Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Klabu ya Simba leo Jumapili February 13 inashuka kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa kucheza na ASEC Mimosas kutoka Ivory coast, kwenye mchezo wa kwanza hatua ya makundi Kombe la Kombe la Shirikisho Barani Afrika CAFCC.
Hautakuwa mchezo mwepesi, bali utakuwa mgumu na wa kusisimua hasa ukizingatia timu zote mbili zina mbinu zinazofanana uwanjani.
Ubora wa Simba SC kwenye uwanja wa Mkapa ni Mentality nzuri kwa wachezaji kucheza kwa kupambana kwa soka lao la kuburudiasha kwa pasi nyingi na ndefu wakianzia chini mpaka kusogea mstari wa kati huku wakisogea pembeni na mashambulizi ya kasi kupitia kati ama pembeni kutoka kwa mabeki Hussein na Kapombe, ambao ni wazuri kwa 'Crossing'
Kwa upande wa ASEC Mimosas ni wana uwezo mkubwa kama timu na kasi yao ni 'dynamic' wanakimbia kwa kasi kwa mashambulizi ya pembeni kutoka kwa wachezaji wao Athohoula na Coulibally.
Nani kuibuka na ushindi? Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10: 00 Jioni Usikose Ukaambiwa.
Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
=====
00' Naaam mpira umeanza uwanja wa Benjamin Mkapa.. Simba SC vs ASEC Mimosas.
05' Simba SC 0-0 ASEC Mimosas
Mpira ni mkali huku mashambulizi yakielekezwa kwa pande zote mbili hata hivyo bado milango ni migumu.
10' ASEC Mimosas wakijaribu lango la Simba SC, lakini mabeki wanakaa imara.
13' Sakho Goooooooooooooaaal gooal
Pape Sakho anawatanguliza Simba SC bao la kwanza kwa tikitaka murua kabisa | Simba SC 1-0 ASEC Mimosas
15' ASEC wanakosa utulivu, shambulizi lao linashindwa kuzaa matunda.
Pape Sakho yupo chini, baada ya kupata rabsha, anaomba kuingia ameingia sasa.
22' Kagereeee loooooo mpira unaginga mlingoti, almanusura Simba SC waandike bao la pili, ilikuwa hatari sana.
26' Kona kuelekea ASEC, inapigwa kona lakini inaokolewa, mpira uko kati na wamiliki ni Simba SC sasa.
30' ASEC wanatumia sana kujilinda kuliko kushambulia, huku Simba SC wakijaribu kuongeza bao la pili, ngoja tuone.
32' wanao mpira ASEC mbele kulee anapiga shuti, lakini Aishi Manula anadaka, ni shambulizi la On Target.
37' ASEC wanajenga kibanda lango la Simba SC, huko Sakho akiwa chini kwa mara nyingine tena
40' Ametoka Pape Sakho na ameingia Mzamur Yassin upande wa Simba SC, mabadikio yasiyokuwa ya ufundi.
44' Peter Banda anakosa nafasi ya kuiandikia Simba SC bao la pili, ilikuwa nafasi nzuri kufunga...Dooooh
45+3' Kuelekea kuwa mapumziko kwenye mchezo huo wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika.
Naaam mpira ni mapumziko ambapo Simba SC wanatoka wakiwa mbele ya bao moja kwa bila dhidi ya ASEC Mimosas.
HT: CAFCC; Simba SC 1-0 ASEC Mimosas
Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Benjamin Mkapa.
47' ASEC Mimosas wameingia kwa kasi kujaribu kusawazisha.. Lakini Simba wapo imara kulinda lango
53' Kagere anashindwa kuunganisha wavuni Krosi ya Banda, ilikuwa nafasi nzuri kwa Simba SC, Umiliki ni wa Simba SC
ASEC wanajenga kibanda tena lango la Simba, Jaribio lao la kufunga linashindikana hapa.
60' Goooooooooooooaaal, ASEC Mimosas wanasawazisha kupitia kwa Aziz Stephanie kwa shuti kali, shughuli ni pevu sasa ni makosa ya mabeki. Simba SC 1-1 ASEC Mimosas.
64' Kona kuelekea ASEC Mimosas inapigwa konaaa inaokolewa na mabeki wa ASEC.
70' ASEC wanamjaribu golikipa Manula, lakini anadaka shuti lile, ilikuwa hatari lango la Simba SC.
71' Kanoute ametolewa nje kwa matibabu baada ya kupata rabsha
74' Ametoka Kagere na ameingia Jonh Bocco, huku Mhilu akichukua nafasi ya Kanoute..Simba SC 1-1 ASEC Mimosas.
Simba SC wanapata mkwaju wa penalty baada ya Mhilu kuchezewa rafu, Kapombe anakwenda kupiga mkwaju wa penalty
80' Kapombe Goooooooooooooaaal gooal, Kapombe anaandika bao la pili.. Simba SC 2-1 ASEC Mimosas
81' Goooooooooooooaaal gooal
Peter Banda anapiga bao la tatu upande wa Simba baada ya kazi nzuri ya Bocco
Simba SC 3-1 ASEC Mimosas
86' Simba SC wanafanya mabadikio. Ametoka Bwalya na Banda na wameingia Nyoni na Patrick mpira unaendelea.
90+4' Kuelekea kumalizika kwa mchezo huu wa CAFCC, Umiliki wa mpira ni wa Simba SC
Almanusura Simba SC waandike bao la nne, baada ya Krosi ya Bocco kutolewa nje na beki wa ASEC
Ni mpira wa adhabu kuelekea Simba SC, Coulibally anaoiga lakini mpira unatoka nje.
Naaam mpira umekwisha ambapo Simba SC wanatoka wakiwa mbele kwa ushindi wa mabao matatu kwa moja dhidi ya ASEC Mimosas
FT, CAFCC; Simba SC 3-1 ASEC Mimosas
......... Ghazwat..........
