Siasa za Mbeya 2005-2010

Siasa za Mbeya 2005-2010

Hivi ni mikoa gani ya Kaskazini ambayo ina maendeleo kuliko Mbeya ukiachia Kilimanjaro?

Mnyika, mbona hukupita kule kwa prof. Mwandosya?

Binafsi ningependa kuona CHADEMA wakitumia hata nusu ya muda wao kuongelea sera zao badala ya kutumia asilimia 100 kuiongelea CCM.

Ukifika uchaguzi, CCM itawatema mafisadi hata 20 na kujifanya kimesikiliza maoni ya wananchi. Inatakiwa kuwashinda CCM hata kwa sera za maendeleo ikiwa ni pamoja na kuonyesha kwamba wilaya ambazo zinaongozwa na wao zina nafuu kimaendeleo kuliko hozo za CCM.
 
Heshima mbele wakuu,tunapozungumzia siasa za Mbeya naomba pia tuzungumzie na wailaya nyingine mbili za ILEJE na CHUNYA(ina majimbo mawili ya uchaguzi ya Lupa na Songwe),binafsi nasikitishwa mno na jinsi wilaya ya Chunya ilivyo kuwa nyuma kimaendeleo licha ya kuwa ina vyanzo vingi tu vya mapato katika nyanja za MADINI(dhahabu),KILIMO(pamba,tumbaku,alizeti na hata mpunga) na UVUVI(kupitia ziwa Rukwa)..Pamoja na yote haya wilaya ya Chunya imezidi kudidimia kimaendeleo,barabara ni mbovu(hasa zinzounganisha wilaya na mkoani za Chunya mjini Mbeya via Kawetere na ile ya Mkwajuni-Mbalizi),hivi tatizo ni nini hasa jamani??????
 
Heshima mbele wakuu,tunapozungumzia siasa za Mbeya naomba pia tuzungumzie na wailaya nyingine mbili za ILEJE na CHUNYA(ina majimbo mawili ya uchaguzi ya Lupa na Songwe),binafsi nasikitishwa mno na jinsi wilaya ya Chunya ilivyo kuwa nyuma kimaendeleo licha ya kuwa ina vyanzo vingi tu vya mapato katika nyanja za MADINI(dhahabu),KILIMO(pamba,tumbaku,alizeti na hata mpunga) na UVUVI(kupitia ziwa Rukwa)..Pamoja na yote haya wilaya ya Chunya imezidi kudidimia kimaendeleo,barabara ni mbovu(hasa zinzounganisha wilaya na mkoani za Chunya mjini Mbeya via Kawetere na ile ya Mkwajuni-Mbalizi),hivi tatizo ni nini hasa jamani??????

Balantanda,

Bahati mbaya mimi siifahamu vizuri Chunya zaidi ya kusikia kuhusu utajiri wa dhahabu. Kuna baadhi ya vijana walikuwa wanatoka kule kwetu kwenda kuchimba dhahabu Chunya, wakirudi wasichana wote wa maana wilayani walikuwa wanakuwa wao. Hizo ndio priorities zetu, ziko mramamrama.

Nafikiri jambo la muhimu ni kwa mkoa kuwa na strategy nzuri ya kuendeleza wilaya zake kwa kuanzia na barabara na kisha maendeleo kwa mtu mmoja mmoja.

Kikwazo kikubwa kiko kwa viongozi wa mkoa ambao hawana vision yoyote. Tumemuongelea Mwakipesile mara nyingi hapa, unategemea litokee nini? Lakini hata waliotangulia walikuwa hivyo hivyo, ni tatizo la nchi, mizee imeng'ang'ania madaraka wakati haina uwezo wa kufanya mabadiliko.

Mimi nilipokuwa mdogo nilikuwa nawasikia hao akina Anangisye, Mwakitwange, Mwangoka, Mwakatumbula, Kasambala nk. walivyokuwa wanahaha kila wilaya kuhimiza maendeleo. Leo hii tuna globalization na kila kiongozi wetu anaweza kuona jinsi wenzetu wanavyotuacha mbele, lakini uwezo wao wa kuleta mabadiliko ni mdogo sana.

