The Supreme Conqueror
JF-Expert Member
- Feb 13, 2017
- 323
- 906
SIKUJUA KICHAA ANAELALA NJE YA JENGO LANGU NI MPELELEZI ANAEMTAFUTA GAIDI WA KIZUNGU NILIYEMUOA BILA MIMI KUJUA NI GAIDI😳🔥
Sehemu ya Kwanza ( 1 )
***************
KILA Mtu
🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
Ilikuwa takribani siku nne zimekatika tangu nianze kumuona mwanaume kichaa nje ya jumba langu akiwa ameketi na makorokoro yake, siku ya kwanza niliogopa kidogo kwani alilala hapo na makorokoro yake mpaka kukakucha, siku ya pili pia alifanya hivyo lakini siku ya tatu nilianza kumuhisi vibaya maana vichaa wengi wamekuwa wakitumiwa na majambazi katika kazi zao atakuja karibu na nyumba yako atapiga kambi wewe utajua ni kichaa kumbe ni msoma ramani. Basi nikataka kwenda kunfukuza lakini roho yangu ilisita kwa woga kwani sura yake ilikuwa inatisha vibaya mno, rundo la nywele chafu lilijikusanya kichwani mwake na isitoshe alikuwa anavuta mamisokoto sijui ni bangi au ni gonzo mwenzenu nikajihami hata kumsogelea.
Basi bwana usiku wa siku hiyo kulinyesha mvua kubwa sana, mvua ilipokatika nikatoka nje na tochi kuzunguka nyumba yangu niangalie usalama maana sikuwa na mlinzi bali nilikuwa naishi mimi tu na mke wangu Clara ambaye ni mzungu, naye tulikutana tu hotelini miezi miwili iliyopita nikiwa kwenye safari zangu za kikazi nikamtongoza akaubali basi nikamkaribisha kwangu na mabegi yake niishi naye wakati tukiendelea kufanya mchakato wa kwenda kutambulishana kwa wazazi. Sikukagua mabegi yake kwani sisi waafrika mila zetu ni mwiko kukagua mabegi ya mgeni japo yalikuwa chumbani kwangu.
Basi bwana wakati nazunguka nyumba yangu huku nikitembeza mwanga wa tochi huku na kule ghafla nikamuona yule kichaa akiwa amekaa palepale anapopenda kukaa na alikuwa amenyeshewa na mvua vibaya mno, nikasema potelea mbali hata awe jambazi siwezi kuruhusu binadamu mwenzangu ateseke vile mimi nimelala ndani, kama anaiba aibe tu, mali hizi ni za kutafuta na tutaziacha duniani. Kwanza angekuwa jambazi asingekubali anyeshewe vile yule ni mwendawazimu" Nilijisemea nafsini mwangu na kwa huruma nikaenda kumchukua, lakini kuna kibegi chake chakavu na kilikuwa kimeloana sana aliking'ang'ania licha ya kumtaka akitupe lakini alikataa katakata, nikaona kubishana na chizi ni kujipa kazi nikamchukua vile vile na kibegi chake, nilienda kumuogesha vizuri bila kujali kwani wote ni wanaume, nilimpa nguo zangu safi avae usiku ule kisha nikamuonyesha chumba alale, aliingia chumbani na hakutaka kuachia kibegi chake nilijiuliza "Kwani hicho kibegi kina nini mbona huyu kichaa hataki kukiachia" nilijiuliza sana lakini mwisho niliona ni tabia ya vichaa kung'ang'ania vitu wanavyovipenda.
Basi nilipohakikisha yule kichaa Kalala na mimi nikarudi chumbani kwangu alipo Clara mke wangu ambapo alikuwa amelala tangu mchana, nilipoingia chumbani nikamkuta anajiandaa maana kuna baadhi ya siku alikuwa akitoka usiku kwa madai ya kwamba anaenda kumpa kampani rafiki yake wa kike kule hotelini asibaki mpweke nami sikuwa namkatalia maana huyo rafiki yake ambaye walikuwa wanakaa naye hotelini ndiye aliyeniruhusu niishi naye na hata siku nilipotoka safarini na Clara tulikuja na rafiki yake lakini yeye alifikia hoteli ya mtaa wapili na kwangu. Alidai ana mtu wake mara kwa mara anamtembelea hivyo anataka amkute hotelini na si kwa mtu.
