Siloam Ministry International Mbezi Beach

Siloam Ministry International Mbezi Beach

Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa
Mungu atusaidie nina ndugu wengi wanaabudu uko, ingawa kuna usiri mwingi ila walikuwa wakimfanya kama Mungu wao, maana badala ya kuomba kwa damu ya Yesu useme unaomba kwa sijui nabii haki sawa naona ni mkanganyiko. Ukurusa wa mwisho wa Biblia ule wa Ufunuo unahitimisha kuwa atayelibadili neno hili mapigo yatampata huwa wanaunyofoa.... ila ingekuwa vizuri waumini wake wakaelezea kiundani hii imani tusijekuwa tunasikia isivyo.
 
Mungu atusaidie nina ndugu wengi wanaabudu uko, ingawa kuna usiri mwingi ila walikuwa wakimfanya kama Mungu wao, maana badala ya kuomba kwa damu ya Yesu useme unaomba kwa sijui nabii haki sawa naona ni mkanganyiko. Ukurusa wa mwisho wa Biblia ule wa Ufunuo unahitimisha kuwa atayelibadili neno hili mapigo yatampata huwa wanaunyofoa.... ila ingekuwa vizuri waumini wake wakaelezea kiundani hii imani tusijekuwa tunasikia isivyo.

hapo kazi ipo na huo waumini hata uwaeleze vipi hawatakuelewa utadhani huwa wanapumbazwa
Mungu atusaidie
 
Leo asubuhi kanisani SILOAM wakati wa maombi ya asubuhi waliweka CD ya nabii Eliya, majirani wakaanza kushangaa kuwa huenda nabii huyu hajafariki au amefufuka.

Habari za uhakika hata ndugu zake hawakuwa wanafahamu km amefariki, inasemekana kuwa mdogo wake anayeitwa Swai aliposikia taarifa hizi aliamua kwenda kanisani, alipofika pale hakuona km kuna msiba, aliwauliza waumini kuhusu viongozi walipo wao wanawaita makuhani wakiwa na kikao juu ghorafani, alipofika walimkarisha kwa kumpa hongera sana, akashangaa kwa nini alikuwa anapewa hongera, aliuliza zaidi kwa nini hongera? alojibiwa kuwa Nabii Eliya alikuwa ameshinda umauti amenyakuliwa na MUNGU, nasikia ndugu yake akauliza kwa hiyo hayupo akajibiwa yeye hayupo amenyakuliwa ili mwili wake umehifadhiwa katika hospitali ya Lugulo. kwa taarifa zaidi mazishi yatakuwa siku ya J4 ambayo ndiyo km jumapili ya kwao.

Hivyo wao wanapeana hongera lkn kwa sasa kumepooza sana. Nabii huyu kwa jina jingine alijiita adamu wa pili. makazi yake yapo bao bao km unaenda bagamoyo, kuna mjengo wa ghorofa km 3, na magate 3 kabla ya kufika mjengoni.
nimecheka kweli hivi hizi ni akili au matope
 
Hatimaye umeamua kuwa mzushi na muongo kama kawaida ya jihadist wote duniani, au wana UWATA wamekurupusha majini yako kwa hasira umeamua kuwaunganisha na matukio ambayo hawahusiki, huko upareni hata UWATA yenyewe haipo, halafu unasema mwanzilishi alitokea huko.
Unasema UWATA ina mashule na miradi mingi, ni upi upo huko upareni?

