REJESHO HURU
JF-Expert Member
- Mar 6, 2014
- 4,451
- 9,374
Watalamu tunaomba msaada wa hili Jambo una mashamba yako ambayo ulinumua kwa hati ya manunuzi ikiwa na jina lako familia inajua mkeo au mumeo anajua tuna mashamba uko Morogoro.
Kutokana na changamoto za hapa na pale unaenda chukua hati unauza lile shamba bila mshirikisha mumeo au mkeo baada ya mda kupita mkeo au mumeo anaenda shambani kule anambiwa shamba lishauzwa mkeo au mumeo anarudi kukuuliza unamwambia ndio niliuza kutokana na changamoto Ile niliona nikikushirikisha utakataa Ila nishauza.
Je sheria inasemaje mke au mume anaweza kwenda kufungua mashitaka kudai fidia kuwa apewe mgao wa pesa iliyopatikana au kufungua mashitaka ya kumfukuza mnunuzi kwa kumwambia katapeliwa
Kutokana na changamoto za hapa na pale unaenda chukua hati unauza lile shamba bila mshirikisha mumeo au mkeo baada ya mda kupita mkeo au mumeo anaenda shambani kule anambiwa shamba lishauzwa mkeo au mumeo anarudi kukuuliza unamwambia ndio niliuza kutokana na changamoto Ile niliona nikikushirikisha utakataa Ila nishauza.
Je sheria inasemaje mke au mume anaweza kwenda kufungua mashitaka kudai fidia kuwa apewe mgao wa pesa iliyopatikana au kufungua mashitaka ya kumfukuza mnunuzi kwa kumwambia katapeliwa
Kwa kiifupi huwezi, na utaingia kwenye migogoro mikubwa sana:
1. Usikubali kununua kitu kwa mtu ambaye kaoa bila sahihi ya Mama, na Mwana familia mmoja ikiwezekana!
2. Aliyenunua hana uhalali kabisa, na ndiyo atakufuata na kukudai fedha zake, ni Kama fraud kabisa!
Kama unataka kumiliki kitu binafsi ukiwa na ndoa sheria inataka ukubaliane na mke/mme wakati wa kununua kwamba hii ni Mali binafsi, na ukitakiwa kuonyesha makubaliano wakati wa kuuza uwe nayo!