Shekhe Jongo analia bungeni sasa!!

Shekhe Jongo analia bungeni sasa!!

Status
Not open for further replies.
Kadhi wa mkoa wa dsm, Sheikh hamid jongo, mwakilishi wa kundi la dini katika bunge la katiba ametoa machozi ya uchungu ya kutukanwa waasisi wa taifa hili mwalim j.k nyerere na sheikh abeid karume. Ameeleza kusikitishwa kwake kwa tabia hiyo ya kutoa matusi na kejeli kwa wazee hao yaliyofanywa na baadhi ya wajumbe wa bunge hilo akisema kuwa mtu akishakufa huachwa bila kusemwa vibaya kwa sababu tayari anakutana/amekutana na mungu ambaye ndio hakimu wa kweli.

amelia na kudondosha chozi na kuwaomba wabunge watumie lugha za staha na kistaarabu

jamani tuache unafiki,mbona mzee joseph warioba,anatukanwa hawa semi?? au nyerere na karume,ndio watu?
 
kwakulia kama umetukaniwa mzazi ni sawa lakini si vinginevyo....tena ukizingatia wazazi wameshakufa zamani!
 
Ni bora sasa tusiwe na mahakama ya kadhi kabisa maana kama makadhi wenyewe ndio
hawa inatia shaka sana, nakumbuka kuna mama mmoja alienda kutaka ushauri kwa sheikh
mmoja mkubwa tu wa Bakwata namsitiri maana ni marehemu kwa sasa yule sheikh akamtongoza
na kumshauri aachane na mumewe naye atamsaidia sana iwapo atakubali kuishi nae, toka siku
hiyo hata akitoa mawaidha Redioni yanaingilia kushoto na kutokea kulia.
 
Naomba nikuulize ww mleta maada ni nn maana ya siasa? Naomba nijibu hilo tu mkuu na unieleweshe nn maana ya siasa?
 
Huyo shekh angelia kukojolewa kwa Qur'an,aache ujuha hapa,nyerere na karumee watamsaidia nn???
 
Unafiki, anaacha kulia Lukuvi kuongea ujinga kanisani, Komba kutishia kuingia kichakani, bi Asha kuporomosha matusi bungeni ana lia kumkosoa Mwl. Nyere? Kichekesho.

Yaani hao siwapendi Intarahamwe wakubwa.
 
Kama kweli ni wa bakwata basi anawajengea uhalali wanaoipinga bakwata kuwa ni tawi la ccm, kwa nn hakuna liberal minds pale Kinondoni?
 
hivi Tanzania tumekosa watu wa kuandika katiba bila kulipwa posho? hii ilikuwa mtego ama kula posho upitishe kariba ya ccm au kosa posho
 
Amelia, achukuliwe bongo movie anaweza kufaa Sana kule kuliko bungeni na msikitini.
 
Alilia kinafiki mno.....sio kilio cha moyoni....mikono yake yote ilificha macho....alipoachia nilishuhudia uso wake ukiwa mkavu kabisa......ndo maana siwapendi BAKWATA
 
Hata viongozi wa dini wanatoa rushwa mbele ya kadannasi daaa!! this is too much (extortion).
 
Huyu Sheikh Ubwabwa nae njaa tu inamsumbua, kuna vitu vingi vya maana vya kutoa machozi lakini sio hilo jambo. Kuna watanzania wangapi wanakufa kutokana na kukosa huduma muhimu za afya lakini hatoi machozi, kuna wakina mama wangapi mahospitalini wanaolala chini na wengine wanne kwenye kitanda kimoja lakini hatujamsikia anamwaga chozi, kuna wanafunzi wangapi wanaishia kukaa chini huku wakikosa walimu mashuleni na hatujamsikia akilalamika.

Na hii iwaendee viongozi wote wa dini wanaoweka maslahi ya matumbo yao kwanza kuliko mahitaji muhimu katika jamii yetu.
 
Hivi ni tusi gani alitukanwa Nyerere? Ni tusi gani alitukanwa Sheikh Karume?
 
Mimi sijui maana ila huwasikia viongizi Wa siasa kua dini na siasa nitofauty jee?serekali mbili na mahakama ya kadhwi nimoja
 
Huyu Sheikh Ubwabwa nae njaa tu inamsumbua, kuna vitu vingi vya maana vya kutoa machozi lakini sio hilo jambo. Kuna watanzania wangapi wanakufa kutokana na kukosa huduma muhimu za afya lakini hatoi machozi, kuna wakina mama wangapi mahospitalini wanaolala chini na wengine wanne kwenye kitanda kimoja lakini hatujamsikia anamwaga chozi, kuna wanafunzi wangapi wanaishia kukaa chini huku wakikosa walimu mashuleni na hatujamsikia akilalamika.

Na hii iwaendee viongozi wote wa dini wanaoweka maslahi ya matumbo yao kwanza kuliko mahitaji muhimu katika jamii yetu.

laki 3 ndugu,alafu siume sikia baasha zinatembea kule mjengoni,nadhani mshika fuko atamtafuta,pale bungeni watu wanatafuta maslai ya matumbo yao na sio wananchi,ndio fursa ya kutengeneza mshiko mkuu,
 
Anamlilia mtu amabaye ameshawahi kumuona? Huyo mwingine unayetaka amlilie alisha muona wapi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom