Shule hii Mbeya iko wapi?

Shule hii Mbeya iko wapi?

Mkuu Kabigi na ndimbo balaa. Ndimbo amenifundisha biology namshukuru sana nimekuwa mtaalam. Nahisi kuna member mmoja humu ni mtoto wa Kabigi.
Dah ndimbo nlikuwa namuwekaga kwenye wakati mgumu sana maana haipiti siku nlikuwa lzma nmzingue alikuwa anaongea mpk anatetemeka
Yes alikuwa mwalimu wa biology

Ova
 
Miaka ya hamsini mpaka baada ya Uhuru mji wa Mbeya ulikuwa na shule ya kati (middle school) iliyojulikana kwa majina ya N.A. (Native Authority) na baadaye L.A. (Local Authority).

Sifa kubwa ya shule hii ni kuweza kutoa viongozi wakubwa wa mashirika ya umma, viongozi hao ni Pro. Matthew Luhanga (makamu chuo kikuu Dar es Salaam), Linford Mbona (mkurugenzi ushirika la reli Tanzania) Elijah Bharuhan(sic) Luhanga (mkurugenzi mkuu Tanesco), Diamond Mwakyembe (mkurugenzi TBS), Nicholas Mbwanji (mkurugenzi NIT) , marubani wa ATC wawili ndugu Mwambapa! na wengine ambao nimewasahau majina, wote hawa ni wale waliondoka kabla ya mwaka 1964.

Kwa orodha hii inaonesha ni jinsi gani shule hii ya L A Middle School ilivyokuwa na viwango vya huu vya msingi wa elimu kuwawezesha kuinhia kwenye vyuo vikuu na kuweza kushika nyadhifa za huu nchini.

Kwa wenye kumbukumbu zaidi ninawakaribisha.
Siku hizi ndipo ilipo Meta Sec. School karibu na Mabatini.
 
Mng'ong'o alihamishiwa mwakaleli baada ya shule kuwa na matokeo mabovu sana ya advance 2016.
Ila sasa hivi kastaafu yuko kwao Njombe.
Alivyohamishwa Mng'ong'o, Mkuu wa shule alikuwa nani?
 
Ada ya elfu mbili mawaziri wengi walishindwa kuilipa, mzee Aikaeli Mbowe, sir G. Kahama, chief Mkwawa ni miungoni ya wazazi walioweza kuwasomesha watoto wao hapo, wanafunzi wengi walikuwa wahindi, walimu wengi na headmaster wazungu, kwa waafrika wachaga wengi, wazungu hasa watoto wa masetla wenye mashamba makubwa wa nchini na nchi za jirani.
Duuh! Mkuu...utakuwa una umri gani?
 
Siku hizi ndipo ilipo Meta Sec. School karibu na Mabatini.
Meta sekondari ni ya wazazi wa CCM, ninayoitafuta lilikuwa ya serikali lilikuwa shule ya bweni na haikuwa mbali sana na uwanja wa mpira wa zamani ilitenganishwa na uwanja wa Raga (rugby). Au CCM ilichukua?
 
Kwa intro tuu ya mtoa mada, anajua hiyo shule ilienda wapi sema ameamua kutuchallange tuu
Sijui ilienda wapi kwani sijawahi kufika huko miaka mingi, niliwahi kuishi Jacaranda nilikuta kuna TBC na kanisa KKKT nikalala mwenye lodge yao siku mbili ila sikushuka bondeni kuona kwani siku wa na muda. Pia Iyunga niliwahi kupita baada ya kuteremka Tazara ila sikupaelewa vizuri kutokana na ujenzi uliofanyika eneo lote. Hata hivyo baadhi ya niliowataja nimekutana nao Dar. ambapo ninaishi tangu miaka ya sitini hapo lilikuwa nasoma Mbeya.
Ninapenda kujua kutokana na sifa ya uwezo wa kutoa viongozi niliowataja ambao wote walisoma wakati mmoja! Hivyo wanafahamiana na sidhani kama kuna shule ya msingi iliyofikia rekodi hii.
 
Machine zilishakufa mkuu..
Ule ukumbi bado upo na pini za loleza nasikia zinapigwa kama kawaida .

Mle ndani paper ikikugonga unaanza kukumbuka ujinga wote uliokuwa unaufanya na watto wa loleza
Nimecheka Sana.nakumbuka siku loleza ikitua kambini tulikua tukitafutana.zile scramble za misosi zinaisha
 
Na swimming pool haijageuzwa dampo
Swimming pool ilikuwa inafagiliwa kila siku. Tena hili lilikuwa eneo la EK la form four.
Form four A, cleaning outside the swimming pool. Form four B, cleaning inside the swimming pool... Hapo assemble mnacheeka.
Ofisi yangu ilikuwa karibu na hiyo swimming pool kwenye jengo la Gymnasium... Basi nilikuwaga naenda kusomea kule night kali, giza balaa nikiangalia kule uwanjani, hadi naogopa kukutana na majini...
 
Naona uzi umevamiwa na wanafunzi wa Iyunga.Je sisi tuliosoma AZANIA tunacomment wapi?
 
Mpaka sasa sijapata jibu, inamaana hiyo shule imeyeyuka! Shule za bodingi za wavulana Mbeya mjini zilikuwa mbili LA (NA) Forest na Santa Joseph (Nzovwe)
 
Niliwahi kuona kwenye luninga mabweni yaliyoungua, nilisikitika na sikuelewa kwa vipi!
Mabweni yamechakaa sana...kuanzia miundo mbinu ya umeme, maji...Madirisha...Ceiling bodi...Sakafu...vyoo...

Sasa licha miundo mbinu kuchakaa, bado kuna wanafunzi walikuwa wanajiunganishia nyaya za umeme kutoka kwenye maungio mbali mbali mabwenini.
 
Back
Top Bottom