Kilichobaki ni mtu mmoja mmoja kusaidia kumuemisha mdogo wake, mtoto wake au ndugu yake labda huko mbele hawa vijana watakuwa na akili na uwezo kuliko sisi kaka/baba, dada/mama zao. Muhimu pia ni kwa wale wenye nafasi kukumbuka nyumbani tunakotoka na kujaribu kusaidia vijana hata kama ni mmoja au wawili. Hatuwezi kukwepa, wote ni sehemu ya hayo matatizo tunayoyaongelea.
 
Balantanda,

Bahati mbaya mimi siifahamu vizuri Chunya zaidi ya kusikia kuhusu utajiri wa dhahabu. Kuna baadhi ya vijana walikuwa wanatoka kule kwetu kwenda kuchimba dhahabu Chunya, wakirudi wasichana wote wa maana wilayani walikuwa wanakuwa wao. Hizo ndio priorities zetu, ziko mramamrama.

Nafikiri jambo la muhimu ni kwa mkoa kuwa na strategy nzuri ya kuendeleza wilaya zake kwa kuanzia na barabara na kisha maendeleo kwa mtu mmoja mmoja.

Kikwazo kikubwa kiko kwa viongozi wa mkoa ambao hawana vision yoyote. Tumemuongelea Mwakipesile mara nyingi hapa, unategemea litokee nini? Lakini hata waliotangulia walikuwa hivyo hivyo, ni tatizo la nchi, mizee imeng'ang'ania madaraka wakati haina uwezo wa kufanya mabadiliko.

Mimi nilipokuwa mdogo nilikuwa nawasikia hao akina Anangisye, Mwakitwange, Mwangoka, Mwakatumbula, Kasambala nk. walivyokuwa wanahaha kila wilaya kuhimiza maendeleo. Leo hii tuna globalization na kila kiongozi wetu anaweza kuona jinsi wenzetu wanavyotuacha mbele, lakini uwezo wao wa kuleta mabadiliko ni mdogo sana.

Kilichobaki ni mtu mmoja mmoja kusaidia kumuemisha mdogo wake, mtoto wake au ndugu yake labda huko mbele hawa vijana watakuwa na akili na uwezo kuliko sisi kaka/baba, dada/mama zao. Muhimu pia ni kwa wale wenye nafasi kukumbuka nyumbani tunakotoka na kujaribu kusaidia vijana hata kama ni mmoja au wawili. Hatuwezi kukwepa, wote ni sehemu ya hayo matatizo tunayoyaongelea.

Nimekusoma mkuu,kwa kweli inasikitisha mno kuona kiongozi badala ya kufikiria namna ya kubuni mikakati ya kuuletea maendeleo mkoa wake lakini anakuwa kiini cha kubuni mikakati ya kurudisha nyuma maendeleo kwa kuleta makundi ya kisiasa mkoani ambayo matokeo yake ni makundi hayo kila kukicha wanajibizana badala ya kushiriki kivitendo na kimawazo katika kuuletea maendeleo mkoa wa Mbeya...Chunya mkuu Dhahabu ilikuwepo na bado ipo niyngi tu tatizo ni kama hilo uliloongea hapo juu,viongozi mkoani na wilayani badala ya kukaa na kubuni ni njia gani zitumike katika kuwasaidia wachimbaji wadogo wa dhahabu wilayani(ambao ndio wengi) wao wanakalia kusimamia makundi tu ya kisiasa..We fikiria barabara inayounganisha wilaya ya Chunya na makao makuu ya mkoa ni kama km 90 tu lakini miaka nenda rudi barabara hii ni bado ya tope tu,mvua ikinyesha haipitiki,sasa sijui priorities za viongozi wa mkoa wa Mbeya ni zipi hasa(ama ndo hayo makundi ya kisiasa??),inasikitisha kwa kweli...
 
Heri ya siku kuu kwa wote. Na kwa wana TKY an KYL Apapigwe.

