Should CHADEMA Fire Zitto?

Should CHADEMA Fire Zitto?

Should Zitto get FIRED from CHADEMA?

  • YES

    Votes: 137 65.9%
  • NO

    Votes: 57 27.4%
  • May be

    Votes: 10 4.8%
  • I don't know

    Votes: 4 1.9%

  • Total voters
    208
Status
Not open for further replies.
Chama

1. Kamaa huamini nguvu ya zito ni din unahaki ni maono yako.

2. Kama huamini ccm imetugawa kwa iman zetu lengo kutudhofisha pia haki yako, rejea kampen za urais kikwete aliimba wimbo huu inchin kote, nawaasa chadema wasiucheze wawaachie ccm single yao kuicheza

3. Chadema iwe ya wote.

adolay,
Unaongea dhana nithibitishie ni lini na wapi Zitto alihubiri udini ni vigezo gani umetumia kumhusisha Zitto na udini? Usijidanganye Chadema si ya wote ina wenyewe.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Zito - kuanguka kwa chadema kwa mwenendo wake wa kutoenda pamoja na chama, yaani yuko zaidi kibinafsi kuliko kichama, na kuonesha dalili za kuanzisha kundi ndani ya chadema ili kuivunja nguvu.
Lakini akijirudi na kuenda pamoja na chama anaweza kuwa msaada mkubwa na kuinuka kwa Chadema.
Ni maoni yangu tu kutokana na mwenendo wa Mh. Zito kuhusiana na Chadema
Nawasilisha..
 
adolay,
Unaongea dhana nithibitishie ni lini na wapi Zitto alihubiri udini ni vigezo gani umetumia kumhusisha Zitto na udini? Usijidanganye Chadema si ya wote ina wenyewe.

Chama
Gongo la mboto DSM


Nataman walau kidogo ungetambua msingi wa hoja yangu. Jitahidi mkuu nakuielewa falsafa.

Nimesema mtego uliotegwa na ccm narudia ccm, tatizo mnapapara katika kurumbana bila kutafakali kwa kina maudhui ndani yake.

Zito mjanja na wajanja zaid wanafaham vigezo vya kwanin anafanya afanyao.

Zito anafaham udhaifu wa watanzania linapokuja suala la iman (narudia muasisi wa dhana hii/silaha hii ni ccm - naumekiri kwa kuniuliza ccm inahusikaje, sasa usipotoshe maudhui ya hoja yangu) huwa hatuhitaji kutafiti wa kuuliza huwa tunakurukupuka kwa kugomea na kususia jambo flan-kisa limegusa iman za watu.

Hiyo ndiyo karata anayocheza nayo zito.
 
Bado nasisitiza subira yavuta heri hatakama matumbo yataendelea kuuma kwa ngojangoja za kuenda pamoja na kundi la akinazito kabwe.

Chadema kwa sasa imeenea nchi zima. Kutoka dar hadi mbeya na rukwa, kutoka dar mpaka ujiji, kutoka dar hadi mto wa mbu, kutoka dar hadi ukerewe, geita hadi mwitongo-mara, kutoka dar had masasi, tandahimba, kyela nk

ANAYESEMA CDM SI YA WOTE INAWENYEWE HAO NDIYO WENYEWE

Zito asifukuzwe ili wenye cdm watulie bila kuyumbishwa na mitego ya ccm.

Kama hoja ya zito ni urais si mchakato upo atajaza form akishinda mchakato akapita ni haki na akishindwa mchakato nihaki pia.

Cdm ni cha watanzania bila kujali iman zao.
 
Zitto siyo mchanga wala mkristo ndio maana! Wachaga hata siku moja huwa hawapendi kushindwa.
Kwahiyo wewe unataka Zitto ashinde kitu gani kwasababu si "mchanga" ama mkristo?Kusema hivyo si ndo udini wenyewe na ukabila huo?Pia usivipangie vyama vingine ambavyo ni wapinzani wako mambo ya kufanya na kuwaambia nani anafaa na nani hafai,hiyo si shughuli ya kumfanyia adui/mpinzani wako,ukifuata matakwa ya adui yako si utakuwa luna?
 
Hapo red sijakuelewa, huenda ulimaanisha spared.
I still have trust in Zitto.
Nasita sana kuamini kuwa this too smart boy could be tempted with money-thing!
Aidha naijutia siku ambayo kamati itagundua na kuweka wazi kuwa Zitto amepokea rushwa in the name of money or whatever token!
Heri ziku hiyo isingalizaliwa chini ya jua!

Tuombe kheri kwani habari nzito hizi,lakini kama utapatikana ushahidi utapatikana basi should be spared!
 
Nataman walau kidogo ungetambua msingi wa hoja yangu. Jitahidi mkuu nakuielewa falsafa.

Nimesema mtego uliotegwa na ccm narudia ccm, tatizo mnapapara katika kurumbana bila kutafakali kwa kina maudhui ndani yake.

Zito mjanja na wajanja zaid wanafaham vigezo vya kwanin anafanya afanyao.

Zito anafaham udhaifu wa watanzania linapokuja suala la iman (narudia muasisi wa dhana hii/silaha hii ni ccm - naumekiri kwa kuniuliza ccm inahusikaje, sasa usipotoshe maudhui ya hoja yangu) huwa hatuhitaji kutafiti wa kuuliza huwa tunakurukupuka kwa kugomea na kususia jambo flan-kisa limegusa iman za watu.

Hiyo ndiyo karata anayocheza nayo zito.

Adolay
Bado unajichanganya na falsafa zako,nahoji huo mtego wa udini unaotumiwa na CCM hoja yako haina mshiko kama ni suala la udini hata CCM yenyewe haitasalimika weka vithibitisho vya hoja zako ni vipi Zitto anahusika?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Hivi shule gani mnazofundishwa kubishana vitu pasipo merits. Nimekuuliza swali rahisi na dogo sana mara ya ngapi sasa?.. Je, unajua maana ya blackmail? hujibu ila unarudia kutoa mifano na matumizi yasiyofanana na neno lenyewe.. Kiingereza mmejifunza wapi? jamani lugha ya watu iacheni andika kiswahili tutakuelewa vizuri sana. Unaponambia mimi nai blackmail Chadema hili ni tusi kubwa sana na kama wewe huoni tusi basi hujui kiingereza isipokuwa cha kusomea darasani kushinda mitihani, hii lugha ya watu brazaa!..umejifunza kuleta balance ya vitu gani, hii elimu gani hii ya unajimu!..
Kama hujaelewa nilichokuandikia kuna shida ama ya kusudia ama ya kukusudia.Kebehi zako hazina tofauti na za Pinda pale Bungeni, huku akishindwa jibu maswali kwa ufasaha na bila kuwa honesty.
Bado nipo right sana ingawa unababaika kudivert vitu kwa kujenga sense ya discredit ili uongeacho kipate kubalika.Wala sijaongea utabiri wowote kwa hio huo unajimu (astrology) sijui umepata wapi?Naona unajtahidi sana kuongezea idea mpya ili kuji boost na baadae uendelee na porojo zako.

Sasa kama hujui hiyo balance niongeayo ni ya vitu gani why should i explain more?Hizo kelele zako za swali rahisi , nami nmekupa jibu rahisi, na kwa upana sana.Ila pamoja na kutojua message unayoipeleka bado unaleta kebehi.
Nimeshakwambia Zitto, Mbowe, Mnyika, Dr.Slaa wote wanapitia hapa JF kila siku na kama niloandika yana uongo wangekuja kupinga niloyaandika na wala sihitaji lolote kutoka kwao ama Chadema kama malipo haramu kwa siri ama ushahidi nilokuwa kinyume cha haki ( I could be sued for that), zaidi ya mimi kuwafahamisha nyote hapa ya kwamba wanachonganishwa makusudi kukorofishana.
Hapa ndipo panaonyesha jinsi ulivyo shallow, na ndipo nikuwa nasubiri.Blackmailing ni zaidi ya kuchukua hela kwa vitisho.Kuna maana nyingine zadi ya moja.Ila zote zinaambatanishwa na vitisho.Na kitisho chako hapa ni kujaribu leta habari kuwa na wengine "wamekosea pia".Sasa hapa hujui ulichoandika na "Tafsiri yake".Hii ni ni wazi kuwa una matatizo,unajiamini sana zaidi ya ukweli wa mambo katika maeneo fulani fulani.N ahii ipo kwa watanzania wengi.

