ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,279
- 7,685
Kimsingi nakubali kwamba amejitahidi kufanya kwa kiasi cha uwezo wake kwani hatuwezi kutarijia mark II kuburuta mabehewa ya treni.Ila kwa haya yanayooneshwa kwa vielelezo vya picha hapa ni maendeleo ya Vitu na siyo maendeleo ya Watu. Tunahitaji kuona maendeleo ya watu badala ya vitu .
1.Je Wakulima maisha yao ya mebadilika?
2.Vipi kuhusu wafugaji hali hii imechangia kuboresha maisha yao na kuondoa migogoro na Wakulima.
3.Je halii hii imepunguza vifo vinavyozuilika vya akina mama na watoto Tanzania.
4.Je raslimali za Taifa zimeshawekwa mikononi mwa wananchi kwa usawa na kwa kadri ya uwezo wa Mwananchi.
Kwa ujumla nadhani alichokifanya ni kumalizia mipango ya wenzake iliyokuwa tayari kwa uwekezaji na akasahau kwamba mipango hiyo ilitakiwa iende sambamba na kuboresha hali ya Maisha ya Mwananchi wa Kawaida.
Hapana ndugu yangu Annael akisha leta sinia la Ubwabwa nyumbani ndo ata haribu kabisa Mimi mbali na kazi yangu ni mkulima mdogo mdogo.Hali yetu ni mbaya mno tunalima mazao hakuna masoko,Kupeleka watoto shule ni ghali sana na hakuna anayejishughulisha kuboresha masoko na bei za pembejeo ambazo ni kubwa sana hazi randani kabisa na bei ya mazao sokoni.
Huko kijijini tunakotumia muda mrefu ukiugua na kwenda Hospitali ni majanga ndugu yangu mtu ukiumwa tumbo panadol,ukiumwa kichwa panadol na Ukiumwa Jino Panadol,typhod panadol na hata malaria ni hivyohivyo.
Tunachokitaka kukiona ni mazingira ya mkulima kuboreshwa halingumu inayomkabili Mkulima kwa mtu ambaye Muda Mrefu yuko mjini hawezi ifahamu.
Hali yetu kiuchumi(wastani wa mapato) ni mbaya kuliko hata wakati wabarabara mbovu ambapo hata ukiuza gunia moja la Mchele ungeweza kupata fedha ya kujikimu kwa sasa gunia hilo ukiliuza bei yake ni ndogo kuliko miaka mitatu iliyopita.Ungejaribu kulitazama jambo hili kwa upande huo ungenielewa nilikuwa na maanisha nini.
Tunahitaji mipango inayotafsiri sera na kubadilisha maisha yetu basi.Hatuhitaji hisani za takrima ya Sinia la Ubwabwa,Kofia Tshirt,Nyamapori wala Kanga.
Hata akingia Dr slaa madarakani leo huwezi kutuaminisha kwamba ataweza kumfanya kila mwanakijiji aweze kuwa na maisha bora hayo unayoyazungumza, kupanga ni kuchagua, hata wewe katika maisha yako binafsi una mengi ambayo hayajatimia, kumalizia mipango ya waliomtangulia pia kunahitaji determination na uwezo wa kifedha, mf vitambulisho vya Taifa mpango ulikuwepo muda mrefu Mzee Mkapa hakuweza kuumalizia lakini yeye amefanikiwa tuache,BIG UP JK.
Kuna watu wana njaa. Ukiwaonyesha mti wenye matunda wanauliza, nani atayachuma hayo matunda?
Ukiwachumia wanauliza, nani atayamenya?
Ukiwamenyea, watasema mbona hujamenya vizuri?
Watu hawa tunao hapa Tanzania pia. Mmoja wao ni Kajunjumele BA
ataTwambie ni kwa kiwango gani ya watanzania zaidi ya 90% ambao wanaishi kwa kilimo ni kwa vipi JK amewaboreshea maisha yao. Nyingi ya nyumba zao bado ni mbavu za mbwa. Hospital nzuri kwao ni zile zilizojengwa na wamisionari kabla ya nchi kupata uhuru. Viwango vyake vilikuwa bora zaidi ya leo. Watu hawa ndio wanawafitini watoto wasifaulu darasa la 7 kwa kuchelea kushindwa karo ya 20,000. Maji safi na salama ni ndoto pamoja nakupatikana mbali na maskani yao. Watoto wanafeli kwa viwango vikubwa. Ukienda polisi au mahakamani unanua karatasi za kuandikia kesi yako huko vijijini. Zimejengwa zahanati zisizo na dawa. Reli zimehujumiwa ili mkopo uimarishe barabra ili magari ya mafisadi yaweze kudumu ktk kusafirisha mizigo na abiria kwa gharama kubwa, akinyonywa mkulima kwa kulipa gharama za usafirishaji na mkulima atalipa mkopo unaochukuliwa kila uchao. Nitaendelea.,.,.,.
ata
Unatokea mkoa gani ndugu ! hamna mbolea za ruzuku huko, ikumbukwe hata akingia huyu Dr Sala wenu mnayemwabudu never hawezi badili hii hali within a second even one term of 5 yrs period. Jambo la msingi ni kipaumbele gani kila utawala umejiwekea natarajia hata katika ngazi ya familia ndivyo ilivyo mnajinyima kwajili ya kupeleka watoto shule. hata kama katika kilimo bado kuna mapungufu ni kwa sababu ya kipaumblele.