JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,309
- 5,464
Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi akizungumza na Wanahabari, leo Machi 24, 2024, mada Miaka Mitatu ya Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.
KUHUSU KAULI YA WAZIRI NDUMBARO
Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema “Katika Lugha za michezo utani ni kitu cha kawaida, mnapozungumza 80% ni utani na 20 ndio ukweli, mkizungumza habari za Simba na Yanga ukang’ang’ana kitu kama kilivyoandikwa utafika hatua utawachosha watu.”
Amesema hayo wakati akifafanua kauli iliyotolewa na Waziri wa Michezo, Damas Ndumbaro kuwa mashabiki watakaguliwa pasi za kusafiria wakati wa Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika itakayohusisha Simba na Yanga kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.
Ameongeza “Hizo ni timu ambazo zinapenda utani, zinapokea ujumbe katika lugha rahisi, si kweli kuwa Waziri alimaanisha kutakuwa na ukaguzi wa Passport, anayehusika na ukaguzi halali ni Idara ya Uhamiaji ambayo hakuitaja alipozungumza.”
Matinyi ameongeza kuwa “Watu wamekomaa na utani hadi Mamelodi wamesikia, wameingia uoga hadi TFF wameamua kuandika barua kuwaeleza suala hilo halipo.”