Sikuabliani na Magufuli kuhusu somo la Historia. Kama ni Uzalendo, watoto watajifunza kwenye somo la URAIA

kuna mambo ya maana ya kupewa msisitizo kwenye elimu lakini sio upumbavu HISTORIA, yaani awamu imewafanya watanzania wawe wajinga zaidi na wasiotambua wanataka nini.
Ngoja niachane na huu ujinga nienda kuangalia mechi
Mawazo kinzani ya wanasiasa hasa wapinzani Tanzania ni MFU, UPOFU, KENGEUFU na ni adui wa MAENDELEO. Hawana jema, hawathamini utamaduni uliowakuza, hawaelewi ni kwanini Ujerumani, China, Urusi ili ujifunze maarifa ya kitaaluma ni sharti ufunzwe lugha yao kwa miaka miwili kwanza? Wanaopinga mpango huu ni vilema wa kufikiri na watabaki hivi hadi mwisho wa dahari.

Mtu anayepinga anatakiwa aoneshe kile alichojifunza kwa kutumia lugha ya kigeni kimemnufaisha yeye na jamii inayomzunguka namna gani kama mfano chanya wa kuigwa.

Wapinzani hamjui nafasi yenu mhimu ya kuhamasisha mambo yenye tija kwa taifa badala yake mnatumika na mabwanyenye kupiga mayowe kuhusu haki, demokrasia na uhuru wakati hamyaishi hayo kwenye maisha yenu ya kawaida katika familia, jamii na kazini-HUFAI wewe na wenzio-Ukiulizwa hapo kuongea lugha yako ya mama utadai nimezaliwa mjini sikufunzwa.

Msisitizo ni kwamba pamoja na masomo historia, kiswahili na uraia lugha za kiingereza, kifaransa, kichina nk ziendelee kufundishwa kwa ustadi, kiufasaha kwa nia ya kuchochea fikra za uzalendo sio mawazo mgando ya kikoloni kama ya kwako. Hapo ulipo kwanza hujui kuzungumza na kuandika lugha ya kiinereza fasaha lakini unashabikia umangi meza.
 
Sasa kama mlisoma na bado yanafundishwa mbona uzalendo hakuna? Hii historia ya Chato itakuja na jipya gani?
Wewe ndio sio mzalendo ndio maana unajiita huna jinsia watu watakuelewaje kwa utambulisho huo?

Kama ulizaliwa baada ya mwaka 1990 wengi wenu ndio hamna uzalendo sio kwa nchi pekee yake lakini hata kwenye familia zenu hakuna maadili na staha.
 
Mawazo kinzani ya wanasiasa hasa wapinzani Tanzania ni MFU, UPOFU, KENGEUFU na ni adui wa MAENDELEO. Hawana jema, hawathamini utamaduni uliowakuza, hawaelewi ni kwanini Ujerumani, China, Urusi ili ujifunze maarifa ya kitaaluma ni sharti ufunzwe lugha yao kwa miaka miwili kwanza? Wanaopinga mpango huu ni vilema wa kufikiri na watabaki hivi hadi mwisho wa dahari.

Mtu anayepinga anatakiwa aoneshe kile alichojifunza kwa kutumia lugha ya kigeni kimemnufaisha yeye na jamii inayomzunguka namna gani kama mfano chanya wa kuigwa.

Wapinzani hamjui nafasi yenu mhimu ya kuhamasisha mambo yenye tija kwa taifa badala yake mnatumika na mabwanyenye kupiga mayowe kuhusu haki, demokrasia na uhuru wakati hamyaishi hayo kwenye maisha yenu ya kawaida katika familia, jamii na kazini-HUFAI wewe na wenzio-Ukiulizwa hapo kuongea lugha yako ya mama utadai nimezaliwa mjini sikufunzwa.

