Shivji: Mimi ni muumini serikali mbili

Shivji: Mimi ni muumini serikali mbili

Ukifuatilia bunge la katiba utagundua hakuna mtu anaetajwa na wajumbe kama Issa Shivji...wanatumia vitabu vyake wanamshambulia wanamtuhumu wanamsifia najiuliza tu why wasimuite akazungumza nao na wakamueleewa? Hakuna kanuni inayoruhusu hilo?

Kuna mtu anaitwa Chabruma ni mjumbe wa jf anaehudhuria vikao vya bunge mjengoni, huenda akatusaidia kufikisha wazo hili kwa mwenyekiti 6 kisha tukapata majibu ya uhakika.
Chabruma pita hapa tafadhali ni muhimu sana.
 
Last edited by a moderator:
Kuna mtu anaitwa Chabruma ni mjumbe wa jf anaehudhuria vikao vya bunge mjengoni, huenda akatusaidia kufikisha wazo hili kwa mwenyekiti 6 kisha tukapata majibu ya uhakika.
Chabruma pita hapa tafadhali ni muhimu sana.

Yaani itasaidia sana
 
Last edited by a moderator:
Ukifuatilia bunge la katiba utagundua hakuna mtu anaetajwa na wajumbe kama Issa Shivji...wanatumia vitabu vyake wanamshambulia wanamtuhumu wanamsifia najiuliza tu why wasimuite akazungumza nao na wakamueleewa? Hakuna kanuni inayoruhusu hilo?
Wakamuelewa? Una maana gani mwenzangu...kwamba wajumbe wa BMLK wameshindwa kumuelewa Shivji na hivyo apewe nafasi ya kutoa ufafanuzi! Ili iweje, aweze kujitetea? Kama ni hivyo sioni kabisa mantiki ya huyo mnafiki kuitwa labda kama hiyo nafasi watapewa wote wanaotajwa kwenye mjadala...naamini wa kwanza kabisa anayehitajika kupewa nafasi hiyo ya kutoa ufafanuzi ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume Mh. Jaji Sinde Joesph Warioba. This would probably make more sense, not Shivji.
 
Njoo msikilize mbunge wenu anasemaje: [h=1]Topic: Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu![/h]
Nimemsikiliza....ila kwa akili yako unadhani alisema mliyokuwa mnawaza...Lissue hakumtukana Nyerere wala kumuita mwongo..aliita CCM kwa ujumla waongo...Lissu alisema Amri na uvunjaji sheria wa Nyerere,ila hakusema jitihada za Nyerere kuficha ukweli..km alikuwa na amri sidhani km angechagua njia ya uongo zaidi ya Amri hiyo hiyo kuzimisha....so usidhani sana km anakusupport
 
Wakamuelewa? Una maana gani mwenzangu...kwamba wajumbe wa BMLK wameshindwa kumuelewa Shivji na hivyo apewe nafasi ya kutoa ufafanuzi! Ili iweje, aweze kujitetea? Kama ni hivyo sioni kabisa mantiki ya huyo mnafiki kuitwa labda kama hiyo nafasi watapewa wote wanaotajwa kwenye mjadala...naamini wa kwanza kabisa anayehitajika kupewa nafasi hiyo ya kutoa ufafanuzi ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume Mh. Jaji Sinde Joesph Warioba. This would probably make more sense, not Shivji.

Chadema mtu akitofautiana na nyinyi tu mnafiki
 
Chadema mtu akitofautiana na nyinyi tu mnafiki

Mkuu, kwani chadema pekee ndo inachukia wanafiki? Ulianza uzi vizuri ila unataka kuuchomekea mambo ya uchama na ukifanya hivyo utaupotezea mtiririko wake. Shusha hoja kwa hoja uzi utakua na faida kwa wengi.
 
Ili nini sasa ?Ili Bunge nalo liandike riwaya badal ya katiba km zake...
 
Ili nini sasa ?Ili Bunge nalo liandike riwaya badal ya katiba km zake...

Nicholas kwema lakini? Hujasalimia watu, hujapumzika tayari unafika na pumzi ndefu unaanza kubamiza maswali! BTW endelea kumsoma mleta mada utaelewa tu au ngoja nimstue akupe ufafanuzi, The Boss ufafanuzi kwa mjumbe tafadhali.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu UKAWA hawatakubari maana Prof Shivji alishatoa msimamo wake ktl group la maprof pale Chuo kikuu na akaelezea history ya muungano na kusema takwimu na hasara za serikali 3, akasema hata mataifa ya nje yatatushangaa hilo wazo tumelitoa wapi.
 
Nicholas kwema lakini? Hujasalimia watu, hujapumzika tayari unafika na pumzi ndefu unaanza kubamiza maswali! BTW endelea kumsoma mleta mada utaelewa tu au ngoja nimstue akupe ufafanuzi, The Boss ufafanuzi kwa mjumbe tafadhali.
Kwema mkuu..huyo boss wala usijisumbe siki atakavyokuja..kwanza alivyoweka habari yake km vile anaamini kuwa Shivji kanyimwa haki ya kujitetea na akienda atafunika....km vile anaamaini atakwenda jisafisha na kuendelea na riwaya zake.......mbona bunge lilijadili sana Mapanki na skendo ya silaha na hawakumuita..?Pia Kagame hawakumuita ila walimsema sana..
 
Last edited by a moderator:
Kwema mkuu..huyo boss wala usijisumbe siki atakavyokuja..kwanza alivyoweka habari yake km vile anaamini kuwa Shivji kanyimwa haki ya kujitetea na akienda atafunika....km vile anaamaini atakwenda jisafisha na kuendelea na riwaya zake.......mbona bunge lilijadili sana Mapanki na skendo ya silaha na hawakumuita..?Pia Kagame hawakumuita ila walimsema sana..

teh teh teh, mkuu mi umenifumbua macho.
 
teh teh teh, mkuu mi umenifumbua macho.
umemwona tena...wapo busy wanataka msafisha km walivyojitahidi kwa zitto ili aweze tumika..si unajua wamewekeza sana.Mbona warioba hawakuomba?
 
Njoo msikilize mbunge wenu anasemaje:

[h=1]Topic: Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu![/h]

Kinachonisikitisha na kunishangaza zaidi ni pale CCM wanapotaka kuwaaminisha watanzania kwamba uwepo wa serikali 3 (serikali ya Tanganyika, Zanzibar na MUUNGANO) eti ni kuvunja muungano. Muungano utavunjikaje wakati katika hizo serikali 3 imo serikali ya Muungano? Hivi hawa INTAHAHAMWE hawana haya? Mtaji wa hawa watu ni ujinga watanzania. Ndio. Eti watanzania wanaaminishwa uongo huo nao wanaukubali!

Hivi jamani mtu ukiwa na nyumba yako ambayo haikidhi mahitaji, ukiamua kuifanyia renovation au ukaibomoa na kujenga nyumba mpya kubwa, imara na bora zaidi, tatizo liko wapi? Ni nini hofu ya CCM katika uwepo wa serikali 3 hadi waanze kuwatisha raia kwamba ikiwa serikali 3 zitaruhusiwa jeshi litachukua nchi? Kama ndivyo basi, sisi raia tunaoteseka chini ya utawala wa CCM tunakaribisha jeshi lije litawale badala ya kuendelea kuishi ndani ya utumwa wa serikali ya CCM.

Watu hawahawa waliwaaminisha watu kwamba vyama vingi vikiruhusiwa, nchi itaingia vitani kama ilivyowahi kutokea huko Rwanda. Walifikai hatua ya kutembea nchi nzima wakionyesha mikanda ya vita ya Rwanda na intarahamwe ili kuwatisha wananchi kuhusu ujo wa vyama vingi. Hatimaye vyama viliruhusiwa na hatujawahi kuona nchi ikiingia vitani. Ama CCM wamezoea kuishi kwa UWONGO, ukweli hawauwezi!
 
Mkuu UKAWA hawatakubari maana Prof Shivji alishatoa msimamo wake ktl group la maprof pale Chuo kikuu na akaelezea history ya muungano na kusema takwimu na hasara za serikali 3, akasema hata mataifa ya nje yatatushangaa hilo wazo tumelitoa wapi.
SHIvji.km zitto, kitila mkumbo etc wanoongozwa na fikra za lumumba wanachagua upande mbaya sana wa historia...
 
Wadau kuna wakati vyombo mbalimbali vya habari viliripoti juu ya mhadhara wa profesa issa shivji na wanafunzi wa vyuo vikuu (udsm) ambapo pamoja na mambo mengine mapendekezo ya serikali tatu yaliyopendekezwa na tume ya jaji waryoba yalipingwa vikali.

Mimi nikiwa ni mmoja wa wanafunzi wa udsm, napenda kuweka wazi kuwa siku hiyo walioruhusiwa kuingia ni vijana wa ccm tu. Na kwamba hata pale wasio wanaccm walipobahatika kupata taarifa juu ya mhadhara huo hawakuruhusiwa kuingia ndani coz waliombwa kuonyesha kadi zao za ccm na kwa vile hawakuwa na hizo kadi walizuiliwa kuingia.

Ninamshangaa mtu kama Profesa Shivji kutumika vibaya kiasi hiki.

Naomba watanzania waendelee kuiamini udsm kwa kuzingatia kuwa wanaccm (kenge) hawakosi katika msafara wa mamba (wasomi makini) hapa udsm.

Nawasilisha.
 
Zamani nilikuwa nasikia tu ujinga wa aina hii kwa baadhi ya wahusika udsm, sikuwa nimeamini kwa kiwango cha juu sana, lakini kwa sasa naamini asilimia mia kuwa kuna wasomi wanatumiwa sana hadi kuweza kukana hata wanachokiamini baada ya kukifanyia tafiti zilizotumia hela nyingi sana tena hela hiyo inaweza kuwa ya walipa kodi
 
Wanamatumbo makubwa, lakini WANANJAA KWELIIIIIIIII........
 
Back
Top Bottom