Sheikh Khalifa Khamis amzushia UDINI Rais Magufuli

Sheikh Khalifa Khamis amzushia UDINI Rais Magufuli

Status
Not open for further replies.
Acha porojo zako.Unaweza kuwa unaumia sana kwa sababu labda huelewi.
Manung'uniko si sehemu ya maisha.Huwezi kumridhisha kila mtu.Yaani kwa akili yako unataka uongozi ugawanywe kama zawadi.Wanaolalamika ni wengi kuanzia Ombaomba,Maafa kagera,Wanafunzi,Wakulima,Wafanyakazi mishahara midogo,Daladala,Mipaka ya nchi na nchi mf.Malawi,Matokeo ya Uchaguzi,Wagonjwa n.k.
Kimsingi ni kuangalia malalamiko gani ni ya Msingi na kuyafanyia kazi.
Hili la kupewa vyeo vya upendeleo eti kwa sababu ni waislamu halina maslahi kwa taifa kwa sababu kila kabila nalo litataka lipewe upendeleo.
Mtu anachaguliwa kulingana na uwezo wake ni si kwa sababu anajua sana kuswalisha au kuhudhuria msikitini.
Basi samahani mheshimiwa.
 
Sidhani kama Rais huteua watu kwa kuhoji dini zao. Pia kuna ukweli kuwa taasisi za elimu za Kikristo zimekuwa zikijitahidi sana kuendeleza watoto kielimu tofauti na taasisi nyingi za Kiislamu ambazo zimekuwa zikihimiza zaidi elimu ya Madrassa na lugha ya Kiarabu.
Acha ulaanifu wako wee kondoo...
 
Lakini pengine badala ya kulalamikia the apparent imbalance katika teuzi za mtukufu rais, twende mbele zaidi na kupendekeza solutions (naamini namna hiyo tunaweza kumsaidia zaidi rais):
- Je, tunaufahamu vizuri utaratibu (wa kisheria?) wa teuzi anazofanya Rais?
- Kuna vigezo ambavyo Rais (kisheria) analazimika kuvizingatia? Je vigezo na taratibu hizo zina uwazi kiasi gani? Kama hakuna vigezo je, isingekuwa vema kuweka vigezo na utaratibu ambao ni wa uwazi zaidi?
- Na je kama vigezo vipo, dini ya mtu ni mojawapo? Kama siyo, kuna umuhimu, sasa, wa kuweka dini kama kigezo kimojawapo au namna fulani ya kuhakikisha balance kati ya dini kuu zilizopo nchini? Hii itasaidia kutoa muongozo kwa Rais yeyote aliyepo madarakani kuhakikisha balance (kama ndivyo tunavyotaka).

Kwa upana wake, mimi nalitizama suala hili kama tatizo la kikatiba. Watanzania tulio wengi, inaelekea, bado ni 'wadini' (i.e. tunapenda kutizama/kupima mambo kutokea kwenye perspective ya dini). Hizi sentiments hata kipindi cha JK zilikuwapo (na yeye akituhumiwa kupendelea wa dini yake). Sasa kama hivyo ndivyo tulivyo, tuweke unafiki pembeni tu na tuweke mambo haya vizuri kwenye katiba yetu ili kutoa "haki" sawa kwa watanzania wote.

Kama kwa dhati kabisa tunaamini kuwa dini haipaswi kabisa kuzingatiwa (katika nafasi husika), then tunahitaji kuweka utaratibu mzuri wa kisheria ambao utaondoa au kupunguzauwezekano wa Rais kupendelea au kuonekana anapendelea dini au kabila au kanda fulani (tunaweza kuanisha nafasi ama vyeo ambavyo tungependa neutrality ya kiwango cha juu na tukaanza na hivyo). Kwa mfano tunaweza kuweka vigezo na pia kwa nafasi hizo zikawa za kuomba na kupitia mchujo wa wazi badala ya kuteuana (wenzetu Kenya wameanza vizuri tu....wao wana tatizo la ukabila zaidi kuliko udini).

Lakini ipo hoja inayotolewa na baadhi ya watu kuwa kwa sababu za kihistoria, dini fulani ina wasomi wengi zaidi kuliko nyingine (na hata makabila fulani yana wasomi wengi zaidi kuzidi mengine) na kwa hivyo kama vigezo ikiwa ni usomi na uzoefu, automatically dini au makabila yenye wasomi wengi yatakuwa na wateule wengi zaidi. Again, kama tunakubali hoja hii na tukiweka unafiki pembeni, tunaweza kuweka utaratibu wa kisheria ambao kunaweza kuwepo kwa affirmative action or positive discrimination (linafanyika hili kwa wanawake) kwa watu wa dini ama makabila tunayodhania hayana wasomi wengi (Kwa mfano kama kuna candidates wa dini mbili wote wanatimiza vigezo, anayetoka kwenye dini ama kabila "kandamizwa" apewe nafasi kwanza/upendeleo).

Lakini tujiulize pia kama mambo haya yatatuweka pamoja zaidi kama taifa au yatazidi kutugawa?
 
ushasema wahindu ...hao si watanzania..tanzania wazawa zipo dini mbili kuu...Uislamu na Ukristo..
Nani alikundanganya? Kwani hizo wakrsto wote ni wazawa,kwani hizo dini zimeanzia Tz.kuna dini nying tu ww huzjui..mim hapa sio mkrsto wala sio muislam na nina dini yangu mbali na hizo unazosema za wazaw na ni mtanzania tena siijui nchi nyingine zaid ya tz....so usiamin viscvyo na kuja kulalamika
 
Lakini pengine badala ya kulalamikia the apparent imbalance katika teuzi za mtukufu rais, twende mbele zaidi na kupendekeza solutions (naamini namna hiyo tunaweza kumsaidia zaidi rais):
- Je, tunaufahamu vizuri utaratibu (wa kisheria?) wa teuzi anazofanya Rais?
- Kuna vigezo ambavyo Rais (kisheria) analazimika kuvizingatia? Je vigezo na taratibu hizo zina uwazi kiasi gani? Kama hakuna vigezo je, isingekuwa vema kuweka vigezo na utaratibu ambao ni wa uwazi zaidi?
- Na je kama vigezo vipo, dini ya mtu ni mmoja wapo? Kama siyo, kuna umuhimu, sasa, wa kuweka dini kama kigezo kimojawapo au namna fulani ya kuhakikisha balance kati ya dini kuu zilizopo nchini? Hii itasaidia kutoa muongozo kwa Rais yeyote aliyepo madarakani kuhakikisha balance (kama ndivyo tunavyotaka).

Kwa upana wake, mimi nalitizama suala hili kama tatizo la kikatiba. Watanzania tulio wengi, inaelekea, bado ni 'wadini' (i.e. tunapenda kutizama/kupima mambo kutokea kwenye perspective ya dini). Hizi sentiments hata kipindi cha JK zilikuwapo (na yeye akituhumiwa kupendelea wa dini yake). Sasa kama hivyo ndivyo tulivyo, tuweke unafiki pembeni tu na tuweke mambo haya vizuri kwenye katiba yetu ili kutoa "haki" sawa kwa watanzania wote.

Kama kwa dhati kabisa tunaamini kuwa dini haipaswi kabisa kuzingatiwa (katika nafasi husika), then tunahitaji kuweka utaratibu mzuri wa kisheria ambao utaondoa au kupunguzauwezekano wa Rais kupendelea au kuonekana anapendelea dini au kabila au kanda fulani (tunaweza kuanisha nafasi ama vyeo ambavyo tungependa neutrality ya kiwango cha juu na tukaanza na hivyo). Kwa mfano tunaweza kuweka vigezo na pia kwa nafasi hizo zikawa za kuomba na kupitia mchujo wa wazi badala ya kuteuana (wenzetu Kenya wameanza vizuri tu....wao wana tatizo la ukabila zaidi kuliko udini).

Lakini ipo hoja inayotolewa na baadhi ya watu kuwa kwa sababu za kihistoria, dini fulani ina wasomi wengi zaidi kuliko nyingine (na hata makabila fulani yana wasomi wengi zaidi kuzidi mengine) na kwa hivyo kama vigezo ikiwa ni usomi na uzoefu, automatically dini au makabila yenye wasomi wengi yatakuwa na wateule wengi zaidi. Again, kama tunakubali hoja hii na tukiweka unafiki pembeni, tunaweza kuweka utaratibu wa kisheria ambao kunaweza kuwepo kwa affirmative action or positive discrimination (linafanyika hili kwa wanawake) kwa watu wa dini ama makabila tunayodhania hayana wasomi wengi (Kwa mfano kama kuna candidates wa dini mbili wote wanatimiza vigezo, anayetoka kwenye dini ama kabila "kandamizwa" apewe nafasi kwanza/upendeleo).

Lakini tujiulize pia kama mambo haya yatatuweka pamoja zaidi kama taifa au yatazidi kutugawa?

moja ya comment za akili sana. haya,malalamiko tangu uhuru ni lazima tukae sasa tuyamalize, maadui zetu watakuja kutuchochea watuvuruge, au sisi wenyewe tutakuja,kuvurugana huko baadae, na ubaya haya mambo yakishaanza tu kutulia ni shida, tutaenfa wapi sisi jamani
 
The Hyper,
''Mwembechai Kiliings...'' kitabu cha Njozi kilichoonya kuhusu haya haya
kilifungiwa 2002 je ndiyo tatizo limekwisha?

Dawa si kufungia magazeti.
Ufumbuzi ni kukabiliana na tatizo kujua ukweli.

Yah,nakubaliana na wewe mkuu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom