kwa hili sintamsamehe hadi siku naingia kaburini na lazima nihakikishe nimemlipia kisasi mdogo wangu.Kitendo alichofanyiwa na Yule shetani si cha kibinadamu na hakivumiliki hata kidogo na ninaapa kwa miungu yote kwamba lazima yeye na wale wote walioshiriki kumuua ndugu yangu wanalipa.Damu ya Vero haiwezi kupotea bure.They must pay ..!!!!!” akasema kwa hasira Loniki huku akigonganisha mikono yake.Akainuka kitandani akaendea kabatini akachukua pakiti la sigara akachomoa moja na kuanza kuvuta huku akipuliza moshi mwingi hewani.
“Sarah naye lazima atanieleza ni kwa nini kila mara amekuwa mtetezi mkubwa wa Patrick. Hata amediriki kuwaalika watu wake msibani.Anaonekana hana uchungu wowote na kifo cha Vero.Lazima naye nipambane naye.Zile fedha zilizotoka kwa akina Patrick nazo lazima zirudi zilikotoka .Itakuwa ni dhihaka kubwa kuzikubali pesa zilizotoka kwa watu waliomuua ndugu yetu.Sintakubali kamwe fedha zile ziendelee kukaa mikononi mwetu.Kama hawatazirejesha zilikotoka nitazirejesha mimi.” Akawaza Loniki huku akiendelea kuvuta sigara kwa fujo.
“Sintarejea London hadi nihakikishe wale wote walioshiriki katika kumuua Vero wamelipa uovu wao.Lazima walipe.Siihitaji hiyo haki ya mahakama,nitaitafuta haki kwa namna ninayojua mimi mwenyewe.” Akawaza Loniki huku akiendelea kupuliza moshi mwingi wa sigara hewani. Akafungua mlango na kutoka mle chumbani akamtafuta shangazi yake
“Shangazi naomba simu yako kuna mtu nahitaji kuwasiliana naye” akasema Loniki na shangazi yake akampa simu Loniki akarejea chumbani kwake akuchukua kitabu ambacho huandika kumbu kumbu zake mbali mbali akautafuta ukurasa ambao ameandika namba mbali mbali za simu akazipata namba alizokuwa anazitafuta akaziandika katika simu na kupiga
“Hallow Linah,Loniki hapa naongea” akasema Loniki baada ya simu kupokelewa.
“wow ! Loniki.!!....ni wewe kweli? Siamini .Umekuja lini shoga yangu.Na mbona umerudi kimya kimya? Akauliza Linah
“ Linah ina maana hujasikia matatizo yaliyonipata?
“Matatizo !!!.Linah akashangaa
“ Ndiyo Linah.Ina maana huna taarifa zozote?
“Mbona unanistua Lonny? Mimi sina taarifa zozote kwa sababu nimerudi mchana wa leo toka Nairobi kuna mizigo yangu ilikwama pale kwa hiyo sifahamu chochote na wala sijajua kama umerudi.Nini kimetokea Lonny?
“Linah nilipatwa na msiba mzito”
“Msiba !!! Linah akastuka
“Pole sana Lonny.Nani kafariki?
“Vero amefariki dunia !
“Vero !? ..Vero huyu mdogo wako?
“Ndiyo.”
“Acha masihara Lonny.”
“Si masihara Linah.Ni kweli Vero amefariki dunia na ni kifo ambacho kimetangazwa sana na nchi nzima wanajua kama Vero amefariki dunia na jioni ya leo tumetoka kumzika katika makaburi ya Kinondoni.”
Kimya kifupi kikapita.Linah akavuta pumzi ndefu na kusema
“Loniki umenistua sana .Bado siamini kama uliyonieleza ni ya kweli”
“Sikudanganyi Linah.Ni kweli kabisa Vero amefariki dunia.Vero hatunaye tena.”
“Ouh my Gosh !!!”
“pole sana Lonny.Kwa kweli ni msiba mzito sana na wala sina taarifa zozote.Loniki nitajitahidi nifike hapo nyumbani kesho asubuhi kwa sababu kwa sasa niko mbali kidogo ”
“Nitashukuru sana kama ukifika Linah ninahitaji sana kukuona.Nina maongezi nawe ya muhimu sana”
“Usijali Lonny nitafika hiyo kesho bila kukosa.Mpe pole sana mama na Sarah”
“Ahsante sana Linah ,tutaonana hiyo kesho” akasema Loniki na kukata simu,akachukua sigara nyingine katika pakiti na kuiwasha akaendelea kuvuta