Serikali ya Kikwete Imefanya nini 2005-2015...

Takwimu hazidanganyi.

Wenye nia njema WOTE wanathamini ujenzi huu wa taifa.

Kama ni kupiga kazi JK amepiga kazi, weakness alizonazo binadamu mwingine yeyote anaweza kuwa nazo. Hongera Mheshimiwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Dakta Jakaya Mrisho Kikwete kwa utumishi wa kutukuka.
 
Ni kweli kafanya mengi mazuri kuzidi wote waliopita. Ila jeshi la Luku v waasi la! La Interahamwe
 
Hayo haya Marekani yanatokea mkuu.
marekani wana jela guantanamo lengo kuu likiwa ni kuwashughulikia watuhumiwa wa ugaidi
  • wapi waliotupa bomu arusha
  • wapi waliofanya uracity
  • wapi wliofanya kwa ulimboka
  • wapi kwa waliofanya kwa kibanda
  • sio sawa kwa usalama wa taifa

security of the people and nation as all first then other thing can go smooth
 
Madeni yanaongezeka sana. Rais anatumia. Mabilioni kwa safari zingine ambazo hata membe .angemwakilisha alafu hamna report ya wazi kuhusu huko ulaya anakoenda kuomba msaada Mimi naona huyu mtu bado anatuongezea wtz mzigo
 
Sisi walimu hatutamsahau kwa kututelekeza,Mishahara duni pamoja na malimbikizo ya walimu tangu mwisho mwa awamu yake ya kwanza hadi leo hii hakuna dalili ya malipo,hii ni dharau ya hali ya juu kwa walimu huku pesa nyingi za nchi ikiliwa na chama chenye wanasiasa wengi serikalini(CCM). Cha kusikitisha wizara nyeti kama ya fedha kushikwa na mwendawazimu kama MWIGULU NCHEMBA yaonyesha ni jinsi gani tusivyo serious na uchumi wa nchi hii. Go Kikwete go,walimu tubaki tunajipanga upya!

Dah pole mwalimu!
 
Madeni yanaongezeka sana. Rais anatumia. Mabilioni kwa safari zingine ambazo hata membe .angemwakilisha alafu hamna report ya wazi kuhusu huko ulaya anakoenda kuomba msaada Mimi naona huyu mtu bado anatuongezea wtz mzigo

Pita Page moja baada ya nyingine, soma maelezo, Tazama Picha, kisha ndio uweke comment yako!
 
Katibu Mkuu CCM Taifa (katikati) akiwa ameongozana na Naibu katibu Mkuu Mh:Mwigulu Nchemba na Mbunge wa singida Mjini mh:Mo Dewji wakati wakutembelea Ujenzi wa Hospitali Kubwa ya Kisasa Singida Mjini.Hospitali itakayokuwa ni tegemeo kwa Mikoa yote ya kanda ya kati
10411906_253761898159379_3499225176874966824_n.jpg

10297688_253758321493070_109559123456669725_n.jpg

10414613_253758318159737_240593174201329880_n.jpg

10387465_253762018159367_5655796002011730266_n.jpg

Moja ya Majengo ya Hospitali Kubwa na Mpya iliyojengwa kwa Nguvu za Mkuu wa Mkoa wa Singida.

IMG_3469.JPG

Kinana akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Singida, alipotembelea kituo cha usambazaji maji Singida Mjini
 
Hivi Ni FAHARI Kushabikia Vimaendeleo BUTU,Huku RASLIMALI Za NCHI Zikitokomea Kwa Kasi Ya Kutisha.....??!!
 
JK ni Rais ambaye anaondoka madarakani bila kuacha kumbukumbu chanya yenye kurithiwa na kuendelezwa. Ni kweli kwamba CCM imekiri kupitia kwa Katibu Mkuu wake Kinana kuwa hali ya wananchi bado ni masikini sana, Hivyo Maisha Bora kwa kila mtanzania ni ndoto za mchana. JK ameshindwa kutekeleza mradi muhimu wa National Identity, mradi huu umeishia kusikojulikana. JK ameshindwa kuwaunganisha watanzania, amesababisha mitafaruku ya kidini kati ya Viongozi wa dini kupitia hoja ya kadhi. Ni JK ambaye ameshindwa kusimamia mchakato wa katiba na hivyo kupata katiba feki inayopingwa na watu makini.. JK ameshindwa hata zoezi la kuandikisha watanzania kwa wakati ili waweze kupiga kura ya maoni. Lakini pia JK amefeli kutekeleza agizo lake la kufanyika kwa kura ya maoni tar 30 April. Na kibaya zaidi JK atashindwa kutoka madarakani kwa muda kwa kikatiba kutokana na kushindwa kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu Oct 2015. huyu ndio JK.
 
Mafanikio makubwa kabisa ya mh. Ni kushindwa kuwasikiliza wananchi na hatimaye kuzalisha migomo isiyokuwa na tija kila kukicha..
 
jk ni rais ambaye anaondoka madarakani bila kuacha kumbukumbu chanya yenye kurithiwa na kuendelezwa. Ni kweli kwamba ccm imekiri kupitia kwa katibu mkuu wake kinana kuwa hali ya wananchi bado ni masikini sana, hivyo maisha bora kwa kila mtanzania ni ndoto za mchana. Jk ameshindwa kutekeleza mradi muhimu wa national identity, mradi huu umeishia kusikojulikana. Jk ameshindwa kuwaunganisha watanzania, amesababisha mitafaruku ya kidini kati ya viongozi wa dini kupitia hoja ya kadhi. Ni jk ambaye ameshindwa kusimamia mchakato wa katiba na hivyo kupata katiba feki inayopingwa na watu makini.. Jk ameshindwa hata zoezi la kuandikisha watanzania kwa wakati ili waweze kupiga kura ya maoni. Lakini pia jk amefeli kutekeleza agizo lake la kufanyika kwa kura ya maoni tar 30 april. Na kibaya zaidi jk atashindwa kutoka madarakani kwa muda kwa kikatiba kutokana na kushindwa kufanyika kwa uchaguzi mkuu oct 2015. Huyu ndio jk.

mafanikio ni mengi sana,moja kubwa kwa yote ni kuleta siasa za udini na hili ndo tunaloliona leo na wote tunaogopa kulizungumzia waziwazi
 
Back
Top Bottom