Simulizi: Milango ya mafanikio

Simulizi: Milango ya mafanikio

SEHEMU YA ISHIRINI

Baada ya safari ngumu yenye vikwazo njiani kutokana na bus walilopanda James Mgaya na mwanaye Samson, walijikuta wanaingia jijini Dar es salaam mida ya saa tano usiku.

Mzee James Mgaya aliita Taxi ikawapeleka hadi nyumbani kwake, ambapo alipokelewa vizuri sana na mkewe,

Mmmmh pole sana na safari mume wangu, yaani sikujua kama mtafika leo hii. aliongea mke wa mzee Mgaya au mama Kulwa kama walivyozoeleka kuitwa na majirani zao.

(Iko hivi)
Mzee Mgaya alikuwa na wake wawili,

Mke wa kwanza alikuwa na watoto watano, ambapo watatu walikuwa wakubwa tu wakiwa wamesoma na Wana kazi zao tayari, na wawili ni mapacha ambao walizaliwa kipindi ambacho mzee Mgaya na mkewe hawakutarajia kama wanaweza kupata tena mtoto kwa umri wao, lakini MUNGU si mwanadamu walijikuta wanapata watoto
mapacha ambao ni rika la Samson.

Mke wa pili alikuwa anaitwa Tausi huyu tangu aolewe kama bibi mdogo hakuwahi kubahatika kupata mtoto, Wala ujauzito wa kusingizia, ugomvi wa Mara kwa Mara Kati ya Tausi na mumewe ulikuwa haukauki, shida ikiwa kwanini hamzalii, na Tausi naye siku zote alijitetea kwamba si yeye Bali ni MUNGU hajaamua kumjalia.

Mume wangu wangu, naona umekuja na mgeni, ni mtoto wa nani huyo?
aliuliza mama Kulwa akiwa anaandaa maji kusudi watu waondoe uchovu.

Ni mtoto wetu, anaitwa Samson. Ni mtoto wa mdogo wangu Elias, nimemchukua kwa lengo la kuja kumsomesha maana hali ya vijijini mke wangu unaijua, mtoto ana akili na kipaji kikubwa lakini kutokana na hali ya maisha unakuta mtoto hatimizi ndoto zake. alijibu Mzee Mgaya

Mmmh kwahiyo wewe baba Kulwa unajiona una uweeeezo wa kusomesha mtoto wa mtu siyo? naona umesahau tu na nilikuwa nakusubiri urudi maana akina Kulwa wenyewe wanatakiwa kwenda Boarding na gharama ya shule yenyewe unaijua, Sasa kwa kujiongeza mzigo tenaaaaaa, kwanza ninyamaze miye hayo mambo utajua mwenyewe, ninachotaka isije ikatokea kikwazo chochote kwa wanangu kisa wewe umeongeza idadi ya unaowasomesha.
Aliongea kwa kujiamini mama Kulwa akionesha hajapendezwa na ujio wa Samson kama mwanafunzi.

James Mgaya na Samson walioga wakatulia sebuleni huku Samson akiwa Hana hata lepe la usingizi badala yake, macho yakiwa yanatalii kwenye sebule kubwa ya nyumba ile, hakika aliviona vitu vingi ambavyo hakuwahi hakuviona kabla.

Mwanangu twende nikakuoneshe chumba ulale, aliongea mama Kulwa huku akimuonesha Samson chumba fulani kizuri kina kitanda kizuri pamoja na mashuka yanayonukia vizuri, lakini kutokana na joto hakuweza kujifunika shuka lolote.

(Chumbani kwa James Mgaya)
Mke wangu Mimi huyu mtoto si kwamba nampeleka hostel huyu shule ambayo anaenda ni ya kutwa ile ya (akitaja jina la shule)wewe unadhani gharama kule watakakosoma kina Dotto, tutamudu kweli? Hapana siyo hivyo Mimi nimefanya msaada kwa ndugu zangu, ili mtoto wao apate elimu.
alimtoa hofu mama Kulwa ambaye alidhani Samson kaja kutibua bajeti ya wanae.

Ahaaa hapo sawa lakini hata hivyo, mbona hiyo shule ingawaje ni ya (Day) kutwa lakini ni nzuri, Tena imefaulisha vizuri sana mwaka huu Kuna wanafunzi wengi wanaenda
A level wakiwa wamefaulu hapohapo, kama huyu mtoto ana nia ya dhati kweli basi hiyo shule si mbaya juhudi zake tu. alikazia mama Kulwa.halafu Kuna tajiri mmoja alikuwa anakuulizia anadai Lile eneo linashindwa kuuzwa kwakuwa wewe haupo, hivyo alidai ukija tu tukwambie.

Mzee Mgaya akawa anasikiliza tu, alikuwa anamjua vizuri mkewe, alikuwa ana roho fulani ya kwanini, lakini hakutaka kumuudhi Wala kumfanya ajisikie vibaya kwa namna yeyote ile , akawa anawaza namna mkewe alivyoisifia ile shule kana kwa ni high school, kama ingekuwa nzuri mke wangu angeng'ang'ania kina Kulwa wakasome shule ya gharama?
alijikuta anawaza mambo mengi.hata hivyo aliwaza kesho aende kwa tajiri fulani ambaye walipanga kuuziana eneo la kupaki magari makubwa.

