Siloam Ministry International Mbezi Beach

Siloam Ministry International Mbezi Beach

Hili kanisa lina mushkeli sana halafu ukicheki ni kanisa la uongo kabisa.
Walishawahi jaribu kimuombea mama mmoja alifariki miaka ya nyuma ili afufuke basi wakamlaza madhabahuni kanisani kwao hakufufuka wala nini alizidi kuvimba mwili yule mama bado kidogo apasuke.Hawa watu ni wapotoshaji kabisa na ukisali pale lazima akili zako kidogo ziwehuke.
Jamaa anapoteza watu wengi sana na waumini humchukulia huyo Kiongozi kama MUNGU wao maana humuimbia nyimbo za kumsifu.

Mmh iyo ndio soloam?!!
 
Kuna watu wamekuwa hawaheshimu maitiu.Mtu akifa wanamsumbua kwa kumnyanyua kumtembeza na hata kupiga vibao ili afufuke.

Mfano mzuri ni wa Kanisa la SLOAMU mbezi beach ambapo toka kiongozi wao NABII ELIYA MUNUO afariki juzi wamekuwa wakiitesa hiyo maiti kwa kuitembeza n.k ili afufuke.Haya ni mateso kwa maiti.Mtu akifa anatakiwa akazikwe sio kumpa mateso namna hiyo

VYOMBO VYA DOLA NA WAANDISHI WA HABARI NENDENI KULE Kanisa la SLOAMU MBEZI BEACH DAR ES SALAAM MKAONE MATESO ANAYOPEWA MAITI.Naambiwa hiyo si mara yao ya Kwanza

Kuweko sheria ya kuheshimu maiti.
Hizi dini nyingine ni za kupiga marufuku,mambo wanayoyafanya hayana tofauti na wachawi.
 
Leo asubuhi kanisani SILOAM wakati wa maombi ya asubuhi waliweka CD ya nabii Eliya, majirani wakaanza kushangaa kuwa huenda nabii huyu hajafariki au amefufuka.

Habari za uhakika hata ndugu zake hawakuwa wanafahamu km amefariki, inasemekana kuwa mdogo wake anayeitwa Swai aliposikia taarifa hizi aliamua kwenda kanisani, alipofika pale hakuona km kuna msiba, aliwauliza waumini kuhusu viongozi walipo wao wanawaita makuhani wakiwa na kikao juu ghorafani, alipofika walimkarisha kwa kumpa hongera sana, akashangaa kwa nini alikuwa anapewa hongera, aliuliza zaidi kwa nini hongera? alojibiwa kuwa Nabii Eliya alikuwa ameshinda umauti amenyakuliwa na MUNGU, nasikia ndugu yake akauliza kwa hiyo hayupo akajibiwa yeye hayupo amenyakuliwa ili mwili wake umehifadhiwa katika hospitali ya Lugulo. kwa taarifa zaidi mazishi yatakuwa siku ya J4 ambayo ndiyo km jumapili ya kwao.

Hivyo wao wanapeana hongera lkn kwa sasa kumepooza sana. Nabii huyu kwa jina jingine alijiita adamu wa pili. makazi yake yapo bao bao km unaenda bagamoyo, kuna mjengo wa ghorofa km 3, na magate 3 kabla ya kufika mjengoni.

kazi ipo
 
Duh. .

Najaribu kufikiri kwamba kama huyu ni Nabii wa mwisho wa kizazi hiki cha nne ina maana hakutakuwa na Nabii mwingine tena?
Atakaye take over hiyo nafasi sijui ataitwaje. ........

Mungu atusaidie

Achana na huo upuuzi wao hawa watu ni waongo wa wazi wazi yaani hata hawakufichi kwamba wanakudanganya.Huyo nabii wao anawafundisha wasiende hospitali wakiumwa huo si utahira kabisa,halafu mtu kama huyu anayeweka maisha ya watu kibao hatarini mnamwambia alale mahali pema.Rest in hell MUNUO,umepoteza wengi kwa kupindisha maandiko na damu zao utadaiwa na Yeye ahukumuye kwa haki pasipo upendeleo.
 
sheria ipo sema tu kwa vile ni issue sensitive ndo mana ku enforce inaleta kila aina ya shida!!
 
Nimepita Leo asubuhi SAA moja na nusu hivi nimekuta wamejazana kwenye Yale mabasi yao sijui wanaenda wapi
 
wandugu nimepata taarifa kuwa ---- mambo mazito yanaendelea kuanzia jana hadi leo kanisani hapo mbezi Beach Makonde..Mwenye habari zaidi atujuze au kama kuna mtu anasali hapo atuambie tafadhali

Haha hao watu ni wa ajabu sana.
 
Ndo zake huyo. Hii post anairusha kwenye threads mbalimbali anazoziona ni za kipuuzi.

katumwa huyo, upotoshaji fani wenzio wanasomea china kasome kwanza urudi ili upotoshe mada ya sloam
 
Hili kanisa lina mushkeli sana halafu ukicheki ni kanisa la uongo kabisa.
Walishawahi jaribu kimuombea mama mmoja alifariki miaka ya nyuma ili afufuke basi wakamlaza madhabahuni kanisani kwao hakufufuka wala nini alizidi kuvimba mwili yule mama bado kidogo apasuke.Hawa watu ni wapotoshaji kabisa na ukisali pale lazima akili zako kidogo ziwehuke.
Jamaa anapoteza watu wengi sana na waumini humchukulia huyo Kiongozi kama MUNGU wao maana humuimbia nyimbo za kumsifu.
hawa jamaa ni wajasiliamali.....
 
Leo asubuhi kanisani SILOAM wakati wa maombi ya asubuhi waliweka CD ya nabii Eliya, majirani wakaanza kushangaa kuwa huenda nabii huyu hajafariki au amefufuka.

Habari za uhakika hata ndugu zake hawakuwa wanafahamu km amefariki, inasemekana kuwa mdogo wake anayeitwa Swai aliposikia taarifa hizi aliamua kwenda kanisani, alipofika pale hakuona km kuna msiba, aliwauliza waumini kuhusu viongozi walipo wao wanawaita makuhani wakiwa na kikao juu ghorafani, alipofika walimkarisha kwa kumpa hongera sana, akashangaa kwa nini alikuwa anapewa hongera, aliuliza zaidi kwa nini hongera? alojibiwa kuwa Nabii Eliya alikuwa ameshinda umauti amenyakuliwa na MUNGU, nasikia ndugu yake akauliza kwa hiyo hayupo akajibiwa yeye hayupo amenyakuliwa ili mwili wake umehifadhiwa katika hospitali ya Lugulo. kwa taarifa zaidi mazishi yatakuwa siku ya J4 ambayo ndiyo km jumapili ya kwao.

Hivyo wao wanapeana hongera lkn kwa sasa kumepooza sana. Nabii huyu kwa jina jingine alijiita adamu wa pili. makazi yake yapo bao bao km unaenda bagamoyo, kuna mjengo wa ghorofa km 3, na magate 3 kabla ya kufika mjengoni.
Huyu bwana Munuo kabla ya kuanzisha dini yake hapo Sloam, tulisali naye pale Mbezi Beach Luth Church.
Na alipora waumini wengi sana toka Mbezi, ila wengi wamekufa kwa imani zao zisizoeleweka.
Namkumbuka mamam mmoja ambaye mume wake alifariki kwa ukimwi.
Alipojiunga hapo aliambiwa atapona tu kwa miujiza, huyo mama akaendelea kupungua kilo hadi naye akaudedi.


Pamoja na kumpa hongera Munuo kwa kupata waumini wengi, lakini hilo neno analolisambaza kwa hakika halitoki kwa Bwana.
 
Acheni uongo nyie kizazi cha shetani,

Tangu jana kuna maombi ya TOBA, hakuna aliyekufa bali kalala tu mjumbe wa mapenzi ya Mungu Eliya Kizazi cha nne.


Kumbe na wewe ni muumini wa hizi dini za digitali????

Wajinga hawaishi chini ya Jua
 
Huyu bwana Munuo kabla ya kuanzisha dini yake hapo Sloam, tulisali naye pale Mbezi Beach Luth Church.
Na alipora waumini wengi sana toka Mbezi, ila wengi wamekufa kwa imani zao zisizoeleweka.
Namkumbuka mamam mmoja ambaye mume wake alifariki kwa ukimwi.
Alipojiunga hapo aliambiwa atapona tu kwa miujiza, huyo mama akaendelea kupungua kilo hadi naye akaudedi.


Pamoja na kumpa hongera Munuo kwa kupata waumini wengi, lakini hilo neno analolisambaza kwa hakika halitoki kwa Bwana.


Dini zimekuwa kama timu za mpira ama Bendi za Muziki...

Wanaporana waumini kama Bendi zinavyoporana Wanamuziki.....

NB:
Nimeamini kuwa Wajinga hawataisha Chini ya Jua.

Poleni sana wafiwa.
 
Acheni uongo nyie kizazi cha shetani,

Tangu jana kuna maombi ya TOBA, hakuna aliyekufa bali kalala tu mjumbe wa mapenzi ya Mungu Eliya Kizazi cha nne.
All along I knew there was something wrong with you!!!!
Ataamka lini?
Habu tushirikishe.
 
Back
Top Bottom