Hautakuwa mchezo mwepesi, bali utakuwa mgumu na wa kusisimua hasa ukizingatia timu zote mbili zina mbinu zinazofanana uwanjani.
Ubora wa Simba SC kwenye uwanja wa Mkapa ni Mentality nzuri kwa wachezaji kucheza kwa kupambana kwa soka lao la kuburudiasha kwa pasi nyingi na ndefu wakianzia chini mpaka kusogea mstari wa kati huku wakisogea pembeni na mashambulizi ya kasi kupitia kati ama pembeni kutoka kwa mabeki Hussein na Kapombe, ambao ni wazuri kwa 'Crossing'
Kwa upande wa ASEC Mimosas ni wana uwezo mkubwa kama timu na kasi yao ni 'dynamic' wanakimbia kwa kasi kwa mashambulizi ya pembeni kutoka kwa wachezaji wao Athohoula na Coulibally.
Nani kuibuka na ushindi? Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10: 00 Jioni Usikose Ukaambiwa.
Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
=====
00' Naaam mpira umeanza uwanja wa Benjamin Mkapa.. Simba SC vs ASEC Mimosas.
05' Simba SC 0-0 ASEC Mimosas
Mpira ni mkali huku mashambulizi yakielekezwa kwa pande zote mbili hata hivyo bado milango ni migumu.
10' ASEC Mimosas wakijaribu lango la Simba SC, lakini mabeki wanakaa imara.
13' Sakho Goooooooooooooaaal gooal
Pape Sakho anawatanguliza Simba SC bao la kwanza kwa tikitaka murua kabisa | Simba SC 1-0 ASEC Mimosas
15' ASEC wanakosa utulivu, shambulizi lao linashindwa kuzaa matunda.
Pape Sakho yupo chini, baada ya kupata rabsha, anaomba kuingia ameingia sasa.
22' Kagereeee loooooo mpira unaginga mlingoti, almanusura Simba SC waandike bao la pili, ilikuwa hatari sana.
26' Kona kuelekea ASEC, inapigwa kona lakini inaokolewa, mpira uko kati na wamiliki ni Simba SC sasa.
30' ASEC wanatumia sana kujilinda kuliko kushambulia, huku Simba SC wakijaribu kuongeza bao la pili, ngoja tuone.
32' wanao mpira ASEC mbele kulee anapiga shuti, lakini Aishi Manula anadaka, ni shambulizi la On Target.
37' ASEC wanajenga kibanda lango la Simba SC, huko Sakho akiwa chini kwa mara nyingine tena
40' Ametoka Pape Sakho na ameingia Mzamur Yassin upande wa Simba SC, mabadikio yasiyokuwa ya ufundi.
44' Peter Banda anakosa nafasi ya kuiandikia Simba SC bao la pili, ilikuwa nafasi nzuri kufunga...Dooooh
45+3' Kuelekea kuwa mapumziko kwenye mchezo huo wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika.
Naaam mpira ni mapumziko ambapo Simba SC wanatoka wakiwa mbele ya bao moja kwa bila dhidi ya ASEC Mimosas.
HT: CAFCC; Simba SC 1-0 ASEC Mimosas
Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Benjamin Mkapa.
47' ASEC Mimosas wameingia kwa kasi kujaribu kusawazisha.. Lakini Simba wapo imara kulinda lango
53' Kagere anashindwa kuunganisha wavuni Krosi ya Banda, ilikuwa nafasi nzuri kwa Simba SC, Umiliki ni wa Simba SC
ASEC wanajenga kibanda tena lango la Simba, Jaribio lao la kufunga linashindikana hapa.
60' Goooooooooooooaaal, ASEC Mimosas wanasawazisha kupitia kwa Aziz Stephanie kwa shuti kali, shughuli ni pevu sasa ni makosa ya mabeki. Simba SC 1-1 ASEC Mimosas.
64' Kona kuelekea ASEC Mimosas inapigwa konaaa inaokolewa na mabeki wa ASEC.
70' ASEC wanamjaribu golikipa Manula, lakini anadaka shuti lile, ilikuwa hatari lango la Simba SC.
71' Kanoute ametolewa nje kwa matibabu baada ya kupata rabsha
74' Ametoka Kagere na ameingia Jonh Bocco, huku Mhilu akichukua nafasi ya Kanoute..Simba SC 1-1 ASEC Mimosas.
Simba SC wanapata mkwaju wa penalty baada ya Mhilu kuchezewa rafu, Kapombe anakwenda kupiga mkwaju wa penalty
80' Kapombe Goooooooooooooaaal gooal, Kapombe anaandika bao la pili.. Simba SC 2-1 ASEC Mimosas
81' Goooooooooooooaaal gooal
Peter Banda anapiga bao la tatu upande wa Simba baada ya kazi nzuri ya Bocco
Simba SC 3-1 ASEC Mimosas
86' Simba SC wanafanya mabadikio. Ametoka Bwalya na Banda na wameingia Nyoni na Patrick mpira unaendelea.
90+4' Kuelekea kumalizika kwa mchezo huu wa CAFCC, Umiliki wa mpira ni wa Simba SC
Almanusura Simba SC waandike bao la nne, baada ya Krosi ya Bocco kutolewa nje na beki wa ASEC
Ni mpira wa adhabu kuelekea Simba SC, Coulibally anaoiga lakini mpira unatoka nje.
Naaam mpira umekwisha ambapo Simba SC wanatoka wakiwa mbele kwa ushindi wa mabao matatu kwa moja dhidi ya ASEC Mimosas
FT, CAFCC; Simba SC 3-1 ASEC Mimosas
......... Ghazwat..........