ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,279
- 7,685
Kazi ya Rais siyo kugawa maendeleo kama BIG ndugu yangu .Soma unielewe ninacho kimaanisha hili si suala la Kichama ni suala la Maslahi ya nchi kama ambavyo wamarekani wanaweza kuhalalisha kuvamia nchi nyingine kwakisingizio cha kueneza Demokrasia na kupinga Ugaidi (lakini ndani wakiwa na nia ya kukidhi kiu yao isiyo kwisha ya kukamata mafuta na gesi kulisha viwanda vyao) kwa Tanzania suala la Kukuza uchumi huku ukisahau Kilimo haina tofauti na kuvaa suti mpya huku ukitembea peku bila viatu. Lazima Taifa liwe na vipau mbele ambapo kwa Tanzania ilitakiwa iwe AFYA, ELIMU, MIUNDOMBINU NA KILIMO.
Wengi tunakimbilia kwenye miundo mbinu hasa barabara kwasababu tunadhani ni jambo linaloonekana kiurahisi na kwa haraka.Tunasahau kwamba Miundo Mbinu hii iliiwe na Manufaa lazima mipango izingatie nyanja nyingine ilikukamilisha ukuaji wa Uchumi kutoka kwenye makaratasi hadi kwa watu (jamii). Tunapokazania uwekezaji katika Miundo mbinu na uwekezaji Mkubwa (madini na Gesi) na wakati huo huo kusahau/kupuuza kilimo ambacho kinaajiri asilimia 80 ya wananchi tutaishia kuwa na maendeleo ya vitu na siyo watu.
Nakubaliana na wewe kwamba kupanga ni kuchagua lakini lazima unapokuwa na madaraka ya kuongoza Nchi ufanye Uchaguzi ulio Bora (an informed Decision) hii nchi ni yetu sote na tunaishi leo hatutakiwi kuishi leo as if tuna jiandaa kwa ajili ya kuishi leo .Lazima mipango na sera itafsiri na kuharakisha maendeleo sasa. Chama chochote kitakachoshindwa kuharakisha maendeleo kiondolewe kwa kura full stop.
Fursa zilizopo kwa nchi yetu ni nyingi sana ila kinachokwamisha ni Uzembe,Wizi.Ufisadi,kutowajibishana na Ubinafsi uliokithiri ambapo kila Mtu anapopata madaraka hafikirii kulitumikia Taifa bali kujitafutia madaraka ya juu zaidi na kudhibiti kama siyo kuwamaliza kabisa wenzake badala ya kukazana kuumaliza umasikini unaolinyonga Taifa hili lililobarikiwa raslimali za kila aina.
Annael umejitahidi. Umetimiza kazi ambayo jk ameipigia kelele siku nyingi ' tangazeni mazuri tunayoyafanya'.
Wekeni pia picha za mauaji ya Mwandishi Mwangosi, Babu Seya kifungoni, waliofukiwa na vifusi vya madini, waliathirika na maji sumu kutoka migodini, jk akianguka jukwaani, magari yakikwsma barabara kutopitika, misululu mirefu akina mama wakutafuta maji kahama, shinyanga, mabomu ya gongo la mboto...uchunguzi ukiendekea, vijana waathirka madawa ya kulevya. this will balance your story, itaonesha uzalendo wako pia.