Serikali ya Tanzania imebariki raia wake kuibiwa kupitia Makampuni ya Michezo ya Kubahatisha

Mfimbo

Member
May 10, 2015
5
11
Makampuni ya michezo ya kubahatisha yameendelea kuongezeka kwa kasi sana nchini Tanzania kuliko nchi nyingine za ukanda wa Afrika Mashariki.

Ongezeko hili linachagizwa na ukweli usiopingika kuwa kumiliki kampuni ya michezo ya kubahatisha ndio njia rahisi zaidi ya kuvuna pesa kutoka kwa watu wa rika mbalimbali.

Kilichonisukuma kuandika andiko hili sio kuhoji uhalali wa makampuni haya ya michezo ya kubahatisha bali namna yalivyopewa uhuru na serikali kuchota pesa za wavuja jasho bila kufuatiliwa kwa huduma zao.

Kinachoendelea kwenye makampuni haya ni zaidi ya utapeli wa kawaida. Leo nitapenda nijikite zaidi kwenye michezo ya kasino (online casino) inayotolewa kwenye makampuni haya mbalimbali hususani game ya AVIATOR na ZEPPELIN.

Michezo hii imekuwa ni hatari sana kwa taifa letu kiuchumi, kiafya na kiakili kwa ujumla. There's no fairness hata kidogo kwenye michezo hii na zaidi ipo kuwaibia watumiaji wa huduma hizo.

Sina uhakika kama serikali huwa inajiridhisha kwenye huduma zinazotolewa na makampuni haya kwa watumiaji. Na kama huwa inafanya hivyo na imeamua kukaa kimya badi ni dhahiri kuwa imebariki taifa lake liendelee kunyonywa na kuharibiwa kiakili.

Serikali ndio mlezi mkuu wa taifa lake na haipaswi kuruhusu na kuhalalisha wizi wa wazi kwa raia wake. Michezo tajwa haiongozwi na bahati kama watu wanavyofikiria bali ni mitambo inayoongozwa na mmiliki wa mitambo husika.

Mmiliki anaamua atakalo kwenye pesa za watumiaji wa huduma na hakuna mechanisms za kufuatilia fairness katika matokeo yanayochakatwa na mtambo.

Jambo baya zaidi ni kuwa michezo hii ina nguvu kubwa sana ya kutengeneza uraibu (addiction) kwa watumiaji wake. Na kutambua hilo ndio maana hata baadhi ya makampuni wameondoa option ya kumruhusu mtumiaji wa huduma kujitoa (permanent self-exclusion) katika tovuti zao na hata ikitokea unamjulisha mtoa huduma juu ya nia ya kujiondoa kwa kufungwa account yako bado sio rahisi kusikilizwa.

Hawaruhusu account yako kufutwa kwa sababu wanaamini you're addicted already na sio rahisi kukaa bila kuifungua account yako.

Kila anayecheza michezo ya online casino ana chance kubwa ya kukumbwa na magongwa ya moyo na yale yanayohusiana na mfumo wa akili. Hivyo, vijana kwa wazee chukueni tahadhali kubwa juu ya michezo ya kubahatisha. Sio kweli kuwa kuna pesa huko za kuchukua kilaini tu.

Hata hao washindi wanaotangazwa kuwa wameshinda pesa nyingi sio issue ya ukweli na most of them are ghost winners na lengo ni kukuaminisha kuwa one day utakuwa wewe.

Serikali ifanye tafiti za kina kujua faida za kodi inayozikusanya kutoka kwa makampuni haya inaendana na madhara yatokanayo na huduma zinazotolewa kwa watumiaji.

Michezo hii hairuhusu vijana kuwa chanzo cha ujenzi wa taifa kiuchumi na mbaya zaidi athari zake zinagusa mpaka nyanja nyingine muhimu kwa maendeleo ya taifa kama vile elimu.

Vijana wa Sekondari, vyuo vya kati mpaka huko university wanaharibika kupitia michezo hii ya kubashiri.

Mwisho niwahimize wazazi tuwe na mfumo mzuri wa malezi ili kuwaepusha watoto wetu kujiingiza kwenye wizi huu ambao unavuna pesa likuki kwa manufaa ya watu wachache.
 
Makampuni ya michezo ya kubahatisha yameendelea kuongezeka kwa kasi sana nchini Tanzania kuliko nchi nyingine za ukanda wa Afrika Mashariki.

Ongezeko hili linachagizwa na ukweli usiopingika kuwa kumiliki kampuni ya michezo ya kubahatisha ndio njia rahisi zaidi ya kuvuna pesa kutoka kwa watu wa rika mbalimbali.

Kilichonisukuma kuandika andiko hili sio kuhoji uhalali wa makampuni haya ya michezo ya kubahatisha bali namna yalivyopewa uhuru na serikali kuchota pesa za wavuja jasho bila kufuatiliwa kwa huduma zao.

Kinachoendelea kwenye makampuni haya ni zaidi ya utapeli wa kawaida. Leo nitapenda nijikite zaidi kwenye michezo ya kasino (online casino) inayotolewa kwenye makampuni haya mbalimbali hususani game ya AVIATOR na ZEPPELIN.

Michezo hii imekuwa ni hatari sana kwa taifa letu kiuchumi, kiafya na kiakili kwa ujumla. There's no fairness hata kidogo kwenye michezo hii na zaidi ipo kuwaibia watumiaji wa huduma hizo.

Sina uhakika kama serikali huwa inajiridhisha kwenye huduma zinazotolewa na makampuni haya kwa watumiaji. Na kama huwa inafanya hivyo na imeamua kukaa kimya badi ni dhahiri kuwa imebariki taifa lake liendelee kunyonywa na kuharibiwa kiakili.

Serikali ndio mlezi mkuu wa taifa lake na haipaswi kuruhusu na kuhalalisha wizi wa wazi kwa raia wake. Michezo tajwa haiongozwi na bahati kama watu wanavyofikiria bali ni mitambo inayoongozwa na mmiliki wa mitambo husika.

Mmiliki anaamua atakalo kwenye pesa za watumiaji wa huduma na hakuna mechanisms za kufuatilia fairness katika matokeo yanayochakatwa na mtambo.

Jambo baya zaidi ni kuwa michezo hii ina nguvu kubwa sana ya kutengeneza uraibu (addiction) kwa watumiaji wake. Na kutambua hilo ndio maana hata baadhi ya makampuni wameondoa option ya kumruhusu mtumiaji wa huduma kujitoa (permanent self-exclusion) katika tovuti zao na hata ikitokea unamjulisha mtoa huduma juu ya nia ya kujiondoa kwa kufungwa account yako bado sio rahisi kusikilizwa.

Hawaruhusu account yako kufutwa kwa sababu wanaamini you're addicted already na sio rahisi kukaa bila kuifungua account yako.

Kila anayecheza michezo ya online casino ana chance kubwa ya kukumbwa na magongwa ya moyo na yale yanayohusiana na mfumo wa akili. Hivyo, vijana kwa wazee chukueni tahadhali kubwa juu ya michezo ya kubahatisha. Sio kweli kuwa kuna pesa huko za kuchukua kilaini tu.

Hata hao washindi wanaotangazwa kuwa wameshinda pesa nyingi sio issue ya ukweli na most of them are ghost winners na lengo ni kukuaminisha kuwa one day utakuwa wewe.

Serikali ifanye tafiti za kina kujua faida za kodi inayozikusanya kutoka kwa makampuni haya inaendana na madhara yatokanayo na huduma zinazotolewa kwa watumiaji.

Michezo hii hairuhusu vijana kuwa chanzo cha ujenzi wa taifa kiuchumi na mbaya zaidi athari zake zinagusa mpaka nyanja nyingine muhimu kwa maendeleo ya taifa kama vile elimu.

Vijana wa Sekondari, vyuo vya kati mpaka huko university wanaharibika kupitia michezo hii ya kubashiri.

Mwisho niwahimize wazazi tuwe na mfumo mzuri wa malezi ili kuwaepusha watoto wetu kujiingiza kwenye wizi huu ambao unavuna pesa likuki kwa manufaa ya watu wachache.
Halafu tunatafuta mchawi kuhusu upungufu wa bidhaa, kumbe muda ambao wengi wetu tungeutumia kubuni mbinu za uzalishaji bidhaa walio wengi tunautumia kubeti, ukiwa na tsh 1000 kwenye simu yako ni mtaji tosha. Asubuhi mpaka jioni tunafanya uchambuzi wa mechi(hii inatuhusu wale tusio na shughuli nyingine). Bado tunasafari ndefu. Vijana wasialaumie, serikali imewatengeneza mazingira bora zaidi ya betting kuliko vyanzo vingine vya kujipatia riziki ambayo italeta ustawi wa taifa ,"Windfall gain" haiwezi kuwa chanzo kikuu cha kipato endelevu.
 
Najiuliza mimi ni mkazi wa Dar es Salaam kila kona kuna hizo sehemu za kubashiri na kwenye simu naona matangazo ya kubashiri lakini sijawahi kujiingiza wala kufungua akaunti za kubashiri.

Mimi nafikiri serikali inabebeshwa mzigo mzito sana, kila kitu lawama kwa serikali, hao walevi wa kubashiri wapambane na hali zao.

Ulevi mwingine ni ushabiki wa simba na yanga nao mtaanza kuilaumu serikali.
 
 
Makampuni ya michezo ya kubahatisha yameendelea kuongezeka kwa kasi sana nchini Tanzania kuliko nchi nyingine za ukanda wa Afrika Mashariki.

Ongezeko hili linachagizwa na ukweli usiopingika kuwa kumiliki kampuni ya michezo ya kubahatisha ndio njia rahisi zaidi ya kuvuna pesa kutoka kwa watu wa rika mbalimbali.

Kilichonisukuma kuandika andiko hili sio kuhoji uhalali wa makampuni haya ya michezo ya kubahatisha bali namna yalivyopewa uhuru na serikali kuchota pesa za wavuja jasho bila kufuatiliwa kwa huduma zao.

Kinachoendelea kwenye makampuni haya ni zaidi ya utapeli wa kawaida. Leo nitapenda nijikite zaidi kwenye michezo ya kasino (online casino) inayotolewa kwenye makampuni haya mbalimbali hususani game ya AVIATOR na ZEPPELIN.

Michezo hii imekuwa ni hatari sana kwa taifa letu kiuchumi, kiafya na kiakili kwa ujumla. There's no fairness hata kidogo kwenye michezo hii na zaidi ipo kuwaibia watumiaji wa huduma hizo.

Sina uhakika kama serikali huwa inajiridhisha kwenye huduma zinazotolewa na makampuni haya kwa watumiaji. Na kama huwa inafanya hivyo na imeamua kukaa kimya badi ni dhahiri kuwa imebariki taifa lake liendelee kunyonywa na kuharibiwa kiakili.

Serikali ndio mlezi mkuu wa taifa lake na haipaswi kuruhusu na kuhalalisha wizi wa wazi kwa raia wake. Michezo tajwa haiongozwi na bahati kama watu wanavyofikiria bali ni mitambo inayoongozwa na mmiliki wa mitambo husika.

Mmiliki anaamua atakalo kwenye pesa za watumiaji wa huduma na hakuna mechanisms za kufuatilia fairness katika matokeo yanayochakatwa na mtambo.

Jambo baya zaidi ni kuwa michezo hii ina nguvu kubwa sana ya kutengeneza uraibu (addiction) kwa watumiaji wake. Na kutambua hilo ndio maana hata baadhi ya makampuni wameondoa option ya kumruhusu mtumiaji wa huduma kujitoa (permanent self-exclusion) katika tovuti zao na hata ikitokea unamjulisha mtoa huduma juu ya nia ya kujiondoa kwa kufungwa account yako bado sio rahisi kusikilizwa.

Hawaruhusu account yako kufutwa kwa sababu wanaamini you're addicted already na sio rahisi kukaa bila kuifungua account yako.

Kila anayecheza michezo ya online casino ana chance kubwa ya kukumbwa na magongwa ya moyo na yale yanayohusiana na mfumo wa akili. Hivyo, vijana kwa wazee chukueni tahadhali kubwa juu ya michezo ya kubahatisha. Sio kweli kuwa kuna pesa huko za kuchukua kilaini tu.

Hata hao washindi wanaotangazwa kuwa wameshinda pesa nyingi sio issue ya ukweli na most of them are ghost winners na lengo ni kukuaminisha kuwa one day utakuwa wewe.

Serikali ifanye tafiti za kina kujua faida za kodi inayozikusanya kutoka kwa makampuni haya inaendana na madhara yatokanayo na huduma zinazotolewa kwa watumiaji.

Michezo hii hairuhusu vijana kuwa chanzo cha ujenzi wa taifa kiuchumi na mbaya zaidi athari zake zinagusa mpaka nyanja nyingine muhimu kwa maendeleo ya taifa kama vile elimu.

Vijana wa Sekondari, vyuo vya kati mpaka huko university wanaharibika kupitia michezo hii ya kubashiri.

Mwisho niwahimize wazazi tuwe na mfumo mzuri wa malezi ili kuwaepusha watoto wetu kujiingiza kwenye wizi huu ambao unavuna pesa likuki kwa manufaa ya watu wachache.
Ajira hakuna mzee.
Acha tucheze betting
 
Kwahy tunapigwa sio juzi nimepiga m3 nimenunua mbolea naenda kulima msimu huu naamin naenda kutoboa wakat hiyo m3 kikawaid ningeisikia kwenye bomba wakuu hakuna kitu kisicho na faida tu kila jambo lina faida yake na hasara zake, mungu mwenyewe anafaida na hasara, hewa inafaida na hasara, nk kwahy kukosa kwa kumi wanne wakipata, inasaidia kuliko tukikosa wote
 
Back
Top Bottom