Wakuu, wale manaotetea uzembe kwa hali na mali hebu jioneeni jinsi uzembe wa walimu unavyoenea kutoka ngazi ya Kata hadi ngazi ya Taifa. Yafuatayo ni baadhi ya maswali yaliyochukuliwa kutoka paper ya mtihani wa chemistry (CSEE) wa mwaka 2016. Tazama jinsi mitihani inavyotungwa kwa kiingereza kibovu na cha kuungaunga. Inasikitisha sana paper moja tu, tena ya mtihani wa kitaifa, inakuwa na makosa mengi kiasi hiki! Prof Ndalichako huwa anajidai kuwa anajua saaana wakati wizara inamshinda kuendesha. Hv anakuwa wapi wakati watumishi hawa waliopo chini ya usimamizi wake wanapoandika kiingereza cha ovyo kama hiki huku akifahamu kwamba hii ni paper ya kitaifa?
Kwa sababu hii, nadhani kuna haja ya kuufanyia marejeo mfumo wetu wa elimu vinginevyo wimbi la vilaza (wanafunzi, walimu, wakufunzi, wahadhiri, nk) litaendelea kutamalaki katika nchi hii huku wakitetewa na vilaza wenzao (na wengine wamo humu
JamiiForums kwa gharama ya upotofu wa kielimu kwa watoto wetu.
View attachment 468495
View attachment 468497