Hivi Wabunge wa Tanzania wana jukumu la kuleta Pork Nyumbani? Je wanaweza kuchunguza matatizo, kubuni njia ya kuyatatua kuandikia proposal kupeleka bungeni na kuishawishi serikali itoe pesa kusaidia? Nani ana jukumu la kugharimia maendeleo ya jimbo?

Je kuna conflict kati ya wizara na matakwa ya mbunge? Kwa mfano kama mbunge anataka barabara katika jimbo lake, Waziri wa mawasiliano ( or is it miundombinu?) ana say hapo?

Ninasema hivyo kwa sababu ingawaje sisi wananchi tuna jukumu la kuendeleza majimbo yetu, wakati mwingine hiyo miradi inahitaji kuwa co-ordinated na kuchangiwa na serikali.
Mfano ni miradi kama usafiri, emergency kama mafuriko na yatokanayo na mafuriko ( njaa na maradhi) Hili ni tatizo sana hasa katika wilaya ya Kyela.
 
Mbona Mbeya wana website? Hii hapa chini:

| Mbeya Region - The United Republic of Tanzania

Nimeingia kwenye hii website, it looks state sponsored, also it has nothing much, looks as if it is still under construction, the information about the region is also very filmsy,is limited to physical borders. I tried to register and was promissed an e-mail which never arrived.

Thanks for the info though.
 
Nimeingia kwenye hii website, it looks state sponsored, also it has nothing much, looks as if it is still under construction, the information about the region is also very filmsy,is limited to physical borders. I tried to register and was promissed an e-mail which never arrived.

Thanks for the info though.

Hata mimi nimejaribu kuifungua hakuna la maana zaidi ya utambulisho na majina ya wilaya zote mkoani,may be iko under construction
 
I believe Jamii Forum should be used to share well researched issues and not whimsical personal vendatta. We ought to be serious because the country needs us!!!
 
Heri ya siku kuu kwa wote. Na kwa wana TKY an KYL Apapigwe.

Hivi Wabunge wa Tanzania wana jukumu la kuleta Pork Nyumbani? Je wanaweza kuchunguza matatizo, kubuni njia ya kuyatatua kuandikia proposal kupeleka bungeni na kuishawishi serikali itoe pesa kusaidia? Nani ana jukumu la kugharimia maendeleo ya jimbo?

Je kuna conflict kati ya wizara na matakwa ya mbunge? Kwa mfano kama mbunge anataka barabara katika jimbo lake, Waziri wa mawasiliano ( or is it miundombinu?) ana say hapo?

Ninasema hivyo kwa sababu ingawaje sisi wananchi tuna jukumu la kuendeleza majimbo yetu, wakati mwingine hiyo miradi inahitaji kuwa co-ordinated na kuchangiwa na serikali.
Mfano ni miradi kama usafiri, emergency kama mafuriko na yatokanayo na mafuriko ( njaa na maradhi) Hili ni tatizo sana hasa katika wilaya ya Kyela.

Hapo umenena malafyale,,,,tatizo hapa pia lipo kwa wabunge wetu,pamoja na usomi wao sio wabunifu katika suala zima la kuandaa vitu kama proposal na kuziwasilisha serikalini(ama hata kwa wafadhili) badala yake wamekaa kulialia tu 'oooh fulani ananifanyia majungu jimboni kwangu'..Kama mtu ni mbunifu na unaleta maendeleo jimboni kwako sidhani kama una haja ya kuwa na wasiwasi/watakiwa kulalamika maana hata kama kuna watu wanakufanyia zengwe jimboni kwako wananchi wataamua kutokana na maendeleo uliyowaletea..Pia ifikie kipindi vingozi watawala na waendaji mkoani(RC,RAS,DCs,DEDs,Wakuu wa idara mbalimbali za halmashauri nk) wasijiingize katika makundi haya ya siasa badala yake wafanye lile lililowapeleka mkoani,maana wanatumia muda mwingi (na sometimes wanakuwa njia panda) katika kujishughulisha na makundi ya kisiasa badala ya kufanya na kuhamasisha shughuli za maendeleo mkoani Mbeya....
 
