Boss la DP World
JF-Expert Member
- Dec 12, 2021
- 1,997
- 7,552
Nimeinukuu toka kwa Millard Ayo.
Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania (GBT) imetimiza miaka 20 tangu kuanzishwa kwake July 01, 2003 ambapo imesema licha kufanikiwa kuchangia pato la Taifa kufikia Tsh. bilioni 170.43 kwa mwaka, ndani ya miaka hiyo pia imefanikiwa kuzalisha ajira 25,000.
“Tumefanikiwa kuongeza ajira kwa Vijana, mchango wa maendeleo wa jamii kutoka kwenye Sekta pia umeongezeka katika kipindi hicho kutoka fursa za ajira 600 kwa mwaka 2006/7 hadi 25,000 kwa mwaka huu 2022/23.
“GBT imechochea pia ongezeko la ubunifu katika aina hizi za michezo kutoka aina tatu ya michezo tu mwaka 2003 hadi kufikia zaidi ya aina saba za michezo ya kubahatisha mwaka 2023.
“Pia, GBT imefanikiwa kuweka mazingira mazuri ya uendeshaji wa Sekta hii na kuvutia makampuni yaliyowekeza katika biashara ya michezo ya kubahatisha kutoka kampuni 9 mwaka 2003 hadi kampuni 67 mwaka 2023”
“Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania (GBT) imefanikiwa kulinda haki za wachezaji na kutatua migogoro baina ya wachezaji na waendeshaji wa kampuni za michezo ya kubahatisha, tangu kuanziswa kwake GBT imekuwa ikipata hati safi ya ukaguzi na imekua mfano kwa baadhi ya nchi za Afrika, hususani ukanda wa Mashariki,Kati na Kusini”
=======
Kumbe kubeti ni ajira rasmi? Ngoja nipambane na bandari zangu nikisema sana naweza kosa yote.
Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania (GBT) imetimiza miaka 20 tangu kuanzishwa kwake July 01, 2003 ambapo imesema licha kufanikiwa kuchangia pato la Taifa kufikia Tsh. bilioni 170.43 kwa mwaka, ndani ya miaka hiyo pia imefanikiwa kuzalisha ajira 25,000.
“Tumefanikiwa kuongeza ajira kwa Vijana, mchango wa maendeleo wa jamii kutoka kwenye Sekta pia umeongezeka katika kipindi hicho kutoka fursa za ajira 600 kwa mwaka 2006/7 hadi 25,000 kwa mwaka huu 2022/23.
“GBT imechochea pia ongezeko la ubunifu katika aina hizi za michezo kutoka aina tatu ya michezo tu mwaka 2003 hadi kufikia zaidi ya aina saba za michezo ya kubahatisha mwaka 2023.
“Pia, GBT imefanikiwa kuweka mazingira mazuri ya uendeshaji wa Sekta hii na kuvutia makampuni yaliyowekeza katika biashara ya michezo ya kubahatisha kutoka kampuni 9 mwaka 2003 hadi kampuni 67 mwaka 2023”
“Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania (GBT) imefanikiwa kulinda haki za wachezaji na kutatua migogoro baina ya wachezaji na waendeshaji wa kampuni za michezo ya kubahatisha, tangu kuanziswa kwake GBT imekuwa ikipata hati safi ya ukaguzi na imekua mfano kwa baadhi ya nchi za Afrika, hususani ukanda wa Mashariki,Kati na Kusini”
=======
Kumbe kubeti ni ajira rasmi? Ngoja nipambane na bandari zangu nikisema sana naweza kosa yote.