Alwatan kamba
Member
- Nov 16, 2020
- 70
- 236
Tumekuwa tukipiga kelele kuhusu matatizo yaliyopo kwenye mfumo wetu wa elimu. Miongoni mwa matatizo hayo ni pamoja na mitaala inayotumika kutowapa wanafunzi maarifa na uwezo wa kujitegemea baada ya kumaliza masomo yao.
Cha kushangaza badala ya kuumiza vichwa kutafuta suluhu ya haya matatizo tunaongeza tena matatizo mengine kwa kuwarundikia wanafunzi mzigo wa somo la historia ya tanzania ambalo sina uhakika kama lina manufaa yoyote kwa wanafunzi katika maisha ya kawaida.
Leo mwanafunzi wa kidato cha sita anayesoma mchepuo wa PCB, PCM, PGM, CBG, CBA,ECA unamwongezea somo la historia la nini kama sio kumtwisha mzigo tu?
Kama inshu ni historia ya tanzania, wanafunzi mpaka sasa wanaisoma katika maarifa ya jamii, uraia na historia, kuna haja gani tena ya kulifanya kuwa somo?. Kwanini lisifundishwe tu kama mada 'topic' inayojitegemea ndani ya masomo mengine kama vile history au maarifa ya jamii?
Labda ni kipya gani kitaongezewa kwenye hilo somo la historia ya Tanzania?. Hivi kuna mwanafunzi anayemaliza darasa la saba asiyejua chimbuko la Tanzania kuwa ni muunganiko wa nchi mbili za Tanganyika na zanzibar?
Au kuna ajenda iliyojificha ambayo hatuijui katika hilo somo la historia ya Tanzania?
Mimi kwa mawazo yangu naona badala ya kuwaongezea wanafunzi vitu ambavyo havina tija ni bora serikali kupitia wizara ya elimu ingetumia huu muda kufumua mitaala ya elimu iliyopo na kuunda mipya itakayowezesha wanafunzi kufundishwa elimu ya vitendo na stadi za kazi ili kuwajengea uwezo wa kujitegemea katika mazingira ya sasa.
Nawasilisha.
Tusisahau kauli mbiu ya sera ya elimu inasema Elimu bora na yenye tija kwa maendeleo ya Taifa inawezekana, wote tutekeleze wajibu wetu.
Cha kushangaza badala ya kuumiza vichwa kutafuta suluhu ya haya matatizo tunaongeza tena matatizo mengine kwa kuwarundikia wanafunzi mzigo wa somo la historia ya tanzania ambalo sina uhakika kama lina manufaa yoyote kwa wanafunzi katika maisha ya kawaida.
Leo mwanafunzi wa kidato cha sita anayesoma mchepuo wa PCB, PCM, PGM, CBG, CBA,ECA unamwongezea somo la historia la nini kama sio kumtwisha mzigo tu?
Kama inshu ni historia ya tanzania, wanafunzi mpaka sasa wanaisoma katika maarifa ya jamii, uraia na historia, kuna haja gani tena ya kulifanya kuwa somo?. Kwanini lisifundishwe tu kama mada 'topic' inayojitegemea ndani ya masomo mengine kama vile history au maarifa ya jamii?
Labda ni kipya gani kitaongezewa kwenye hilo somo la historia ya Tanzania?. Hivi kuna mwanafunzi anayemaliza darasa la saba asiyejua chimbuko la Tanzania kuwa ni muunganiko wa nchi mbili za Tanganyika na zanzibar?
Au kuna ajenda iliyojificha ambayo hatuijui katika hilo somo la historia ya Tanzania?
Mimi kwa mawazo yangu naona badala ya kuwaongezea wanafunzi vitu ambavyo havina tija ni bora serikali kupitia wizara ya elimu ingetumia huu muda kufumua mitaala ya elimu iliyopo na kuunda mipya itakayowezesha wanafunzi kufundishwa elimu ya vitendo na stadi za kazi ili kuwajengea uwezo wa kujitegemea katika mazingira ya sasa.
Nawasilisha.
Tusisahau kauli mbiu ya sera ya elimu inasema Elimu bora na yenye tija kwa maendeleo ya Taifa inawezekana, wote tutekeleze wajibu wetu.