Shule hii Mbeya iko wapi?

Shule hii Mbeya iko wapi?

Huu uzi unanikumbusha shule yangu ya sekondari Meta. Kuna mwalimu hapo mtata alikuwa anachapa bakora si mchezo akiitwa Mwaigwisye. Alikuwa mwalim wa nidham wkt huo. Alijenga uadui mkubwa sana na wanafunzi hasa O-level kutokana na tabia yake ya kutosikiliza excuses za wanafunzi hata kama ni za ukweli.

Kuna siku huyu ticha akataka kumwadhibu mwanafunzi wa A-level kwa kosa la kufuga ndevu. Yule jamaa akambadilikia pale pale assembly wakaanza kuzichapa kavu na yule ticha.

Sasa wale wanafunzi wa O-level walikuwa karibu pale na vile wasivyompenda yule mwalimu wakamuunganishia kisago yule ticha utafikiri wanapiga mwizi ilibaki kidogo wamwuue yule ticha palepale.
 
Mkuu Kabigi na ndimbo balaa. Ndimbo amenifundisha biology namshukuru sana nimekuwa mtaalam. Nahisi kuna member mmoja humu ni mtoto wa Kabigi.
Mkuu kuna mwalimu alikua anaitwa Mwandumbya na Mwambene,nilikua nawagwaya sana.
 
Meta sekondari ni ya wazazi wa CCM, ninayoitafuta lilikuwa ya serikali lilikuwa shule ya bweni na haikuwa mbali sana na uwanja wa mpira wa zamani ilitenganishwa na uwanja wa Raga (rugby). Au CCM ilichukua?
Olikuwa Meta sasa iliendaje ccm sijuhi hii ni kutokana na stories za wahenga kipindi hicho.
 
Mkuu kama umesoma Sangu Sec School bila shaka utakuwa unayajua haya maeneo Msichoke Pub.. upande wa pili ukivuka barabara ya lami...kulikuwa na mishkaki na pombe za kienyeji hapo.....Savoi Bar...na Vamponji...moja kati ya maeneo ambayo tumegonga sana ulabu enzi hizo...
Mkuu Vamponji tena teh teh, pale pana kitimoto balaa.
 
Yeah ndo mimi karibu na Meta Sec School....ww ni nani mdau usije kuta nakufahamu....maana kama ulikuwa unajua hadi ninapokaa ww noma...
Mkuu inawezekana tunafahamiana sana tu na Member wengine wapo humu Jf, sometimes tulikuwa tunashinda kwenye kijiwe cha fundi viatu pale opposite na mitaa yenu.
 
Mkuu inawezekana tunafahamiana sana tu na Member wengine wapo humu Jf, sometimes tulikuwa tunashinda kwenye kijiwe cha fundi viatu pale opposite na mitaa yenu.
Sawa kabisa pale chini ya mti .....pembeni ya njia ya kwenda Meta secondary...hawa jamaa unawafahamu...Jagwer...Mundundu Biz...babu....
 
Sawa kabisa pale chini ya mti .....pembeni ya njia ya kwenda Meta secondary...hawa jamaa unawafahamu...Jagwer...Mundundu Biz...babu....
Generali jaguar nlimkuta sangu
Aise si alikuwa mbabe wa shule

Ova
 
Kuna siku walikuwa wanacheza Kalobe na Nsenga basi wakaanza kupigana.... Daah Kyege akasema Iyunga tuuzime ule ugomvi daah tuliwachapa wale watoto balaa sana
Hahahahab.kyege alikuwa mibangi sana .

Alishawahi kunitibua karakana pale siku moja nikamcheki na meno yake ya rangi rangi zile nikasema poa tu tusikutane mtaa
 
Yaa Jagwa alikuwa ni mbabe...na crue yake walikuwa wakivuta bangi kaburi la boby...
Hao wakati tunaingia form 0ne sangu walikuja wanapita kila darasa wananyanganya madadtari na mabegi na pesa....Kuna siku tunaenda toi wakatugumia
Dah wacha tudinshianeee.......wakasema Nyie madogo wabishi sana
Alafu mponjoli malakasuka naye alikuwepo sangu Sema walituzidi darasa

Ova
 
Adolph namfahamu alikuja kuwa board member wa atc pia
Nakumbka nlipo kuwa dogo mbeya alikuwa akinipitia tukawa tunaenda kumtembelea mzee Walden black mamba kwake

Ova
Mzew Walden naye si yule chotara mj general was JWtz
 
Back
Top Bottom