Shekhe Jongo analia bungeni sasa!!

Shekhe Jongo analia bungeni sasa!!

Status
Not open for further replies.
Kweli ukiipenda CCM lazima uwe chizi! Mzee mtu mzima kulia bungeni ili uonekane una uchungu na chama ni uchizi! Mie sijapenda huo uchuro
 
Viongozi wa dini ni watu muhimu sana kwenye siasa hasa wakati wa tofauti zao.Mfano Afrika ya Kati,baada ya wanasiasa kuharibu leo viongozi wadini ndiyo wanahangaika kutafuta marithiano kati ya dini mbili kuu waislamu na wakristu.

Lakini wanaumuhimu zaidi wakiwa neutral kuliko kuegemea upande mmoja.
 
Wakati nikiangalia na kusikiliza Mjadala wa Bunge la katiba Yenu , Zamu ya Kadhi wa Mkoa wa Dar es salaam ya kuchangia aliangua kilio kisichozidi sekunde 3 bila kutoa Machozi akidai kusikitishwa na watu wanaomtukana Mwl.Nyerere, Jambo la kushangaza ni Mashekhe hawa hawa BAADHI kwenye mihadhara yao Umdhihaki Baba wa taifa kuwa ndiye aliyeleta mfumo kristo na kurudisha maendeleo yao Nyuma, Je hilo chozi Shekhe ni kwa sababu umewezeshwa au ? Tuache unafiki, kweli Jehanamu tutakwenda wengi. NAWASILISHA
 
Binafsi sikuona akilia ila aliigiza kulia kwa madai kuwa waliotangulia hawatakiwi kusemwa vibaya. Kilichonisikitisha ni jinsi naye alivyoshindwa kujenga hoja ya kwanini anataka serikali 2. Anasema serikali zingine yaani 3 au 1 zitavunja Muungano. Kivipi hakueleza? Nikajiuliza je alisoma vizuri lengo la waasisi? Serikali 2 was transtional kuelekea kwenye moja. Jambo hili limechukua miaka 50 sasa bila kutekelezwa. Yeye haoni kuwa waasisi wamedhalauliwa kwa mawazo yao kutokutekelezwa! Ameshindwa kuelewa kuwa Zanzibar walishatengeneza katiba yao inayovunja katiba ya Muungano. Nimemchukulia kama mtu anayetafuta fadhila flani hivi. Ni aibu kwa kiongozi wa dini kushabikia mawazo yanayopingana na mawazo ya wananchi walio wengi. Pole yake.
 
Wakati nikiangalia na kusikiliza Mjadala wa Bunge la katiba Yenu , Zamu ya Kadhi wa Mkoa wa Dar es salaam ya kuchangia aliangua kilio kisichozidi sekunde 3 bila kutoa Machozi akidai kusikitishwa na watu wanaomtukana Mwl.Nyerere, Jambo la kushangaza ni Mashekhe hawa hawa BAADHI kwenye mihadhara yao Umdhihaki Baba wa taifa kuwa ndiye aliyeleta mfumo kristo na kurudisha maendeleo yao Nyuma, Je hilo chozi Shekhe ni kwa sababu umewezeshwa au ? Tuache unafiki, kweli Jehanamu tutakwenda wengi. NAWASILISHA
ali act nilikuwa namcheki kama Bongo movie vile poor quality
 
Amelia, achukuliwe bongo movie anaweza kufaa Sana kule kuliko bungeni na msikitini.

Kina Makongoro wangejiua kama ni hivo, ila kweli ni muigizaji maana jina lake linafaa Kaole!
 
Hivi ni tusi gani alitukanwa Nyerere? Ni tusi gani alitukanwa Sheikh Karume?
Mkuu hawa viongozi wa dini uko jehanamu watakuwa kuni,wanafki sijapata kuona,wakirudi uraiani utawasikia wakitoa mahubiri "Ndugu zangu msiseme uwongo Mola anachukizwa na waongo",wakati wanaongoza kwa uwongo na unafki..
 
shehe Ubwabwa Huyo. Hana maana..! Aliambiwa aigize kulia bahati mbaya imetoka sauti tu ya kuigiza kulia lakini macho makavu hakuna Hata tone la machozi..
 
Familia ya Nyerere haijasema babao katukanwa,then mzee warioba mbona ndo anayetukanwa????
 
Familia ya Nyerere haijasema babao katukanwa,then mzee warioba mbona ndo anayetukanwa????alomweka yule mzee Kigamboni ni nani????
 
huyu ni mnafiki mkubwa sana mimi nimemwangalia vizuri sana wkt huo mnaosema kuwa aliangua machozi ukweli ni kwamba hakua hata na dalili ya tone la chozi bali na usanii mtupu,nawaomba bongo movies wamfuate yule skhehe ni msanii bora wa mwaka.
 
utumwa wa kipato ni utumwa mbaya duniani kinacho sumbua ni utumwa tuu. wa posho wanaopokea na siyo kusimamia ukweli juu ya katiba mpya, ameshindwa kuongelea uhuru wa mahakama ya kadhi na kubaki kulia kwa sababu ya utumwa wa fikra na kipato
 
Katika jambo lisilokuwa la kawaida shekhe hamidi jongo aliangua kilio kwa kukerwa na watu wanaowatukana viongozi na waasisi wa taifa yaani mwl nyerere na karume
source tbc1

Machozi ya mtu mzima huwa na sababu zaidi ya moja mkuu...what if analilia malengo yake kutotimia baada ya kuwa na kila dalili ya bunge kuisha mapema kabla ya muda uliopangwa?...chunguza kwa makini zaidi mkuu...
 
Ni msanii tu, kwa nini asingetoka nje? Ni njaa na anatamani aendelee kulamba 300000 kwa siku! Inawezekana ni walewale mainterahamwe waliojificha kwenye kichaka cha dini!
 
Shehe analia kusemwa vibaya Nyerere badala ya Kulia zile kauli za Lukuvi alizozitoa kanisani na kuwabagua Waislam kuwa Serikali 3 zikipita Zanzibar itakuwa na Serikali ya Kiislam, ni vema sasa kwa karne hii tukasoma vyote elimu Dunia na hiyo ya dini ili tuwe na upeo wa kuelewa mambo sio kama hawa wenzetu walioishia na elimu ya aina moja.

Njaa haina uchaguzi mkuu unaweza kufanya kitu ambacho nafsi yako haitaki.
 
Amemuiga Pinda!
Anasema amekosa usingizi siku tatu kuwaza jinsi Waasisi walivyotukana.

Ameanza kulia na kutoa machozii!!

Anasema kumtukana Karume na Nyerere ni sawa na kumtukana baba ake mzazi.

Huyo Sheikh ni mnafik na msanii. Eti hajalala! Jana nimemuona kwa macho yangu kupitia TV kalala bungeni fofofo.
 
Hao masheikh wa CCM ndo umetufikisha hapa tulipo waislam, wanauza mali za waislam, wakiguswa serikali inawalinda, mi nadhani alikuwa analipa fadhila, nawahurumia sana watumwa wa mawazo
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom