KakaKiiza
Platinum Member
- Feb 16, 2010
- 11,947
- 9,460
- Thread starter
- #81
Lakini hao hao waliokuwa nyuma ya mpango huo wakapewa uwaziri mimi sijui hii nchi hakuna wenye maono au mtu akiisha ingia pale magogoni basi mipango yote inavurugika??maana hata kwenye kampeni na utendaji tofauti!!aisee KakaKiiza mie nilisononeka sana pale viongozi wetu walipokubali kukiua kiwanda cha kusafisha mafuta (TIPPER).. maumivu yote tunayoyapata sasa na mfumuko huu wa bei umechangiwa kwa kiwango kikubwa na kuuliwa kwa kiwanda kile.. Nakumbuka wakati ule yanaletwa mafuta machafu.. yanasafishwa hapa hapa kwa gharama ndogo na ndani kupata sampuli kama tano hivi.. Ninaamini kabisa kama TIPPER ingelikuwako bado kusingelikuwa na gharama kubwa ya mafuta kama leo.. Ulikuwa ni uhaini wa kiwango cha juu.. Ndio maana Mwalimu alisema kama mtu akikupa mawazo ya kijinga na wewe unajua kwamba mawazo aliyokupa ni ya kijinga na ukayakubali basi atakudharau sana.. Leo tunadharauliwa mno.. foreigners wanajua chochote watakacho Tanzania watakipata.. Loliondo ni mfano mwingine wa wazi kabisa..
Mfano shirika kama ATC kulikuwa na na aja ya kuunza njia au kuingia ubia na Alliance air??tena yanakufa tukiyaona hivi hivi!
Mimi nilienda national service nikawa na jamaa mmoja alikuwa meneja pale sokoine drive alikuwa akiniadithia mipango ya THB nikajua nitakuwa na nyumba karibuni!!Aliitwa BRUCE NYAMWANGI.R.I.PBRUCE!Nilivyo ingia uraiani nakuta hata benki hakuna watu wana haha kutafuta kazi eti shirika limeuzwa!KakaKiiza ninaikumbuka Bank ya Nyumba Tanzania.. ninaikumbuka Matsushita.. Phillips.. Kiuta.. Metal box.. kiwanda cha kutengeneza mabox cha kibo..
Hii ikifa nachinja Ng'ombe 2 japo sijawahi kuchinja!CCM inaniuma sana hadi leo!
Wewe unaanzisha kitu ndani ya CCM UNAONDOKA UNADHANI KUNA MTU WAKUSIMAMIA HUKO NYUMA??sasa hivi wamekuja na hii kitu inaitwa Export processing zone(epz). cha ajabu ni kuwa wamegeuza kuwa magodown wakikodishia wachina na wahindi na sasa inegeuka ni Import na sio export.