Sikia maajabu haya ya Mwalimu wa shule ya Kata

Sikia maajabu haya ya Mwalimu wa shule ya Kata

Acha wivu dogo hebu sema ticha alitakiwa aulizeje hapo. Alafu ushasema shule ya kata mshahara anaolipwa unatosha kuwafundisha hivyo ukitaka wafundishwe vizuri kamuongezee mshahara
 
Jamaa alishakuja hapa na story ya kwenda kumtembelea jamaa yake chuo kikuu akakuta watu wanaangalia porno akaponda eti badala ya kusoma wanaangalia mambo yetu.

Sasa na hii ya huyu ticha kisa amemaliza chuo kikuu kakosea ngeli jamaa anachonga.

Ninahisi jamaa kinamuuma sana kushindwa kwenda chuo kikuu ndo maana kila mara anakuwa anawatafutia kasoro watu qa chuo kikuu.

Hii lugha sio yetu, ukimsikiliza rais wa nchi mwenyewe gramar zinanchomoa pamoja na kuwa amesoma, amekaa wizara ya mambo ya nje, ulaya na US anaenda kama vile mimi navyoenda Ubungo Posta na ni Rais lakini bado ngeli ni shida.
Mbona sasa unatudanganya? Raisi Samia anaongea kiingereza kilichonyooka,labda wewe ndo Huwa unaongea broken.
 
Msingi wa mwalimu ndiyo tatizo.Anyway ndo mazao yenyewe hayo.
 
Achilia mbali makosa ktk kizungu chake... kwangu mimi ata angetumia vitendo tu bila kuongea lugha yoyote endapo walengwa wakamuelewa Lengo linakua lishatimia
 
Leo nimetembelea shule moja ya Kata nikashuhudia kituko cha mwaka kutoka kwa mwalimu mmoja shuleni hapo.

Mwalimu huyo amehitimu Chuo Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) hivi karibuni na akaajiriwa moja kwa moja kufundisha katika shule hiyo ya Kata.

Wakati akiendelea kufundisha nilimsikia akiwauliza wanafunzi swali hili: WHERE DOES IT LOCATED?

Inaonekana ni mwalimu wa somo la Jiographia, hivyo alikuwa akiwauliza wanafunzi wake wamtajie location ya kitu fulani kwenye ramani.

Jamani, hapa ndipo shule za kata zilipotufikisha. Ikiwa mhitimu wa Chuo Kikuu anaongea kiingereza kibovu kama hiki, tena mbele ya wanafunzi,mnategemea wanafunzi anaowafundisha watapata maarifa gani kutoka kwake?

Chukulia huyu ni mwalimu wa Kidato Cha Kwanza, wanafunzi wake wanaoambiwa kila siku "SPEAK ENGLISH" wataiga kiingereza gani kutoka kwake? Si ndio atawapoteza kabisa?

Ikiwa walimu hawajui kiingereza unategemea nini kutoka kwa wanafunzi wao? Haya ndio madhara ya serikali yetu kuchanganya elimu na siasa. Tumekwisha hasa!!
Dah
Kipimo ni kimombo?

Basi sawa
 
Msingi wa mwalimu ndiyo tatizo.Anyway ndo mazao yenyewe hayo.
CCM na hizi shule zake za kata zisizo na walimu weledi ndio wametufikisha hapa.
 
Suppose to be "where is it located" but who cares mzee english sio lugha yetu ebu tuwe wazalendo kwenye hili, ujuzi wa mtu hauusiani na kuwa grammatical vizuri. Mfano english inayozungumzwa USA ilileta utata mwingi mpaka wakatengenezewa dictionaries zao na hawafuati British english sasa wewe endelea kuwa mtumwa kenge maji wewe..
 
Hebu fikiria hata paper ya NECTA inayopitiwa na wataalamu wengi kabla ya kuwa published inakuwa na makosa ya kipuuzi kama haya? Unategemea nini? Nchi ngumu sana hii.
1691768850255.png
 
CCM na hizi shule zake za kata zisizo na walimu weledi ndio wametufikisha hapa.
Kwani nI mwalimu wa english huyo?? Acha ujinga bwana..kuna professors kibao wa kihindi wanafundisha vyuo vikoo vikubwa duniani na wanazungumza english mbovu kuliko. English ni lugha kama kilivyo kichaga au kisukuma tu acha ushamba.
 
Suppose to be "where is it located" but who cares mzee english sio lugha yetu ebu tuwe wazalendo kwenye hili, ujuzi wa mtu hauusiani na kuwa grammatical vizuri. Mfano english inayozungumzwa USA ilileta utata mwingi mpaka wakatengenezewa dictionaries zao na hawafuati British english sasa wewe endelea kuwa mtumwa kenge maji wewe..
Correct✔️✅✔️✅✔️✅✍️
 
Kwani nI mwalimu wa english huyo?? Acha ujinga bwana..kuna professors kibao wa kihindi wanafundisha vyuo vikoo vikubwa duniani na wanazungumza english mbovu kuliko. English ni lugha kama kilivyo kichaga au kisukuma tu acha ushamba.
Kwa kuwa sio mwalimu wa English anaruhusiwa kuongea broken kuwapotosha wanafunzi? Acha ujinga mkuu.
 
Kwa kuwa sio mwalimu wa English anaruhusiwa kuongea broken anawapotosha wanafunzi? Acha ujinga mkuu.
Je hakutumia lugha ya vitendo?? Je wanafunzi hawakuelewa??hayo nayo tungetamani kuyajua
 
Mimi SUA pia nilisikia Kingereza cha ajabu namna hiyo.Inaelekea ndio hali halisi ya vyuo vyetu kwa sasa.Very pathetic indeed.
Hebu fikiria hata paper ya kitaifa (2016)inakosewa kijinga namna hii unategemea nini? Halafu kuna vilaza humu wanawatetea vilaza wenzao. Hii nchi ya kipuuzi sana.
1691769441523.png
 
Mimi SUA pia nilisikia Kingereza cha ajabu namna hiyo.Inaelekea ndio hali halisi ya vyuo vyetu kwa sasa.Very pathetic indeed.
Kuna lecturer mmoja kutoka UDOM alinishangaza sana pale niliposoma questionnaire aliyoiandaa kwa wanafunzi wake. Inasikitisha sana.
 
Mbona sasa unatudanganya? Raisi Samia anaongea kiingereza kilichonyooka,labda wewe ndo Huwa unaongea broken.
Hahahaha! Mkuu umekurupuka. Mtoa mada anamuongelea JK sio chifu Hangaya. Tazama tarehe ya uzi hapo juu 😀 😀 😀 😀 😀 😀
 
Je hakutumia lugha ya vitendo?? Je wanafunzi hawakuelewa??hayo nayo tungetamani kuyajua
Aliwapotosha wanafunzi kwa makusudi au kwa kutokujua. Usitetee uzembe mkuu. Kwanini asiingie darasani na dictionary kama kingereza kinampiga chenga? Au kwanini asiende kusoma English Course kwa Ras Simba?
 
Back
Top Bottom