Basi Clara alipoondoka usiku ule nikabaki na maswali kichwani mwangu." Huyu mwanamke licha ya mvua yote hii kunyesha lakini hajaona haja ya kulala hivi ni kweli huwa anaenda kwa rafiki yake? Na begi lake dogo kabeba mbona hili kubwa limetiwa kufuli kuna nini ndani yake? Mh🤔 huku kukaribisha watu usiowafahamu vizuri ndani na mabegi huku hapana?" Niliwaza kisha nikaenda kuchukua plaizi ili nivunje lile kufuli nione ndani ya begi kuna nini halafu nirudishie kufuli kitaalam maana kazi hizo niliziweza.
Basi nikahangaika na kufuli mpaka likachomoka. Nikaanza kufungua nzipu taratibu huku mikono ikinitetemeka, ile natupia macho ndani ya begi😳 ghafla moyo wangu ulipasuka paaa mithili ya ukuni mkavu baada ya kuona slaha kali za kivita ambazo toka nizaliwe sijawahi kuziona. Macho yalinitoka 😳 kama dudumizi lilikabwa na kiazi cha moto kooni, ghafla uso wote ukaloa jasho licha ya chumba changu kuwa na kiyoyozi.. haraka nika.....
Niliyenda kuchukua plaizi ili nivunje lile kufuli kwenye begi la Clara ili nione ndani ya begi kuna nini halafu nirudishie kufuli la watu kitaalam maana kazi hizo niliziweza. Basi nikahangaika na kufuli mpaka likachomoka. Nikaanza kufungua nzipu taratibu huku mikono ikinitetemeka mithili ya mtu aliyeshika kambale ambaye bado yupo hai, basi ile tu natupia macho ndani ya begi😳 ghafla moyo wangu ulipasuka paaa mithili ya ukuni mkavu baada ya kuona slaha kali za kivita ambazo toka nizaliwe sijawahi kuziona. Macho yalinitoka 😳 kama dudumizi lilikabwa na kiazi cha moto kooni, ghafla uso wote ukaloa jasho licha ya chumba changu kuwa na kiyoyozi.. haraka nikaanza taratibu za kulirudishia lile kufuli kwa utaalam zaidi lakini wakati huo mtungo wa mawazo yalikuwa yakipenyeza kichwani kwangu sio kawaida.
"Mh huyu mwanamke anafanya kazi gani, mbona ana silaha kali hivi? au ni jambazi lakini mbona ni mpole vile na sura yake imejaa utashi wa kimahaba kiasi kile, hapana pengine kuna mtu anamtumia lakini jambazi hawezi kuwa na sura tamu kiasi kile" Niliongea mwenyewe kimoyomoyo na kujijibu mwenyewe kiufupi nilikuwa nimepagawa. "Lakini pengine huyu Clara ni jambazi nisijipe moyo kwa upole wake na mapenzi anayonipa kitandani nikamuona ni mwema laaaa hasha ! Hata simba ni hatari sana lakini kwenye mapenzi anatulia kama maji mtungini, hapa nisijipe moyo Brighton nimeangukia kwenye penzi la jambazi yani nimeyakanyaga kama sio kuyatimba" nilijisemea baada ya kumaliza kurudishia kufuli kwenye lile begi.
Nikakaa kitandani kisha nikavuta pumnzi ndefu na kushusha huku mkono ukiwa shavuni kwa mawazo "Mh na huyu kichaa ni kichaa kweli au geresha, kichaa gani anakubali kuogeshwa na apewe nguo nyingine avae bila kuleta utata wowote, sasa mbona na kile kibegi chake chakavu kilichonyeshewa na mvua ameking'ang'ania? kina nini ndani yake? Mbona sura yake ni kama mzungu chotara?
Kuna kitu si bure🤔 huenda ikawa huyu kichaa ni mpelelezi maana ndio kawaida yao unalikuta jitu linajidai chizi kumbe lipo kazini usione minywele ile ukasema chizi hapana ni askari wa usalama aliambiwa afuge manywele na mandevu maana kuna kazi anatakiwa kupewa miaka miwili badae hivyo anatakiwa awe katika muonekano wa kichaa. Inawezekana kabisa na huyu ni mpelelezi, anampeleleza Clara. Jamani Bryhton mimi si nitaambiwa nashirikiana na Clara wakati sijawahi kuiba hata kuku?" Niliwaza huku moyo ukinidunda vibaya mno.
Basi usiku huo wa manane nikatoka chumbani kwangu taratibu kwa mwendo wa kinyonga, nikaenda kusimama mlangoni mwa yule kichaa na kuaikilizia, nilimsikia akkoroma hapo nikabaini Kalala, basi nikajaribu kufungua mlango ajabu mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani na funguo, kidogo nikashangaa na kujiuliza " kichaa gani anafunga mlango kwa ndani au kuna taarifa gani anaficha zisijulikane?" Hapo nikagundua yule si kichaa bali ni mtu maalum katika kitengo maalumu. Basi nikajiongeza kuchungulia ndani kupitia tobo la kuingizia funguo.
Kumbe alifunga mlango na kutoa funguo mlangoni, hapo nikasema yes acha nikachukue funguo ya ziada nifungue taratibu mlango wa huyu kichaa, nichukue kile kibegi nione ndani yake kuna nini ili kujihakikishia kwamba naishi na watu wa aina gani ndani ya nyumba yangu. Nikafanya hivyo hatimaye nikafanikiwa kuingia ndani ya chumba kile..... Jamani Nyieeee..... Nyiee acheni tu kwani baada ya kuzama ndani haraka nika.
" Mh kichaa gani anaetambua kwamba muda wa kulala mlango unatakiwa ufungwe kwa ndania? 🤔Hapana huyu si kichaa bali kuna kitu au ama taarifa anaficha zisijulikane?" Niliwaza na hapo nikagundua yule si kichaa bali ni mtu maalum katika kitengo maalumu na kujifanya kote ni kichaa si kichaa bali pale yupo kazini. Basi mimi nikajiongeza kuchungulia ndani kupitia tobo la kuingizia funguo. Kumbe alifunga mlango na kutoa funguo mlangoni, hapo nikasema yes acha nikachukue funguo ya ziada nifungue taratibu mlango wa huyu kichaa, nichukue kile kibegi nione ndani yake kuna nini ili kujihakikishia kwamba naishi na watu wa aina gani ndani ya nyumba yangu.
Nikafanya hivyo hatimaye nikafanikiwa kuingia ndani ya chumba kile, huku nikitetemeka. Mara ghafla akaacha kukoroma😳 haraka nikakichukua kile kibegi na kutoka nacho nje taratibu kisha nikasimama pale mlangoni kwa muda kidogo nikisikilizia kama ataamka ama laa, mara akaanza tena kukoroma, taratibu nikaufunga ule mlango kwa nje na funguo. Haraka nikaelekea chumbani na kile kibegi chakavu ambacho hata mtoto wa fukara hawezi kubebea madaftari maana kilichakaa mno.
Basi nilipofika chumbani nikaketi Kitandani na kukifungua kile kibegi, kwanza nilikuta mfuko wa plastick uliofungwa, hapo nikagundua mfuko ule ni kwaajili ya kuzuia mvua isiloanishe vitu vilivyopo ndani yake. Nikautoa ule mfuko nje na kuufungua, kwanza nilishangaa 😳 kukuta simu na vitabu viwili, kimoja likiwa ni cha katiba ya America. Nikaikagua ile simu ilikuwa na paswed na iliwekwa vibration, bado tomaso nikaendelea kukagua zaidi ndani ya kile kitabu cha katiba, nilikuta picha ya yule kichaa akiwa amevalia gwanda la Marekani lenye nyota tano, na alikuwa nazifu huwezi kumdhania.
Tomaso niliendelea kukagua huku mikono ikinitetemeka mithili ya mgonjwa wa degedege, nikakuta vitambulisho vingi, usalama wa Taifa na vitengo vingi ambavyo yule kichaa alipitia akiwa kama mtumishi Marekani, nikakuta pasport ya kusafiria na nakala kadhaa. "Mh Mungu wangu yani vitu vyote hivi muhimu asiwe na hata bastola ya kumlinda je akivamiwa maana vyote ni Orginal na sio copy🤔 au bastola kaitoa akaweka uvunguni? Inawezekana" Niliwaza huku nikiendelea kupekua pekua.
Na ndipo ghafla😳 nikakutana na picha ya Clara imewekewa X na kwa nyuma iliandikwa "most wanted" yani anatafutwa kwa udi na uvumba, pia nikaona karatasi inayomuelezea Clara, macho yalinikodoka 😳 huku nikisoma, looo kumbe Clara ni jambazi kuu lililoua mamia ya watu nnchini Marekani yeye na mwenzake, pia akavunja mabenki mengi na kuiba pesa nyingi lakini haitoshi akamuua mtoto wa mbunge wa jimbo la California na ndipo akamua kutoroka yeye na mwenzake na inasemekana walitoroka na silaha kali walizoziiba kwenye kambi ya jeshi la kimarekani, Dah hakika nilikosa nguvu maana ni dhahiri zile silaha kwenye begi la Clara ndizo zilizoibiwa kwenye kambi ya jeshi la kimarekani.
"Mh Bryhton mie sasa nimeingia mkenge huku kushobokea wazungu hovyo na kukaribisha watu nisiowafahamu kwa undani nyumbani kwangu sasa kumeniweka pabaya sijui nifanyaje?🤔" Niliwaza na hapo nikaamua nirudishe taratibu vitu vya yule kichaa chumbani kwake maana alionekana ni mtu hatari sana, kabla sijaamka kitandani pale nilipoketi ili nirudishe vitu vya watu mara 😳 nikamsikia akiongea kwa jazba chumbani kwake tena kwa kingereza "aaaa! Nimeibiwa aaaa hapana haiwezekani" aliongea mwenyewe huku akifungua ule mlango wa chumba chake kwa ufunguo kwani alikuwa na funguo yake tofauti na ile yangu ya ziada niliyotumia kwenda kuchukua kibegi chake ili nimpekue.
Wakati anafungua mlango wake, haraka nikakitupia kile kibegi uvunguni kwangu huku nikitetemeka mpaka meno. Mara nikamsikia akitembea kwenye korido ya kuja chumbani kwangu. Mweee! Mweee ! Mweee Nilizidi kutetemeka na kuhisi haja kubwa ghafla, mara mlango wa chumba changu ukagongwa 😳 hapo nika...
Acheni nirudi maana ingekuwa ni wewe tayari ungeshajinyea walahi?
Unajua nini kiliendelea hakikisha unapomaliza kusoma unalike na kucoment ili usipitwe na moto huu🔥🔥🔥🔥🔥
Muendelezo soma: Sikujua kichaa anayelala nje ya jengo langu ni mpelelezi anayemtafuta gaidi wa Kizungu niliyemuoa bila mimi kujua ni gaidi
Sehemu ya Kwanza ( 1 )
***************
KILA Mtu
🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
Ilikuwa takribani siku nne zimekatika tangu nianze kumuona mwanaume kichaa nje ya jumba langu akiwa ameketi na makorokoro yake, siku ya kwanza niliogopa kidogo kwani alilala hapo na makorokoro yake mpaka kukakucha, siku ya pili pia alifanya hivyo lakini siku ya tatu nilianza kumuhisi vibaya maana vichaa wengi wamekuwa wakitumiwa na majambazi katika kazi zao atakuja karibu na nyumba yako atapiga kambi wewe utajua ni kichaa kumbe ni msoma ramani. Basi nikataka kwenda kunfukuza lakini roho yangu ilisita kwa woga kwani sura yake ilikuwa inatisha vibaya mno, rundo la nywele chafu lilijikusanya kichwani mwake na isitoshe alikuwa anavuta mamisokoto sijui ni bangi au ni gonzo mwenzenu nikajihami hata kumsogelea.
Basi bwana usiku wa siku hiyo kulinyesha mvua kubwa sana, mvua ilipokatika nikatoka nje na tochi kuzunguka nyumba yangu niangalie usalama maana sikuwa na mlinzi bali nilikuwa naishi mimi tu na mke wangu Clara ambaye ni mzungu, naye tulikutana tu hotelini miezi miwili iliyopita nikiwa kwenye safari zangu za kikazi nikamtongoza akaubali basi nikamkaribisha kwangu na mabegi yake niishi naye wakati tukiendelea kufanya mchakato wa kwenda kutambulishana kwa wazazi. Sikukagua mabegi yake kwani sisi waafrika mila zetu ni mwiko kukagua mabegi ya mgeni japo yalikuwa chumbani kwangu.