Msisitizo ni kwamba pamoja na masomo historia, kiswahili na uraia lugha za kiingereza, kifaransa, kichina nk ziendelee kufundishwa kwa ustadi, kiufasaha kwa nia ya kuchochea fikra za uzalendo sio mawazo mgando ya kikoloni kama ya kwako. Hapo ulipo kwanza hujui kuzungumza na kuandika lugha ya kiinereza fasaha lakini unashabikia umangi meza.
nimetoka kapa, sijaelewa ulichoandika. Mengine niweke akiba ya maneno
 
Tatizo la nchi linapokuwa halina dira ya Taifa kwa sekta zote. Rais akisema anataka hesabu ifutwe sababu haoni faida basi inafutwa !! Kuna wakati walifuta michezo mashuleni bila sababu za msingi - baada wakarusidha bila kutuambia kwa nini walifuta mara ya mwazo.

kwa hiyo wanafunzi wa High school wanaosoma HGL wajiandae kusoma Shahada yao ya kwanza ya Sheria kwa kwa lugha ya kiswahili...
 
Kwa jinsi siku hizi mijadala inavyoendeshwa huku JF haina tofauti kijiwe cha wahuni........

Kwani mtu unashindwa vipi kujibu hoja kinzani pasipo kutoa lugha chafu.......??

Iko wapi ile dhana ya jf kuwa Home of great tinker....??
 
Lengo kubwa la somo la historia ni kumfanya mwanadamu ajifunze yaliyopita ulimwenguni kote (siyo Tanzania tu) na hivyo kumwepusha kurudia makosa ya huko nyuma. Na wala siyo kufundisha uzalendo.

BTW, nani kamdanganya JPM kuwa uzalendo unafundishwa darasani? Uzalendo maana yake ni upendo wa raia yeyote kwa nchi yake?

Sasa nani amewahi kufundishwa kupenda kitu, mtu(mke/mume/dada/kaka/baba/mama) au nchi? Upendo kwa nchi ni zao la Uhuru, Haki na usawa kwa raia.


Sasa kama hata haki ya kuchagua na kuchaguliwa inaporwa nani ataipenda nchi hii? Kama watu wanalalamika kuhusu ajira, mishahara duni masoko ya mazao hakuna, biashara zinakufa, Uhuru wa kujieleza unabinywa nani ataipenda Tanzania?

Kwahiyo hapa ninaona JPM ana nia ya kutaka jina lake liandikwe kwenye vitabu vya historia, awe anasomwa kama msukuma wa kwanza kuwa rais.

Ndiyo hicho tu anachokitafuta JPM hakuna kingine. Kutafuta sifa tu ndiyo kuna msumbua. Ningemwelewa kama angeshauri uzalendo utiliwe mkazo kwenye somo la uraia.
Hivi hili agizo linaambatana pia na zuio la kufundishwa histroria nyingine yoyote ile tofuti na ile ya Tanzania pekee?
 
Hapa naamua kuwa OBJECTIVE, somo la history ndilo linalompa mtu "sprit of Patriotism "

Hiyo ni moja ya OBJECTIVE ya somo la HISTORIA.
Mathalani Kitendo cha MKWAWA,BWANA HERI,ABUSHIRI ,YUSUPH BIN OMARY MAKUNGANYA,KINJEKETILE, Kuupinga utawala wakoloni kwa kuchukua silaha.

Wanafunzi wansposoma ,wanahamasika kabisa ,wanakuwa inspired kuipigania nchi, kuipenda wakitumia mfano mzuri wa hao mashujaa waafrikawaloishi miaka ya 1880's

Mh Rais kama kazungumzia kuwa somo la history linawajenga watu kuwa wazalendo YUPO SAHIHI asilimia 100%.

Kuhusu Civics somo la Uraia kiasi kikubwa linabase kwenye haki za Raia na wajibu.

MIMI NI MWALIMU MTAALAMU WA MASOMO HAYO MAWILI.

2018 nilifaulisha civics na darasa langu lilikiwa 20 kitaifa,2019 History tena 20 kitaifa.

Nimetoa maoni kama Mtaalamu mbobezi katika masomo hayo.

Katika kauli ya Rais yupo sahihi 100% tusiwe tunampinga kwa kila kitu,mambo mengine tuwe OBJECTIVE.

UKANA SHILUNGO.🙏🙏🙏

Yes, your President is right 100%...

Nionavyo mimi ni hiki, kuwa, mleta mada na wewe kuna point mnai - miss...

Kwamba, ishu siyo kukubaliana au kutokukubaliana kufundishwa somo la Historia ya Tanzania kwa sababu inafundishwa hadi sasa...

Chukua mtaala na muhitasari wa somo la Uraia (Civics) Shule za Sekondari. Kidato cha kwanza kuna mada ya "OUR NATION" ikieleza historia ya Taifa letu (Tanzania) kwa undani na ufasaha sana...

Mwanafunzi huyu huyu akiingia kidato cha II atakutana na mada inayokazia mambo haya haya (historia ya Tanzania) ktk mada ya "OUR GOVERNMENT" ambamo ndani yake atafundishwa mpaka UNION OF TANGANYIKA & ZANZIBAR na sababu za muungano huo..

Haishii hapo tu, bali atafundishwa mpaka KATIBA YA TANZANIA sura kwa sura na ibara kwa ibara pamoja na HUMAN RIGHTS na DEMOCRACY kwa ujumla. Swali la kujiuliza la watu kutokuwa wazalendo ni kwa sbb wanafunzi hawafundishwi somo la Uraia kwa Kiswahili au ni nini...?

Mimi nadhani maswali ambayo ningependa tuyajibu wote katika mjadala huu ni haya mawili au matatu;

1. Kama ishu ni HISTORIA YA TANZANIA tayari inafundishwa kwa ukamilifu wake ktk masomo ya Historia yenyewe, Uraia/Siasa na Maarifa ya Jamii. Sasa kwanini, hiki kinachodhaniwa ni tatizo la Uzalendo miongoni mwa Watanzania, lipo pamoja na kufundishwa historia yao...?

2. Je, tunadhani tatizo ni historia hii kufundishwa kwa Kiingereza badala ya Kiswahili kiasi cha kuanzisha somo la Historia ya Tanzania kwa Kiswahili na kudhani hilo ndilo litakuwa suluhisho..?

3. Kwa maoni yangu, tatizo la nchi yetu si watu kutokuwa wazalendo kwa nchi yao. Ni tatizo la tafsiri ya "UZALENDO" kutofautiana kwa wanavyoelewa viongozi na vile wanavyoelewa wananchi wanaowaongozwa na viongozi hawa...

Hapa ndipo ilipo shida na mikwaruzano yote hii ya tofauti ya kimitizamo kati ya tabaka la watawala (viongozi) na watawaliwa (wananchi)...

Viongozi wetu hawa wa kuchaguliwa tafsiri ya "uzalendo" kwao ni wananchi kuwapenda viongozi wao bila kujali chochote. Kutofanya hivyo, kwao wananchi hao wanakuwa hawana uzalendo na lazima itafutwe namna kuwafanya wawe wazalendo...

WAKATI;

Sisi wananchi tunaamini kuwa, maana na tafsiri ya "UZALENDO" ni mtu kuipenda nchi yake na kuwa tayari hata kuifia. Na hii kiuhalisia ndilo lipo ndani ya mioyo ya wananchi karibu wote wa nchi hii...

Wanachofanya viongozi wetu hawa kwa sasa akiwemo Rais Magufuli mwenyewe ni kujaribu kuitoa mbegu hii ndani ya mioyo ya watu na kupanda mbegu nyingine ya wananchi kutukuza na kupenda viongozi wao badala ya nchi na kwamba hiyo ndiyo iwe maana na tafsiri mpya ya "UZALENDO"...

Huu ndiyo msukumo uliopo nyuma ya hiki kinachoendelea na kinachotaka kufanyika sasa kuanzishwa kwa kinachoitwa somo jipya la HISTORIA YA TANZANIA eti kufundisha watu UZALENDO...

Lakini ukweli ni kuwa kuna watu wanataka kuandikwa na majina yao yatumike kutajwa huko mashuleni. Nothing more, Nothing less...
 
Hapa naamua kuwa OBJECTIVE, somo la history ndilo linalompa mtu "sprit of Patriotism "

Hiyo ni moja ya OBJECTIVE ya somo la HISTORIA.

Mathalani Kitendo cha MKWAWA, BWANA HERI, ABUSHIRI, YUSUPH BIN OMARY MAKUNGANYA, KINJEKETILE, Kuupinga utawala wakoloni kwa kuchukua silaha.

Wanafunzi wansposoma, wanahamasika kabisa, wanakuwa inspired kuipigania nchi, kuipenda wakitumia mfano mzuri wa hao mashujaa Waafrika waloishi miaka ya 1880's

Mh Rais kama kazungumzia kuwa somo la history linawajenga watu kuwa wazalendo YUPO SAHIHI asilimia 100%.

Kuhusu Civics somo la Uraia kiasi kikubwa linabase kwenye haki za Raia na wajibu.

MIMI NI MWALIMU MTAALAMU WA MASOMO HAYO MAWILI.

2018 nilifaulisha civics na darasa langu lilikiwa 20 kitaifa, 2019 History tena 20 kitaifa.

Nimetoa maoni kama Mtaalamu mbobezi katika masomo hayo.

Katika kauli ya Rais yupo sahihi 100% tusiwe tunampinga kwa kila kitu, mambo mengine tuwe OBJECTIVE.

UKANA SHILUNGO.🙏🙏
Mathalani Kitendo cha MKWAWA, BWANA HERI, ABUSHIRI, YUSUPH BIN OMARY MAKUNGANYA, KINJEKETILE, Kuupinga utawala wakoloni kwa kuchukua silaha. Hawa uliowatumia kama mfano wao walijifunza uzalendo kupitia historia ipi.
 
Lengo kubwa la somo la historia ni kumfanya mwanadamu ajifunze yaliyopita ulimwenguni kote (siyo Tanzania tu) na hivyo kumwepusha kurudia makosa ya huko nyuma. Na wala siyo kufundisha uzalendo.

BTW, nani kamdanganya JPM kuwa uzalendo unafundishwa darasani? Uzalendo maana yake ni upendo wa raia yeyote kwa nchi yake?

Sasa nani amewahi kufundishwa kupenda kitu, mtu(mke/mume/dada/kaka/baba/mama) au nchi? Upendo kwa nchi ni zao la Uhuru, Haki na usawa kwa raia.

Sasa kama hata haki ya kuchagua na kuchaguliwa inaporwa nani ataipenda nchi hii? Kama watu wanalalamika kuhusu ajira, mishahara duni masoko ya mazao hakuna, biashara zinakufa, Uhuru wa kujieleza unabinywa nani ataipenda Tanzania?

Kwahiyo hapa ninaona JPM ana nia ya kutaka jina lake liandikwe kwenye vitabu vya historia, awe anasomwa kama msukuma wa kwanza kuwa rais.

Ndiyo hicho tu anachokitafuta JPM hakuna kingine. Kutafuta sifa tu ndiyo kuna msumbua. Ningemwelewa kama angeshauri uzalendo utiliwe mkazo kwenye somo la uraia.
Acha wahangaike. Hakuna mzalendo wakati hajui kesho yake. Uzalendo haujengwi kwa historia ya nchi.
Bali uzalendo hujengwa na haki ,usawa , furaha, na uhuru katika Taifa.
 
Hapo nadhani tatizo lilikuwa mtihani... tafakari
80% kupata F haina maana watoto na waalimu wao nchi nzima walikuwa wajinga kiasi hicho. Naamini wachambuzi wa maswali walifanya marekebisho mabovu.
Navyo fahamu mitihani ya taifa hutokana na uchambuzi wa maswali yanayoletwa kwenye baraza la mitihani na waalimu wabobezi toka shule bora kisha hufanyika marekebisho kidogo kuyafanya yawe fikirishi... Na hapo ndio tatizo hutokea.

Yanaweza kuwa fikirishi mpaka yakawapoteza watoto wasijue swali linawataka wajibu kipi.
Sawa. Mwaka jana na mwaka juzi ikikuwaje kwa somo hilohilo?

Na wewe unaona kupaumbele chetu kwa sasa iwe somo la "Historia ya Tanzania" kunzia darasa 1 hadi form six? Kweli? Nchi ni yetu, Rais ni wetu na tunampenda.....lakini tuseme ukweli (kuwa honest sio dhambi).
 
Hapa naamua kuwa OBJECTIVE, somo la history ndilo linalompa mtu "sprit of Patriotism "

Hiyo ni moja ya OBJECTIVE ya somo la HISTORIA.

Mathalani Kitendo cha MKWAWA, BWANA HERI, ABUSHIRI, YUSUPH BIN OMARY MAKUNGANYA, KINJEKETILE, Kuupinga utawala wakoloni kwa kuchukua silaha.

Wanafunzi wansposoma, wanahamasika kabisa, wanakuwa inspired kuipigania nchi, kuipenda wakitumia mfano mzuri wa hao mashujaa Waafrika waloishi miaka ya 1880's

Mh Rais kama kazungumzia kuwa somo la history linawajenga watu kuwa wazalendo YUPO SAHIHI asilimia 100%.

Kuhusu Civics somo la Uraia kiasi kikubwa linabase kwenye haki za Raia na wajibu.

MIMI NI MWALIMU MTAALAMU WA MASOMO HAYO MAWILI.

2018 nilifaulisha civics na darasa langu lilikiwa 20 kitaifa, 2019 History tena 20 kitaifa.

Nimetoa maoni kama Mtaalamu mbobezi katika masomo hayo.

Katika kauli ya Rais yupo sahihi 100% tusiwe tunampinga kwa kila kitu, mambo mengine tuwe OBJECTIVE.

UKANA SHILUNGO.🙏🙏
Kama wewe ni Mwalimu basi....utakua unafundisha Tuition mkuu.
Yaani unasema Civics inaongelea Haki za Binadamu zaidi ...daah nimecheka kweli
 
Kama wewe ni Mwalimu basi....utakua unafundisha Tuition mkuu.
Yaani unasema Civics inaongelea Haki za Binadamu zaidi ...daah nimecheka kweli
Hawa ndiyo unakuta muda wote wanashangilia kila kinachosemwa. Ukitafuta sabb hupati. Kumbe ni uwezo wao wa kuelewa na kupambanua mambo mdogo sana.
 
Hawa ndiyo unakuta muda wote wanashangilia kila kinachosemwa. Ukitafuta sabb hupati. Kumbe ni uwezo wao wa kuelewa na kupambanua mambo mdogo sana.
Yaani acha mkuu...topic kama Our Nation,Responsible Citizen,Life Skills ,Government, Family,Culture etc asmilia kubwa zinamjenga mtoto kuipenda nchi yake. Lakini tufaham kua madikteta wengi wanakua na hulka ya hivyo ya kuwaona watu wengine kua sio wazalendo bali wao ndiyo wazalendo sana.Wanaweza ata kubadili au kufuta masomo au kupiga marufuku vitabu au masomo flani eg Hitler
 
Kama wewe ni Mwalimu basi....utakua unafundisha Tuition mkuu.
Yaani unasema Civics inaongelea Haki za Binadamu zaidi ...daah nimecheka kweli
Wewe ni BONGOLALA KWEL.

, KWA KUKUSAIDIA ,HIYO NI SIMPLE DEFINITION YA CIVICS,inadeal na HAKI ZA RAIA NA WAJIBU ZA RAIA.


Ni aibu hujui maana na Longo la CIVICS.

SHAME ON YOU DUDE!!

By the way WANAWAKE WENGI WANAWAZA KAMA UNAVYOWAZA MWANAMKE WEWE. 🤨🤨😃😃😃🤣🤣🤣
 
Mathalani Kitendo cha MKWAWA, BWANA HERI, ABUSHIRI, YUSUPH BIN OMARY MAKUNGANYA, KINJEKETILE, Kuupinga utawala wakoloni kwa kuchukua silaha. Hawa uliowatumia kama mfano wao walijifunza uzalendo kupitia historia
Bongolala, ni sawasawa na wewe kuuliza YAI NA KUKU KIPI CHA KWANZA? AU YAI ALITAGA NANI??

Narrow minded person, ubongo wa "INZI,MENDE"

🤣🤣🤣🤨🤨🤨😶😶😂😂😃🤣😃🤣
 
Yes, your President is right 100%...

Nionavyo mimi ni hiki, kuwa, mleta mada na wewe kuna point mnai - miss...

Kwamba, ishu siyo kukubaliana au kutokukubaliana kufundishwa somo la Historia ya Tanzania kwa sababu inafundishwa hadi sasa...

Chukua mtaala na muhitasari wa somo la Uraia (Civics) Shule za Sekondari. Kidato cha kwanza kuna mada ya "OUR NATION" ikieleza historia ya Taifa letu (Tanzania) kwa undani na ufasaha sana...

Mwanafunzi huyu huyu akiingia kidato cha II atakutana na mada inayokazia mambo haya haya (historia ya Tanzania) ktk mada ya "OUR GOVERNMENT" ambamo ndani yake atafundishwa mpaka UNION OF TANGANYIKA & ZANZIBAR na sababu za muungano huo..

Haishii hapo tu, bali atafundishwa mpaka KATIBA YA TANZANIA sura kwa sura na ibara kwa ibara pamoja na HUMAN RIGHTS na DEMOCRACY kwa ujumla. Swali la kujiuliza la watu kutokuwa wazalendo ni kwa sbb wanafunzi hawafundishwi somo la Uraia kwa Kiswahili au ni nini...?

Mimi nadhani maswali ambayo ningependa tuyajibu wote katika mjadala huu ni haya mawili au matatu;

1. Kama ishu ni HISTORIA YA TANZANIA tayari inafundishwa kwa ukamilifu wake ktk masomo ya Historia yenyewe, Uraia/Siasa na Maarifa ya Jamii. Sasa kwanini, hiki kinachodhaniwa ni tatizo la Uzalendo miongoni mwa Watanzania, lipo pamoja na kufundishwa historia yao...?

2. Je, tunadhani tatizo ni historia hii kufundishwa kwa Kiingereza badala ya Kiswahili kiasi cha kuanzisha somo la Historia ya Tanzania kwa Kiswahili na kudhani hilo ndilo litakuwa suluhisho..?

3. Kwa maoni yangu, tatizo la nchi yetu si watu kutokuwa wazalendo kwa nchi yao. Ni tatizo la tafsiri ya "UZALENDO" kutofautiana kwa wanavyoelewa viongozi na vile wanavyoelewa wananchi wanaowaongozwa na viongozi hawa...

Hapa ndipo ilipo shida na mikwaruzano yote hii ya tofauti ya kimitizamo kati ya tabaka la watawala (viongozi) na watawaliwa (wananchi)...

Viongozi wetu hawa wa kuchaguliwa tafsiri ya "uzalendo" kwao ni wananchi kuwapenda viongozi wao bila kujali chochote. Kutofanya hivyo, kwao wananchi hao wanakuwa hawana uzalendo na lazima itafutwe namna kuwafanya wawe wazalendo...

WAKATI;

Sisi wananchi tunaamini kuwa, maana na tafsiri ya "UZALENDO" ni mtu kuipenda nchi yake na kuwa tayari hata kuifia. Na hii kiuhalisia ndilo lipo ndani ya mioyo ya wananchi karibu wote wa nchi hii...

Wanachofanya viongozi wetu hawa kwa sasa akiwemo Rais Magufuli mwenyewe ni kujaribu kuitoa mbegu hii ndani ya mioyo ya watu na kupanda mbegu nyingine ya wananchi kutukuza na kupenda viongozi wao badala ya nchi na kwamba hiyo ndiyo iwe maana na tafsiri mpya ya "UZALENDO"...

Huu ndiyo msukumo uliopo nyuma ya hiki kinachoendelea na kinachotaka kufanyika sasa kuanzishwa kwa kinachoitwa somo jipya la HISTORIA YA TANZANIA eti kufundisha watu UZALENDO...

Lakini ukweli ni kuwa kuna watu wanataka kuandikwa na majina yao yatumike kutajwa huko mashuleni. Nothing more, Nothing less...
Aksante mkuu, umejibu law weledi wa hali ya juu mno. 🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom