Mommadou Keita
JF-Expert Member
- Oct 8, 2013
- 230
- 237
Sehemu ya 1
JINA lake kamili aliiitwa Meddie Manyara. Hii ilikuwa ni mara yake ya kwanza kukanyaga katika majengo ya Shule ya Sekondari ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Meddie alikuwa amehamia katika shule hiyo na kujiunga kidato cha nne akitokea Tabora alikokuwa akisoma katika Shule ya Sekondari ya Uyui.
Sababu kubwa ya kujiunga na shule hiyo, ilikuwa ni kukaa karibu na kaka yake, Omary Manyara ambaye alikuwa maarufu zaidi kwa watu wengi kwa jina la Ommy.
Ommy alikuwa mtoto wa kwanza wa familia ya Mzee Tuesday Manyara iliyokuwa na watoto saba, alikuwa mwajiriwa wa serikalini.
Pamoja na kufanya kazi serikalini hakukuwa ndugu yake yeyote aliyefahamu kwa ufasaha hasa kaka au ndugu yao huyo alikuwa akiifanya kazi gani. Hakuna aliyekuwa akiijua taaluma yake.
Ndugu na jamaa wengi waliridhika tu walipofahamu kaka yao, ndugu yao alikuwa akifanya kazi serikalini.
Na hata Ommy, hakupenda kuyaweka maisha yake hadharani. Alikuwa msiri sana katika mambo na mipango yake mingi. Ndugu, jamaa na marafiki walifarijika zaidi kutimiziwa shida zao bila ya kufahamu undani zaidi wa kazi yake.
Shida za maisha yao zilimhusu moja kwa moja lakini kazi yake haikuwahusu ndugu na jamaa zake, hivyo hawakutambua alikuwa akijihusisha na nini.
Uwezo wake wa kifedha ulizua maneno kwa baadhi ya watu, wengi walisema alikuwa akitumia majini kupata pesa na wengine wakidai alikuwa akitumiwa na baadhi ya viongozi wakubwa wa serikalini katika kazi zao binafsi. Baadhi ya watu walimhusisha Ommy na makundi ya Freemason.
Hata hivyo, kulikuwapo na vitu vichache vilivyowafanya watu hao washindwe kumhusisha navyo. Vitu hivyo ni biashara za kuuza madawa ya kulevya na ujambazi. vitu vilivyowafanya washindwe kumhusisha Ommy na mambo hayo ni kutokana na kumuona akiendesha au kuendeshwa katika magari yalikuwa na nembo za serikali, Adam na Hawa.
Lakini walimpa tuhuma nyingine ambazo hata mwenyewe alipozisikia zilimshangaza na kumfanya aishie kutabasamu kwa uchungu. Wapo waliodai mali zote alizokuwa akizimiliki zilikuwa za vigogo wa serikalini ambao walikuwa wakificha umiliki wao kupitia yeye.
Mbali na kufanya kazi serikalini, Ommy alikuwa na vyanzo vingine vingi vya kumuingizia mapato ya kila siku.
Alikuwa na ukwasi mkubwa kwa kumiliki nyumba kadhaa za kupangisha, hoteli na magari ya kutosha, alikuwa na magari ya biashara kwa ajili ya kukodisha katika shughuli mbalimbali.
Pia, alimiliki malori ya mizigo yaliyokuwa yakisafiri kwenda nchi za jirani. Pia, alimiliki magari kadhaa ya kifahari kwa ajili ya matumizi ya familia yake na ndugu zake. Pamoja na kumiliki nyumba na vitu vingine lakini bado Ommy alikuwa akiishi katika nyumba ya serikali maeneo ya Kichangachui, Masaki jijijni Dar es Salaam.
Kaka huyo mkubwa wa familia ya Mzee Manyara, aliendesha maisha yake na mkewe, Fetty Amma wakiwa na watoto wao wawili, mmoja akiwa shule ya msingi katika mojawapo kati ya shule za msingi mojawapo kati ya zenye umaarufu mkubwa jijini Dar es Salaam.
Mwingine akiwa bado mdogo zaidi.