Heri ya siku kuu kwa wote. Na kwa wana TKY an KYL Apapigwe.

Hivi Wabunge wa Tanzania wana jukumu la kuleta Pork Nyumbani? Je wanaweza kuchunguza matatizo, kubuni njia ya kuyatatua kuandikia proposal kupeleka bungeni na kuishawishi serikali itoe pesa kusaidia? Nani ana jukumu la kugharimia maendeleo ya jimbo?

Je kuna conflict kati ya wizara na matakwa ya mbunge? Kwa mfano kama mbunge anataka barabara katika jimbo lake, Waziri wa mawasiliano ( or is it miundombinu?) ana say hapo?

Ninasema hivyo kwa sababu ingawaje sisi wananchi tuna jukumu la kuendeleza majimbo yetu, wakati mwingine hiyo miradi inahitaji kuwa co-ordinated na kuchangiwa na serikali.
Mfano ni miradi kama usafiri, emergency kama mafuriko na yatokanayo na mafuriko ( njaa na maradhi) Hili ni tatizo sana hasa katika wilaya ya Kyela.

Hapo umenena malafyale,,,,tatizo hapa pia lipo kwa wabunge wetu,pamoja na usomi wao sio wabunifu katika suala zima la kuandaa vitu kama proposal na kuziwasilisha serikalini(ama hata kwa wafadhili) badala yake wamekaa kulialia tu 'oooh fulani ananifanyia majungu jimboni kwangu'..Kama mtu ni mbunifu na unaleta maendeleo jimboni kwako sidhani kama una haja ya kuwa na wasiwasi/watakiwa kulalamika maana hata kama kuna watu wanakufanyia zengwe jimboni kwako wananchi wataamua kutokana na maendeleo uliyowaletea..Pia ifikie kipindi vingozi watawala na waendaji mkoani(RC,RAS,DCs,DEDs,Wakuu wa idara mbalimbali za halmashauri nk) wasijiingize katika makundi haya ya siasa badala yake wafanye lile lililowapeleka mkoani,maana wanatumia muda mwingi (na sometimes wanakuwa njia panda) katika kujishughulisha na makundi ya kisiasa badala ya kufanya na kuhamasisha shughuli za maendeleo mkoani Mbeya....
 
I believe Jamii Forum should be used to share well researched issues and not whimsical personal vendatta. We ought to be serious because the country needs us!!!

Wewe nawe!!!!,wa wapi wewe??,kwamba vitu vinavyojadiliwa hapa kuhusu siasa za Mbeya sio reseached issues????,umetumwa nini???,acha hizo mkulu.....jazba hazisaidii...Hoja hujibiwa kwa hoja na si jazba..Ubarikiwe sana
 
Nimeingia kwenye hii website, it looks state sponsored, also it has nothing much, looks as if it is still under construction, the information about the region is also very filmsy,is limited to physical borders. I tried to register and was promissed an e-mail which never arrived.

Thanks for the info though.

Hao jamaa wamesaidiwa kutengenezewa hiyo website lakini hata kuweka data tu kunawashinda. Yaani huko nyumbani mtu anaweza kuwekewa chakula mpaka mdomoni lakini bado akashindwa kumeza.

Tuna safari ndefu mno Tanzania.

Wapigieni simu hapo mkoani na kuwapa changamoto, vinginevyo hakuna kitakachofanyika.

Inabidi tuanze kuwasukuma vinginevyo wataendelea kulala. Tusikata tamaa, mkoa ni wetu wote.

Nita foward baadhi ya comments zenu kwa wale ninao wafahamu. Kama mna info ambazo zinaweza kusaidia kuimarisha hiyo website kwa faida ya mkoa ninaweza kuwaunganisha na watu walioitengeneza ili waziongezee. Jamani huko nyumbani tunachechemea wakati sasa inatakiwa tuwe tunakimbia.
 
Hapo umenena malafyale,,,,tatizo hapa pia lipo kwa wabunge wetu,pamoja na usomi wao sio wabunifu katika suala zima la kuandaa vitu kama proposal na kuziwasilisha serikalini(ama hata kwa wafadhili) badala yake wamekaa kulialia tu 'oooh fulani ananifanyia majungu jimboni kwangu'..Kama mtu ni mbunifu na unaleta maendeleo jimboni kwako sidhani kama una haja ya kuwa na wasiwasi/watakiwa kulalamika maana hata kama kuna watu wanakufanyia zengwe jimboni kwako wananchi wataamua kutokana na maendeleo uliyowaletea..Pia ifikie kipindi vingozi watawala na waendaji mkoani(RC,RAS,DCs,DEDs,Wakuu wa idara mbalimbali za halmashauri nk) wasijiingize katika makundi haya ya siasa badala yake wafanye lile lililowapeleka mkoani,maana wanatumia muda mwingi (na sometimes wanakuwa njia panda) katika kujishughulisha na makundi ya kisiasa badala ya kufanya na kuhamasisha shughuli za maendeleo mkoani Mbeya....

Balantanda,

Hapo umepigilia misumari kweli. Ukiweza ku deliver hakuna atakayekuletea majungu. Wababaishaji ndio utawasikia kila siku ni kelele tu. Kule Rungwe kuna wajuaji wengi mno lakini mbona prof. Mwandosya amepita 2000 na 2005 bila kupingwa? Hata wapinzani huwa hawaendi kule.

Mwanadamu hachagui jirani yake, inabidi ujifunze kuishi na kila mtu kuanzia manyang'au mpaka malaika.
 
kudumaa maendeleo ya mkoa wa mbeya sio bahati mbaya ila ni mkakati maalumu ambao umetengenezwa katika kuhakikisha mkoa huo unazidi kudumaa. Uteuzi wa Mwakipesile kuwa RC umeochangia kuongezeka kwa mivurugano na migogoro ya mara kwa mara na kuwafnya wananchi na viongozi wasifikirie habari za maendeleo. Kuna baadhi ya wakulu hawalali zaidi ya kuwaza namna ya kumdhibti Mwandosya. Nina habari kuwa wafuatao waliteuliwa with extra instructions za kumdhibiti Prof Mark: DC Kyela, DC mbeya mjini, RC mwakipesile, Katibu CCM (rungwe), katibu CCM mkoa( mrithi wa Kikungwe). Sasa hawa wote wakijiunga na Nawab mulla( M/kiti CCM mkoa), Mwang'onda (mbunge kuteuliwa), Florence Kyendesya (mbunge Viti maalumu CCM), na huyu anayegombea mbeya vijijini (CCM) Mwanjali ) mkoa hauwezi kuendelea kabisa. Huyu mgombea wa CCM sidhani hata kama kamaliza elimu ya kidato cha nne, labda kama alijiendeleza baadaye. Ila piga ua kidato cha sita hajakanyaga, any way elimu ya darasani mtu anaweza ku argue kuwa siyo muhimu, ila huyu jamaa hata IQ yake iko chini sana, uwezo wa kuchanganua mambo na kujenga hoja makini kwa hapo yupo chini kabisa. Kilichomfikisha hapo yeye alikuwa ni mwana mtandao orijino wa kutupwa uchaguzi wa mwaka 2005

Kuna mtu aliniambia kuwa Jaka Mwambi alipoteza nafasi yake baada ya kumpigia debe kinamna Mwandosya katika uchaguzi wa NEC mbeya- kuna mtu analijua hili atuhabarishe



Miaka ya nyuma SADC walitaka kujenga makao makuu yao Mbeya eneo la Uyole, Lkini kiongozi mmoja nasikia akawaambia SADC wajenga makao makuu yao mkoa mojawapo wa kaskazini. Jamaa wakakataa wakaamua kujenga Botswana.

Ona ilivyochukua muda mrefu kujenga uwanja wa ndege, kubadili chuo cha MTC kuwa chuo kikuu, nk.
 
Hivi inakuwaje mbunge unafanya ziara kwenye jimbo lako? Muda mwingine wote unakuwa wapi? Nilikuwa nategemea wakae kwenye majimbo yao hasa kwa wakati ambao sio wa bunge.


Bunge huwa lina kamati mbali mbali ambazo hufanya kazi zake wakati vikao vya bunge vinapokuwa vimeahirishwa. Kamati hizi ni kama vile za Uchumi na Fedha, Hesabu za Serikali kuu, Hesabu za Serikali za mitaa, Maadili na Madaraka ya Bunge, Katiba na Sheria n.k. Wengi wa wabunge wetu wanakuwa anafanya kazi za kamati hizi wakati huo, kwa hiyo hii huchangia sana kutokuwepo majimboni mwao muda mwingi. Lakini pia wabunge wana safari nyingi za kikazi nje ya nchi, hasa zinazotokana na kamati hizi, kwa hiyo hizi nazo zinachangia sana kuwafanya wasiwepo majimboni mwao.
Sio kwamba wabunge wote wapo ndani ya kamati hizi, wengine ni watoro tu wasiopenda kuwepo majimboni mwao kipindi kisicho cha vikao vya bunge, nadhani hawa ndio hasa ambao Malafyale Mtanzania unakomaa nao. Wengi pia huishi miji ambayo ni tofauti na Majimbo yao, ingawa wanawakilisha majimbo ambayo hawaishi. hili nalo ni tatiz kubwa sana hapa kwetu.
 
Malafyale Mwanjelwa, mansions za watu wa Kyela unazosema wamejenga huko Mbeya ziko sehemu gani? Watu waliojenga nyumba za maana hapo mjini Mbeya wengi ni wakinga toka Makete!!Malafyale unawafananisha watu kutoka kyela na Wapemba, wapi na wapi?? Wapemba wanamsimamo hawayumbishwi, nyie wa Kyela Mwakipesile mtu mzima anakubali kutumiwa kuwahujumu ndugu zake anasahau kuwa huo uRC unakikomo na atarudi kuishi Kyela.!!Hayo mambo ya kitamaduni unayoyasema yanawafanya watu wa kyela kuwa nyuma kimaendeleo ; ndio hayo niliyowahi kusema hapo awali kuwa hilo ni jukumu la viongozi kuwaelimisha watu wao[ sio kuwagawia fedha!!] ili waepukane na imani potofu. Kuwaelimisha wananchi ni jambo la msingi mahala popote watu wanapotaka maendeleo ama sivyo wataishia kuchunana ngozi as a result watu wataogopa hata kwenda mashambani kulima. Kuhusu maendeleo ya wilaya ya Chunya nadhani tatizo kubwa kule ni committed leadership, viongozi wengi wa wilaya ile ni wasanii; mfano mdogo tu ni wakati Lowassa alipokuwa waziri mkuu na kulitembelea jimbo la Songwe, wananchi walipomzomea Mbunge wao wa wakati ule na kumlalamikia kuwa alikuwa hakuwatembelea toka alipochaguliwa!! Wabunge wa wilaya hii inabidi watumie muda wao mwingi huko majimboni kwao kwa bahati mbaya wabunge wote wa Chunya makazi yao na familia zao yako Dar Es Salaam!!
 
Malafyale Mwanjelwa, mansions za watu wa Kyela unazosema wamejenga huko Mbeya ziko sehemu gani? Watu waliojenga nyumba za maana hapo mjini Mbeya wengi ni wakinga toka Makete!!Malafyale unawafananisha watu kutoka kyela na Wapemba, wapi na wapi?? Wapemba wanamsimamo hawayumbishwi, nyie wa Kyela Mwakipesile mtu mzima anakubali kutumiwa kuwahujumu ndugu zake anasahau kuwa huo uRC unakikomo na atarudi kuishi Kyela.!!Hayo mambo ya kitamaduni unayoyasema yanawafanya watu wa kyela kuwa nyuma kimaendeleo ; ndio hayo niliyowahi kusema hapo awali kuwa hilo ni jukumu la viongozi kuwaelimisha watu wao[ sio kuwagawia fedha!!] ili waepukane na imani potofu. Kuwaelimisha wananchi ni jambo la msingi mahala popote watu wanapotaka maendeleo ama sivyo wataishia kuchunana ngozi as a result watu wataogopa hata kwenda mashambani kulima. Kuhusu maendeleo ya wilaya ya Chunya nadhani tatizo kubwa kule ni committed leadership, viongozi wengi wa wilaya ile ni wasanii; mfano mdogo tu ni wakati Lowassa alipokuwa waziri mkuu na kulitembelea jimbo la Songwe, wananchi walipomzomea Mbunge wao wa wakati ule na kumlalamikia kuwa alikuwa hakuwatembelea toka alipochaguliwa!! Wabunge wa wilaya hii inabidi watumie muda wao mwingi huko majimboni kwao kwa bahati mbaya wabunge wote wa Chunya makazi yao na familia zao yako Dar Es Salaam!!



Ile ya Wapemba sikuwa na maana hiyo. Hivi umewahi enda kule Pemba wewe!? Msimamo ni pamoja na maendeleo ya nchi yako au kwenu. Siyo kelele tu za siasa.

I mean, pamoja na hao wa Makete na Njombe, lakini pia na wa-Kyela.
Mimi sidhani kama mbunge pekee ana jukumu la kubadilisha Kyela. Wewe pia na yule. Wote mnatakiwa mwende kule kuwaelimisha watu. Hii mambo ya mbunge, mbunge,,,,, au viongozi, mimi napingana nayo sana.Wewe Usipooanza ku-act hata mbunge awe anakaa na ninyi huko huwezi badilika.

Bwana Bubesi, anza wewe, pia majaji kibao wenye asili ya kule wamejazana Dar, mkuu wako wa majeshi, watu elite kibao wa huko wako Dar na shemu zingine wametulia tu. waanze hawa then wengine watafuata. Sasa hivi kama unavyosema, conflicts za Mwakyembe na Mwakipesile ndiyo zina-stall maendeleo. Kama wewe na wengine mngekuwa na nyumba za kuwavutia kufanya vocations angalau za mwezi mmoja mmoja kule unadhani mngemkumbuka Mwakyembe?

Lakini nisome kwa makini. Sina maana Mbunge hafai kuwepo. Ndiyo maana yupo
 
Malafyale Mwanjelwa, mansions za watu wa Kyela unazosema wamejenga huko Mbeya ziko sehemu gani? Watu waliojenga nyumba za maana hapo mjini Mbeya wengi ni wakinga toka Makete!!Malafyale unawafananisha watu kutoka kyela na Wapemba, wapi na wapi?? Wapemba wanamsimamo hawayumbishwi, nyie wa Kyela Mwakipesile mtu mzima anakubali kutumiwa kuwahujumu ndugu zake anasahau kuwa huo uRC unakikomo na atarudi kuishi Kyela.!!Hayo mambo ya kitamaduni unayoyasema yanawafanya watu wa kyela kuwa nyuma kimaendeleo ; ndio hayo niliyowahi kusema hapo awali kuwa hilo ni jukumu la viongozi kuwaelimisha watu wao[ sio kuwagawia fedha!!] ili waepukane na imani potofu. Kuwaelimisha wananchi ni jambo la msingi mahala popote watu wanapotaka maendeleo ama sivyo wataishia kuchunana ngozi as a result watu wataogopa hata kwenda mashambani kulima. Kuhusu maendeleo ya wilaya ya Chunya nadhani tatizo kubwa kule ni committed leadership, viongozi wengi wa wilaya ile ni wasanii; mfano mdogo tu ni wakati Lowassa alipokuwa waziri mkuu na kulitembelea jimbo la Songwe, wananchi walipomzomea Mbunge wao wa wakati ule na kumlalamikia kuwa alikuwa hakuwatembelea toka alipochaguliwa!! Wabunge wa wilaya hii inabidi watumie muda wao mwingi huko majimboni kwao kwa bahati mbaya wabunge wote wa Chunya makazi yao na familia zao yako Dar Es Salaam!!

Bules,

Ndugu yangu Mwanjelwa aliposema wana Kyela wamejenga Mbeya, nikaona nikae kimya maana sikuwa na data.

Inabidi tuendelee kuwapigia kelele hawa waheshimiwa labda wataamka huko Dar wanakolala.

Wengi wao wakifika kwenye majimbo yao wanafikia guest house.
 
Ile ya Wapemba sikuwa na maana hiyo. Hivi umewahi enda kule Pemba wewe!? Msimamo ni pamoja na maendeleo ya nchi yako au kwenu. Siyo kelele tu za siasa.

I mean, pamoja na hao wa Makete na Njombe, lakini pia na wa-Kyela.
Mimi sidhani kama mbunge pekee ana jukumu la kubadilisha Kyela. Wewe pia na yule. Wote mnatakiwa mwende kule kuwaelimisha watu. Hii mambo ya mbunge, mbunge,,,,, au viongozi, mimi napingana nayo sana.Wewe Usipooanza ku-act hata mbunge awe anakaa na ninyi huko huwezi badilika.

Bwana Bubesi, anza wewe, pia majaji kibao wenye asili ya kule wamejazana Dar, mkuu wako wa majeshi, watu elite kibao wa huko wako Dar na shemu zingine wametulia tu. then wengine watafuata. Sasa hivi kama unavyosema, conflicts za Mwakyembe na Mwakipesile ndiyo zina-stall maendeleo. Kama wewe na wengine mngekuwa na nyumba za kuwavutia kufanya vocations angalau za mwezi mmoja mmoja kule unadhani mngemkumbuka Mwakyembe?

Lakini nisome kwa makini. Sina maana Mbunge hafai kuwepo. Ndiyo maana yupo


Mwanjelwa,

Ni kweli ni wajibu wa wote kushiriki kwenye maendeleo ya wilaya/mkoa/nchi yetu.

Huko kwenye baadhi ya wilaya za Mbeya ukifanya chochote cha maana tayari majungu na maneno yanaanza. Wengine hatuogopi hayo majungu.

Kuna jamaa alipoanza kujenga ghorofa lake Kyela wakasema atarogwa na ghorofa kuanguka. Bahati nzuri hakusikia na sasa kuna wengine wameiga na kujenga nyumba za maana Kyela.

Kibaya ni kwamba hakuna hata kiongozi mmoja aliyeenda kuwaona hao jamaa na kuwatakia heri. Hata pale walipokwama kwa muda, hakuna hata kiongozi aliyeenda na kuwaambia kulikoni. Badala yake unasikia maneno ya mitaani kibao. Wengine wanaenda hata kushawishi vyombo vya fedha visitoe misaada. Huko wilayani kuna maajabu makubwa sana.

Ushauri wangu ni mmoja, fanya unachoweza bila kuwaangalia hao wanasiasa. Labda kuna siku wataamka na kuona kuna haja ya kuunga mkono maendeleo kwenye wilaya zao. Hata huyu Mwakipesile akiona watu wameamka, itabidi na yeye afuate tu mkondo wa maendeleo.

Wanachofikiria wao ni kwamba kila anayefanya jambo la maana kule nyumbani basi anataka ubunge wao.

Ni aibu mtu ana nyumba za maana Dar au hata nje ya nchi, unarudi kwenu inakuwa kama unaingia kwenye zizi la ng'ombe. Wengine wanashindwa hata kupeleka familia zao nyumbani.

Kuna mengi ya Mbeya siwezi kuandika hapa kwa kuhofia kuendeleza migogoro, ila tunajua wazi kuna viongozi wengi wa huo mkoa wanakwamisha maendeleo kwa njia mbalimbali. Siku ikifika tutakuja kuwaambia bila kuwaficha. Wana muda wa kubadilika kabla ya kuumbuliwa huko mbeleni.
 
Mkuu Mtanzania[ Malafyale] nadhani wewe ni mzoefu wa siasa za mkoa huu, na hili la wilaya ya Chunya unalionaje? Naamini unaifahamu Chunya vizuri sana, kuna kitu gani kinachokwaza maendeleo huko ilihali wilaya ina rasilimali kibao?
 
Last edited:
Back
Top Bottom