Basi bwana wakati nazunguka nyumba yangu huku nikitembeza mwanga wa tochi huku na kule ghafla nikamuona yule kichaa akiwa amekaa palepale anapopenda kukaa na alikuwa amenyeshewa na mvua vibaya mno, nikasema potelea mbali hata awe jambazi siwezi kuruhusu binadamu mwenzangu ateseke vile mimi nimelala ndani, kama anaiba aibe tu, mali hizi ni za kutafuta na tutaziacha duniani. Kwanza angekuwa jambazi asingekubali anyeshewe vile yule ni mwendawazimu" Nilijisemea nafsini mwangu na kwa huruma nikaenda kumchukua, lakini kuna kibegi chake chakavu na kilikuwa kimeloana sana aliking'ang'ania licha ya kumtaka akitupe lakini alikataa katakata, nikaona kubishana na chizi ni kujipa kazi nikamchukua vile vile na kibegi chake, nilienda kumuogesha vizuri bila kujali kwani wote ni wanaume, nilimpa nguo zangu safi avae usiku ule kisha nikamuonyesha chumba alale, aliingia chumbani na hakutaka kuachia kibegi chake nilijiuliza "Kwani hicho kibegi kina nini mbona huyu kichaa hataki kukiachia" nilijiuliza sana lakini mwisho niliona ni tabia ya vichaa kung'ang'ania vitu wanavyovipenda.
Basi nilipohakikisha yule kichaa Kalala na mimi nikarudi chumbani kwangu alipo Clara mke wangu ambapo alikuwa amelala tangu mchana, nilipoingia chumbani nikamkuta anajiandaa maana kuna baadhi ya siku alikuwa akitoka usiku kwa madai ya kwamba anaenda kumpa kampani rafiki yake wa kike kule hotelini asibaki mpweke nami sikuwa namkatalia maana huyo rafiki yake ambaye walikuwa wanakaa naye hotelini ndiye aliyeniruhusu niishi naye na hata siku nilipotoka safarini na Clara tulikuja na rafiki yake lakini yeye alifikia hoteli ya mtaa wapili na kwangu. Alidai ana mtu wake mara kwa mara anamtembelea hivyo anataka amkute hotelini na si kwa mtu.
Basi Clara alipoondoka usiku ule nikabaki na maswali kichwani mwangu." Huyu mwanamke licha ya mvua yote hii kunyesha lakini hajaona haja ya kulala hivi ni kweli huwa anaenda kwa rafiki yake? Na begi lake dogo kabeba mbona hili kubwa limetiwa kufuli kuna nini ndani yake? Mh🤔 huku kukaribisha watu usiowafahamu vizuri ndani na mabegi huku hapana?" Niliwaza kisha nikaenda kuchukua plaizi ili nivunje lile kufuli nione ndani ya begi kuna nini halafu nirudishie kufuli kitaalam maana kazi hizo niliziweza.
Basi nikahangaika na kufuli mpaka likachomoka. Nikaanza kufungua nzipu taratibu huku mikono ikinitetemeka, ile natupia macho ndani ya begi😳 ghafla moyo wangu ulipasuka paaa mithili ya ukuni mkavu baada ya kuona slaha kali za kivita ambazo toka nizaliwe sijawahi kuziona. Macho yalinitoka 😳 kama dudumizi lilikabwa na kiazi cha moto kooni, ghafla uso wote ukaloa jasho licha ya chumba changu kuwa na kiyoyozi.. haraka nika.....
Niliyenda kuchukua plaizi ili nivunje lile kufuli kwenye begi la Clara ili nione ndani ya begi kuna nini halafu nirudishie kufuli la watu kitaalam maana kazi hizo niliziweza. Basi nikahangaika na kufuli mpaka likachomoka. Nikaanza kufungua nzipu taratibu huku mikono ikinitetemeka mithili ya mtu aliyeshika kambale ambaye bado yupo hai, basi ile tu natupia macho ndani ya begi😳 ghafla moyo wangu ulipasuka paaa mithili ya ukuni mkavu baada ya kuona slaha kali za kivita ambazo toka nizaliwe sijawahi kuziona. Macho yalinitoka 😳 kama dudumizi lilikabwa na kiazi cha moto kooni, ghafla uso wote ukaloa jasho licha ya chumba changu kuwa na kiyoyozi.. haraka nikaanza taratibu za kulirudishia lile kufuli kwa utaalam zaidi lakini wakati huo mtungo wa mawazo yalikuwa yakipenyeza kichwani kwangu sio kawaida.
"Mh huyu mwanamke anafanya kazi gani, mbona ana silaha kali hivi? au ni jambazi lakini mbona ni mpole vile na sura yake imejaa utashi wa kimahaba kiasi kile, hapana pengine kuna mtu anamtumia lakini jambazi hawezi kuwa na sura tamu kiasi kile" Niliongea mwenyewe kimoyomoyo na kujijibu mwenyewe kiufupi nilikuwa nimepagawa. "Lakini pengine huyu Clara ni jambazi nisijipe moyo kwa upole wake na mapenzi anayonipa kitandani nikamuona ni mwema laaaa hasha ! Hata simba ni hatari sana lakini kwenye mapenzi anatulia kama maji mtungini, hapa nisijipe moyo Brighton nimeangukia kwenye penzi la jambazi yani nimeyakanyaga kama sio kuyatimba" nilijisemea baada ya kumaliza kurudishia kufuli kwenye lile begi.
Nikakaa kitandani kisha nikavuta pumnzi ndefu na kushusha huku mkono ukiwa shavuni kwa mawazo "Mh na huyu kichaa ni kichaa kweli au geresha, kichaa gani anakubali kuogeshwa na apewe nguo nyingine avae bila kuleta utata wowote, sasa mbona na kile kibegi chake chakavu kilichonyeshewa na mvua ameking'ang'ania? kina nini ndani yake? Mbona sura yake ni kama mzungu chotara?
Kuna kitu si bure🤔 huenda ikawa huyu kichaa ni mpelelezi maana ndio kawaida yao unalikuta jitu linajidai chizi kumbe lipo kazini usione minywele ile ukasema chizi hapana ni askari wa usalama aliambiwa afuge manywele na mandevu maana kuna kazi anatakiwa kupewa miaka miwili badae hivyo anatakiwa awe katika muonekano wa kichaa. Inawezekana kabisa na huyu ni mpelelezi, anampeleleza Clara. Jamani Bryhton mimi si nitaambiwa nashirikiana na Clara wakati sijawahi kuiba hata kuku?" Niliwaza huku moyo ukinidunda vibaya mno.
Basi usiku huo wa manane nikatoka chumbani kwangu taratibu kwa mwendo wa kinyonga, nikaenda kusimama mlangoni mwa yule kichaa na kuaikilizia, nilimsikia akkoroma hapo nikabaini Kalala, basi nikajaribu kufungua mlango ajabu mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani na funguo, kidogo nikashangaa na kujiuliza " kichaa gani anafunga mlango kwa ndani au kuna taarifa gani anaficha zisijulikane?" Hapo nikagundua yule si kichaa bali ni mtu maalum katika kitengo maalumu. Basi nikajiongeza kuchungulia ndani kupitia tobo la kuingizia funguo.
Kumbe alifunga mlango na kutoa funguo mlangoni, hapo nikasema yes acha nikachukue funguo ya ziada nifungue taratibu mlango wa huyu kichaa, nichukue kile kibegi nione ndani yake kuna nini ili kujihakikishia kwamba naishi na watu wa aina gani ndani ya nyumba yangu. Nikafanya hivyo hatimaye nikafanikiwa kuingia ndani ya chumba kile..... Jamani Nyieeee..... Nyiee acheni tu kwani baada ya kuzama ndani haraka nika.
" Mh kichaa gani anaetambua kwamba muda wa kulala mlango unatakiwa ufungwe kwa ndania? 🤔Hapana huyu si kichaa bali kuna kitu au ama taarifa anaficha zisijulikane?" Niliwaza na hapo nikagundua yule si kichaa bali ni mtu maalum katika kitengo maalumu na kujifanya kote ni kichaa si kichaa bali pale yupo kazini. Basi mimi nikajiongeza kuchungulia ndani kupitia tobo la kuingizia funguo. Kumbe alifunga mlango na kutoa funguo mlangoni, hapo nikasema yes acha nikachukue funguo ya ziada nifungue taratibu mlango wa huyu kichaa, nichukue kile kibegi nione ndani yake kuna nini ili kujihakikishia kwamba naishi na watu wa aina gani ndani ya nyumba yangu.
Nikafanya hivyo hatimaye nikafanikiwa kuingia ndani ya chumba kile, huku nikitetemeka. Mara ghafla akaacha kukoroma😳 haraka nikakichukua kile kibegi na kutoka nacho nje taratibu kisha nikasimama pale mlangoni kwa muda kidogo nikisikilizia kama ataamka ama laa, mara akaanza tena kukoroma, taratibu nikaufunga ule mlango kwa nje na funguo. Haraka nikaelekea chumbani na kile kibegi chakavu ambacho hata mtoto wa fukara hawezi kubebea madaftari maana kilichakaa mno.
Basi nilipofika chumbani nikaketi Kitandani na kukifungua kile kibegi, kwanza nilikuta mfuko wa plastick uliofungwa, hapo nikagundua mfuko ule ni kwaajili ya kuzuia mvua isiloanishe vitu vilivyopo ndani yake. Nikautoa ule mfuko nje na kuufungua, kwanza nilishangaa 😳 kukuta simu na vitabu viwili, kimoja likiwa ni cha katiba ya America. Nikaikagua ile simu ilikuwa na paswed na iliwekwa vibration, bado tomaso nikaendelea kukagua zaidi ndani ya kile kitabu cha katiba, nilikuta picha ya yule kichaa akiwa amevalia gwanda la Marekani lenye nyota tano, na alikuwa nazifu huwezi kumdhania.
Tomaso niliendelea kukagua huku mikono ikinitetemeka mithili ya mgonjwa wa degedege, nikakuta vitambulisho vingi, usalama wa Taifa na vitengo vingi ambavyo yule kichaa alipitia akiwa kama mtumishi Marekani, nikakuta pasport ya kusafiria na nakala kadhaa. "Mh Mungu wangu yani vitu vyote hivi muhimu asiwe na hata bastola ya kumlinda je akivamiwa maana vyote ni Orginal na sio copy🤔 au bastola kaitoa akaweka uvunguni? Inawezekana" Niliwaza huku nikiendelea kupekua pekua.
Na ndipo ghafla😳 nikakutana na picha ya Clara imewekewa X na kwa nyuma iliandikwa "most wanted" yani anatafutwa kwa udi na uvumba, pia nikaona karatasi inayomuelezea Clara, macho yalinikodoka 😳 huku nikisoma, looo kumbe Clara ni jambazi kuu lililoua mamia ya watu nnchini Marekani yeye na mwenzake, pia akavunja mabenki mengi na kuiba pesa nyingi lakini haitoshi akamuua mtoto wa mbunge wa jimbo la California na ndipo akamua kutoroka yeye na mwenzake na inasemekana walitoroka na silaha kali walizoziiba kwenye kambi ya jeshi la kimarekani, Dah hakika nilikosa nguvu maana ni dhahiri zile silaha kwenye begi la Clara ndizo zilizoibiwa kwenye kambi ya jeshi la kimarekani.
"Mh Bryhton mie sasa nimeingia mkenge huku kushobokea wazungu hovyo na kukaribisha watu nisiowafahamu kwa undani nyumbani kwangu sasa kumeniweka pabaya sijui nifanyaje?🤔" Niliwaza na hapo nikaamua nirudishe taratibu vitu vya yule kichaa chumbani kwake maana alionekana ni mtu hatari sana, kabla sijaamka kitandani pale nilipoketi ili nirudishe vitu vya watu mara 😳 nikamsikia akiongea kwa jazba chumbani kwake tena kwa kingereza "aaaa! Nimeibiwa aaaa hapana haiwezekani" aliongea mwenyewe huku akifungua ule mlango wa chumba chake kwa ufunguo kwani alikuwa na funguo yake tofauti na ile yangu ya ziada niliyotumia kwenda kuchukua kibegi chake ili nimpekue.
Wakati anafungua mlango wake, haraka nikakitupia kile kibegi uvunguni kwangu huku nikitetemeka mpaka meno. Mara nikamsikia akitembea kwenye korido ya kuja chumbani kwangu. Mweee! Mweee ! Mweee Nilizidi kutetemeka na kuhisi haja kubwa ghafla, mara mlango wa chumba changu ukagongwa 😳 hapo nika...
Acheni nirudi maana ingekuwa ni wewe tayari ungeshajinyea walahi?
Unajua nini kiliendelea hakikisha unapomaliza kusoma unalike na kucoment ili usipitwe na moto huu🔥🔥🔥🔥🔥
Muendelezo soma: Sikujua kichaa anayelala nje ya jengo langu ni mpelelezi anayemtafuta gaidi wa Kizungu niliyemuoa bila mimi kujua ni gaidi