Ni vema ukaongelea dini yako, vipi Boko haramu na Khalifa wa ISIS wanaendeleza sunna za kubaka wale watoto na kuchinja watu?
very cheap mind set better to IPR
 
hapo kazi ipo na huo waumini hata uwaeleze vipi hawatakuelewa utadhani huwa wanapumbazwa
Mungu atusaidie
Unajua watu huwa wakiwa desperate wanalishwa maneno bila kujijua unakiri na kuingia maagano.... kumbuka Ukristo pia kuna ukiri wa Imani na rejea Rumi 10:9 kwakuwa ukimkiri Yesu kwa kinywa chako kuwa ni Bwana na kuamini moyoni mwako kuwa Mungu alimfufua ktk wafu utaokoka... sasa kama unatabia ya kukiri imani au kuamini ktk binadamu badala ya Yesu ujue unaingia imani mpya na usishangae kwa mengine yanayokutokea. Ila tuache wenye imani hii wengi humu pia watakua kuweka wazi hili
 
Nafikiri tatizo lililolipotiwa sio kudanganya CV, ila kudanganya kwamba anaumwa na kuendelea kulipwa mshahara wakati tayari ameacha kazi. Mbaya zaidi yeye ni kiongozi wa nchi. Sasa mimi nilidahni Kikwete alifanya home yake vizuri katika kuteua timu yake, lakini kwa kashfa hii inaonekana uteuzi wake una walakini. Kumbuka huyu ni kiongozi wa pili kuibuka na udanganyifu ukiacha wale waliodanganya PhD zao!

Heee
Hii post vp tena hapa...
 
kweli kabisa kazi ipo sumu, blind faith ni kitu kibaya mno, unakanyaga msumari wa tetanus unakataa tiba ukiamini utapona kwa miujiza, mungu anatufundisha tujifunze kujisaidia naye atatenda alichofanya ni sawa na

-unazama mtoni unamuomba mungu akuokoe ghafla unaona tawi la mti, badala ya kulishika na kuendelea kumwomba mungu wewe unaliacha
-unamuona mnyama mkali kabisa mbele yako badala ya kutimua mbio huku ukimwomba mungu we we ndio kwanza unamsogelea
- wenzako wanadamka kwenda kazini huku wakimwomba mungu wewe unajifungia chumbani siku nzima na maombi ukiomba utajiri

mifano ni mingi
hata Yesu mwenyewe alipojaribiwa nyikani na shetani akamwambia kama wewe ni mwana wa Mungu jirushe Mungu atakuandalia malaika wakudake hhaahahaahh Yesu zilimchaji mara mbia akaona du nikijirusha ikabadilika itakuawa soo akapigilia msumari usimjaribu Bwana Mungu wako sasa hawa hawajifunzi unafikiri Yesu alishindwa kujirusha ili aoneshe nguvu za babaye aliyemtuma???? Aliona mambo yakibadilia ni aibuuuu!!!
 
Unajua watu huwa wakiwa desperate wanalishwa maneno bila kujijua unakiri na kuingia maagano.... kumbuka Ukristo pia kuna ukiri wa Imani na rejea Rumi 10:9 kwakuwa ukimkiri Yesu kwa kinywa chako kuwa ni Bwana na kuamini moyoni mwako kuwa Mungu alimfufua ktk wafu utaokoka... sasa kama unatabia ya kukiri imani au kuamini ktk binadamu badala ya Yesu ujue unaingia imani mpya na usishangae kwa mengine yanayokutokea. Ila tuache wenye imani hii wengi humu pia watakua kuweka wazi hili
kabisaa Biblia inasema siku za mwisho manabii wengi wauongo watatokea na watatumia jina la yesu kufanya miujiza, shika sana imani yako usiyumbishwe huku mara kule.
 
Kuna watu wamekuwa hawaheshimu maitiu.Mtu akifa wanamsumbua kwa kumnyanyua kumtembeza na hata kupiga vibao ili afufuke.

Mfano mzuri ni wa Kanisa la SLOAMU mbezi beach ambapo toka kiongozi wao NABII ELIYA MUNUO afariki juzi wamekuwa wakiitesa hiyo maiti kwa kuitembeza n.k ili afufuke.Haya ni mateso kwa maiti.Mtu akifa anatakiwa akazikwe sio kumpa mateso namna hiyo

VYOMBO VYA DOLA NA WAANDISHI WA HABARI NENDENI KULE Kanisa la SLOAMU MBEZI BEACH DAR ES SALAAM MKAONE MATESO ANAYOPEWA MAITI.Naambiwa hiyo si mara yao ya Kwanza

Kuweko sheria ya kuheshimu maiti.

Ni kweli si mara yao ya Kwanza, walifanya hivyo kule Kyela mkoani Mbeya, wakafanikiwa kufufua maiti wanne, tena kule Machame wakainua maiti moja, na kuchinja wachawi vigagula wawili (in de spiritual realm) hakuna waandishi wala Media yoyote iliyobebea bango hilo.
kwa hiyo wamezoea waacheni jamani
 
Jaman me ninasali siloam pia bt wa2 weng wanaongea vitu wasivyovijua bt mwenye swal aniulize na ii sio dini ni kanisa jaman mtofautshe din znazofahamika ni wakristo na waislam kwa tanzania siloam ni kanisa wala c dini wala dheheb
 
Ni kweli si mara yao ya Kwanza, walifanya hivyo kule Kyela mkoani Mbeya, wakafanikiwa kufufua maiti wanne, tena kule Machame wakainua maiti moja, na kuchinja wachawi vigagula wawili (in de spiritual realm) hakuna waandishi wala Media yoyote iliyobebea bango hilo.
kwa hiyo wamezoea waacheni jamani

Unaweza weka hati zao za kifo (death certificates) na picha za hao waliofufuka, namba zao za simu,mahali wanapoishi,namba za nyumba zao na ndugu wa karibu na wakazi wa karibu kama majirani,na watu ambao si waumini wa kanisa lenu n.k wanaoweza thibitisha kuwa kweli hao watu walikuwa wamefariki na mkawafufua ?

Maana kufa si siri ni kitu wazi kwa wengi na hata kufufuka wengi waweza sema ndiyo huyu mtu alikuwa kafa na sasa kafufuka.Tupe hizo taarifa za hao wafu wafufuka walipo tutafuatilia wenyewe kuhakiki.
 
Ni kweli si mara yao ya Kwanza, walifanya hivyo kule Kyela mkoani Mbeya, wakafanikiwa kufufua maiti wanne, tena kule Machame wakainua maiti moja, na kuchinja wachawi vigagula wawili (in de spiritual realm) hakuna waandishi wala Media yoyote iliyobebea bango hilo.
kwa hiyo wamezoea waacheni jamani
Duu.... inaonekana huko kyela hamna wanaokufa!
 
Jaman me ninasali siloam pia bt wa2 weng wanaongea vitu wasivyovijua bt mwenye swal aniulize na ii sio dini ni kanisa jaman mtofautshe din znazofahamika ni wakristo na waislam kwa tanzania siloam ni kanisa wala c dini wala dheheb

Nini maana ya siloam na vipi kuhusu hili la kukataa matibabu.
 
Labda sielewi, eti "..maiti inateswa..", navyojua mimi kitu kisicho na uhai hakisikii maumivu wala raha, hivyo kusema kuitesa maiti sielewi maana yake ni nini! Je, kuitembeza au kuisimamisha ni mateso makubwa zaidi kuliko kuifukia kwa "tani 7" za mchanga? Sielewi!

Nadhani si kuitesa bali ni "kuidhalilisha tu", mtu akisha kufa roho yake ikaacha mwili, huo mwili ni wa kuuhifadhi chini ya ardhi yaani kuuzika ukaozee huko uwe mbolea kwa mimea nk. Waumini hao wanatakiwa kuheshimu sheria ya Mungu, yaani ukizaliwa iko siku utakufa, na ukifa ni kuzikwa.
 
Tafadhali andika kitu ukiwa na uhakika usiandike kws vile unajisikia kuandika usije kujichumia laana!
 
Back
Top Bottom