Simulizi: Milango ya mafanikio

Simulizi: Milango ya mafanikio

Kiukweli kupitia hii stori imenikumbusha magumu niliyowahi kupitia maishani hasa kwa ndugu pale nilipokiishi majumbani kwao,hakika walininyanyasa sana ila nashukuru nilikomaa mpaka nikavuka salama ila leo nimekuwa juu kuliko wao na watoto wao,kuna muda huwa nakaa nasema hivi kweli nikifa hawa wanangu nani atawapenda na kuwajali ?
Tupo wengi tuliopitia kwa ndugu . Namie Ni Kama samsoni.
Hao walikuwa wanakula maganzi ama maukali ya maisha. Yaani shukuru mwanao akinyanyaswa. Sikubaliani kulea mtt kiraharaha ama kimayai Bali naamini kumlea kijeshi
 
Ni kweli kabisa kwenye kusaka mafanikio Kuna hitaji uvumilivu na Imani ya kiwango kikubwa
Mkuu watu tunapitia magumu sana lakini ndio hivyo Imani, uvumilivu na utulivu unahitajika sana. Mimi mwenyewe nina historia ngumu sana ndani ya miaka hii 10 iliyopita. Imani +Utulivu +Uvumilivu ni vitu vya muhimu sana.
 
Mkuu watu tunapitia magumu sana lakini ndio hivyo Imani, uvumilivu na utulivu unahitajika sana. Mimi mwenyewe nina historia ngumu sana ndani ya miaka hii 10 iliyopita. Imani +Utulivu +Uvumilivu ni vitu vya muhimu sana.
Cha muhimu ni kumuomba MUNGU +kuongeza juhudi na kutokata tamaa mapema.
 
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA

Mzee Mgaya alikaa kwa kutulia kwenye kiti huku akijaribu kujizuia hasira zake.
Vipi tena wewe upo huku unajua unaweza kuwapa watu wasiwasi, Mimi hata sikujua kama upo huku , ulichofanya siyo kizuri kwani unaweza kutuweka roho juu tukawaza vingine. aliongea Mzee Mgaya kwa sauti ya kivivu kisha akainuka na kuelekea usawa wa chumbani, ambapo na mkewe mama Kulwa alimfuata muda huohuo

Enhee niambie dogo kitabu kinase make, aliuliza Jose kwa sauti ya kirafiki huku akichukua begi la Samson na kuanza kupitia madaftari yake.

Nashukuru MUNGU mambo si mabaya sana, japo changamoto hazikosekani kaka. alijibu Samson

Mama Kulwa alitoka akamuita Samson watoke wakaongelee nje, huku wakimuacha Jose akipekuapekua Papers za Samson.

Samson niambie mwanangu maana nimegundua ujio wako hapa si wa kawaida, lakini pia baba yako naona kama hampo sawa naye Kuna nini hebu tafadhali niambie Kila kitu usinifiche, aliongea kwa shauku ya kimbea mama Kulwa.

Samson akaanza kueleza kuanzia baba yake na Tausi walivyosafiri kuelekea Tanga, lakini pia walivyorudi huku wakiwa wamebadilika na kumchukia ghafla bila sababu,
Lakini pia maneno aliyoongea Tausi asubuhi ya siku hiyo akimtuhumu Samson kuwa mchawi , yalimpa majibu ya wapi walikokuwa wameenda. aliweka kituo Samson.

Kwahiyo, hata huyu baba Kulwa anakosa busara za moja kwa moja na kusikiliza upuuzi wa Tausi, yaani heshima aliyojijengea halafu jamii isikie haya aliyokufanyia kifaranga kama wewe nani atamuelewa? au Mr anachanganyikiwa? hebu mwanangu turudi ndani nikaongee naye, aliongea mama Kulwa huku wakiingia ndani na kumkuta Mzee Mgaya akiwa karibu na mwanaye Jose wakiangalia baadhi ya matokeo ya Samson ambapo muda wote Jose alitikisa kichwa akionesha anakubali uwezo wa Samson.

Aiseeeh yaani kichwa hiki kama kingekuwa high school ingependeza sana, nahitaji kuona anavyofika mbali huyu dogo, aliongea Jose kwa furaha sana.

