Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 16,315
- 33,809
Unajaribu kutuelekeza kule kwa akina CUF na Uamsho ambako kila asubuhi hushinda katika mikutano kumtukana Nyerere laanatulah. Wakimaliza hapo wanatoa idadi ya watu waliohudhuria mkutano baasi mambo safi.Mtaipataje Tanganyika bila kupinga hadharani fikra za Nyerere aliyeiuwa? Inatakiwa kwa dhati kabisa mseme wazi kuwa Nyerere alifanya makosa kuiuwa Tanganyika, hapo mtaeleweka, bila hivyo? itatumika fimbo ya Nyerere na fikra za Nyerere na nyinyi hamuwezi kuukubali ukweli kuwa alikosea. Sijui unafaham?
Leo mnatafuta pakutokea, kila ataekuja na lake mtalitafutia sababu, mara oohh Shivji hivi, mara Oooh Warioba vile, mara Oooh Kikwete vile.
Amkeni na mseme tu Nyerere alifanya makosa makubwa sana kuiuwa Tanganyika, mbona hapo mnapata kigugumizi?
Na bila kukataa fikra za Nyerere kuhusu huu Muungano mtatafuta sana scapegoat.
Sasa mnailaumu Zanzibar ndiyo inawanyima Tanganyika yenu? mimi naona Wazanzibari wanawasaidia sana kwenye hii cause yenu ya kuitafuta Tanganyika lakini nyinyi ndio msiojijuwa muanzie wapi. Upo hapo ulipo? Anzeni kwa kuzipinga fikra za Nyerere kuhusu huu muungano, hiyo ndio shortcut pekee ya kupazia malalamiko yenu. Ukipenda usipende hilo halikwepeki.
Kimachotokea Dodoma ni ushahidi, kwasababu wale wale wznz wanaopinga muungano ndio wamefyata na kwa kura ya wazi kuisaidia CCM.Akina Jusa waliosoma kwa Nyerere na wasiotaka muungano ndio wanaandika kanuni.
Ukiwauliza hasa wanataka nini huwezi kupata majibu yanayolingana, kinachowaungnisha ni matusi dhidi ya Nyerere.
Kusimama na kusema Nyerere alifanya makosa hakuleti jibu la tatizo.
Ukweli wa kwamba CCM wanaficha mkataba unaeleza vema kuliko kutukana.
Kikwete anamkono wake kwa hili tena mkubwa tu.
Ameshindwa kusimamia dhamira yake akiongozwa na njia mbili.
Warioba kasema alichosikia kwa wananchi, historia itamhukumu kwa ukweli huo
Shivji, ah kanishangaza aliposema msingi wa muungano ni kugawana madaraka.
Akala matapishi ya maandiko yake.
Tunachosema ni kuwa Tanganyika itazinduka, hapo kila mtu atabeba mtoto wake.
Ni muhimu kuieleza Tanganyika kuliko kutumia akili na nguvu kumtukana Nyerere.
Hayupo na wala hatarudi na jibu.
Kumtukana ni kuridhisha nafsi kwa uongo, ni kuficha shati halafu uliibe mwenyewe.
CUF na Uamsho wanaweza, wengine hatujafika walipo na hatupendi kuelekea huko.
Si kila njia inaenda pema, nyingine zinaelekea porini au chooni.