Ndugu zangu katika hali ya siasa sijawahi kumuona mtu asiye na adabu wala hekima kama Shibuda. Shibuda alianza kwa kumtishia rais Jakaya kuwa angeweza kugombea na kumuondoa katika utawala ndani ya ccm. Baada ya kuona kuwa anaota ndogo za alasiri,aliamua kuchanga hela ya kumchukulia mh.rais fomu za kugombea urais. Shibuda aliamua kuhama ccm kwa kukejeli na kurusha vijembe vya ajabu ajabu kwa mwenyekiti wake wa zamani mh.Kikwete,akaenda chadema akapata ubunge. Alipoambiwa afuate masharti ya cdm ya kuisusia hotuba ya yule aliyesema hana uwezo wa kumuongoza na kuliongoza taifa,bado akaendelea kukataa na kuhudhuria. Pia akaudhuria sherehe ya kumwapisha waziri mkuu wakati chama chake kilipinga. Akaja katika maandamano ya cdm akawaponda na kuwadharirisha mh.Nape, mwakyembe na mzee sitta kuwa ni wanasaliti,wanafiki na ndumila kuwili kwa kuwa ni wanachama na waanzilishi wa CCJ. Watu wakajua siri nyingi zilizojificha katika nyoyo za wanaccm hawa. Pia kawaharibia uaminifu na uadilifu katika ccm. Kama haitoshi Shibuda alipewa ilani ya chadema ambayo pia ndani yake inayokataza kuwa na posho zisizo na mashiko pamoja na kuyakataa mashangingi,kama 'punguani' ameenda bungeni na kupinga hadharani na anataka posho ipande. Cha ajabu hata ccm kupitia waziri mkuu wameweka wazi kuwa posho zitaondolewa au kuunganishwa na mishahara ili ikatwe kodi. Sasa Shibuda anaipinga cdm akiwa ndani na anaipinga ccm akiwa nje,alaf anadai vyama vingne ni mamluki,je shibuda anasimama wapi? Kwa kumpinga Zitto na mbowe,nape,jk,6,mwakyembe,sasa anataka tuone kuwa yeye tu ndo yuko msafi??! Chadema ichukueni kadi ya shibuda muiweke makumbusho. Shibuda hatapata mwenyeji mwingine kwa tabia zake za ajabu. Kabla hapajakuwa na harakati za kudai haki sawa,zamani wazee wetu wangesema Shibuda ana tabia za kike. Ila kwa kuwa ishaonekana sio sahihi kuwasema wanawake,basi hata mi sitasema ivo. Shibuda kama ni mti basi ni mpapai,hafai kwa kujengea,hafai kwa kuni,hafai kwa kuchomwa hata mkaa,zaidi hatofaa hata kujengea daraja. Siwezi kumuita shibuda mamluki ndani ya cdm ila namuona kama mtu anayekosa malezi na kuota sharubu. Chadema muweke kando uyu mtu,arudishe kadi,turudi kwenye uchaguzi ili hata ikiwezakana twende maswa kama ccm na cdm kuwaomba wananchi kura bila ya kuwa na shibuda. Mwache aende kama mgombea binafsi au hata ajiunge chama cha tatu kama watamwitaji. Taifa lisisumbuke na mtu uyu maana alipotoka ccm tukajua labda kachoshwa, kaenda ccj hakukaa,kaja cdm na sasa analeta maajabu. Iyo inaonesha kuwa yeye ndo mwenye vilema. Chadema mfukuzeni Shibuda.