Shirika gani lilikufa na bado linakuuma?

Shirika gani lilikufa na bado linakuuma?

You sure want me to cry Natalia!tena mkate ulikuwa bomba ule!

ule mkate ulikuwa unatengenezwa na National Milling Corporation (NMC).. ule mkate ulikuwa ni noma ali.. unaweza ukaula mkavu mpaka ukaisha na ukautafuta mwingine..
 
Last edited by a moderator:
TANGANYIKA PACKERS
DSC_3206[1].jpg
Ukizungumzia Nyama/MEAT Dar enzi hizo hapa ndio ilikuwa kila kitu,,Machozi yananitoka
 
Pamba Engineering ya Nyakato Mwanza, KAURU, RUREKU, kuna hii kitu ilikuwa inaitwa NGOMATI pale Songea ilikuwa full umbaku, Relwe, TITIKOO, RTC
 
ule mkate ulikuwa unatengenezwa na National Milling Corporation (NMC).. ule mkate ulikuwa ni noma ali.. unaweza ukaula mkavu mpaka ukaisha na ukautafuta mwingine..
We acha mkuu!mbona maumivu tu yaliyobaki!
 
Wana bodi najua wengi wenu mnakumbuka baadhi ya mashirika yalifilisiwa na mengine kubinafisishwa kwa bei ya chee!mfano NBC namengineyo mengi!ila mimi nakumbuka mashirka kama NASACO,TANGANYIKA PAKERS,TACOSHIL;MANG'ULA,FAIBERBOARD,GENERAL TYRE,na mengineyo!mimi lina niuma GENERAL TYRE je wewe?

aisee KakaKiiza mie nilisononeka sana pale viongozi wetu walipokubali kukiua kiwanda cha kusafisha mafuta (TIPPER).. maumivu yote tunayoyapata sasa na mfumuko huu wa bei umechangiwa kwa kiwango kikubwa na kuuliwa kwa kiwanda kile.. Nakumbuka wakati ule yanaletwa mafuta machafu.. yanasafishwa hapa hapa kwa gharama ndogo na ndani kupata sampuli kama tano hivi.. Ninaamini kabisa kama TIPPER ingelikuwako bado kusingelikuwa na gharama kubwa ya mafuta kama leo.. Ulikuwa ni uhaini wa kiwango cha juu.. Ndio maana Mwalimu alisema kama mtu akikupa mawazo ya kijinga na wewe unajua kwamba mawazo aliyokupa ni ya kijinga na ukayakubali basi atakudharau sana.. Leo tunadharauliwa mno.. foreigners wanajua chochote watakacho Tanzania watakipata.. Loliondo ni mfano mwingine wa wazi kabisa..
 
Last edited by a moderator:
Relwe na mabasi yao nikikumbuka inaniuma sana,nyumba za wafanyakazi pale Iringa zilikuwa za kisasa
 
E bana basi nimeUtafuta sana huo mkate mikoani bila kuupata kumbe kiwanda kushney!tena siha wa arusha ilikua balaa
 
Mimi kcu inaniuma sana wazee walipigishwa shule leo hii wanakula wameshindwa kurudisha fadhila kwa kurivive hili shirika ili wakulima wasomeshe na watoto wengine. So sad

BCU/Balimi!!! -----------so sad RIP
 
Mimi naona walifanya makosa sana maana tulikuwa na viwanda vingi sana na ilibidi tukae tuandae mpango kazi wakubinafsisha kuliko tulivyofanya sasa hivi na hii ndo ilisababisha kifo cha Mwalimu Nyerere...............Hataari sana mfano Tanganyika Peckers walimpa Admijee akang'oa mashine zote motor na akafanya kiwanda ghara sasa maana ya kubinafsisha ilikuwa kuwapa watu wenye uwezo kuboresha zaidi siyo kubadirisha matumizi maana baada ya serikali kujitoa rasimi katika maswala ya kuendesha uchumi kwa kuendesha shughuli za uzalishaji!Kama mimi nakuwa rais ninawawajibisha wote waliohusika na kuhujumu taifa hili hasa katika mchakato wakubinafsisha mashirika!!

sasa hivi wamekuja na hii kitu inaitwa Export processing zone(epz). cha ajabu ni kuwa wamegeuza kuwa magodown wakikodishia wachina na wahindi na sasa inegeuka ni Import na sio export.
 
Tanganyika packers iliniuma sana, tena aliyeiua akaanza na zereu mia-mia

nchi yenye wafugaji na mifugo ya kutosha tumekua hovyo kabisa
 
Back
Top Bottom