Pamoja na yote, watu wengi walivutiwa na kumpenda Ommy kwa sababu alikuwa mtu wa kujichanganya katika makundi ya watu tofauti. Hakuwa na tabia ya kuwabagua watu kwa hali zao za maisha, aliwasaidia wote ndugu na marafiki kwa misaada ya aina mbalimbali. Alifanya hivyo bila ya kinyongo wala hinda.
Ni Ommy ndiye aliyewaomba wazazi wake wamruhusu Meddie ahamie Dar es Salaam kutoka Tabora ili aweze kumsaidia kwa karibu zadi katika masomo yake na baada ya kuhitimu amtafutie kibarua cha kumfanya aendeshe maisha yake.
Ommy alichukua jukumu la kumsomesha mdogo wake ili kuwasaidia wazazi wake.
***
MEDDIE tayari alishayazoea mazingira ya Shule ya Kinondoni, alipata marafiki wengi aliokuwa akisoma nao katika darasa moja kutokana na uchangumfu wake.
Mbali na wanafunzi wa darasa lake pia, Meddie alifahamiana na marafiki waliokuwa wakisoma katika madarasa mengine shuleni hapo.
Lakini kati ya marafiki zake wote, mmoja tu kati yao ndiye aliyekuwa mtu wake wa karibu zaidi kuliko wengine wote, huyu aliitwa Harry Mikael. Wawili hao walitokea kufanana kwa baadhi ya tabia na matendo yao. Na siku zote waswahili wanasema, ‘ndege wa rangi moja huruka pamoja’.
Wote walikuwa ni vijana wanaojipenda kwa kuwa unadhifu, pia muda mwingi walizungumza kuhusu michezo hususan soka, ngumi, muziki na kupenda wasichana. Katika hili la kupenda wasichana, Meddie alimwacha rafiki yake kwa umbali mrefu sana.
Hakuwa mtu aliyeweza kuficha hisia zake, mara nyingi alipenda kuwaangalia na kuweka msimamo wake kwa mwanamke aliyetokea kuvutiwa naye, hakuwa muoga.
Unaweza kusema Harry alikuwa ni muoga, kwani alikuwa akifanya mambo yake kwa taratibu sana, alikuwa akichukua muda mrefu kutafakari jambo na kulitolea au kulifanyia uamuzi.
Harry hakuwa mwepesi kutekwa na hisia za kimapenzi na alikuwa mgumu kuonyesha hisia zake kwa mapema.
Pamoja na tofauti hizo, bado ilikuwa ni vigumu kuwatenganisha wawili hao, ambao muda mwingi walikuwa pamoja hata baada ya kutoka shuleni.
Kama hawakuwa pamoja, basi kila mmoja alifahamu mwenzake alikuwa wapi wakati huo na alikuwa akifanya nini.
Hata wikiendi ambayo walikuwa hawakutani shuleni lakini walipanga mipango yao na kukutana kwa ajili ya mazungumzo katika viunga mbalimbali.
Wakati mwingine waliambatana na dereva kwenda kutanua kwenye viwanja vya burudani au kufundishwa jinsi ya kuendesha gari. Haijkuwa jambo la ajabu kuwakuta katika Ufukwe wa Bahari ya Hindi, maeneo ya Oysterbay, maarufu kama Ufukwe wa Coco.
Hiyo ndiyo sababu iliyowafanya kila alipokuwepo Meddie na Harry awepo na kila alipokuwepo Harry na Meddie alikuwapo. Na kila mmoja alifahamu siri, udhaifu na nyendo za mwenzake kwa ufasaha.
Maswahiba hao hawakufichana kitu, pamoja na Meddie kuishi Kichangachui, Masaki na Harry alikuwa akiishi Upanga. Baada ya wiki moja tangu ajiunge shuleni, Meddie aliyazoea mazingira ya shule hiyo iliyoko katika kitongoji cha Kinondoni.
Hali hiyo ilitokana na uchangamfu wake pamoja na ukaribu wake na rafiki yake aliyechukua jukumu la kumtambulisha kwa watu mbalimbali shuleni kwao.
Asubuhi moja Meddie alikuwa akiingia shuleni akiwa ndani ya gari ya kaka yake, Toyota Cresta Gx 100. Hakuwa nyuma ya usukani, bali aliketi pembeni akiendeshwa na mmoja kati ya madereva waliokuwa wakilipwa na kaka yake.
Gari lilikuwa getini kwa ajili ya kusubiri kuruhusiwa kuingia ndani ya uzio wa shule na dereva alikuwa akisubiri geti lifunguliewe. Kwa bahati nzuri macho ya Meddie yakanaswa na kitu. Tangu yaliponaswa na kitu hicho hayakuweza kujinasua na kuangalia pembeni, yalibaki katika mtego ule uliyoyanasa.
Macho yake yalivutiwa na mmoja kati ya wanafunzi wa kike aliyekuwa akiingia shuleni hapo kupitia geti la watembea kwa miguu. Macho ya Meddie hayakubanduka kutoka kwa msichana yule aliyekuwa akitembea kwa mwendo wa haraka kuwahi kuingia ndani ya shule hiyo.
Meddie alikamatwa na pumbazo la akili kadiri alivyoendelea kumwangalia mwanafunzi yule.
Hakuacha kumwangalia. Aliendelea kumwangalia hadi alipopotea kwenye upeo wa macho yake. Hata baada ya kupotea kwenye upeo wa macho yake, bado Meddie hakutosheka, aliendelea kutazama upande ule aliokuwa ameelekea msichana yule. Alikuwa akiangalia upande ule kama vile bado alikuwa akimuona yule aliyekuwa akimwangalia.
Taswira ya mwanafunzi yule wa kike ilibaki akilini mwake. Mara baada ya gari kuruhusiwa kuingia ndani ya geti, haraka Meddie alishuka na moja kwa moja alifuata uelekeo ule ambao mwanafunzi yule wa kike alikuwa ameelekea.
Tayari alikuwa ameshachelewa, aliyemfuata alishaenda zake na ingekuwa vigumu kutambua safari yake ilikuwa imeishia wapi.
***
HAKUWA na budi kurudi darasani kwake. Meddie alionekana kutawaliwa na furaha au hali ya ushawishi wa kutaka kufahamu kitu fulani. Harry alipomuona rafiki yake akiingia darasani, alihisi siku hiyo alikuwa na kitu ambacho hakikuwa cha kawaida. Meddie alionekana kutawaliwa na furaha ya kati kwa kati.
Harry alimwangalia rafiki yake hadi alipoketi karibu yake. Marafiki hao walikuwa wakikaa karibu kabisa darasani ili kurahisisha mazungumzo ya habari zao za hapa na pale. “Aisee… kuna kitu nimekiona leo hatariii….” Alisema Meddie baada ya kusalimina na jamaa yake kwa sauti ya chini, kuonesha hakutaka mtu mwingine asikie kile alichokuwa akikizungumza.
“Kitu gani…?” alinong’ona Harry huku akiachia tabasamu lenye udadisi.
“Nimemuona mtoto mkali sana… yaani kama sio malaika basi atakuwa ni malkia fulani hivi kutokana na mwonekano wake…” “Umemuona wapi?” Harry aliendelea kudadisi.
“Hapo nje, alikuwa akiingia shuleni tena ameelekea madarasa ya huku, nilijaribu kumfuatilia lakini nilikuwa nimechelewa….” alisema Meddie.
“Huku…” alisema Harry huku akionyesha mkono kule ambako Meddie alikuwa amemwelekeza.
“Ndio,” aliitikia Meddie.
“Huku kuna madarasa ya kidato cha pili na cha tatu,” Harry alifafanua.
“Basi acha tu…” Meddie hakuweza kumalizia kauli yake baada ya mwalimu kuingia darasani na wao kutakiwa kusimama na kutoa salamu kwake.
Baada ya vipindi viwili vya masomo kumalizika, marafiki hao walitoka darasani kwa ajili ya mapumziko ya saa nne, Meddie na Harry kama kawaida yao walikwenda kutafuta kifungua kinywa.
Walitoka nje kabisa ya shule wakielekea kwenye mgahawa maarufu uliopachikwa jina la Kuti Kavu, njia nzima Meddie alikuwa akizungumzia habari zilizommhusu yule msichana aliyemuona asubuhi. Harry alitamani sana kumwona ili aweze kumtambua, pamoja na sifa zote alizopewa na rafiki yake bado hazikutosha kumfanya amtambue msichana huyo.
“Nakushangaa, Harry yaani wewe umenitangulia shuleni lakini macho yako hayajamuona yule binti....? Haiwezekani,” alisema Meddie.
“Inategemea, unachokiona wewe sicho ninachokiona miye, kila mtu ana macho yake,” alijitetea Harry.
“Hata kama lakini sio kwa kiumbe kama kile, naamini, shule nzima hakuna msichana mrembo kama yule,” alisisitiza Meddie.
“Unajua Kinondoni imesheheni wasichana warembo na wa aina mbalimbali na wote ni warembo. Kuna wasichana wa Kiarabu, Kihindi na hata Maafrikasti wa kila aina, sasa siwezi kujua wewe umemuona nani?”
“Niliyemuona hakuwa Mwarabu, hakuwa Mzungu wala hakuwa Mhindi na sio shombeshombe kama unavyofikiria.
“Ni mswahili na sidhani kama kuna Mhindi, Mwarabu, Mzungu au shombe yeyote anayeweza kumfikia kwa uzuri wake…. Yule anafaa kuvikwa taji la Miss Kinondoni au kuitwa malaika kama sio malkia wa Kinondoni.”
“Sijui atakuwa ni nani huyo binti….?” Alijiuliza Harry huku akijaribu kuwafikiria baadhi ya wasichana wanaliokuwa wakisoma shuleni pale ambao waliaminika kuwa ni walimbwende haswa.
“Anaweza kuwa nani?” Harry alitafakari kwa mara nyingine akiwaza kisha akaendelea;
“…Labda anaweza kuwa Mwantumu, Jackie, Maua, Edna, Asia, Raya au Nancy kama sio Suzzie…” “Kuna majina matamu umeyataja, yanafanana na urembo wa binti yule, lakini siwezi kulijua jina lake halisi ni lipi kati ya hayo,” alisema Meddie wakati Harry alipowataja baadhi ya wasichana walioaminika na kutajwa na watu wengi kuwa ni warembo shuleni kwao.
Meddie hakujua binti yule alikuwa akimiliki jina gani kati ya majina hayo mazuri yaliyotajwa na Harry.
ITAENDELEA JUMATANO
JINA lake kamili aliiitwa Meddie Manyara. Hii ilikuwa ni mara yake ya kwanza kukanyaga katika majengo ya Shule ya Sekondari ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Meddie alikuwa amehamia katika shule hiyo na kujiunga kidato cha nne akitokea Tabora alikokuwa akisoma katika Shule ya Sekondari ya Uyui.
Sababu kubwa ya kujiunga na shule hiyo, ilikuwa ni kukaa karibu na kaka yake, Omary Manyara ambaye alikuwa maarufu zaidi kwa watu wengi kwa jina la Ommy.
Ommy alikuwa mtoto wa kwanza wa familia ya Mzee Tuesday Manyara iliyokuwa na watoto saba, alikuwa mwajiriwa wa serikalini.
Pamoja na kufanya kazi serikalini hakukuwa ndugu yake yeyote aliyefahamu kwa ufasaha hasa kaka au ndugu yao huyo alikuwa akiifanya kazi gani. Hakuna aliyekuwa akiijua taaluma yake.
Ndugu na jamaa wengi waliridhika tu walipofahamu kaka yao, ndugu yao alikuwa akifanya kazi serikalini.
Na hata Ommy, hakupenda kuyaweka maisha yake hadharani. Alikuwa msiri sana katika mambo na mipango yake mingi. Ndugu, jamaa na marafiki walifarijika zaidi kutimiziwa shida zao bila ya kufahamu undani zaidi wa kazi yake.
Shida za maisha yao zilimhusu moja kwa moja lakini kazi yake haikuwahusu ndugu na jamaa zake, hivyo hawakutambua alikuwa akijihusisha na nini.
Uwezo wake wa kifedha ulizua maneno kwa baadhi ya watu, wengi walisema alikuwa akitumia majini kupata pesa na wengine wakidai alikuwa akitumiwa na baadhi ya viongozi wakubwa wa serikalini katika kazi zao binafsi. Baadhi ya watu walimhusisha Ommy na makundi ya Freemason.
Hata hivyo, kulikuwapo na vitu vichache vilivyowafanya watu hao washindwe kumhusisha navyo. Vitu hivyo ni biashara za kuuza madawa ya kulevya na ujambazi. vitu vilivyowafanya washindwe kumhusisha Ommy na mambo hayo ni kutokana na kumuona akiendesha au kuendeshwa katika magari yalikuwa na nembo za serikali, Adam na Hawa.
Lakini walimpa tuhuma nyingine ambazo hata mwenyewe alipozisikia zilimshangaza na kumfanya aishie kutabasamu kwa uchungu. Wapo waliodai mali zote alizokuwa akizimiliki zilikuwa za vigogo wa serikalini ambao walikuwa wakificha umiliki wao kupitia yeye.
Mbali na kufanya kazi serikalini, Ommy alikuwa na vyanzo vingine vingi vya kumuingizia mapato ya kila siku.
Alikuwa na ukwasi mkubwa kwa kumiliki nyumba kadhaa za kupangisha, hoteli na magari ya kutosha, alikuwa na magari ya biashara kwa ajili ya kukodisha katika shughuli mbalimbali.
Pia, alimiliki malori ya mizigo yaliyokuwa yakisafiri kwenda nchi za jirani. Pia, alimiliki magari kadhaa ya kifahari kwa ajili ya matumizi ya familia yake na ndugu zake. Pamoja na kumiliki nyumba na vitu vingine lakini bado Ommy alikuwa akiishi katika nyumba ya serikali maeneo ya Kichangachui, Masaki jijijni Dar es Salaam.
Kaka huyo mkubwa wa familia ya Mzee Manyara, aliendesha maisha yake na mkewe, Fetty Amma wakiwa na watoto wao wawili, mmoja akiwa shule ya msingi katika mojawapo kati ya shule za msingi mojawapo kati ya zenye umaarufu mkubwa jijini Dar es Salaam.
Mwingine akiwa bado mdogo zaidi.
Pamoja na yote, watu wengi walivutiwa na kumpenda Ommy kwa sababu alikuwa mtu wa kujichanganya katika makundi ya watu tofauti. Hakuwa na tabia ya kuwabagua watu kwa hali zao za maisha, aliwasaidia wote ndugu na marafiki kwa misaada ya aina mbalimbali. Alifanya hivyo bila ya kinyongo wala hinda.
Ni Ommy ndiye aliyewaomba wazazi wake wamruhusu Meddie ahamie Dar es Salaam kutoka Tabora ili aweze kumsaidia kwa karibu zadi katika masomo yake na baada ya kuhitimu amtafutie kibarua cha kumfanya aendeshe maisha yake.
Ommy alichukua jukumu la kumsomesha mdogo wake ili kuwasaidia wazazi wake.
***
MEDDIE tayari alishayazoea mazingira ya Shule ya Kinondoni, alipata marafiki wengi aliokuwa akisoma nao katika darasa moja kutokana na uchangumfu wake.
Mbali na wanafunzi wa darasa lake pia, Meddie alifahamiana na marafiki waliokuwa wakisoma katika madarasa mengine shuleni hapo.
Lakini kati ya marafiki zake wote, mmoja tu kati yao ndiye aliyekuwa mtu wake wa karibu zaidi kuliko wengine wote, huyu aliitwa Harry Mikael. Wawili hao walitokea kufanana kwa baadhi ya tabia na matendo yao. Na siku zote waswahili wanasema, ‘ndege wa rangi moja huruka pamoja’.
Wote walikuwa ni vijana wanaojipenda kwa kuwa unadhifu, pia muda mwingi walizungumza kuhusu michezo hususan soka, ngumi, muziki na kupenda wasichana. Katika hili la kupenda wasichana, Meddie alimwacha rafiki yake kwa umbali mrefu sana.
Hakuwa mtu aliyeweza kuficha hisia zake, mara nyingi alipenda kuwaangalia na kuweka msimamo wake kwa mwanamke aliyetokea kuvutiwa naye, hakuwa muoga.
Unaweza kusema Harry alikuwa ni muoga, kwani alikuwa akifanya mambo yake kwa taratibu sana, alikuwa akichukua muda mrefu kutafakari jambo na kulitolea au kulifanyia uamuzi.
Harry hakuwa mwepesi kutekwa na hisia za kimapenzi na alikuwa mgumu kuonyesha hisia zake kwa mapema.
Pamoja na tofauti hizo, bado ilikuwa ni vigumu kuwatenganisha wawili hao, ambao muda mwingi walikuwa pamoja hata baada ya kutoka shuleni.
Kama hawakuwa pamoja, basi kila mmoja alifahamu mwenzake alikuwa wapi wakati huo na alikuwa akifanya nini.
Hata wikiendi ambayo walikuwa hawakutani shuleni lakini walipanga mipango yao na kukutana kwa ajili ya mazungumzo katika viunga mbalimbali.
Wakati mwingine waliambatana na dereva kwenda kutanua kwenye viwanja vya burudani au kufundishwa jinsi ya kuendesha gari. Haijkuwa jambo la ajabu kuwakuta katika Ufukwe wa Bahari ya Hindi, maeneo ya Oysterbay, maarufu kama Ufukwe wa Coco.
Hiyo ndiyo sababu iliyowafanya kila alipokuwepo Meddie na Harry awepo na kila alipokuwepo Harry na Meddie alikuwapo. Na kila mmoja alifahamu siri, udhaifu na nyendo za mwenzake kwa ufasaha.
Maswahiba hao hawakufichana kitu, pamoja na Meddie kuishi Kichangachui, Masaki na Harry alikuwa akiishi Upanga. Baada ya wiki moja tangu ajiunge shuleni, Meddie aliyazoea mazingira ya shule hiyo iliyoko katika kitongoji cha Kinondoni.
Hali hiyo ilitokana na uchangamfu wake pamoja na ukaribu wake na rafiki yake aliyechukua jukumu la kumtambulisha kwa watu mbalimbali shuleni kwao.
Asubuhi moja Meddie alikuwa akiingia shuleni akiwa ndani ya gari ya kaka yake, Toyota Cresta Gx 100. Hakuwa nyuma ya usukani, bali aliketi pembeni akiendeshwa na mmoja kati ya madereva waliokuwa wakilipwa na kaka yake.
Gari lilikuwa getini kwa ajili ya kusubiri kuruhusiwa kuingia ndani ya uzio wa shule na dereva alikuwa akisubiri geti lifunguliewe. Kwa bahati nzuri macho ya Meddie yakanaswa na kitu. Tangu yaliponaswa na kitu hicho hayakuweza kujinasua na kuangalia pembeni, yalibaki katika mtego ule uliyoyanasa.
Macho yake yalivutiwa na mmoja kati ya wanafunzi wa kike aliyekuwa akiingia shuleni hapo kupitia geti la watembea kwa miguu. Macho ya Meddie hayakubanduka kutoka kwa msichana yule aliyekuwa akitembea kwa mwendo wa haraka kuwahi kuingia ndani ya shule hiyo.
Meddie alikamatwa na pumbazo la akili kadiri alivyoendelea kumwangalia mwanafunzi yule.
Hakuacha kumwangalia. Aliendelea kumwangalia hadi alipopotea kwenye upeo wa macho yake. Hata baada ya kupotea kwenye upeo wa macho yake, bado Meddie hakutosheka, aliendelea kutazama upande ule aliokuwa ameelekea msichana yule. Alikuwa akiangalia upande ule kama vile bado alikuwa akimuona yule aliyekuwa akimwangalia.
Taswira ya mwanafunzi yule wa kike ilibaki akilini mwake. Mara baada ya gari kuruhusiwa kuingia ndani ya geti, haraka Meddie alishuka na moja kwa moja alifuata uelekeo ule ambao mwanafunzi yule wa kike alikuwa ameelekea.
Tayari alikuwa ameshachelewa, aliyemfuata alishaenda zake na ingekuwa vigumu kutambua safari yake ilikuwa imeishia wapi.
***
HAKUWA na budi kurudi darasani kwake. Meddie alionekana kutawaliwa na furaha au hali ya ushawishi wa kutaka kufahamu kitu fulani. Harry alipomuona rafiki yake akiingia darasani, alihisi siku hiyo alikuwa na kitu ambacho hakikuwa cha kawaida. Meddie alionekana kutawaliwa na furaha ya kati kwa kati.
Harry alimwangalia rafiki yake hadi alipoketi karibu yake. Marafiki hao walikuwa wakikaa karibu kabisa darasani ili kurahisisha mazungumzo ya habari zao za hapa na pale. “Aisee… kuna kitu nimekiona leo hatariii….” Alisema Meddie baada ya kusalimina na jamaa yake kwa sauti ya chini, kuonesha hakutaka mtu mwingine asikie kile alichokuwa akikizungumza.
“Kitu gani…?” alinong’ona Harry huku akiachia tabasamu lenye udadisi.
“Nimemuona mtoto mkali sana… yaani kama sio malaika basi atakuwa ni malkia fulani hivi kutokana na mwonekano wake…” “Umemuona wapi?” Harry aliendelea kudadisi.
“Hapo nje, alikuwa akiingia shuleni tena ameelekea madarasa ya huku, nilijaribu kumfuatilia lakini nilikuwa nimechelewa….” alisema Meddie.
“Huku…” alisema Harry huku akionyesha mkono kule ambako Meddie alikuwa amemwelekeza.
“Ndio,” aliitikia Meddie.
“Huku kuna madarasa ya kidato cha pili na cha tatu,” Harry alifafanua.
“Basi acha tu…” Meddie hakuweza kumalizia kauli yake baada ya mwalimu kuingia darasani na wao kutakiwa kusimama na kutoa salamu kwake.
Baada ya vipindi viwili vya masomo kumalizika, marafiki hao walitoka darasani kwa ajili ya mapumziko ya saa nne, Meddie na Harry kama kawaida yao walikwenda kutafuta kifungua kinywa.
Walitoka nje kabisa ya shule wakielekea kwenye mgahawa maarufu uliopachikwa jina la Kuti Kavu, njia nzima Meddie alikuwa akizungumzia habari zilizommhusu yule msichana aliyemuona asubuhi. Harry alitamani sana kumwona ili aweze kumtambua, pamoja na sifa zote alizopewa na rafiki yake bado hazikutosha kumfanya amtambue msichana huyo.
“Nakushangaa, Harry yaani wewe umenitangulia shuleni lakini macho yako hayajamuona yule binti....? Haiwezekani,” alisema Meddie.
“Inategemea, unachokiona wewe sicho ninachokiona miye, kila mtu ana macho yake,” alijitetea Harry.
“Hata kama lakini sio kwa kiumbe kama kile, naamini, shule nzima hakuna msichana mrembo kama yule,” alisisitiza Meddie.
“Unajua Kinondoni imesheheni wasichana warembo na wa aina mbalimbali na wote ni warembo. Kuna wasichana wa Kiarabu, Kihindi na hata Maafrikasti wa kila aina, sasa siwezi kujua wewe umemuona nani?”
“Niliyemuona hakuwa Mwarabu, hakuwa Mzungu wala hakuwa Mhindi na sio shombeshombe kama unavyofikiria.
“Ni mswahili na sidhani kama kuna Mhindi, Mwarabu, Mzungu au shombe yeyote anayeweza kumfikia kwa uzuri wake…. Yule anafaa kuvikwa taji la Miss Kinondoni au kuitwa malaika kama sio malkia wa Kinondoni.”
“Sijui atakuwa ni nani huyo binti….?” Alijiuliza Harry huku akijaribu kuwafikiria baadhi ya wasichana wanaliokuwa wakisoma shuleni pale ambao waliaminika kuwa ni walimbwende haswa.
“Anaweza kuwa nani?” Harry alitafakari kwa mara nyingine akiwaza kisha akaendelea;
“…Labda anaweza kuwa Mwantumu, Jackie, Maua, Edna, Asia, Raya au Nancy kama sio Suzzie…” “Kuna majina matamu umeyataja, yanafanana na urembo wa binti yule, lakini siwezi kulijua jina lake halisi ni lipi kati ya hayo,” alisema Meddie wakati Harry alipowataja baadhi ya wasichana walioaminika na kutajwa na watu wengi kuwa ni warembo shuleni kwao.
Meddie hakujua binti yule alikuwa akimiliki jina gani kati ya majina hayo mazuri yaliyotajwa na Harry.
ITAENDELEA JUMATANO