Asubuhi kulipokucha Samson alikuwa wa kwanza kuamka licha ya kuwa aliingia kulala mida mibovu, akaja kukaa sebuleni kama kinda la ndege ambalo halijui mama yake yuko wapi
alijikunyata pale, Mara akatokea mdada ambaye alimsalimia na kuanza kupiga deki huku akiwa anamuongeleshaongelesha Samson.

Unaitwa nani?

Naitwa Samson.

Umekuja na nani, na mzee?

Samson alitikia kwa kutikisa kichwa.

Basi nenda kakae nje maana hapa nafanya usafi mdogo wangu. alishauri yule mdada.

Samson akiwa nje, aliona vitu vingi ikiwemo magari mawili madogo lakini pia aligundua kumbe nyumba ile ilikuwa kubwa tofauti na alivyoina usiku, wakati akiwaza hayo walikuja watoto ambao walivaa vest na vikaptura vinavyofanana, lakini pia hata nywele zao zilizokatwa vizuri zilifanana, si hivyo tu hata wenyewe walifanana sana, kiasi kwamba akimwangalia huyu kama huyu, hakika alishangaa kuona watu wanafanana namna ile. Walibaki wakiangaliana na Samson bila kusalimiana Wala kuongeleshana,

Baadaye mama yao alitoka,
Heeeeeh na mgeni na wewe umeamka, Bora tu ungeendelea kulala upunguze usingizi mwanangu maana mmelala mida mibaya sana, hebu njoo huku baba , alimuita Samson,

Jamani wanangu, Kuna huyu mwenzenu amekuja na baba ametoka mkoani, au kijijini alikotoka baba yenu, anaitwa Samson. alimtambulisha . Akina Kulwa wakaitikia huku wakitabasamu wakionesha wamefurahi ujio wa ndugu yao.

Na wewe Samson huyu anaitwa Kulwa au Festo jina la shuleni na huyu anaitwa Dotto au Felix, Tena mnalingana kweli nyie ni Classmates, aliongea mama Kulwa huku akiwachekesha chekesha ikiwa ni mbinu ya kumuweka Samson kisaikolojia ili asijisikie vibaya yaani azioee haraka.

Kulwa muite dada yenu naye nimwelekeze mgeni, dada alikuja.
Wewe huyu anaitwa Samson ni mmoja ya wanafamilia watakaokuwa wanaishi hapa hivyo anapaswa asikilizwe kama unavyowasikiliza kina Kulwa, Tena huyu ndiyo unaye hapahapa kumbuka kina Kulwa wao siku tatu baadaye wataenda kukaa boarding sawa.

Basi dada wa kazi alionesha kukubaliana na yule mgeni, ambaye yeye alimuona tangu alfajiri.
Wakati wakipiga stori za vichekesho pale nje mzee Mgaya alitoka haraka akiwa kavaa suit yake ya kijivu iliyomkaa vyema, alisalimia juu juu Kisha akaingia kwenye gari huku akiamrisha afunguliwe geti atoke . kweli ikawa hivyo.

Samson aliwaza kwanini baba yake huyo hata hajamsalimia kutaka kujua ameamkaje, mawazo Yale mama yake aliyatambua....

Sam usijali huyu babako mkubwa ndivyo alivyo unaweza sema kakuchukia ila ndo alivyo muda wote yeye ana haraka tu.
Walizidi kumtembeza na kumzungusha Samson kwenye ile nyumba huku akishangaa vitu vingi vigeni kwenye upeo wa macho yake.

*************************************

Baada ya kumaliza shughuli zilizompeleka huko, alijikuta ananyoosha moja kwa moja hadi Temeke, ambako alikuwa anaishi mke wake mdogo aitwae Tausi.

Dah karibu sana my husband jamani, nilikumiss, nikamiss na kumiss yaani tulijua umefia mkoani, si hivyo tu mama Kulwa alienda mbali zaidi akijua labda umeenda kuoa mkoani maana hamchelewagi nyie.

Aliongea kwa kudeka Tausi huku akiwa amekumbatiana kimahaba na mumewe, hata James mwenyewe joto Kali la mapenzi huwa anapata kwa Tausi mwanamke mdogo sawa na wanae japo alikuwa anakaribia 40.

Karibu ndani my love, alikaribisha kwa madaha Tausi huku akiwa anabebika inavyotakiwa, hakika ubabe wa James Mgaya huwa unaishia huko mitaani na siyo kwa Tausi. Hapa alitakiwa kuwa sex na si vinginevyo.

Mke wangu, nashukuru nimewakuta wazima wote nikimaanisha kuanzia dada yako kule na wote kiujumla, ila nimekuja na mtoto wa ndugu yangu ambaye nimeamua kumsaidia ili nimsomeshe hivyo muda wowote nitamleta umuone maana Kuna Leo na kesho naweza kupoteza maisha mkawa hamumtambui. aliweka kituo mzee Mgaya.

Sasa my, yupo wapi huyo mtoto? Yupo kwa mama Kulwa siyo, ninachosikitika ni kwamba Mimi hapa Sina mtoto na umri huu unatambua fika kwamba nahitaji faraja, nakuwa mpweke sana kwanini usingemleta aje aishi huku kuliko kujazana sehemu ambayo Kuna watu wengi. alihoji Tausi.

Aaaah ujue nimemwandikisha shule iliyo karibu na kule ni kama kilomita moja tu kutoka nyumbani, hivyo kwakuwa bado ni mgeni nikaona Bora ile shule. alijitetea mzee Mgaya.