Baba Kulwa, na wote tuliopo hapa ndani hebu naombeni tusikilizane,
Naomba kujua baba Jose una tatizo gani na huyu mtoto. aliuliza mama Kulwa

Tatizo, tatizo gani? Mimi Sina matatizo na nwanangu kwani kakuambia nini, maana hata ulivyoingia hapa Mimi nimeshtuka Kuna jambo nimeliona halipo sawa, Sasa ni vyema wote tutajua ili kama mtoto kakukwaza aonywe, huyu siyo wa kumnunia, kwanza unachekesha sana mtoto huyu si kama mjukuu tu kwako? Jambo gani limekuudhi kiasi cha kumkalia kimya? aliuliza Mama Kulwa.

(Huku akicheka)Yaani wewe leo hii wakumuonea huruma Samson, huruma hiyo imeanza lini, au unataka uonekane mwema sana, Samson nimemtoa mkoani huku shule tukimtaka asome iliyokaribu na hapa , na kuishi aishi hapa ambapo ndiyo nyumba yangu kubwa watu wote wanajua wewe ndiye malkia wa mzee Mgaya na wageni wangu wote huwa wanafikia hapa, je nani amesababisha Samson ahame hapa siyo wewe? Ni Mara ngapi ulionesha humpendi lakini nikawa nazuia nikijua leo kesho mtakaa sawa lakini mambo yalizidi kuharibika nikaamua kumuhamisha Samson.
aliongea kwa hasira na dharau Mzee Mgaya.

Nimehangaika naye huyu toka kijijini hadi kufika naye hapa, matokeo yake yalichakachuliwa huku wajanja wakitaka kupora haki yake lakini nilipambana mpaka kufikia kufanikisha suala hili iweje leo nimchukie Samson, hajafikia hata Moja ya nane ya malengo yangu namuachaje? tatizo ni wewe ulishindwa kuishi na huyu mtoto nani asiyejua? Hivyo usianze kujiona mwema sana mbele ya mwanao Jose, wewe ni mke wangu nakujua vizuri sana tu. aliongea Mzee Mgaya

Weeeeeeee tena ishia hapohapo Mimi ni mama najua mtoto analelewa vipi, malezi ambayo ulitaka kumpa huyu mtoto siyo kabisa, unadhani huko kwao alikotoka alikuwa hafanyi kazi, Sasa ilifikia hatua unamkataza asinisaidie kazi ulikuwa na maana gani? kwakuwa na Mimi Nina misimamo yangu, nikaona mpeleke sehemu ambayo hatofanya kazi, huyu mtoto Mimi simchukii Wala si kama simpendi na akiamua kurudi hapa tutampokea kwa mikono miwili lakini lazima afanye kazi,
Eti wewe kwa Tausi huwa kazi yako ni kula tu na kutulia? aliulizwa Samson.

Akaitikia kwa kutikisa kichwa kuwa huwa anafanya kazi.

Mama Kulwa akaendelea............

Sasa wenzangu mmekuja na jambo kubwa zaidi mkimuita huyu mtoto mchawi, kweli jamani mbona mna dhambi hivyo?
Yaani Tausi aseme nini asikilizwe, atakuja kukufanya ukose heshima na Imani kwenye jamii kwa kuendelea kusikiliza Kila upuuzi wake.
Mama Kulwa aliongea bila uoga wowote akionesha kujiamini sana.

Mzee Mgaya alifura kwa hasira sana huku akitamani aseme neno lakini uwepo wa mwanaye Jose ulifanya adhibiti hali yake.

Kwa upande wa Jose yeye alikuwa kimya sana hakujibu neno lolote huku akiwaomba wazazi wake wakapumzike kisha na yeye akiingia kwenye chumba chake, hali kadhalika Samson akaingia kwenye chumba chake huku moyo Ukiwa unamuuma sana kwani kitendo Cha watu kuwa wanapishana kwa sababu yake, alijikuta anakata tamaa, sasa sehemu ambayo aliitegemea kuwa anaweza kuishi vyema kwa Tausi, nako kuligeuka kwa moto mbaya zaidi hata Mzee Mgaya naye alikuwa yupo upande wa Tausi hivyo ilimuwia vigumu mno.

Asubuhi aliamka akamkuta mama Kulwa nje wakasalimiana.

Mwanangu pole sana, hata hivyo usijali yule Malaya Tausi alileta fitina hadi kufikia wewe kuhama hapa lakini , unajisikiaje kuambiwa wewe ni mchawi?
Ina maana umetukanwa wewe na familia yako , yaani wazazi wako wote wanaonekana wachawi, sasa unawezaje kuishi hiyo sehemu,
Mwanangu ipo siku utapewa sumu kwani tayari mpo kwenye mashindano na familia ya Tausi,
Na asili ya mashindano lazima apatikane mshindi.
Sasa baba yangu Samson unadhani unaweza kushinda? aliongea mama Kulwa huku akimtisha sana Samson.

Samson alifungua geti kwa nguvu huku maneno yale yakimtisha sana , alifika shule huku ile hali ya yeye kuishi kama digidigi ikimuumiza sana mbaya zaidi alishindwa kujua hatma ya Nini kitatokea, akahisi kuwa hana muda anaweza kuacha shule , hakuwaza kuhusu kuhama shule,
Nani atamuhamisha?
Mtu ambaye alimfanyia mipango yote kuanzia kijijini kwao Hadi mjini lakini Sasa aliona kabisa hakuna tumaini la kuendelea kusoma.

Itaendelea.......................
 
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA

Mzee Mgaya alikaa kwa kutulia kwenye kiti huku akijaribu kujizuia hasira zake.
Vipi tena wewe upo huku unajua unaweza kuwapa watu wasiwasi, Mimi hata sikujua kama upo huku , ulichofanya siyo kizuri kwani unaweza kutuweka roho juu tukawaza vingine. aliongea Mzee Mgaya kwa sauti ya kivivu kisha akainuka na kuelekea usawa wa chumbani, ambapo na mkewe mama Kulwa alimfuata muda huohuo

Enhee niambie dogo kitabu kinase make, aliuliza Jose kwa sauti ya kirafiki huku akichukua begi la Samson na kuanza kupitia madaftari yake.

Nashukuru MUNGU mambo si mabaya sana, japo changamoto hazikosekani kaka. alijibu Samson

Mama Kulwa alitoka akamuita Samson watoke wakaongelee nje, huku wakimuacha Jose akipekuapekua Papers za Samson.

Samson niambie mwanangu maana nimegundua ujio wako hapa si wa kawaida, lakini pia baba yako naona kama hampo sawa naye Kuna nini hebu tafadhali niambie Kila kitu usinifiche, aliongea kwa shauku ya kimbea mama Kulwa.

Samson akaanza kueleza kuanzia baba yake na Tausi walivyosafiri kuelekea Tanga, lakini pia walivyorudi huku wakiwa wamebadilika na kumchukia ghafla bila sababu,
Lakini pia maneno aliyoongea Tausi asubuhi ya siku hiyo akimtuhumu Samson kuwa mchawi , yalimpa majibu ya wapi walikokuwa wameenda. aliweka kituo Samson.

Kwahiyo, hata huyu baba Kulwa anakosa busara za moja kwa moja na kusikiliza upuuzi wa Tausi, yaani heshima aliyojijengea halafu jamii isikie haya aliyokufanyia kifaranga kama wewe nani atamuelewa? au Mr anachanganyikiwa? hebu mwanangu turudi ndani nikaongee naye, aliongea mama Kulwa huku wakiingia ndani na kumkuta Mzee Mgaya akiwa karibu na mwanaye Jose wakiangalia baadhi ya matokeo ya Samson ambapo muda wote Jose alitikisa kichwa akionesha anakubali uwezo wa Samson.

Aiseeeh yaani kichwa hiki kama kingekuwa high school ingependeza sana, nahitaji kuona anavyofika mbali huyu dogo, aliongea Jose kwa furaha sana.

Baba Kulwa, na wote tuliopo hapa ndani hebu naombeni tusikilizane,
Naomba kujua baba Jose una tatizo gani na huyu mtoto. aliuliza mama Kulwa

Tatizo, tatizo gani? Mimi Sina matatizo na nwanangu kwani kakuambia nini, maana hata ulivyoingia hapa Mimi nimeshtuka Kuna jambo nimeliona halipo sawa, Sasa ni vyema wote tutajua ili kama mtoto kakukwaza aonywe, huyu siyo wa kumnunia, kwanza unachekesha sana mtoto huyu si kama mjukuu tu kwako? Jambo gani limekuudhi kiasi cha kumkalia kimya? aliuliza Mama Kulwa.

(Huku akicheka)Yaani wewe leo hii wakumuonea huruma Samson, huruma hiyo imeanza lini, au unataka uonekane mwema sana, Samson nimemtoa mkoani huku shule tukimtaka asome iliyokaribu na hapa , na kuishi aishi hapa ambapo ndiyo nyumba yangu kubwa watu wote wanajua wewe ndiye malkia wa mzee Mgaya na wageni wangu wote huwa wanafikia hapa, je nani amesababisha Samson ahame hapa siyo wewe? Ni Mara ngapi ulionesha humpendi lakini nikawa nazuia nikijua leo kesho mtakaa sawa lakini mambo yalizidi kuharibika nikaamua kumuhamisha Samson.
aliongea kwa hasira na dharau Mzee Mgaya.

Nimehangaika naye huyu toka kijijini hadi kufika naye hapa, matokeo yake yalichakachuliwa huku wajanja wakitaka kupora haki yake lakini nilipambana mpaka kufikia kufanikisha suala hili iweje leo nimchukie Samson, hajafikia hata Moja ya nane ya malengo yangu namuachaje? tatizo ni wewe ulishindwa kuishi na huyu mtoto nani asiyejua? Hivyo usianze kujiona mwema sana mbele ya mwanao Jose, wewe ni mke wangu nakujua vizuri sana tu. aliongea Mzee Mgaya

Weeeeeeee tena ishia hapohapo Mimi ni mama najua mtoto analelewa vipi, malezi ambayo ulitaka kumpa huyu mtoto siyo kabisa, unadhani huko kwao alikotoka alikuwa hafanyi kazi, Sasa ilifikia hatua unamkataza asinisaidie kazi ulikuwa na maana gani? kwakuwa na Mimi Nina misimamo yangu, nikaona mpeleke sehemu ambayo hatofanya kazi, huyu mtoto Mimi simchukii Wala si kama simpendi na akiamua kurudi hapa tutampokea kwa mikono miwili lakini lazima afanye kazi,
Eti wewe kwa Tausi huwa kazi yako ni kula tu na kutulia? aliulizwa Samson.

Akaitikia kwa kutikisa kichwa kuwa huwa anafanya kazi.

Mama Kulwa akaendelea............

Sasa wenzangu mmekuja na jambo kubwa zaidi mkimuita huyu mtoto mchawi, kweli jamani mbona mna dhambi hivyo?
Yaani Tausi aseme nini asikilizwe, atakuja kukufanya ukose heshima na Imani kwenye jamii kwa kuendelea kusikiliza Kila upuuzi wake.
Mama Kulwa aliongea bila uoga wowote akionesha kujiamini sana.

Mzee Mgaya alifura kwa hasira sana huku akitamani aseme neno lakini uwepo wa mwanaye Jose ulifanya adhibiti hali yake.

Kwa upande wa Jose yeye alikuwa kimya sana hakujibu neno lolote huku akiwaomba wazazi wake wakapumzike kisha na yeye akiingia kwenye chumba chake, hali kadhalika Samson akaingia kwenye chumba chake huku moyo Ukiwa unamuuma sana kwani kitendo Cha watu kuwa wanapishana kwa sababu yake, alijikuta anakata tamaa, sasa sehemu ambayo aliitegemea kuwa anaweza kuishi vyema kwa Tausi, nako kuligeuka kwa moto mbaya zaidi hata Mzee Mgaya naye alikuwa yupo upande wa Tausi hivyo ilimuwia vigumu mno.

Asubuhi aliamka akamkuta mama Kulwa nje wakasalimiana.

Mwanangu pole sana, hata hivyo usijali yule Malaya Tausi alileta fitina hadi kufikia wewe kuhama hapa lakini , unajisikiaje kuambiwa wewe ni mchawi?
Ina maana umetukanwa wewe na familia yako , yaani wazazi wako wote wanaonekana wachawi, sasa unawezaje kuishi hiyo sehemu,
Mwanangu ipo siku utapewa sumu kwani tayari mpo kwenye mashindano na familia ya Tausi,
Na asili ya mashindano lazima apatikane mshindi.
Sasa baba yangu Samson unadhani unaweza kushinda? aliongea mama Kulwa huku akimtisha sana Samson.

Samson alifungua geti kwa nguvu huku maneno yale yakimtisha sana , alifika shule huku ile hali ya yeye kuishi kama digidigi ikimuumiza sana mbaya zaidi alishindwa kujua hatma ya Nini kitatokea, akahisi kuwa hana muda anaweza kuacha shule , hakuwaza kuhusu kuhama shule,
Nani atamuhamisha?
Mtu ambaye alimfanyia mipango yote kuanzia kijijini kwao Hadi mjini lakini Sasa aliona kabisa hakuna tumaini la kuendelea kusoma.

Itaendelea.......................

Shukrani Mkuu….Tuongezee episodes zngne tusindikize hii Xmass
 
SEHEMU YA AROBAINI

Siku hiyo Samson alikuwa mvivu kushinda maelezo, hakujishughulisha na chochote darasani, hakuweza kujadiliana lolote na mtu yeyote.
Hata walimu walipoingia kwa zamu kwenye vipindi vyao, alijikuta anatimiza wajibu tu ili asishtukiwe na kupewa adhabu ila tayari saikolojia yake haikuwa sawa.

Muda wa kurudi ulifika, hakuwa na sehemu nyingine ya kwenda zaidi ya kwa mama Kulwa, ambapo licha ya kuwa walishavurugana kiasi cha yeye kuhama pale, lakini safari hii aliona ni afadhali kule, alizipita nyumba kadhaa akawa ameshafika tayari, kabla ya kuingia ndani alizisikia sauti nyingi akagundua huenda watu wameongezeka humu ndani japo hakujua ni akina nani.
aliingia akakutana uso kwa uso na Rahma akashangaa huyu kafikaje huku, na kaja kufanya nini.

Naona umeamua kunikimbia Samson, jana nakusubiri hadi ilipofika saa tatu usiku nikakata tamaa nikasema hapa hatorudi tena, enhee niambie habari za kutoka jana, alisalimia Rahma.

Nzuri tu, japo si sana kwasababu nilitamani nirudi kule lakini niliogopa mamdogo Tausi ujue alinikoromea sana ile asubuhi hivyo niliogopa sana nikaamua kuja huku. aliongea kwa hisia sana Samson.

Mmmmh ila mamdogo hata sijui Wana ajenda gani na baba maana ile Jana si wewe tu hata Mimi alianza kunitukana Mara anikosoe jambo hili Mara aniambie hili, sikumuelewa tu kiukweli, lakini pia wakaanza kugombana na baba yaani ugomvi mkubwa ila nashukuru baba aliamua kuondoka sikujua akielekea wapi. aliweka kituo Rahma.

Labda ndiyo muda aliokuja huku kwani alinikuta nipo hapa, alijibu Samson.

Ila leo alikuja kaka mmoja hivi sijui mnamwita nani, alikuja peke yake akatuambia tujiandae ana mazungumzo na sisi pamoja na familia nzima inayomuhusu Mzee Mgaya na hapa watu wote wapo ndani ila wanasubiriwa huyo kaka yako wametoka sijui wameelekea wapi pamoja na baba lakini pia na wewe ulikuwa unasubiriwa
kwani walidai maongezi yanakuhusu na wewe hivyo kikao kitaanza ukirudi.
alifafanua Rahma huku Samson mapigo ya moyo yakiongezeka, kwanini kikao? Hapa Kuna usalama kweli maana nauona mwisho wa masomo yangu. aliwaza kimoyomoyo.

Samson aliingia ndani akawaamkia wale mama zake wale na kupitiliza hadi chumbani ili akabadilishe nguo alizopewa Jana na mama Kulwa ambazo ni za wale watoto mapacha akina Kulwa .
Akiwa chumbani alisikia namna wanawake wanavyoongea kwa furaha huku wakicheka, yaani watu watatu tu, walifunga sebule utadhani watu kumi, Catherine au Cathy mwanamke mdogo kuliko wote mwenye kuzijua stori za mjini lakini pia ni rafiki wa mama Kulwa ambaye anampenda sana Jose lakini huwa hilo jambo haliwezekani, lakini Tausi mwanamke mjanja na mnafiki anayejifanya anamuheshimu mama Kulwa pamoja na mama Kulwa mwenyewe, wote waliongea wakicheka na kugonga viganja kwa furaha
Samson alishangaa unafiki wa wanawake wale, kwani namna ambavyo Kila mmoja humchukulia mwenzake alijua huenda huwa hawaongei kabisa wakikutana.

Mzee Mgaya na mwanaye Jose walirudi huku wakimuulizia Samson kama amerudi wakaambiwa yupo na hata yeye alitoka huku akikaribishwa akae kikao kikaanza.

Kwanza nashukuru wote tupo wazima kama hivi, hakika ni jambo la kumshukuru MUNGU sana, na niwashukuru wote wazazi wangu watatu , yaani Mzee Mgaya mwenyewe, Mama yangu mzazi, na mama yangu mdogo (Tausi) kwa kunikubalia ombi langu la kuweza kuwakutanisha. Hebu tunaomba mmoja atufungulie sala fupi.
aliweka kituo Jose.

Watu waliangaliana hakuna aliyejua aanzie wapi Mzee Mgaya akajikuta kaanza kupiga ishara ya msalaba Kisha akafungua kikao kile kwa Sala nzuri kabisa yenye kugusa.
akapigiwa makofi huku mama Kulwa akimtania,
Sijaamini kama sala hii inatoka kwenye kinywa chako aisee yaani nimejikuta nabarikiwa.

Mimi nimesoma shule za wazungu seminary kuanzia la kwanza mpaka darasa la nane na Kila jambo lilikuwa linaanza kwa Sala,hivyo ni pombe tu hizi za ukubwani zinatufanya tunisahau hata vitu vidogo. alijibu mzee mgaya

Ok, sawa kabisa ila naomba asiyekuwa mwanafamilia hii atupishe kidogo kama itawezekana, (hapa Jose alimlenga Cathy)
Sasa mwanangu hapa Kuna nani mgeni mbona wote sisi tunaishi kama ndugu kuna tatizo yeye kuwepo hapa baba? aliuliza mama Kulwa lakini Cathy kwa kujiongeza akaamua ku step back akitoka nje ya sebule ile.

Kwanza awali ya yote niwapongeze wote kwa kuweza kumpokea mdogo wangu Sam kwa moyo wa upendo na mkaishi naye, hakika ni jambo kubwa ambalo kwa uzoefu wangu wa kutembea nchi mbalimbali, nimegundua jamii nyingi hazipendi kuishi na mtoto kirahisi, na hata hapa nchini kwetu wengi wameweka msimamo wa kutompokea mtu yeyote hata kama ni mtoto wa nani, watu wapo kwaajili ya familia zao walizozitengeneza tu, aliongea Jose huku wote wakimsikiliza kwa makini, akaendelea.............

Nimesikia malalamiko kadhaa kipindi fulani kuhusu ugomvi wa wazazi wangu, hadi kufikia kuumizana lakini pia Mzee wangu ukawekwa lockup jambo hili lilinihuzunisha sana, why wazee wangu nimekaa na nyinyi utoto wangu wote sikuona mkipigana kwanini sasa mkaanza hayo mambo kwenye umri huu, nikashauri huyo kijana ahamishwe atafutiwe sehemu nyingine, ndipo niliposikia yupo kwa mama mdogo Lakini Nako nasikia hali si nzuri na haya mambo ni mabichi kabisa, kwanini inakuwa hivyo? Huyu mtoto ana tabia gani ambazo zinasababisha yeye kuwa Kila mtu anashindwa kukaa naye? Tafadhali baba yangu weka hadharani ili tujue dogo tunaanza naye vipi, aliweka kituo Jose.

Mzee Mgaya hakuwa na sababu maalum za kuonesha kwanini wanamchukia Samson, alizidi kukataa na kudai kama angekuwa hampendi Wala hamtaki Samson angemrudisha kijijini
Kwani ndiye mwenye mamlaka na Samson amsomeshe au aamue kuachana naye.aliongea kiujeuri Mzee Mgaya akijivunia cheo cha yeye kuwa baba.

Jose, first born wa mzee Mgaya ambaye ni mwenye Elimu yake
Dark, tall, msikivu, mtulivu mwenye busara alitambua nguvu ya Tausi kwa mzee Mgaya akaamua kutumia busara.

Sasa ajenda kuu ya kikao hiki kifupi ni kuamua hatma ya Samson nyinyi kama wazazi wangu watatu, tunaomba mpendekeze wapi kijana wenu anaweza kuishi bila bughudha au asikere watu, aliuliza Jose.

Mzee Mgaya akadakia,
Huyu ataishi hapa kuanzia leo, kwanza mimi nilishamkataza tangu siku nyingi, asikae sehemu nyingine tofauti na hapa Mimi wake zangu wote nawajua, hivyo viwango vyao vya uvumilivu kwa Kila mmoja navijua
Hakuna binadamu asiyekuwa na hasira, ila shida ni pale unapoihifadhi hasira yako kifuani, Hilo ni tatizo .
Kwani hata biblia imeandika
Hasira hukaa kifuani mwa mtu mpumbavu.
alisema Mzee Mgaya huku safari hii akionesha anamlenga Tausi kwa Yale maneno.

Hakuna tatizo Mzee wangu, sisi sote hapa ni familia yako hivyo lolote unaloamua lenye kutuingia vichwani basi Kila kitu kitakuwa sawa, japo Samson kule kwa mamdogo napo ni nyumbani ni watu umekaa nao, umeishi nao hivyo siyo unamaliza miezi bila kuonana nao kama upo mbali si jambo jema sana.aliongea Jose kwa mtego.

Ni kweli kabisa pale ni kwake, na hata kile chumba ni chake muda wowote akijisikia hata kulala itakuwa sawa tu ajisikie yupo nyumbani kabisa, lakini pia nikupongeze kwa kuweza kutuunganisha Tena na dada yangu nikakanyaga Tena kwenye nyumba hii hakika umebarikiwa Jose. Amebarikiwa mama yako mzazi na wote wslioshuhudia jambo hili nadhani matatizo ya Samson yamekuwa chachu ya Mimi kupatana na dada yangu (mama Kulwa) aliongea Tausi huku wakikumbatiana na mama Kulwa wakionesha hisia kali sana.

Mzee Mgaya aliipenda sana ile hali kuliko hata masuala ya Samson, aliujua unafiki wa wanawake kwamba haya ni maigizo tu, lakini alifurahi zaidi kwani aliona Kuna kitu kitapungua maana wanawake walikuwa wanasemana kiasi Cha kumtisha Mzee Mgaya.

Walimaliza vyema kikao Chao huku Jose akiwa man of the match maana mzee Mgaya alijua yale mambo hayangewezekana badala yake, wangezua ugomvi zaidi, hivyo kuisha salama lilikuwa jambo jema sana.

Wakati wapo pale ukumbini wakipiga stori za kawaida Samson aligundua Tausi anamwangalia sana tena Kwa jicho la mahaba kabisa, yaani Kila wakikutanisha macho, uso wa Tausi uliongea jambo, Samson aliamua kutoka na kwenda kukaa karibu na wanapopark magari yao, na Tausi akaja usawa uleule.

Sasa Sam si tunaenda nyumbani, eeh si Kuna vitu vyako, hutaki kwenda kuchukua. aliongea Tausi kwa sauti ya chini sana.

Kwani mamdogo una wasiwasi gani kwanza huyu bro lazima atawarudisha na gari usiku huu huu na Mimi nakuja kuchukua begi langu na nitarudi naye. alijibu Samson huku akiwa na mashaka na Tausi, anataka nini kwangu huyu.

Itaendelea................................
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom