Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,703
- 218,231
Wakuu, poleni sana na Majukumu yenu ya kila siku, Naomba kuchukua nafasi hii kuwashukuru wote mliochangia kusambaza taarifa zote za uchaguzi za Chadema ikiwa ni pamoja na kusambaza kampeni kali za kiwango cha juu za Tundu Lissu Mgombea Urais wa Chadema, ambaye anatajwa kama Mgombea bora kabisa wa Urais kuwahi kutokea barani Africa tangu kuumbwa kwa Mbingu na Ardhi.
Wahenga walisema tangu awali kwamba kidole kimoja hakivunji chawa, bila mshikamano wa wadau wote nyinyi kampeni za Tundu Lissu zisingefikia mafanikio ya 96% ambayo ilifika tangu juzi, Kwa niaba ya Chadema na kwa niaba ya Lissu Mwenyewe nachukua nafasi hii bila kuwataarifu kushukuru kila mdau aliyejitolea fedha, muda, nguvu na bando lake ili kusambaza taarifa za kampeni za Lissu, ni imani yangu kwamba Mungu Mwenyezi atawalipa kwa kazi hii iliyotukuka.
Natambua mchango wa kila mmoja na nauheshimu sana, lakini Kipekee naomba kuwashukuru wafuatao kwa niaba ya wengi, JAMIIFORUMS pamoja na Moderator kwa masahihisho na miongozo, Mungu awalinde watu hawa na mabaya yote katika kipindi walichosaliwa nacho hapa duniani, Shukrani zingine ziende kwa CHADEMA Makao Makuu.
Si rahisi kushukuru watu wote kwenye andiko hili, bali shukrani zetu zimfikie kila mmoja aliyesambaza kampeni za Lissu popote alipo , mmefanya kazi ya kutukuka mno! Nina hakika Mungu atawalipa bila shaka.
Mungu ibariki JF, Mungu ibariki CHADEMA, Mungu mbariki Rais Mpya Tundu Lissu.
Wahenga walisema tangu awali kwamba kidole kimoja hakivunji chawa, bila mshikamano wa wadau wote nyinyi kampeni za Tundu Lissu zisingefikia mafanikio ya 96% ambayo ilifika tangu juzi, Kwa niaba ya Chadema na kwa niaba ya Lissu Mwenyewe nachukua nafasi hii bila kuwataarifu kushukuru kila mdau aliyejitolea fedha, muda, nguvu na bando lake ili kusambaza taarifa za kampeni za Lissu, ni imani yangu kwamba Mungu Mwenyezi atawalipa kwa kazi hii iliyotukuka.
Natambua mchango wa kila mmoja na nauheshimu sana, lakini Kipekee naomba kuwashukuru wafuatao kwa niaba ya wengi, JAMIIFORUMS pamoja na Moderator kwa masahihisho na miongozo, Mungu awalinde watu hawa na mabaya yote katika kipindi walichosaliwa nacho hapa duniani, Shukrani zingine ziende kwa CHADEMA Makao Makuu.
Si rahisi kushukuru watu wote kwenye andiko hili, bali shukrani zetu zimfikie kila mmoja aliyesambaza kampeni za Lissu popote alipo , mmefanya kazi ya kutukuka mno! Nina hakika Mungu atawalipa bila shaka.
Mungu ibariki JF, Mungu ibariki CHADEMA, Mungu mbariki Rais Mpya Tundu Lissu.