Hapana , nakataa wewe Mimi hunipendi tu ni Mara ngapi nakwambia tutafute housegirl wa kusaidiana naye kazi hapa lakini unanipiga chenga, Sasa nakwambia hiyo shule atasoma huko huko na kukaa atakaa kwangu, kama nauli za Daladala nitalipa , mbona Kuna wanafunzi miaka yote wanasoma shule za mbali na Kila kitu kinakaa sawa. niletee huyo mtoto akae na Mimi umesema anaitwa nani,aliuliza Tausi.

Anaitwa Samson, alijibu kinyonge mzee Mgaya.

Je , Tausi au mke mdogo wa Mzee Mgaya anataka Nini kwa Samson?

Itaendelea..............
 
Jamaa anatibu watu tulieni. Chukueni kitabu muda huo msome,hata kuhusu mind zetu tulizopewa. "I count him a braver the one who who conquer himself not the one who conquer the enemy. The enemy within us can do harm but the enemy outside us can do no harm to us" by mijamaa fulani iliyoishi na kutawala Zama hizo before christ
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA.

Baada ya mzee Mgaya kupishana kidogo na mkewe, alibadilisha mada ili kuweka mambo sawa, maana shetani alikuwa karibu mno.
Alikaa na Tausi huku wakipeana mapenzi motomoto, na hii ilichangiwa na umri wa Tausi kwa bado alikuwa mdogo.

Jioni ya siku hiyo mzee Mgaya akiwa kapumzika kwenye nyumba yake ndogo, alifikiria jambo moja, akaona kama Kuna kaukweli fulani toka kwa mke mdogo...

Mama Kulwa, ni mtu mzima, sina shaka naye juu ya malezi ya mtoto huyu, ila ana kasumba ya unyanyasaji, na Mimi nilivyo mtu wa kusafiri safiri inaweza ikawa shida, maana ni mkali mno.akiwaza Mzee Mgaya akijaribu kuhesabu madada wa kazi waliopita pale kwake huku wengine wakiwa hawakumaliza hata wiki moja, yote ni sababu ya mkewe kwa ukali wake. akaona ni kweli alikurupuka kimuhamishia shule iliyopo karibu na kwa mke mkubwa ni Bora hata angekaa kwa mkewe Tausi akihisi huenda Samson atakuwa free.

*************************************
Usiku wa saa tatu mama Kulwa na familia yake walikuwa mezani wakipata Chakula Cha usiku, huku watu wote wakiwa Wana nyuso za furaha, kasoro Samson tu..

Vipi baba yangu mbona umekuwa mnyonge, una tatizo gani,
Unaumwa?
au Chakula si kitamu baba?
Mama Kulwa aliuliza maswali kiutani huku akimsoma Samson,
ili ajue anawaza nini.

Hapana mama nipo kawaida tu,
alijitetea Samson.

Mawazo ya Samson hayakuwa kwenye ile familia, ila alianza kukumbuka nyumbani,
Alimkumbuka mama yake,
Aliwakumbuka dada zake,
Si ndugu tu, hata baadhi ya mazingira aliyoacha nyumbani kwao aliyamisi kwa muda mfupi mno.

Kwanini aliyawaza hayo?
Ni kwamba mabadiliko ya ratiba ya kula, kutoka saa Saba aliyoizoea Hadi saa kumi kasoro, kulimuumiza sana, hata hivyo alisahau kuwa alishaonywa na kutahadharishwa na wazazi wake siku mbili tu zilizopita.

Muda wa kulala Samson aliingia kwenye chumba chake huku akiwa na mawazo kibao, suala la shule na taratibu zinazoendelea pale hazikumridhisha sana, alianza kujiona mpweke, Kila akifikiria kuhusu namna atakavyoishi pale, huko shule kutakuwaje, alianza kujilaumu kwanini alikubali kusoma ni Bora angebaki kijijini tu.
Lakini pia ajiuliza kuhusu kutokuwepo kwa baba yake mkubwa, yaani kutwa nzima hakumuona hili lilimpa mawazo zaidi kwakuwa akihisi katelekezwa na mtu pekee anayemtegemea na kumwamini.
aliwaza sana.

Asubuhi kulikucha, kama kawaida alikuwa wa kwanza kuamka safari hii akifikia nje, ambako alimkuta mama yake mkubwa akiwa anasaidiana kufanya kazi na housemaid.

Baada ya kusalimiana waliendelea na mazungumzo,

Mbona mapema sana Sam, wenzio bado wamelala jamani, alihoji mama Kulwa huku akimuonesha tabasamu la upendo ili Samson asijisikie vibaya.

Baada ya Samson kumuona yule mama yupo vizuri akamuuliza swali lake.....

Mama tangu Jana asubuhi baba sijamuona Tena, kwani kasafiri,?

(Huku akicheka)
Hapana mwanangu yupo kwa mama yako mwingine, na leo atakuja kwasababu inatakiwa muende kwa Headmaster akakutambulishe pamoja na kupeleka barua zako, siyo mbali shule ipo nyuma tu hapo.

**************************************Mzee Mgaya aliamka mapema huku akipitia maeneo ya mjini, kuonana na baadhi ya wadau na wazee wenzie kwaajili ya kujadili masuala fulani.
akiwa kule mjini alishangaa kukutana na headmaster wa shule ambayo atasoma Samson, baada ya kusalimiana , walijikuta wanaingia kwenye gari la mzee Mgaya ili waongee zaidi.

Aisee mwalimu, nimefurahi sana kukuona, hata hivyo nilikuwa nataka kuja shuleni kwako, kwaajili ya kuja kukuletea Yale makaratasi, lakini pia nikuoneshe na mwanaelimu mwenyewe, (huku akijichekesha)
Umuone. aliweka kituo Mzee Mgaya.

Haina shida, mzee wangu hata hivyo hakuna haja ya kuleta hizo documents wewe ikifika jumatatu mlete aje aungane na wenzake Kila kitu kitakuwa sawa. alifafanua yule mwalimu.

Mzee Mgaya akakanyaga mafuta Hadi nyumbani kwake ambapo aliikuta familia yake ikiwa salama tu. Aliingia ñdani akafanya shughuli zake Kisha akawaita watoto wake pamoja na Samson akiwaambia wajiandae ili waende kwa mama yao mdogo akamtambulishe Samson.

Baba Kulwa, labda kama sijakusikia vizuri umesema unawapeleka wanangu wapi? alihoji mama Kulwa.

Tunaenda kwa mwenzio kule ila tunarudi muda si mrefu mke wangu. alijibu mzee Mgaya.

Kwahiyo baada ya huyo Malaya wako kushindwa kuniroga Mimi na wanangu, ukaona Bora uwapeleke ili akawatie wazimu kabisa ili washindwe kuendelea na masomo?
Hebu na nyie wajinga shukeni, mnawezaje kucheza na nyoka mwenye sumu kali. aliropoka mama Kulwa.

Mzee Mgaya alijisikia vibaya ila hakutia neno akawa njia panda aende au asiende?

Itaendelea.......................
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA.

Baada ya mzee Mgaya kupishana kidogo na mkewe, alibadilisha mada ili kuweka mambo sawa, maana shetani alikuwa karibu mno.
Alikaa na Tausi huku wakipeana mapenzi motomoto, na hii ilichangiwa na umri wa Tausi kwa bado alikuwa mdogo.

Jioni ya siku hiyo mzee Mgaya akiwa kapumzika kwenye nyumba yake ndogo, alifikiria jambo moja, akaona kama Kuna kaukweli fulani toka kwa mke mdogo...

Mama Kulwa, ni mtu mzima, sina shaka naye juu ya malezi ya mtoto huyu, ila ana kasumba ya unyanyasaji, na Mimi nilivyo mtu wa kusafiri safiri inaweza ikawa shida, maana ni mkali mno.akiwaza Mzee Mgaya akijaribu kuhesabu madada wa kazi waliopita pale kwake huku wengine wakiwa hawakumaliza hata wiki moja, yote ni sababu ya mkewe kwa ukali wake. akaona ni kweli alikurupuka kimuhamishia shule iliyopo karibu na kwa mke mkubwa ni Bora hata angekaa kwa mkewe Tausi akihisi huenda Samson atakuwa free.

*************************************
Usiku wa saa tatu mama Kulwa na familia yake walikuwa mezani wakipata Chakula Cha usiku, huku watu wote wakiwa Wana nyuso za furaha, kasoro Samson tu..

Vipi baba yangu mbona umekuwa mnyonge, una tatizo gani,
Unaumwa?
au Chakula si kitamu baba?
Mama Kulwa aliuliza maswali kiutani huku akimsoma Samson,
ili ajue anawaza nini.

Hapana mama nipo kawaida tu,
alijitetea Samson.

Mawazo ya Samson hayakuwa kwenye ile familia, ila alianza kukumbuka nyumbani,
Alimkumbuka mama yake,
Aliwakumbuka dada zake,
Si ndugu tu, hata baadhi ya mazingira aliyoacha nyumbani kwao aliyamisi kwa muda mfupi mno.

Kwanini aliyawaza hayo?
Ni kwamba mabadiliko ya ratiba ya kula, kutoka saa Saba aliyoizoea Hadi saa kumi kasoro, kulimuumiza sana, hata hivyo alisahau kuwa alishaonywa na kutahadharishwa na wazazi wake siku mbili tu zilizopita.

Muda wa kulala Samson aliingia kwenye chumba chake huku akiwa na mawazo kibao, suala la shule na taratibu zinazoendelea pale hazikumridhisha sana, alianza kujiona mpweke, Kila akifikiria kuhusu namna atakavyoishi pale, huko shule kutakuwaje, alianza kujilaumu kwanini alikubali kusoma ni Bora angebaki kijijini tu.
Lakini pia ajiuliza kuhusu kutokuwepo kwa baba yake mkubwa, yaani kutwa nzima hakumuona hili lilimpa mawazo zaidi kwakuwa akihisi katelekezwa na mtu pekee anayemtegemea na kumwamini.
aliwaza sana.

Asubuhi kulikucha, kama kawaida alikuwa wa kwanza kuamka safari hii akifikia nje, ambako alimkuta mama yake mkubwa akiwa anasaidiana kufanya kazi na housemaid.

Baada ya kusalimiana waliendelea na mazungumzo,

Mbona mapema sana Sam, wenzio bado wamelala jamani, alihoji mama Kulwa huku akimuonesha tabasamu la upendo ili Samson asijisikie vibaya.

Baada ya Samson kumuona yule mama yupo vizuri akamuuliza swali lake.....

Mama tangu Jana asubuhi baba sijamuona Tena, kwani kasafiri,?

(Huku akicheka)
Hapana mwanangu yupo kwa mama yako mwingine, na leo atakuja kwasababu inatakiwa muende kwa Headmaster akakutambulishe pamoja na kupeleka barua zako, siyo mbali shule ipo nyuma tu hapo.

**************************************Mzee Mgaya aliamka mapema huku akipitia maeneo ya mjini, kuonana na baadhi ya wadau na wazee wenzie kwaajili ya kujadili masuala fulani.
akiwa kule mjini alishangaa kukutana na headmaster wa shule ambayo atasoma Samson, baada ya kusalimiana , walijikuta wanaingia kwenye gari la mzee Mgaya ili waongee zaidi.

Aisee mwalimu, nimefurahi sana kukuona, hata hivyo nilikuwa nataka kuja shuleni kwako, kwaajili ya kuja kukuletea Yale makaratasi, lakini pia nikuoneshe na mwanaelimu mwenyewe, (huku akijichekesha)
Umuone. aliweka kituo Mzee Mgaya.

Haina shida, mzee wangu hata hivyo hakuna haja ya kuleta hizo documents wewe ikifika jumatatu mlete aje aungane na wenzake Kila kitu kitakuwa sawa. alifafanua yule mwalimu.

Mzee Mgaya akakanyaga mafuta Hadi nyumbani kwake ambapo aliikuta familia yake ikiwa salama tu. Aliingia ñdani akafanya shughuli zake Kisha akawaita watoto wake pamoja na Samson akiwaambia wajiandae ili waende kwa mama yao mdogo akamtambulishe Samson.

Baba Kulwa, labda kama sijakusikia vizuri umesema unawapeleka wanangu wapi? alihoji mama Kulwa.

Tunaenda kwa mwenzio kule ila tunarudi muda si mrefu mke wangu. alijibu mzee Mgaya.

Kwahiyo baada ya huyo Malaya wako kushindwa kuniroga Mimi na wanangu, ukaona Bora uwapeleke ili akawatie wazimu kabisa ili washindwe kuendelea na masomo?
Hebu na nyie wajinga shukeni, mnawezaje kucheza na nyoka mwenye sumu kali. aliropoka mama Kulwa.

Mzee Mgaya alijisikia vibaya ila hakutia neno akawa njia panda aende au asiende?

Itaendelea.......................
Tunashukuru dokta wetu
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI

Baada ya muda fulani mzee Mgaya alikuwa na Samson, kwenye gari huku akiwa na mawazo juu ya mkewe mkubwa kuwa na mawazo mabaya kwa Tausi.

Mama Kulwa sijui yupoje yaani, miaka yote kumsingizia Binti wa watu kuwa anamroga, yaani utu uzima wake wote anashindwa kuwa na busara na kuyaacha haya yapite? Hata kama ana chuki moyoni mwake maana asilimia nyingi wake wenza huwa hawapendani, lakini ndiyo aoneshe chuki hadharani vile kiasi Cha kuwazuia watoto wasiende kwa mama yao mdogo?

Hii chuki na mbegu mbaya anayoipanda baadaye itakuja kuisambaratisha familia nafikiri kuna haja ya kufanya kitu kabla mambo hayajaharibika. aliwaza mzee Mgaya huku akikata kona kuingia barabara kubwa.

Kwa upande wa Samson yeye shingo ilikuwa na tabu ya kugeuzwa Kila muda, kutokana na kushangaa majengo makubwa ambayo hakuamini macho yake huku Dar es salaam aliyokuwa akisimuliwa ikiwa tofauti na anavyoiona.

Walipokelewa vizuri na Tausi huku, akionesha tabasamu zuri la upendo kwa wageni wake.

Jamaaani my husband karibuni, karibu tena, bila shaka huyu ndiye mgeni wetu Samson.
aliongea kwa mbwembwe huku wageni wakikaribishwa moja kwa moja kwenye meza ya Chakula.

Eeeeeh uko vizuri mwenzangu ulijuaje kama Nina njaa maana nimejikuta nazunguuuuka mjini hata breakfast sikupata.
aliongea Mzee Mgaya huku akiwa na pupa ya kujipakulia mwenyewe kile Chakula .

Lakini my haya yote sikufanya kwa bahati mbaya uliniambia kwamba utakuja na wageni, Tena uliniambia na akina Kulwa watakuja , vipi mbona ....... alijikuta anashindwa kumalizia sentensi yake huku akimwangalia mumewe kwa makini.

Akina Kulwa unawafahamu, hivyo mgeni ambaye ilikuwa lazima afike hapa ni huyu kijana Samson.
alijibu Kwa mikato.

Unajua nimeandaa Chakula kingi kwa kuzingatia idadi ya watu, kwakuwa uliniambia mwenyewe, kwahiyo hiki kinaenda kuharibika tu masikini.
aliongea Tausi huku akilifunua Hotpot lake na kuangalia jinsi Chakula kilivyokingi.

Hivi ni vyakula tu mke wangu, yaani unasikitika hizo kilo mbili zako za mchele? Mwaka fulani kwenye birthday ya my first born niliwahi kualika watu kwenye tafrija ndogo iliyohusisha mambo mawili kwanza ulikuwa birthday yake, pili alikuwa katoka kumaliza chuo hivyo tukamfanyia kasherehe fulani,
Majirani walialikwa, na watu wengi mbalimbali lakini ilipofika saa tano asubuhi ukatokea msiba mzito wa jirani yangu marehemu mzee
(akimtaja jina)

Basi watu wote tulisitisha zoezi la tafrija majirani wakaondoka kuelekea mita kama miatano tu ulipo msiba, hata Mimi na mama Kulwa tuliiahirisha tafrija yetu tukaelekea kwenye msiba ule wa mtu mzito, hakuna aliyekuwa na hamu hata ya kula Tena.
aliweka kituo mzee Mgaya

Nakumbuka sana, Kuna baadhi ya watu wachache walichomoka msibani na kuja kugonga geti ili mwanao awapakulie chakula nasikia walikula na kusaza lakini bado asilimia themanini ya Chakula kiliharibika. aliongeza Tausi akionesha tukio analikumbuka vizuri.

Baada ya kumaliza kula utambulisho uliendelea,

Mke wangu huyu ni mtoto wa mdogo wangu kabisa, na kutokana na kuridhishwa na matokeo yake ya mitihani mbalimbali nilijikuta nashawishika kumsaidia mdogo wangu, lakini pia kumsaidia huyu mwanangu (akimpigapiga mgongoni Samson)

Japokuwa kulikuwa na changamoto kubwa sana kwenye uhamisho wake ni baada ya walimu wake kufanya uhuni fulani ambao Mimi bila kushirikisha watu wakubwa huenda tusingefanikisha jambo hili.

Na wewe samson, huyu ni mke wangu mwingine maana nasikia uliniulizia kule mbona sijarudi, ni kwamba ukiona sionekani kule basi nipo huku.

Samson alitikia kwa kichwa akionesha kukubaliana na pia aligundua upendo fulani wa kweli toka kwa tausi, alijikuta akipapenda ghafla kwa Tausi japo mandhari na uzuri wa nyumba kule kwa akina Kulwa ni kuzuri zaidi, lakini alipapenda kwa Tausi.

Samson, Mimi ni mama yako mdogo naitwa Tausi, nadhani si vyema sana kukutajia jina langu lakini nitafanyaje Sina mtoto mtaani kote hapa wananiita kwa jina langu,

Kuwa na amani kama Kuna msaada wowote utahitaji hata Ukiwa kule usisite kuniambia,kama Nina uwezo na naafford........

Alikatishwa baada ya mzee Mgaya kumminyia jicho ili aache kuweka mambo mengi wazi, maana angemchanganya Samson, hivyo wakabadili stori.

Mke wangu wiki hii nataka walianza shule Hawa najua sitakuwa bize sana nataka kuanza kukagua miradi yangu yote, maana nashangaa hakuna hata anayeleta hela na pia ni siku nyingi sijatembelea mashine zangu za uzalishaji wa mbao (Sawmill) mbaya zaidi nasikia kuwa wateja wameongezeka wanaleta mizigo nadhani huu ni muda muafaka wa kuwa karibu tunaibiwa ujue. alitania mzee Mgaya huku akiinuka kwenye kiti chake na kutoka nje.

Baada ya kutoka nje mzee Mgaya Tausi aliitumia fursa ile kutaka kumpeleleza Samson mambo fulani ikiwemo kushawishi ahamie kwake,

Sawa mama, ila Mimi kumbuka si mwenyeji wa mji huu, hata ukisema nirudi kule kwa mama mkubwa Wala hata sijui naanzia wapi, kuja huku nitakuja ila lazima niwe na mwenyeji.
alijitetea Samson.

Sasa mke wangu Mimi naondoka na kesho nawapeleka akina Kulwa huko shuleni kwao tayari kwa kuanza maisha mapya, najua hawatakuwa wapweke kwakuwa wapo wawili, ila nitawamisi wanangu. alisema Mzee Mgaya bila kujua kama anazidi kumuudhi Tausi ambaye huwa hapendi umtambie suala la watoto mbele yake.

Mimi naona mke wangu nikuage na Leo sitarudi hapa nataka niamkie kule iwe rahisi kupunguza foleni barabarani, wakaingia kwenye gari na Samson tayari wakirudi ndani.

Tausi ni mwanamke fulani anajiamini sana kuanzia mtaani hadi kazini kwake, ila kuwa alone kulimtesa sana, na yote hayo alijua mchawi wake ni mama Kulwa alishindwa kujua ni lini atapata mtoto kitendo Cha mke mkubwa kupata watoto mapacha huku yeye akiwa Hana mtoto, aliumia sana,alimuona mchawi wa maisha yake ni mama Kulwa

alihitaji kuwa na mtu angalau wa kulinda nyumba yake, na kwa mtazamo wake aliona Samson kijana aliyetambulishwa muda si mrefu angemfaa.

Kwa upande wa mama Kulwa naye alijua mchawi wa maisha yake ni Tausi, kitendo Cha yeye kupata watoto kwenye umri mkubwa tena mapacha aliona ni baraka toka kwa MUNGU mwenyewe lakini ni kipindi ambacho alizisikia maneno mengi ya shombo toka kwa tausi akiitwa mchawi.

Mzee Mgaya alipiga honi kutaka afunguliwe mlango Mara baada ya kukaribia geti la nyumba yake, alishangaa kuona geti likifunguliwa na mkewe ambapo si kawaida..

Haya baba naona umeenda kwa changudoa wako, umepewa ulichopewa lengo uje utuangamize humu ndani, haya kama unachakufukia, fukia baba. Najua unampenda sana yule aliyeharibu kizazi kwa umalaya wake na leo hii unataka kuwaua wanangu ili umfurahishe yule kahaba Sasa nakwambia niuwe Mimi kwanza kuuuutwa nzima unazurura Mara uende huku Mara huku una Nini wewe baba Kulwa ? aliendelea kubwata yule mama ambaye hata kitenge alichovaa kilimvuka na kubaki na gauni lake tu.

Mama vipi twende ndani mama yangu kwani Kuna nini, alihoji dada wa kazi huku akimtoa boss wake na kuingia ndani , wakati huo Mzee Mgaya alimpuuza tu, anamjua wazi ni mlevi wa pombe alitambua vyema kama atakuwa kaonja, hata wanae wakina Kulwa walichukulia kawaida tu maana wanalijua gubu la mama yao.

Kwa upande wa Samson alikuwa na hofu kubwa sana, alimuona rasmi mama yule alivyo mkali sana, alizidi kutetemeka huku akiingia ndani kwa uoga.Mama Kulwa alikuwa ni nusu kichaa hasa akikasirika,aliwaza namna atakavyoishi naye akajikuta ana kibarua kikubwa Cha kuhakikisha hamuudhi yule mama, ambaye ni nesi mstaafu aliyefanya kazi miaka mingi hospital ya taifa Muhimbili .Samson akajikuta anaanza kuona mahali pale ni kwa moto

Itaendelea......... ............
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI

Baada ya muda fulani mzee Mgaya alikuwa na Samson, kwenye gari huku akiwa na mawazo juu ya mkewe mkubwa kuwa na mawazo mabaya kwa Tausi.

Mama Kulwa sijui yupoje yaani, miaka yote kumsingizia Binti wa watu kuwa anamroga, yaani utu uzima wake wote anashindwa kuwa na busara na kuyaacha haya yapite? Hata kama ana chuki moyoni mwake maana asilimia nyingi wake wenza huwa hawapendani, lakini ndiyo aoneshe chuki hadharani vile kiasi Cha kuwazuia watoto wasiende kwa mama yao mdogo?

Hii chuki na mbegu mbaya anayoipanda baadaye itakuja kuisambaratisha familia nafikiri kuna haja ya kufanya kitu kabla mambo hayajaharibika. aliwaza mzee Mgaya huku akikata kona kuingia barabara kubwa.

Kwa upande wa Samson yeye shingo ilikuwa na tabu ya kugeuzwa Kila muda, kutokana na kushangaa majengo makubwa ambayo hakuamini macho yake huku Dar es salaam aliyokuwa akisimuliwa ikiwa tofauti na anavyoiona.

Walipokelewa vizuri na Tausi huku, akionesha tabasamu zuri la upendo kwa wageni wake.

Jamaaani my husband karibuni, karibu tena, bila shaka huyu ndiye mgeni wetu Samson.
aliongea kwa mbwembwe huku wageni wakikaribishwa moja kwa moja kwenye meza ya Chakula.

Eeeeeh uko vizuri mwenzangu ulijuaje kama Nina njaa maana nimejikuta nazunguuuuka mjini hata breakfast sikupata.
aliongea Mzee Mgaya huku akiwa na pupa ya kujipakulia mwenyewe kile Chakula .

Lakini my haya yote sikufanya kwa bahati mbaya uliniambia kwamba utakuja na wageni, Tena uliniambia na akina Kulwa watakuja , vipi mbona ....... alijikuta anashindwa kumalizia sentensi yake huku akimwangalia mumewe kwa makini.

Akina Kulwa unawafahamu, hivyo mgeni ambaye ilikuwa lazima afike hapa ni huyu kijana Samson.
alijibu Kwa mikato.

Unajua nimeandaa Chakula kingi kwa kuzingatia idadi ya watu, kwakuwa uliniambia mwenyewe, kwahiyo hiki kinaenda kuharibika tu masikini.
aliongea Tausi huku akilifunua Hotpot lake na kuangalia jinsi Chakula kilivyokingi.

Hivi ni vyakula tu mke wangu, yaani unasikitika hizo kilo mbili zako za mchele? Mwaka fulani kwenye birthday ya my first born niliwahi kualika watu kwenye tafrija ndogo iliyohusisha mambo mawili kwanza ulikuwa birthday yake, pili alikuwa katoka kumaliza chuo hivyo tukamfanyia kasherehe fulani,
Majirani walialikwa, na watu wengi mbalimbali lakini ilipofika saa tano asubuhi ukatokea msiba mzito wa jirani yangu marehemu mzee
(akimtaja jina)

Basi watu wote tulisitisha zoezi la tafrija majirani wakaondoka kuelekea mita kama miatano tu ulipo msiba, hata Mimi na mama Kulwa tuliiahirisha tafrija yetu tukaelekea kwenye msiba ule wa mtu mzito, hakuna aliyekuwa na hamu hata ya kula Tena.
aliweka kituo mzee Mgaya

Nakumbuka sana, Kuna baadhi ya watu wachache walichomoka msibani na kuja kugonga geti ili mwanao awapakulie chakula nasikia walikula na kusaza lakini bado asilimia themanini ya Chakula kiliharibika. aliongeza Tausi akionesha tukio analikumbuka vizuri.

Baada ya kumaliza kula utambulisho uliendelea,

Mke wangu huyu ni mtoto wa mdogo wangu kabisa, na kutokana na kuridhishwa na matokeo yake ya mitihani mbalimbali nilijikuta nashawishika kumsaidia mdogo wangu, lakini pia kumsaidia huyu mwanangu (akimpigapiga mgongoni Samson)

Japokuwa kulikuwa na changamoto kubwa sana kwenye uhamisho wake ni baada ya walimu wake kufanya uhuni fulani ambao Mimi bila kushirikisha watu wakubwa huenda tusingefanikisha jambo hili.

Na wewe samson, huyu ni mke wangu mwingine maana nasikia uliniulizia kule mbona sijarudi, ni kwamba ukiona sionekani kule basi nipo huku.

Samson alitikia kwa kichwa akionesha kukubaliana na pia aligundua upendo fulani wa kweli toka kwa tausi, alijikuta akipapenda ghafla kwa Tausi japo mandhari na uzuri wa nyumba kule kwa akina Kulwa ni kuzuri zaidi, lakini alipapenda kwa Tausi.

Samson, Mimi ni mama yako mdogo naitwa Tausi, nadhani si vyema sana kukutajia jina langu lakini nitafanyaje Sina mtoto mtaani kote hapa wananiita kwa jina langu,

Kuwa na amani kama Kuna msaada wowote utahitaji hata Ukiwa kule usisite kuniambia,kama Nina uwezo na naafford........

Alikatishwa baada ya mzee Mgaya kumminyia jicho ili aache kuweka mambo mengi wazi, maana angemchanganya Samson, hivyo wakabadili stori.

Mke wangu wiki hii nataka walianza shule Hawa najua sitakuwa bize sana nataka kuanza kukagua miradi yangu yote, maana nashangaa hakuna hata anayeleta hela na pia ni siku nyingi sijatembelea mashine zangu za uzalishaji wa mbao (Sawmill) mbaya zaidi nasikia kuwa wateja wameongezeka wanaleta mizigo nadhani huu ni muda muafaka wa kuwa karibu tunaibiwa ujue. alitania mzee Mgaya huku akiinuka kwenye kiti chake na kutoka nje.

Baada ya kutoka nje mzee Mgaya Tausi aliitumia fursa ile kutaka kumpeleleza Samson mambo fulani ikiwemo kushawishi ahamie kwake,

Sawa mama, ila Mimi kumbuka si mwenyeji wa mji huu, hata ukisema nirudi kule kwa mama mkubwa Wala hata sijui naanzia wapi, kuja huku nitakuja ila lazima niwe na mwenyeji.
alijitetea Samson.

Sasa mke wangu Mimi naondoka na kesho nawapeleka akina Kulwa huko shuleni kwao tayari kwa kuanza maisha mapya, najua hawatakuwa wapweke kwakuwa wapo wawili, ila nitawamisi wanangu. alisema Mzee Mgaya bila kujua kama anazidi kumuudhi Tausi ambaye huwa hapendi umtambie suala la watoto mbele yake.

Mimi naona mke wangu nikuage na Leo sitarudi hapa nataka niamkie kule iwe rahisi kupunguza foleni barabarani, wakaingia kwenye gari na Samson tayari wakirudi ndani.

Tausi ni mwanamke fulani anajiamini sana kuanzia mtaani hadi kazini kwake, ila kuwa alone kulimtesa sana, na yote hayo alijua mchawi wake ni mama Kulwa alishindwa kujua ni lini atapata mtoto kitendo Cha mke mkubwa kupata watoto mapacha huku yeye akiwa Hana mtoto, aliumia sana,alimuona mchawi wa maisha yake ni mama Kulwa

alihitaji kuwa na mtu angalau wa kulinda nyumba yake, na kwa mtazamo wake aliona Samson kijana aliyetambulishwa muda si mrefu angemfaa.

Kwa upande wa mama Kulwa naye alijua mchawi wa maisha yake ni Tausi, kitendo Cha yeye kupata watoto kwenye umri mkubwa tena mapacha aliona ni baraka toka kwa MUNGU mwenyewe lakini ni kipindi ambacho alizisikia maneno mengi ya shombo toka kwa tausi akiitwa mchawi.

Mzee Mgaya alipiga honi kutaka afunguliwe mlango Mara baada ya kukaribia geti la nyumba yake, alishangaa kuona geti likifunguliwa na mkewe ambapo si kawaida..

Haya baba naona umeenda kwa changudoa wako, umepewa ulichopewa lengo uje utuangamize humu ndani, haya kama unachakufukia, fukia baba. Najua unampenda sana yule aliyeharibu kizazi kwa umalaya wake na leo hii unataka kuwaua wanangu ili umfurahishe yule kahaba Sasa nakwambia niuwe Mimi kwanza kuuuutwa nzima unazurura Mara uende huku Mara huku una Nini wewe baba Kulwa ? aliendelea kubwata yule mama ambaye hata kitenge alichovaa kilimvuka na kubaki na gauni lake tu.

Mama vipi twende ndani mama yangu kwani Kuna nini, alihoji dada wa kazi huku akimtoa boss wake na kuingia ndani , wakati huo Mzee Mgaya alimpuuza tu, anamjua wazi ni mlevi wa pombe alitambua vyema kama atakuwa kaonja, hata wanae wakina Kulwa walichukulia kawaida tu maana wanalijua gubu la mama yao.

Kwa upande wa Samson alikuwa na hofu kubwa sana, alimuona rasmi mama yule alivyo mkali sana, alizidi kutetemeka huku akiingia ndani kwa uoga.Mama Kulwa alikuwa ni nusu kichaa hasa akikasirika,aliwaza namna atakavyoishi naye akajikuta ana kibarua kikubwa Cha kuhakikisha hamuudhi yule mama, ambaye ni nesi mstaafu aliyefanya kazi miaka mingi hospital ya taifa Muhimbili .Samson akajikuta anaanza kuona mahali pale ni kwa moto

Itaendelea......... ............
moneytalk njoo kumenoga uku
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom