Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 397
- 993
Fuatilia matangazo ya moja kwa moja kwenye shughuli kuaga mwili wa Edward Lowassa inayofanyika leo tarehe 2/23/2024 katika viwanja vya Karimjee Dar es Salaam.
Salamu kutoka kwa viongozi mbalimbali
Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye: Tunayo mengi ya kumkumbuka Lowassa
Rais Mstaafu Ali Mohamed Shein: Lowassa alikuwa akinivutia kwenye utendaji wake.
Jaji Joseph Warioba
1995 Lowassa alinitafuta akiwa na uchungu sana baada ya kuambiwa Nyerere ndio aliyetia ugumu kuwania Urais. Nilimtia moyo, hakukata tamaa.
2008 Lowassa alinitafuta baada ya kujiuzulu, alisema hakutendewa haki, wamemuhukumu bila kumsikiliza, alinitafuta tukazungumza, nilimwambia haya ni mambo ya kisiasa, asikate tamaa.
Alikuwa alipenda elimu, ni mtu mwenye imani kuwa ana wajibu wa kutumikia taifa, hakuwa mangimeza, alikuwa mtu wa vitendo, pamoja na mapungufu yake hakuwa mtu anayependa kugombana na watu, alikuwa kiongozi mvumilivu, alikuwa ni kiongozi mwenye sifa ya kuwa kiongozi, mwenye maono.
Jakaya Kikwete: Lowassa ametoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya nchi yetu, na ameacha alama zitakazokumbukwa daima.
Rais Hussein Mwinyi: Nimejifunza kutoka kwa Lowassa Uzalendo, uwajibikaji, ushirikiano na makundi mbalimbali na pamoja na kuweka mbele maslahi ya nchi.
Makamu wa Rais Philip Mpango: Alikuwa mtetezi wa maslahi wa wananchi wake wa Monduli, nasi tunapaswa kumuiga katika utumishi wetu
Salamu kutoka kwa viongozi mbalimbali
Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye: Tunayo mengi ya kumkumbuka Lowassa
Rais Mstaafu Ali Mohamed Shein: Lowassa alikuwa akinivutia kwenye utendaji wake.
Jaji Joseph Warioba
1995 Lowassa alinitafuta akiwa na uchungu sana baada ya kuambiwa Nyerere ndio aliyetia ugumu kuwania Urais. Nilimtia moyo, hakukata tamaa.
2008 Lowassa alinitafuta baada ya kujiuzulu, alisema hakutendewa haki, wamemuhukumu bila kumsikiliza, alinitafuta tukazungumza, nilimwambia haya ni mambo ya kisiasa, asikate tamaa.
Alikuwa alipenda elimu, ni mtu mwenye imani kuwa ana wajibu wa kutumikia taifa, hakuwa mangimeza, alikuwa mtu wa vitendo, pamoja na mapungufu yake hakuwa mtu anayependa kugombana na watu, alikuwa kiongozi mvumilivu, alikuwa ni kiongozi mwenye sifa ya kuwa kiongozi, mwenye maono.
Jakaya Kikwete: Lowassa ametoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya nchi yetu, na ameacha alama zitakazokumbukwa daima.
Rais Hussein Mwinyi: Nimejifunza kutoka kwa Lowassa Uzalendo, uwajibikaji, ushirikiano na makundi mbalimbali na pamoja na kuweka mbele maslahi ya nchi.
Makamu wa Rais Philip Mpango: Alikuwa mtetezi wa maslahi wa wananchi wake wa Monduli, nasi tunapaswa kumuiga katika utumishi wetu