Sheikh Khalifa Khamis amzushia UDINI Rais Magufuli

Sheikh Khalifa Khamis amzushia UDINI Rais Magufuli

Status
Not open for further replies.
Kwa masiku kadhaa Sheikh Khalifa amekuwa akisikika na kauli yake ya kumtuhumu Rais Magufuli kuwajaza Wakristo wengi kwenye nafasi zake za uteuzi.

Aidha Sheikh huyo aliongezea kwa kusema kuwa licha ya uwepo wa suala hili la udini Rais Magufuli ameweka wazi upendeleo wake wa kikanda ambapo watu wa kanda ya Ziwa wameonekana kung’ara kwa kuteuliwa katika nafasi za uongozi kwa wingi zaidi kuliko watu wa kanda yoyote hapa nchini.

Akizungumzia suala hilo na waandishi wa gazeti la Mizani la November 11, 2016 Sheikh Khalifa Khamis alieleza kuwa katika nafasi 10 walizotumbuliwa Waislam ni nafasi 1 tu ndiyo aliyopewa Muislam.

Sheikh Khalifa alizidi kufafanua kuwa Wenyeviti wa bodi mbalimbali walioteuliwa na Rais Magufuli 18 ni Wakristo na 1 tu ndiyo Muislam.

Makatibu Tawala wa Wilaya Wakristo ni 81% huku Waislam wakiambulia 19% tu. Wakuu wa wilaya Wakristo ni 71% na Waislam ni 21%.

Makatibu Tawala wa mikoa 137 ni Wakristo na 16 tu ndiyo Waislam. Wakurugenzi wa Halmashauri za wilaya na majiji Wakristo ni 185 na Waislam ni 36 tu.

Kitu pekee anachopaswa kutambua Sheikh Khalifa Khamis ni kwamba Rais Magufuli hateui mtu kwa kuangalia dini bali anaangalia taaluma na uwezo wa kuongoza.

Kukiwa na kitengo kinachohitaji uwakilishi wa dini hapo ndo tunapaswa kuangalia usawa wa uwakilishi wa kidini. Pia anapaswa kutambua kuwa Tanzania haina Wakristo na Waislam tu, kuna watu wa dini tofauti tofauti na wasio na dini pia, je hao amewaweka kwenye kipengele gani?

Hizi ni njama tu za kutaka kumrudisha nyuma Rais wetu kipenzi cha Watanzania wengi. Watanzania tunahitaji MAENDELEO na AMANI tu, mambo ya dini tunayaacha kwenye nyumba za ibada. Tunapofika kwenye sekta za umma hatusemi tena mambo ya dini zetu, bali kauli yetu huwa ni moja tu nayo ni HAPA KAZI TU.

Ni jambo la kusikitisha sana kuona kiongozi mkubwa wa dini akitoa tuhuma za uongo na uzushi kwa Kiongozi Mkuu wa wa nchi yetu.

Sheikh Khalifa anakiuka misingi ya imara ya taifa letu iliyowekwa na baba wa Taifa Mwl Julius Nyerere ya kupiga vita udini na ukabila.

Udini na ukabila ni mbegu mbaya sana ambayo siyo tu haifai kupandwa kwenye ardhi yetu bali haipaswi hata kutunzwa majumbani mwetu, isije mea hata kwa bahati mbaya.

Mataifa mengi yameshuhudia machafuko na mauaji ya kutisha kwa udini na ukabila. Hakuna hata Mtanzania mmoja anayetamani kuona mfano wa mauaji ya Kimbari ya Rwanda au vita ya Biafra Nigeria ikitokea hapa kwetu.
Mlete mada umeileta vizuri kweli kweli
Ila nahisi huijui ile sera ya siri waliyoiita OPARESHI VILEMBE iliyokua ikiendelea serikalini lkn kama hujui hebu chukua muda kidoogo tu kuifanyia utafiti kisha utajua tu ni kwann wanalalamika.

Wala usijitoe ufahamu....
Angalia ktk mifano uliyoitoa ya Rwanda na Nigeria, machafuko yalitokea baada ya kuona kundi moja kuhisi linakandamizwa na kudhulumiwa baadhi ya mambo.

Kama rais alikua halijui hili basi alijue kuwa anapaswa kuangalia uteuzi wake uwe na sura ya kitaifa, kwa kawaida anayeumizwa ndie hua analalamika au kupiga kelele..... kama watu wengine hawajalalamika si kigezo cha kufanya wengine wasilalamike kwa yale wanayoona hawajatendewa sawa.

Rais ana nia njema tu na taifa letu na hata uteuzi wake mie siutilii shaka ila kama watu wanalalamikia hilo basi yampasa kuliangalia tena na tena ktk teuzi zake zijazo.
 
Uchaguzi ule, ukiwa unayaangalia mambo kwa upana zaidi utaona kuwa ulikuwa ni mchuano wenye Factors nyingi, kwa jinsi ninavyoona, factor mojawapo ni Udini. Kulikuwa na kambi kuu tatu

1) Wakatoliki
2) Waprotestanti
3) Waislamu.

Mpambano ulikuwa zaidi kati ya Wakatoliki na Protestanti hasa Walutheri. Kwa upande wa waislamu wao hawakuwa na mzuka sana wa kidini katika huu mchuano, hawa unaweza kusema ni kama kundi la " Undecided" yaani wangepigia yoyote tu.

Ukiangali kambi ya Wakatoliki ilikuwa ni BWM, JPM, na machinery nzima ya kanisa katoliki

Ukija upande wa Walutheri kambi yao iliongozwa na watu kama , EL, FAM, JM, FTS na machinery nzima ya kanisa la kilutheri, hawa walifikia hata kujiaminisha kuwa sasa ni zamu yao!

Hata hivyo kanisa katoliki ni more powerful lina mtandao mpana zaidi na limeibuka kidedea!.

Sasa linajikita katika system kwa uimara zaidi, kuhakikisha maslahi yake yako intact kwa muda mrefu ujao!. Hata hivyo wawe makini kwa sababu jamii ikishaona aina ya inequalities, hiyo jamii haiwi inara, utaifa unakuwa katika hali fulani loose! Ni hatari sana.
 
Kwani wameteuliwa ili wakafaye ibada au watumikie taifa? Msipende kuongea vitu kwa hisia Bali angalieni tija hakuna dini kwenye selikari ya Tanzania
Kama unalijua hilo kwanini iwe bahati mbaya ya kuteuliwa wakristo pekee?

Kwanini hatuoni waislaam wenye uwezo wakiteuliwa kama mnajua hawatapendelea?

Au mnawaona waislaam ni wanyonge ndani ya nchi waliotumia mali zao kudai uhuru wake?

Mbona Kikwete hakuwa mbaguzi
Mpangawangu,
Tatizo hili ni la muda mrefu sana.
Msome Mwalimu Nyerere anasema nini kuhusu tatizo hili:

''Tarehe 5 Novemba, 1985 kabla hajastaafu urais, Nyerere aliwahutubia wazee wa Dar es Salaam. Hotuba hii ilijaa simanzi, Nyerere akikumbuka jinsi Waislam walivyompokea Dar es Salaam kwa mapenzi makubwa ingawa yeye alikuwa Mkristo. Wazee hawa wengi wao walikuwa wanachama wa zamani wa TANU waliomuunga mkono Nyerere wakati wa kudai uhuru. Nyerere aliusifia mchango wa Waislam katika kipindi kile kigumu cha kudai uhuru. Nyerere alisema kuwa upogo katika elimu uliorithiwa na serikali yake kutoka kwa Waingereza baina ya Waislam na Wakristo yeye ameuondosha katika kipindi cha utawala wake:

Waislam wametupa nafasi kupitia sera yetu ya elimu, kurekebisha upogo. Sasa nipo katika hali ya kufarahisha kwa kuwa wakati mwingine sielewi kama Mbunge mpya, Waziri, au Katibu Mkuu katika wizara zetu za serikali, ni Muislam au Mkristo au hana dini labda pale jina lake la kwanza linapotoa utambulisho. Na hata hivyo hiyo siyo njia ya kuaminika kutoa utambulisho wa dini kwa kuwa tuna Wakristo wenye majina ya Kiislam, na Waislam wenye majina ya Kikristo. Kuvumiliana huku nyie ndiyo sababu; nilichofanya mimi ni kuzungumzia maadili haya kwa niaba yenu.[1]''

Hapo chini ni uchambuzi wangu ambao upo katika kitabu cha Abdul Sykes:

Hotuba hii ilikuwa ya ulaghai. Ukweli ni kuwa miongo mitatu baada ya uhuru Waislam hawajanufaika chochote wako katika hali ile ile aliyowaacha wakoloni au mbaya zaidi. Sivalon (1992) amefichua kuwa Kanisa limeweza kujenga himaya yake ambayo inahodhi 75% ya viti katika Bunge la Tanzania. Kati ya viti hivyo 70% vipo mikononi mwa Wakatoliki na vilivyobaki vimegawika kati ya Waislam na Wakristo wa madhehebu nyingine.[1] Baada ya kupatikana uhuru, Kanisa lilipohisi wasiwasi, limeweza kwa urahisi kabisa kuwazuia na kuwadhibiti Waislam. Serikali imeweza kutumia nguvu iliyokuwanayo katika kudhibiti siasa kuzuia harakati za Waislam kudai fursa sawa na Wakristo katika kugawana madaraka katika serikali. Kanisa limehakikisha kuwa kupinduliwa kwa ukoloni si kizingiti kwa Ukristo, ingawa ingetegemewa kuwa Kanisa lingedhirika kwa kuanguka kwa ukoloni. Katika miaka yake zaidi ya mia moja, Kanisa lilikuwa limestarehe kama muokozi wa nafsi na watu wenyewe. Kanisa lilikuwa salama na halikupambana na msukosuko wowote kutoka kwa serikali kwa kuwa lilikuwa Kanisa ndilo lilishika hatamu ya serikali.''
 
Kama hali ipo hivyo, Basi bado tutaona mengi sana miaka 9 ijayo. Na hakuna atakayeweza kufungua kinywa chake.
 
Sasa
Sheikh anataka kama ilivyo NSSF jinsi yule Dr. Dau alivyofanya au? Maana pale wamejaa wa upande wa dini ile tu, kama ilivyokuwa TRA walijaa wa K'njaro tu. Zama hizo zimepitwa na wakati.
sasa mmejaaa wakatoliki na kanda ya ziwa
 
Uchaguzi ule, ukiwa unayaangalia mambo kwa upana zaidi utaona kuwa ulikuwa ni mchuano wenye Factors nyingi, kwa jinsi ninavyoona, factor mojawapo ni Udini. Kulikuwa na kambi kuu tatu

1) Wakatoliki
2) Waprotestanti
3) Waislamu.

Mpambano ulikuwa zaidi kati ya Wakatoliki na Protestanti hasa Walutheri. Kwa upande wa waislamu wao hawakuwa na mzuka sana wa kidini katika huu mchuano, hawa unaweza kusema ni kama kundi la " Undecided" yaani wangepigia yoyote tu.

Ukiangali kambi ya Wakatoliki ilikuwa ni BWM, JPM, na machinery nzima ya kanisa katoliki

Ukija upande wa Walutheri kambi yao iliongozwa na watu kama , EL, FAM, JM, FTS na machinery nzima ya kanisa la kilutheri, hawa walifikia hata kujiaminisha kuwa sasa ni zamu yao!

Hata hivyo kanisa katoliki ni more powerful lina mtandao mpana zaidi na limeibuka kidedea!.

Sasa linajikita katika system kwa uimara zaidi, kuhakikisha maslahi yake yako intact kwa muda mrefu ujao!. Hata hivyo wawe makini kwa sababu jamii ikishaona aina ya inequalities, hiyo jamii haiwi inara, utaifa unakuwa katika hali fulani loose! Ni hatari sana.
Kwa sababu za kihistoria katoliki wametawala tangu Uhuru na wataendelea sana kutawala
 
Udini hauna misingi imara,unapotokea ni lazima tukosoe na tupinge,kwakuwa udini huo unaonekana wazi kwa takwimu zilizopo,musiingize maagizo ya kanisa katika maamuzi ya taifa.
Hili ni taifa la wenye dini na wasio na dini.
 
Nchi hii Waislamu ni watu wa Amani vinginevyo kingekuwa kishanuka kitambo na Amani ya Nchi hii ni kwa sababu ya Waislamu.
 
Daah mambo yako wazi kabisa hata KUTUDANGANYA TU LIJAMAA LIMESHINDWA.
 
Watu wengi watatumwa sana kuja kuleta uzi za kukinga serikali.. Eti "Raisi wetu kipenzi cha watu"
 
Nilijua tu, teuzi za mheshimiwa kwa jinsi zilivyokaa ni time bomb, nilijua zitaback fire tu at a certain position in time, naona tayari chungu kinafukuta.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Kama kuna mambo amabayo siyapendi ni udini na ukabila, haya hayajawahi kumnufaisha mtu wala nchi zaidi ya kuharibu tena yanaharibu vibaya sana, tujitafakaeri tusichokonoe yasiyo na manufaa.
 
Viongozi wote wakristo walioongoza Tanzania wanaongozwa na udini katika kuteuwa viongozi. Na anapotokea kiongozi muislam huwa wanamtazama kwa macho matatu na kumjengea wigo wakumdhibiti kisirisiri.
 
Watanzania wanataka kuona maendeleo ya haraka ktk kila sekta na sio kusikia mambo ya Udini!!
Watanzania wanahitaji kiongozi/viongozi wazalendo ambao watawatumikia kwa nguvu zao zote bila kujali dini!
KIONGOZI yeyote anye mbagua Mtanzania mwenzake kwa sababu tu ya dini yake, asiwe na nafasi na aondolewe haraka sana!
 
Swala siyo Udini, Swala ni shule. Fanya sampling ndogo tu Angalia sasa hivi hata kwenye majina ya wahitimu wa shule za msingi na sekondari. Chunguza hayo majina mengi ni ya Dini gani? Halafu rudi kwenye takwimu, wakristo na waislam wapi ni wengi? Watu wamekaa kuchunguza udini Bila hoja za Msingi.
Takwimu zako zinakupa picha ya uhaba wa fikra,kwa nafasi gan mpka walio na elimu ni wakristo waislam hawapo?hili jambo lipo wazi kbsa ishu sio utendaj ishu maagzo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom