Mwafrika wa Kike
JF-Expert Member
- Jul 5, 2007
- 5,185
- 56
In the early eighties nilipokuwa nawatembelea wenzangu waliobahatika kuingia UDSM niliwakuta wakihangaikia maji. Kama sijakosea ni wakati huo wakajengewa vyoo vya shimo ambapo mtu ukitoka unanuka dawa ya choo. Sasa watoto wao wameingia hapo hapo na matatizo waliyoyakuta baba na mama zao bado yapo. Wamekaa miaka zaidi ya miaka 20 bila kutatuliwa matatizo ya msingi na bado mnataka wawe wastahimilivu? Ustahimilivu una mwisho na mwisho wake mara nyingi si mzuri!
P.S. Karibu tena Bin Maryam!
Hili ndilo tatizo kubwa la nchi yetu. Kila kizazi kinataka kusukumizia matatizo kizazi kijacho. Mwisho wa mambo ndiyo yale ya COngo na Rwanda yanatokea bila watu kujua.