Shibuda aishangaa demokrasia ya CHADEMA

Huyu shibuda akifutwa uanachama litakuwa fundisho kwa wengine....anachofanya Shibuda ni kupingana na ilani ya chama,huu ni sawa na uhaini kwa chama
Mkuu!!!
naogopa sana kusema kwamba WATANZANIA wanafuata WATU na si VYAMA!! Huenda akifukuzwa akaondoka na WATU WAKE!!! na inawezekana sana watu HAO ndio MTAJI kwa CHAMA!!! Naogopa sana PICHA ya aina hiyo!

NDIO MAANA NIMEWAHI KUSEMA NA KUWAUNGA MKONO WALIOSEMA "BADO HATUJAWA NA WANASIASA MAKINI NA VYAMA MAKINI VYA SIASA VYA KUIONDOSHA CCM MADARAKANI!"

Ndio maana vyama vyetu vinashabikia mamluki wanaokuja bila kutazama madhara yake...
 
Ndugu zangu, kuna watu wanasema Shibuda afukuzwe wengine wanasema asifukuzwe. Mimi naona asifukuzwe kwa sababu zifuatazo:

A. Akifukuzwa huenda kanda ya ziwa nzima ikaichukia Chadema kwa kuwa kanda ya Ziwa ni theluthi moja ya wapiga kura wa Tz.

B. Akifukuzwa huenda watu kama kina Wenje na Prof Kahigi( Wasukuma) wakakwazika na wakaamua kuchukua maamuzi yatakayokiumiza chama.

C. Akifukuzwa akaenda CCM na kufanikiwa kupata jimbo tena atakuwa amepata sababu ya kuiandama Chadema zaidi ndani ya bunge na CCM watamshangilia zaidi kwa kuwa atakuwa ameijua zaidi Chadema.

D. Akibaki Chadema huenda akawa na madhara kidogo kuliko kuwa nje ya Chadema. La msingi ni kuenda naye taratibu hadi 2015 kisha Chama kitafute candidate mwingine.

E. NCCR-Mageguzi iliparaganyika baada ya kuanza kufukuzana viongozi.
 
Wakati wa hotuba ya rais kufungua bunge hakuwa ndani., kwa hiyo hakuungana na wabunge wenzake kutoka nje. Kwenye hafla iyosusiwa ya kumsimika waziri mkuu alikuwepo jioni. kwenye maandamano yote yaliyo fanywa na CHADEMA mikoa yote wala shibuda hakutajwa wala kuonekana. Kupitisha budget Shibuda hakusema ndiyo wala hapana . hakuwepo tena. Juzi ametetea posho ambayo ni haramu kwa chama chake.

Sasa: ADHABU YA KUMTIMUA CHADEMA ITEKELEZWE MARA MOJA ILI ASIENDELEE KUTUMIWA NA MAGAMBA. MAMULUKI HUYU NI WAKUOGOPA KAMA UKOMA.
 
Jaman huyo Shibuda alizoea ccm bongo lala CDM hawez afu anakua kama mzigo kwa wenzake.Muda mwingine ni vyema kujitambua kabla hujajoin mahali husika
 
Naomba ni shauri kitu kidogo ambacho ni kwa manufaa ya CDM na wapenzi wa Demokrasia, nakubaliana kwa asilimia mia moja kwamba anao uhuru wa kutoa maoni yake na kwamba katika mfumo mzima wa ujenzi hoja za chama hawezi kukidhuru chama kama mambo yake yataonekana hayana maana na hakuna wa kuyashughulikia. Hata hivyo kinyume chake ni hatari zaidi kwa chama. Kumshughulikia kwa kosa ambalo chama hakijafanya maamuzi ya pamoja ni kosa la jinai kisiasa. Kwa nini tunataka Shibuda awe ajenda humo ndani? kwa manufaa ya nani? nimewahi kuona serious bypartisan politics in developed demokracy na nikashuhudia mbung mmoja kwa wakati fulani akipigia agenda ya chama kingine kwa wenzetu it has never been an issue, ndiyo maana ya uhuru mpana wa kutoa maoni kwa wabunge. Iwe marekani au Uingereza chama kimoja kujaribu kulazimisha Wabunge kufanya maamuzi kinyume na maono yao ni kuminya demokrasia. Chama kinahitaji kwaelewesha wabunge wake kusimamia yale ambayo chama kinayapigania ikitokea ana mani tofauti that diffrences must be respected and encouraged by every advocate of freedom of expression.
Hili la Shibuda siyo issue kwa cdm
achana naye

Point nzito sana hii, na wana CDM wanatakiwa waoneshe kweli CDM ni tofauiti na CCM... Juzi hapa U.S congress ilipitisha resolutions juu ya Libya, moja ikapita na ingine ikawa blocked. Moja iliyopita ni kusupport funding kwa majeshi na U.S operations in Libya na iliyokwama ni kutambua rasmi ushiriki wa majeshi ya marekani Libya. Na votes ukizitazama closely, utaona kuna wabunge waliovote across their party lines na haijawahi kuwa issue. Actually kwa resolution iliyokwama wabunge 70 wa chama anachotoka rais Obama walipinga despite hillary clinton kuwapa "seminar" juu ya umuhimu wa kusupport resolution.

Sasa kama CDM wako mstari wa mbele kudai katiba mpya, moja ya mambo yanayopigiwa kelele ni hii ya ubunge wa mtu kuwa mali ya chama badala ya wananchi waliomchagua jimboni. Nadhani ni wakati wa CDM kujenga ngozi ngumu na kujitofautisha na CCM na kutolerate such changamoto ambazo soon zitakuwepo kwenye katiba mpya.
 
huyu jamaa anauchu wa madraka ndo mana alivyopotezewa maswa kwenye kura za maoni
akajitupa cdm wala hakuwa na nia ya dhati ya cdm soo inabidi wampotezee km wanaona
analeta mambo mbofumbofu
 
Imefika muda sasa Wasukuma kutoka kanda ya ziwa kuachana na CDM chama cha kikanda na kikabila, Shibuda ananyanyashwa kutoka na Usukuma wake angekuwa ametoka kaskazini wala usingesikia maneno yoyote ya kashfa! Shibuda nakushauri ili swala kawashitakie wazee wa Kisukuma kama ulivyomshitaki Wenje, kwa wazee wa Mwanza na wazee wakakuelewa kama Wenje ni Mkenya hawana tena shida nae amalize kipindi chake aende zake kwao Kenya, Wasukuma mnaona mnavyodharauliwa na CDM.Mbona kina Selasini wanaipongeza CCM kila siku ata siku moja hawajaguswa au kwa sababu ni Wachagga!.

when i joined this forum,JUST YESTERDAY, I made a promise not to argue with NON THINKERS, unfortunately I couldn't resist lol - I didn't know that WASUKUMA are from the SOUTHERN Tanzania(and this explains all about your void, i think i have to go back to school!!!
My Prof. used to tell me never discuss anything with fools as they will let you fly low where they used to and eventually they'll defeat you with their flying low experience, absit iniuria verbis Mr. Ritz!!! My Prof didnt know that some fools do not fly at all and Ritz is a living example!!!
I apologize to my mind for engaging in this useless conversation with a far useless person like Ritz!!!!
 
Shibuda is playing 'ignorance'! Anajua anachokifanya wala asijidai kushangaa. Kama kuna mtu alikuwa anajiuliza kwa nini hii nchi ni maskini basi jibu ni kwa sababu ya watu kama Shibuda. Watu wanakabidhiwa madaraka ya kusimamia rasilimali za nchi na ustawi wa umma lakini wanaamua kwa makusudi mazima kuwa walinzi wa mali za umma. Hivi Shibuda anasimamia nini? maslahi ya wapiga kura wake au ustawi wa 'waporaji'?
 
chadema ni chama makini na kina watu makini na wenye upeo mkubwa wa kusoma mambo na matukio mabalimbali. kutokana na sifa hizo naomba uongozi wa juu wa chama ukae mapema na kutoa azimio la kumuondoa shibuda ndani ya chama kabla hajajenga mizizi nadani ya chama kwa manufaa ya chama. hatua zinazochukuliwa kwa madiwani waliochakachua msimamo wa chama arusha,zitumike kumuwajibisha Shibuda.
 
wewew ni mchovu tu tunakufahamu,hao wazee wa kisukums na mipasho ya kizaramo wapi na wapi?kama ni vijana ndani ya cdm wanao wa kutosha.umezoea mipasho ya kwenu na hiyo mipasho ndiyo iliyotufikisha hapa tulipo .chadema ni kiboko yenu na vibaraka mnaojaribu kuwaingiza humo watatemwa na mfumo chadema.habari ndio hiyo.
CDM ingekua kiboko ya CCM mngepata majimbo ya kutosha lakini kati ya majimbo 239 mlipata 26 pamoja na huyo Shibuda! Na mgombea wenu wa Urais yule Mzinzi akapigwa na JK!
 
Nina hamu sana kusikia wasaliti wa sera mbadala za wananchi wakichinjiwa baharini...

Mimi binafsi simkubli Shibuda toka amehamia CHADEMA. Ni mtu mwenye jazba, hasira, mropokaji, mswahili halafu top in top ni
mpenda madaraka saaana.

Asije akajidanganya kuwa Shinyanga wamechagua mtu. Wale wanachagua jembe lolote toka CHADEMA hata akiwa bwana Eliesikia ndio anaomba kura. Majimbo 8 Manne CHADEMA, Moja mjini liliharibika na CCM matatu(moja la jembe Lembeli).

myVision:
Mi ninachotaka CHADEMA wasimung'unye maneno wala kufinyanga hiyo kesho au kesho kutwa baada ya kikao tumpe Tiketi apotelee mbali.
Tuacha woga lile jimbo tunashinda sisi kama sisi CHADEMA.
 
unajitahidi kufitini ili CDM iingie kwenye mgogoro usio wa lazima lakini utashindwa tuuuuuuuuuuuuuuuuuuu aliyekuajiri kwa hilo ameula wa chuya CDM wanayo mambo makubwa ya kushughulikia siyo hilo la Shibuda. CCM waanze kufukuza Mwakyembe, Sita na Mnauye
 
"Nitashangaa kama nitaitwa na kiongozi yoyote wa kambi yetu ya upinzani au Chadema kwa tuhuma za kutoa maoni yangu huru niliyoyatoa bungeni jana (juzi), hata nilipokuwa CCM nilipenda kusahihisha palipokuwa na makosa"."Sitarajii Chadema kuna viongozi wanaweza kudidimiza demokrasia na uhuru wa kutoa maoni, wakati chama kinafanya maandamano kutoa maoni huru kwa Watanzania. Kama mimi sitakiwi kutoa maoni huru basi hakunaslahi binafsi, tutambue kwamba mbunge anapozungumza bungeni anasema kwa maana pana kwa watu wenye mitazamo tofauti kwa lengo la kuleta fikra endelevu".Alisema kwamba hana habari kama wabunge wote wa Chadema walikutana na kukubaliana kuikataa posho ya vikao vya Bunge.Shibuda akifafanua zaidi suala hilo la posho japo kwenye Ilani ya Uchaguzi wa 2010 ya chama chake ilitaka kupunguza posho hizo za vikao pamoja na mshahara wa mbunge, alisema, "Ilani ya Uchaguzi ni mpango kazi wa kuendeleza programu ya chama kilichopo madarakani, kwa hiyo hivi sasa hapa bungeni bila kujali itikadi zetu wabunge tunaunganishwa na programu ya kuendeleza nchi, utawala bora na uongozi wa kuongoza fikra za Watanzania". Add this page to your favorite Social Bookmarking websites Sijui!! Lakini kuna ka ukweli hapa na ndio maana wakubwa wa humu (Jamii Forum) hamleti mjadala![/QUO Huyu bwana inaonekana haendani na wana Cdm mana haiwezekani akaenda tofauti na msimamo wa chama,wamtimue tuu
 
Mjadala huu umeongea makosa makubwa ya Shibuda kuwa: Hana ushirikiano wa pamoja na wenzake, he is not well informed of what is going on in CDM, Anatoa msimamo tofauti na chama chake, ni CCM akifanya upelelezi CDM, Hahudhurii vikao vya chama/wabunge wenzake na anabwabwaja nje tu


Ambacho sikukiona na hoja muhimu aliyoisema shibuda katika habari kuu kwamba….
- Atashangaa sana na hatarajii kama CDM kuna viongozi wanaweza kudidimiza demokrasia na uhuru wa kutoa maoni huru, wakati chama kinafanya maandamano kutoa maoni huru kwa Watanzania. Kama yeye hatakiwi kufanya hivyo, basi nini maana ya kuandamana kutoa maoni kwa Watanzania".
- Mbunge anapozungumza bungeni anasema kwa maana pana kwa watu wenye mitazamo tofauti kwa lengo la kuleta fikra endelevu".
- Hana habari kama wabunge wote wa Chadema walikutana na kukubaliana kuikataa posho.

Nikiongelea highlights hapo juu, Moja: Je Demokrasia inayopiganiwa na CDM ni ile ya uamuzi wa (Chama) wa pamoja au ile ya mtu kuwa huru kutoa mawazo kwenye mambo yanayoathiri maisha yake? Pili: Je Shibuda ni mbunge wa Maswa kupitia CDM au mbunge wa CDM kupitia kupitia wilaya ya Maswa; Tatu: Je ni wabunge wote walikaa wakakubaliana kwenye hili, na kwa nini liwe hili tu la ‘posho' na isiongezwe na mishahara ya wabunge kama ilivyoainishwa katika ilani ya CDM ya mwaka 2010.

Swali la mwisho kwa mwenye kufikiri: Je kabla ya kumsajili Shibuda kuwa mchezaji wa CDM kuna sehemu yoyote iliyomtaka abadilishe misimamo yake ambayo ilifahamika sana toka alipokuwa jumuia ya wazazi? Labda kikubwa ni kwa CDM kuwa na orodha ya watu ambao ingependa wajiunge na chama chao ili kuepuka migongano iliyowahi kujitokeza kuanzia kwa kina Wangwe (RIP), Zito, Kafulila, na sasa Shibuda. Na ili hilo lifanikiwe itabidi wapate watu wenye sifa kuu ya kudumisha fikra sahihi za ‘kidemokrasia' za Mwenyekiti na Katibu wa CDM.
 
"Nitashangaa kama nitaitwa na kiongozi yoyote wa kambi yetu ya upinzani au Chadema kwa tuhuma za kutoa maoni yangu huru niliyoyatoa bungeni jana (juzi), hata nilipokuwa CCM nilipenda kusahihisha palipokuwa na makosa"."Sitarajii Chadema kuna viongozi wanaweza kudidimiza demokrasia na uhuru wa kutoa maoni, wakati chama kinafanya maandamano kutoa maoni huru kwa Watanzania. Kama mimi sitakiwi kutoa maoni huru basi hakunaslahi binafsi, tutambue kwamba mbunge anapozungumza bungeni anasema kwa maana pana kwa watu wenye mitazamo tofauti kwa lengo la kuleta fikra endelevu".Alisema kwamba hana habari kama wabunge wote wa Chadema walikutana na kukubaliana kuikataa posho ya vikao vya Bunge.Shibuda akifafanua zaidi suala hilo la posho japo kwenye Ilani ya Uchaguzi wa 2010 ya chama chake ilitaka kupunguza posho hizo za vikao pamoja na mshahara wa mbunge, alisema, "Ilani ya Uchaguzi ni mpango kazi wa kuendeleza programu ya chama kilichopo madarakani, kwa hiyo hivi sasa hapa bungeni bila kujali itikadi zetu wabunge tunaunganishwa na programu ya kuendeleza nchi, utawala bora na uongozi wa kuongoza fikra za Watanzania". Add this page to your favorite Social Bookmarking websites Sijui!! Lakini kuna ka ukweli hapa na ndio maana wakubwa wa humu (Jamii Forum) hamleti mjadala![/QUO Huyu bwana inaonekana haendani na wana Cdm mana haiwezekani akaenda tofauti na msimamo wa chama,wamtimue tuu
 
Swali la mwisho kwa mwenye kufikiri: Je kabla ya kumsajili Shibuda kuwa mchezaji wa CDM kuna sehemu yoyote iliyomtaka abadilishe misimamo yake ambayo ilifahamika sana toka alipokuwa jumuia ya wazazi? Labda kikubwa ni kwa CDM kuwa na orodha ya watu ambao ingependa wajiunge na chama chao ili kuepuka migongano iliyowahi kujitokeza kuanzia kwa kina Wangwe (RIP), Zito, Kafulila, na sasa Shibuda. Na ili hilo lifanikiwe itabidi wapate watu wenye sifa kuu ya kudumisha fikra sahihi za ‘kidemokrasia' za Mwenyekiti na Katibu wa CDM.

Ukiuliza maswali muhimu kama haya, mzee wangu washabiki wa humu ndani watakuambia ukapimwe akili
 
demokrasia ya chama kinachoongozwa kwa taratibu za mtei na familia itatoka wapi.shibuda wewe nyamaza tu mwenye taasisi kasema. wenzako hao wanaitikia zidumu fikra za mwanzishaji. Zitto aliambiwa mtoto kaa chini huwezi gombea uenyekiti. kafulila alifulia huko huko kwa kumpinga mwenyekiti.akili ya kuambiwa changanya na yako.
We nawe huna jipya unaonekana wa magamba
 
Back
Top Bottom