Kama humpendi achana nae kwa amani,hizo tabia,sijui anaweza kuwa mama mzuri asikudanganye mtu,baada ya mda mawazo hayo yatayeyuka.Hakuna kitu kigumu kama kulala na kuamka na mwanamke usie na hisia nae,nasema ni ngumu sana sababu nimepitia,na mimi nilikuwa na mawazo hayo hayo.
Baada ya mda utaanza kumchukia huyo mwanamke utaona ni mateso kuwa nae,au utakaa nae sababu unamhurumia tu.
Fikiri una manyege yako alafu kila ukimangalia wa ubavuni mwako kitu inasinyaa yenyewe,kama mbwa kaona kobra.Lakini ukitoka nje tu kila mwanamke unamuona mzuri.Yaani usijaribu,utamtesa tu mtoto wa watu.Wengi wanaosema mke mzuri sio sura wala umbo,hawajakutana na hili.Kweli kuna wakati mwengine inabidi u 'compromise' kidogo lakin lazima kuwe na asilimia flani ya hisia/kuvutiwa na mwanamke,wanaume ni watu wa kutamani sana.