Walianza na Chacha Wangwe, walipoona hana manufaa wakamwondoa sasa wanamtumia Zitto kama mtaji wa kuibomoa Chadema na nasema tena viongozi wa Chadema wanalijua hili isipokuwa nyie washbiki wa pembeni ndio mnaleta ajizi na hata huu Udini uliopo sasa. hakuna mawasilaino mazuri kati ya Zitto na Mbowe miaka sasa na sababu ilikoanzia nazijua ila sina sababu ya kuanika. Kama wao wana mashaka na niloyaandika waje hapa halafu tutaona mwisho wa hoja hii itatufikisha wapi!.. am down with it!
Mkandara mbona unasound kama loosers, ambao wanapenda jifanya kuwa waachwe wafanye wafanyalo kwa vile wanadhani kuwa wao ndio wanajua tuu.Mbona vitu vingine ni logical na havihitaji court eveidence hapa.Nilishakuambia
si siri kuwa CCM wapo busy kuvunjwa upinzania kwa gharama kubwa na njia nyingi zaiid ya hii unayong`ang`ania kama vile ndio mgunduzi pekee.Pia nilikuwambia kuwa CDM imekuwa dynamic sana kiasi cha kufanya CCM wawe off target.Ukaleta porojo na negation zako.Ila sasa unthibitisha kwa huo mfano wa Wangwe.
Naona unapenda create sense kuwa wengine wapo guilty ili uhalalishe porojo na kutaka nyamazisha wengine na habari zako kuwa una inside story.Hatuhitaji inside story katika vitu vinavyoelezeka ligically.Hayo mengine utayatoa kama mahakama inahitaji.

Mh.sikatai kuwa una uelewa mkubwa na pengine una list ya vyeti na awards nyingi sana.Ila haimaanishi kuwa uwe arrogant.Duniani imeshuhudia mengi sana yakiwapo ya waliodhani wamehodhi fikra na elimu kujikuta wengine wakifanya mamabo ambayo hata wao hawajui wamesoma wapi?Naona uanonyesha kutokuwa na tofauti na TBC waliokuwa wakidhani kuwa tasnia ya habari za redio na TV wao ndio wameshikilia, huku siku hizi kuna kitu kipya kinaitwa citizen journalism.
Na pengine nikwambie najua mengi zaidi ya unavyofikiria na siwezi kuandika hapa JF wala sijaambiwa na hata mmoja wao kuhusu mtu mwingine. Hizi ni habari nilizozipata toka reliable sources hata kabla sijajiunga na Chadema way back baada ya uchaguzi wa mwaka 2005.
Hakuna aliyekuuliza hayo hapa labda kama yanakuchoma kwa ndani na unajiskia yaanika ila sikushauri.Issue ni kuwa reasoning imekuwa problem kati yangu na wewe+ego uliyo nayo, unaweza aanika yote ila rationally bado ukawa hujajinasua ulipokwama kuliko sababishwa na approach zako kuhusu wengine.Mkuu usijisahau hujahodhi fikra za watu.
Hivyo naelewa source na mgogoro uliopo baina ya Zitto na uongozi wa Chadema na nimeweka wazi kabisa kwamba vimepikwa. Na hata wanapokosea iwe Mnyika, Mbowe au Dr.Slaa huweka wazi hapa JF simwogopi mtu wala sina ubia na mtu isipokuwa penye sifa zao huwapa sifa hizo. Nenda kasome mada nilizoanzisha kuhusu Zitto halafu unambie nategemea Chadema wanilipe nini ili niwape nini?..
Nilishakujibu na hiyo si kitu kipya sana amabcho hakijasemwa.Hapa issue ni kuwa Zitto anaonekana kuzama huko, sasa ni yeye ajitoe au apigwe chini.Sasa nini kinakushinda fikiria hapa mpaka urefushe thread kubishana na mimi?

Weather umekwepa risasi million or more, bado hakuzui risasi inayoelekea moyo wako isikuue?Ndio kama kuhusu huyo jamaa yako kama si wewe nae kafanya mengi kwa manufaa ya chama na nchi bado akiamua kufanya moja la kuua chama hakuna wa kumwachia.Mzee kuna practices hazifanyai kazi kama logic yako inavyokutuma.Dakatari anaokoa maisha ya watu wengi sana na kila siku ila siku akiua basi sheria humuadhibu.
Wewe unayerukia bandwagon ndio mwenye matatizo, na Nimesema kama hutaki unaacha mkuu wangu kuliko kuendelea kumpakaza Zitto wakati tunayajua makosa yake na wapi mnapika ili kuleta uhasama ndani ya chama ati afukuzwe? who the hell are you?.
Iam nobody mkuu.ha ha...ila ujue message sahihi si lazima itolewe na binadamu na wa whatever calibre unayodhani.Hata computer zinatoa message, mbwa nao huwa wantoa message.So angalia reasoning yako isiingiliwe na fikra zao, au hata hisia zako.
Hujanisoma mkuu.Zitto ni inspirational ,lakini haimaaminishi hapotei na hawezi sahihishwa hata na junior wake?Hii ndio elimu ya Kibongo ndio inakuongoza bila kujijua.Unadhani elimu ni one-way traffic.Nimekuwa clear sana kuwa simchukii mh. Zitto, na wala discussion haitaki jua kuwa ni kweli kuwa kafanya au lah, ila jinsi alivyojibehave katika hiki kipindi hakirishi watu na ndicho tunachokigombania hapa ila kwa vile .Kazi yako ni kumpa mbwa jina baya ili ummalize umekuwa ukijaribu play victim, accusse wengine kwa mambo mengi humu ,watu wanataka Zitto aface reality na si kuplay victim ,ajibu tuhuma kwa busara,aanze kujenga taswira njema katika chama kama kaona kafikia kikomo cha kukubaliana na mambo ya chama au hata anadhnai anataka hamia sehemu nyingine basi atoke bila kuchafua chama.Dunia ina watu wenye busara sana na sidhani kwanini Zitto asiwe mmojawapo kama mambo hayawork on hisi side?Wapo watu (mke/mume) ambao huachana na kuvunja ndoa in private wamesamaheana ila kwa jinsi walivyoichafua ndoa yao huwa wanaona kuwa si rahisi mambo kuwa the SAME AGAIN.na hivyo kuachana ila siku zote kauli zao ni very responsible, huwa wanalindana katika public hata wakitofautiana in private, huwezi msikia mmoja akirukia shutuma za uzinzi dhidi ya mwenzie na kusema kuw ahata mimi niliachana naye kwa suala hilohilo.Zitto anaonekana kuwa suala la Ukabila, sijui ukanda na Udini dhidi ya CDM halina uzito.Ni vigumu kwa mwanasiasa makini kutoona wingi wa watu katika CDM na hisia za nchi juu ya kutaka ukombozi kuwa ni very sensitive issue.Huko ni kuwa Irresponsible, hata kama baaddhi ya mambo anaamini yana usahihi fulani.Kuna vitu ni OK ila si right.
He has done things wrong, so were others na kinachohitajika ni kuelekezana sio kukashifu ktk vitu ambavyo huna ushahidi tena vimepandikizwa na watu wanaotaka kukivuruga chama. Shida yako nini hasa?..Unataka nikwambie makosa ya wengine, kwani wao ndio mada hii ama nachoweza kusema hata wao wanayafanya makosa ktk mada zinazowahusu, labda fanya kunitafuta humu JF utaniona sehemu kibao nachangia kwa mtazamo wangu na simwachi mtu.

- Nimemaliza, na sina haja wala sababu ya kuendelea na mjadala huu..

Kutuhumiwa tuu kwa mwanasiasa ni hukumu tosha ndugu yangu,na kutokuwa respnsible ni kama kukiri.Huo ushahidi mwingine ni mahakama ndio wanahitaji.Mi sishitaji kufuata historia yako kuhusu makovu ya kukwata usoni na shindoni ili nijenge wasiwasi na uaminifu wako(wasiwasi kuwa wewe unaweza kuwa mwizi).Cha kwanza na salama zaidi ni kulinda property zangu ,kwani kuanza ulizia ni kujiweka pabaya kwako na kwa jamii kuwa sikuamini na kukushutumu.Nilishasema tayari raia wengi na pengine viongozi wa cdm wana mashaka na Zitto katika vitu vingi na anayoyafany ain public yanaongeza uzito wa imani hiyo kuliko kupunguza kama mnavyoshindwa toa hayo.Imagine inchi watu bado wanaamini kuwa Nyerere bado ni rahisi, au hata Nyerere ni position ya URAIS hadi miaka hii ambayo mzee hayupo?Lini itafika habari kuwa kuwa Zitto hakueleweka?

Mkandara wala huhitaji kuwa milatant na mnazi kama wale watu ambao huwa wanajidai kuwa wanajua historia ya uhuru kuliko wengine, n ahivyo kunyamazisha wengine ili waweze pitisha agenda zao.

Mbona discussion nzima hahitaji court evidence, ni conventional wisdom tuu.Hizo evidence kibao au hata ujuaji unaoutaka nimeshakuonyesha mara nyingi kuwa si lazima sana katika mambo yanayohusu mitazamo na ushauri.

Mashukuru umesema mjadala ufe nami nilipenda sana ufe.Ciao
 
Let us wait and see. Please our movements should never ever be obstructed by things like that. In every generation there is a mision. Our mision and vision now should be change change change,it can be done and very soon.....play your part.
 
Huyo anayesema chama cha machame sasa kichwa hicho ni kichwa au matopr.? hawa ndio wale masabuli anasema wanafikiri kwa kutumia makalio,weka hoja yenye ujazo,wewe mwanaume bwana!!!!!!!!!!!!!!
 
Kumekuwepo na kupoteza muda kwingi humu nadni kwa vile hakun nia njema kwa kiasi cha kutosha angalia mambo kwa uhalisia.

Watu wanapiga kelele kuwa CDM ni chama cha kichaga hadi baadhi ya wasomi na wanajiita intellectual wanapotelea huko kwa vile hisia na chuku zimetawala. wengine wanadai kuwa kuwa na cha kidini.Wengine sijui ukanda ila wote wameingizwa na fikra na mchezo mchafu wa CCM.

Tungalie haya mambo kwa staili hii:
1.UKABILA--Kama CDM wangekuwa na Ukabila na Nia ya kufanya Hivyo nini kingewashinda hata kama CCM wangepiga kelele katika TV zote ,makanisa na na misikiti yote?Hakuna ubishi kuna wachaga walozezi nchi nzima na nje ya nchi kwa wingi.Hata sehemu baguzi wameweza lobby hadi "KUPATA MAKAZI YA KUDUMU NA KUKUBALIKA NA WATU MUHIMU KUFIKIA MALENGO YAO". Wanaweza fanya hivyo kufikia malengo ya chama na kabila lao.
-Wachaga wana share kubwa katika Media(magazeti, TV, radio, BillBoards, Printing etc , records za video na audio katika mabasi na ndege, achilia mbali nafasi za matangazo katika body za magari na ndege).

wachaga wana viwanda wanaweza fanya cultural brainwashing kwa wafanyakazi wao kama wafanyavyo waarabu kwa wafanyakazi wao.

-Wachaga wana mabaa yenye kujumuisha burudani nyingine nyingi katika maeneo hot katika miji yote na wilaya zote.

2.CDM NA UDINI.
- Wachaga wapo wengi sana katika makanisa, na wapo Wakristu wengi sana katika CCM yenyewe.CDM ingeweza tumia sana makanisa kuwashawishi wana CCM Wakristu kwa kuwapa mifano ya kauli za CCM zipingazo Imani yao.

-Wangekuwa wakijinasibu hivyo bila kificho, mbona akina Membe ,Sitta,Lowasa, Hata Rostam Aziz, na wengine wengi wameingia makanisani kwa fujo,kwa vile wanajua kuwa kupata access katika pool kubwa ya wapiga kura wakritu ni kupitia makanisa.Na waumini wana uwezekano mkubwa wa kuwamini wanaokubali imani yao.Na cdm wangeafanikiwa kwa vile viongozi wao wana mvuto binafsi (brand by themselves), achilia mbalia factors kama ujana, kuonekana ni wa kisasa katika dunia inayotamani vitu vipya

3.UKANDA. Wangetumia makabila ya ukanda wa Kaskazini kuchukua nafasi muhimu nchi nzima, kwa kutumia resources zote za watu wa ukanda wa kaskazini dunia nzima nahakuna ambaye angeweza zuia hilo.Propaganda nzuri za kuibua mashujaa wa Kaskazini, treasure za kaskazini, zingelainsiha sana view za watu wengine juu ya Kaskazini.Na baadaye kujenga tabaka la elites and favourites kutoka kaskazini.Hakuna asiyewakubali wachaga katika ujasiriamali.Hata wasiokuwa na elimu achilia mbali kutojua kiswahili kidogo sana achilia mbali lugha ingine kutoa kichaga.


KUHUSU WATU KUKWAMA JUU YA ZITTO.
CDM wanaweza mpiga chini Zitto kwa vigezo vy akawaida vya chama na hata kwa hivyo vya CCM(udini, Ukabila na ukanda),mbona ccm wameonyesha vyote hivi hadharani ila bado halionekani wala lalamikiwa?CDM wakiamua kuwa wakorofi wanamtoa na bado wakiamua kuwa wa sifa ZA CCM kuwa ni wakabila, Bado wanaweza weka mchaga mlowezi na kashika Jimbo.(mchaga akilobby vizuri wenyeji watagawanyika na wapo watakoukuwa na mifano hai ya mazri ya Mchaga kuliko ya Mzawa wa asili ingine).Wapo watu wenye asili ya kigoma wengi tuu wenye mafanikio binafsi na hawajfanya Kitu kwao zaidi ya kuwa wasaliti na wahofia kulogwa.

Arusha hadi waarusha waliwahi weka tambiko asiingie kabila ingine katika ubunge na umeya.Mbona wachaga wameshapatimba hadi wamechoka, na bado wana uwezekano wa kuingia kila uchaguzi ukiitishwa.

Uchina wanawaua sana waislam kuliko nchi yoyote inayotumia mitazamo ya kuhusisha dini na Ugaidi.Tena wanawaua kwa kiasi cha kuwaogopesha hadi wamarekani kuwarudisha nyumbani mara wanapoonekana kuwa hawakuwa na makosa ya kigaidi, kwavile China bado atakwenda waua kwa vile anawaona kama waasi.Israel wameweka wazi kuwa wanafanya lobbying ndania ya US, na wanafight kuhakikisha kuwa kura ya Veto ya US ipo kwa ajili ya matumizi yao.Nani kaweza zuia hilo?

Watu wanaoamini kuwa kama NIA ya kumpiga chini mh Zitto haiwezekani kwa sababu ya sijui kuwa Zitto ni smart,au kwa sababu anaweza lipua chama, au kwa sababu CCM watakuwa proved right(uzushi wa UKABILA,UDINI, na Ukanda) ni watu wanaoamini katika impossibilities na ni janga katika ukombozi.CCM wameinyesha na kuyatenda yote katik autawala huu n abado wan awananchi kiabo ambao wameamua kujidanganya kuwa hili si tatizo na pengine CCM waifanya kama kutania.

Kumchomoa Zitto weather kakosea au lah, kama kweli ni lengo la chama linaweza fanyika na mapema msmaji wa chama aktangaza kuwa jama kapigwa chini na kwa sababu za kubuni ilimradi ziendane na vitabia vyake vya karibuni.Mengine unayaacha jamii iyakuze kwa fikra za wasomi wetu ambao wengi ni rahisi kuwa programmed sana. Hata CCM wenyewe waliomtuma utawakuta wakiandika uozo wa kusupport CDM.Kauli kama "Wewe ni mkorofi na mbishi sana-Tulikuambia kuwa CDM ni chama cha udini,ukanda na Ukabila ukabisha". Masikio ya wananchi yatauwa yakisikia kuwa "jamaa ni mkorofi na mbishi ndio maana CDM wakamtoa" na kelele zake zitasikika kama kujitapatapata, na media nyingi kwa ujinga ua uelewa wataandika habari za kummaliza kwa nia ya kunfanya asibeke CCM kwa vile hakuweza vunja chama na kaisha kisasa na hivyo kujikuta wakihalalisha maamuzi ya CDM.

Naona watetezi wanazi wa Zitto hawawezi vuka mtego kama wa hii scenario. Kuwa Boss katika Public Office halafu ukaangukia katika mapenzi na Binti wa cheo cha chini sana kwako halafu ukatamani kumuoa bila kuingia katika matatizo na kabila ya kina bibi Malya na anilea Nkya kwa kutumia cheo chako vibaya na Kufanya udhalilishaji.Pia kujiaminisha kuwa binti naye hajakutumia kama Ngazi ya kukimbia ukali wa maisha unaobanwa mshahara kiduchu. Kiongozi jasiri anaweka mezani malengo, na vikwazo vya kuyafikia na rules ambazo hazipaswi kiukwa halafu unalianzisha.
 
Let us wait and see. Please our movements should never ever be obstructed by things like that. In every generation there is a mision. Our mision and vision now should be change change change,it can be done and very soon.....play your part.
Well said. Hapa najua hata Zitto atanichukia sana kwani my stance ni strong sana kwamba awajibike au hata awajibishwe. Kuna vitu hata mwenyezi Mungu kaviweka pamoja na adhabu zake.Yaani ukiamua kata shingo kienyeji kama unavyokata kucha lazima ufe.Ukizidisha mipaka aliyokuwekea katika kujiheshimu n akuheshmu amri zake lazima upate matukeo ya makosa hapo hapo.

Sasa kama Zitto anahamua kuwa irresponsible akaamua kujiweka katika suicidal Position kuwa Either Yeye or this generational mission (under M4C) sound stupid. Si mbaya CDM wakalink matendo yake na Destruction yake mwenyewe. Bus likipata mwendo, awe dereva, awe konda, awe abiria, auhata mhudumu , akitoke adirisha la mbele na kujirudhi ili akalizue basi kwenda ,basi takuwa kachagua kosa zuri kwani hukumu haina utata km angeamua kanyaga break moja kwa moja.Zitto hakutaka tumia tools(Party machinery procedures) za Basi kaamua Jump kupitia kioo cha mbele(public scene and arrogance) ili akazuie basi kwenda ambayo ni nzuri kuliko angerukia katika break na kusababisha ajali kwa wengine(Kucheza kama pandikizi).Ugumu wa task ni kwamba ka paly role iliyohitaji arrogance,uharaka na kwa vile hakuangalia uwezo wake kihalisia. Sasa arrogance na papara zilimfikisha mahali pa kugundua akiwa amechelewa kuwa yeye si kichwa hivyo ila kuna karama fulani aliyokuwa kitembelea katika CDM.Sasa ananing`inia dirishani kwa mbele ya gari si ashuke tuu akazuie gari.Kwa CDm wanaweka grill kwa ndani, game linakuwa kosa na adhabu kwa pamoja.Aokote vyote.
 
Adolay
Bado unajichanganya na falsafa zako,nahoji huo mtego wa udini unaotumiwa na CCM hoja yako haina mshiko kama ni suala la udini hata CCM yenyewe haitasalimika weka vithibitisho vya hoja zako ni vipi Zitto anahusika?

Chama
Gongo la mboto DSM
mkuu hapo unaitetea ccm ama unamtetea Zitto?
 
Nicholas, Lugha ya watu inache kama ilivyo, hujui maana ya Blackmail ama hujui matumizi yake.. Una balance nini kama hutangulizi ku Check yaani hata hueleweki unazungumza vitu gani. Unabwabwaja hovyo kana kwamba ukumbi huu unathamini maelezo mengi yasiyiokuwa na mpango, mbona ya Chacha Wangwe niliyasema toka mwanzo au hukusoma?. Mara nafanana na Pinda yaani sijui nilivyo Shallow, sijui na sound loosers, sijui hiyo loosers ndio nini kwangu na umelipata wapi?.. yaani basi nakuacha kama ulivyo! ama kweli kiingereza kimepata msemaji..
 
Let us wait and see. Please our movements should never ever be obstructed by things like that. In every generation there is a mision. Our mision and vision now should be change change change,it can be done and very soon.....play your part.
Ok basi nakubaliana na wewe mkuu.
JB WISER,kama humung'unyi maneno,na wewe ni mwanachadema,mbona sikuona mchango wako hapa?
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom