Simulizi: Milango ya mafanikio

Simulizi: Milango ya mafanikio

SEHEMU YA AROBAINI NA SITA

Mida ya saa kumi jioni, Samson alimuaga mama yake kuwa anaenda kwenye group discussion ambapo hakukuwa mbali na nyumbani kwao.

Sasa Sam mwananguuuu, kwanini Kila siku wewe uwe unaenda kusoma huko na kumbuka umekuwa ukirudi usiku, kwanini hao wenzio na siku moja moja wasije hapa kwako?
aliuliza mama Kulwa.

Sawa mama nimekuelewa sana, ila sisi kwenye group letu tumependekeza kukutania kwa mwl {akitaja jina} pale Kuna wanafunzi wa madarasa ya juu nao huwa wanafanya discussion zao pale, hivyo tumeamua na sisi kukutana pale ili pindi kama Kuna mada inatushinda basi tunaomba msaada kwa wenzetu.alijibu Samson.

Sawa ila kumbuka kuzingatia muda,maana huu mji tunaujua wenyewe, alitahadharisha mama Kulwa.

Wakati Samson anatoka nje ya geti,
Hamadi, alikutana na Tausi au mama yake mdogo akiwa anashuka kwenye Taxi, wakasalimiana,
Enheee vipi mwenzetu na mabegi wapi tena, aliuliza Tausi.

Naenda nyuma tu hapo huwa tunajisomea na marafiki zangu,alijibu Samson akitaka kupiga hatua kwenda atakapo.
Lakini akashikwa mkono na Tausi.

Vipi Baba yako Mzee Mgaya yupo? Maana ana siku kadhaa nyumbani hajaja? Tausi aliuliza.

Hapana baba yupo nje ya Dar, kaenda sehemu ambako amesema anataka kwenda kufanya mahesabu kwani kapata tenda ya kutengeneza milango ya shule. alijibu Kwa kifupi Samson.
Vizuri sana,hebu nambie huyu mpumbavu Rahma bado yupo hapa, maana mtoto mjinga sijapata kuona, yaani siku ya tano kang'ang'ania kukaa hapa anadhani Hawa nao ni ndugu zake? Hebu kwanza niingie ndani. aliongea Tausi huku akisukuma mlango wa geti dogo kwa nguvu Samson kuona vile ikabidi naye aingie ndani maana alijua hali huenda isiwe shwari.

Haya niambie wewe mtoto Malaya usiye na mipaka, usiye kuwa na adabu, umekaa hapa siku zote hata aibu huna mtoto wa kike, haya tufanye anatokea mtu anakuuliza huyu mama upoje nae, utamjibu nini?
Maana si ndugu yako, Wala wewe si mfanyakazi wake, halafu unawezaje kuwaamini watu baki kiasi hicho? Kipindi nakuleta mjini nilikuasa kuhusu, mazoea au kumwamini mtu haraka, lakini wewe msungo usiyefundwa husikii Wala huelewi.
Tausi alizidi kuropoka huku akiwa hajasalimia mtu yoyote mle ndani.

Wakati huo mama Kulwa alikaa kwa kutulia akiwa anamtazama Tausi kwa umakini namna anavyofoka, huku Rahma akiwa kasimamisha zoezi lake la kufua akiwa nusu nusu ,asimame, au akae,
Amjibu Tausi au asimjibu,
Uso wake ulionesha hasira za wazi huku akionesha anataka kulia.

Najua, tena najua kilichokuleta huku, na nikwambie tu kuwa wakijua lengo lako, watakufukuza kama mbwa Malaya wewe, mtoto mdogo unaendekeza ukahaba, najaribu kukuonya unanikimbia,
Tena unakimbilia kwa watu tu ambao si ndugu zako, kwanza ngoja nikuoneshe, Tausi alimrukia Rahma na kutaka kumpiga, bahati nzuri mwanaume mmoja mwenye nguvu aliwatenganisha huku naye akiwa na malalamiko kadhaa, si mwingine ni dereva Taxi aliyemleta Tausi.

Wewe dada mimi unanichukuliaje?
Hebu nipe hela yangu, Mimi niondoke hela tena nimekufanyia msaada tu kutoka kule hadi huku mbali hivi ningejua nisingekuja, alicomplain yule dereva.

Kwani Kuna nini baba, tena nashangaa unaingia ndani kwangu bila hata hodi, aliuliza mama Kulwa.

Samahani sana mama, Mimi ni dereva nimemleta huyu aunt, Sasa nashangaa ananisubirisha hapo nje, halafu alivyopanic nikaona atanichelewesha, Mimi natafuta hesabu mama. aliongea kwa uchungu dereva.

Acha ujinga na wewe uliambiwa hela yako sikupi, kwanza pale kituoni hata sikukuita wewe, ulijipendekeza tu,umri huo bado unagombania abiria na vijana,Mimi dereva wangu huwa ananivumilia, aliongea Tausi huku akimrushia hela yule jamaa,Kisha dereva wa watu akaiokota ile hela na kutokomea

Hebu watu wote njooni ndani kwanza na Samson funga geti na kufuli maana naona watu wanaingia tu humu kama choo cha umma.

Kwanza mdogo wangu Tausi nikusalimie, eeh nianze Mimi maana mtoto wa kike umefika tu na kuanza kutiririka maneno bila kujali hii ni nyumba ya mtu mwenzangu
Aliongea kwa utulivu mama Kulwa.

Kwanza dada nisamehe tu, kwakweli Nina jazba sana, huyu Binti alichofanya mpaka Sasa simuelewi nashindwa nikulaumu wewe au yeye,
Wewe dada umewezaje kukaa na mtoto wa mtu sikuzote,
Na yeye anawezaje kukaa kwa mtu muda wote huo? Tausi alianza kumlaumu mama Kulwa.

Tausi, nakuita kwa jina lako, Kuna vitu vingi unakosea na vinakushinda, kwanza unakosea kuniuliza hivyo,
Umekuja hapa umeanza kupiga kelele kwenye nyumba yangu sijakuuliza. nimekuita kwa upole tuongee ndani tuweke sawa haya mambo, umetukana weweee lakini nimekuacha tu, hii ni nyumba yangu inaheshimika na watu wengi, unadhani watu waliosikia neno Malaya na matusi kibao uliyotukana watatuchukuliaje wakazi wa humu,
Sasa naelewa kwanini Mzee Mgaya kasema Samson arudi hapa, labda ni nidhamu mbovu uliyokuwa nayo.

Unasema Rahma siyo ndugu yangu ni kweli, lakini huwa Kuna sababu zinazofanya watu wajenge undugu, wote hapa watatu nyinyi Mimi kikawaida siwajui.

Wewe ni mke wa mume wangu, hivyo tayari una undugu na Mimi.

Samson ni mtoto wa shemeji yangu hivyo ni mwanangu pia,
Huyu Rahma kakimbilia hapa pindi mmekwaruzana, najua alijua ni wapi anaenda asingekuja hapa kama hatufahamu sisi, huo ukurasa naufunga haya naomba shoga yangu uniambie Nini kinasababisha ugombane na Binti mdogo kama huyu, yaani kwanza inashangaza ujue,
aliweka kituo mama Kulwa.

Dada nisikufiche huyu mtoto, ana tabia mbaya sana na ndugu zake wanamtafuta wanasema nimsafirishe aende nyumbani kwao Tanga, Mimi sitaweza kukaa naye kwasababu tutakuja kufikishana pabaya, alileta sababu za uongo Tausi.

Mnajua wawili nyinyi mna ugomvi mkubwa sana halafu mkiulizwa mna majibu mepesi sana, yasiyoingia akilini, sasa niseme tu wazi kuwa, Mzee Mgaya anarudi leo hii na yeye ndiye atakuja kumleta rahma kwako , maana kwa hali hii nawaona kabisa mlivyo kama paka na panya hivyo sitaruhusu huyu aondoke.

Mama Kulwa samahani Mimi Kwa mamdogo siendi na kama narudi Tanga nitatokea hapa, ananiita Malaya wakati umalaya kaanza yeye, au anafikiri sijui tunachogombania, Mimi kwanza sitaki kwenda Tanga Wala wapi Mimi kama mtataka niwe mfanyakazi wa humu ndani, nitakubali ila si kwenda kwa mamdogo. aliongea Rahma akionesha kukerwa na akimaanisha liwalo na liwe.

Mama Kulwa alizidi kushangaa tu kwani hakujua chochote,
Kwa upande wa Samson alianza kuona hata njaa inapotea ghafla,
Na hofu kubwa ilitanda moyoni mwake, aliona jinsi Rahma na Tausi walivyo na hasira, na kwenye hasira mtu anaweza kuropoka chochote kile bila kujali itakuwaje na majuto huja baadaye.

Eti Sam wewe umeishi na Hawa watu kipindi kirefu, vipi huwa wapo hivi hivi maana siwaelewi?
aliuliza Mama Kulwa.

Sijawahi kuiona hii hali, ndiyo kwanza naona, siku zote tuliishi kama ndugu tukiwa na furaha sana tu Sasa hata sijui ni kwanini inakuwa hivi, watu hawaeleweki. alijibu Samson.

Halafu wewe mpuuzi wewe ndiyo chanzo cha matatizo yote, Sasa nitakukomesha mchawi mkubwa wewe, kila sehemu ukikaa wewe lazima kutokee matatizo na Dada nikwambie tu kuwa huyu mwanga kurudi hapa lazima kutatokea matatizo utakuja kuniambia.
aliongea Tausi huku akibana mkoba wake na kutoka nje kwa hasira.

Samson nenda kafungue mlango maana Mimi hata siwaelewi ngoja arudi mzee Mgaya atajua cha kufanya, yanini Mimi niumize kichwa kwa watoto wasio wangu. aliongea kwa dharau mama Kulwa.

Wakati Samson anafungua mlango ili Tausi atoke, Tausi akavunja ukimya.
Samson naomba haya masuala yasikuumize kichwa ila sharti langu ni Moja naomba uage si bado mapema! Jifanye unaenda kwa marafiki zako, halafu twende kwangu, na usipofanya hivi, nitamwambia Mzee Mgaya ulitaka kunibaka na Nina ushahidi maana Kuna bukta yako ya blue ninayo. aliongea Tausi akiwa hatanii.

Moyo ulimuenda mbio Samson ni kweli nguo yake ilipotea na aliitafuta bila mafanikio ila alipuuza tu kuwa huenda ilipotea, hakuwaza kuwa imechukuliwa na mtu, na kutokana na alivyotishwa ilibidi atii amri ya Tausi.

Sasa mamdogo inabidi utangulie si vizuri kuongozana, alijitetea Samson

Hilo mimi silijui, uje usije utajua mwenyewe. alijibu Kwa kujiamini Tausi hasa baada ya kuusoma uso wa Samson na kukiri kuwa ana uoga fulani akajiona kasukuma kete ya ushindi akaondoka zake.

Muda wa saa mbili usiku, Samson alifika kwa Tausi akimkuta yupo na kanga tu huku akionesha hajavaa kitu chochote ndani.

Habari za muda huu mamdogo, alisalimia Samson.

Huko kijijini kwenu ulikotoka mama yako mzazi hana wadogo zake ambao utawaita mama zako wadogo? au mama yako alikwambia na Tausi naye umuite mama yako eeeh. aliongea Tausi huku akitabasamu kimahaba.

Sasa nikuiteje? Samson aliuliza huku ujio wa huku akiwa hajaupenda ni kwasababu alilazimishwa tu.

Wakati Tausi akijiandaa kuja mahali alipo Samson, mlango ulisukumwa , do mwingine alikuwa ni Mzee Mgaya akiwa na mfuko mdogo, Tausi alimrukia na kumkumbatia Mzee Mgaya akijifanya alim miss sana.

Habari za siku my husband mbona ghafla halafu nilienda kumfuata Rahma kule kwa Dada mama Kulwa nikaambiwa umesafiri my mbona hukuniaga ? aliongea kwa kujibebisha Tausi.

Subiri nitakwambia, ndiyo maana nimekuja, halafu mbona mnaacha geti wazi vile halafu, mmekaa tu ndani bila wasiwasi, mmesahau timeshaibiwa Mara ngapi humu ndani ohooooh haya nyie jisahaulisheni tu.
aliongea Mzee Mgaya huku Samson akijikuta ni yeye alisahau kufunga.

Mke wangu kwanza samahani niliondoka ghafla nilienda huko njia za kusini lakini ni vijiji vya katikati tu ndani ya Mkoa wa Pwani. Kunaitwa Ikwiriri, huko nimegundua upatikanaji wa miti ya furniture kiurahisi, ingawaje nimekaa siku chache ila nimefanikiwa kupata data kadhaa ambazo nimezipenda na uzuri hapo ni jirani yaani kwa gari binafsi ni masaa mawili na nusu tu kutoka hapa mjini. alifafanua mzee Mgaya

Sasa my hujaja na gari umeacha wapi,maana ujio wako sikuzote huwa ni honi ya gari nashangaa leo umekuja kimyakimya.
aliongea kwa kuzuga Tausi.

Wala sijaja kimyakimya, ni kwamba lazima ningegonga geti, lakini lilikuwa wazi eti. Nikajikuta naingia kwa tahadhari nikijua labda ni wezi.
Kuhusu gari nimeliacha huko huko, kwasababu limeharibika yaani gari linanisumbua acha tu hata hivyo Kuna fundi nimewasiliana naye ataenda kulivuta ataleta mjini na pia najipanga ninunue lingine maana ipo siku lile gari litanilaza porini.
aliongea Mzee Mgaya huku wote wakicheka kasoro Samson aliyekuwa na hofu.

Halafu mke wangu, huu uvaaji gani mbele ya mwanao, na kila siku nakwambia mbona huelewi wewe.
Halafu huyu Sam naye hapa kafuata nini,? Eti Sam ulisahau Nini hapa. aliuliza

Kuna vitabu vyangu , kule nyumbani sivioni Sasa nikimuuliza mamdogo kama aliviona akadai yeye hajui, nikasema basi nitakuja kuangalia mwenyewe. aliongopa Samson huku Tausi akitoa tano ya hewani jinsi Samson alivyojitetea .

Mzee Mgaya aliwaangalia Tausi na Samson kwa zamu Kisha akainuka na kuingia chumbani bila kusema chochote.huku ikionekana hajaridhishwa na majibu ya Samson

Itaendelea...................
 
SEHEMU YA AROBAINI NA SITA

Mida ya saa kumi jioni, Samson alimuaga mama yake kuwa anaenda kwenye group discussion ambapo hakukuwa mbali na nyumbani kwao.

Sasa Sam mwananguuuu, kwanini Kila siku wewe uwe unaenda kusoma huko na kumbuka umekuwa ukirudi usiku, kwanini hao wenzio na siku moja moja wasije hapa kwako?
aliuliza mama Kulwa.

Sawa mama nimekuelewa sana, ila sisi kwenye group letu tumependekeza kukutania kwa mwl {akitaja jina} pale Kuna wanafunzi wa madarasa ya juu nao huwa wanafanya discussion zao pale, hivyo tumeamua na sisi kukutana pale ili pindi kama Kuna mada inatushinda basi tunaomba msaada kwa wenzetu.alijibu Samson.

Sawa ila kumbuka kuzingatia muda,maana huu mji tunaujua wenyewe, alitahadharisha mama Kulwa.

Wakati Samson anatoka nje ya geti,
Hamadi, alikutana na Tausi au mama yake mdogo akiwa anashuka kwenye Taxi, wakasalimiana,
Enheee vipi mwenzetu na mabegi wapi tena, aliuliza Tausi.

Naenda nyuma tu hapo huwa tunajisomea na marafiki zangu,alijibu Samson akitaka kupiga hatua kwenda atakapo.
Lakini akashikwa mkono na Tausi.

Vipi Baba yako Mzee Mgaya yupo? Maana ana siku kadhaa nyumbani hajaja? Tausi aliuliza.

Hapana baba yupo nje ya Dar, kaenda sehemu ambako amesema anataka kwenda kufanya mahesabu kwani kapata tenda ya kutengeneza milango ya shule. alijibu Kwa kifupi Samson.
Vizuri sana,hebu nambie huyu mpumbavu Rahma bado yupo hapa, maana mtoto mjinga sijapata kuona, yaani siku ya tano kang'ang'ania kukaa hapa anadhani Hawa nao ni ndugu zake? Hebu kwanza niingie ndani. aliongea Tausi huku akisukuma mlango wa geti dogo kwa nguvu Samson kuona vile ikabidi naye aingie ndani maana alijua hali huenda isiwe shwari.

Haya niambie wewe mtoto Malaya usiye na mipaka, usiye kuwa na adabu, umekaa hapa siku zote hata aibu huna mtoto wa kike, haya tufanye anatokea mtu anakuuliza huyu mama upoje nae, utamjibu nini?
Maana si ndugu yako, Wala wewe si mfanyakazi wake, halafu unawezaje kuwaamini watu baki kiasi hicho? Kipindi nakuleta mjini nilikuasa kuhusu, mazoea au kumwamini mtu haraka, lakini wewe msungo usiyefundwa husikii Wala huelewi.
Tausi alizidi kuropoka huku akiwa hajasalimia mtu yoyote mle ndani.

Wakati huo mama Kulwa alikaa kwa kutulia akiwa anamtazama Tausi kwa umakini namna anavyofoka, huku Rahma akiwa kasimamisha zoezi lake la kufua akiwa nusu nusu ,asimame, au akae,
Amjibu Tausi au asimjibu,
Uso wake ulionesha hasira za wazi huku akionesha anataka kulia.

Najua, tena najua kilichokuleta huku, na nikwambie tu kuwa wakijua lengo lako, watakufukuza kama mbwa Malaya wewe, mtoto mdogo unaendekeza ukahaba, najaribu kukuonya unanikimbia,
Tena unakimbilia kwa watu tu ambao si ndugu zako, kwanza ngoja nikuoneshe, Tausi alimrukia Rahma na kutaka kumpiga, bahati nzuri mwanaume mmoja mwenye nguvu aliwatenganisha huku naye akiwa na malalamiko kadhaa, si mwingine ni dereva Taxi aliyemleta Tausi.

Wewe dada mimi unanichukuliaje?
Hebu nipe hela yangu, Mimi niondoke hela tena nimekufanyia msaada tu kutoka kule hadi huku mbali hivi ningejua nisingekuja, alicomplain yule dereva.

Kwani Kuna nini baba, tena nashangaa unaingia ndani kwangu bila hata hodi, aliuliza mama Kulwa.

Samahani sana mama, Mimi ni dereva nimemleta huyu aunt, Sasa nashangaa ananisubirisha hapo nje, halafu alivyopanic nikaona atanichelewesha, Mimi natafuta hesabu mama. aliongea kwa uchungu dereva.

Acha ujinga na wewe uliambiwa hela yako sikupi, kwanza pale kituoni hata sikukuita wewe, ulijipendekeza tu,umri huo bado unagombania abiria na vijana,Mimi dereva wangu huwa ananivumilia, aliongea Tausi huku akimrushia hela yule jamaa,Kisha dereva wa watu akaiokota ile hela na kutokomea

Hebu watu wote njooni ndani kwanza na Samson funga geti na kufuli maana naona watu wanaingia tu humu kama choo cha umma.

Kwanza mdogo wangu Tausi nikusalimie, eeh nianze Mimi maana mtoto wa kike umefika tu na kuanza kutiririka maneno bila kujali hii ni nyumba ya mtu mwenzangu
Aliongea kwa utulivu mama Kulwa.

Kwanza dada nisamehe tu, kwakweli Nina jazba sana, huyu Binti alichofanya mpaka Sasa simuelewi nashindwa nikulaumu wewe au yeye,
Wewe dada umewezaje kukaa na mtoto wa mtu sikuzote,
Na yeye anawezaje kukaa kwa mtu muda wote huo? Tausi alianza kumlaumu mama Kulwa.

Tausi, nakuita kwa jina lako, Kuna vitu vingi unakosea na vinakushinda, kwanza unakosea kuniuliza hivyo,
Umekuja hapa umeanza kupiga kelele kwenye nyumba yangu sijakuuliza. nimekuita kwa upole tuongee ndani tuweke sawa haya mambo, umetukana weweee lakini nimekuacha tu, hii ni nyumba yangu inaheshimika na watu wengi, unadhani watu waliosikia neno Malaya na matusi kibao uliyotukana watatuchukuliaje wakazi wa humu,
Sasa naelewa kwanini Mzee Mgaya kasema Samson arudi hapa, labda ni nidhamu mbovu uliyokuwa nayo.

Unasema Rahma siyo ndugu yangu ni kweli, lakini huwa Kuna sababu zinazofanya watu wajenge undugu, wote hapa watatu nyinyi Mimi kikawaida siwajui.

Wewe ni mke wa mume wangu, hivyo tayari una undugu na Mimi.

Samson ni mtoto wa shemeji yangu hivyo ni mwanangu pia,
Huyu Rahma kakimbilia hapa pindi mmekwaruzana, najua alijua ni wapi anaenda asingekuja hapa kama hatufahamu sisi, huo ukurasa naufunga haya naomba shoga yangu uniambie Nini kinasababisha ugombane na Binti mdogo kama huyu, yaani kwanza inashangaza ujue,
aliweka kituo mama Kulwa.

Dada nisikufiche huyu mtoto, ana tabia mbaya sana na ndugu zake wanamtafuta wanasema nimsafirishe aende nyumbani kwao Tanga, Mimi sitaweza kukaa naye kwasababu tutakuja kufikishana pabaya, alileta sababu za uongo Tausi.

Mnajua wawili nyinyi mna ugomvi mkubwa sana halafu mkiulizwa mna majibu mepesi sana, yasiyoingia akilini, sasa niseme tu wazi kuwa, Mzee Mgaya anarudi leo hii na yeye ndiye atakuja kumleta rahma kwako , maana kwa hali hii nawaona kabisa mlivyo kama paka na panya hivyo sitaruhusu huyu aondoke.

Mama Kulwa samahani Mimi Kwa mamdogo siendi na kama narudi Tanga nitatokea hapa, ananiita Malaya wakati umalaya kaanza yeye, au anafikiri sijui tunachogombania, Mimi kwanza sitaki kwenda Tanga Wala wapi Mimi kama mtataka niwe mfanyakazi wa humu ndani, nitakubali ila si kwenda kwa mamdogo. aliongea Rahma akionesha kukerwa na akimaanisha liwalo na liwe.

Mama Kulwa alizidi kushangaa tu kwani hakujua chochote,
Kwa upande wa Samson alianza kuona hata njaa inapotea ghafla,
Na hofu kubwa ilitanda moyoni mwake, aliona jinsi Rahma na Tausi walivyo na hasira, na kwenye hasira mtu anaweza kuropoka chochote kile bila kujali itakuwaje na majuto huja baadaye.

Eti Sam wewe umeishi na Hawa watu kipindi kirefu, vipi huwa wapo hivi hivi maana siwaelewi?
aliuliza Mama Kulwa.

Sijawahi kuiona hii hali, ndiyo kwanza naona, siku zote tuliishi kama ndugu tukiwa na furaha sana tu Sasa hata sijui ni kwanini inakuwa hivi, watu hawaeleweki. alijibu Samson.

Halafu wewe mpuuzi wewe ndiyo chanzo cha matatizo yote, Sasa nitakukomesha mchawi mkubwa wewe, kila sehemu ukikaa wewe lazima kutokee matatizo na Dada nikwambie tu kuwa huyu mwanga kurudi hapa lazima kutatokea matatizo utakuja kuniambia.
aliongea Tausi huku akibana mkoba wake na kutoka nje kwa hasira.

Samson nenda kafungue mlango maana Mimi hata siwaelewi ngoja arudi mzee Mgaya atajua cha kufanya, yanini Mimi niumize kichwa kwa watoto wasio wangu. aliongea kwa dharau mama Kulwa.

Wakati Samson anafungua mlango ili Tausi atoke, Tausi akavunja ukimya.
Samson naomba haya masuala yasikuumize kichwa ila sharti langu ni Moja naomba uage si bado mapema! Jifanye unaenda kwa marafiki zako, halafu twende kwangu, na usipofanya hivi, nitamwambia Mzee Mgaya ulitaka kunibaka na Nina ushahidi maana Kuna bukta yako ya blue ninayo. aliongea Tausi akiwa hatanii.

Moyo ulimuenda mbio Samson ni kweli nguo yake ilipotea na aliitafuta bila mafanikio ila alipuuza tu kuwa huenda ilipotea, hakuwaza kuwa imechukuliwa na mtu, na kutokana na alivyotishwa ilibidi atii amri ya Tausi.

Sasa mamdogo inabidi utangulie si vizuri kuongozana, alijitetea Samson

Hilo mimi silijui, uje usije utajua mwenyewe. alijibu Kwa kujiamini Tausi hasa baada ya kuusoma uso wa Samson na kukiri kuwa ana uoga fulani akajiona kasukuma kete ya ushindi akaondoka zake.

Muda wa saa mbili usiku, Samson alifika kwa Tausi akimkuta yupo na kanga tu huku akionesha hajavaa kitu chochote ndani.

Habari za muda huu mamdogo, alisalimia Samson.

Huko kijijini kwenu ulikotoka mama yako mzazi hana wadogo zake ambao utawaita mama zako wadogo? au mama yako alikwambia na Tausi naye umuite mama yako eeeh. aliongea Tausi huku akitabasamu kimahaba.

Sasa nikuiteje? Samson aliuliza huku ujio wa huku akiwa hajaupenda ni kwasababu alilazimishwa tu.

Wakati Tausi akijiandaa kuja mahali alipo Samson, mlango ulisukumwa , do mwingine alikuwa ni Mzee Mgaya akiwa na mfuko mdogo, Tausi alimrukia na kumkumbatia Mzee Mgaya akijifanya alim miss sana.

Habari za siku my husband mbona ghafla halafu nilienda kumfuata Rahma kule kwa Dada mama Kulwa nikaambiwa umesafiri my mbona hukuniaga ? aliongea kwa kujibebisha Tausi.

Subiri nitakwambia, ndiyo maana nimekuja, halafu mbona mnaacha geti wazi vile halafu, mmekaa tu ndani bila wasiwasi, mmesahau timeshaibiwa Mara ngapi humu ndani ohooooh haya nyie jisahaulisheni tu.
aliongea Mzee Mgaya huku Samson akijikuta ni yeye alisahau kufunga.

Mke wangu kwanza samahani niliondoka ghafla nilienda huko njia za kusini lakini ni vijiji vya katikati tu ndani ya Mkoa wa Pwani. Kunaitwa Ikwiriri, huko nimegundua upatikanaji wa miti ya furniture kiurahisi, ingawaje nimekaa siku chache ila nimefanikiwa kupata data kadhaa ambazo nimezipenda na uzuri hapo ni jirani yaani kwa gari binafsi ni masaa mawili na nusu tu kutoka hapa mjini. alifafanua mzee Mgaya

Sasa my hujaja na gari umeacha wapi,maana ujio wako sikuzote huwa ni honi ya gari nashangaa leo umekuja kimyakimya.
aliongea kwa kuzuga Tausi.

Wala sijaja kimyakimya, ni kwamba lazima ningegonga geti, lakini lilikuwa wazi eti. Nikajikuta naingia kwa tahadhari nikijua labda ni wezi.
Kuhusu gari nimeliacha huko huko, kwasababu limeharibika yaani gari linanisumbua acha tu hata hivyo Kuna fundi nimewasiliana naye ataenda kulivuta ataleta mjini na pia najipanga ninunue lingine maana ipo siku lile gari litanilaza porini.
aliongea Mzee Mgaya huku wote wakicheka kasoro Samson aliyekuwa na hofu.

Halafu mke wangu, huu uvaaji gani mbele ya mwanao, na kila siku nakwambia mbona huelewi wewe.
Halafu huyu Sam naye hapa kafuata nini,? Eti Sam ulisahau Nini hapa. aliuliza

Kuna vitabu vyangu , kule nyumbani sivioni Sasa nikimuuliza mamdogo kama aliviona akadai yeye hajui, nikasema basi nitakuja kuangalia mwenyewe. aliongopa Samson huku Tausi akitoa tano ya hewani jinsi Samson alivyojitetea .

Mzee Mgaya aliwaangalia Tausi na Samson kwa zamu Kisha akainuka na kuingia chumbani bila kusema chochote.huku ikionekana hajaridhishwa na majibu ya Samson

Itaendelea...................
Salute Mkuu
 
SEHEMU YA AROBAINI NA SITA

Mida ya saa kumi jioni, Samson alimuaga mama yake kuwa anaenda kwenye group discussion ambapo hakukuwa mbali na nyumbani kwao.

Sasa Sam mwananguuuu, kwanini Kila siku wewe uwe unaenda kusoma huko na kumbuka umekuwa ukirudi usiku, kwanini hao wenzio na siku moja moja wasije hapa kwako?
aliuliza mama Kulwa.

Sawa mama nimekuelewa sana, ila sisi kwenye group letu tumependekeza kukutania kwa mwl {akitaja jina} pale Kuna wanafunzi wa madarasa ya juu nao huwa wanafanya discussion zao pale, hivyo tumeamua na sisi kukutana pale ili pindi kama Kuna mada inatushinda basi tunaomba msaada kwa wenzetu.alijibu Samson.

Sawa ila kumbuka kuzingatia muda,maana huu mji tunaujua wenyewe, alitahadharisha mama Kulwa.

Wakati Samson anatoka nje ya geti,
Hamadi, alikutana na Tausi au mama yake mdogo akiwa anashuka kwenye Taxi, wakasalimiana,
Enheee vipi mwenzetu na mabegi wapi tena, aliuliza Tausi.

Naenda nyuma tu hapo huwa tunajisomea na marafiki zangu,alijibu Samson akitaka kupiga hatua kwenda atakapo.
Lakini akashikwa mkono na Tausi.

Vipi Baba yako Mzee Mgaya yupo? Maana ana siku kadhaa nyumbani hajaja? Tausi aliuliza.

Hapana baba yupo nje ya Dar, kaenda sehemu ambako amesema anataka kwenda kufanya mahesabu kwani kapata tenda ya kutengeneza milango ya shule. alijibu Kwa kifupi Samson.
Vizuri sana,hebu nambie huyu mpumbavu Rahma bado yupo hapa, maana mtoto mjinga sijapata kuona, yaani siku ya tano kang'ang'ania kukaa hapa anadhani Hawa nao ni ndugu zake? Hebu kwanza niingie ndani. aliongea Tausi huku akisukuma mlango wa geti dogo kwa nguvu Samson kuona vile ikabidi naye aingie ndani maana alijua hali huenda isiwe shwari.

Haya niambie wewe mtoto Malaya usiye na mipaka, usiye kuwa na adabu, umekaa hapa siku zote hata aibu huna mtoto wa kike, haya tufanye anatokea mtu anakuuliza huyu mama upoje nae, utamjibu nini?
Maana si ndugu yako, Wala wewe si mfanyakazi wake, halafu unawezaje kuwaamini watu baki kiasi hicho? Kipindi nakuleta mjini nilikuasa kuhusu, mazoea au kumwamini mtu haraka, lakini wewe msungo usiyefundwa husikii Wala huelewi.
Tausi alizidi kuropoka huku akiwa hajasalimia mtu yoyote mle ndani.

Wakati huo mama Kulwa alikaa kwa kutulia akiwa anamtazama Tausi kwa umakini namna anavyofoka, huku Rahma akiwa kasimamisha zoezi lake la kufua akiwa nusu nusu ,asimame, au akae,
Amjibu Tausi au asimjibu,
Uso wake ulionesha hasira za wazi huku akionesha anataka kulia.

Najua, tena najua kilichokuleta huku, na nikwambie tu kuwa wakijua lengo lako, watakufukuza kama mbwa Malaya wewe, mtoto mdogo unaendekeza ukahaba, najaribu kukuonya unanikimbia,
Tena unakimbilia kwa watu tu ambao si ndugu zako, kwanza ngoja nikuoneshe, Tausi alimrukia Rahma na kutaka kumpiga, bahati nzuri mwanaume mmoja mwenye nguvu aliwatenganisha huku naye akiwa na malalamiko kadhaa, si mwingine ni dereva Taxi aliyemleta Tausi.

Wewe dada mimi unanichukuliaje?
Hebu nipe hela yangu, Mimi niondoke hela tena nimekufanyia msaada tu kutoka kule hadi huku mbali hivi ningejua nisingekuja, alicomplain yule dereva.

Kwani Kuna nini baba, tena nashangaa unaingia ndani kwangu bila hata hodi, aliuliza mama Kulwa.

Samahani sana mama, Mimi ni dereva nimemleta huyu aunt, Sasa nashangaa ananisubirisha hapo nje, halafu alivyopanic nikaona atanichelewesha, Mimi natafuta hesabu mama. aliongea kwa uchungu dereva.

Acha ujinga na wewe uliambiwa hela yako sikupi, kwanza pale kituoni hata sikukuita wewe, ulijipendekeza tu,umri huo bado unagombania abiria na vijana,Mimi dereva wangu huwa ananivumilia, aliongea Tausi huku akimrushia hela yule jamaa,Kisha dereva wa watu akaiokota ile hela na kutokomea

Hebu watu wote njooni ndani kwanza na Samson funga geti na kufuli maana naona watu wanaingia tu humu kama choo cha umma.

Kwanza mdogo wangu Tausi nikusalimie, eeh nianze Mimi maana mtoto wa kike umefika tu na kuanza kutiririka maneno bila kujali hii ni nyumba ya mtu mwenzangu
Aliongea kwa utulivu mama Kulwa.

Kwanza dada nisamehe tu, kwakweli Nina jazba sana, huyu Binti alichofanya mpaka Sasa simuelewi nashindwa nikulaumu wewe au yeye,
Wewe dada umewezaje kukaa na mtoto wa mtu sikuzote,
Na yeye anawezaje kukaa kwa mtu muda wote huo? Tausi alianza kumlaumu mama Kulwa.

Tausi, nakuita kwa jina lako, Kuna vitu vingi unakosea na vinakushinda, kwanza unakosea kuniuliza hivyo,
Umekuja hapa umeanza kupiga kelele kwenye nyumba yangu sijakuuliza. nimekuita kwa upole tuongee ndani tuweke sawa haya mambo, umetukana weweee lakini nimekuacha tu, hii ni nyumba yangu inaheshimika na watu wengi, unadhani watu waliosikia neno Malaya na matusi kibao uliyotukana watatuchukuliaje wakazi wa humu,
Sasa naelewa kwanini Mzee Mgaya kasema Samson arudi hapa, labda ni nidhamu mbovu uliyokuwa nayo.

Unasema Rahma siyo ndugu yangu ni kweli, lakini huwa Kuna sababu zinazofanya watu wajenge undugu, wote hapa watatu nyinyi Mimi kikawaida siwajui.

Wewe ni mke wa mume wangu, hivyo tayari una undugu na Mimi.

Samson ni mtoto wa shemeji yangu hivyo ni mwanangu pia,
Huyu Rahma kakimbilia hapa pindi mmekwaruzana, najua alijua ni wapi anaenda asingekuja hapa kama hatufahamu sisi, huo ukurasa naufunga haya naomba shoga yangu uniambie Nini kinasababisha ugombane na Binti mdogo kama huyu, yaani kwanza inashangaza ujue,
aliweka kituo mama Kulwa.

Dada nisikufiche huyu mtoto, ana tabia mbaya sana na ndugu zake wanamtafuta wanasema nimsafirishe aende nyumbani kwao Tanga, Mimi sitaweza kukaa naye kwasababu tutakuja kufikishana pabaya, alileta sababu za uongo Tausi.

Mnajua wawili nyinyi mna ugomvi mkubwa sana halafu mkiulizwa mna majibu mepesi sana, yasiyoingia akilini, sasa niseme tu wazi kuwa, Mzee Mgaya anarudi leo hii na yeye ndiye atakuja kumleta rahma kwako , maana kwa hali hii nawaona kabisa mlivyo kama paka na panya hivyo sitaruhusu huyu aondoke.

Mama Kulwa samahani Mimi Kwa mamdogo siendi na kama narudi Tanga nitatokea hapa, ananiita Malaya wakati umalaya kaanza yeye, au anafikiri sijui tunachogombania, Mimi kwanza sitaki kwenda Tanga Wala wapi Mimi kama mtataka niwe mfanyakazi wa humu ndani, nitakubali ila si kwenda kwa mamdogo. aliongea Rahma akionesha kukerwa na akimaanisha liwalo na liwe.

Mama Kulwa alizidi kushangaa tu kwani hakujua chochote,
Kwa upande wa Samson alianza kuona hata njaa inapotea ghafla,
Na hofu kubwa ilitanda moyoni mwake, aliona jinsi Rahma na Tausi walivyo na hasira, na kwenye hasira mtu anaweza kuropoka chochote kile bila kujali itakuwaje na majuto huja baadaye.

Eti Sam wewe umeishi na Hawa watu kipindi kirefu, vipi huwa wapo hivi hivi maana siwaelewi?
aliuliza Mama Kulwa.

Sijawahi kuiona hii hali, ndiyo kwanza naona, siku zote tuliishi kama ndugu tukiwa na furaha sana tu Sasa hata sijui ni kwanini inakuwa hivi, watu hawaeleweki. alijibu Samson.

Halafu wewe mpuuzi wewe ndiyo chanzo cha matatizo yote, Sasa nitakukomesha mchawi mkubwa wewe, kila sehemu ukikaa wewe lazima kutokee matatizo na Dada nikwambie tu kuwa huyu mwanga kurudi hapa lazima kutatokea matatizo utakuja kuniambia.
aliongea Tausi huku akibana mkoba wake na kutoka nje kwa hasira.

Samson nenda kafungue mlango maana Mimi hata siwaelewi ngoja arudi mzee Mgaya atajua cha kufanya, yanini Mimi niumize kichwa kwa watoto wasio wangu. aliongea kwa dharau mama Kulwa.

Wakati Samson anafungua mlango ili Tausi atoke, Tausi akavunja ukimya.
Samson naomba haya masuala yasikuumize kichwa ila sharti langu ni Moja naomba uage si bado mapema! Jifanye unaenda kwa marafiki zako, halafu twende kwangu, na usipofanya hivi, nitamwambia Mzee Mgaya ulitaka kunibaka na Nina ushahidi maana Kuna bukta yako ya blue ninayo. aliongea Tausi akiwa hatanii.

Moyo ulimuenda mbio Samson ni kweli nguo yake ilipotea na aliitafuta bila mafanikio ila alipuuza tu kuwa huenda ilipotea, hakuwaza kuwa imechukuliwa na mtu, na kutokana na alivyotishwa ilibidi atii amri ya Tausi.

Sasa mamdogo inabidi utangulie si vizuri kuongozana, alijitetea Samson

Hilo mimi silijui, uje usije utajua mwenyewe. alijibu Kwa kujiamini Tausi hasa baada ya kuusoma uso wa Samson na kukiri kuwa ana uoga fulani akajiona kasukuma kete ya ushindi akaondoka zake.

Muda wa saa mbili usiku, Samson alifika kwa Tausi akimkuta yupo na kanga tu huku akionesha hajavaa kitu chochote ndani.

Habari za muda huu mamdogo, alisalimia Samson.

Huko kijijini kwenu ulikotoka mama yako mzazi hana wadogo zake ambao utawaita mama zako wadogo? au mama yako alikwambia na Tausi naye umuite mama yako eeeh. aliongea Tausi huku akitabasamu kimahaba.

Sasa nikuiteje? Samson aliuliza huku ujio wa huku akiwa hajaupenda ni kwasababu alilazimishwa tu.

Wakati Tausi akijiandaa kuja mahali alipo Samson, mlango ulisukumwa , do mwingine alikuwa ni Mzee Mgaya akiwa na mfuko mdogo, Tausi alimrukia na kumkumbatia Mzee Mgaya akijifanya alim miss sana.

Habari za siku my husband mbona ghafla halafu nilienda kumfuata Rahma kule kwa Dada mama Kulwa nikaambiwa umesafiri my mbona hukuniaga ? aliongea kwa kujibebisha Tausi.

Subiri nitakwambia, ndiyo maana nimekuja, halafu mbona mnaacha geti wazi vile halafu, mmekaa tu ndani bila wasiwasi, mmesahau timeshaibiwa Mara ngapi humu ndani ohooooh haya nyie jisahaulisheni tu.
aliongea Mzee Mgaya huku Samson akijikuta ni yeye alisahau kufunga.

Mke wangu kwanza samahani niliondoka ghafla nilienda huko njia za kusini lakini ni vijiji vya katikati tu ndani ya Mkoa wa Pwani. Kunaitwa Ikwiriri, huko nimegundua upatikanaji wa miti ya furniture kiurahisi, ingawaje nimekaa siku chache ila nimefanikiwa kupata data kadhaa ambazo nimezipenda na uzuri hapo ni jirani yaani kwa gari binafsi ni masaa mawili na nusu tu kutoka hapa mjini. alifafanua mzee Mgaya

Sasa my hujaja na gari umeacha wapi,maana ujio wako sikuzote huwa ni honi ya gari nashangaa leo umekuja kimyakimya.
aliongea kwa kuzuga Tausi.

Wala sijaja kimyakimya, ni kwamba lazima ningegonga geti, lakini lilikuwa wazi eti. Nikajikuta naingia kwa tahadhari nikijua labda ni wezi.
Kuhusu gari nimeliacha huko huko, kwasababu limeharibika yaani gari linanisumbua acha tu hata hivyo Kuna fundi nimewasiliana naye ataenda kulivuta ataleta mjini na pia najipanga ninunue lingine maana ipo siku lile gari litanilaza porini.
aliongea Mzee Mgaya huku wote wakicheka kasoro Samson aliyekuwa na hofu.

Halafu mke wangu, huu uvaaji gani mbele ya mwanao, na kila siku nakwambia mbona huelewi wewe.
Halafu huyu Sam naye hapa kafuata nini,? Eti Sam ulisahau Nini hapa. aliuliza

Kuna vitabu vyangu , kule nyumbani sivioni Sasa nikimuuliza mamdogo kama aliviona akadai yeye hajui, nikasema basi nitakuja kuangalia mwenyewe. aliongopa Samson huku Tausi akitoa tano ya hewani jinsi Samson alivyojitetea .

Mzee Mgaya aliwaangalia Tausi na Samson kwa zamu Kisha akainuka na kuingia chumbani bila kusema chochote.huku ikionekana hajaridhishwa na majibu ya Samson

Itaendelea...................
moneytalk njoo be
 
SEHEMU YA AROBAINI NA SABA

Tausi aliinuka akijifunga kitenge chake vizuri, huku akimkonyeza Samson kuwa asijali chochote kwani huenda mzee Mgaya hajagundua kitu chochote, akaingia zake jikoni kuandaa chakula, Samson akiwa peke yake kwenye kiti aliwaza kuondoka tu kwani kengele za hatari zililia kichwani mwake ila alishindwa amuage nani maana baba yake kaingia ndani na mama yake mdogo yupo chumbani.

Wewe kijana bado hujanijibu swali langu, nimekuuliza hapa umefuata nini? usitake nianze kuamini kuwa huenda niliyoyasikia ni kweli. Mzee Mgaya aliuliza.

Baba , Mimi kama nilivyokueleza nilifuata vitu vyangu , na hata hivyo nimefika muda si mrefu kwani hata Hilo geti ni Mimi nilisahau kufunga
alijitetea Samson.

Heee mume wangu kwani hayo masuala hayaishi tu, umemuuliza kafuata nini kakujibu, yanini tena kurudia rudia maswali?
Mume wangu acha ushari bwana kwanza hapa Samson ni kwake Mimi sioni sababu ya wewe kushituka kumkuta hapa.aliongea Tausi akionesha haogopi chochote toka kwa mzee Mgaya.

Wewe Kaa kimya, tena utulie Kuna vitu vinaendelea kwenye hii nyumba Mimi sivielewi, kwanza naomba kujua wewe na mwanao Rahma ugomvi wenu ni nini? aliuliza mzee Mgaya.

Swali hili lilimshtua Samson lakini pia hata Tausi mwenyewe alibabaika nalo kiasi,

Ugomvi ni ugomvi tu, huwa hauna sababu maalum, yule ni msichana aliyepevuka tayari, Mimi kama mzazi au mlezi wake Nina jukumu la kuhakikisha anaenda na kukua kwenye misingi imara kinyume na hapo ataangukia kwenye mikono mibaya, najua fika unayatambua haya yote, unasahau kuwa miaka ile ulikuwa unawaadhibu sana wanao?
Lengo lilikuwa nini?
Si ili waishi kwenye maadili sahihi?
Rahma ni mwanangu Mimi nina haki ya kumrudisha kwenye mstari sahihi anune afanyaje, lakini lazima nifanye hivyo. aliweka kituo Tausi

(akicheka) mke wangu Mimi siyo mtoto mdogo, siku ile Rahma alivyokuja kwa dada yako mama Kulwa, nilihisi hatari hasa baada ya kuwa haweki wazi kilichosababisha
Mgombane, lakini nashukuru nilikuta upo salama , wakati narudi Kuna mtu aliniomba lift nimsaidie kwani alikuwa anaenda mbali kidogo, tukiwa kwenye gari aliongea mambo mengi sana yanayowahusu wawili nyinyi , Samson na wewe mke wangu, lakini nilimpinga huyo mtu , nikadhani labda kwakuwa nimemsaidia usafiri kaona ngoja aropoke mambo Yale, lakini leo Kuna picha naipata, kama inaniingia akilini hivi.
Mzee Mgaya aliongea kwa hisia huku akiwakazia macho Tausi na Samson kwa zamu.

Mapigo ya moyo yaliongezeka kwa Samson, hofu iliingia akihisi huenda mzee Mgaya kagundua Kila kitu, ila alijikaza ile hali isionekane kwani kwa kufanya hivyo angejulikana haraka.

Sasa mume wangu huyo mtu alikwambia nini, na ni nani? Maana bado sikuelewi tu baba. aliongea Tausi.

Utanielewa tu, ila wewe Sam naomba uondoke sasaivi sawa, tena iwe Mara yako ya mwisho kuja hapa, aliyekwambia wewe una undugu na huyu ni nani? aliuliza Mzee Mgaya.

Kwani wewe Mzee vipi mbona unamuandama huyu mtoto vipi , Mimi unaniudhi bwana, unaongelea vitu hata havieleweki. aliongea Tausi bila kujua anaamsha mashetani ya mzee Mgaya.

Mzee Mgaya aliinuka na kumshika shingoni Tausi, mithili ya mtu anayetaka kunyofoa koromeo, huku akimburuza chumbani kwake,
Hivi unadhani sijasikia mambo yako wewe una tabia mbaya sana, mbona sitaki kuamini, na ndiyo maana yule mmbea sikutaka kumuamini, lakini tayari Kuna kitu nakiona wewe wa kukaa vile kihasara , mapaja nje mbele ya yule mtoto? Una maana gani? aliuliza mzee Mgaya

(Huku akilia)
Wee niue, niue tu hao waliokwambia hivyo hawakuombei mema hata kidogo, wameniandama weeee , wakaharibu biashara yangu kwa kuniibia, Sasa wamehamia kwako lengo uniue wafurahi , Sasa nimegundua Kila kitu, hivi kwa akili yako unadhani Mimi naweza kutembea au kulala na Samson, huyu ni wa lini,huyu si mwanangu kabisa, Samson ni mwanao kama akina Jose tu, Mila na desturi za kwetu hata kama angekuwa mtu mzima kwakuwa ni mwanao, anakuita baba sipaswi hata kuwa na utani naye, sasa kwanini wewe uhisi vitu vibaya kama hivyo,

Kumbe ndiyo maana maswali yakawa hayaishi kumbe unawaza vitu hivyo, mume wangu leo umejua kunidhalilisha, yaani naanzaje kutembea na Samson, kweli?
Halafu kumbe huna ushahidi yaani ni mmbea na mnafiki mmoja kakutia ujinga na wewe unakuja kuniambia, yaani ulivyo na busara hivyo, ninavyokuamini , umeshindwa kuchuja vitu vidogo kama hivi Kisha ukaja kunidhalilisha.

Uuuuiiiiuwiiii, Tena umenikaba , umeniumiza , eti una wasiwasi natembea na Sam, kweli wewe unazeeka vibaya, huo uzee unakujia vibaya mno, mmmmh weeeeeeee
Haya bwana nashukuru mume wangu, uliniletea mwanao kisa wanagombana na dada kule, ukaniambia hawaelewani, Mimi nikakaa naye kwa hizo siku kadhaa nilimchukulia kama mwanangu, alipokosea nilimuonya, alipofanya vizuri nilimpongeza kama mwanangu zawadi na nilivyoona anastahili nilimpa ili kutengeneza uhusiano mzuri kama mama na mtoto, huku mstari wa heshima Kati yetu Ukiwa vilevile.

Sasa nikushangae wewe mume wangu, kunihisi vibaya , sikatai una haki ya kunihisi na mwanaume yeyote kwa mujibu wa akili zako, Mimi si mkeo? lakini kitendo cha kunihisi eti nimelala na Samson umenikosea pakubwa mno, na kesho Mimi nahitaji kwenda kwa huyo mtu aliyekwambia habari hizi ili nimjue tu, sihitaji kuongea naye chochote, ila nimuone tu sura yake,
Tausi aliongea huku alifungua mlango wa chumbani na kuja sebuleni na kumkuta Samson kajikunyata akiwa kabana ukutani, akionekana alikuwa anasikiliza maongezi yao .

Mke wangu, my wife eeh njoo chumbani huku Sasa huko unaenda kufanya nini lengo lako Samson asikie maongezi yetu eeh, alishauri mzee Mgaya .

Asikie Mara ngapi, kila kitu kasikia , Alijibu Tausi , huku Mzee Mgaya akiwa na kazi ya kumbembeleza Tausi, akihisi Yale aliyoyasikia kwa wambea wake si ya kweli, akilinganisha na alivyojitetea Tausi.

Samson saizi ni saa tano, na foleni zimepungua , nakuomba uende nyumbani, kesho ni shule hivyo ni vema ukalale karibu na shule.
aliamrisha Mzee Mgaya

Sasa kumfukuza mtoto usiku huu una maana gani mume wangu? alihoji Tausi.

Acha aende tu, kwani si anapanda gari hapo tu, atafika tu, wewe Samson wahi bwana!
alisema Mzee Mgaya.

Baada ya muda fulani Samson alifika nyumbani, akiwakuta mama Kulwa, Cathy ambaye ni rafiki wa mama Kulwa pamoja na Rahma wakiwa wanaongea nje ya geti.

Wewe Sam, ulikuwa wapi maana tumekutafuta hadi tumechoka, Mama kaja kuniamsha hapa eti umepotea tumeenda hadi kule kwenye group lenu pale kwa mwalimu, tumeambiwa hukwenda kabisa, vipi ulikuwa wapi?
aliuliza Cathy.

Nilienda kwa mamdogo Tausi Temeke kufuata vitu vyangu,maana nahisi nilisahau kule, alijitetea.

Ulimuaga nani kama unaenda huko, na kwanini unapenda kutupa Presha wewe mtoto? Hata watoto wangu hawakuwa hivi, kwanini wewe unapenda kunisumbua hivi? alilalamika mama Kulwa.

Samson alikaa kimya huku akipewa vidonge vyake na Cathy,
Wakati huo Rahma alianza kucheka Kisha akauliza,
Sasa Samuuuu unasema Kuna vitu ulifuata kwa mamdogo , je viko wapi mbona uko mikono mitupu?

Samson hakuwa na jibu

Tulia shoga yangu,huu ni usiku twendeni tukapumzike, kesho atakuwa na majibu , namsubiri Baba Jose tuje tumuulize kwa pamoja, siwezi kuishi na mtoto mswahili mimi, aliongea mama Kulwa Kisha watu wote wanatawanyika.

Usiku Samson hakulala, akiwaza namna Tausi alivyo muongo na alivyomshawishi Mzee Mgaya Hadi akalainika, Lakini suala la mama Kulwa kusema anakuja kumuuliza maswali mbele ya Mzee Mgaya, yalimkata maini Samson akakosa Raha kwani anamjua mama Kulwa alivyo huwa hashindwi na huwezi kumdanganya kirahisi.

Itaendelea..,............
 
SEHEMU YA AROBAINI NA SABA

Tausi aliinuka akijifunga kitenge chake vizuri, huku akimkonyeza Samson kuwa asijali chochote kwani huenda mzee Mgaya hajagundua kitu chochote, akaingia zake jikoni kuandaa chakula, Samson akiwa peke yake kwenye kiti aliwaza kuondoka tu kwani kengele za hatari zililia kichwani mwake ila alishindwa amuage nani maana baba yake kaingia ndani na mama yake mdogo yupo chumbani.

Wewe kijana bado hujanijibu swali langu, nimekuuliza hapa umefuata nini? usitake nianze kuamini kuwa huenda niliyoyasikia ni kweli. Mzee Mgaya aliuliza.

Baba , Mimi kama nilivyokueleza nilifuata vitu vyangu , na hata hivyo nimefika muda si mrefu kwani hata Hilo geti ni Mimi nilisahau kufunga
alijitetea Samson.

Heee mume wangu kwani hayo masuala hayaishi tu, umemuuliza kafuata nini kakujibu, yanini tena kurudia rudia maswali?
Mume wangu acha ushari bwana kwanza hapa Samson ni kwake Mimi sioni sababu ya wewe kushituka kumkuta hapa.aliongea Tausi akionesha haogopi chochote toka kwa mzee Mgaya.

Wewe Kaa kimya, tena utulie Kuna vitu vinaendelea kwenye hii nyumba Mimi sivielewi, kwanza naomba kujua wewe na mwanao Rahma ugomvi wenu ni nini? aliuliza mzee Mgaya.

Swali hili lilimshtua Samson lakini pia hata Tausi mwenyewe alibabaika nalo kiasi,

Ugomvi ni ugomvi tu, huwa hauna sababu maalum, yule ni msichana aliyepevuka tayari, Mimi kama mzazi au mlezi wake Nina jukumu la kuhakikisha anaenda na kukua kwenye misingi imara kinyume na hapo ataangukia kwenye mikono mibaya, najua fika unayatambua haya yote, unasahau kuwa miaka ile ulikuwa unawaadhibu sana wanao?
Lengo lilikuwa nini?
Si ili waishi kwenye maadili sahihi?
Rahma ni mwanangu Mimi nina haki ya kumrudisha kwenye mstari sahihi anune afanyaje, lakini lazima nifanye hivyo. aliweka kituo Tausi

(akicheka) mke wangu Mimi siyo mtoto mdogo, siku ile Rahma alivyokuja kwa dada yako mama Kulwa, nilihisi hatari hasa baada ya kuwa haweki wazi kilichosababisha
Mgombane, lakini nashukuru nilikuta upo salama , wakati narudi Kuna mtu aliniomba lift nimsaidie kwani alikuwa anaenda mbali kidogo, tukiwa kwenye gari aliongea mambo mengi sana yanayowahusu wawili nyinyi , Samson na wewe mke wangu, lakini nilimpinga huyo mtu , nikadhani labda kwakuwa nimemsaidia usafiri kaona ngoja aropoke mambo Yale, lakini leo Kuna picha naipata, kama inaniingia akilini hivi.
Mzee Mgaya aliongea kwa hisia huku akiwakazia macho Tausi na Samson kwa zamu.

Mapigo ya moyo yaliongezeka kwa Samson, hofu iliingia akihisi huenda mzee Mgaya kagundua Kila kitu, ila alijikaza ile hali isionekane kwani kwa kufanya hivyo angejulikana haraka.

Sasa mume wangu huyo mtu alikwambia nini, na ni nani? Maana bado sikuelewi tu baba. aliongea Tausi.

Utanielewa tu, ila wewe Sam naomba uondoke sasaivi sawa, tena iwe Mara yako ya mwisho kuja hapa, aliyekwambia wewe una undugu na huyu ni nani? aliuliza Mzee Mgaya.

Kwani wewe Mzee vipi mbona unamuandama huyu mtoto vipi , Mimi unaniudhi bwana, unaongelea vitu hata havieleweki. aliongea Tausi bila kujua anaamsha mashetani ya mzee Mgaya.

Mzee Mgaya aliinuka na kumshika shingoni Tausi, mithili ya mtu anayetaka kunyofoa koromeo, huku akimburuza chumbani kwake,
Hivi unadhani sijasikia mambo yako wewe una tabia mbaya sana, mbona sitaki kuamini, na ndiyo maana yule mmbea sikutaka kumuamini, lakini tayari Kuna kitu nakiona wewe wa kukaa vile kihasara , mapaja nje mbele ya yule mtoto? Una maana gani? aliuliza mzee Mgaya

(Huku akilia)
Wee niue, niue tu hao waliokwambia hivyo hawakuombei mema hata kidogo, wameniandama weeee , wakaharibu biashara yangu kwa kuniibia, Sasa wamehamia kwako lengo uniue wafurahi , Sasa nimegundua Kila kitu, hivi kwa akili yako unadhani Mimi naweza kutembea au kulala na Samson, huyu ni wa lini,huyu si mwanangu kabisa, Samson ni mwanao kama akina Jose tu, Mila na desturi za kwetu hata kama angekuwa mtu mzima kwakuwa ni mwanao, anakuita baba sipaswi hata kuwa na utani naye, sasa kwanini wewe uhisi vitu vibaya kama hivyo,

Kumbe ndiyo maana maswali yakawa hayaishi kumbe unawaza vitu hivyo, mume wangu leo umejua kunidhalilisha, yaani naanzaje kutembea na Samson, kweli?
Halafu kumbe huna ushahidi yaani ni mmbea na mnafiki mmoja kakutia ujinga na wewe unakuja kuniambia, yaani ulivyo na busara hivyo, ninavyokuamini , umeshindwa kuchuja vitu vidogo kama hivi Kisha ukaja kunidhalilisha.

Uuuuiiiiuwiiii, Tena umenikaba , umeniumiza , eti una wasiwasi natembea na Sam, kweli wewe unazeeka vibaya, huo uzee unakujia vibaya mno, mmmmh weeeeeeee
Haya bwana nashukuru mume wangu, uliniletea mwanao kisa wanagombana na dada kule, ukaniambia hawaelewani, Mimi nikakaa naye kwa hizo siku kadhaa nilimchukulia kama mwanangu, alipokosea nilimuonya, alipofanya vizuri nilimpongeza kama mwanangu zawadi na nilivyoona anastahili nilimpa ili kutengeneza uhusiano mzuri kama mama na mtoto, huku mstari wa heshima Kati yetu Ukiwa vilevile.

Sasa nikushangae wewe mume wangu, kunihisi vibaya , sikatai una haki ya kunihisi na mwanaume yeyote kwa mujibu wa akili zako, Mimi si mkeo? lakini kitendo cha kunihisi eti nimelala na Samson umenikosea pakubwa mno, na kesho Mimi nahitaji kwenda kwa huyo mtu aliyekwambia habari hizi ili nimjue tu, sihitaji kuongea naye chochote, ila nimuone tu sura yake,
Tausi aliongea huku alifungua mlango wa chumbani na kuja sebuleni na kumkuta Samson kajikunyata akiwa kabana ukutani, akionekana alikuwa anasikiliza maongezi yao .

Mke wangu, my wife eeh njoo chumbani huku Sasa huko unaenda kufanya nini lengo lako Samson asikie maongezi yetu eeh, alishauri mzee Mgaya .

Asikie Mara ngapi, kila kitu kasikia , Alijibu Tausi , huku Mzee Mgaya akiwa na kazi ya kumbembeleza Tausi, akihisi Yale aliyoyasikia kwa wambea wake si ya kweli, akilinganisha na alivyojitetea Tausi.

Samson saizi ni saa tano, na foleni zimepungua , nakuomba uende nyumbani, kesho ni shule hivyo ni vema ukalale karibu na shule.
aliamrisha Mzee Mgaya

Sasa kumfukuza mtoto usiku huu una maana gani mume wangu? alihoji Tausi.

Acha aende tu, kwani si anapanda gari hapo tu, atafika tu, wewe Samson wahi bwana!
alisema Mzee Mgaya.

Baada ya muda fulani Samson alifika nyumbani, akiwakuta mama Kulwa, Cathy ambaye ni rafiki wa mama Kulwa pamoja na Rahma wakiwa wanaongea nje ya geti.

Wewe Sam, ulikuwa wapi maana tumekutafuta hadi tumechoka, Mama kaja kuniamsha hapa eti umepotea tumeenda hadi kule kwenye group lenu pale kwa mwalimu, tumeambiwa hukwenda kabisa, vipi ulikuwa wapi?
aliuliza Cathy.

Nilienda kwa mamdogo Tausi Temeke kufuata vitu vyangu,maana nahisi nilisahau kule, alijitetea.

Ulimuaga nani kama unaenda huko, na kwanini unapenda kutupa Presha wewe mtoto? Hata watoto wangu hawakuwa hivi, kwanini wewe unapenda kunisumbua hivi? alilalamika mama Kulwa.

Samson alikaa kimya huku akipewa vidonge vyake na Cathy,
Wakati huo Rahma alianza kucheka Kisha akauliza,
Sasa Samuuuu unasema Kuna vitu ulifuata kwa mamdogo , je viko wapi mbona uko mikono mitupu?

Samson hakuwa na jibu

Tulia shoga yangu,huu ni usiku twendeni tukapumzike, kesho atakuwa na majibu , namsubiri Baba Jose tuje tumuulize kwa pamoja, siwezi kuishi na mtoto mswahili mimi, aliongea mama Kulwa Kisha watu wote wanatawanyika.

Usiku Samson hakulala, akiwaza namna Tausi alivyo muongo na alivyomshawishi Mzee Mgaya Hadi akalainika, Lakini suala la mama Kulwa kusema anakuja kumuuliza maswali mbele ya Mzee Mgaya, yalimkata maini Samson akakosa Raha kwani anamjua mama Kulwa alivyo huwa hashindwi na huwezi kumdanganya kirahisi.

Itaendelea..,............
Shukrani Boss
 
Mkuu ninaifuatilia kwa karibu hii story. Kudos Ila jitahidi ifike mpk mwisho mkuu.
 
SEHEMU YA AROBAINI NA NANE

Kelele na stori za hapa na pale zilitawala kwenye darasa la akina Samson, wapo waliokuwa bize kujisomea mtu mmoja mmoja, wapo waliodiscuss kivikundi akiwemo Samson na kundi lao la wanafunzi sita akiwemo msichana mmoja, hili ni group ambalo lilichukiwa na wanafunzi wenzao wakiliona ni kundi limekaa kibaguzi sana.

Kwanza lilikuwa group la wanafunzi smart kichwani ambao, walikuwa na ile janja janja ya kujichanganya na wanafunzi wa madarasa ya juu, hivyo kuongeza madini mengi.

Pili ni group la fighters nje ya masomo, hakuna mwanafunzi yeyote wa alithubutu kuwasogelea, kwani ilikuwa ni kawaida kukuta mwanafunzi wa form one anamvimbia kifua mtu mzima, kitu ambacho kwenye shule nyingi si kawaida.

Samson hakuwa na nguvu sana za kupigana, ila alibebwa na lile kundi kwa uthubutu wake, alikuwa na mikwara kiasi kwamba huwezi kumsogelea, lakini pia alisifika kwa mademu, ilikuwa ni kawaida Samson kumkuta yupo na demu aliyemzidi umri, huku wanafunzi wenzake wakijiuliza anawapataje?
Huyo ndiye Samson.

Pili kulikuwa na Abdallah au Dullah huyu alisifika kwa vitu vya magendo, madaftari na kalamu za wizi vyote alikuwa navyo,ilikuwa ni kawaida kumkuta ana vitabu vyenye mihuri ya shule nyingine,alivipataje?haikujulikana.
japo kichwani hakuwa vizuri sana .

Mwingine alikuwa ni msichana ambaye alikuwa na akili sana, na alitegemewa sana na lile kundi, huku akisifika kwa kuwaunganishia mademu, madomozege wote na yeye akiwa hana boyfriend, yeye na kitabu, kitabu na yeye.
Hili ni kundi la wanafunzi sita, ambalo hufanya discussion zao kwa mwalimu wa nidhamu wa shule yao.

Hebu keleleni nyie, hivi ni kwanini nyinyi kila siku darasa lenu mnaongoza kwa makelele? Mtashikiwa fimbo mpaka lini, eeh,
Hebu na nyie mliokaa kivikundi Kila mmoja arudi kwenye kiti chake.
Ni mwalimu wa nidhamu wa shule ile, almaarufu mwalimu Eagle.
aliitwa hivyo kutoka na uwezo wa kuona kitu na kusikia, alikuwa na tabia ya kunyata na kusimama dirishani Kisha akawamark wanafunzi kadhaa Nini wanafanya.

Jamani, Mimi Sina kipindi kwa leo naomba tu niwaachie test ya maswali kadhaa, si mnajua tunakaribia kufanya mitihani ya muhula wa pili? aliuliza

Wanafunzi wakamjibu.

Eeeeeh ninyi ni form two watarajiwa, hivyo lazima Kila mmoja ahakikishe anazingatia kilichomleta shuleni,
Jana Kuna wazazi ambao ni majirani zangu, walikuwa wanamtafuta mtu mmoja sitomtaja jina, mida ya saa tano usiku nikagongewa mlango, eti watu wanatafuta mtoto wao ambaye sitamtaja jina lake.

Eti class ni sahihi mwanafunzi yeyote kuwa nje ya nyumbani kwao muda huo?
Alikuwa wapi?
Alikuwa anafanya Nini?
Tuna maswali mengi ya kujiuliza, lakini naomba huyo mtu anayejijua, ajirekebishe, ajitahidi kufuata kile kilichomleta hapa shuleni,
Hapa nyinyi wote mnatengeneza misingi ya maisha yenu, au hamuoni kama maisha ni magumu.
Shauri zenu nawaambieni.
aliongea mwalimu yule Kisha akatoka akiwaacha wanafunzi wakiangaliana ni nani huyo, Kila mmoja akiwa na shauku ya kujua, lakini ilikuwa ngumu, ni kundi la Samson tu, ndiyo lilijua ni nani anaongelewa, pia hawakuwa tayari mwanafunzi yeyote ajue.
Wakapiga kimya, huku Samson akijichangamsha ili asijulikane.

***************************************
Samson alirudi nyumbani akamkuta Mzee Mgaya nje, akiwa kavaa vizuri sana huku akiwa na funguo za gari la mkewe akionekana ana safari fulani

Enhee vipi msomi naona unarudi, vipi masomo yanaendaje maana kazi yako kuzurula tu. aliongea kiutani Mzee Mgaya.

Hapana baba, Mimi nasoma ila kwa leo kutakuwa na mechi Kati ya wanafunzi na walimu, hivyo na Mimi ni mmoja wa wachezaji wa Leo.
aliongea Samson huku akimsoma Mzee Mgaya na kugundua yupo vizuri tu maana alihisi yale mambo ya Jana yake asije kuwa kayapatia ufumbuzi.

Ehee waooooh, kumbe unacheza mpira, unacheza namba ngapi wewe, au unanidanganya maana sikuwahi kusikia hata ukiongelea stori za mpira. aliongeza mzee Mgaya huku akionesha kafurahi kusikia na Sam ni mchezaji.

Mimi nacheza namba saba, japo tukikosa Full back namba mbili huwa nacheza pia hiyo namba. alijibu Samson.

Basi sawa ni vizuri, ila nakukumbusha kuchukua tahadhari, unaweza kuvunjika huko, mwisho wa siku ukashindwa kutimiza ndoto zako, sisemi ni jambo baya unafanya hapana ila be careful.
alitahadharisha Mzee Mgaya.

Samson Mimi na baba yako tunatoka tunaenda kumuona mgonjwa huko nje ya mji tunaweza kurudi usiku sana hivyo ongezeni umakini sawa? alisema mama Kulwa akiwa kapendeza sana na suti yake ya kijivu , huku viatu vyenye visigino virefu vikimkaa vyema.

Wewe Binti naomba niletee mkoba wangu, halafu na wewe shoga yangu basi ujitahidi kupunguza uzito wewe joto lote hili umejifunga kichwani hadi miguuni khaaah. alitania mama Kulwa huku Rahma akitabasamu.

Ni utaratibu na namna anavyoifahamu Dini kwa uelewa wake, hata umshawishi Rahma vipi hangekukubalia akae kichwa wazi au avae nguo za kuonesha maungo yake licha ya kuwa dhambi ya uzinifu haikumuacha salama lakini sehemu zingine alikuwa poa.

Sasa Sam na Mimi naruhusiwa kuja huko shuleni kwako nije kukuona unavyocheza? aliuliza kiutani Rahma.

Ni sawa tu ila vitu vya hapa ushaandaa, maana mama unamjua alivyo na mdomo. alihoji Samson.

Mimi tena, haya niachie mimi wewe kama unaniruhu nije sawa.
Kwakuwa kutoka hapo kwao na ulipo uwanja wa shule hakukuwa mbali walitumia dakika kadhaa tu kufika huku kukiwa na wanafunzi wengi waliokuwa wanasubiri kwa hamu mtanange ule, lakini pia raia kadhaa walikuwepo wakija kuwaangalia wachezaji watano ambao walichukuliwa mtaani kwaajili ya kujazia timu ya walimu ambayo ilikuwa na wachezaji pungufu.

Kila mwanaume rijali alianza kumshangaa Rahma, Binti mwenye sura nzuri yenye mvuto huku akiwa kamganda Samson kiasi cha Sam kuwa na kaaibi fulani,miluzi toka kwa wanafunzi watukutu pamoja na watu wa mtaani iliongezeka wapo walioonesha kutania tu, na wapo ambao walikuwa serious.

Sasa Rahma Kaa na wasichana waleeeee naona kule Kuna utulivu, Sam akimuelekeza mgeni wake.

Mwalimu mmoja ambaye alikuwa ni kijana akisifika kwa usafi na utanashati wa hali ya juu huku Miwani ikiwa haimtoki machoni, alimfuata Samson na kumuuliza.

Wewe Samson yule ni mwanafunzi wa shule gani maana hapa sijawahi kumuona, maana naona kama ni Islamic school huyu. aliuliza yule mwalimu.

Hapana, yule hasomi anakaa nyumbani. Alijibu Kwa kifupi Sam.

Jibu lile la kuonesha hasomi lilimpagawisha yule mwalimu kiasi cha Samson kuhisi kitu.

Vipi Sasa kule anaenda wapi , naomba umuite aje akae kwenye viti hapa , anakaaje kule. alihoji yule mwalimu aliyeonesha tamaa za ngono za wazi.

Kule nimemwelekeza Mimi Wala hakuna shida, atakaa tu kulekule
Samson alijibu kivivu kwani alishatambua lengo la yule mwalimu.

Wewe acha dharau mjinga nini, Mimi si nimekwambia ukamuite au, unabishana na mimi eehh. Yule mwalimu alitumia ubabe wa cheo chake.Na Sam kabla hajafanya chochote filimbi ya refaree ilianza kuwaita wachezaji wa pande zote huku Kila mchezaji akiingia kwa stahili yake, kubwa zaidi uwanja ulilipuka vicheko baada ya mwalimu fulani mnene na mtu mzima naye kuwa kwenye first eleven huku wataalam wakishindwa kujua anaenda kucheza namba gani.

Wachezaji walijipanga mstari mmoja huku refa akiwapa mawaidha fulani, wakati huo Samson macho yalikuwa nje, alishangaa kuona yule mwalimu akimshika mkono Rahma akimleta huku walikokaa makamisaa,
Karoho fulani ka wivu kenye ubaridi kalimpitia Samson, alishuhudia yule mwalimu akimshikashika Rahma ambaye alionekana hapendezwi na anayofanyiwa, Samson hasira na wivu vilichanganyika vikaanza kumtafuna.

Ndani ya dakika kumi na tano za kipindi cha kwanza Samson alitolewa huku baadhi wakishindwa kujua kwanini hakuonesha makeke yake? Halafu mbona wapinzani ni wepesi tu watu walitegemea Samson angeonesha uwezo wa hali ya juu, Nini kimefanya awe vile hakuna aliyejua, Samson alitoka huku macho yakiwa kwa yule ticha aliyekuwa anajichekesha na Rahma,
Masikini Samson aliumia sana Tena mno. Yule Rahma baada ya kumuona Samson akataka kuinuka aje kwa Samson lakini yule mwalimu akawa anamzuia.samson alijuta kumleta Rahma pale uwanjani.

Milango ya mafanikio
Simulizi inayogusa maisha ya Samson kwenye safari yake ya kusaka Elimu, nini kitatokea endelea kuifuatilia simulizi hadi mwisho.

Itaendelea.........................
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom